Namshukuru Mwenyezi Mungu, kwa kuniongezea mwaka mwingine katika maisha yangu....kuna wengine walizaliwa siku kama hii lakini hawapo duniani kusherekea siku yao.
Hongera kwa mimi na wengine wote waliozaliwa siku kama hii......uzee nao ndo huuoo unanivizia KARIBUNI KUSHEREHEKEA NAMI:-)
Showing posts with label miaka. Show all posts
Showing posts with label miaka. Show all posts
Friday, January 5, 2018
Saturday, January 5, 2013
LEO NI SIKU YANGU YA KUZALIWA ....MIAKA INAKWENDA JAMANI
Sunday, June 3, 2012
LEO KIJANA ERIK ANATIMIZA MIAKA 12...HONGERA ERIK!!!
Tarehe kama ya leo 3/6/2000 familia iliongezeka, alizaliwa kijana huyo Erik na leo hii anatimiza miaka 12. Erik, sisi wazazi, dada, ndugu pia marafiki wote tunakutakia kila la heri katika yote unayofanya. Kama vile masoma, yako, kwa vile unapenda sana michezo kama vile mpira wa miguu, flow boll na michezo mingine basi tunakutakia juhudi snyingi. Erik anasoma darasa la tano kwa sasa karibu ataanza la sita. Mwenyezi Mungu na akubariki uwe mtiiifu, mwenye juhudi kimasoma na mengine yote. DUH! KAMA MCHEZO LEO MIAKA 12. HONGERA KWA SIKU YA KUZALIWA ERIK.!!!!
Thursday, January 5, 2012
LEO NI SIKU YANGU YA KUZALIWA!!!
NAPENDA PIA KUSHEHEREKEA SIKU HII KWA WIMBO HUU:-)
NAMSHUKURU MUNGU KWA YOTE, FAMILIA YANGU PIA NINYI NDUGU ZANGU NA MARAFIKI WOTE NA NASEMA NAWAPENDENI SANA:-)
Tuesday, December 13, 2011
Hongera kaka John Mwaipopo kwa kuongeza mwaka"!!!
Monday, November 14, 2011
HONGERA KWA SIKU YA KUZALIWA MTANI WANGU FADHILI MTANGA!!
Leo ni ni siku huyu kijana alizaliwa na blogg ya Maisha na Mafanikio inapenda kumtakia HONGERA KWA SIKU HII. Kwani ni siku muhimu sana kwake na pia kwetu kwani tumekuwa kama ndugu sasa. Basi ngoja tuselebuka siku hii pamoja na kaka huyu kwa wimbo huu nina imani ni nyimbo azipendazo.....HONGERA FADHY!!!
Wednesday, September 28, 2011
HONGERA KWA SIKU YA KUZALIWA KAKA YANGU SHABAN KALUSE!!!
Napenda kuchukua nafasi na KUMPONGEZA KAKA YANGU WA HIARI SHABAN KALUSE kwa siku yake ya kuzaliwa. Shaban Kaluse ni kaka mmoja ambaye ni mshauri mzuri sana , msikilizaji, sio mbinafsi. nk. Nikuambieni kitu kimoja? Ni hivi mimi au pia watu wengine wanafikiri kaka, dada au ndugu ni yule uliyezaliwa naye tumbo moja yaani mama mmoja na baba mmoja. LA HASHA. Kaka huyu amekuwa KAKA kweli na amekuwa mwema sana katika familia ya akina NGONYANI. HONGERA SANA KWA KUTIMIZA MIAKA 40 NI MIAKA MINGI MWENYEZI MUNGU AKULINDE NA AKUJALIE AFYA NJEMA!!!
Friday, June 3, 2011
HONGERA KWA SIKU YA KUZALIWA KWAKO ERIK !!!/Grattis på Födelsedagen Erik!!!
Leo ni siku /tarehe ambayo kijana huyu alianza maisha yake. Yaani alizaliwa ni miaka kumi na moja iliyopita tarehe 3/6/2000 alizaliwa kijana Erik. Na leo anatimiza miaka 11. Kama mumuonavyo Erik anapenda sana mpira wa miguu, floorball /innebandy. Pia mziki pia. HONGERA KWA SIKU YAKO YA KUZALIWA ERIK NA UWE NA SIKU NZURI. PIA KILA LA KHERI KATIKA MASOMO YAKO, NA KATIKA MAISHA YAKO.!!!!!!!
Wednesday, April 27, 2011
HONGERA KWA SIKU YA KUZALIWA KWAKO DA´MIJA MWANAMKE WA SHOKA!!!

