Showing posts with label simulizi mbalimbali. Show all posts
Showing posts with label simulizi mbalimbali. Show all posts

Thursday, February 7, 2013

ULIJUA KWAMBA SABABU YA KUWAITA JINA "WAZUNGU" LILITOKANA NA-----

Kuna mzungu aliniuliza maana ya neno mzungu. Nikamwambia haihusiani kabisa na rangi bali inatokana na wale weupe wa kwanza waliofika Afrika na hawakujua wanakwenda wapi, hivyo walikuwa wanazunguka ovyo! Kuna stori nilisimuliwa nikiwa mdogo, kuna kundi la wazungu walifika kijijini. Walikaribishwa vizuri na Chifu wakaondoka. Baada ya wiki mbili wazungu hao hao wakarudi pale kijijini. Chikfu kauliza, "Jamani, hao si ndo tuliwaaga majuzi!" Mzungu kashangaa hakufika popote bali anatembea katika mduara!
Imenukuliwa kutoka kwa Da’Chemi kwenye
blogu yake - “SwahiliTime”.