Kabila la Wamatengo ni Kabila la Asili, halijaundwa kwa kutokana na makabila mengi yaliyochanganyika kama ilivyokuwa kwa kabila la Wangoni, ndio maana hata lugha yake haijaathiriwa na lugha zingine kwa kiasi kikubwa.
Ni makabila machache tu yaliyotoka katika koo nyingine ukoo wa akina KAPINGA, KOMBA (Hanze), MAPUNDA na LUANDA; ni koo ambazo ziliingia kutoka upangwa. Vile vile koo kama akina NDIMBO na NCHIMBI zilitoka Magharibi ya pwani ya ZIWA NYASA. Koo hizi ambazo zilitoka nje hazikuleta athari katika lugha ya kimatengo, ukizingatia kuwa koo hizo zilikuwa chache kiidadi kuliko wenyeji wa asili ya nchi ya UMATENGO.
MAKITA KAYUNI wa ukoo wa akina NDUNGURU ambaye ni Babu kati ya watawala waliokuwa machifu katika nchi ya Umatengo mwishoni inasadikika kuwa, kwa asili alitoka kabila la WANINDi, aliishi chini ya mlima Matogoro karibu na Songea.
Alipoingia MPUTA MASEKO katika nchi ya Ungoni. MAKITA KAYUNI alishindwa kupigana naye akasalimisha jeshi lake kisha akajiunga naye na akapata fursa ya kujifunza mbinu za kivita.
Kayuni alijipatia uhuru wa kufanya chochote na kwenda kokote alikotaka baada ya Mputa Maseko kufukuzwa katika Wilaya ya Songea, akaamua kuhamia katika nchi ya umatengo huko LITEMBO ambako alipokelewa kwa ukarimu mkubwa mno na KAWANILA HYERA pamoja na LIHUHU KINUNDA.
Kayuni alikuwa na ufundi katika masuala vita pamoja na akili ya maisha, watu wa Litembo (Wamatengo) waliona anafaa kuwa kiongozi; alipokufa Kawamila bwana Makita alichaguliwa kuwa mrithi wake.
Baba wa Kayuni Mzee Kapitingana alifika Litembo na kuweka makazi yake; licha ya kwamba Kayuni hakuishi Litembo maisha yake yote lakini alizaliwa katika ardhi ya Litembo kwa Ndenya Ndunguru. Kayuni alipewa jina la ukoo wa Mama yake kwa kuwa Baba yake Mzee Kapitingana hakulipa Mahari.
Familia ya Makita kipindi cha Mputa Maseko (1864 -1865)
Ukoo wa Babu, Baba, Makita na Familia yake waliishi Litembo, familia ya Makita ilifika Litembo baada ya Mputa Maseko kuikimbia Songea mwaka 1864s.
Inaelezwa mwaka 1866s Kayuni alipata bahati ya kuzaliwa; hivyo kuna uhakika kwamba Makita Kayuni aliuawa akiwa na umri mkubwa kwenye vita ya mwisho kati ya Wangoni na Wamatengo ambayo ilikuwa miaka minne kabla ya kifo cha Nkosi Mharule kilichotokea mwaka 1885.
MAKAZI YA WAMATENGO NA TAKWIMU ZAO KABLA YA WANGONI KUJA SONGEA
Kabla ya Wangoni kuja Songea na kujenga Makazi yao, Wamatengo waliishi katika vijiji ambavyo vilitengana tengana au kutawanyika (Musi musi) kama vile Litembo, Mapera, Ungima (Ngima), Hanga, Kitogota, Kimati, Nkuka, Ungwindi, Baruma, Matiri (karibu na Milima ya Lilengalenga).
Wamatengo walipata shida sana kulinda Miji yao dhidi ya vita ya Wangoni walipoelekea umatengoni ili kufanya makazi yao. Kundi kubwa la watu wailishi katika Bonde la Litembo.
Mwandishi Fullborn amefafanua kwamba, kijiji cha Makita kilikuwa na watu 5,000 kwa mujibu wa Sensa iliyofanywa na Wajerumani mwaka 1904 huku idadi kubwa ya watu ikitoka katika bonde la Litembo katika eneo la Makita, suala ambalo lilipelekea ulinzi kuwa mdogo wakati wa vita.