Napenda kukutakia siku yako ya kuzaliwa kheri na baraka tele. Mwenyezi Mungu na akulinde uwe salama pia uwe na afya njema siku zote. Na pia uwe bibi kizee ili uweze kucheza na wajukuu wako pia vijukuu. HONGERA SANA KWA SIKU YAKO HII TUKUFU KWA KUONGEZA LIMWAKA:-) UWE NA SIKU NZURI NA WALA USITHUBUTU KUTUNYIMA HIYO KEKI!!!
Zaidi unaweza kumwona mwanamke huyu wa shoka kwa kubonyeza Da´Mija.
Monday, January 3, 2011
HONGERA KWA SIKU YA KUZALIWA KAKA MFALME MROPE
Nakutakia kila la kheri sio leo tu ila kila wakati utakapofanya jambo/mambo yako. Kaka huyu anapatikana hapa. HONGERA SANA KWA SIKU YAKO YA KUZALIWA!!! .
Wednesday, October 13, 2010
HONGERA SHANGAZI YANGU PAULINA ARIANNA BANDIO KWA KUTIMIZA MWAKA MMOJA
Binafsi nitakuita Shangazi/rafiki yangu. Lakini kuna wengine watakuita
binti, mtoto, binamu, mpwa n.k.
Shangazi/rafiki yangu Paulina leo ni siku kubwa sana kwako. Ni mwaka sasa
umepita tangu uyaanze maisha yako. Yaani leo unatimiza mwaka 1(mmoja) kwa
kweli miaka inakimbia sana, ni juzi tu ulikuwa kachanga leo hii umekuwa
binti wa kuweza kukutuma utuchotee maji ya kucnywa na karibuni tu utatupikia
na hata ugali.
Blog ya Maisha na Mafanikio inapenda kutoa pongezi nyingi sana kwa wazazi wa binti Paulina ambao ni Mubelwa na Esther Bandio kwa malezi
mazuri wampayo mtoto Paulina. Mwenyezi Mungu awazidishia nguvu ili muzidi
kumlea mtoto huyu na awe kama ninyi wenyewe.
Unaweza kuwatembela Mubelwa.
binti, mtoto, binamu, mpwa n.k.
Shangazi/rafiki yangu Paulina leo ni siku kubwa sana kwako. Ni mwaka sasa
umepita tangu uyaanze maisha yako. Yaani leo unatimiza mwaka 1(mmoja) kwa
kweli miaka inakimbia sana, ni juzi tu ulikuwa kachanga leo hii umekuwa
binti wa kuweza kukutuma utuchotee maji ya kucnywa na karibuni tu utatupikia
na hata ugali.
Blog ya Maisha na Mafanikio inapenda kutoa pongezi nyingi sana kwa wazazi wa binti Paulina ambao ni Mubelwa na Esther Bandio kwa malezi
mazuri wampayo mtoto Paulina. Mwenyezi Mungu awazidishia nguvu ili muzidi
kumlea mtoto huyu na awe kama ninyi wenyewe.
Unaweza kuwatembela Mubelwa.
Tuesday, October 12, 2010
Tuesday, September 28, 2010
HONGERA KWA SIKU YA KUZALIWA KAKA YANGU SHABAN KALUSE

Kaka Shaban Kaluse
Napenda kukutakia HONGERA kwa siku yako ya kuzaliwa, na nakutakia kila la kheri kwa kila jambo utakalotenda liwe jema na pia nakutakia maisha mema, upendo na amani itawale katika familia yako. Na halafu uwe na mafanikio kwa kila utakalo tenda. Halafu najiuliza hivi siku hizi sijui upo wapi wewe kaka wa utambuzi ? HAYA HONGERA SANA KWA SIKU HII MUHIMU KATIKA MAISHA YAKO. HONGERA KAKA SHABAN!!!!!. Kwa kutaka kujua mambo ya mwanautambuzi huyo gonga hapa.
Tuesday, August 10, 2010
HERI KWA SIKU YA KUZALIWA KAKA MUBELWA T. BANDIO
Ni jambo la kumshukuru Mola kwa kututunza tangu siku ile tuzaliwapo mpaka kila mwaka kuongeza mwaka mmoja zaidi. Na leo ni siku kubwa sana kwako. Maana umetimiza makumi matatu sasa ni safari ndefu sana. HONGERA SANA. NA MOLA AKUBARIKI PIA AIBARIKI FAMILIA YAKO.Saturday, May 15, 2010
HONGERA KWA SIKU YAKO YA KUZALIWA MZEE WA LUNDU NYASA
Tuesday, April 27, 2010
HONGERA KWA SIKU YA KUZALIWA DA MIJA/MWANAMKE WA SHOKA!!
