Saturday, November 7, 2009

MAISHA NI KURIDHIKA NA ULICHONACHO!!!!

Hapa wakati ni kikongwe!

Sio lazima kuendesha Mercedes, Land Rove, X6 au Hummaer ili kujiona wa maana. Watu wenye furaha sio muhimu kuwa na kila kitu kizuri. Tufurahie kile (kitu )tulichonacho.
!!!!!!!!JUMAMOSI NJEMA JAMANI!!!!!

Thursday, November 5, 2009

DAWA YA MAPENZI.......... HADITHI.!!!!!

Palitokea Mwanamke, aliyekuwa ametolewa, akashindwa kuishi vizuri na mumewe. Kwa hivyo mumewe hakuridhika naye akaamua atafute mwanamke atayemfaa zaidi, aishi naye. Kwa wivu, yule mke wa kwanza, akatafuta dawa ya kuweza kumrudisha mume wake. Akatafuta dawa aina nne. Aina ya kwanza, ilikuwa ya kujipaka mwilini, aina ya pili, ya kutilia yule mawanaume kwenye chakula, aina ya tatu, ilikuwa ya kuoganayo, aina ya nne, ilikuwa ya kuchoma kwa moto. Hizo dawa aliamini zitamfanya mume wake, amwache mke wa pili, na kwamba mapenzi yao yataongezeka, kwa hivyo wataishi pamoja tena. Baada ya kuzipata dawa hizo na kuzitumia kikamilifu, bado hali ikawa ile ile, hakuna lililobadilika. Mumewe akaendelea kuishi na mkewe wa pili.

Yule mke wa kwanza, akaenda kwa bibi kizeemmoja ambaye alisifiwa kuwa mganga hodari akamwomba amsaidie. Bibi kizee hakusita akamwambia akatafute ubongo wa Fisi, yaani akamuue Fisi ampasue na kuuleta ubongo ukiwa bado mzima! Ubongo huo, ndio utatumika kutengenezea dawa ya mapenzi.

Mwanamke akarudi nyumbani akaanza kufikiria jinsi atakavyomtega Fisi na kumuua. Akapata wazo la kununua nyama na kuikata vipande, kuviweka njiani ambapo fisi hupendelea kupita mara kwa mara. Kesho yake akakuta ule mtego mtupu, na nyama imeliwa. Akanunua nyama kwa wingi akaiweka toka pale alipotega jana yake njiani pote mpaka nyumbani kwake. Fisi walipofika, kwa uroho na ujinga wao kana tunavyowafahamu, wakaanza jula vile vipande vya nyama mpaka ndani ya nyumba ya yule mwanamke. Akamkuta yule mwanamama amejitayarisha vizuri na shoka. Kwa nguvu zake zote. Akampiga kipigo kimoja tu na yule Fisi akafa hapo hapo. Akampasua kicwani akatoa ubongo, na akaenda nao kwa bibi kizee mganga.

Alipofika, bibi kizee akauliza: “Mwanangu, umeniletea ile dawa niliyokutumia?” Mwanamama akajibu. “Ndiyo mama, lakini nimeipata kwa shida sana!” Akamkabidhi bibi kizee ule ubongo wa Fidi. Alipokwisha upokea akakaa kitako akafikiri sana. Halafu akasema: “Mwanangu, sasa nitakueleza kila kitu vizuri sana umetumie akili na ujuzi mwingi, kutega Fisi na kumwua. Sasa nenda ukatumie akili na ujuzi wako wotw ulionao, ili uweze kupata mapenzi ya mumeo, ili uweze kupata mapenzi ya mumeo tena. Nina maanisha kusema, lazima uwe msafi, uvae vizuri na upikie chakula kizuri mume wako. Vile vile, jaribu kujipendezesha kwa mume wako kwa kila hali. Utaona mumeo anarudi nyumbani na kumuacha mke aliyekuwa naye sasa hivi, na mataishi kwa amani na furaha.

Aliporudi nyumbani, akafanya, yote aliyoambiwa na yule bibi kizee. Haukupita muda, mumewe akamfukuza mke wa pili na akarudi nyumbani kwa mke wake wa kwanza. Wakaishi vyema kwa mika mingi sana mpaka vifo vikawatengenisha.

FUNDISHO:- Inaaminika kuwa, watu wanapoishindwa kuishi pamoja katika ndoa, hutumia dawa za kienyeji kwa sababu ya kusitawisha maisha yao.

Wapo akian mama wengi amabao wanaamini kabisa kwamba kuna dawa ya mapenzi.
Lakini ukweli ni kwamba, dawa ya mapenzi ni moja tu nayo ni: Kuhakikisha kwamba, kina mama wanaheshimu ndoa zao na kutii waume zao. Nyumba yenye mapenzi, inamfanya mume apende kukaa nyumbani, na asitembee tembee ovyo.

Nimeitoa katika kitabu cha HADITHI na visa kutoka Tanzania.

Wednesday, November 4, 2009

KARIBUNI KANDA YA KUSINI TUCHEZE MGANDA-RUVUMA/SONGEA



Kama unatamani nyumbani fanya kama mimi sikiliza ngoma za asili na ikibidi cheza pia, haya karibu tuungane kwa ngoma hii ya mganda.

MWANAUME WA MIAKA 112 AMUOA BINTI WA MIAKA 17

Umri ni namba tu!!
Mamia ya watu walihudhuria sherehe za harusi ya mzee Ahmed Muhamed Dore mwenye miaka 112 akiaoana na binti aitwaye Safia Adulleh mwenye miaka 17.
“Leo Mungu ameniwezesha kufikia ndoto yangu” alisema mzee Ahmed Muhamed Dore baada ya kuoana na binti mbichi kabisa kutoka maeneo ya Galguud huko katikati ya Somalia.

Mambo yanayovutia kuhusu hii ndoa
Wanafamilia wa binti wanasema binti yao amefurahi kupata mume.
Bwana harusi alikuwa anasubiri kwa karibu zaidi binti aendelea kukua hadi amshauri waoane bila kumlazimisha bali kumvutia kwa upendo ili waoane.
Ni ndoa ya aina yake kwenye eneo ya Horn of Africa kwa babu miaka 112 kuoana na binti wa miaka 17.
Wapo watu ambao hawaridhiki na tofauti ya umri ingawa katika sheria za kiislamu inaruhusiwa.
Wapo waliofurahi na kukiri kwamba umri si kizuizi linapokuja suala la ndoa na kupendana.
Bwana harusi tayari ana watoto na wajukuu 114 huku kijana wake wa kwanza akiwa na miaka 80.
Bado anaamini huyu mke mpya ataendelea kumzalia watoto.
Zaidi anakiri kwamba ni Baraka sana kuwa na mtu unayempenda na akaendelea kukutunza.

Soma zaidi BBC

Tuesday, November 3, 2009

KITABU CHA MAISHA NA MAFANIKIO......

SEHEMU YA PILI...................

Huwezi kuwa kamili bila mwingine kukamilika

Sisi kama binadamu tunajipenda na hakuna awezaye kulizuia jambo hili. Lakini kujipenda kwa ziada kunaweza kuzuilika kama mtu ataamua. Kujipenda kwa ziada ndiko ambako kunapelekea dunia kuwa kama ilivyo leo kwa upande wa uharibifu. Yale yote ambayo hayakwenda sawa kufuatana na mpango wa Mungu yamesababishwa na uziada wa kujipenda kwa binadamu, Mpango wa Mungu ni kuwa na dunia ambayo haina makovu wala vidonda. Lakini dunia hii tunamoishi imejaa vidonda na makovu zaidi kuliko uzima. Vidonda na makovu haya, kama ambavyo tumesema ni matokeo ya binadamu kujipenda kupita kiasi, kujipenda ambako kunamfanya adhani kwamba yeye anastahili zaidi kuliko mwingine na kumfanya awe pia mvivu wa kufikiri.

