Showing posts with label ndoa. Show all posts
Showing posts with label ndoa. Show all posts

Thursday, May 18, 2017

MAMA HIVI ULIMPA MUNGU SHILINGI NGAPI?


Baada ya miaka saba ya ndoa bila kupata mtoto, Magreth alimuambia mumewe Benjamin kuwa atafute mwanamke mwingine wa kuzaa naye. Walishahangaika sana kuzunguka mahospitalini na kwa waganga wa kienyeji bila mafanikio.

Nyumba yao ilikua na amani na Ben alishakubaliana na ile hali, lakini ndugu zake walikua wanasumbua sana, walimtukana mkewe matusi mengi, wakimuambia kula, kulala anawajazia choo, walimnyanyasa sana na Mage hakuwa na raha.

Aliona njia pekee ni kumruhusu mumewe kuoa mwanamke mwingine ili angalau apate mtoto na ndugu zake waache kumsakama. Ben hakuwa tayari kuoa mwanamke mwingine, alikataa katakata lakini mkewe alisisitiza huku akitishia kuondoka kama asingeoa mke mwingine.

Siku moja Ben aliamua kuwaita ndugu zake wote, na wote waliitikaa wito  aliwaambia ana kitu kikubwa cha kuwaambia kwani na yeye alishachoka suala la mtoto na alitaka kufanya mamauzi makubwa. Wakiwa na shauku ya kujua ni nini walifika.

Ben aliwapokea vizuri na baada ya chakula Ben alimuambia mkewe akachukue begi liko kitandani. Ndugu zake walitabasmu wakijua mtoto wao kaamka na sasa anamfukuza mkewe ili atafute mke mwingine na kupata mtoto.

Mkewe alienda kitandani, alichukua begi kubwa na kulileta pale. Ndugu walikaa kimya, Ben alilichukua na kulifungua, lilikua limejaa pesa tu, noti za shilingi elfu kumi  zimepangwa vizuri.

Kila mtu alishangaa na hata mkewe alishangaa. Ben alianza kuongea. “Ndugu zangu nimewaita hapa kwa kuwa  nina tatizo kubwa nyie wote mna watoto Mungu kawabariki hata wewe mdogo wangu hapa ni mjamzito na Mungu akijaalia utajifungua salama.

Lakini mimi na mke wangu Mungu hajatubariki kuwa na  watoto” Alitulia kidogo huku akifuta machozi, yaliyotaka kudondoka. “Sasa nimewaita hapa mnisaidie kitu kimoja tu. Nianze na wewe Mama kwani kila siku umekua ukiniambia kuhusu mjukuu.

Aliongea huku akimgeukia Mma yake. “Chochote mwanangu…” Mama yake aliitikia kwa shauku. “Ninachotaka Mama ni kwamba uniambie ulimpa Mungu shilingi ngapi mpaka akakupa watoto…

Maana mimi nimejaribu imeshindikana, hizi ni hela zote nilizonazo benki na  kesho nitaongea na Dalali ili tuuze nyumba mimi na mke wangu tukapangishe lakini tupate mtoto.”

Alitulia kidogo, watu wote walimshangaa, lakini aliendelea. “Ndugu zangu nisaidieni, nyie mna watoto mlimpa Mungu shilingi ngapi au nini mlitoa, mlimuona wapi mkampelekea, mimi nipo tayari kutoa kila kitu katika maisha yangu ili tu na mimi niitwe Baba na mke wangu aitwe Mama.

Niambieni tu ni bei gani Mungu anapokea?” Wote walinyamaza kimya, hakuna aliyeongea tena, walimuangalia huku wakiangaliana kwa aibu. Hakuna aliyejaribu kunyanyua mdomo.

“Sasa ndugu zangu kama hamjui kiasi ambacho Mungu anapokea ili kutoa watoto basi sitaki kusikia tena hili suala. Mimi na mke wangu tuna furaha, sitaki mtuingilie, siku mkitaja mtoto mje mniambie anauzwa wapi na bei gani nitanunua!

Kama nyie mlinunua au ni wajanja sana mpaka mkampata nifundisheni huo ujanja….Mama…” Alimgeukia Mama yake. “Nakupenda sana lakini mimi sina uwezo wa kujipa mtoto, kama unajua Mungu anataka kiasi gani basi niambie ila kama na wewe hujui basi sitaki umsumbue mke wangu.

Kila siku mnampigia kelele kuwa hazai hazai hivi mnafikiri yeye hataki mtoto, mnafikiri yeye hataki kuitwa Mama, sasa mimi nimemaliza, hizi pesa narudisha ndani siku mkisikia Mungu anauza watoto basi niambieni nitakuja kununua la sivyo mtuache na ndoa yetu..”

Alimaliza kuongea, wote walitoka kimyakimya bila kuongea chochote. Tangu siku hiyo hakukuwa na maneno tena ya mtoto wala nini. Ben na mkewe bado hawajajaaliwa kupata mtoto, wameamua kuasili mtoto yatima na wanaishi naye kama mtoto wao na wote wanafuraha.

***** Imeandikwa Na. Iddi Makengo

Kabla hujamnyanyasa mtu kwa kitu ambacho hana uwezo nacho hembu jiulize wewe ulimpa nini Mungu mpaka akakupa hicho kitu?

 Kwani kuna watu ambao wanadhani kuwa Mungu anawapenda wao zaidi na wao ni bora kuliko wengine.

Tuesday, March 14, 2017

MAISHA:- BAADA YA KUISHI MIKA 60 SASA WAFUNGA NDOA

Mzee wa miaka 98 aoa bibi  wa miaka 88 baada ya kuishi pamoja muda wa miaka 60 huku wakichunguzana.
WAZO: NIMEPENDA UAMUZI WAO.

Wednesday, February 17, 2016

WOSIA WA BABA KWA BINTI YAKE

Aliyoyasema baba siku moja kabla bintie hajafunga ndoa....

Binti yangu, kuanzia kesho hutakuwa ukiitwa tena jina langu. Utakuwa na furaha kuolewa na mwanaume uliyempenda. Usinikumbuke sana mimi kwasababu nimeshatimiza majukumu yangu. Sasa ni wakati wa kutimiza majukumu yako.



Kuanzia utoto wako, nimekulea vema kwa neema za Mungu. Ila kabla hujasema mbele ya kasisi kuwa unakubali kuolewa ningependa nikueleze kuhusu kuishi na mwanaume na maisha ya ndoa kiujumla.



Unakumbuka ulivyokua umekaribia kufanya mtihani wako wa mwisho wa kidato cha sita? Unakumbuka Ulikuja kwangu na nikakupa Tsh laki moja kwa ajili ya maandalizi ya mtihani? Sawa,  ingawa nilikupa mimi, lakini ukweli ni kwamba pesa ile ilikuwa sio yangu.



Najua siku zote ulikua ukijua kuwa mimi ndiye niliyekuwa nikikulipia ada. Ukweli ni kwamba mimi nilikuwa nimefirisika sina mbele wala nyuma...lakini mama yako alinipa pesa zake. Angeweza kukupa wewe moja kwa moja ila aliamua kunipa mimi kwanza.



Hii inamaanisha nini mwanangu, muunge mkono/msaidie mume wako! Muda mwingine atakuwa kama amechanganyikiwa kutokana na ugumu wa maisha, madeni na vinginevyo ingawa ataonekana yuko sawa ila akilini mwake anayo hofu na majonzi makuu...atahisi hutaweza kumthamini tena kwa vile mambo yamemuendea kombo. Huo ndio muda utakao kubidi kuwa nae bega kwa bega ukimfariji.



Mwanangu njia sahihi ya kumuonesha mume wako kua unampenda ni kumuheshimu, najua inaweza tokea ukabishana nae, ukakwaruzana nae ila mwisho wa siku mwache ajue kuwa heshima yako kwake iko pale pale.



Mwanangu, unakumbuka siku ile nilipomkalipia vibaya sana mama yako? Alifanya nini? Alibaki kimya kabisa. Unakumbuka pia siku ile mama yako alivyonijia juu? Nilifanya nini? Nilibaki kimya kabisa! Binti yangu jifunze kuwa kimya muda mwingine pale mume wako atakapokuwa na hasira. Mmoja kati yenu atakapokuwa na hasira na gadhabu nyingi mmoja lazima atulie kimya. Kama wote mtaanza kupandishiana hasira tatizo hapo ndio huibuka. Na matatizo ya ndoa ndio huanzia hapo.



Mwanangu, kitu cha kwanza kujua kuhusu mume wako ni chakula anachokipenda. Kama anapenda vyakula vya aina nyingi weka katika akili yako. Usiache mpaka aombe chakula siku zote muandalie.



Kuna siku mama yako alinidaka nikiwa nimemshika mwanamke mwingine mkono, hakuwa mchepuko wangu ila ni rafiki yangu niliyepotezana nae kitambo. Mama yako aliponiona hakuanzisha ugomvi na yule mwanamke. Aliondoka kimya kimya.



Nilikuwa na hofu kuu kurudi nyumbani, ningemwambia nini anielewe? Lakini niliporudi nyumbani hakunisema chochote. Aliniandalia chakula mezani kama kawaida. Ila nafsini nilijiona kama nina hatia. Nikaanza kumuomba msamaha.



