Friday, September 29, 2017

TEMBO ZAIDI YA LA KI MOJA WAMEUAWA KATIKA HIFADHI YA SELOUS MKOANI RUVUMA


Hayo yamebainishwa katika maadhimisho ya siku ya tembo kitaifa katika mji mdogo wa LUSEWA wilayani NAMTUMBO mkoani ruvuma katika pori la hifadhi ya wanyama pori SELOUS

Thursday, September 28, 2017

HII IWE PICHA YA WIKI....KATIKA WANYAMA NIWAPENDAO TWIGA NI NAMBA MOJA....

Wiki inakaribia kwisha sasa leo ni ALHAMIS nami nimeona hii iwe picha ya wiki hii sio mbaya kama ikiwezekana kufanya utalii wa ndani ili kupumzisha akili...
Chanzo cha picha ni kutoka kwa blog ya Mjegwa.  PANAPO MAJALIWA TUTAONANA. UJUMBE: TUKUMBUKANE SISI  SOTE NI WANANDUGU

Monday, September 25, 2017

WIKI HII TUANZE NA ZILIPENDWA KWA NJIA YA UJUMBE WA MZIKI


NAWATAKIENI WOTE MWANZO MWEMA WA SIKU AMBAYO KILA WIKI INAANZA NA JUMATATU:-) KAPULYA WENU.

Friday, September 22, 2017

BLOG YA MAISHA NA MAFANIKIO IMECHAGUA HII PICHA IWE PICHA YA WIKI

Napenda kuwatakieni wote mtakaopita hapa mwanzo mwema wa mwisho wa wiki tusisahau kutakiana hali, kwani salamu ni nusu ya kuonana...PANAPO MAJALIWA TUTAONANA TENA AMANI NA FURAHA ITAWALE MIOYONI  MWENU. MNAPENDWA WOTE!

Thursday, September 21, 2017

MAZINGIRA NA BARABARA ZAKE MKOANI RUVUMA....TUTAFIKA KWELI?


Barabara ya Lituhi-Songea yafungwa  na wananchi wa Ruanda kwa sasabu ya vumbi za magari.....

Wednesday, September 20, 2017

TUKUMBUKE ZAMANI:- HISTORIA YA TAIFA LETU KATIKA PICHA.......

DAR ES SALAAM:- WANAWAKE WAFUNGWA WAKITENGENEZA BARABARA
ASKARI WAPO KATIKA GWARIDE  KATIKA HOSPITAL YA OCEAN ROAD 

Tuesday, September 19, 2017

VITU VYA ASILI NI BORA ZADI KULIKO VYOVYOTE VILE...TUVITHAMINI...NI KAZI ZA MIKONO YETU TUKUMBUKE

 MIKOBA YA ASILI
BANGILI
TUDUMISHE UTAMADUNI WETU/VITU VYETU VYA ASILI ILI KIZAZI KIJACHO KIJE KUJUA HAYA. NAWATAKIENI KILA LA KHERI...

Monday, September 18, 2017

WIKI HII NI WIKI YA KUMBUKUMBU: ANGALIA HIINIMEIKUTA KWA MDOGO WANGU KOERO MKUNDI AKISEMA, DADA YASINTA NIMEISHITUKIA JANJA YAKO....ENDELEA

Dada yangu akiweka mikakati
Kwa dada yangu Yasinta,

Nimesikitishwa sana na kile ulichobandika katika blog yako ukidai kuwa wewe hutaki kuwa mwanaharakati wa kututetea sisi wanawake na watoto zetu, kama nilikunukuu vizuri umesema kuwa kuandika kwako makala za kutetea haki za wanawake sio kwamba unayo dhamira ya kuanzisha NGO.

Umedai kuwa hujawahi kuota na wala kuwaza kufanya kazi hiyo, bali unaamini kwamba, kuwa mwanaharakati haimaanishi kuwa na Organization. Kwamba huwezi kuwatetea wanawake na watoto isipokuwa mpaka uwe na NGO.