Ni binadamu wachache sana ambao wako tayari kukaa chini na kujiuliza kama kweli wana tofauti na wengine. Ni wachache kwa sababu kila mmoja anaamini kwamba ni taofauti na mweingine, iwe ni kwa mwenye mali au asio nayo, iwe ni kwa mwanamke au mwanaume, au kwa msomi au asiyesoma, kila mmoja anaamini kwamba ana tofauti na mwingine. Anashindwa binadamu kujua kwamba, yeye kama binadamu hana tofauti na binadamu mwingine.

Labda tukumbushane kwamba binadamu hawi binadamu kwa sababu ana magari makubwa mia moja au ana nyumba za fahari mji mzima, lakini pia hawi binadamu kwasababu anashinda na kulala na njaa au anatembea makalio yakiwa nje kwa ulitima (Umaskini). Binadamu anakuwa binadamu kwa sababu kuna sifa ambazo hupatikana kwake na kwa mwingine bila kujali huyo mwingine yukoje kimwili na kihali.

Kushindwa huku ndiko ambako huwafanya binadamu kuwapa wenzao kile ambacho kama wengepewa wao kungezuka balaa kubwa. Binadamu wamekuwa wakijaribu kuridhisha miili yao na pengine nafsi kama siyo tamaa zao kwa kuwafanyia wengine lile ambalo kwao lingekuwa ni gumu sana kulivumilia.

Leo hii kuna binadamu ambao kwa kujali fedha wanauza sumu kwa binadamu wenzao. Kwa kutaka fedha huuza vyakula ambavyo wanajua wazi kwamba, vitawashuru afya za wengine na kuwauwa. Wanauza vyakula hivyo wakiwa na uhakika kwamb, baada ya muda fulani, hao waliouziwa wataugua kansa au maradhi mengine hadi kufa. Lakini ni wazi wao wasingekubali kufanyiwa jambo hilo.

Kuna wale ambao kwa matumizi ya vyeo vyao huwakosesha wengine haki zao kwa sababu tu wengine hao hawana nguvu na uwezo wa kupambana nao. Hawa kwa makusudi huwafanya watu wengi kuishi katika ulitima wa kudumu wakati wangeweza kuinuka na kuishi kama wao.

Kuna kundi kubwa la binadamu ambalo kamwe halijawahi kufanya jema kwa wengine, halijawahi kutamka jema kwa wengine na halijawahi kufikiria jema kwa wengine. Kundi hili lina watu ambao wao kila siku wanafikiria ni kwa namna gani watatumia ujinga wa wengine kwa manufaa yao, ujinga wa wengine kwa kujupatia ziada na “kutanua” huku wengine hao wakiporomoka na kuingia kwenye shimo la kiza cha ukosefu na majuto.

Umefika wakati ambapo inabidi tuanze kuhushimu nguvu za maumbile, inabidi tuanze kuhushimu ubinadamu katika ujumla wake. Inabidi tujue kwamba kinachotufanya tusimame leo na kujidai, kujuvuna na kujiona tu bora sana ni kwa sababu kuna banadamu wengine wanaotuzunguka. Kinachotufanya leo hii tutamani kuonekana wakubwa zaidi, wenye uwezo zaidi na wenye heshima zaidi ni kuwepo kwa binadamu hata kidogo kama tunavyodhani, bila binadamu wengine kuwepo.

Mbaya zaidi ni kwamba, sisi siyo binadamu kamili kama wenzetu siyo kamili. Ukamilifu wao ndiyo unatupa sisi ukamilifu. Ukitaka kuthibitisha jambo hili unaweza, kwani ni rahisi sana. Hebu anza sasa kutenda yale ambayo hata wewe ungependa kutendewa na kuacha kuwatenda wengine yale ambayo hata wewe usingependa kutendwa. Tuna uhakika baada ya muda fulani utagundua ukweli fulani na bila shaka utawasiliana nasi kutufahamisha. Hutapoteza chochote kufanya jaribio hilo bila shaka.
MWISHO.......
Makala hii nimeichukua kutoka kwenye kitabu cha Maisha na Mafanikio kilichoandikwa na Hayati Munga Tehenan ambaye alikuwa ni Mwalimu mzuri wa maarifa ya Utambuzi akitoa elimu hiyo kupitia magazeti yake ya Jitambue, vitabu na semina zake nchini Tanzania kabla ya kufariki dunia.

Monday, November 2, 2009

KITABU CHA MAISHA NA MAFANIKIO......

SEHEMU YA KWANZA...........

Kila binadamu anajipenda, ingawa wengine hujipenda zaidi kiasi kwamba hujiona wao wenyewe tu, kama kwamba wako peke yao hapa duniani. Kwa kujipenda kwao sana, wengi huingia mahali ambapo huamini kuwa matatizo na shida zao maishani ni matokeo ya wale wanaowaita adui zao wa aina mbalimbali. Kwa kujipenda kwao zaidi husahau kabisa kwamba bila wengine kuwepo na kukamilika, wao pia siyo kamili. Mada hii inaelezea namna ambavyo adui wa watu wengi ni watu hao wenyewe na siyo wengine na inafafanua kuhusu ukamilifu wa binadamu usivyowezekana pale ambapo wengine hawajakamilika.

Mbu anapokuuma utapata malaria huwa unahesabu kama adui yako. Unaweza kutangaza kwa maringo na kujivuna kwamba uko kwenye kampeni ya kumuangamiza adui mbu ili uondokane na adha ya malaria. Lakini je, ni kweli mbu ndiye adui yako?

Siku hizi kuna virusi vya HIV ambavyo vinahesabiwa kama maadui wa watu wote. Kila kona hapa duniani kuna juhudi za kila aina katika kupambana na virusi hivi. Ukimuuliza mtu atakwambia, virusi hawa ndiyo adui zetu katika suala la maradhi haya, lakini je, kuna ukweli wowote katika hili? Kila mtu anafahamu vizuri mazingira ya aina mbalimbali ambao kwake huyaita adui, kila mtu anawafahamu watu wa aina mbalimbali kwake kwa sababu mbalimbali anawaita adui zake na kila mtu anafahamu vizuri vitu fulani maalum ambavyo kwa sababu fulani anaviita na kuamini kwamba ni adui zake.

Lakini huenda hakuna ambaye anajua ni kiasi gani tabia, mienendo na mawazo yake ni adui zake wakubwa. Ni mara chache sana na ni watu wachache sana ambao wako tayari kujiuliza na kukiri kwamba, tabia mienendo na mawazo yao kwa kiasi kikubwa sana huwa vinawadhuru na kuwaumiza, kuwaharibia mipango yao na maisha kwa ujumla, kuliko wanavyodhani kwamba athari hizo hutoka nje yao.

Ni wachache kwa sababu, binadamu hujipenda sana kiasi ambacho huogopakufunua macho zaidi na kuukabili udhaifu alionao. Ukweli ni kwamba, kama mtu atataka kuishi bila kujidanganya, atagundua kuwa hata mbu na virusi wa ukimwa siyo adui zetu atagundua kuwa kwamba, tabia mienendo na mawazo yetu ndiyo adui zetu. Kama mtu ataamua kujikinga dhidi ya mambo yote yanayoweza kumwambukiza virusi wa ukimwi au kuishi katika mazingira ya mbu wengi na kuchukua tahadhari dhidi ya wadudu hao, anakuwa amemkwepa kwa karibu asilimia tisini huyu au hawa anaowaita adui zake.