Kuanzia siku ile sikukaa kumtazama mwanamke wa pembeni mara mbili. Nani anajua? Je kama mama yako angegombana na mimi siku ile, labda ningeondoka nyumbani nakuangukia katika mikono ya mwanamke yeyote tu barabarani akanipoze. Muda mwingine ukimya huleta ufumbuzi mkubwa kuliko ugomvi.



Sahau kuhusu riwaya za mapenzi ulizosoma ulipokuwa shuleni. Unakumbuka filamu za kihindi na za kimarekani? Unakumbuka filamu za kitanzania na Kinaijeria? Unakumbuka tamthiliya za kifilipino? Nyimbo za westlife unazikumbuka? Sahau kabisa hayo mambo mwanangu! Usitegemee vitu ulivyokua ukiviona huko vitakuwepo katika ndoa yako. Maisha halisi ni tofauti na hadithi za kufikirika.



Kitu cha mwisho nachotaka nikuambie... Unakumbuka jinsi ulivyozaliwa? Sijawahi kukwambia! Baada ya ndoa yetu mimi na mama yako mambo yalikuwa magumu. Na mama yako ilimlazimu afanye kazi mbili kusaidia  familia. Nami pia nilikuwa nikifanya hivyo.


Nilikuwa nikirudi nyumbani saa moja jioni na mama yako alikuwa akirudi saa mbili usiku akiwa amechoka. Lakini tulipoenda kulala hakuninyima chakula cha usiku kitandani. Na kwa jinsi hii ndipo ulipozaliwa. Usijenge tabia ya kumyima mumeo chakula chake akipendacho cha usiku. Maana kufanya hivyo sio kumkomoa bali ni kuiharibu ndoa yako kwa mikono yako mwenyewe.


Kuwa mke mwema, na utakuwa binti yangu nitakae jivunia mpaka naingia kaburini........



Kila ka kheri binti yangu.
CHANZO CHA HABARI HII NI HAPA

Thursday, August 27, 2015

JINSI MALEZI YETU YA UTOTONI YANAVYOWEZA KUATHIRI NDOA ZETU

Habari za leo ndugu zanguni leo nimeamka nikiwa na fikra nyingi sana juu ya jambo hili la malezi yetu ya utotoni yanvyoweza kuathiri ndoa...Naanza na mfano huu:-  Patrick na Maria  ni mke na mume, kila mmoja amelelewa malezi tofauti.
Patrick alisema  tangu nakua au napata akili, nilizoea kumuona baba akirudi nyumbani muda wowote anaotaka na sijawahi kusikia ugomvi wowote toka kwa mama kuhusu kuchelewa huko.
Kwenye akili yangu, nikaamini kwamba, kumbe mwanamme anaweza kurudi muda wowote nyumbani hata kama ni usiku wa manane. Pia niliwahi kumsikia mzee mmoja akimwambia mzee mwenzake ambaye alikuwa anaomba amruhusu aondoke ili awahi nyumbani.... alimwambia hivi.... wewe ni mwanamme bwana, unawahi nyumbani kufanya nini? Au unaenda kupika? Maneno haya yalimuumiza sana mzee yule na mwisho aliamua kubaki wakaendelea kunywa pombe yao taratibu huku akimshukuru kwa ushauri wake mzuri.
Maneno haya yakazidi kumfanya Patrick aamini kwamba kumbe mwanamme hapaswi kurudi mapema nyumbani, alianza kuwaza na kujisemea kimoyomoyo,  na mimi  nikioa nitakuwa nafanya hivyohivyo kwani huo ndio uanaume.
Kwa upande wa pili, Maria  mke wangu kakulia kwenye familia ya mzee Mapunda ambayo baba alikuwa anarudi mapema sana nyumbani, na binti Maria  akaamini kwamba kumbe mwanamme anapaswa awahi kurudi nyumbani. Hajawahi kusikia ugomvi wowote kutoka kwa baba na mama yake.
Watu hawa wawili ambao wamekulia malezi tofauti wakaoana, wakawa mke na mume.
Siku za mwanzo bwana Patrick  alikuwa anawahi kurudi nyumbani kama ilivyo ada ya mapenzi mapya. Ndoa ilikuwa na furaha kubwa sana
Baada ya miezi miwili kupita, mume akaanza kuchelewa kurudi nyumbani kitendohiki  kilimuumiza sana bi Maria , akahisi mume wake kapata mchepuko ( mwanamke wa nje), ugomvi ukachukua mkondo wake, bi Maria akaanza kumnyima unyumba mume wake, akatumia tendo kama silaha ya kumwathibu mumewe, furaha iliyokuwepo kwenye ndoa hii ikayeyuka ghafla, paradiso iliyokuwepo ndani ya ndoa hii ikageuka na kuwa jehanamu, ikabaki historia, ikawa asubuhi ikawa jioni, maisha yakaendelea.
Mume akazidisha kuchelewa, hamu ya mapenzi ikampanda, akaamua kutafuta mwanamke wa pembeni ili apozee hamu zake.
Siku moja wanandoa hawa wakaamua kwenda kupata ushauri kwa mtaalamu wa masuala ya ndoa. Baada ya kuwasikiliza akawaeleza kwa kina namna jinsi malezi yao utotoni yalivyopelekea kuharibu ndoa yao. Akawapa mtihani wachague, wafuate malezi ya mke au mume? Kwa kuwa mume alikuwa akimpenda sana mkewe akashauri wafuate malezi ya mke ya yeye kuwahi nyumbani mapema.
Huwezi amini sasa hivi ndoa ya bi Maria na bwana Patrick ina amani na furaha maradufu ukilinganisha na wakati wanaoana.
Hebu na wewe jiulize kwenye ndoa yako, kwa nini huelewani na mwenzi wako?

Wednesday, August 12, 2015

MAISHA NA JAMII:- ZITAMBUE SIFA SITA ZA MSINGI ZA MWANAMKE ALIYE MKE BORA!

Mithali 14:1 "Kila mwanamke aliye na Hekima hujenga nyumba yake,bali aliye mpumbavu
huibomoa kwa mikono yake."

Kuna mithali isemayo "MAJUTO NI MJUKUU", ni kawaida kwa wanandoa kuangalia na
kulaumiana juu ya matatizo yanayojitokeza, badala ya kutafakari chanzo cha matatizo. Matatizo
mengi ya ndoa yanatokana na wanandoa kutokuwa na elimu ya ndoa na kutofuata ushauri wa Mungu
aliyeanzisha Ndoa. Baadhi ya sifa zamwanamke mwenye hekima pia soma mithali 31:10-31.

-Hufumbua kinywachake kwa hekima, na sheria ya wema katika ulimi wake huwashauri wengine kwa ukarimu mithali (31:26). Wanawake wengi hawajui kuutumia ulimi / ukali,maneno ya mikato, matusi, ukaidi n.k. kwao ni mambo ya kawaida wengi wanatawaliwa na HASIRA na WIVU, akiona mumewe anacheka na wanamke ni kosa la jinai, mwanamke anafura wala hata hawezi kuongea, hali ya hewa inabadilika hata paka nyumbani wanatambua kuwa hali ni mbaya.

-Hufanya kazi kwa moyo na huamka alfajiri na mapema.Kuna wanawake ambao ni wavivu
kupindukia, inafika wakati hata kutandika kitanda anamtuma House Girl, wanaume ni rahisi sana
kuvutwa na anayemhudumia kwa ukaibu, House girl akiandaa chakula, mara kitanda, mara maji ya
kuoga, mara apige deki chumbani n.k. Haitachelewa mwanaume kulipa fadhili kwa wema
anaotendewa.

-Ni msafi na anajua kuandaa mavazi yanayofaa kwa familia yake.
Kuna wanawake ambao ni wachafu/ usishangae kukuta sufuria kwenye makochi, chumba cha kulala
ni stoo ya nepi za mkojo na nguo chafu,wengine kuoga ni anasa. Mwanamke ni MAJI, sharti
mwanamke awe msafi muda wote, Wanaume wote wanapenda usafi,marashi hata ya mchina
yasikose,mwanamke hakikisha "Reception" inakuwa safi na kuwa katika hali ya kumfanya mume
ajisikie kujipumzisha kwa raha mustarehe.

-Jali na timiza mahitaji ya NDOA kwa mume wako.
Sulemani anasema mwanamke mwema “Taa yake haizimiki usiku”, kuna wanawake wavivu kwa
swala hili, pia kuna wanaopenda kulipa visasi kwa kuwanyima waume zao huduma, utakuta wiki

nzima mama apanda kitandani huku amevaa “KOMBATI”  utafikiri ni askari anaendavitani. Wanaume
ni sawa na Mbuzi ambao hawachelewi kukata kamba wakikosa majani walipofungwa, Fanya makosa
yote lakiniusijefanya  ujinga wa kumkomoa mume kwa kumnyima huduma ya ndoa,  hilo ni kosa la
jinai. Hakikisha huduma hizo zinaboreshwa, nenda na wakati ili mradi isiwe kinyume na taratibu za
Mungu.