Pia ukabainisha kuwa umeamua kuweka mambo hadharani maana kuna vimbelembele washaanza kujifanya yule shehe wa Mwembe chai aliyetabiri kuwa mwana CCM yeyote atakayechukua fomu za kutaka kugombea urais kwa kumpinga Rais wa sasa Muheshimiwa Kikwete basi atakufa ghafla kwa kubanwa na ngiri. Vimbelembele hao wamekutabiria kuwa kwa kuandika kwako vimakala vya kujifanya una huruma sana na wanawake wanaonyanyaswa na waume zao ni kamchakato kako ka kuelekea kuanzisha Organization ya kuwatetea wanawake nchini.

Duh! Samahani dada nilisahau kukupa heshima yako. Nakupa shikamoo zako wewe na mumeo. Habari za huko ughaibuni mlipo, nasikia kuwa kuna baridi sana kiasi kwamba mabarafu yamejaa kila mahali mpaka chooni. Samahani kwa kutaja chooni, nimesahau kuwa hilo sio neno la kistaarabu, nilikuwa namaanisha toilet.

Dada kama nilivyoanza katika utangulizi wa barua hii, ni kwamba nimeishitukia janja yako. Unajua tangu uhamie ughaibuni dada umekuwa na akili sana.

Sio wewe mwaka juzi ulipokuja huku nyumbani ulianzisha NGO ya kutetea haki za wanawake na watoto kwa kushirikiana na yule binamu yako anayezaliwa na yule shangazi, ambaye analazimisha undugu baada ya kusikia kuwa umeolewa na mzungu kwa kudai kuwa eti zamani alikuwa akimbeba baba yako wakati bibi na babu yako wakienda shamba.

Huyu binamu yako ambaye inasemekana alifeli zaidi ya mara saba kuingia kidato cha pili huko Songea katika ile shule iliyoko pale Mfaranyaki, karibu na ule muembe dodo unaotumiwa na mafundi baiskeli ndiye uliamua kumshirikisha kuanzisha NGO yenu wenyewe ambayo mliipa jina la Ruhuwiko NGO for woman and children crying everyday.
Taasisi hiyo ambayo imesajiliwa na katibu kata ilikuja kwa kasi ya ajabu na inatishia kuvunja ndoa za watu, na mojawapo ya ndoa iliyovunjika ni ile ya yule mzee Ngatura mwenye wake saba.

Ndao iliyovunjika ni ya yule binti machepele wa saba kuolewa na yule mzee. Nadhani unamkumbuka yule binti aliyewahi kufumaniwa na mke wa mwalimu wa kufundisha ngoma za asili pale shuleni, na kutokana na umahiri wa kucheza lizombe yule binti alipewa Umanju wa kuongoza ngoma na mwalimu na kutokana na kupewa cheo hicho mwalimu wa ngoma akamgeuza kuwa kijumba kidogo chake na makutano yao yakawa kule kwenye shamba la kijiiji, na kama unavyojua wambea wa kijiji wakamjuza mke wa mwalimu wa ngoma na hivyo kuwekewa mtego na kufumaniwa. Si unakumbuka jinsi alivyopigwa mpaka akachaniwa nguo zote? Basi kutokana na aibu si ndio akahamishiwa katika shule ya jirani na baba yake ili kukwepa aibu.

Basi huyu binti baada ya kuachika huku akiongozwa na binamu yako wanataka mali za yule mzee zigawanywe sawa kwa sawa la sivyo kesi inapelekwa mahakaam kuu.
Hivi ninavyo kuandikia kuna mashauri zaidi ya wanawake 30 wanaotaka kuachana na wanaume zao kwa kutegemea kugawana mali walizochuma na wanaume zao. Kampeni hiyo ya kuachanisha wanandoa inaongozwa na hiyo NGO yenu na anayeingoza uasi huo wa kuvunja ndoa za watu ni huyo binamu yako.

