Showing posts with label mali. Show all posts
Showing posts with label mali. Show all posts

Tuesday, September 30, 2014

KAMA MNATAKA MALI!!!!


Nadhani wengi hasa mlio na umri wangu mnakumbuka kitabu hiki au vitabu hivi ya TUJIFUNZE LUGHA YETU. Leo nimekumbuka shairi hili...haya fuatana nami......

Karudi baba mmoja, toka safari ya mbali,
Kavimba yote mapaja, na kutetemeka mwili,
Watoto wake wakaja, ili kumtaka hali,
Wakataka na kauli, iwafae maishani.

Akatamka mgonjwa, ninaumwa kweli kweli,
Hata kama nikichanjwa, haitoki homa kali,
Roho naona yachinjwa, kifo kinanikabili,
Kama mwataka kauli, semeni niseme nini.

Yakawatoka kinywani, maneno yenye adili,
Baba yetu wa thamani, sisi tunataka mali,
Urithi tunatamani, mali yetu ya halali,
Sema iko wapi mali, itufae maishani.

Baba aliye kufani, akalibi lile swali,
Ninakufa maskini, baba yenu sina hali,
Neno moja lishikeni, kama mnataka mali,
Kama mnataka mali, mtayapata shambani.

Wakazidi kumchimba, baba mwenye homa kali,
Baba yetu watufumba, hatujui fumbo hili,
Akili yetu nyembamba, haijajua methali,
Kama tunataka mali, tutapataje shambani?

Kwanza shirikianeni, nawapa hiyo kauli,
Fanyeni kazi shambani, mwisho mtapata mali,
Haya sasa burianai, kifo kimeniwasili,
Kama mnataka mali, mtayapata shambani.

Alipokwisha kutaja, fumbo hili la akili,
Mauti nayo yakaja, roho ikaacha mwili,
Na watoto kwa umoja, wakakumbuika kauli,
Kama mnataka mali, mtayapata shambani.

Fumbo wakatafakari, watoto wale wawili,
Wakakata na shauri, baada ya siku mbili,
Wote wakawa tayari, pori nene kukabili,
Kama mnataka mali, mtayapata shambani.

Wakazipanda shambani, mbegu nyingi mbalimbali,
Tangu zile za mibuni, hata zitupazo wali,
Na mvua ikaja chini, wakaona na dalili,
Kama mnataka mali, mtayapata shambani.

Shamba wakapalilia, bila kupata ajali,
Mavuno yakawajia, wakafaidi ugali,
Wote wakashangilia, usemi wakakubali,
Kama mnataka mali, mtayapata shambani.

Wakawanunua ngómbe, majike kwa mafahali,
Wakapata na vikombe, mavazi na baiskeli,
Hawakuita pombe, sababu pombe si mali,
Kama mnataka mali, mtayapata shambani.

Wakaongeza mazao, na nyumba za matofali,
Pale penye shamba lao, wakaihubiri mali,
Walikiweka kibao, wakaandika kauli,
KAMA MNATAKA MALI, MTAYAPATA SHAMBANI.
NA HAPA NI MWISHO....!!!!

Wednesday, October 12, 2011

ETI MALI NI YA MWENYEWE?

Kipengele cha JUMATANO cha MARUDIO YA MADA, baada ya kuweka hiyo hapo ya kaka Kitururu nikawa natembea tembea tena mitaani nikakutana na hii hapa kaaazi kwelikweli ebu tujadili kwa pamoja hii nayo nimeikuta kijijini kwetu

Inaonekana kuwa mara baada ya kufa mfanyibiashara mkubwa basi aghalabu biashara hiyo huenda sawa.

Hivi majuzi nilipanda moja ya mabasi mabasi ya safari ndefu ambayo wakati wanaanza safari zao ilikuwa na huduma mbalimbali kama za kutoa maji, kuonyesha sinema/video, pipi, biskuti nk.

Huduma kwa wateja pia zilikuwa safi ambapo mlikuwa mwatangaziwa mlipofika na kadhalika. Nilishangazwa na hali ya sasa ya basi hili na nilipouliza nkaambiwa...'huna habari? Mwenye mali keshakufa so watoto ndo wanaoendesha kampuni'

Swali: kwani mwenye kampuni asipokuwepo ndo mambo yaende ndivo sivo?

Je yawezekana yatokeayo Tanzania kwa sasa ni kwa kuwa mwenye mali-Mwl. Nyerere-hayupo? Je kuna siku nasi biashara ya kulinda rasilimali zetu na kuiongoza nji vema ikawa swafi kama biashara nyingine?

Tuesday, October 19, 2010

Ataka talaka kwa nguvu ili aolewe na mwenye pesa


Mwanamke mmoja alitoa kioja baada ya kudai talaka kinguvu huku jamii iliyomzunguka ikimshangaa kwa kilichosemekana kuwa amepata mwanaume mwenye fedha.

Mwanamke huyo, alipokuja kwa wifi yake,kumueleza akamwambie kaka yake ampe talaka kwa kuwa alichoshwa na tabia zake,na kumuamuru akiwa hajampa talaka hiyo ataondoka hata kama hajapewa talaka.

“Mimi namuomba talaka kaka yako hataki kunipa ana maana gani? mimi simuhitaji tena nimechoshwa na dhiki mimi, anipe karatasi langu niondoke nyumbani kwake” na asiponipa naenda bakwata lazima aitoe” alifoka dada huyo kwa sauti bila hata aibu

Wifi huyo alijaribu kumuuliza alikosewa nini na kaka yake huyo, na swali hilo hakutaka kulijibu na kumueleza kuwa yeye anachohitaji ni talaka hahitaji maswali,

Hata hivyo mwanamke huyo ilifahamika na ndugu zake kuwa,alikuwa akitaka kuolewa na mwanaume mwingine ambaye alimuona atambadilisha kimaisha kwa kuwa ndugu zake hao alidai mwanaume huyo alikuwa na fedha zaidi ya mume wake wa sasa. Habari hii nimeipata Simon wa samvande