Showing posts with label hali ya hewa. Show all posts
Showing posts with label hali ya hewa. Show all posts

Monday, December 28, 2015

PALE HALI YA HEWA INAPOBADILIKA...LEO ASUBUHI ILIVYOKUWA/DET SNÖAR!

Mila na desturi au nisema ni mazoea ya nchi nyingi za Ughaibuni/ulaya siku ya Krismas kuwa na thaluji yaani kweupe huko nje lakini krismas hii haikuwa hivi hasa Swedan badala yake theluji imeanguka jana 27/12 mpaka leo 28/12 na kamera ya maisha na mafanikio imebahatika kupata picha hizi kama uonavyo...
Wakati mwingine ni safi kuacha gari na baiskeli na hapo ndipo utakapofaidi mambo angalia hii picha  hapa nilikuwa nikitoka mazoezi ya asubuhi:-) pia ni vizuri kutembea/kimbia na kamera......

 Basi nikalipokaona hako kajua nikaanza kuimba kala kawimbo ka mchakamchaka ....Jua lile...nikabadili nikaanza kuimba Idiamini akifa mimi siwezi kulia......Kama nilivypsema Ujenzi unabana ila leo nimepata kamuda...na pia sasa nitapumzika kidogo na ujenzi mpaka huu mwaka uishe ndo tutaendelea...Bado siku 4-3½ hivi kuufikia mwaka  mpya...TUOMBEANA  ILI TUWEZE KUUONA ...NI MIMI KAPULYA WENU!!


Sunday, January 12, 2014

JUMAPILI YA LEO HALI YA HEWA ILIKUWA HIVI, KWANGU MIMI NAWEZA NIKASEMA HALI YA HEWA IMECHAFUKA.....BARIDI -10C...HAPA BAADHI YA PICHA NILINASA LEO

 Kuanzia jana asubuhi mpaka leo bado theluji inaanguka tu ebu angalia hapa ukiangalia kwa makini sana kushoto kwako ni lile enoa ambalo tumezoea kuiona bustani ya Kapulya lakini sasa mmmhhh! haiwezekani kabisa ....hata hivyo ni lazima kutoka nje ingawa ni -10C huko nje....angalia hapa ....

 ...hapa tupo nje ni siku ya wazazi na watoto wao kuwa nje kwa vile ni siku maalumu kwa darasa la binti yetu. Ni kwamba wamepata na wageni kutoka Colombia kutokana na darasa lake kusoma lugha ya spanish wao walikuwa kule Colombia mwaka jana na sasa waColombia wamefika hapa  juzi. Kwa hiyo wazazi na watoto ni jambo la muhimu kuwapokea wageni na kuwaonyesha nini kufanya...ila duh! wameshangaa kwani ni baradi mno ...hata hivyo wanafurahia hali hii.
Mama maisha na Mafanikio alivovalia tayari kwa kupambana na baridi ya leo lakini, wee bwana haikuwa joto vidole vilikufa ganzi kabisa  hata kama ningeenda kwa daktari na kuchomwa sindano nisingesikia maumivu...Si ajabu kuonekana kama tembo maana mtu unajitahidi  kuvaa nguo nzito ila kuepukana na baridi.....Hiii ndio JUMAPILI YANGU YA LEO..PANAPO MAJALIWA TUTAONANA TENA. JUMAPILI NJEMA KWA WOTE.


Monday, December 9, 2013

TUANZA WIKI HII NA TAARIFA HII/BUSTANI MPAKA MWAKANI MWEZI WA SITA :-(

 Hapa ilikuwa mwezi wa sita-tisa mwaka huu ..ni kutoka tu nje na kuchuma mboga na kula ......
THELUJI IMEANZA
Na sasa eneo hilo hilo leo linaonekana hivi. Inabidi nisubiri mpaka mwakani mwezi wa sita tena. Kaaazi kwelikweli....mmhhh labda nitumie makopo sijui?? Je mna ushauri wowotw ule?

Monday, December 3, 2012

HIVI NDIVYO HALI YA HEWA ILIVYOKUWA FINLAND LEO!!!

Hali ya leo Finland...hapa kwetu bado haijaangua kihivyo ila kuna baridi kali sana kiasi kwamba ile kutoka tu nje pua inasinyaa kabisa....Mwaka huu itakuwa kali kwelikweli...JIONI NJEMA KWA WOTE.....

Friday, September 7, 2012

PALE HALI YA HEWA INAPOBADILIKA /UPWEKE UNAINGIA PIA!!!

 Sasa ndio ule wakati baridi inaanza kunyemelea. Kama uonavyo katika picha majani siyo ya kijani tena isipokuwa ni njano njano. Höst "majira baridi ya kuputika majani"na baada ya hapa kutakuwa na baridi zaidi theruji..brrrrriii. Na sasa  kwa watu waliozoea kujichanganya  ni ngumu sana hakuna mtu/jirani anaonekana nje. Kaaazi kwelikweli..NIWATAKIENI MWISHO WA JUMA MWEMA..TUKISHIRIKIANA/UNGANA TUTAFANIKISHA TU.