Kila siku, hata pale ambapo tunatangaza kamba akina fulani ni adui zetu, huwa tunafanya hivyo kwa makosa kwa sababu tu ya kujipenda na hivyo kujipendelea katika kuutazama ukweli. Tunapofilisika tunajitahidi sana kutafuta maadui wa hali hiyo, huku tukiwa tumesahau kwamba tabia zetu ndizo zinazotufilisi. Tunaposhindwa kupata tunachokitafuta maishani, hatuzitazami tabia, mitazamo,mienendo, imani na mawazo yetu, bali tunatazama nje yetu ili kumpata adui. Ilivyo ni kwamba, kama tunatafuta adui, kwa sababu tunataka kumpata ni lazima tutampata. Hivyo tukishampata tutaamini kabisa kwamba huyu ni adui yetu na kuziweka nguvu zetu hapo kujaribu kupambana naye.

Inachukua muda, na wakati huo tunakuwa tumechelewa sana tunapokuja kugundua kwamba tuliyemdhani ni adui alikuwa ndani mwetu. Lakini kwa bahati mbaya sana ni kwamba huwa hatufanikiwi kungámua kwamba huyu tunadhani ni adui yetu siyo adui yetu. Kwa hali hiyo, huwa tunaishi katika katika dhiki, misukosuko na nuksi zisizokwisha tukijaribu kupambana na adui ambaye siye, huku adui yetu akiwa ni sisi wenyewe. Kupigana huku na adui asiyekuwepo popote bali ndani mwetu huweza hata kutupotezea maisha yetu. Kwa nini basi kabla hatujatangaza au kudhani fulani ndiye adui yetu, tusitazame au kuzigundua kwanza tabia zetu, mienendo, imani, na mawazo yetu? Wanasema wataalamu wa nyanja zote za kimaisha katika nadharia zao nyingi kuhusu maisha kwamba, adui wa mtu ni mtu mwenyewe. Tulitafakari hilo kwa makini.

Tusipolitazama kwa makini tutajikuta kila siku tukizidi kuongeza idadi ya maadui huku hali zetu kielimu, kiuchumi na kijamii kwa ujumla zikizidi kudorora. Zitazidi kudorora kwa sababu yule tunayemdhani ni adui yetu atatupitezea muda wetu na kutusumbua sana, wakati adui yetu tunaye ndani mwetu na tunaweza kumuondoa kwa saa kadhaa tu kama tutamgundua.

Kwa nini huwa ni vigumu kwetu kmjua au kumgundua adui yetu pale mambo yetu yanaposhindwa kwenda kama tulivyotarajia au kutaka? Ni kwa sababu tumefundishwa na mazoea kwamba sisi ni vitu vilivyo nje yetu na hivyo, kusimama au kuanguka katika maisha yetu hutegemea wengine na mazingira ya nje yetu. Tunapopata fedha na kuzitumia vibaya, hatujikagui na kujiuliza kama chanzo cha kufikia hatua hiyo siyo sisi wenyewe, bali tunaanza kuwaambia wake zetu kwamba wana nuksi au kuwasingizia jirani zetu kwamba wametuendea kwa waganga kutuharibia bahati zetu.

Tunapotoka nje kwenye ndoa zetu na kufanya uzinzi, hatuko tayari kujikagua ili kuuona ukweli, bali tunachoweza kufanya ni kuwasingizia wake au waume zetu kwamba wao ndiyo chanzo kwa sababu hawatujali, kwa sababu ni dhaifu wa tendo la ndoa au kwa sababu hawana fedha. Ni vigumu kwetu kujiuliza kama sisi siyo chanzo au kujiuliza mchango wetu kwenye suala zima. Tunajipenda sana na kuamini kwamba sisi ni watu nav itu vinavyotuzunguka.

Tunapopoteza kazi zetu hatujikagui kama sisi wenyewe hatukuchangia kufukuzwa huko, kwani adui zetu siku zote wako nje yetu na ni lazima tutawatafuta. Tunaweza kumnyooshea kidole cha lawama bosi wetu au walio chini yetu, tunaweza kudai kwamba ni jirani au ndugu zetu ambao ati siku zote hawakuwa wakifurahia mafanikio yetu. Ndiyo ubaya wa kujipenda na kuamini kwamba adui zetu wako nje yetu na ni lazima kila linalokwenda kinyume na matarajio yetu liwe limesababishwa na watu hao au mazingira hayo. Umefika wakati ambapo inabidi tubadilike sana na kuanza kuujua ukweli kwamba sisi ndiyo waamuzi na waendeshaji wa maisha yetu.Kila linalotutokea ni matokeo ya tabia, mienendo na mawazo yetu.

Makala hii nimeichukua kutoka kwenye kitabu cha Maisha na Mafanikio kilichoandikwa na Hayati Munga Tehenan ambaye alikuwa ni Mwalimu mzuri wa maarifa ya Utambuzi akitoa elimu hiyo kupitia magazeti yake ya Jitambue, vitabu na semina zake nchini Tanzania kabla ya kufariki dunia.

ITAENDELEA...............

Saturday, October 31, 2009

MUZIKI NI MOJA YA STAREHE KATIKA MAISHA


JUMAMOSI NJEMA KWA WOTE KUMBUKENI SIO UGIMBI/ULANZI MWINGI:-)!!!!!

Friday, October 30, 2009

WIKI ILIYOPITA TULIONA MAJINA TUWAITAYO WATOTO WETU:- NGOJA LEO TUANGALIA MAJINA YA UBINI(VIB0NGO) TULIYONAYO!!

Hivi haya majina ya ukoo/ubini(vibongo) alianza kupata nani wanadamu, wanyama au ndege?

Ninekuwa nikijiuliza hili swali na nimewauliza watu wengi hivi haya majina tuliyonayo nani alianza kupata/kuitwa? Yaani kwa mfano:-Ngonyani, Nguruwe, Nyati, Tembo, Komba, Mwaipopo, Sungura, Soko, Mapunda, nyoka, kunguru, Mbawala, Kifaru. Tujadili pamoja......

Thursday, October 29, 2009

KUPOTEA KWA SIKU CHACHE + JIBU KWA DA MIJA KUHUSU PICHA HII HAPA CHINI!!!!

Kwanza kabisa napenda kuwataka wote radhi kwa kupotea kwa siku hizi chache. Ila sasa nimerudi tena na TUPO PAMOJA.
Pili napenda kumjibu Da Mija swali lake "Yasinta ile picha yako pale juu kabisa katikati uliipiga lini? naizimia sana." Jibu ni hili Da mija nilipiga mwaka 1992 nikiwa Wilima Sec. huko Madaba-Matetereka. Natumaini nimejibu kama ulivyotegemea dadangu.

Dada Subi:- Kutangaza mabadiliko ya tovuti

Naomba nafasi katika blogu yako kuwataarifu wasomaji kuwa tovuti ya mpya ya wavuti.com imechukua nafasi ya iliyokuwa nukta77.com na nukta77.blogspot.comNaomba yeyote aliyekuwa ameweka linki ya nukta77 aihariri na kuweka wavuti.com
Karibuni sana kutembelea kwa taarifa za nafasi za masomo na kazi kwa burudani na bila kusahau habari na porojo!Asanteni.wavuti.com

Sunday, October 25, 2009

JUMAPILI NJEMA WANDUGU:- LEO NI DOMINIKA YA 30 YA MWAKA B!!!!!!

Kuwa na furaha sio kuwa na mali mengi. Isipokuwa ni kupenda/kupendwa na kuwa na tumaini/matumaini!!!

KRISTU..........TUMAINI LETU

Friday, October 23, 2009

BARUA KUTOKA SWEDEN: Hatujiamini, tutaendelea kutawaliwa na wazungu

Baada ya kuisoma barua hii nimeona si mbaya kama nikiiweka hapa ili wengi waisome na na tujadili kwa pamoja.