Ni furaha kuwa na rafiki kama Da Mija na leo ni siku tukufu kwako. Ni siku ambayo ulitokea hapa duniani . Napenda kukutakia yote mema, uishi miaka mingi uwe bibi kizee na wajukuu wengi uwe nao. Mija, kama wote tunavyomfahamu alizaliwa hapa dunuani ili awe mwanamke wa shoka nakuheshimu na pia nakupenda sana .HONGERA KWA SIKU YA KUZALIWA RAFIKI YANGU na MWANAMKE WA SHOKA WETU!!!!!!
Saturday, April 24, 2010
HONGERA KWA SIKU YAKO YA KUZALIWA MARIA FIDELIA NKUGI BINTI WA Chacha o'Wambura a.k.a Ng'wanambiti!
Friday, March 5, 2010
Heri ya Siku ya Kuzaliwa Mume,Baba na Shemeji pia Rafiki yetu
Ni siku yako leo mwl. Klayson
Tunaanza na kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa sala hii :- SALA YA MKE KUMWOMBEA MUMEWE
Ee Bwana , ni ajabu,
Jinsi fikra zangu zinavyomrudia kila mara
Huyu, mume wangu,
Mwenzi anayeshiriki maisha yangu kwa namna ya pekee.
Ninapofagia nyumba na mazingira yake,
Nataka kutengeneza nyumba nzuri kwa ajili yake.
Ninapopika chakula vizuri,Napenda kumfurahisha.
Ninaponunua nguo mpya na kujaribu kuonekana mrembo,
Ni kwa ajili yake tena, Ee Bwana.
Na ninaweza kukuambia kwamba
Ninamwonea fahari,
Anafanya kazi kwa bidii ili kupata riziki yetu;
Ni mtu mwenye haki, mwadilifu,
Naye hujitahidi kutufurahisha.
Kwangu, yeye ni mpole na mwangalifu.
Hunijali na kuonyesha kweli kwamba anajali.
Hunifanya mimi nijiamini mwenyewe,
Anajua jinsi ya kuondoa hofu zangu,
Hunipatia usalama na upendo ambao nahitaji sana.
Ee Bwana, ninakuomba,
Umbariki na umlinde.
Katika safari zake, umfikishe salama.
Kazini mwake, umpe fanaka
Na hapa, nyumbani petu naomba apate amani na heri.
Bwana, unisaidie mimi pia
Niweze kuwa yule mke anayehitaji.
Unifanye niwe mtu anayeweza kumwamini daima,
Mwanamke ambaye anaweza kumfurahia,
Niweze kumsaidia asahau matatizo yake,
Niweze kuondolea mbali hofu zake na kupunguza uchungu wake.
Bwana, Wewe ndiwe uliyenipa mume huyu,
Na katika yeye,Umenipatia sehemu ya nafsi yako mwenyewe.
Ninakusifu kwa ajili yake, Ee Bwana.
Na leo twakumbuka siku muhimu saana maishani mwako. Siku iiliyoanzisha yote mazuri/mema tujivuniayo maishani kwa uwepo wako. Ni SIKU HII ULIYOZALIWA
Zaidi mtembelee Mwalimu Klayson http://matetereka.blogspot.com/
Tunapenda kusindikiza siku hii na mwanamziki ambaye anampenda sana kwa wimbo huu wa DR. REMMY ONGALA Uitwao NARUDI NYUMBANI ni.
Ee Bwana , ni ajabu,
Jinsi fikra zangu zinavyomrudia kila mara
Huyu, mume wangu,
Mwenzi anayeshiriki maisha yangu kwa namna ya pekee.
Ninapofagia nyumba na mazingira yake,
Nataka kutengeneza nyumba nzuri kwa ajili yake.
Ninapopika chakula vizuri,Napenda kumfurahisha.
Ninaponunua nguo mpya na kujaribu kuonekana mrembo,
Ni kwa ajili yake tena, Ee Bwana.
Na ninaweza kukuambia kwamba
Ninamwonea fahari,
Anafanya kazi kwa bidii ili kupata riziki yetu;
Ni mtu mwenye haki, mwadilifu,
Naye hujitahidi kutufurahisha.
Kwangu, yeye ni mpole na mwangalifu.
Hunijali na kuonyesha kweli kwamba anajali.
Hunifanya mimi nijiamini mwenyewe,
Anajua jinsi ya kuondoa hofu zangu,
Hunipatia usalama na upendo ambao nahitaji sana.
Ee Bwana, ninakuomba,
Umbariki na umlinde.
Katika safari zake, umfikishe salama.
Kazini mwake, umpe fanaka
Na hapa, nyumbani petu naomba apate amani na heri.
Bwana, unisaidie mimi pia
Niweze kuwa yule mke anayehitaji.
Unifanye niwe mtu anayeweza kumwamini daima,
Mwanamke ambaye anaweza kumfurahia,
Niweze kumsaidia asahau matatizo yake,
Niweze kuondolea mbali hofu zake na kupunguza uchungu wake.