Wageni waliobahati kutembelea katika kijiji cha Makita wanafafanua kwamba mitetemeko yote inayohusiana na milima ya Litembo ilijengwa vibanda, mapango katika milima ya Litembo yalitumika kwa ajili ya kujificha wakati wa vita. Bro. Laurentius Brenner aliyapima baadhi ya mapango mwaka 1906 na akaandika mambo muhimu aliyoyabaini.
“Wamatengo wengi wanaishi katika mapango. Sehemu zingine katika hivi vibanda havionyeshi kama wanaishi watu, lakini wanaishi pale, inaonekana miamba mikubwa ndio nyumba zao.
Inavyotokea wazungu wanajitokeza kwao hujificha kwenye miamba hiyo; katika baadhi ya mapango hakuna anayeweza kuingia akiwa wima, nililiona pango mojawapo liliokandikwa kwa udongo ambalo lilijazwa kuni pande zote”
“Ni jambo la kushangaza pango hilo lilikuwa na kina cha mita mbili hadi tatu, hadi kukifikia chumba kulikuwa na ngazi zilizoelekea katika eneo la kuchota maji. Hata hivyo palikuwepo na mapango mengine ambayo haikuwa rahisi kuona mlango wa kuingilia, ila shimo dogo la kutokea moshi lilionekana”
“Mapango mengine yana kina lakini hayaruhusu mwanga wa jua kuingia wala kupenya, inaonekana watu huyatumia wakati wa usiku tu! kuna baadhi ya mapango yana mlango wa pili ambao ni ngumu mno kuuona kwa macho, uenda unatumika wakati wa hatari tu!” alisema Brenner.
Kama si Mapango Wamatengo wangeteketezwa na Wangoni
Hata katika kipindi cha Mputa Maseko na hawaya Wangoni walifanya mashambulizi ya kivita dhidi ya kabila la Wamatengo na kuteka mali za Wamatengo na mifugo yao.
Wamatengo walipoamua kuishi katika bonde la Litembo jeshi la Wangoni lilipata shida mno wakati wa mapambano mara nyingi walirudi ungonini bila kutekeleza mipango yao ya kuwasambaratisha Wamatengo.
Vita ya maana yenye kukumbukwa ni ile iliyotokea mwaka 1885 ambayo ilikuwa ni vita ya mwisho kati yao. Makita alishauriwa na baadhi ya watu kwamba amdharau Nkosi Mharule na kutuma baadhi ya watu wakachukue aina ya nyasi ziitwazo ‘Sekela” ili kuzungushia wigo kwenye vibanda vyake.
Kitendo ambacho kilimfanya chifu Mharule achukie kwa kudharauliwa na Makita na hivyo akaenda umatengoni kupambana nao. Inaelezwa kwamba Mfanyabiashara Litunu alitumwa umatengoni, alipita katika ardhi ya wamatengo kuelekea Ziwa Nyasa, inasadikia njiani alishambuliwa na watu ambao iliilezwa walikuwa ni Wamatengo.
Kutokana na kupea kwa urafiki kati ya Litunu pamoja na Mharule hivyo hata biashara zake zilikuwa chini ya utawala wa Nkosi Mharule, hivyo Mharule alipata sababu za kuwapiga Wamatengo na wakati huo alikuwa amehamia sehemu iitwayo karibu na Matomondo kwenye barabara inayoelekea Mbambabay.
Kuuawa kwa Makita katika vita baina ya Wangoni na Wamatengo
Manduna wa Kingoni walioshiriki kwenda kupiga vita hiyo katika nchi ya Wamatengo ni pamoja na Nduna Songea, Sanangula, Mpangile, Chikuse na wengine. Wakati wa vita hiyo Makita mwenyewe alisimama juu ya mwamba mkubwa ili kuwapa moyo Askari wa Kimatengo.
Wakati vita ilipokuwa imepamba moto katika vijiji mbali mbali mke wa Makita alikuwa na mume wake muda wote juu ya mwamba huku akimwaga dawa ya vita toka kwenye kikapu chake na kumtia moyo ili Wamatengo waweze kushinda katika vita ambayo ilidumu kwa muda mrefu bila kufikia ukomo.
Askari wa kingoni kwa kutumia bunduki yake alimtungua Makita akiwa juu ya Mwambo huo kisha akadongoka na kupoteza maisha pale pale, tukio hilo lilipelekea Askari wa makita kujisalimisha mikononi mwa Askari wa Kingoni na wakajitangazia ushindi na wakafanya sherehe.