KUJIAMINI ni jambo la maana sana katika maisha ya kila siku ya mwanadamu. Kujiamini katika kila uamuzi unaofanya na kila kitu unachofanya ndio siri kuu ya mafanikio ya mwanadamu yeyote. Bila kujiamini, hakuna chochote utakachofanikiwa na kila siku utakuwa 'mtumwa' wa wengine.

Kujiamini ni muhimu na chachu ya maendeleo si katika maisha ya mtu binafsi tu, bali hata katika taasisi kama vile serikali, mashirika ya umma na mashirika binafsi. Ili taasisi au shirika lolote liendelee, ni lazima kuongozwa na wataalamu waliobobea na wenye kujiamini kwa maamuzi na matendo.

Sababu kubwa ya nchi yetu kuendelea kuwa masikini ni kuwa na viongozi wasiojiamini na kuendekeza utegemezi hasa kwa wazungu.

Viongozi wetu bado wanaamini kuwa wazungu wanajua kila kitu kinachohusiana na nchi kupiga hatua mbele kimaendeleo. Wanaamini kuwa wazungu ndio wenye kujua mbinu na mikakati ya kufuta umaskini katika nchi yetu. Hawaamini kama Watanzania wana uwezo wa kujiendeleza wenyewe bila kutegemea usaidizi wa watu wa nje.

Viongozi wetu wanadanganyika kirahisi wanapoona nchi nyingi za Ulaya na Marekani zimeendelea, hivyo wanadhani kuwa wazungu ndio 'mwarobaini' wa matatizo yetu, ndio maana wakati wote wanajidhalilisha wao wenyewe na sisi wananchi wao kwa ujumla kwa kuwapigia magoti wazungu kuwaomba 'watuendeleze.'Wanaamini kuwa wao pekee (wazungu) ndio wenye akili hapa duniani, na sisi ni kama ‘misukule’ tu!

Kila kukicha viongozi wetu na Afrika kwa ujumla wanapishana katika nchi za Ulaya na Marekani kwenda kuomba misaada, wanaamini kuwa bila misaada hawawezi kuendesha nchi zao, wamekuwa akina 'Matonya,' wanatembeza kibakuli. Sijui wameona nani au nchi gani duniani iliyoendelea kwa kutegemea cha kuomba.

Viongozi wetu wanawaheshimu na kuwanyenyekea watawala wa Ulaya na Marekani kuliko hata wananchi tuliowaweka madarakani, wanakubali kila wanaloambiwa na ‘mabwana wakubwa'hawa.

Kwa mfano, wakati ule walipoambiwa wayabinafsishe (wayauze) mashirika na makampuni yote ya umma kwa hoja eti serikali haiwezi kufanya kazi mbili, yaani kuongoza nchi na wakati huo huo kufanya biashara, walikubaliana na ushauri huo bila hata ya kuhoji au kuja kwa wananchi kutuuliza maoni yetu, wakaanza kuuza mali zetu moja baada ya nyingine, na walipomaliza kuuza hawakuja kutuambia wamepata kiasi gani cha fedha.

Lakini ukiwauliza leo kama tumeendelea baada ya kuuza mashirika na makampuni ya umma? Hawatakujibu kitu, watabaki wanakutolea macho tu ingawa jibu wanalo, lakini wanapata kigugumizi kulisema kwa sababu wanaona haya kwa kuwa walitapeliwa au waliingizwa mjini na wazungu.

Tazama, wakati huu wa tatizo la kiuchumi lililowakuta wazungu hawa hawa ambao tunawaamini kuwa ‘waganga’ wa matatizo yetu ya kiuchumi, wakati makampuni yao mengi yakifilisika, wanakimbilia hazina za serikali zao na kuchota mabilioni ya dola, pauni na euro za umma ili kuyaokoa, wanadai wanalinda nafasi za kazi kwa raia wao, sisi makampuni na mashirika yetu yalipotetereka, wakatuambia tuyabinafsishe (tuwauzie wao).

Tatizo letu kubwa ni kutojiamini. Na hili halipo kwa viongozi wetu tu, bali pia kwa wananchi wa kawaida. Wengi wetu tunaamini kuwa mzungu ni mweledi kuliko sisi, hatujui kuwa wazungu wengi ni mbumbumbu wa masuala mengi tu kuliko waswahili.

Ninachojaribu kusisitiza hapa ni Watanzania na Waafrika kwa ujumla kujitambua na kujiamini kuwa tunaweza kufanya mambo makubwa kuliko hata wazungu, katika kila nyanja ya maisha ya mwanadamu, iwe ni kiuchumi, kisayansi na hata kiteknolojia.

Ipo mifano hai ya nchi zilizokuwa taabani kiuchumi na kijamii kuliko hata sisi, lakini kwa kuwa walijitambua na kujiamini, walichukua hatua ambazo leo zinawafanya kuwa tishio dhidi ya wazungu waliotangulia kupata maendeleo ya kiuchumi, kisayansi na kiteknolojia.

Nchi kama vile China na India ni mfano wa kuigwa na nchi nyingine zinazoendelea. Wachina kwa sasa ndio tishio pekee dhidi ya Marekani kiuchumi, na wakati huu wa mparaganyiko wa uchumi katika Marekani na Ulaya, China imetwaa uongozi wa uchumi duniani na inalitumia kikamilifu tatizo hili kukwea katika kilele na kuipiku Marekani. Wachina pia hawako nyuma katika maendeleo ya sayansi na teknolojia.

Mwasisi wa Taifa letu, hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius K. Nyerere, alikuwa kiongozi pekee wa nchi hii aliyekuwa na nia na maono ya dhati ya kujinasua kutoka katika minyororo ya ukoloni wa wazungu.

Mwalimu alitaka Tanzania ijitegemee kwa kila kitu, ndio maana alianzisha siasa ya Ujamaa na Kujitegemea, ambamo Watanzania tulishuhudia viwanda vya huduma mbalimbali vikijengwa nchi nzima.

Mtazamo wa mbali wa Mwalimu ulikuwa kuhakikisha kuwa ifike wakati Tanzania iwe na ‘viwanda-mama,’ yaani viwanda vya kuzalisha malighafi kwa ajili ya viwanda vingine, haya yalikuwa malengo thabiti ya kujitegemea.

Mwalimu alifanikiwa kwa sababu alikuwa kiongozi mwenye kujitambua na anayejiamini, na alitaka pia Watanzania wote wajitambue na kujiamini. Lakini kwa bahati mbaya waliompokea wawakuliona hilo.

Ndio maana miaka 24 imepita sasa tangu Mwalimu ang'atuke uongozi, lakini hakuna chochote walichoongeza, zaidi ya kuuza kila kitu tulichokuwa nacho na kujaribu kufisidi hata kile kidogo tulichobaki nacho.

Kwahiyo, kama kweli tunataka kuwa taifa huru na kukomesha ukoloni wa wazungu, hatuna budi kuchukua hatua sasa. Viongozi tuliowapa dhamana ya kutuongoza wanapaswa kutuongoza katika jitihada hizo za kujikomboa, vinginevyo tutaendelea kutawaliwa na wazungu

Na George Maziku, Sundsvall, Sweden toka gazeti la mwananchi

Thursday, October 22, 2009

NIMEUTAMANI KWELI MLO HUU/NAKUMBUKA MBALI NYASA!!!!!


Yaani hapa roho inauma kweli , nakula kwa kuingalia picha hii, basi tu sijui mwenzangu nanyi hivyohivyo. Mbaya zaidi hapa unga siku hizi haupatikani Sijui nijaribu kupika ugali na unga gani? Ok karibuni basi tule msosi tayari.



