Showing posts with label amani na upendo. Show all posts
Showing posts with label amani na upendo. Show all posts

Saturday, August 23, 2014

Sunday, July 7, 2013

NAPENDA KUWATAKIENI WOTE DOMINIKA HII YA 14 YA MWAKA C

Simba huyu anatisha kweli utafanya nini ukikutana naye njiani?. Lakini kuna adui mwingine mbaya na anayetisha zaidi kuliko simba, Ndiyo maaana mtume petro anatuonya akisema " Nuwe macho; kesheni. Maana adui yenu, ibilisi, huzungukazunguka kama simba angurumaye akitafuta mawindo". NAWATAKIENI WOTE MTAKAIPITA HAPA JUMAPILI NJEMA SANA,.......KAPILYA

Friday, December 9, 2011

SALAMU ZA KUSHUREKEA MIAKA 50 YA UHURU TANZANIA KUTOKA SWEDEN...

Familia hii haiko nyumba katika siku hii ya kusherehekea miaka 50 ya Uhuru. Ingawa mwanafamilia mmoja hayupo katika picha. MUNGU IBARIKI TANZANIA, WABARIKI VIONGOZI WAKE, HEKIMA UMOJA NA AMANI MUNGU IBARIKI TANZANIA NA WATU WAKE IBARIKI TANZANIA ....

Thursday, October 28, 2010

TANZANIA NAIPENDA SANA NA NADUMISHA AMANI NA MSHIKAMANO!

Tanzania; Utulivu na Amani ni siraha yetu, tudumishe Amani yetu tunu yetu njema. Tunu hii tumepewa kwa upendeleo...hatukuinunua kwa fedha tunu hii, bali Amani imetawala...Amani ni namba moja Tanzania.
Madaraka yasituchanganye, utajili usituchanganye, bali amani ni mhimu na ni namba moja kwa Tanzania. Tunapo kosoana wapendwa, tunapo elezana ukweli...Amani itawale daima! kwenye shida na kwenye furaha, kwenye njaa na kwenye huzuni...Amani itawale daima!
Tukumbuke ametupa bure, tukimwuzi ataiondoa Amani hii...tuitunze kama yai tunu hii njema ya Amani, tuilee na tuipambe vizuri tunu hii njema, tuitunze ili nayo itutunze, tuilishe na tuinyweshe daima kwa Utulivu na Amani sisi Watanzania hasa katika kipindi hiki cha uchaguzi mkuu.
IDUMU DAIMA AMANI TANZANIA.

-Mimi kila ninapopata wakati mgumu wa kutafakari, wanapotupeleka viongozi wetu, huwa natafuta solitude kwenye Amani waliotuachia Wazee wetu wa enzi za Mwalimu, Baba wa Taifa letu. Unajua Amani ni kila kitu, hata kama umezingirwa na mafisadi...lakini walau unapata wasaa wa kuburudisha roho yako ukiwa kwenye Amani yako.
Mwalimu Nyerere, Baba wa Taifa letu, alicheza sana aliposema; Ukabila uishie utani, dini iwe ni mapenzi ya mtu na nafsi yake. Maneno haya yametuweka hapa tulipo leo. Nasikitika tu generation ya watoto wetu, maana sisi Baba zao tunadhani Amani hii tuliyo nayo Mungu anaona aibu kutuondolea na kuwapa wenye akili na mapenzi nae.

MUNGU IBARIKI AFRIKA, MUNGU IBARIKI TANZANIA NA WATU WAKE WOTE!

Makala hii nimeipenda na nimeona si mbaya nikiibadika hapa. Ni kutoka kwa kaka Baraka CHibiriti. Duh! naa sasa ni siku tatu tu zimebaki kwa kweli naiombea nchi yetu Tanzania uchaguzi uwe wa amani. Mwenyezi Mungu atutangulie.

Sunday, March 21, 2010

Nawatakieni Jumapili njema wote na neno Upendo!!!

Ufanyacho upendo:-

Upendo kidogo ni kama jua, ambalo ni rafiki yetu wa daima. Hufukuza baridi, kuimarisha mazao yetu na kuyaivisha. Hivyo ndivyo ufanyavyo upendo; kama jua. Katika kupendana, yule mwenye kupendwa hibadilika. Anabadilishwa kutoka hali ya mashaka, wasiwasi, hofu, upweke na kutoamini; anakuwa mtu mwingine kabisa. Mwanzoni alikuwa mwenye hofu na mashaka, sasa ni mwenye kujiamini na kuthubutu kutenda. Badala ya uchungu na upweke, imekuwa furaha na heri. Ni kama nyoka abadilishaye ngozi yake ya zamani kwa wakati fulani, na kubaki na ngozi mpya. Kwa upendo aliopata mtu huyu amefanywa kuwa mpa.

Mara nyingi twasikia watu wakisema , "Huyu mvulana anampendaje msichana huyu?" au " nini cha kuvutia alicho nacho Bwana huyu?" Haina maana kuuliza kwa nini twampenda mtu mwingine. Kama ni mapendo kweli, hatumpendi mtu kwa kuwa ana vitu fulani vya kuvutia wala hatumpendi ingawa ana kasoro, bala tunampenda mtu aliye ndani ya yote haya.

Na kwa kweli tunaweza kupata maana kamili ya upendo kutoka kwa Mungu peke uyake ambaye Neno lake latuambia

upendo: huvumiliam hufadhili,
Upendo: hauhusudu,
Upendo: hautabakari, haujivuni,
Upendo: haukosi kuwa na adabu, hautafuti mambo yake,
Upendo: hauoni uchungu, hauhesabu mabaya
Upendo: haufurahii udhalimu, bali hufurahi pamoja na kweli
Upendo: huvumilia yote, huamini yote, hutumaini yote, na hustahimili yote
(1 Wakorintho 13: 4-7)
NAPENDA KUWATAKIENI WOTE JUMAPILI/DOMINIKA HII YA 12 YA MWAKA HUU. MWENYEZI MUNGU AWA NANYI WOTE. AMINA



Tuesday, November 11, 2008

KATIKA MAISHA NI VIZURI KUWAFARIJI MWENYE MATATIZO

Huu ni ushauri wangu mimi kwa wewe iliye na rafiki aliye na matatizo:-

1) Kama rafiki yako ana matatizo usiogope kumwuuliza hali yake kwa ujumla hata kama hali yake inaonekana si nzuri. Kama una matatizo halafu watu/marafiki wanakuuliza U HALI GANI utajisikia amani yaani kuna watu ambao wanakujali haupo peke yako.

Wakati mwingine kunatokea mambo ambayo si kweli na watu wanafikiri kuwa tayari yule mwenye matatizo amepata msaada mtu wa kuongea naye, wakati kumbe wewe upo peke yako kwa hiyo kuuliza ni muhimu sana.

2) Piga simu au nenda ili kujua mpatwa matatizo ana hali gani. Pia pika chakula, nenda kwake na mle pamoja. Wakati matatizo yanapotokea, inakuwa ngumu kuelezea vitu ulivyozoea kufanya kila siku. Kama una watoto inakuwa ngumu zaidi kuwatunza wakati upo kwenye matatizo/majonzi.

3) Onyesha upendo wako, bila kuonekana ni usumbufu kwa mpatwa matatizo, uwe nusu nusu. Usizidishe au usipunguze. HAPO NDIPO UTAWEZA.

Thursday, October 23, 2008

LAKE -MANYARA


Kwanza nilifikiri nimefika mbinguni, kwa kweli watanzania inabidi tujivunie sana nchi yetu nzuri.