Wangoni walirudi katika ardhi yao huku wakiwa na Mateka mengi pamoja na mali zao, baadhi ya waliotekwa ni Makita Ndunguru ndugu yake Makita Kayuni ambaye alitekwa na watu wa Sanangula; lakini baada ya kuwasili huko Sanangula aliteuliwa kuwa kiongozi wa Wamatengo wa Sanangula.
Mtoto mkubwa wa Makita Kayuni alirithi kiti cha Baba yake na akatawala nchi ya Wamatengo kwa mika mingi, mwaka 1897 wakati wa utawala wa Mandawa Wajerumani walifika Songea.
Machi 1902 Wamatengo waliwaasi Wajerumani na wakakataa kulipa kodi kwenye serikali ya Kijerumani na wakachoma moto shule ya msingi Litembo ambayo ilianzishwa na Padre Yohannes Hafliger wa Kigonsera tarehe 11-9-1901.
Kitendo hicho kiliisha mara moja wakati wa utawala wa Mandawa na baadaye alimwachia madaraka mdogo wake Mtwara ili kumpa heshima ambaye naye aliitawala umatengo yote. Vita ya Maji Maji ilipoingia umatengoni hawakupenda kushirikiana na Wangoni ambao ni maadui zao wa zamani ili kuwapiga wajerumani.
Kufuatia kifo cha Mtwara, cheo chake kilichukuliwa na Tekambwani mtoto mwingine wa Makita Kayuni, ambaye alifariki baada ya kutawala kwa kipindi kifupi. Watoto wengine wa Makita Kayuni waliikosa fursa ya kuitawala nchi ya umatengo kwa kuwa walikuwa wadogo mno hivyo wazee wa kimatengo wakamchagua Kapungu na akawa chifu wao.
Mwaka 1916, Waingereza walipoichukua Tanganyika na kuitawala kwa mabavu, Kapungu aliondolewa madarakani kisha akawekwa Makita Kipwele Kayuni mtoto wa mtoto wa Makita Kayuni wa I.
Baadaye alilithiwa na Magnus b. Bunungu na baadaye Mrithi wake akawa Yohannes Christomus Makita Kayuni, jina la Makita kutoka Makita Kayuni II Kipwele.
Showing posts with label wangoni. Show all posts
Showing posts with label wangoni. Show all posts
Tuesday, January 21, 2020
Friday, May 30, 2014
Tuesday, November 12, 2013
BLOG YA MAISHA NA MAFANIKIO IMECHAGUA NGOMA HII IKIWA IMECHEZWA NA "ZAMBIA NGONI" IMENIKUMBUSHA LIZOMBE.....NGOMA YA ASILI
Msione kimya nipo niseme tu nilikuwa nimebanwa ila sasa nipo. Napenda kuwatakieni wote kila la kheri.Kapulya
Tuesday, June 18, 2013
NIMEFANYA UTAFITI KATIKA MILA NA DESTURI ZA WANGONI UPANDE WA NDOA NA KUCHUMBIA/KUOA MKE KUZAA...MTOTO WA KIUME NA KIKE!!!!
Kugega mdala= Kuoa mke
Kama wote tujuavyo:- Kijana na msichana wakikua, wanaoa. Kwa wangoni, mtoto wa kuime hata kama akikua na kuoa atakuwa bado anahitajika kwenda vitani. Kipindi hicho yupo vitani inabidi aonyeshe nguvu zake zote. Kijana ambaye hajaenda vitani huitwa "lijaha". Kijana aliyerudi toka vitani huitwa "lidoda". Mwanamkewa kuolewa inabidi awe wa uhakika, anayeweza kufanya kazi za nyumbani. Inabidi aweze kutafuta kuni, kuchota maji, kutwanga kupika ugali/chakula, kupika pombe na awe mchangamfu/mcheshi achekaye na watu wote mtaani/kijijini.
Ndoa haifungwi ndani ya ukoo. Kwa wangoni hairuhusiwi ni mwiko kuoa/kuolewa na mke/mume ambaye ana jina moja la ukoo. kama watu wakioana kiukoo, wazee wataulizia kwanza kama ukoo huo ni wa karibu au wa mbali? (vitepulana) wataapishwa. Watu wanaogopa kuoana ndani ya ukoo kwa vile watoto watakaozaa watakufa wote au watapata kifafa au hata waliokufa (mahoka) watakasirika. Watu wenye Kifafa na wenye ukoma ni mwiko kuoana.