-Mwanamke anatakiwa kujua kupika chakula kitamu, ambacho famiia itafurahi.
wanawake wengi hasa siku hizi hawajui kupika, ndio maana utakuta wanaumewengi wanaishia kula
hotelini au kwa mama ntilie, kama umetokabara basi usione aibu kujifunza kwa watu wa pwani namna ya kuunga nazi kwa chakula. Akina mama ni wajibu wao kujifunza Mapishi, mchicha peke yake unaweza kuwa na mapishi zaidi ya 10, Wanaume wanapenda chakula  chenye ladha “Taste”, mfanye mume akumbuke chakula cha nyumbani.

-Mwamini mume wako, wivu na hisia mbaya ni adui wa ndoa yako. Usitoe siri za ndoa yenu kwa
mashoga au ndugu zako.

Muda wote muombe Mungu akupatie hekima ya kuongea pindi tatizo linapotokea, muombee mume wako ili Mungu amsaidie pia awe na hekima ya kutunza ndoa kwa uadilifu na upendo”.
CHANZO: GAZETI LA MWENGE TOLEO LA JANUARI 2015

Thursday, March 27, 2014

PALE WAZAZI WANAPOAMUA KUWACHAGULIA WATOTO WAO WACHUMBA NA MWISHO WAKE MAISHA YANAPOKUWA MATESO...JE? NANI WA KULAUMIWA?

Mara nyingi sana nimekuwa nikifikiri hili jambo la kuchaGULIWA MCHUMBA. Nimekuwa nikijiuliza je ni nani ataishi na huyu mume au mke? Kwa bahati nzuri leo nimeamka nikiwa nikisoma mail zangu nimekutana na hii habari ambayo nimetumiwa na msomaji wa Maisha na Mfanikio...Jiunge nami na kisa hiki za huyu mdada.....
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
Kuna mwanadada mmoja ambaye ni miongoni mwa watu wasomi sana. Amemaliza chuo hapa Milimani. Wakati alipokuwa chuoni alibahatika kupata mchumba walikubaliana kuoana. Na walikuwa katika maelewano mazuri katika uchumba wao.

Baada ya uchumba huo kuendelea, aliamua kumpeleka kwa wazazi wake na kuwafahamisha kuwa mimi nimepata mtu ambaye naona atanifaa katika maisha  yangu. Baada ya kuwafahamisha, mama habari hiyo, mama wa dada huyo alikubaliana na wazo lake la kutaka kuolewa na huyo mchumba wake, lakini upande wa baba yake kulikuwa na shaka. Huyu binti alikuwa karibu sana na baba yake na aligundua kuwa baba yake hataki kukubaliana na wazo lake. Baada ya mazungumzo ya hapa na pale na baadaye mvulana yule kuondoka, binti alimfuata baba na kuzungumza naye na akasema kwa jinsi nilivyomuona huyo mvulana hakufai. Binti akamwambia si vizuri kumhukumu mtu kwa kumwangalia tu. Mimi nimekuwa naye kwa muda mrefu namfahamu vizuri sina shaka naye. Baba yake bado hakukubaliana na hilo lakini upenda wa mama yake hakukuwa na shida.

Uchumba uliendelea na yule mvulana akasema inaonyesha baba yake hataki kabisa, lakini nitaumia sana endeapo kama bado ataendelea kuwa na msimamo wake huo. Ni mtu ambaye nimekuzoea, tumeheshimiana sana. Yule binti akamwambia kila kitu kinawezekana na itawezekana tu.

Siku moja yule binti akiwa katika mizunguko yake ya hapa na pale akiwa mjini, alikutana na kaka mmoja akiwa katika mavazi ya kijeshi, na alikuwa na mwonekano mzuri sana, lakini cha kucshangaza yule kaka baada ya kumwona binti huyu aliduwaa. Baada ya kuduwaa kwa kipindi aliamua kumfuata binti na kumsalimia na kumwuliza kila kitu, na baadaye walianza kuwasiliana mawasiliano ya kawaida kabisa. Lakini mwanajeshi huyo alikuwa na mawazo tofauti, na ndipo siku moja akamweleza  kuwa angetamani siku moja awe mke wake. Yule binti akamwambia hapana, mimi tayari nina mtu wangu na tunaheshimiana sana, mwanajeshi akamwambia sawa. Kwa vile ni marafiki alimrudisha mpaka kwao, kumbe lengo lake yule kijana ni kutaka kujua binti anaishi wapi.
Na ndipo siku moja yule kijana aliamua kwenda peke yake nyumbani kwa wazazi wa binti huyo na kukutana na baba yake (Baba wa binti). Na ndipo alipozungumza ukweli wa kile alichokiona na lengo lake ni lipi. Na mzee aliweza kumdadisi kijana na kumweleza kila kitu. Kwa wakati huo yule binti pamoja na mama yake walikuwa hawapo na binti aliporudi akalezwa na baba yake kuwa kuna kijana mmoja alikuja yupo hivi na hivi aamenieleza kila kitu, nadhani huyo ndiye atakayekufaa. Binti alamwambia hapana, wewe ndiye umemwona na mimi itabidi nimwone. Baaye yule mjeshi akaja wakazungumza.
Baada ya mazungumzo marefu ya hapa na pale yule kijana mjeshi aliamua kuondoka, na kwa kuwa binti hakutaka kukofishana na baba yake aliamua kukubaliana na mawazo yake na baadaye wakamwita tena kijana huyo mjeshi. Baadaye taratibu zote za kuoana na mjeshi huyo zikafanyika, kisha binti huyo alienda kwa mchumba wake wa kwanza na kumweleza yote yaliyotokea na kumrudishia pete ya uchumba waliyovishana hapo awali. Kijana huyo alisikitika sana kwa uamuzi aliouchukua lakini hakuwa na jinsi aliamua kufuata shinikizo la baba yake. Hatimaye baadaye yule binti aliolewa na mwanajeshi na ndoa ilifungwa kanisani.
Baada ya ndoa tu, kilichotokea sasa hivi ni kwamba kosa kidogo tu anaambuliwa kipigo ambacho hajawahi kukipata, kiasi kwamba inampeleka kumkumbuka yule wa kwanza ambaye walikuwa wakiongea naye kwa utaratibu kabisa.
Ndipo baadaye binti (ambaye sasa ni mke wa mwanajeshi) akamfuata yule mchumba wake wa kwanza na kumweleza kila kinachotekea. Lakini kijana huyo aliajaribu kumweleza namana ya kufanya ili waendelee kuishi vizuri na mume wake na kuzidi kumwombea ili waishi vizuri.
Kwa wakati huu kijana huyo alikuwa bado hajaoa na anamweleza binti kuwa itachukua muda mrefu kwa sababu kwanza, itabidi nikusahau wewe, pili nikae chini  nitulie, tatu nianze upya. Hivyo itachukua muda sana.
Kikubwa zaidi ni kuwa binti hyuyo amekubali kuolewa na mwanajeshi kwa shinikizo la baba yake, lakini kinachoendelea ni kwamba kosa dogo tu anaambulia kipigo kisicho cha kawaida. Na kinachomuuma zaidi huyo dada ni kuwa walipotoka nje walienda sehemu ile ile ambayo walikuwa wakienda na mvulana yule wa kwanza na hivyo kuumia zaidi

Swali la Kapulya:- Je? huu kweli ni uungwanana? je? ungekuwa wewe ungmsikiliza baba au ungefuata jinsi moyo wako unavyopenda?

Sunday, March 2, 2014

KATIKA JUMAPILI HII YA KWANZA YA MWEZI HUU WA TATU TUANGALIA HILI, MKE:- FURAHA YA MUME WAKE!

Kitabu cha Mithali kinaeleza jinsi mwanamke mkamilifu alivyo, mwanamke aliye furaha na fahari ya mume wake. Mwanamke huyu anafanya kazi zake kwa bidii, ana hekima, ni mwaminifu na hutunza kwa uaminifu watu na vitu vya nyumbani. (Mit. 31:10-31)

Friday, May 24, 2013

MAISHA YA NDOA:- MKE NA MUME!!

Nipo kazini mara nasikia simu yangu ya mkononi ujumbe ukiingia, nachukua kuangalia ni nani na nini..nakutana na ujumbe huu na maagizo :- Kuwa  "wape wanandoa wote unaowafahamu ujumbe huu. Mungu na  awatie nguvu!! Ameeeen....!!" Na kwa vile najua wengi ninaowafahamu wanapita hapa nikaona itakuwa njia nzuri kuweka hapa...na ujumbe wenyewe ni kama ifutavyo:-
"Ukiona mko vizuri kwenye ndoa, Usimsifu mumeo/mkeo, Endelea kumtukuza Mungu na kuweka maombi ya akiba. Usitoke bila KUMWOMBEA mkeo/mumeo.
Jifunze pia kumwelewa mwenzako na kutokuuona udhaifu wake kama sababu ya wewe kumfanyia mabaya. Zungumza naye, mtie moyo, mshauri katika usiyoyapenda, mweleze uliyonayo.
Ondoa maswali nafsini mwako. Pata majibu sahihi kutoka kwake. KUMBUKA NI NYAKATI ZA MWISHO. Taasisi ya shetani isiyotaka ichanue ni NDOA. Ikiharibika familia nayo inaharibika. TAFAKARI"....IJUMAA NJEMA NA MWANZO MWEMWA WA MWISHO WA JUMA!!!