Bwana, Wewe ndiwe uliyenipa mume huyu,
Na katika yeye,Umenipatia sehemu ya nafsi yako mwenyewe.
Ninakusifu kwa ajili yake, Ee Bwana.
Na leo twakumbuka siku muhimu saana maishani mwako. Siku iiliyoanzisha yote mazuri/mema tujivuniayo maishani kwa uwepo wako. Ni SIKU HII ULIYOZALIWA
Zaidi mtembelee Mwalimu Klayson http://matetereka.blogspot.com/
Tunapenda kusindikiza siku hii na mwanamziki ambaye anampenda sana kwa wimbo huu wa DR. REMMY ONGALA Uitwao NARUDI NYUMBANI ni.
Sunday, February 21, 2010
HONGERA KWA SIKU YA KUZALIWA KWAKO CAMILLA !!

Miaka 12 imepita leo tangu binti yetu Camilla azaliwe. Ni binti ambaye anapenda sana kusoma, kuandika, kucheza mpira wa mikono (handball) pia anapenda aina ya mziki wa kupuliza au (trombone. ) Twakuomba Mwenywezi Mungu uwe /uzidi kumbari binti yetu Camilla azidi kuwa kama alivyo. Na pia twakoomba uzidi kutupa sisi wazazi/walezi nguvu ya kumlea ili azidi kuwa binti mwema na mwenye busara. CAMILLA HONGERA SANA KWA SIKU YA KUZALIWA.
mama mdogo Koero anasema
Hata hivyo ningependa kufanya sala fupi kwa ajili yako.
‘Nakutakia sherehe njema ya siku yako ya kuzaliwa na natumaini kila jema lililosemwa na wote waliokutakia sherehe njema ya siku yako ya kuzaliwa litatimia. Mungu atakubariki uwe na afya njema na ukue kwa umri na kimo na pia mungu akujaze na Hekma na Busara na uwe na uzingativu katika masomo yako’
Aaamen..............
Pia maneno haya ya mjomba Mzee wa Changamoto ni mazuri sana na ndio nimemwomba mama ayaweke hapa mbele Ahsante "mjomba"
Dah!!!
Sijui nianze na lipi hapa?
Ok.... Kwanza POLE na HONGERA kwa wazazi.
Kwa wale waliopitia uzazi na ulezi wanajua kuwa HONGERA ya kulea ni vema ikaambatana na POLE yake. Ni kwa kuwa kulea ni zaidi ya kazi. Ni zaidi ya wajibu.
Lakini HONGERA kwa mara ya tena kwa baadhi ya yale niyajuayo kwa "Mjomba" Camilla. Kwa kuendelea kupenda asili za atokako, kupenda kujua na kuongea lugha ya asili ya Mama. Kupeda na kufanya kazi kama kilimo, usafi, kuchota maji na nyingine nilizoona ukifanya wakati wa likizo ndeeefu ya Ruhuwiko.
Hongera kwa wazazi kwa kuanzisha haya yote.
Kwa "Mjomba" Camilla. Uko ulivyo na unavyotakiwa kuwa. Unayotenda ndiyo yenye uzuri kuliko mtazamo wa wengi kuhusu watu. Ninalomaanisha hapa ni kuwa UNA MATENNDO MAZURI AMBAYO NDIO TAFSIRI YA UZURI.
Tatizo pekee la umri unaokabiliana nao sasa (na pengine miaka 8 ijayo) ni kuwa watoto wenye umri huu "hujiona wenye akili zaidi ya yeyote huamini marafiki kuliko wazazi" na huamini kuwa wako mbele na sahihi kimawazo kuliko wazazi.
Najua umekuwa msikivu na mtii kwa wazazi, basi hilo ndilo nikuombealo na kukusihi uliendele.
U-mrembo kwa Taswira tuonazo na TABIA tujuazo.
Baraka kwako katika miaka teleee ijayo.
HERI YA SIKU YA KUZALIWA "Mjomba"
Friday, February 19, 2010
Hongera Kwa Siku Ya Kuzaliwa Kaka SAVIO!!!!
Wote tunakutakia kheri sana kwa siku hii maalum kwako kwa kutimiza miaka. Twakutakia mafanikio mema katika maisha na kila jambo ufanyalo pia familia yako . Kumbuka kwamba sisi ndugu, marafiki, wajombo, watoto, shemeji twakupenda sana. HONGERA KWA SIKU YA KUZALIWA KAKA SAVIO.!!!!
Kwa vile leo pia ni Ijumaa basi ngoja tusherehekee siku yako kwa kipande hiki cha muziki:-)
Subscribe to:
Posts (Atom)







