Showing posts with label chai. Show all posts
Showing posts with label chai. Show all posts

Sunday, July 13, 2014

TUANZE JUMAPILI HII NA KIKOMBE CHA CHAI...NINYIME VITU VYOTE LAKINI SIO CHAI!!!

You´re Just my Cup of Tea,
Our Love Warms my Heart.
Najua wote mnajua mie ni mpenzi sana wa chai tena ile isiyo na sukari(Chingambu) :-).
BASI NIWATAKIENI WOTE JUMAPILI NJEMA SANA. UPENDO NA AMANI ITAWALE KATIKA NYUMBA ZETU.

Sunday, November 24, 2013

HIVI NDIYO ULIVYOKUWA MLO WA ASUBUHI YA JUMAPILI YA LEO /CHAPATI KWA CHAI!!

 Chapati zinasukumwa huku chai ikiandaliwa
 chapati zinakaangwa
 chapati tayari kwa kuliwa
Na hivi ndivyo meza ilivyoandaliwa Jumapili hii ya leo. Chapati bado zipo na chai pia karibuni kujumuika nasi. NAWATAKIENI WOTE MTAKAOPITA HAPA JUMAPILI YENYE BARAKA NA UPENDO. MWENYEZI MUNGU NA AWE NANYI. AMINA......KAPULYA/KADALA.

Monday, August 12, 2013

TUANZE JUMATATU HII KWA MLO HUU WA ASUBUHI YA LEO CHAI CHAPATI ZA KUTENGENEZWA KWA MIKONO YANGU MIMI KAPULYA...!!

 Nimekumbuka nikiwa nimeshaanza kukaanga kuwaonyesha tangu mwanzo..ni hivi unahitaji unga wa ngano, chumvi kidogo, sukari kidogo, mafuta  na maji moto hivi nifanyavyo mimi .Unakanda unga na hivyo nilivyotaja na baadaye unasukuna na hapa chapati ikiwa kwenye flampeni inakaangwa 
Na hapa tayari zipo zinasubiri walaji, chapati, kuna chai ya rangi na ya maziwa na wale wanaotumia sukari ipo kwenye hichi kibweta cheusi kwa hiyo karibuni sana tujumuuke.JUMATATU NJEMA KWA WOTE.

Tuesday, April 16, 2013

KANGA YA VIKOMBE VYA CHAI...NIMEIPENDA HII KANGA!!!!!

Maandishi yanasema ISIKUHADAE RANGI TAMU YA CHAI NI SUKARI...Hivi ni kweli?

Wednesday, November 21, 2012

MARA YA MWISHO KULA CHAKULA/MAGIMBI ILIKUWA KIHESA -NJOMBE KWA CHAI YA RANGI

Hapa ni magimbi kabla hajamenywa na ....

....hapa tayari yamemenywa na kuchemshwa tayari kwa kula. Magimbi unaweza kula kama chakula cha asubuhi, mchana au jioni. Ila mimi nimeyatamani sana leo na ningeyale kama chakula cha asubuhi hii ya leo kwa....
.

......kikombe hiki cha chai ya rangi  ila sasa.... haya ngoja nile kwa macho. Je? wewe mara ya mwisho ni lini umekula magimbi?

Saturday, May 5, 2012

JINSI YA KUTENGENEZA CHAPATI..


Kuna msomaji wa Maisha na Mafanikio aliniomba kujua jinsi ya kutengeza "recipe" ya chapati . Maana kila yeye anapojaribu huwa haziwi kama atakavyo yaani laini. Ndugu msomaji naokuomba jaribu kufanya kama hapa kwenye hii video. Mie nimejaribu na nimefaulu tena leo asubuhi ndo ulikuwa mlo wangu kwa chai. NAKUTAKIE KILA LA KHERI NAJUA UTAWEZA NA UTAFURAHIA. JUMAMOSI NJEMA KWA WOTE ....

Sunday, February 5, 2012

JUMAPILI NJEMA...KARIBUNI CHAI KWA MIHOGO YA KUCHEMSHA!!!!