MTENGA
Kwa kingoni cha zamani neno mtenga lilifahamika kama mtu aanyenunua au kuuza vitu. Pia Mtenga ni mtu auzaye mtoto wa kike. Yeye ndiye anayetoa mahali ya mwanzo na mahali yote kwa ukoo wa msichana.
VIPI KUTAFUTA MKE:-
Wenye mtoto wa kiume watakapo kumwoza kijana wao, wazazi wengine wanamtafutia mke, Wazazi wengine wanamwacha kijana wao ajitafutie mke ampendaye. Kama wame/watamwona msichana mzuri watatafuta mtu/ndugu ambaye watamtaka na watamwelekeza nini wanataka. Na huyo anaweza akawa MTENGA wao. Mtenga huyo ataanza kuulizia kisirisiri mambo ya wazazi wa msichana yule na ukoo wake wote na halafu ataenda kuwaeleza wazazi wa mtoto wa kuime. kama wazzi wakiona ya kuwa ni msichan huyu atamfaa kijana wao kama mke ,watenga wataenda kwa wazazi wa msichana tena na kutoa taarifa ya posa. Kama wenye binti watakataa, watenga/mtenga itabidi awabembeleze.....Itaendelea
Kama wote tujuavyo:- Kijana na msichana wakikua, wanaoa. Kwa wangoni, mtoto wa kuime hata kama akikua na kuoa atakuwa bado anahitajika kwenda vitani. Kipindi hicho yupo vitani inabidi aonyeshe nguvu zake zote. Kijana ambaye hajaenda vitani huitwa "lijaha". Kijana aliyerudi toka vitani huitwa "lidoda". Mwanamkewa kuolewa inabidi awe wa uhakika, anayeweza kufanya kazi za nyumbani. Inabidi aweze kutafuta kuni, kuchota maji, kutwanga kupika ugali/chakula, kupika pombe na awe mchangamfu/mcheshi achekaye na watu wote mtaani/kijijini.
Ndoa haifungwi ndani ya ukoo. Kwa wangoni hairuhusiwi ni mwiko kuoa/kuolewa na mke/mume ambaye ana jina moja la ukoo. kama watu wakioana kiukoo, wazee wataulizia kwanza kama ukoo huo ni wa karibu au wa mbali? (vitepulana) wataapishwa. Watu wanaogopa kuoana ndani ya ukoo kwa vile watoto watakaozaa watakufa wote au watapata kifafa au hata waliokufa (mahoka) watakasirika. Watu wenye Kifafa na wenye ukoma ni mwiko kuoana.
MTENGA
Kwa kingoni cha zamani neno mtenga lilifahamika kama mtu aanyenunua au kuuza vitu. Pia Mtenga ni mtu auzaye mtoto wa kike. Yeye ndiye anayetoa mahali ya mwanzo na mahali yote kwa ukoo wa msichana.
VIPI KUTAFUTA MKE:-
Wenye mtoto wa kiume watakapo kumwoza kijana wao, wazazi wengine wanamtafutia mke, Wazazi wengine wanamwacha kijana wao ajitafutie mke ampendaye. Kama wame/watamwona msichana mzuri watatafuta mtu/ndugu ambaye watamtaka na watamwelekeza nini wanataka. Na huyo anaweza akawa MTENGA wao. Mtenga huyo ataanza kuulizia kisirisiri mambo ya wazazi wa msichana yule na ukoo wake wote na halafu ataenda kuwaeleza wazazi wa mtoto wa kuime. kama wazzi wakiona ya kuwa ni msichan huyu atamfaa kijana wao kama mke ,watenga wataenda kwa wazazi wa msichana tena na kutoa taarifa ya posa. Kama wenye binti watakataa, watenga/mtenga itabidi awabembeleze.....Itaendelea
Saturday, June 1, 2013
MWEZI MPYA NIMEANZA HIVI:- NIMEFURAHI SANA KUUPATA WIMBO HUUU ..EBU SIKILIZA NA UNGANA NAMI KUCHEZA ..EEEHHHH CHEKETU
HUU NI WIMBO WA ASILI AMBAO NI WA WENYEJI WA MKOA WA RUVUMA NCHINI TANZANIA.