Tuesday, May 14, 2013

WANANDOA NA KAULI HIZI: HATA VIKOMBE KABATINI HUGONGANA, ITAKUWA SIE?

Je unadhani au kuamini kwamba kuna ndoa ambazo wanandoa wake hawagombani kabisa? Kama unaamini hivyo, basi unajidanganya na labda unaishi katika dunia ya peke yako.
Ni jambo lenye ukweli wa kutosha kabisa kwamba wanandoa wote duniani hutokea kugombana, lakini kugombana huko hutokana na migongano au mizozo ya muda tu ambayo huweza kutatuliwa na pande mbili kama wakiamua kufanya hivyo.
Wewe unayesoma hapa, napenda kukuambia ukweli kwamba usiogope migogoro ya ndoa, kwani hicho ni kitu ambacho kamwe huwezi kukiepuka. Kuna msemo mmoja unatumika sana huko nyumbani usemao, " hata vikombe kabatini hugongana itakuwa wana ndoa?" Hii ina maana gani, ina maana kwamba haiwezekani watu kuishi pamoja halafu msiwe mnatofautiana, na kama ukiona hivyo, jua kwamba hiyo ndoa si salama kwani siku yoyote bomu litapasuka na madhara yake yatakuwa ni makubwa kuliko kawaida.
Kuna watu ambao hata kama wamekosewa na wenzi wao hunyamaza kimya na kumeza hasira zao, wengine huogopa kuwakabili wenzi wao na kuzungumzia jambo linalowakera kwa kuhofia kuonekana kama wana kasoro au ghubu. Jambo hili ni hatari sana.
Kumkabili mwenzi wako na kumwambia hisia zako kama amekukosea au amekwenda kinyume na matarajio yako ni jambao la maana sana katika kudumisha uhusiano. Lakini naomba nitahadharishe kwamba, ni vyema kufanya hivyo bila kumshusha, kubeza au kusimanga kwani hiyo sio dalili nzuri ya upendo.
Inashauriwa kwamba wanandoa au wapenzi wanapokwaruzana inabidi wajadili tofauti zao bila kusigishana, kila mmoja akitaka kuwa mshindi, hiyo haitasaidia kuimarisha ndoa bali itaongeza tatizo. Ni vyema upande unaohusika na tatizo, uwajibike na kuomba radhi kwa ustawi wa ndoa, huo ndio ukomavu.

Kutojadili mgogoro kwa wanandoa na kuupatia ufumbuzi wa tatizo huwafanya wandoa kuwa mbali kihisia, na athari zake ni kuwakuta wanandoa wakiwa wageni wa kila mmoja kwa mwenzake, yaani hakuna mawasiliano, kila mtu na lwake.
Jambo la msingi kwa wanandoa ni kujadili tofauti zao pindi linapojitokeza jambo linalomkera mmoja wa wanandoa, kwani hakuna jambo linaloweza kujitatua lenyewe bila kutatuliwa na wandoa husika. Kuacha jambo lolote bila kulitafutia suluhu ni sawa na kutega bomu, ambapo siku likilipuka madhara yake ni makubwa sana.
Unaweza kukuta mwanandoa anakereka na mambo madogo madogo ya mwenzi wake lakini hasemi, ingawa yanamkera kupita kiasi akitegemea huyo mwenzi wake atajua na kuacha, thubutu…..inapotokea siku yeye amekosa jambo dogo tu na huyo mwenzi wake akamsema, basi atatumia fursa hiyo kuanza kujibu mapigo kwa kueleza yale yanayomkera kutoka kwa mwenzi wake, na hapo itakuwa kila mtu anavutia kwake kama mwamba ngoma………na aamini nawaambia kuwa kamwe hawezi kupatikana mshindi katika jambo hilo, kwani mjadala huo unaweza kutoka nje ya mada kila mmoja akijitahidi kutafuta makosa ya mwenzi wake hata yale yaliyotokea wakati wa uchumba wenu ili mradi vurugu tupu.
Inatakiwa wanandoa wajadili kila jambo linalojitokeza hadi kulipatia suluhu, vinginevyo ni kuichimbia ndoa yenu kaburi la mapema. Wakati mwingine unaweza kukuta mwanamke analalamika juu ya kutoridhishwa kwake na matumizi ya mumewe, na hapo mume naye ataanza kukumbusha juu ya matumizi yasiyo ya lazima yaliyofanywa na mke huko nyuma. Mke naye hataridhika atakumbushia jambo lingine na lingine hadi hata mada iliyokuwa ikijadiliwa inasahaulika.
Jambo lingine ni kujumuisha mambo, matumizi ya maneno kama, mara nyingi, kila wakati au mara kwa mara si mazuri sana. Unaweza kukuta mtu mwenzi wake amekosea jambo halafu mwenzie anamwambia “Kila mara huwa unafanya hivi” au mara nyingi huwa unafanya hivyo…..Hii ni hatari kwa ustawi wa wanandoa, kwani kwa kujumuisha ni sawa na kumwambia mwenzi wako kuwa kila mara yeye ndiye mkosaji.
Kwa haya niliyoyaeleza hapa sina maana kwamba huu ndio muarobaini pekee wa kuimarisha mahusiano kwa wanandoa, bali ni moja ya mambo muhimu kati ya mengi ambayo yakizingatiwa na wanandoa wote basi ndoa yao itakuwa imara Tujadili pamoja………..

Thursday, April 18, 2013

KWA MARA NYINGINE TUANGALIE JAMBO HILI :-MTOTO/KIJANA AFUNGA NDOA NA MAMA YAKE MZAZI BAADA YA BABA YAKE KUFARIKI -SONGEA!!!

Katika pitapita nimekutana na hii mimi na Tanzania ...nikakumbuka hii nikaona niweka hapa  maisha na mafanikio... haya hebu wasikilize maelezo yao pia wanajamii wengine...

Sijui hapa itakuwa laani au ni ukosefu wa akili...inasikitisha sana kwa kweli....Jioni njema kwa wote mtakaopita hapa..Bibi kaongea na kingoni bwana :-)

Monday, November 19, 2012

JUMATATU HII TUNANZE NA SWALI HILI? NINA KASORO GANI?

Jerome na Sesilia walikuwa wamemaliza miaka mitatu tangu waoane. Jerome alikuwa fundi wa saa. Alikuwa amejenga duka lake dogo nje ya nyumba yao. Kila siku, isipokuwa Jumapili, watu waliweza kumkuta hapo. Alipenda kuimba wakati akifanya kazi na kama hakuwa akiimba, basi redio ilikuwa ikicheza muziki kwa sauti kubwa na safi kwa wapita njia wote kusikia.

Watu waliwafahamu kama watu wawili wenye raha. kabla ya kufunga ndoa, Sesilia hakuwahi kuishi mjini. Miaka yake ya kwanza nyumbani mwao mpya ilimshangaza kwa vile alivyowaona watu wakiharakisha kwenda huku na kule. Katika kijiji chake alimokuwa, maisha yalikuwa tofauti sana na tena ya polepole zaidi. Lakini hapa kelele zilikuwa nyingi mno, milio ya honi hasa za watu wenye taksi, na sauti za watu wakiitana.

Lakini alikuwa anafurahi kuvumilia yote haya kwa ajili ya ndoa yake kwani alimpenda sana Jerome. Alijua ya kwamba Jerome alimpenda pia. Hakuongea sana juu ya jambo hilo, lakini Sesilia aliweza kuliona kwa namna alivyokuwa anamwangalia, katika utaratibu wa sauti yake na katika kumtunza kwake. Alizoea kuimba alipokuwa akifagia nyumba. Huko nje pia Jerome naye alikuwa akiimba na sauti zao kwa pamoja ziliwaambia watu waliopita karibu kwamba hiyo ilikuwa ndiyo nyumba yenye raha.

Siku moja, Sesilia akiwa sokoni, alisikia jambo lililomtia uchungu sana. Lucy, kutoka katika kijiji chake, alimwambia kwamba jioni iliyopita alikuwa amemwona Jerome akiingia katika nyumba ya wageni.

"Kwa nini lakini?" Sesilia aliwaza. "Bila shaka siyo kuwa na mwanamke mwingine" Ndiyo Lucy alikuwa na hakika alikuwa ndiye Jerome. Sesilia alijaribu kujisadikisha kwamba bila shaka haikuwa hivyo lakini hakuweza kufukuza wasiwasi mkubwa uliokuwepo moyoni mwake. Alifahamu kwamba watu wengi kati ya watu wake hawakuona kwamba ni jambo baya sana kwa mtu wa ndoa  kuwatembelea wanawake wengine. lakini aliamini ya kwamba ndoa yao ilikuwa tofauti na ndoa nyingine nyingi.