NGOJA LEO TUANGALIE BAADHI YA METHALI ZETU KUANZIA A MPAKA Z

  1. A. Akili ni nywele, kila mtu ana zake.
    Asiyefunza na mamaye, hufunzwa na Ulimwengu.
  2. B. Baada ya dhiki, faraja.
    Bendera hufuata upepo.
  3. C. Chema chajiuza, kibaya chajitembeza.
    Cheruru – Si ndo! Ndo! Ndo!.
  4. D. Damu nzito kuliko maji.
    Dawa ya moto ni moto.
  5. F. Fumbo mfumbie mjinga, mwerevu hulingámua.
    Fimbo iliyo mkononi, ndiyo iuayo nyoka.
  6. G. Ganda la mua la jana, chungu kaona kivuno.
    Gonga gogo usikilize mlio wake.
  7. H. Hapana siri ya watu wawili.
    Heri kujikwaa dole kuliko kujikwaa ulimi.
  8. I. Ikiwa hujui kufa tazama kaburi
    Iliyopita si ndwele, ganga ijayo.
  9. J. Jogoo la shamba haliwiki mjini.
    Jungu kuu halikosi ukoko.
  10. K. Kulea mimba si kazi, kazi kulea mwana.
    Kinyozi hajinyoi na akijinyoa hujikata.
  11. L. Lisemwalo lipo:- Ikiwa halipo, lipo nyuma linakuja.
    Lisilokuwepo moyoni halipo machoni.
  12. M. Mcheka kilema hafi bila kumfika
    Mficha uchi hazai.
  13. N. Nnzi kufa juu ya kidonda si haramu.
    Ndugu wakigombana, chukua jembe ukalime, wakipatana chukua kapu ukavune.
  14. P. Penye uermbo ndipo penye urimbo.
    Penye mafundi hapakosi wanafunzi.
  15. R. Radhi ni bora kuliko mali.
  16. S. Siku utakayokwenda uchi, ndiyo siku utayokytana na mkweo.
    Sumu ya neno ni neno.
  17. T. Tamaa mbele, mauti nyuma.
    Tonga si tuwi.
  18. U. Ukitaka kula nguruwe, chagua aliyenona.
    Ulipendalo hupati, hupata ujaliwalo.
  19. V. Vikombe vikikaa pamoja havina budi kugongana.
    Vita vya panzi ni furaha ya kunguru.
  20. W. Wema hauozi.
    Werevu mwingi mbele kiza.
  21. Y. Yaliyopita si ndwele, tugange yaliyomo na yajayo.
    Yote yangáayo usidhani ni adhabu.
  22. Z. Zimwi likujualo, halikuli likakwisha.

Wednesday, October 21, 2009

HONGERA KWA SIKU YA KUZALIWA KAKA,MJOMBA,SHEMEJI NA RAFIKI PIA JAMAA YETU!!


Hapa ni Mikumi 2005!!
Imefika siku nyingine tena, ya kumpongeza kaka yangu mwingine siku yako ya kuzaliwa. Najionea fahari sana kuwa na kaka wengi. Huyu ni kakangu wa tano kuzaliwa na leo ametimiza miaka makumi matatu na kidogo!!!!!






HONGERA KAKA SELAFIM KWA SIKU HII MAALUMU KWAKO UWE NA WAKATI MZURI.

Tuesday, October 20, 2009

KWA NINI TUNAWAPA WATOTO WETU MAJINA KAMA HAYA????

Ni juzi tu nilikuwa naongea na rafiki mmoja kuhusu majina. Nimeona niandike machache na tujadili kwa pamoja:-

Majina yenyewe ni kama haya:- Matokeo, Maneno, Sikujua, Zawadi, Mashaka, Matatizo, Asante, Baraka, Wasiwasi, Sikudhani, Shida, Huzuni, Halimoja, Majuto, Bahati, Mapambano, Tuombe, Maombi, Tumaini, Masikitiko, Maua nk.
Na huku kwetu kusini yaani Songea (wangoni) wanawaita watoto majina kama haya wa kike Kachiki na wa kiume Kadoda. Maana ya majina haya angalia kwenye kamusi ya kingoni:-)

Monday, October 19, 2009

Salma: Kwa nini alifungiwa ndani kwa miaka 24?

