Sunday, May 13, 2012

JUMAPILI NJEMA NA TUSALI SALA YA BABA YETU!!

SALA KUU

Baba yetu uliye Mbinguni,
Jina lako litukuzwe,
Ufalme wako ufike,
Utakalo lifanyike , duniani kama Mbinguni.
Utupe leo mkate wetu wa kila siku,
Utusemehe makosa yetu, kama tunavyowasamehe na sisi waliotukosea.
Usitutie katika vishawishi, lakini utuokoe maovuni.(Kwa kuwa ufalme ni wako, na nguvu, na utukufu, hata milele. Amina
HII SALA IMEBEBA MAOMBI YOTE, LIKIWEMO LA KUSAMEHEWA DHAMBI NA KUOMBA RIZIKI.
UKISALI  HII , HUNA HAJA YA KUSALI VINGINE VYOVYOTE.
FANYA HIVYO KILA SIKU, KILA UPATAPO MUDA.
Basi ngoja dada Rose Muhando aikamilishe jumapili hii ni wimbo huu UTAMU WA YESU!!

JUMAPILI NJEMA SANA KWA WOTE NA WOTE MNAPENDWA!!


4 comments:

Rachel Siwa said...

Asante sana da'Yasinta, j'2 njema kwako na familia na woooteee wapitao Ruhuwiko!!!!!mama mama UTAMU WA YESU!!

Ndugu Nkwazi N Mhango said...

Amina na ubarikiwe na familia yake.

ray njau said...

5 Je, Yehova husikiliza sala zote? Fikiria yale aliyowaambia Waisraeli waasi katika siku za nabii Isaya: “Hata mjapotoa sala nyingi, mimi sisikilizi; mikono yenu imejaa umwagaji wa damu.” (Isaya 1:15) Kwa hiyo, matendo fulani yanaweza kumfanya Mungu asisikilize sala zetu. Basi, ili sala zetu zisikilizwe na Mungu, ni lazima tutimize matakwa fulani muhimu.

6 Takwa moja muhimu ni kuwa na imani. (Marko 11:24) Mtume Paulo aliandika: “Bila imani haiwezekani kamwe kumpendeza [Mungu] vema, kwa maana yule anayemkaribia Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko na kwamba yeye huwa mthawabishaji wa wale wanaomtafuta kwa bidii.” (Waebrania 11:6) Mbali na kuamini kwamba kuna Mungu anayesikiliza na kujibu sala, mengi yanahitajiwa ili kuwa na imani ya kweli. Imani huthibitika kwa matendo yetu. Maisha yetu ya kila siku yanapaswa kuthibitisha kwamba tuna imani.—Yakobo 2:26.

7 Pia Yehova anataka wale wanaosali, wafanye hivyo kwa unyenyekevu na unyoofu. Tuna kila sababu ya kuwa wanyenyekevu tunapozungumza na Yehova, sivyo? Kwa kawaida, watu huzungumza na mfalme au rais, kwa heshima, wakitambua cheo chake cha juu. Basi, tunapaswa kumheshimu Yehova hata zaidi tunapozungumza naye. (Zaburi 138:6) Kwa kweli, yeye ni “Mungu Mweza-Yote.” (Mwanzo 17:1) Tunaposali kwa Mungu, tunapaswa kumfikia kwa njia inayoonyesha kwamba tunatambua kwa unyenyekevu hali yetu mbele zake. Unyenyekevu huo utatuchochea kusali kwa unyoofu kutoka moyoni mwetu, na kuepuka sala za kidesturi au za kurudia-rudia.—Mathayo 6:7, 8.

8 Ikiwa tunataka Mungu atusikilize, tunapaswa kutenda kulingana na sala zetu. Yehova anatarajia tujitahidi kadiri ya uwezo wetu kutenda kulingana na sala zetu. Kwa mfano, tukisali “Utupe leo mkate wetu kwa ajili ya siku hii,” ni lazima tufanye kwa bidii kazi yoyote tunayoweza kufanya. (Mathayo 6:11; 2 Wathesalonike 3:10) Tukisali atusaidie kushinda udhaifu fulani wa kimwili, ni lazima tuwe waangalifu na kuepuka mambo au hali zinazoweza kututia majaribuni. (Wakolosai 3:5) Mbali na matakwa hayo muhimu, kuna maswali kuhusu sala ambayo tungependa kujibiwa.
KUJIBU MASWALI FULANI KUHUSU SALA

9 Tunapaswa kusali kwa nani? Yesu aliwafundisha wafuasi wake wasali kwa ‘Baba yetu aliye mbinguni.’ (Mathayo 6:9) Hivyo, sala zetu zinapaswa kuelekezwa kwa Yehova Mungu peke yake. Hata hivyo, Yehova anataka tutambue cheo cha Mwana wake mzaliwa wa pekee, Yesu Kristo. Kama tulivyojifunza katika Sura ya 5, Yesu alitumwa duniani ili awe fidia na kutukomboa kutoka katika dhambi na kifo. (Yohana 3:16; Waroma 5:12) Yeye ndiye Kuhani Mkuu na Hakimu aliyewekwa rasmi. (Yohana 5:22; Waebrania 6:20) Hivyo, Maandiko yanatuagiza tutoe sala zetu kupitia Yesu. Yeye mwenyewe alisema: “Mimi ndiye njia na kweli na uzima. Hakuna anayekuja kwa Baba ila kupitia kwangu.” (Yohana 14:6) Ili sala zetu zisikiwe, ni lazima tusali kwa Yehova tu kupitia Mwanaye.

Yasinta Ngonyani said...

Rachel"kachiki"!
Mwal.NN Mhango na
kaka Ray Ahsante sana kwa kuwa nami jumapili hii. Mbarikiwe sana.