Showing posts with label sambusa. Show all posts
Showing posts with label sambusa. Show all posts

Friday, May 23, 2014

VYAKULA NILIVYOTAMANI IJUMAA YA LEO.....SAMBUSA NA EMBE!!!


Leo nimetamani kweli SAMBUSA kitu ambacho kinachosha ni kwamba nimewahi kujaribu kutengeneza na sikuweza kama inavyotakiwa na huchukua muda mwiiiingi sana. Sijui kuna njia rahisi zaidi? Halafu......

.....nikajikuta naota ndoto ya hili tunda EMBE...Songea ndo zinakwisha kwisha sasa....Kaaaazi kwelikweli ngoja niache kuota .....IJUMAA NA MWISHO MWEMA WA JUMA!!

Friday, June 12, 2009

IJUMAA YA LEO NAWAKARIBISHENI SAMBUSA ZA NYAMA ASIYEKULA NYAMA ZIPO ZA MBOGA PIA KARIBUNI SANA

VIPIMO
(Manda ya sambusa ya tayari Kiasi zinavyouzwa
Kiasi cha sambusa 40-50)
Mafuta ya kukaangia Kiasi
Nyama ya Kusaga kilo moja na nusu 3LB (Pounds)
Thomu na tangawizi iliyosagwa 2 Vijiko vha chai
Pilipili mbichi iliyosagwa 1 Kijiko cha chai
Pilipili manga 1 kijiko cha supu
Garam masala 1 kijiko cha supu
Chumvi Kiasi
Vitunguu maji vilivyokatwa
(chopped) 3 Vidogo au 2 Vikubwa
Kotmiri iliyokatwa (chopped) Kiasi

NAMNA YA KUTAYARISHA NA KUPIKA

1. Pika nyama ya kusagwa kwa kutia chumvi, thomu na tangawizi, pilipili na ndimu.
2. Kabla haija kauka tia Garam masala.
3. Zima moto acha kidogo ipoe tia vitunguu na kotimiri.
4. Funga sambusa katika manda kama kawaida.
5. Pika sambusa katika mafuta ya moto hadi ziwe nyekundu na zikiwa tayari kuliwa.