Aliamua kutosema neno lolote. Atasubiri na kufungua macho. Jerome alionekana kama hali yake ni ya kawaida lakini hapa na pale Sesilia alitambua badiliko katika mwenendo wake kwake. Ama, haya yalikuwa ni mawazo yake tu? hakuweza kusema.
Jioni moja, baada ya chakula cha jioni, Jerome alimwambia Sesilia kwamba alikuwa anakwenda kutembea. "Nimeketi kutengeneza saa kutwa kucha, na nisiponyosha miguu ninahofu nitasahau namna ya kutembea", alimwambia haya haku akifunga mlango wa duka lake.
Alipomfuata nyuma barabarani, Sesilia aliona aibu ya kufanya hivyo. Lakini ilimbidi kujua. Labda alikuwa anakwenda kwa wanawake. Walikuwa wanaelekea kwenye nyumba ambayo Lucy alikuwa amemwelezea. hata hivyo mtu aliyeweza kuwa na sababu nyingine za kutembea kwenye mtaa huu. Labda Jerome hakujali alikuwa anakwenda wapi.

Moyo wa Sesilia ulisimama alipomwona Jerome akiingia kwa mlango wa nyuma wa baa /nyumba ya wageni
maalumu ambayo waliishi wanawake. Kumbe, Lucy alikuwa amesema kweli. Akijawa na uchungu, huzuni na hasira, Sesilia alirudi nyumbani polepole. Alijiuliza: "Nina kasoro gani? kwanini Jerome ana haja ya kumwendea mwanamke mwingine? Kwa nini hakai nami? Nina kasoro gani?"
Sesilia hakuweza kujua kilichokuwemo akilini mwa Jerome. Hakuweza kujua kwamba Jerome alikuwa amezoea raha aliyokuwa nayo na kwamba sasa alitaka kuonja kitu kipya, alitaka kugundua mambo mapya na pia alitaka watu wapya wamtosheleze. Sesilia hakujua hayo lakini aliazimia atamfundisha Jerome asikose uaminifu tena----yaani hata naye Sesilia atapata mpenzi.
Je? Unafikiri nini kilimfanya Jerome afanye kama alivyofanya?


Wednesday, August 29, 2012

MTOTO/KIJANA AFUNGA NDOA NA MAMA YAKE MZAZI BAADA YA BABA YAKE KUFARIKI -SONGEA!!!



Mke na Mume, Bi Condorada Ngonyani (70) na Bw. Joseph Mapunda, ambao ni Mama na Mwanawe, wakiwa nje ya nyumba ya Mganga, wakati walipofikishwa kwa suala hilo la Mama Mzazi na Mwanawe kufunga ndoa.
*********************************************************************************

Na Mwandishi Wetu, Namtumbo Ruvuma
MARA kadhaa kumekuwa kukijitokeza matukio mbalimbali ya kustaajabisha, kusikitisha na kutisha na mengine yakihisiwa kuwa ni imani za kishirikina, ambapo mengi ya matukio hayo ambayo hutokea si kwingine ni hapa hapa nchini kwetu, huwaacha watu hoi na maswali mengi yasiyokuwa na majibu.
Kwa mara nyingine tena tukio la kushangaza na kutoaminika kama ni kweli ambalo huwezi hisi kuwa ni la imani za kishirikina, kwani wahusika wote wamefanya hivyo kwa malengo na kuweka wazi sababu za kufanya hivyo japo si sahihi kwa itikadi za kidini, mila na destuli za mtanzania.
Tukio hili ni Mama Condorada Ngonyani (70) mkazi wa mkoani Ruvuma, ambaye aliamua kufunga ndoa na mtoto wake wa tatu wa kiume wa kimzaa na kuishi naye kinyumba kama mke na mume, ambapo wameonekana wao kama wao kuwa wapo sahihi na kuwashangaa wanadam, majirani zao na Jamii kwa ujumla kuingilia mapenzi yao.

Wananchi wapatao 400, wa mkoa wa Ruvuma walijitokeza kushuhudia kimbwanga hii wakati uongozi wa Serikali ya Mtaa walipoamua kuwafuatilia na kuwahoji na kuitisha mkutano wa wanakijiji na kuwaweka hadharani, ambapo Wananchi wa Mkoa wa huo wameiomba Serikali kupitia Wizara ya Maendelo ya Jamii, Jinsia na watoto, kufuatilia kwa karibu suala hilo na kuwaondoa hofu wananchi kama kuna sheria inayomruhusu Mtoto na Mama Mzazi kuweza kuishi kindoa.

Alipohojiwa Mama huyo, Condorada Ngonyani, anasealisema kuwa mara tu baada ya kufariki mume wake, Mzee Mapunda, yeye aliamua kumchagua mtoto wake huyo Joseph Mapunda, ili amrithi baba yake katika kuumiliki mwili wake kama ambavyo alikuwa akifanya Baba yake mzazi, ili kuondokana na tamaa na vishawishi wa kiulimwengu.
Alisema kuwa baada ya uteuzi huo walifunga ndoa ya kimila japo kuna baadhi ya wanafamilia hawakufurahishwa na tukio ama jambo hilo, lakini yeye aliamua kufunga masikio na kuamua kuvunja amri ya sita na mtoto wake huyo wa kumzaa.
Tukio kama hili ni mara ya kwanza kutokea kwa mkoa wa Ruvuma na hata kwa Tanzania nzima, ambapo wakaazi wa Ruvuma wamekuwa wakibaki na maswali mengi juu ya tukio hilo na kuhoji Jamii sasa inaelekea wapi kwa baadhi ya Watanzania kuibomoa wenyewe mila na desturi zetu.
Kwa upande wake, Joseph Mapunda, yeye anasema kuwa upendo na mahaba anayoyapata kutoka kwa mkewe huyo ambaye ni mama yake mzazi, hajawahi kuyapata kokote na kusema kuwa wanapendana sana na wanaheshimiana kama mke na mume.
Josepha amehiji kulikoni wanadam kuwafuatilia katika mapenzi yao na kusema kuwa ''hawa watu wanaotufuatilia hadi leo hii kutuweka hadharani namna hii, wanataka nini kwetu?''.
Wananchi hao waliofurika kwa Mganga wa Jadi Flora Ndembo, wilaya ya Namtumbo Mkoani Ruvuma, wameiomba Serikali kuingilia kati suala hilo na kuchukua hatua kisheria ili iwe fundisho kwa wanatanzani wengine wenye akili kama hizo za kuharibu mila na desturi za kitanzania kirahisi kama hivyo. Picha na Songea Habari

Bi. Condorada Ngonyani. ''Nawashangaa wanadam kuingilia mapenzi yangu, mtuache''.
Bwana, Joseph Mapunda, ''Wananchi mtatutakia nini na mapenzi yetu''?
CHANZO:HAPA  NA PIA UNAWEZA KUSOMA HAPA. ..
.................................................................................................................................................................
Habari hii imenigusa sana, jamani kumwoa mama yako mzazi /kuolewa na mtoto wako uliyemzaa  kweli? kwanini wasingeishi tu kama mama na mtoto ? huko tunakoenda sasa ni balaa tu. Dunia imekwisha jamani au nini hii sasa...mama ana miaka sabini ...nimeishiwa maneno ya kusema nimebaki natafakari bila kupata jibu....Maisha haya jamani .....

Saturday, June 9, 2012

AU TU TUMALIZE JIONI YA JUMAMOSI HII KIHIVI:-MAISHA YA NDOA/MARRIAGE!!

 A man and his fiancé were married. It was a large celebration. All of their friends and family came to see the lovely ceremony and to partake of the festivities and celebrations. A wonderful time was had by all. The bride was gorgeous in her white wedding gown and the groom was very dashing in his black tuxedo. Everyone could tell that the love they had for each other was true. A few months later, the wife comes to the husband with a proposal: “I read in a magazine, a while ago, about how we can strengthen our marriage. “She offered. "Each of us will write a list of the things that we find a bit annoying with the other person. Then, we can talk about how we can fix them together and make our lives happier together." The husband agreed. So each of them went to a separate room in the house and thought of the things that annoyed them about the other. They thought about this question for the rest of the day and wrote down what they came up with. The next morning, at the breakfast table, they decided that they would go over their lists. "I'll start, “offered the wife. She took out her list. It had many items on it. Enough to fill 3 pages, in fact. As she started reading the list of the little annoyances, she noticed that tears were starting to appear in her husband’s eyes. "What's wrong? “she asked.” nothing “the husband replied, “keep reading your list." The wife continued to read until she had read all three pages to her husband. She neatly placed her list on the table and folded her hands over top of it. "Now, you read your list and then we'll talk about the things on both of our lists. “She said happily. Quietly the husband started, “I don't have anything on my list. I think that you are perfect the way that you are. I don't want you to change anything for me. You are lovely and wonderful and I wouldn't want to try and change anything about you." The wife, touched by his honesty and the depth of his love for her and his acceptance of her, turned her head and wept. IN LIFE, there are enough times when we are disappointed, depressed and annoyed. We don't really have to go looking for them. We have a wonderful world that is full of beauty, light and promise. Why waste time in this world looking for the bad, disappointing or annoying things when we can look around us, and see the wondrous things before us? I believe that WE ARE THE HAPPIEST when we see and praise the God and try our best to forego the mistakes of others. Nobody's perfect but we can find perfection in them to change the way we see them. It is necessary to understand the difficulties and be a helping hand to each other....THAT BRIGHTENS THE RELATIONSHIP.
Habari hii nimetumiwa na msomaji wa Maisha na Mafanikio nami nimeona tusinyimane habari kama hizi.