Mlemavu wa viungo Salma Mkomwa

Mama yake asimulia kisa cha kupata ulemavu

SIMULIZI ya msichana Salma Mkomwa (26) wa Morogoro kufungiwa nyumbani kwao kwa miaka 24 bila kutoka ndani imewashtua wengi hasa baada ya kujitokeza kwenye vyombo vya habari kuomba msaada wa kumwezesha kujikwamua.
Wengi wamekuwa wakijiuliza kisa cha kufungiwa kwa msichana huyo mlemavu kwa kipindi chote hicho. Wapo waliowashutumu wazazi wake na wengine wakidhani kwamba walistahili kupewa elimu juu ya malezi ya mtoto wao badala ya shutuma, alimradi kila mtu alisema lake.
Ili kujua kisa na mkasa, nilifunga safari hadi Kijiji cha Kichangani, Morogoro anakoishi msichana huyo kujua kulikoni? Nilikutana na kuzungumza kwa kina na mama yake, Mwanangavia Sewa.
Alijibu swali la kwa nini alimfungia binti yake kwa miaka 24... "Hatukuwa na uwezo wa kufanya chochote na wala hatukujua hata pa kuanzia baada ya Salma kuanza matatizo haya. Sababu kubwa ni kwamba hali ilikuwa ngumu."
Baada ya majibu hayo, mama huyo alianza kueleza mambo ambayo anadhani ndiyo chanzo cha binti yake huyo ambaye ni mtoto wa pili kati ya sita aliojaaliwa kupata ulemavu huo.
Akiwa na mimba ya miezi tisa, alifunga safari ya kutoka hapo Morogoro kwenda Handeni, Tanga kwa ajili ya kujifungua. Anakumbuka hiyo ilikuwa mwaka 1982.
Wiki moja kabla ya kumpata mtoto huyo, alikwenda shambani kuvuna ndizi, baada ya kupata mkungu wake, alijitwisha tayari kwa safari ya kurudi nyumbani. Akiwa njiani alidondoka.
"Kama unavojua mambo ya kijijini nilijifungua kwa mkunga sikujifungulia hosipitali lakini mwanangu Salma alikuwa mzima kabisa" anasema na kuendelea:
"Lakini wiki moja baada ya kujifungua mtoto akawa analia kupita kiasi kuna kulia kwa mtoto kawaida lakini yeye alizidi hadi kuwashtua watu nyumbani. Tukampeleka Zahanati ya Mzindu, Handeni walipompima wakasema mtoto hana tatizo lolote, wakatupa vidonge lakini hali ilibaki vilevile."
"Baada ya mwezi mmoja miguu ilianza kuvimba usawa wa magoti. Ikabidi nifunge safari kurudi Morogoro na kwenda Hospitali ya Mkoa.
Nilipomfikisha akapigwa x-ray sehemu za magoti ili kujua tatizo. Majibu yakaonyesha kuwa sehemu hizo zimeachana na damu haitembei.
"Madaktari wakasema nimechelewa hawezi kunyooshwa tena mifupa imekomaa. Wakati huo alikuwa na umri wa mwezi mmoja. Nadhani hii yote imetokana na kutojifungulia hospitali labda tatizo lingeweza kujulikana mapema."
Baada ya majibu hayo ilirudi nyumbani. Hali ya Salma iliendelea kuwa mbaya. Aliishia kupewa dawa za kutuliza maumivu na kupunguza uvimbe uliokuwapo miguuni.
Alipofikisha miaka mitano alipata nafuu. Uvimbe ulikoma hata kulialia kulipungua. Wakati wote huo mikono yake haikuwa na tatizo hata kidogo lakini siku zilivyozidi kusonga nayo ikawa inajikunja pamoja na miguu.
"Madaktari walishindwa jinsi ya kufanya na hatukuweza hata kununua gari la kumsaidia ndiyo maana ilibidi akae tu ndani kwa muda wote huo."
Habari kuhusu Salma zilijulikana baada ya Taasisi ya Faraja Trust Fund ambayo inashughulika na watoto wanaoishi katika mazingira magumu kutembelea nyumbani kwao.
Hata hivyo, hawakuwa wamekwenda kwa ajili yake bali mdogo wake wa kiume ambaye amekataa kwenda shule akiwa darasa la tano.
"Ilikuwa kama ndoto na sitakuja kusahau siku ile ambayo alikuja mlezi kutoka Faraja ambaye alikuwa akishugulika na watoto ambao wanaishi katika mazingira magumu na wasiopenda shule akiwemo mdogo wangu ndipo akanikuta," anasema Salma.
"Siku alipokuja nilikuwa ndani. Aliniona lakini aliondoka bila kuniambia kitu chochote hadi mwaka 2006 alipokuja tena na mama Ligaya alinipiga picha na kuipeleka katika Kituo cha Faraja."
Alipelekwa katika kituo hicho na baada ya kufika huko, Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Dk Lucy Nkya kwa kushirikana na shirika hilo walimpokea na kumpatia baiskeli pamoja nyuzi sita kwa ajili ya kuanza kufuma kwa kuwa tayari alikuwa na ujuzi huo.
"Namshukuru Mungu picha hizo zilipokwenda huko zilipokewa na hatimaye nilipata baiskeli ambayo inanisaidia katika maisha yangu kwani siwezi kutembea bila ya baiskeli."
Katika kipindi alichokuwa ndani alikuwa akijifunza kushona kwa kutumia chelewa za ufagio kwani hakuwa na uwezo wa kununua sindano ya kufumia vitambaa.
"Ninaweza kufuma vifuko vya kuhifadhia simu na tai na namshukuru Mungu naviuza Sh2,000 na watu wananunua. Shirika (Faraja), lilinipeleka katika maonyesho ya Sabasaba na hapo watu mbalimbali walielewa nini ninachofanya. Niliuza bidhaa zangu na kupata Sh200,000 na kupata msingi wa kuuza mkaa."
Fedha zinazopatikana katika shughuli zake wakati mwingine humsaidia mama yake ambaye ni mfanyabiashara wa mbogamboga hasa anapokosa bidhaa.
Salma hawezi kutembea wala kutambaa na hiyo ni changamoto kubwa katika maisha yake kwani anapokosa mtu wa kumsogeza alipo hulazimika kubaki hapo alipo liwepo jua au mvua.
Anayo tamaa kubwa ya kupata elimu lakini anasema wazazi wake hawana uwezo wa kumpeleka shule. Anatamani angejitokeza msamaria mwema kumsaidia pengine hiyo ingekuwa sehemu ya kujikomboa kimaisha.
"Nitashukuru pia kama nitapata mahala pa kuishi kwani hapa mazingira ni magumu. Baba ana wake wawili wote wanakaa katika nyumba hii na ana watoto 14 ambao wanamtegemea baba huyo na nyumba hiyo hivyo."
"Naomba tu Mungu mama yangu asitangulie mbele za haki kwani nitapata shida lakini kama nina nyumba yangu kidogo afadhali nitaweza kujisitiri."
Mwanamke aliyemfichua msichana huyo ni Jalia Lupapulo ofisa wa kituo hicho cha faraja chenye makao yake Kihonda, Morogoro. Anaungana naye kuomba wasamaria wema wamsadia akisema hajawahi kusoma. Kituo hicho hivi sasa kipo katika mchakato wa kumtafutia mwalimu maalumu.
Baadhi ya wataalamu wa tiba ya mifupa wanasema kwamba tatizo Salma linaweza kutibika kwa kupunguza kiwango cha ulemavu alichonacho.
"Nikimuona naweza nikajua tatizo ni nini hata kama ana umri mkubwa anaweza akasaidiwa tatizo likapungua ama siyo kwisha kabisa," alisema daktari mmoja.
Na Mahija Mpera gazeti la mwananchi

Sunday, October 18, 2009

JUMAPILI NJEMA KWA WATU WOTE KATIKA DUNIA HII!!!!!

Maisha ya bwana wetu Yesu kristo

Saturday, October 17, 2009

JUMAMOSI NJEMA WOTE:- TUMSIKILIZE LAMECK dITTO NA WIMBO WIVU WA KUPENDA.

video

Mara nyingi mapenzi huambatana na wivu, ni kama mapacha. Nimeupenda msemo huu mapenzi bila wivu ni kama chai bila sukari (chai bila sukari wala kitafuno) Ili mapenzi yakolee, wivu lazima uwepo .

Friday, October 16, 2009

KUMUITA MKEO MAMA…AU MUMEO BABA KWELI….NI HAKI?


Ni kawaida sana kumsikia mke akimuita mume baba, au mume kumuita mke mama...jamani mbona yapo majina mengi ya kuitana kama vile mpenzi, kipenzi, habib, na mengine mengi. Na kama mna mtoto ndio rahisi zaidi yaani kumuita mama fulani au baba fulani. Ila si mama au baba. Mama anaheshima yake mambo yote unayoyafanya na mkeo kweli anastahili kuitwa mama??!...au unayoyafanya na mumeo unaweza muita mumeo baba???

Au hata majina ya ubatizo (ya kwanza) tuitane. Au kama kule kwetu kusini wanaitana vibongo yaani majina ya ukoo kama Na-Ngonyani, Na-Nyoni, Na-Komba nk. Na waBena/waHehe wao wanasema Sa au Se badala ya Na kwa hiyo itakuwa kwa wao. Sa-Mgaya, Sa-Mwageni, Sa-Mbilinyi kama kuna wabena na wahehe mnisaidie kama nimekosea. Na hiyo ya kuita Na na Sa ni kwa akina mama tu isije ukamwita mwanaume pia.

Pia sasa kuna mtindo wa kuwaita wazazi wetu babu na bibi yaani tunawita kama watoto wetu wanavyoita. Mara nyingi nimekuwa nawasikia watu wakisema ni bibi alipiga simu ukimuuliza bibi yako bado anaishi anasema hapana ni mama yangu lakini kwa vile watoto wanasema bibi /babu basi nami nasema hivyo. Na babu yako utamwitaje?
Naomba mnisaidie kufafanua hapo!!!!!!

TUSISAHAU UTAMADUNI WETU TINGATINGA (BATTIK) NI KAZI YA MIKONO YETU/NI UBUNIFU WETU

Hapa naona kazi zimezidi kidogo lakini tutafika tu.

Sisi ni wamoja tunatwanga

Na sisi pia tunatoka kuchota maji
Ni mapambo lakini pia yana maelezo yake kwa hiyo inakuwa raha katika nyumba kuwa na mapambo kama haya. NAPENDA KUWATAKIENI WOTE IJUMAA NJEMA KWA PICHA/TINGATINGA/BATIKI HIZI.
UKITAKA KUJUA MENGI USISITE KUULIZA.


Thursday, October 15, 2009

LAITI KAMA NINGEKUFAHAMU KABLA.........HADITHI YA KUFIKIRIKA

Miaka mitano iliyopita nilikuwa natafuta mke wa kumuoa ambaye angekuwa na sifa nizitakazo. Nilikuwa natafuta msichana mzuri wa wastani maana sikutaka kuoa mke mzuri kupindukia asije niua bure kwa presha na jakamoyo. Nilikuwa natafuta binti atakanikubali kama nilivyo na mapungufu yangu na mimi niliahidi kumkubali na mapungufu yake ili mradi asiwe ni mwenye tamaa ya kupenda sana pesa na mfujaji.
Awe na staha na anayeweza kukabiliana na hali yoyote, niwe nacho, nisiwe nacho au kwa kifupi tupendane kwa shida na raha.