WIMBO HUU UNAPATIKANA KWENYE ALBAM MWANA WA SHULI SHULI, MAANA YAKE MTOTO WA SHULE. WOTE MUWE NA JUMAMOSI NJEMA MIE HAPA NIPO HOI KABISA..KACHIKI NA WENGINE HAYA TWENDEEE twende mpaka asubuhi.....
Tuesday, April 9, 2013
PALE WATU WANAPOJIULIZA KWA NINI WANGONI WANA VIBONGO/MAJINA YA UKOO KAMA WANYAMA????
Dhumuni la leo ni kutaka kumjibibu dada msaidizi katika mada hii swali lake lilikuwa kama lifuatavya hapa chini
Mija Shija Sayi said...Yasinta umependezaje?
Hebu naomba utusaidie wadau wako kwamba, ni kwanini wangoni majina yao mengi wamechukua kwa wanyama?
Ngonyani, Mapunda.. n.k, Je kuna historia yoyote? Kaka S mtaalamu wa mambo ya Tamaduni,swali hili unaweza tusaidia pia..
Asanteni..
------------------------------------------------------------------------------------------------------------
nami nitajaribu kujibu kama ifuatavyo....
Wangoni wanajulikana sana kwa kuwa na mvibongo/majina ya wanyama wa pori, na hata wanyama wa nyumbani ama majina ya miti au hata ya nyasi. hii ilianzia pale ukoo wa mwanzo ulitoka wapi, wangoni wana majina ambayo yanaelezea kile wanachokifanya, jinsi walivyokuwa hapo kale nk- Walipoanza kutembea na kupiga vita na watu wengine ndo hapo wakaongezea na majina ya wanyama, ndege na ya miti. kwa mfano:- Cawe, Gama, Kapungu, Komba, Kunguru, Mbawala, Nyati, Nguruwe, Ngonyani, Soko, Nyoka na Tembo.....na mengine mengi sitaweza kuyataja yote maana ni mengi mno..
Mija Shija Sayi said...Yasinta umependezaje?
Hebu naomba utusaidie wadau wako kwamba, ni kwanini wangoni majina yao mengi wamechukua kwa wanyama?
Ngonyani, Mapunda.. n.k, Je kuna historia yoyote? Kaka S mtaalamu wa mambo ya Tamaduni,swali hili unaweza tusaidia pia..
Asanteni..
------------------------------------------------------------------------------------------------------------
nami nitajaribu kujibu kama ifuatavyo....
Wangoni wanajulikana sana kwa kuwa na mvibongo/majina ya wanyama wa pori, na hata wanyama wa nyumbani ama majina ya miti au hata ya nyasi. hii ilianzia pale ukoo wa mwanzo ulitoka wapi, wangoni wana majina ambayo yanaelezea kile wanachokifanya, jinsi walivyokuwa hapo kale nk- Walipoanza kutembea na kupiga vita na watu wengine ndo hapo wakaongezea na majina ya wanyama, ndege na ya miti. kwa mfano:- Cawe, Gama, Kapungu, Komba, Kunguru, Mbawala, Nyati, Nguruwe, Ngonyani, Soko, Nyoka na Tembo.....na mengine mengi sitaweza kuyataja yote maana ni mengi mno..
Friday, March 16, 2012
UNAJUA KISA CHA WANGONI KUAMKIANA MONILE??
Ni hivi:- Kulikuwa na mzungu pale Peramiho aliyejenga lile kanisa. Na aliishi miaka mingi pale Peramiho. Mzungu huyo alikuwa na tabia ya kuamka asubuhi na kupita kuwatembelea watu majumbani mwao. Yaani kwa nia ya kuwajulia hali wazee na vijana. Yeye alipenda sana kutembea kwa mguu, toka Peramiho Hospitali mpaka njia panda ya kwenda Mbinga. Kijiji kimoja kiitwacho Lipokela. Na baadaye kurudi.
Sasa yeye kwa kuwa alikuwa hajui kiswahili na alitaka kujifunza. Basi alikuwa ana wasalimia ile GOOD MORNING!
Kwa mkato yaani MORNING na wale wazee wakawa wanamuuliza tukujibuje? Naye aliwaaambia mujibu MORNING. Basi wale akina BAMBU wakawa sasa ni kila mtu wakimuona asubuhi wanasema MONILE.... wanajibishana MINILEEE...Kisha wanamalizia TUWAONE....jibu lake ..YEOO..Yaani tumemwona leo mzungu ndiyoo.