Wednesday, May 30, 2012

UNATAKA KUMUACHA MKE MKOROFI? FANYA HIVI.........!


Ni ile JUMATANO YA KIPENGELE CHA MARUDIO NA LEO NIMEIKUTA HII KWA KAKA YANGU WA HIARI KALUSE Hebu soma na halafu tujadili kwa pamoja.KARIBU...



Kuna wanaume ambao wametokea kuoa wanawake ambao wana tabia mbaya . ninaposema kuwa na tabia mbaya sina maana ya mwanamke kuwa Malaya, maana hiyo ni fasili rahisi ya tabia mbaya kwa watu walio wengi. Ninaposema tabia mbaya nina maana kwenda kinyume na matarajio ya mume na pengine hata kwenda kinyume na matarajio ya jamii. Mwanamke ambaye ana tabia kama ghubu, mdomo mdomo (mkosoaji), mtapanyaji wa mali, mpenda makuu na tabia nyingine za aina hiyo, ni mwanamke ambaye kwa kiasi kikubwa anaweza kumsababishia mume matatizo ya kimwili na kisaikolojia. Mwanamke wa aina hii anaweza hata kuathiri makuzi ya watoto na kuathiri uhusiano na mume na watu wengine waliyo karibu yake. Kama mwanamke wa aina hii ameolewa na mume mweledi ndoa inaweza isiyumbe sana, lakini hii ina mipaka na kiwango chake.

Kuna wakati matatizo haya huweza kufika mbali zaidi kiasi kwamba huanza kumwathiri mume. Mwanaume ambaye huchukua kila uamuzi unaohusu maisha yake kwa hadhari kubwa, anaweza kuendelea kuishi na mke huyu. Lakini mara nyingi kuendelea kuishi na mke huyu kuna maana ya matatizo zaidi kuliko ufumbuzi. Bila shaka mmeshawahi kusikia wanaume ambao wanalalamika kuhusu tabia mbaya za wake zao (hata hapa JF wapo wengi sana), lakini huku wakiendelea bado kuwa na wake hao. Ukiacha sababu ya kugawana mali, wanaume wengi huwa wanafikiria mambo mengi ambayo huwazuia kuchukua uamuzi wa kuachana na wake hao.

Nimeona itakuwa vizuri kuwaambia wanaume hawa kwamba, kama ndoa zao zimefikia mahali ambapo zinataka kuwatia kichaa, wakiwa na uhakika kwamba wake zao ndio wenye matatizo na sio wao, (hili inabidi waliangalie kwa makini) inabidi wafanye uamuzi kwa kujiangalia wao na watoto wao zaidi kuliko watu au vitu vingine. Baadhi ya mambo ya kuangalia ni haya:

1. Kuathirika kwao: wajiulize wanaumia kiasi gani kimwili na kisaikolojia kwa kuendelea kuishi kwao na wanwake hawa. Kama ni ghubu na kukosolewa, kunawaathiri kiasi gani,? Na kama ni utumiaji mbaya wa mali unawaathiri kwa kiasi gani? Kama athari za tabia mbaya alizo nazo mwanamke zinafaa kudharauliwa na mume anaweza kuzidharau ni vyema akafanya hivyo, na kuendelea na maisha. Na kama akiona kuzidharau tabia hizo itakuwa na maana ya angamio kwake na pengine mbaya zaidi kwa watoto, inabidi hiyo iwe ni sababu ya msingi kuachana na mke huyo.

2. Ndugu watasemaje: wanaume wengi hukwamia hapo. Kama wake zao wanaelewana vizuri na baadhi ya ndugu, au hata wazazi wao, wanaume hushindwa kutoa maamuzi wa kuwaacha kwa hofu ya kulaumiwa na kushangawa. Wakati mwingine mume huyu anaelewena sana na watu wa upande wa pili, yaani ndugu wa mke na hasa wazazi na pengine wote. Hiki nacho ni kikwazo kikbwa sana, kwani mume hufikiria jinsi atakavyoonekana kwa watu hawa, pale atakapoamua kuchukua uamuzi wa kumuacha mkewe.

3. Sifa moja nzuri: pamoja na kuwa na matatizo, kila binadamu anaweza kuwa na upande mzuri. Kama mwanamke huyu ana sifa fulani ambayo ni nzuri sana, tuseme ni mpishi hodari sana na mkarinu kwa wageni , au labda ni mwaminifu sana katika ndoa, mwanaume anaweza kukwama kutoa uamuzi kwa kudhani au kujidanganya kwamba huenda anaweza asipate mwanamke mwingine mwenye sifa kama hizo. Huku ni kujidanganya kwa sababu kila sifa aliyo nayo binadamu fulani, ya kitabia, ipo kwa binadamu mwingine hata kama siyo wengi.

Ukweli ni kwamba mwanaume anaweza kushindwa kumpa talaka mkewe ambaye anakaribia kumuuwa kwa matatizo yake kwa sababu ambazo mtu mwingine anaweza kuzishangaa. Lakini jambo la msingi kwa mwanaume kama huyu ni kujaribu kupima kwa makini, je hizo sababu zinazomfanya asite kuachana na mkewe huyu zina nguvu au maana kuliko maisha yake, hasa mwili na akili yake?.
Angalizo: Sishauri watu kuachana, lakini nashauri watu kujua kwamba ndoa zenye mashaka makubwa ni hatari kwa afya na maisha yao. 
TUKUTANE TENA PANAPO MAJALIWA..JUMATANO NJEMA.

Saturday, May 26, 2012

JUMAMOSI HII TUANGALIA JINSI NDOA NDOANA INAVYOKUWA....!!!!


Mmmmhh hapa kaaaaazi kwelikweli!!! NATUMAINI JUMAMOSI YAKO ITAKUWA NJEMA...

Wednesday, April 18, 2012

NAMNA YA KUTOKA KWENYE UTUMWA WA NDOA…….

Habari za leo..Ni ile JUMATANO YA KIPENGELE CHA MARUDIO YA MAMBO MBALIMBALI. Leo nimeperuzi kwa kakangu Kaluse na kukutana na hii mada. KARIBUNI TUJADILI KWA PAMOJA.
Sio lengo langu kuwafundisha wanawake namna ya kuachana na wapenzi au waume zao. Lakini hebu fikiria kwamba kila wakati wanandoa au wapenzi wako kwenye vita. Hakuna amani, hakuna masikilizano. Kutwa nzima mtu anawaza kuhusu uhusiano wake mbaya hadi anashindwa hata kufanya kazi. Je, hali kama hii ina maana kwa mtu kuendelea kuwa kwenye ndoa?