Pamoja na sifa nyingine ndogo ndogo, lakini muhimu ni upendo na amani vitawale nyumbani kwangu.
Hatimaye nilimpata Binti Yasinaty, na kukutana kwetu kulikuwa ni kama muujiza, nakumbuka siku hiyo nilipanda daladala nikielekea kazini na kwa bahati kiti nilichokalia kilikuwa ni cha mwisho upande wa dirishani. Wakati nakaa nikahisi kukalia kitu kigumu, nilipopapasa ilikuwa ni simu mpya kabisa tena ya bei mbaya kama sikosei wakati huo ilikuwa inauzwa shilingi laki nne kwa wakati huo, kumbuka kwamba hapa nazungumzia habari ya miaka mitano iliyopita.

Kwa bahati mbaya simu ile ilikuwa imezimwa, na nilipojaribu kuiwasha iliwaka na kuzima kuashiria kwamba betri yake iliisha chaji. Niliiweka mfukoni na kujiuliza kuwa ile simu ilikuwa ni ya nani, sikusikia mtu kulalamika kwamba amepoteza simu na niliogopa kuuliza maana nilichelea mtu kujitokeza na kusema kwamba ni yake ilihali sio yakwake.

Nilifika ofisini na kuanza kazi, baadae nilimuita katibu muhtasi wangu na kumwomba anisaidie kutafuta chaji ya ile simu kwa kuwauliza wafanyakazi pale ofisini, nilikuwa na shauku ya kumfahamu mwenye simu ile ili nimrudishie, kwani nilikuwa namuoana dhahiri akisikitika kwa kupotelewa na simu yake, kwa jinsi ilivyoonekana ilikuwa bado ilikuwa ni mpya kabisa na ilikuwa haijatumika zaidi ya wiki.

Katibu wangu muhtasi hakufanikiwa kuipata ile chaja ya ile simu. Niliweka ile simu kwenye droo ya ofisini kwangu ili jioni nikitoka nipitie nayo kariakoo ninunue chaja yake.
Ilipofika jioni alikuja mchumba wangu ambaye tulitofautiana wiki iliyopita na kuamua kutengana naye. Sikutaka kuonana naye na nilimwambia katibu wangu muhtasi amwambie kuwa niko bize na sitaki afike tena pale ofisini kwangu.

Ukweli ni kwamba nilimpenda sana lakini kitendo chake cha kukuta mwanaume mwingine chumbani kwake tena akiwa amelala kitandani kwake halafu anajidai kunidanganya kuwa eti ni binamu yake hakikunifurahisha kabisa. Nakumbuka nilisafiri kikazi kwenda Mbeya, na ilikuwa nikae kule kwa wiki moja, lakini ilitokea dharura huku Makao makuu Dar ikabidi nirudi baada ya siku mbili tu na nilipofika kwa kuwa ilikuwa ni usiku kama saa mbili niliamua kupitia kwa mchumba wangu ambaye alikuwa akiishi Mwengeili kupata chakula cha jioni kabla sijaenda kwangu Maeneo ya Sinza. Nilipofika nilimkuta akiwa nje akipika, lakini aliponiona alishtuka sana akabaki kinywa wazi, hakunipokea alibaki ameduwaa, nikahisi kuna jambo. Nilimsalimia alijibu kwa wasiwasi nilipotaka kuingia ndani, alinizuia, na huku akiongea kwa sauti yenye kutetemeka aliniambia eti ndani kuna binamu yake kaja na amejipumzisha kitandani kwake, nilishtuka. Niliiingia ndani moja kwa moja na kumkuta kijana amelala kitandani nilipomuhoji kuwa yeye ni nani na anafanya nini pale akaniambia kuwa yuko pale kwa girlfriend wake na alitaka kujua eti mimi ni nani..Sikutaka kuzua ugomvi, nilimwambia kuwa pale ni kwa dada yangu na nilifika kumsalimia, nilimuomba radhi kwa kuingia bila hodi, ila nilimshauri aharakishe kulipa mahari ili tujue kuwa dada yetu anaye mtu, ili wakati mwingine tubishe hodi, niliongea kwa utani, yule kijana alimsifia sana mchumba wangu kuwa ni mzuri hasa na anajua kupenda, alibwabwaja mambo mengi na upuuzi wao wanaofanya nikiwa sipo, niliongea naye kwa utani mwingi na kuaga na kuondoka, lakini moyoni roho ilikuwa ikiniuma kweli. Nilikuwa nampa yule binti karibu kila kitu alichohitaji, lakini kumbe hakuridhika bado akawa na mwanaume mwingine.

Nilitoka na nilimkuta kajiinamia pale nje, sikumuaga nikaondoka zangu. Nilipofika nyumbani nilimtumia ujumbe mfupi wa simu ya kiganjani nikimwambia kuwa kuanzia siku hiyo ilikuwa ni mwisho wa uhusiano wetu. Hakijibu na siku iliyofuata alipiga simu lakini sikupokea, alibadilisha namba na nilipopokea na kugundua kuwa ni yeye nilikata simu, baadae zilifuata ujumbe kadhaa wa simu yake ya kiganjani akitaka tuonane ili tuyamalize. Sikumjibu. Na ndio akaamua kuja ofisini.

Nilimpigia simu katibu muhtasi wangu na kumuamuru amwambie yule binti aondoke pale ofisini. Niliambiwa kuwa amekataa, nilimpigia simu dereva wangu na kumuuliza kama gari limeshatoka gereji, akanijibu kuwa gari litatoka baadae kidogo, nikamwambia akitoka gereji aende nalo nyumbani kisha kesho asubuhi anifuate. Gari langu liliharibika siku mbili zilizopita, hivyo nililazimika kupanda daladala au taxi kama nikiwa na dharura. Niliondoka pale ofisini nikimuacha akiongea na katibu wangu muhtasi na kuondoka zangu. Nilikodi taxi na wakati niko njiani nikakumbuka kuhusu ile simu, lakini niliisahau ofisini, kwa hiyo sikupitia kariakoo tena. Nilikwenda moja kwa moja hadi kwa rafiki yangu anayeishi maeneo ya kijitonyama na kupoteza muda huko hadi usiku ndio nikarudi nyumbani.

Siku iliyofuata dereva alinifuata na kunipeleka ofisini, nilipofika nilimpa ile simu na kumtuma akanitafutie chaja ya ile simu. Baadae alirudi akiwa na chaja ya simu ile na kunikabidhi. Niliichaji na ilipojaa niliiwasha ziliingia ujumbe kadhaa kutoka kwa watu waliokuwa wakimtafuta mwenye simu ile, nilipozisoma niligundua mwenye simu ile alikuwa anaitwa Yasinaty, nilikata shauri nimpigie mmoja wa watu waliokuwa wametuma ujumbe ambaye alionekana kuwa ni mama yake. Nilipompigia simu na kuuliza kama anamjua mwenye simu kwanza alitaka kujua mimi ni nani na kwa nini simu ya mwanaye ninayo mimi. Nilimsimulia kila kitu na nilimuomba ampe mwanae namba yangu ya simu na kumuomba amwambie awasiliane na mimi ili nimpe simu yake. Yule mama alifurahi sana na kunishukuru sana, kumbe ile simu Yasinaty alitumiwa na kaka yake aishie Ughaibuni.