Basi toka miaka hiyo mpaka leo WANGONI wanasalimiana hivyo. Ikiwa Asubuhi MONILE...MONILE ..TUWAONE BAMBU ...YEOOO
SIKU NJEMA NDUGU ZANGUNI!!!!
Sasa yeye kwa kuwa alikuwa hajui kiswahili na alitaka kujifunza. Basi alikuwa ana wasalimia ile GOOD MORNING!
Kwa mkato yaani MORNING na wale wazee wakawa wanamuuliza tukujibuje? Naye aliwaaambia mujibu MORNING. Basi wale akina BAMBU wakawa sasa ni kila mtu wakimuona asubuhi wanasema MONILE.... wanajibishana MINILEEE...Kisha wanamalizia TUWAONE....jibu lake ..YEOO..Yaani tumemwona leo mzungu ndiyoo.
Basi toka miaka hiyo mpaka leo WANGONI wanasalimiana hivyo. Ikiwa Asubuhi MONILE...MONILE ..TUWAONE BAMBU ...YEOOO
SIKU NJEMA NDUGU ZANGUNI!!!!
Friday, April 8, 2011
MAJINA YETU/LEO TUANGALIE MAJINA YA KISUKUMA!!!
Kuna wakati niliwahi kuandika kuhusu majina/vibongo vya wangoni. Kwa kujikumbusha zaidi au kwa wale waiowai kusoma basi ingia hapa .Utaona hayo majina na pia maoni ya watu. Na sasa leo katika upekuzi wangu nimekutana na majina ya wenzetu Wasukuma ebu angalia hapa napo, majina haya nimeyapata Jamii Foum.
Majina ya Kisukuma
1. Masanja Mawenge 2.N'kwabi N'gwanakilala 3.Rupondije Inuka 4.Mabula Nkwimba 5.Nyeunge Maneno 6.Budodi Nzobhe ya Siketi JidulamabambasiN'gwanangwa Masabhuda, Masumbuko, Wangaluke, Nchimika, Ng'wana Malundi, shindike Bunani Jidalu, Jidiku ikong'oro, Igunani Matanda, Isungangwanda Kidalu, 6: Sawaka Ng'wana gandila, Itendegu Jibinza, Shija, Mabura, Kasase, Nzungu, Midelo, Lufulo Ndama Nyangwaka Ndili, Lisolilo Ligasu, Kaswalala Buyonzi, Nyanzobe Mayunga, Ngw'ana Nh'wani, Jodoki Mpembele, Ngwizukulu jilala, nyanzala ng'wandu, mwanasabuni lushanga, manyilizu shiganga, kabadi madilisha, mashenene masagida, chenge saguda, pula kiheka, tabu lukelesha, ngasa ingombe, masanja malale, malila lushumbu, luhende mwanansale, Ngosha Magonya, Manyanza, Jongh'ela, Nkulukulu, Ngw'alali, Ngh'ungulu, Zanzui, Sanagu, Shushu. TUKUTANE TENA WAKATI MWINGINE!!!!!! IJUMAA NJEMA KWA WOTE!!!!
Thursday, November 12, 2009
TUSISAHAU LUGHA ZETU ZA ASILI/KINGONI:- MLYELELU = MLO/MILO
Mwenzenu leo nimetamni kweli kuongea kingoni hii ndio sababu nimeamua kuandika hapa:-
Mlyelelu
Mngoni ilya mara ppadatu kwa kuhwela, Kulawuka, muhi, kulalila. Vandu vangi vilya lukumbi lumonga tu kwa kuhwela. Lukumbi lungi lwa muhi ilya kwa kunonganonga vyakula videbevidebe ngita, liyawu, mbubudu, madonga, matevele, matoki, yembe matangamanga nk.
Kulawuka
Lukela pakuyimuka mungoni ilawuka. Pakulawuka ihopa wuji, lukumbi lungi ihopa wuji na kulyelela vimungulu au manyawu gatelekanu, au gayochanu, ama wuji na chimbwinya cha mayawu galovekanu au ga bundula. Ligono lingi ilawuka chimbala che vakuchipolosa huti. Kadeni vangoni valaukayi kilu, hinu ugali wa kulya kilu vikemela ngunguluku.