Saturday, July 21, 2012

KATIKA MAISHA KUPUMZIKA NI MUHIMU/RAHA JIPE MWENYEWE!!!!

Unapokuwa na mapumziko ya siku mbili tatu hivi kabla hujapata likizo kamili basi unakimbia na kujificha hapa (SUMMER HOUSE/SOMMARSTUGA). Mahali ambapo unaweza kupumzika tu hakuna eti ngoja niangalia mtandaoni kuna nini HAKUNA.
Na ukitokwa na jasho au ukijisikia uchovu basi ni kujitupa tu majini huna haja ya kwenda mbali kutafuta maji.......

 Ila kula ni muhimu ..akina mama wapo jikoni, na hapo ni mzee wa nyumba na pia ni raha kufikiwa na wageni aliyevaa kofia ni mgeni wetu mzee Masawe.......

 ...Wanapofika wageni ni raha kwani siku hii nilipata zawadi ambayo nilikuwa naitamani siku nyingiiiiii:-) Hiyo hapo juu UTAMADUNI !!!

 Tunapojisikia hamu ya samaki basi ni kuchukua boti na kwenda  kujaribu...wavuvi wadogo haoooo  wanakwenda kutafuta kitoweo....
Baada ya muda wanarudi mikono mitupu hakuna kitoweo...hivi ndivyo ilivyokuwa siku mbili/tatu nilipokuwa kimya...NAWATAKIENI WOTE JUMAMOSI NJEMA.....KAPULYA:-)

Thursday, September 29, 2011

WAKATI WA WATU KUNUNA UNAKARIBIA, VICHEKO VYOTE NA TABASAMU VYA SUMMER VYAFIKIA UKINGONI!!!/HÖST/AUTUMN = MAJIRA YA BARIDI YA KUPUKUTIKA MAJANI BRRRR!

Mmmmh! Kazi inaanza sasa. Kaziiiii kwelikweli, maana mtu unavaa nguo na mwisho unaonekana kama una kilo elfu kumi. Haya ngoja niache.

Ila pia ni wakati mzuri sana hasa miti inapopata rangi nzuri kama huu hapo juu inapendeza kusema kweli...Tatizo humwoni mtu ...pia ni kipindi kizuri kwenda mstuni kuchuma uyoga ila unatakiwa kujisitiri kweli .... huu mti rangi zake nipezipenda sana ila muda si mrefu majani yote yatapukutika na kuuacha na vijiti tu au mti unakuwa "uchi":-(


Wednesday, November 10, 2010

Brrrrrrr! Msimu wa baridi umeanza/theluji imeanza kuanguka tangu jana jioni na inaendelea!!!

Sasa kimeanza kipindi kile cha baridi theruji imeanza kuanguka tangu jana jioni hapa ni leo asubuhi saa moja na nusu hivi. Yaani hapa kaazi kwelikweli natamani ningekuwa napigiwa na jua....
Na hapa babu Erik anajiandaa kwa kwenda shule na baiskeli yake. Ni saa mbili kasorobo asubuhi hii.

Hapa saa tatu asubuhi. Mmmm baridi we acha tu.


Na hapa mzee wa nyumba naye anaaga ni saa tatu na nusu kuelekea anakowajibika.



Wednesday, October 1, 2008

TABIA TA NCHI ( Yaani joto upepo mvua n.k) CLIMATE

Hali ya hewa inabadilika nchi anzazo miaka ya zamani kulikuwa na baridi (theruji) nyingi sasa ni joto. Kiasi kwamba mimea ya afrika inastawi ughaibuni wakati wa baridi kali.
Jambo jingine ambalo ni muhimu sana ni kwamba watu wanakata miti juu ya mlima kilimanjaro na halafu hawapandi mingine.Hii inasababisha kuyeyuka kwa ile theruji iliyopo pale kileleni. Labda niseme kwa ujumla si vizuri kukata miti sehemu yoyote na kuacha bila kupanda mipya. Tusisahau ya kwamba ni muhimu tukate na tupande miti tena.

The Gulf Stream hii ina nguvu sana na inahakikisha hali ya hewa iwe joto kiasi. Inasemekana katika bara la Ulaya kama barafu itayeyuka basi maji yote ya baharini The Gulf Stream itazuia. Kwa hiyo The Gulf Stream inasaidia kwa bara la Ulaya kuwa na joto.

Inasemekana mwaka 2010 Ughaibuni itakuwa na baridi kama Sibiria na Afrika Mashariki kutakuwa na ukama. Kwa hiyo itabidi tuhamie katika Sayari nyingine au tupunguze dioksidi ya kabon (CO2) . Na hii ni haraka inabidi tuanze sasa.