Mchana nilipigiwa simu na Yasinaty na tuliongea mengi na alionekana ni binti mchangamfu kweli, alinimbia kuwa anafanya kazi kwenye Hoteli moja ya kitalii maarufu iliyoko katikati ya jiji, nilimuahidi kumpitia kazini kwake jioni nikitoka ofisini.
Nilimpitia jioni na kama alivyonielekeza kuwa yuko reception nilimkuta pale akimalizia kazi na aliniomba nimsubiri kweye kijimgahawa kilichopo pale ndani, kwa kuwa mimi sio mnywaji wa pombe niliagiza juisi ili kumsubiri. Baadae alinipitia pale nilipokaa na kunimbia kuwa anatoka hivyo tukutane nje kwani anakwenda kubadili sare za kazini. Alitoka na kunikuta nje nikimsubiri, alipanda kwenye gari na nilimuomba dereva wangu atupeleke Hoteli nyingine ya kitalii maarufu pale hapa jijini ili tupate kahawa na Yasinaty. Tulifika pale tuliagiza vinywaji. Nilitumia wasaa ule kumtazama vizuri Yasinaty, alikuwa ni binti mrembo sana, na mchangamfu hasa, naamini alistahili kufanya kazi reception.

Nilimkabidhi simu yake na yakafuata maongezi mengine ya kujuana na simulizi za hapa na pale. Huo ndio ukawa mwanzo wa kujuana na Yasinaty, ambaye baadae alikuja kuwa mke wangu mpenzi.

Laiti kama ningekufahamu kabla Yasinaty………………….

Habari hii nimetumiwa na msomaji wa blog hii ya MAISHA ambaye anasheherekea ndoa yake kutimiza miaka mitano leo. Na nimeona si vibaya kama nikiweka hapa.

MUZIKI NI MOJA YA MAISHA TUMSIKILIZE DADA NURU LEO



Maisha yetu wengine hawawezi kuishi bila kusikiliza mziki hata siku moja na wengine hawawezi kusikiliza redio hata siku moja na wengine kusoma vitabu na magazeti. Kila mtu anapata habari kwa namna ya pekee. Haya leo nimeona tumsikilize Mwanablog mwenzetu Da Nuru the lihgt.!!!!

Monday, October 12, 2009

WANANDOA NA KAULI HIZI: HATA VIKOMBE KABATINI HUGONGANA, ITAKUWA SIE?

Je unadhani au kuamini kwamba kuna ndoa ambazo wanandoa wake hawagombani kabisa? Kama unaamini hivyo, basi unajidanganya na labda unaishi katika dunia ya peke yako.

Ni jambo lenye ukweli wa kutosha kabisa kwamba wanandoa wote duniani hutokea kugombana, lakini kugombana huko hutokana na migongano au mizozo ya muda tu ambayo huweza kutatuliwa na pande mbili kama wakiamua kufanya hivyo.

Wewe unayesoma hapa, napenda kukuambia ukweli kwamba usiogope migogoro ya ndoa, kwani hicho ni kitu ambacho kamwe huwezi kukiepuka. Kuna msemo mmoja unatumika sana huko nyumbani usemao, " hata vikombe kabatini hugongana itakuwa wana ndoa?" Hii ina maana gani, ina maana kwamba haiwezekani watu kuishi pamoja halafu msiwe mnatofautiana, na kama ukiona hivyo, jua kwamba hiyo ndoa si salama kwani siku yoyote bomu litapasuka na madhara yake yatakuwa ni makubwa kuliko kawaida.

Kuna watu ambao hata kama wamekosewa na wenzi wao hunyamaza kimya na kumeza hasira zao, wengine huogopa kuwakabili wenzi wao na kuzungumzia jambo linalowakera kwa kuhofia kuonekana kama wana kasoro au ghubu. Jambo hili ni hatari sana.

Kumkabili mwenzi wako na kumwambia hisia zako kama amekukosea au amekwenda kinyume na matarajio yako ni jambao la maana sana katika kudumisha uhusiano. Lakini naomba nitahadharishe kwamba, ni vyema kufanya hivyo bila kumshusha, kubeza au kusimanga kwani hiyo sio dalili nzuri ya upendo.

Inashauriwa kwamba wanandoa au wapenzi wanapokwaruzana inabidi wajadili tofauti zao bila kusigishana, kila mmoja akitaka kuwa mshindi, hiyo haitasaidia kuimarisha ndoa bali itaongeza tatizo. Ni vyema upande unaohusika na tatizo, uwajibike na kuomba radhi kwa ustawi wa ndoa, huo ndio ukomavu.

Kutojadili mgogoro kwa wanandoa na kuupatia ufumbuzi wa tatizo huwafanya wandoa kuwa mbali kihisia, na athari zake ni kuwakuta wanandoa wakiwa wageni wa kila mmoja kwa mwenzake, yaani hakuna mawasiliano, kila mtu na lwake.

Jambo la msingi kwa wanandoa ni kujadili tofauti zao pindi linapojitokeza jambo linalomkera mmoja wa wanandoa, kwani hakuna jambo linaloweza kujitatua lenyewe bila kutatuliwa na wandoa husika. Kuacha jambo lolote bila kulitafutia suluhu ni sawa na kutega bomu, ambapo siku likilipuka madhara yake ni makubwa sana.

Unaweza kukuta mwanandoa anakereka na mambo madogo madogo ya mwenzi wake lakini hasemi, ingawa yanamkera kupita kiasi akitegemea huyo mwenzi wake atajua na kuacha, thubutu…..inapotokea siku yeye amekosa jambo dogo tu na huyo mwenzi wake akamsema, basi atatumia fursa hiyo kuanza kujibu mapigo kwa kueleza yale yanayomkera kutoka kwa mwenzi wake, na hapo itakuwa kila mtu anavutia kwake kama mwamba ngoma………na aamini nawaambia kuwa kamwe hawezi kupatikana mshindi katika jambo hilo, kwani mjadala huo unaweza kutoka nje ya mada kila mmoja akijitahidi kutafuta makosa ya mwenzi wake hata yale yaliyotokea wakati wa uchumba wenu ili mradi vurugu tupu.

Inatakiwa wanandoa wajadili kila jambo linalojitokeza hadi kulipatia suluhu, vinginevyo ni kuichimbia ndoa yenu kaburi la mapema. Wakati mwingine unaweza kukuta mwanamke analalamika juu ya kutoridhishwa kwake na matumizi ya mumewe, na hapo mume naye ataanza kukumbusha juu ya matumizi yasiyo ya lazima yaliyofanywa na mke huko nyuma. Mke naye hataridhika atakumbushia jambo lingine na lingine hadi hata mada iliyokuwa ikijadiliwa inasahaulika.

Jambo lingine ni kujumuisha mambo, matumizi ya maneno kama, mara nyingi, kila wakati au mara kwa mara si mazuri sana. Unaweza kukuta mtu mwenzi wake amekosea jambo halafu mwenzie anamwambia “Kila mara huwa unafanya hivi” au mara nyingi huwa unafanya hivyo…..Hii ni hatari kwa ustawi wa wanandoa, kwani kwa kujumuisha ni sawa na kumwambia mwenzi wako kuwa kila mara yeye ndiye mkosaji.

Kwa haya niliyoyaeleza hapa sina maana kwamba huu ndio muarobaini pekee wa kuimarisha mahusiano kwa wanandoa, bali ni moja ya mambo muhimu kati ya mengi ambayo yakizingatiwa na wanandoa wote basi ndoa yao itakuwa imara Tujadili pamoja………..

HONGERA KWA SIKU YA KUZALIWA DA SUBI!!


Ni furaha kuwa na rafiki kama Da Subi na leo ni siku tukufu kwako. Ni siku ambayo ulitokea hapa duniani . Napenda kukutakia yote mema, uishi miaka mingi uwe bibi kizee na wajukuu wengi uwe nao. Subi ni mtu mtukutu sana kwa hilo nakuheshimu na pia nakupenda sana .HONGERA KWA SIKU YA KUZALIWA RAFIKI YANGU!!!!!!