Ugali wa muhi
Ugali wa muhi vangi vilya lilanga pamuhana. Vandu vangi vilya he muhi, yitosha chevilawuka lukele. Vanu vangi vilya ugali lukela na kuhamba kumahengu mpaka chimihi nde pevilya ugali wa kulalila.
Ugali wa kulalila
Uwu nde ugali wa kuhambila kugana. Ndava ya mahengu ga muhi, lukumbi lwa kulya ugali wa kulalila nakumanyikana. Vangi vilya kwkona kulizwarara, vangi pakuyingila ngúku kugona, vangi kilu ya chitita.
Vyakulya vya Mngoni
Ugali: Chakulya cha kawaida cha mngoni ni ugali. Uvi ugali wa malombi, ugali wa mayawu gakondowoli au bundura. Uvi ugali wungi wa ulehi na ugali wa mapemba.
Wali: Kuna sambali zamahele za mpunga, ngita lingwindimba, kula na bwana, faya, bungare, sindano nk.
Ugali ama wali vilyelela likolo ngita, nyama, likolo la manyahi, ngowani, ngundi, chipele, mangatungu, chikandi, chimbondi, mawungu, madede, mbeleveta nk.
Ugali vibakulila mchiheneku au mulupalu na likolo vibakulila mu mkere. Vilya ugali kwa mawoko au kwa lukorombi. Vyakula vingi nde ngita mdojolela, mbatata, vingovi, maboga makumbu, nk.
Naona niishia hapa kwa leo mmmmhhh roho yangu imefurahi kuandika hapa ni kama nimeongea na mtu ana kwa ana. Raha jipe mwenyewe mwaya.
Mlyelelu
Mngoni ilya mara ppadatu kwa kuhwela, Kulawuka, muhi, kulalila. Vandu vangi vilya lukumbi lumonga tu kwa kuhwela. Lukumbi lungi lwa muhi ilya kwa kunonganonga vyakula videbevidebe ngita, liyawu, mbubudu, madonga, matevele, matoki, yembe matangamanga nk.
Kulawuka
Lukela pakuyimuka mungoni ilawuka. Pakulawuka ihopa wuji, lukumbi lungi ihopa wuji na kulyelela vimungulu au manyawu gatelekanu, au gayochanu, ama wuji na chimbwinya cha mayawu galovekanu au ga bundula. Ligono lingi ilawuka chimbala che vakuchipolosa huti. Kadeni vangoni valaukayi kilu, hinu ugali wa kulya kilu vikemela ngunguluku.
Ugali wa muhi
Ugali wa muhi vangi vilya lilanga pamuhana. Vandu vangi vilya he muhi, yitosha chevilawuka lukele. Vanu vangi vilya ugali lukela na kuhamba kumahengu mpaka chimihi nde pevilya ugali wa kulalila.
Ugali wa kulalila
Uwu nde ugali wa kuhambila kugana. Ndava ya mahengu ga muhi, lukumbi lwa kulya ugali wa kulalila nakumanyikana. Vangi vilya kwkona kulizwarara, vangi pakuyingila ngúku kugona, vangi kilu ya chitita.
Vyakulya vya Mngoni
Ugali: Chakulya cha kawaida cha mngoni ni ugali. Uvi ugali wa malombi, ugali wa mayawu gakondowoli au bundura. Uvi ugali wungi wa ulehi na ugali wa mapemba.
Wali: Kuna sambali zamahele za mpunga, ngita lingwindimba, kula na bwana, faya, bungare, sindano nk.
Ugali ama wali vilyelela likolo ngita, nyama, likolo la manyahi, ngowani, ngundi, chipele, mangatungu, chikandi, chimbondi, mawungu, madede, mbeleveta nk.
Ugali vibakulila mchiheneku au mulupalu na likolo vibakulila mu mkere. Vilya ugali kwa mawoko au kwa lukorombi. Vyakula vingi nde ngita mdojolela, mbatata, vingovi, maboga makumbu, nk.
Naona niishia hapa kwa leo mmmmhhh roho yangu imefurahi kuandika hapa ni kama nimeongea na mtu ana kwa ana. Raha jipe mwenyewe mwaya.
Saturday, October 11, 2008
LIZOMBE NGOMA YA WANGONI
Subscribe to:
Posts (Atom)