Hapa nazungumzia wale ambao wanashindwa kutoka kwenye uhusiano, ambao wanajua kabisa kwamba, unawatesa na kuwaumiza. Kuna sababu nyingi kwa nini watu hawa wanashindwa, lakini nyingine zinatokana tu na kutojua namna ya kutoka, sio utegemezi wa aina yoyote.
Moja ya sababu, ambazo ninaziona sana hasa kwa wanawake ni kujali jamii itasemaje. Mtu anaona kabisa uhusiano haufai na anatamani kutoka . lakini anajiuliza, hivi watasemaje? Kuna wakati ndugu wanamwambia, yeye ndiye mkorofi. Kama hii ndio sababu anachotakiwa kufanya mwanandoa ni kuhakikisha kwamba anajifunza kuishi kama yeye. Nijuavyo mimi, hata wanandugu au jamii hata ikisema vipi, anayeumia au kuepuka kuumia au kuuawa ni yule aliye kwenye mateso ya ndoa
Jambo la kujiliza hapa ni kama, jamii ndiyo inayopigwa, kutukanwa, kutelekezwa au kudhalilishwa? Lakini jambo kubwa zaidi la kufahamu ni kwamba mtu alishaolewa maana yake ni mtu mzima mwenye haki ya kuamua juu ya maisha yake. Akisubiri ndugu wamwamulie, basi huyo bado ni mtoto..
Jambo lingine ni lile la, je nikimwacha nitapata mwingine? kwani wanaume siku hizi ni shida sana? Ni ujinga unaowafanya wengi kuuliza swali hilo. Unahitaji mwingine wa nini? Unahitaji mwingine ili maisha yako yawe ya maana zaidi au? Kama hakuna mwingine ni vyema kwa sababu maana yake ni kwamba hakuna mwingine wa kukutesa. Lakini wanasaikolojia wanaamini kwamba, ‘kila bidhaa ina mnunuzi.’ Kama unataka mwingine, hata ukiwa na miaka sitini utampata. Huwezi kumpata wakati ukiwa ndani ya tanuru la mateso. Ni lazima utoke kwanza.
Kuna wale wanaoshindwa kutoka kwa sababu wanaamini kwamba mwanamke haruhusiwi kutoa talaka. Hi siyo kweli. Kuna wanaoshindwa kutoka kwa sababu dini zao zinakataza kuachana, hii pia siyo kweli. Mwanamke au mwanaume, yeyote anaweza kuomba talaka na ikatolewa, kama kuna sababu zenye kukidhi haja hiyo. Chombo pekee kinachoweza kutoa talaka au kuidhinisha wanandoa kuachana ni Mahakama, siyo dini au taasisi nyingine. Kinachoitwa ‘talaka tatu’ kwa mfano, ni ushahidi tu, na sio talaka.
Kuna wale ambao hawako tayari kutoka kwenye uhusiano mgumu kwa sababu ya mali. Wanaogopa watagawana mali na wenzao, jambo ambalo hawako tayari kulifanya na mara nyingi hawa ni wanaume. Wapo pia wanawake ambao wao ndio waliokuwa watafutaji wakuu. Swali la kujiuliza ni hili. ‘Ni kipi bora, ni mali au ni amani na utulivu na uhai wako?’ kama ni mali, basi hakuna anayeweza kukuingilia kwenye uamuzi wako.
Lakini, kwa ufahamu tu, ni kwamba, pasipo na amani, mali haina maana na pasipo na amani uhai ni wa kubahatisha pia.
Wengine wanashindwa kutoka kwenye husiano kwa sababu wazazi wa mume na ndugu wanampenda sana. Anaogopa kuwaudhi kwa kuondoka kwenye ndoa ya mateso ya mtoto wao na ndugu yao. Anataka wafurahi, hivyo hawezi kuondoka. Huu nao ni upungufu.
Hivi unakuwa umeolewa na ndugu na wazazi au na mume? Lakini, kwani ukiondoka utashindwa kuwa karibu na watu hawa? Hutashindwa na pengine urafiki wenu utakuwa wa kudumu. Ukiendelea kukaa kwenye ndoa ya mateso kuna siku utakosana hata na hawa, maana unaweza ukalipukwa ukamuuwa mtoto au ndugu yao.
Kuna wale wanaoshindwa kutoka kwenye uhusiano mgumu kwa sababu wana watoto na wanaogopa kwamba, watoto wao watateseka. Hivi ni kuteseka kupi kubaya, kule kwa utotoni au ukubwani? Mtoto anayeishi kwenye ndoa yenye vurugu, anaharibikiwa kuanzia utotoni hadi ukubwani. Lakini, hata hivyo kuachana kwa wazazi, sio lazima kuwe na maana ya watoto kuteseka.
Kuna wakati hata watoto wanamwambia mama atoke kwenye ndoa, halafu mama huyo huyo anadai anakaa kwenye ndoa hiyo kwa sababu ya watoto! Kuna haja ya kujiuliza maswali kwa upana zaidi.
Ukitaka kutoka kwenye ndoa ngumu jiulize maswali haya. Je, ndoa hii ni kwa faida ya nani? Je, niliolewa au kuoa ili kupata shida au amani na upendo? Je, bila ndoa,nisingeweza kuishi mwenyewe? Tafuta mifano ya wasio na ndoa ambao wanafurahia maisha.
Jiulize ni kwa kiasi gani wengine wanasaidia kukusukuma zaidi kwenye ndoa hiyo? Jiulize ukamilifu wako. Je, wewe ni nusu mtu au mtu kamili? Kama ni mtu kamili , basi ishi kama mtu kamili. TUONANE TENA PANAPO MAJALIWA JUMATANO IJAYO. UPENDO DAIMA!!

Wednesday, November 30, 2011

SWALI LILILONIKERA KWA MIAKA MINGI!!!

Nimeshindwa kuvumilia mwenzenu, kwani hili jambo/swali limekuwa likinikera miaka sasa.

Ni hivi:- Hivi kwanini mwanamke mjane anweza kuishi peke yake mudamrefu au hata milele bila kuolewa tena na mwanamume mwingine? Maana ukiangalia asilimia kubwa ya wanaume wajane huwa hawaishi muda mrefu peke yao huwaa wanaoa tena.

Nina mfano mmoja, bibi yangu mzaa mama:- Babu alifariki mwaka 1980 na bibi amekuwa mjane mpaka Mwenyezi Mungu alipomchukua 2005. Na mafano mwingine nilionao ni baba mmoja nimfamuye mkewe alifariki 2004 na yeye 2006 tayari alipata mwanamke mwingine na kufunfa naye ndoa 2008.
Je?Hapa ndo kusema wanawake wanawapenda zaidi waume zao/wana uchungu zaidi kuliko wanaume?
NAOMBA TUJADILI KWA PAMOJA SWALA HILI JAMANI... KAPULYA WENU!!!!!

Tuesday, November 15, 2011

KUOLEWA NA WANAUME WAWILI!!

Baada ya kusoma habari hii nimekuwa nikijiuliza ya kwamba kwanini kujipa taabu hasa pale asipojua kama uzauzito huu ni wa nani? Kwa sababu inaonekana, hata kama anawawekea zamu hata hivyo imekuwa ngumu kujua nani na baba. Katika jamii yetu "tumezoa" kuona wanaume ndo wanaoa wake 2-4 na anawawekea zamu na hata wakiwa wazawazito inajulikana ni yeye mume/bwana ndiyo baba. Kama mke hajawa mjanja na kutoka nje kwa kushindwa kusubiri zamu yake.. Sasa hii ya kuolewa na wanaume wawili kaaazii kwelikweli. Palipo na wengi haliharibiki nenoo. Naamini mtanisaidia kuelewa jambo hili!!!

Thursday, June 23, 2011

MIAKA NANE YA NDOA, LAKINI HAYA MAUZA UZA NINAYOYASHUHUDIA NABAKI KUJIULIZA, TATIZO NI MALEZI AU NI WAPAMBE?

