Thursday, November 30, 2017

Tuesday, November 28, 2017

KUMBUKUMBU. ...BISI

Nimekumbuka sana chakula hiki. Ukiweka na chumvi...kuteremshia ni kikombe kikubwa cha maji.....

Monday, November 27, 2017

TUMALIZE JUMATATU YA MWEZI HUU WA KUMI NA MOJA KWA MTINDO HUU....UREMBO WA ASILI

 Heleni ....ambazo ni kazi za mikono ya watu kwa ubunifu safi  kabisa
Na hapa ni pia ubunifu mzuri kabisa wa viatu/sandosi. 
NAPENDA KUCHUKUA NAFASI HII NA KUWATAKIENI WOTE MTAKAOPITA HAPA JUMATATU NJEMA SANA NA OMBI LANGU NI KWAMBA TUDUMISHE UTAMADNI WETU....Kapulya wenu...!

Thursday, November 23, 2017

NDUGU ZANGU:- TUTAFARI KWA PAMOJA MALEZI YA WATOTO WETU

 

Ukimkosoa sana mtoto na kumkaripia mara nyingi unampunguzia ujasiri na uwezo wa kujitegemea awapo mtu mzima.
Msaidie kwa upole, muelekeze, mtie moyo, akikosea mweleze jinsi Mungu anavyoumia kwa kosa alilolitenda.
Usimwambie kuwa hana jema hata moja hasa akiwa binti, maana siku moja kuna vijana wataona jema lake na watamwambia kisha ataweka USIKIVU Wake kwao.
Muombee mwanao/wanao, Mfundishe/wafundishe kuomba mwenyewe/wenyewe  Bwana atamsaidia/wasaidia.
Hii ni pamoja kumchapa mtoto viboko, ni kumwongezea usugu tu 

Wednesday, November 22, 2017

MSIMU WA BARIDI ....THERUJI YA KWANZA KUANGUKA KUONA NYASI TENA MPAKA MWEZI WA NNE:-(

Leo huku nje ni kimbembe thuriji imeanza kuanguka juzi, lakini leo ndo kwanza inazidi na upepo juu....Ni taarifa tu kwa ufupi. Nawatakieni siku njema.

Monday, November 20, 2017

NI WIKI NYINGINE NA JUMATATU NYINGINE...TUANZE WIKI NA PICHA HII YA KITAMADUNI KABISA

Wanawake  wakitwanga  nimekumbuka mbali sana  nilikuwa nikipata shida sana kutwanga watatu au wanne....:-)

Wednesday, November 15, 2017

Tuesday, November 14, 2017

NIMEKUMBUKA MKAO HUU NA PIA KUJUMUIKA NA KULA KWA PAMOJA

Nimekumbuka miaka hile ya mwaka -47 wakati watu tulikuwa tunakaa kwa pamoja na kula tena sahani moja. Siku hizi  ni marachache sana kuona hii. Kwa kweli inanisikitisha

Friday, November 10, 2017

NAWATAKIENI MWISHO WA JUMA UWE MWEMA

Binafsi nafurahia taswira hii ya Moshi...ebu angalia Mlima wetu Kilimanjaro unavyoonekana....MWISHO MWEMA WA WIKI.

Wednesday, November 8, 2017

KOCHI LA LILILOTENGENEZWA KWA MITI NA KAMBA ZA KATANI.....!

Tudumishe utamaduni wetu na kuyaenzi na mambo yetu ya utamaduni wetu. Nimependa hii kochi.

Tuesday, November 7, 2017

LEO NIMEKUMBUKA ZILIPENDWA


Hakika nisikilizipo miziki aina hii nakuwa na furaha ya pekee maana mtu waweza kusikiliza na kujifunza kitu ...JUMANNE NJEMA WAPENDWA WA ZILIPENDWA.

Monday, November 6, 2017

JUMATATU HII YA KWANZA YA MWEZI HUU TUANZE NA UASILI...MAVAZI YA ASILI

Tubadilike sasa,  tuthamini utamaduni wetu, tuachane na hisia za kimwili, turudi katika utamaduni wetu wa asili ya mwafrika, tukumbuke mavazi yetu ya asili kama ilivyo pichani ili tudumishe mila na desturi zetu

Wednesday, November 1, 2017

NASHANGAA MARA HII TUNAANZE MWEZI MPYA NAMI NIMEONA TUANZE MWEZI HUU KIHIVI...

Mdada anashanga utadhani anatoka usingizini ...lakini hapo ni kwamba anashanga kumbe leo ni mwezi mpya....natumaini wenzangu hajashangaa kama mimi Kapulya....
PANAPO MAJALIWA...