Hivi sasa hali ni tete pale kijijini na wazee wa kijiji wameitisha kikao cha dharura kujaldili hali hiyo na wanatishia kuchangishana nauli ili waje Dar kumuona muheshimiwa rais ili anusuru ndoa zao zinazoelekea shimoni. Pia wanataka binamu yako huyo aondolewe haraka pale kijijini kwa ile staili ya kuwekewa karantini asikanyage tena pale kijijini iwe ni kwa sherehe au misiba.

Hata hivyo katika utetezi wake binamu yako huyo amejitetea kuwa eti hiyo kampeni ya kuachanisha ndoa za watu ni idea yako yaani kwa kiingereza suggestion yako maana alidai kuwa yeye siye msemaji mkuu wa hiyo NGO, bali ni mtekelezaji wa kile unachokiagiza ukiwa huko ughaibuni.

Sasa dada kwa kutaka kutuchota akili unajidai kuwa hutaki kuwa mwanaharakati wakati tayari ulishakuwa mwanaharakati tangu mwaka juzi. Kwa kuwa unatafuta umaarufu ili kutengeneza mazingira ya kupanua wigo wa hiyo NGO yako kutoka kijijini hadi kuwa NGO ya kitaifa baada ya kuona kule Ruhuwiko umeanza kupoteza umaarufu na ndio maana unataka kupata maoni ya wasomaji wako katika ile staili ya mchomeko, yaani ku bip kwa kiingereza.

Dada samahani naomba univumilie kwa haya ninayoyasema maana mie sitaki uje kuumbuka baadae, kwani Dar es salaamu sio sawa na Ruhuwiko, huku kuna ushindani wa hii biashara ya NGO, usipoangalia utatapeliwa wewe, kuna watu huku ni wasanii ile mbaya, anaweza kuja mwanamke akajidai amegombana na mumewe, na akipata msaada huyooo anaenda kuendelea na ndoa yake kama kawaida. Ukitaka kupanua wigo wa NGO yenu ihamie huku Dar inabidi utafute mganga ambaye anaweza kumwangalia mteja akajua kama huyu ana matatizo kweli au msanii tu.
Dada huku Dar NGO ni mradi wa watu wajanja ambao hutumia staili ya matatizo yenu ndio tijara yetu, na wengi wao ni wale walioshindwa kutofautisha ile dhana kujiajiri na kujitolea. Kwa wao kuitolea maana yake ni kuwekeza kwa kutumia matatizo ya wengine.

Yaani siamini kuwa na wewe umeingia katika kamtindo hako kwa kutafuta fedha kwa kutumia matatizo ya wengine. Nashawishika kuamini kuwa na wewe umefulia kimawazo, kwani hiyo mbinu yako nimeishitukia dada. Hapa Dar humpati mtu labda Kamala na Chacha kwani nao eti ni wanaharakati wa kuwatetea vijana…….LOL

Kwa leo naomba niishie hapa nikipata muda nitakujuza mengi juu ya NGO za hapa Dar.

Nakutakia siku njem

Friday, September 15, 2017

ZILIPENDWA KWELI NI DHAHABU...VAZI LA MAUA-MAUA NA MKANDA JUU....

Nimekumbuka sana zamani...ebu angalia hii picha. Sijui ilikuwa ni mtindo kusimama kwenye miti au maua..? Maana nimejiuliza hata jibu sijapata.  Na pia mtindo wa nyweleJe? mnamfahamu huyu mdada?
IJUMAA NJEMA KWA ATAKAYEPITA HAPA!

Thursday, September 14, 2017

PICHA MOJA MWONEKANO TOFAUTI...SWALI JE? MWONEKANO UPI WAMFAA DADA HUYU?

Kwanza ilikuwa hivi ....