Ndio, leo hii natimiza miaka nane ya ndoa, lakini nikiwa peke yangu.
Sio kwamba mwenzangu katangulia mbele ya haki, au amesafiri, la hasha,
yupo, tena hapa hapa mjini, yu buheri wa afya kabisa.
Siku kama ya leo, ilikuwa ni furaha isiyo kifani mimi na mume wangu
tulikuwa tumesimama madhabahuni tukila kiapo cha ndoa mbele ya wazazi
wetu, ndugu, jamaa na marafiki. Nakumbuka nilikuwa nimemuangalia mume
wangu usoni wakati alipokuwa akitamka yale maneno ya mwisho ya kiapo
yasemayo, “mpaka kifo kitakapotutenganisha” Alikuwa akionekana dhahiri yale maneno yalitoka katika moyo wake ambao
ulijaa upendo wa hali ya juu, upendo ambao kwangu mimi niliuona
dhahiri ni maalum kwa ajili yangu. Nilimuamini sana mume wangu tangu
aliponitamkia miezi kumi na nane iliyopita kwamba ananipenda na
angependa tuoane.
Naikumbuka vizuri sana siku nilipokutana na mume wangu, ni siku ambayo
kamwe sitakuja kuisahau katika maisha yangu, sijui nisemeje lakini
ninachoweza kukushirikisha wewe msomaji ni kwamba, huyu alikuwa ndiye
mwanaume wa kwanza kukutana naye na moyo wangu kulipuka katika penzi
zito lisilo na mfano.
Mwanzoni mwa maisha yetu ya ndoa, nilianza kuhisi jambo, kwani
nilianza kushuhudia ndugu wa mume wangu wakiwa ndio washauri wakuu wa
mume wangu. Nilijikuta kila mara nikiwa nimeachwa nje kwa kila jambo,
yaani nilikuwa sishirikishwi kabisa katika mambo muhimu ya kifamilia
jambo ambalo lilikuwa linaniuma sana.
Kwa kuwa mume wangu ana uwezo kifedha kwa kiasi fulani, amejikuta
akiwa amezungukwa na ndugu kiasi kwamba wao ndio wamekuwa wakimtegemea
kwa kila kitu mpaka kusomeshewa watoto, na wanahisi labda ndugu yao
angeweza kuwasaidia zaidi, kama sio uwepo wangu yaani kuolewa kwangu.
Nadhani hapo nyuma alikuwa akiwapa misaada mingi sana na huenda tangu
anioe kumetokea upungufu wa misaada tofauti na zamani kwa sababu ya
majukumu ya kifamilia ambayo hakuwa nayo hapo nyuma.
Katika kila ndoa kama mnavyojua kuna kutofautiana kimitizamo na
kukwaruzana kwa hapa na pale kitu ambacho hakiepukiki. Ila kitu
kilichokua kina ni sikitisha ni pale tu mwenzangu anapokua hajali
ushauri wangu na kufata ule wa ndugu zake.
Nilipokuwa najaribu kumshauri mwenzangu, anakuwa ni mkali kupindukia,
ilifika mahali nikajiona kama mtumishi wa ndani.
JUU YA KIDONDA UKAWEKWA MSUMARI WA MOTO
Nikiwa bado nasakamwa na yeye mwenyewe pamoja
na ndugu zake, na kama hiyo haitoshi mnamo Januari mwaka
huu nikampoteza baba yangu.
Ulikuwa ni msiba mzito sana kwangu, kwani, baba yangu alikua kama
ndiye baba wa mume wangu, ametusaidia sana walau kufikia hapa
tulipofika. Alikuwa ni baba mwenye busara sana na mwenye upeo wa hali
ya juu katika masuala ya kifamilia. Alikua akitatua matatizo yetu
mengi sana pale tunapokwaruzana na kutaka kusawazishwa ili maisha
yapate kuendelea.
wakati tunajiandaa na kumaliza 40 tangu baba yangu afariki, siku moja
akaja dada yangu kwa baba mkubwa ambaye ameolewa na mjomba wa
mume wangu. Dada yangu ambaye nilitarajia angekuwa upande wangu, alinitamkia bila kutafuna maneno kuwa wanafamilia ya mume wangu wamefurahi sana na pia
kufanya sherehe baada ya Baba yangu kufariki kwani sasa matakwa yao ya
mimi kuachika yatatimia, hakuishia hapo alitoa maneno mengi ya
kashfa dhidi yangu. Wakati wote mie nilibaki kimya nikiwa siamini kile
kinachotokea mbele yangu.
Baada kusema yale aliyosema na roho yake kuridhika aliondoka huku
akiendelea kunipiga vijembe. Nilibaki pale kwenye kiti kama
walivyonikuta nikitafakari juu ya kadhia ile….. Naam baada a
kutafakari mtiririko wa matukio yaliyopita kati yangu na mume wangu
tangu baba yangu afariki nilianza kuamini maneno ya ndugu zake. Kwani
tangu baba yangu afariki nilianza kuona mwenzangu anabadilika,
hanijali tena na alikuwa na majibu ya ovyo ovyo hata kama namuuliza
jambo la msingi. Nadhani alikuwa ananiheshimu japo kwa kiasi kidogo
kwa sababu ya kumuogopa baba, na kwa kuwa baba ameshafariki, sasa ni
nani nitamkimbilia ili kutaka kusawazishwa pale tutakapokuwa
tunatofautiana………..Nikajua sasa nimekwisha, nilijikuta nikitamka
maneno hayo kwa sauti, nilishtuliwa na sauti yake akinijibu, “ni bora
umelifahamu hilo mapema” hata sikujua aliingia pale ndani saa ngapi?
Hata sikumjibu, nilibaki kumwangalia tu kisha nikaguna, niliingia
chumbani na kujitupa kitandani, ambapo nilipitiwa na usingizi mzito.
Nilishtuliwa na mwenetu pekee wa kiume ambaye ndio alikuwa ametimiza
miaka 6, alikuwa amerudi kutoka shule. Niliamka na kumkumbatia
mwanangu huku machozi yakinitoka. Mwananu alishtuka na kuniuliza,
“mama unalia?” Nilimdanganya kuwa nimemkumbuka babu yake, yaani baba
yangu, mwanangu aliniambia pole na nilimuona dhahiri na yeye akiwa
amegubikwa na uso wa huzuni.
Sikujua kwamba ule ulikuwa ndio mwanzo wa Segere, kwani baada ya
kumaliza 40 ya baba siku kama ya 5 hivi, nakumbuka ilikuwa ni Februari
18, 2011, ulizuka ubishani kati yangu na mume wangu ambao ulizua mzozo
mkubwa tu. Nilijikuta nikapandwa na hasira na kumbwatukia yale maneno
yote niliyoambiwa na ndugu zake.
Mwenzangu katika hali ya taharuki alikasirika sana na nilishangaa
kumuona akichukua baadhi ya nguo zake chache na vyeti vyake akatia
kwenye gari na kuondoka zake, kwa kuwa ilikua usiku wa manane
nikampigia mama mkwe simu kumueleza, maana lolote laweza tokea. Kwa
ufupi mama hakuchukua hatua yeyote ile, na wala hakuja kwangu kujua
sababu ya mume wangu kuondoka katika mazingira ya kutatanisha.
Hata hivyo nililala nikijipa moyo kuwa huenda atarudi kwani alikuwa
amekunywa pombe kidogo, na labda kutokana na hasira na ndio maana
akaamua kuondoka, ingawa jambo lile kwa kweli lilinishtua kwa sababu
tangu tumeoana haijawahi kutokea tukatofautiana kiasi cha mume wangu
kuikimbia nyumba yake. Ndugu msomaji labda unaweza ukashangaa
nikikueleza kwamba mpaka leo hii ambapo ndoa yetu inatimiza miaka 8
sijamtia machoni mume wangu.
Juhudi za kumsihi mama mkwe atusuluhishe zimegonga mwamba kwani
alinitamkia waziwazi kwamba amemchukua mtoto wake na anaishi naye
nyumbani kwake mpaka hasira zitakapo muisha! Alienda mbali zaidi na
kudai kwamba haoni sababu ya kukaa kikao maana hakuna mtu katika ukoo
wangu ambaye wanaweza kumuita na kuongea naye!
Kauli hiyo iliniuma sana. Nilijiuliza, hivi ina maana mimi kufiwa na
wazazi wangu hakuna ndugu yangu anayestahili kuthaminiwa na ndugu wa
mume wangu? Je ina maana hata yale maneno waliyonieleza kuwa
wamefurahia baba yangu kufariki ni kweli?
NAJIULIZA!
Je nifanyaje? Nianze mchakato wa kudai talaka ili niwe huru? Kwa kweli
sina uhakika hata kama tukisuluhishwa sidhani kama tutaweza kuishi kwa
amani, maana kuishi na mtu huku ukiwa unajiuliza je tukigombana
ataondoka tena? na hiyo kama ataondoka nitakuwa na hali gani? mgonjwa?
sina kazi? sina uwezo wa kutunza mtoto? Maswali ni mengi kwa kweli.
Jambo hili linaniumiza sana maana nilijua nimekwisha pata asilimia
kubwa ya vitu ambavyo nilikua navihitaji katika maisha kwa mfano
tayari nimeshapata mume, mtoto, kazi nzuri kwa hiyo nilichokua nawaza
ni maisha ya kiroho, lakini sasa imenilazimu nirudi tena kujipanga
upya.
Dada Yasinta nimeona nikutumie mkasa wangu huu ili kuwashirikisha
wadau wa kibaraza chako cha MAISHA NA MAFANIKIO, kibaraza ambacho mimi
ni msomaji mzuri na nimekuwa nikifuatilia mijadala mingi unayoiweka
hapo ambayo inawavutia wasomaji wengi ambapo maoni na michango
inayotolewa ni darasa tosha.
Ni imani yangu wasomaji wa kibaraza hiki watatumia busara zao na kutoa
maoni na mitizamo yao kwa uhuru na haki bila kupendelea upande wowote.
Sikueleza hayo hapo juu ili kujidhalilisha, bali kutaka kupata
suluhisho ya kile ambacho nakabiliana nacho nikiamini kwamba sisi kama
binaadamu kuna wakati tunahitahi ushauri kutoka kwa wenzetu ili tumudu
kukabiliana na changamoto za maisha.
Natanguliza shukrani zangu za pekee kwako na kwa wadau wote wa Blog
popote pale Duniani.

Ni mimi msomaji wako.
Dada Gly

Thursday, April 21, 2011

HESHIMA KWA WANAWAKE

Kweli huu uungwana?


Acheni niwape heshima iliyotukuka wanawake woote;
IMAGINE:

ANAKUFUMANIA: Analia, ananyamaza, anasononeka, unambembeleza anakuelewa
anakusamehe halafu anasahau!!!

UNAZAA NJE YA NDOA: Anasononeka na kulia sana. Anakuchukia lakini baadaye
anakusamehe. Halafu analea mtoto uliyemzaa nje kwa upendo. Kama ni
kuchukiwa atachukiwa mtoto, si wewe uliyefanya umalaya!

UNARUDI USIKU WA MANANE UKIWA MTUNGI: Anakukaribisha, anakuandalia
chakula, unagoma kula. Anahifadhi chakula alichokuandalia bila
manung'uniko.

UNAAMKA ASUBUHI NA MAHANGOVER: Anakuandalia staftahi (saa nyingine unagoma
kutumia staftahi yake unakimbilia baa kwenda kunywa Supu na kuzimua. Wala
halalamiki!

CHAKULA CHA USIKU: Ushapiga mtungi wako, unataka huduma. Unamrukia, hamna
maandalizi unamuumiza. Anavumilia ili akuridhishe. Na kesho yake tena
inaweza tokea hii; hana kinyongo!

UNAJIANDAA KWENDA KIBARUANI: Unakuta kashakuandalia viwalo, suruwale
imenyooshwa kama ya askari trafiki, shati limepigwa pasi ya maana! Nguo
ulizovua jana zimeshalowekwa tayari kwa kufanyiwa usafi! Ulichomuudhi jana
kashasahau na kukusamehe!

UNAMPA UJAUZITO: Anauthamini, anautunza anajifungua kwa uchungu, mtoto
anakuachia wewe umpe jina, la kwake halimo kabisa kwenye majina
atakayotumia mtoto! Na pamoja na uchungu wa kuzaa, bado yuko radhi
kukuzalia mtoto mwingine na mwingine tena!

Na mengine meeeeengi sana wanafanyiwa hawa watu lakini WANASAMEHE,
WANAVUMILIA! Ni watu muhimu sana hawa watu maishani mwangu!

HIVI INGEKUWA WANAUME TUNAFANYIWA HIVI INGEKUWAJE?

Nimeipenda habari hii na nimeona niwahabarisha na wenzangu kwani elimu ni kuelimishana. habari hii imetoka Jamii Forum.