Showing posts with label methali. Show all posts
Showing posts with label methali. Show all posts

Thursday, August 21, 2014

KISWAHILI:- METHALI ZETU!!

1. Usimwamshe aliyelala, utalala wewe.
2. Usipoziba ufa utajenga ukuta.
3. Usitukane mkunga na uzazi bado.
4. Uso mzuri hauhitaji urembo.
5. Vikombe vikaka pamoja havina budi kugombana.
6. Waraka ni nusu ya kuonana.
7. Wagombanao ndio wapatanao.
8. Usiache mbachao kwa msala upitao.
9. Mchumia juani, hula kivulini.
10. Mla nawe hafi nawe ila mzaliwa nawe.
Ni hizi tu kwa leo ila nawe kama una mojo, mbili tatu usisite kuweka hapa eilimu ni kugawana. Haya siku na kazi njema . Wenu Kapulya:-)

Wednesday, May 14, 2014

NI MUDA MREFU SASA UMEPITA :- METHALI ZETU....

Nimeona usipite muda zaidi bila kuzikumbuka METHALI  zetu basi ungana nami  katika hizi chache nilizozikumbuka leo:-

1. Aninyimaye mbaazi, kanipunguzua mashuzi
2. Biashara haigombi.
3. Chanda chema huvikwa pete.
4. Dua la kuku halimpati mwewe.
5. Fimbo ya mbali haiui nyoka.
6. Kikulacho ki nguoni mwako.
7. Kosa moja haliachi mke.
8. Lisilokuwepo moyoni halipo machoni.
9. Mapenzi ni kikohozi hayaweza kufichika.
10. Mficha uchi hazai.
BLOG YA MAISHA NA MAFANIKIO INAWATAKIENI WOTE SIKU NJEMA SANA NA WOTE MNAPENDWA:-)

Tuesday, January 7, 2014

NI JUMANNE YA KWANZA YA MWAKA HUU 2014 NAMI NIMEONA TUIANZA KWA MTINDO HUU:- METHALI ZETU!!! UNAZIKUMBUKA HIZI?:-)

1. Asiyekuwepo machoni, na moyoni hayupo.
2. Bendera hufuata upepo.
3. Chururu- si ndo, ndo, ndo.
4. Dua tupu haliachi kuvuma.
5. Fuata nyuki ule asali.
6. Hakuna msiba usiokuwa na mwenziwe
7. Heri kufa macho kuliko kufa moyo.
8. Ikiwa hujui kufa, tazama kaburi,
9. Jogoo la shamba haliwiki mjini.
10. Kimya kingi kina mshindo mkuu.
SIKU YAKO IWE NJEMA SANA NAWE KAMA UNA METHALI UIKUMBUKAYO KARIBU KUISEMA/ANDIKA.

Tuesday, September 3, 2013

TUSISAHAU METHELI ZETU ZA KISWAHILI....!!!!!

1. Yaliyopita si ndwele, tugange yajayo.
2. Yote yangáayo usidhani ni dhahabu.
3. Ungelijua alacho nyuki, usingelionja asali.
4. Radhi ni bora kuliko mali.
5. Ndugu wakigombana, chukua jembe ukalime, wakipatana chukua kapu ukavune.
NAWATAKIENI JUMANNE NJEMA WOTE NA KAMA UNA METHALI PIA ONGEZEA:-)

Thursday, April 4, 2013

TUSISAHAU METHALI ZETU....!!!!!

1. Watu tunawadhania ni marafiki, mara nyingine ni maadui.. Mpelelezi si rafiki.
2. Mtu akitaka kupata cheo, awe na heshima kwa wakubwa.
3. Kama ukipata mali kwa kazi yako, weka akiba kwa siku za uzee.
4. Ufuate mashauri na maneno ya watu wenye akili.
5. Mtu ana maneno mazuri na matamu, lakini nia yake ni mbaya.
6. Ukiwa mgeni katika nchi, uelekee kadiri watu walivyo.
7. Wakiwa wakubwa wawili, watapata ugomvi, hawawezi kukaa pamoja.
8. Mtu akitangaza habari ya uongo, ni vigumu kusahihisha maneno yake.
9. mtu anaweza kukuchekelea kwa mdomo, lakini katika moyo ana mawazo mengine.
10. Ujitahidi mwenyewe na Mungu atakusaidia.
TUTAENDELEA KUKUMBUSHANA KILA WIKI ILI TUSISAHAU..NA KAMA KUNA MMOJA ANA NYINGINE ANAWEZA KUONGEZEE TU...SIKU NJEMA SANA PANAPO MAJALIWA TUTAONANA TENA...KAPULYA

Tuesday, August 14, 2012

METHALI ZETU:- METHALI ZAFAA SANA KWA MAFUNDISHO YA ADILI!!!!

