Leo tuangalia mji wa SONGEA:-
Songea ni mji nchini Tanzania ambao ni makao makuu ya Mkoa wa Ruvuma. Kulingana na sensa ya mwaka 2002 idadi ya wakazi wake ilihesabika kuwa 131,336. Kuna barabara ya lami kutoka Songea kupitia Njombe hadi barabara kuu ya Dar es Salaam - Mbeya. Barabara ya kwenda pwani kupitia Tunduru na Masasi ni mbaya mara nyingi haipitiki wakati wa vua haswa..ila sasa iko mbioni kutengenezwa...
JIOGRAFIA KIDOGO:-
Mji wa Songea uko kimo cha M 1210 juu ya UB katika nchi ya Ungoni kwenye nyanda za juu za kaskazini za Tanzania. Chanzo cha mtu Ruvuma kipo karibu na mji.
HISTORIA:-
Jina Songea ni kumbukumbu ya chifu Songea wa Wangoni aliyekuwa na ikulu yake hapo wakati wa kuenea kwa wa ukoloni wa Ujerumani akauwawa na Wajerumani wakati wa vita ya majimaji.
Mji wa Songea (iliandikwa Ssongea wakati ule) ulianzishwa mwaka 1897 kama kituo cha kijeshi cha Kijerumani. Ukakua kuwa makao makuu ya utawala wa mkoa wa Songea wa Afrika ya Mashariki ya Kijerumani.
Mazinginra ya mji yaliathiriwa vibaya na vita ya majimaji na ukandamizaji wake na Wajerumani.
Songea ikaendelea kuwa makao makuu ya mkoa wakati wa utawala wa Uingereza katika Tanganyika na baada ya uhuru katika Tanzania huria.....HII NI HISTORIA/GEOGRAFIA YA MJI WA SONGEA...