Thursday, July 30, 2015

NGUO ZA ASILI NA UREMBO WINGINE KWA BAADHI YA NCHI ZA AFRIKA!

 MAASAI/TANZANIA/KENYA
 ZULU/AFRIKA YA KUSINI
 ETHIOPIA
UGANDA
Nimependezwa/napendezwa kuona baadhi ya nchi na makabia wanaendeleza mavazi yetu ya asili....Ngoja nami nitafuta vazi la asili la kingoni:-)

Tuesday, July 28, 2015

BUSTANI YETU NA MAENDELEO YAKE:- MAVUNO YA MARA YA PILI

Ni Mchicha mboga Maboga na Figiri  nimechuma na nimechemsha na kuweka akiba si mnajua akiba haiozi...Hii ndi kazi ya mikono yangu, mtoto wa mkuli ni mkulima:-) Ila msiogope  sijahifadhi yote karibuni tujumuike.

Monday, July 27, 2015

SAFARI YETU YA TANZANIA NA ZANZIBAR TULIPATA BAHATI YA KUNUNUA PICHA HIZI ZA TINGATINGA UTAMADUNI WETU:-)

 TWIGA HUYU
Na hapa ni aina ya wanyama wote walioko Afrika/Tanzania...WANAZIITA PICHA ZA TINGATINGA.....TAYARI ZIMEKWISHA BANDIKWA UKUTANI.

Sunday, July 26, 2015

HILI NI CHAGUA LA BLOG YA MAISHA NA MAFANIKIO KUWA HII NI PICHA YA WIKI:- JUMAPILI NJEMA KWA WOTE

Sasa hapa sijui tusema ni  kumpendeza Jogoo au? Unafikiri Jogoo anapenda kuvaa hivyo kweli?...Haya Niwatakieni JUMAPILI NJEMA SANA! AMANI NA UPENDO VITAWALE KATIKA FAMILIA ZETU.

Wednesday, July 22, 2015

KANGA NA MISENO /MAANDISHI YAKE.....

Hivi kweli MAPENZI ni pesa? Mmmmhhh ningeomba tujadili pamoja hapa inawezekana mimi nimeelewa vibaya....Kapulya wenu:-)

Tuesday, July 21, 2015

MAWAZO MAKUBWA YA KUFIKIRISHA .....

Mvulana mmoja maskini alikuwa akiangalia gari la bwana mmoja ambaye alikuwa tajiri, tajiri alimchukua yule mvulani na kumwendesha katika lile gari. Mvulani  akasema una gari nzuri sana. Je? hili gari si ghali sana? Tajiri akamjibu, ndiyo ni ghali sana ila mimi nilipewa na kaka yangu kama zawadi.
Mvulana akawa anafikiri. Tajiri akamuuliza unawaza nini? Ebu ngoja, nawe unataka kuwa na gari kama hili eehh? Mvulana akamjibu HAPANA....NATAKA KUWA KAMA KAKAYAKO!!!

Saturday, July 18, 2015

BUSTANI YETU NA MAENDELEO YAKE...KAZI YA MIKONO YANGU

 Hapa ni MCHICHA upo katika hali nzuri kidogo
 Na hapa ni mboga MABOGA sisi wanguni tunasemana LIKOLO LA NANYUNGU/PITIKU:-)
Na hapa mnaona ndo mara ya kwanza kuchuma hiyo mboga ya Maboga na mchicha na pembeni mnaona ni pilipili. Kwa hiyo kwa jioni ya leo ni kujichana tu. KARIBUNI TUJUMUIKE NDUGU ZANGU:-) ni mimi Kapulya wenu.

Friday, July 17, 2015

SWALI/WAZO LA LEO!

Kama kungekuwepo na ndoto za kununua, je? Ni ndoto gani wewe ungenunua?

Tuesday, July 14, 2015

MSIONA KUADIMIKA NIPO....TUPO PAMOJA

Ningependa kuwanongóneza kuwa nipo likizo. Ila nitajitahidi kuwa nanyi pia kinamna ili tusisauliana..ila mmmhhh kuwasahau ndugu si rahisi...WOTE MNAPENDWA NA TUPO PAMOJA. UTAMADUNI/KIMASAI:-)UDUMU MILELE

Saturday, July 11, 2015

NAPENDA KUWATAKIENI WOTE MWISHO WA JUMA UWE MWEMA..

Hili ni vazi langu la leo au mwenekano wangu wa leo na napenda kuwatakia wote JUMAMOSI NJEMA AU MWISHO WA JUMA MWEMA. KAPULYA.

Tuesday, July 7, 2015

NGOMA YA ASILI YA MGANDA KATIKA MKOA WA RUVUMA!!

Ngoma ya asili ya Mganda ilinogesha katika ufunguzi wa stendi ya Mabasi mjini Mbinga Mkoani Ruvuma Julai 19,2014, stendi hiyo ilifunguliwa na Rais Jakaya Mrisho Kikwete wakati akiwa Mkoani Ruvuma katika ziara ya Kikazi kukagua miradi ya maendeleo.

Sunday, July 5, 2015

UNAKUMBUKA HII? :-) MAHINDI YA KUKAANGA

Mahindi ya kukaanga:- hapa sasa iwe hii siku kunanyesha mvua basi  ndo utaona utamu wa mahindi ya kukaanga kwa mtindo huu....JUMAPILI NJEMA WANDUGU.