1. Penye urembo ndipo penye urimbo.
2. Radhi ni bora kuliko mali.
3.Siku utakayokwenda uchi, ndiyo siku utakayokutana na mkweo.
4. Ukitaka kula nguruwe, chagua iliyenona.
5. Ulipendalo hupati, hupata ujaliwalo.
6. Ungelijua alocho nyuki, usingekula asali.
7. Vyako, vyako na mwenzio; vikikupata ni vyako peke yako.
8. Wagombanao ndio wapatanao.
9.Yote yangáayo usidhani ni dhahabu.
10. Zimwi likujualo, halikuli likakwisha.
Tusisahau methali zetu, tuwetunazitumia katika mafundisho. Pia tuwaambia na kizazi kijacho. Maana hii ndio asili yetu......

Thursday, May 10, 2012

TUSISAHAU METHALI ZETU/BAADHI NI IMANI ZA USHIRIKINA (SUPERSTITIONS)!!

1.Kuku wakionekana kama wananongónezana basi patafika wageni ghafla.
2. Kuweka mikono kichwani bure tu, kunaleta kifo cha mzee wake mtu.
3. mtu akiinuka akaona nguo imeganda matakoni basi inaonyesha kuwa mtu huyo ana tabia ya kusema uwongo.
4. Mwanamke hali ndizi pacha(hasa mwenye mimba) kwa kuchelea kuzaa watoto pacha..
5. Ukiona mwasho juu ya kiganja cha mkono wa kilia utapokea fedha.
6. Kiganja cha mkono wa kushoto kikikuwasha ni alama ya kutumia fedha.
7. Ukijikwaa mguu wa kulia pana heri inakungoja huko uendako.
8. Ukijikwaa mguu wa kushoto utafikwa na maafa huko uendako.
UKIWA NA METHELI NAWE UNAWEZA KUONGEZEA NA NDIYO KUJIFUNZA MENGI!!!

Thursday, April 26, 2012

TUKUMBUKE METHALI ZETU!!!

1. Shida ingekuwa sumu tungekufa wengi.
2. Mwisho wa biashara yoyote ni faida au hasara.
3. Mpe akupaye, ukimpa asiyekupa ni sawa na kutupa.
4. Nyumba ya udongo haipingwi deki.
5. Hata mbuyu ulianza kama mchicha.
6. Kucheke sio dalili ya wema kwa mwenzio.
7. Usilie kwa kupigwa lia kwanini umepigwa
8. Akupendaye katika shida ndiye rafiki wa kweli.
9. Raha ya pilau ni kula kwa mkono
10. Usimchokoze kichaa ukiwa unakaa kwenye nyumba yenye vioo.
KILA LA KHERI.

Monday, December 13, 2010

NGOJA LEO TUANGALIE METHALI ZETU:- METHALI ZAFAA SANA KWA MAFUNDISHO YA ADILI!!!

1.Asiyefunzwa na mamaye, hufunzwa na ulimwengu.
2. Baada ya dhiki, faraja.
3. Baba wa kambo si baba.
4. Chema chajiuza, kibaya chajitembeza.
5. Chombo kilichopikiwa Sakaki, hakiachi kunuka vimba.
6. Damu nzito kuliko maji.
7. Dawa ya moto ni moto.
8. Fadhili za punda, mashuzi; na msihadhari ni ngómbe.
9. Fumbo mfumbie mjinga , mwerevu hulingámua.
10. Ganda la mua la jana, chungu kaona kivuli.
11. Gonga gogo usikilize mlio Wake.
12. Hakuna siri ya watu wawili.
13. Hasira, hasara.
14. Ihsani haiozi.
15. Jungu kuu halikosi ukoko.
16. Jambo usilolijua ni kama usiku wa kiza
17. Kila mlango na ufunguo Wake.
18. Kulea mimba si kazi´, kazi kulea mototo