Showing posts with label baridi. Show all posts
Showing posts with label baridi. Show all posts

Wednesday, November 22, 2017

MSIMU WA BARIDI ....THERUJI YA KWANZA KUANGUKA KUONA NYASI TENA MPAKA MWEZI WA NNE:-(

Leo huku nje ni kimbembe thuriji imeanza kuanguka juzi, lakini leo ndo kwanza inazidi na upepo juu....Ni taarifa tu kwa ufupi. Nawatakieni siku njema.

Monday, December 28, 2015

PALE HALI YA HEWA INAPOBADILIKA...LEO ASUBUHI ILIVYOKUWA/DET SNÖAR!

Mila na desturi au nisema ni mazoea ya nchi nyingi za Ughaibuni/ulaya siku ya Krismas kuwa na thaluji yaani kweupe huko nje lakini krismas hii haikuwa hivi hasa Swedan badala yake theluji imeanguka jana 27/12 mpaka leo 28/12 na kamera ya maisha na mafanikio imebahatika kupata picha hizi kama uonavyo...
Wakati mwingine ni safi kuacha gari na baiskeli na hapo ndipo utakapofaidi mambo angalia hii picha  hapa nilikuwa nikitoka mazoezi ya asubuhi:-) pia ni vizuri kutembea/kimbia na kamera......

 Basi nikalipokaona hako kajua nikaanza kuimba kala kawimbo ka mchakamchaka ....Jua lile...nikabadili nikaanza kuimba Idiamini akifa mimi siwezi kulia......Kama nilivypsema Ujenzi unabana ila leo nimepata kamuda...na pia sasa nitapumzika kidogo na ujenzi mpaka huu mwaka uishe ndo tutaendelea...Bado siku 4-3½ hivi kuufikia mwaka  mpya...TUOMBEANA  ILI TUWEZE KUUONA ...NI MIMI KAPULYA WENU!!


Monday, December 3, 2012

HIVI NDIVYO HALI YA HEWA ILIVYOKUWA FINLAND LEO!!!

Hali ya leo Finland...hapa kwetu bado haijaangua kihivyo ila kuna baridi kali sana kiasi kwamba ile kutoka tu nje pua inasinyaa kabisa....Mwaka huu itakuwa kali kwelikweli...JIONI NJEMA KWA WOTE.....

Friday, March 12, 2010

Majira katika mwaka:- kaskazi/baridi, kiangazi, masika na kipupwe hapa Sweden!!

Nipo juu ya mlima Kilimanjaro!!Majira ya baridi kali , ni mwezi huu wa tatu na hapa ilikuwa jumamosi iliyopita

Hapa baridi inaanza ni mwezi wa nane mwaka 2009 (autumntime) Höst. Ni majira ya kupukutika kwa majani.
Hapa ni 2009 mwezi wa nne-tano (Springtime) Majira ya kuchipua.


Na hapa ni mwaka 2008 (Summertime) Majira ya joto hapa tupo mji wa Karlstad nje ya tangi kubwa la maji.

NAPENDA KUWATAKIENI WOTE MWISHO MZURI WA JUMA HILI , MUWE NA WAKATI MZURI NA AFYA NJEMA !!!!!


Wednesday, September 30, 2009

HÖST/AUTUMN = MAJIRA YA BARIDI YA KUPUKUTIKA MAJANI BRRRRRRR!!!!

Hapa ni leo mchana kama saa nane hivi

Nadhani mnaona vazi la leo ni tafaouti na picha nyingine kwani sasa baridi imeanza leo asubuhi iliwa -0.4C. Waliofika Njombe, Iringa Makambako na pia Mbeya wanajua. Mmmmh kazi inaanza sasa kaziiiii kwelikweli, maana mtu unavaa nguo na mwisho unaonekana kama una kilo elfu kumi. Haya ngoja niache.

Wednesday, September 3, 2008

HÖST= AUTUMN MAJIRA YA KUPUKUTIKA KWA MAJANI

Mmmh! Sasa mapambano yameanza, yaani hapa Sweden kwa sasa ni majira ya baridi, kupukutika majani. Kuna upepo, baridi, mvua, jua kidogo halafu giza pia limeanza kuingia mapema kidogo.

Huwezi kuamini miezi mitatu iliyopita kulikuwa kunapendeza sana maua mazuri na joto kali kama Bongo. Yaani watu tulikuwa tunavaa nguo nyepesi na kandambili au pekupeku. Lakini sasa mmh haiwezekani ni lazima kuvaa sweta nzito na pia viatu(raba) kusema kweli kipindi hiki natamani sana kuwa Tz.

Na ni wakati huu watu wengi wanapata mafua na pia kukoho. Na hapa ni mwanzo tu, baadaye ndo itakuwa kazi zaidi, ambayo inanichosha sana yaani kuvaa koti kubwa, soksi, viatu vizito, kofia na glavu(glove) Hapo ndo mtu unapoonekana mnene kama tembo. Mmmh! Maisha kazi kweli

Sunday, March 30, 2008

Machi 30,2008 HALI YA HEWA/PASAKA

Naam! wasomaji nafikiri mmesoma blug yangu kuhusu pasaka. kama hujasoma basi chukua fulsa na usome. Kwa kweli nakuambieni ama kweli watu wana mila na desturi. nimeshuhudia sio kula mayai tu kama nilivyosema isipokuwa kuyapaka rangi tofauti baada ya kuchemshwa. Haya sasa najua sehemu nyingine kama Afrika (TZ) pasaka imesheherekewa na jua/joto. Sio hapa kuna baridi na pia theruji ilianguka. Samahani kidogo nimeingia kwenye hali ya hewa hii yote ni kwa sababu sikutegemea kutakuwa na baridi kali hivi. Nafikiri ni kwa sababu hali ya hewa imebadilika kwani hii theruji ilibidi iwe krismas sio sasa. Lakini sasa inaonekana kuna mabadiliko. Ngoja nirudi kwenye Pasaka tena, kama nilivyosema. jumamosi kuu ndio sikukuu kubwa hapa sio Jumapili (pasaka kwa sisi ) nina maana watu wengi pamoja namimi tunajua kuwa jumapili dio PASAKA.
Katika blogu ya mdogo wangu KARIBU NYASA amenikumbusha mbali sana. Yaani ameniacha hai kabisa. Maana inaonekana huko Pasaka ilikuwa nzuri sana wamatengo na ngoma zao, wangoni/wamanda na zao pia vinywaji nk. mpaka natamani.

Na; Yasinta Ngonyani