Mihogo ya kuchemsha.......
Na chai ya rangi

Karibuni tujumuika, mimi napenda zaidi mihogo ya kuchemsha. kuna wengine wanapenda ya kuweka nazi, karanga au nyanya na vitunguu. Je wewe unapenda mihogo yako itayarishweje? Haya ngoja niwatakieni wote jumapili njema sana. Mimi nakunywa chai yangu hapa maana baridi si mchezo!!!!

Friday, September 16, 2011

KARIBUNI KIKOMBE CHA CHAI...NINYIME VITU VYOTE LAKINI SIO CHAI!!!


You´re Just my Cup of Tea,

Our Love Warms my Heart.

Najua wote mnajua mie ni mpenzi sana wa chai tena ile isiyo na sukari(Chingambu) :-).

Kichwa cha habari hapo juu kinasema kuwa "NINYIME VITU VYOTE LAKINI SI CHAI" Duh ! naungama ni kwamba nimesema uongo kwani mimi ni mdhaifu/mpenzi sana wa smaki pia kama ilivyo kwenye chai......



Ngoja tusikilize wimbo huu wa Nuru ft Mr Chocolate Flavour - Muhogo Andazi!!!




NAPENDA KUWATAKIENI WOTE MWANZO MWEMA WA MWISHO WA JUMA ....MUWE NA AFYA NJEMA , AMANI NA FURAHA ZITAWALE NYUMBANI MWENU/WAKO.......IJUMAA NJEMA!!!!

Friday, November 5, 2010

DUKA LA MTANDAO

Habari njema kwa Ndugu zangu Watanzania mnaoishi nje ya Tanzania, Tumefungua Duka la Mtandao(Onlineshop) la kuuza Chai na Kahawa ya Tanzania tuu. linaitwa Chai & kahawa Online Shop(www.chaikahawa.com) na liko Stockholm, Sweden.tunaweza kuuza na kusambaza chai na kahawa kwa mteja yeyote aliyopo nchi yeyote duniani. wote mnakaribishwa Kununua na kujivunia bidhaa zetu.

Kwa Mawasiliano,Maoni,Ununuzi wasiliana nasi kwa kutumia email info@chaikahawa.com au piga simu,tuma ujumbe mfupi(sms) + 46762878341.

NB:website iko kwenye Flash, kama utapata tabu kuifungua download flash adobe

Wednesday, October 27, 2010

Chai inapunguza mshtuko wa moyo!!!

Unajua kuwa kunywa chai vikombe vitatu kwa siku au zaidi kunapunguza mshtuko wa moyo kwa asilimia 21. Haya jamani tunywa chai!!!!

Wednesday, February 10, 2010

Karibuni Wote Kikombe Hiki Cha Chai!!!!!

You´re Just my Cup of Tea,
Our Love Warms my Heart.
Najua wote mnajua mie ni mpenzi sana wa chai tena ile isiyo na sukari(Chingambu) :-).

Sunday, September 13, 2009

NAWATAKIENI JUMAPILI NJEMA KWA MLO HUU MTAMU WA NDIZI.


VIPIMO

Ndizi Mbivu 6
Nazi Kikopo 1
Sukari Vijiko 3 vya chakula
Hiliki Kijiko 1

NAMNA YA KUTAYARISHA NA KUPIKA

1) Menya ndizi kisha zipasue kati utoe ule moyo wa kati.
2) Zikate size unayopenda mwenyewe, kisha uzipange ndani ya sufuria.
3) Weka maji kiasi na uzichemshe ndizi kidogo, karibu ya kuiva mimina tui.
4) Mimina sukari na hiliki ndani ya ndizi na ziwache zichemke mpaka tui libaki kidogo.
5) Ziondoe jikoni na uziweke kwenye sahani tayari kwa kuliwa. Huu ni mlo wangu wa leo karibuni.

KIDOKEZO:

Ni nzuri sana kuliwa na kitu cha chumvi kama nyama ya kukausha au kuku wa kuchoma.

Sunday, March 15, 2009

KARIBUNI CHAI BORA+JUMAPILI NJEMA



Ukitaka kukosana nami basi ninyime chai, tena bila sukari hapo tutakosana sana. Kama wasemavyo wakati wowote ni wakati wa chai.