Baadaye dada yangu Mariam akaona kuna vitu vinakosekana  kama uonavyo  alivyoorodhesha katika picha....
Miaka imepita na jana ndipo nilipotumiwa hii picha kwa mfano huu. Hakika sikuitambua kabisa. Na bado sijitambui  maana hiyo si tabia yangu...Je wewe msomaji unauonaje huu mfano wa hii picha ya Kapulya ya mwisho?
NAWATAKIENI JIONI NJEMA KWA WALE WATAKAOPITA HAPA KIBARAZANI....KAPULYA MDADISI WENU

Tuesday, September 12, 2017

VYAKULA AVIPENDAVYO KAPULYA WENU ...AU KUNA MWINGINE ANAPENDA KAMA MIMI??

NI WALI NA KUNDE...KWETU UNGONINI TWAITA (NGUNDI MANGI)
Baada ya chakula nilipenda sana haya matunda ...kwa mara nyingine tena kikwetu twaita MADONGA....
Nikikosa hivyo basi nakula uyoga....Je wewe kuna chakula hujala siku nyingi na sasa watamani kukila? Nawatakieni wote jioni njema!!!

Monday, September 11, 2017

NI SIKU NYINGINE PIA WIKI NYINGINE NA NI JUMATATU....

Nawatakieni siju hii ya Jumatatu na wiki hii iwe yenye furaha na amani...pia nawatakieni yote mtakayofanya yawe yenye mafanikio mazuri.  PANAPO MAJALIWA TUTAONANA TENA !

Wednesday, September 6, 2017

SOKONI SONGEA... KUMBUKUMBU

Bado tuangalie Songea kwetu kama muonavyo hapa ni nje ya soko kuu la Songea.... TUONANE TENA WAKATI UJAO.

Tuesday, September 5, 2017

Monday, September 4, 2017

TUANZE WIKI HII NA NENO FURAHA: HIVI KWANINI KUN SIKU MTU HUKOSA FURAHA?


Ndiyo...Furaha inatokana na ridhiko la ndani la mtu bila kuhusisha vitu vya nje. Mtu akishajua namna sahihi ya kuipata furaha basi hataipoteza kamwe. Yoyote anaeipoteza furaha huyo anakuwa anaitafuta nje yake kwenye mazingira ya nje.....
Lazima atakuja kuikosa siku moja kwasababu mazingura ya nje sio rafiki sana na binadamu kwasababu hubadilika badilika....

Mfano kuna wakati wa jua, masika na kiangazi za kawaida...
Kama umepanga kwenda kulipwa mapato yako fulani na umewekeza furaha yako kwenye hela halafu mvua ikanyesha lazima tu furaha yako itapotea....
Kuridhika kwa ndani kuna maana ya kujikubali jinsi ulivyo bila kutegemea hali ya nje iko namna gani...
Utakapo jikubali namna ulivyo kamwe hutajutia wala kukosa furaha hata siku moja

Saturday, September 2, 2017

UJUMBE WA LEO:- KILA AITAZAMAYE KESHO YAMPASA KWANZA AIMALIZE LEO:- ACHA NIKUDOKEZE JUU YA MAISHA YA LEO...

1.Ishi kwa UPENDO usio na Unafiki.
2.Ishi na FURAHA isiyo na mipaka.
3.Ishi kwa AMANI na kila Mtu.  
4.Usiweke MAMBO yako wazi kwa kila mtu kwani binadam hatufanani.
5.Jiheshimu kwani HESHIMA yako inatokana na jinsi ulivyo.
6.Kuwa MVUMILIVU katika kila jambo ili kufikia mafanikio.
7.Weka MSAMAHA mbele kwa kila anaekukosea na unaemkosea.
8.MISUKOSUKO ni sehemu ya maisha na ndio hatua ya kuvuka ili kufanikiwa katika MAISHA hivyo usikate tamaa.
9.Omba na kumshkuru MWENYEZI MUNGU kwa kila jambo kwani yeye ndiye anayekupa UHAI.
TUMALIZIE NA WIMBO HUU ....