Showing posts with label liuli. Show all posts
Showing posts with label liuli. Show all posts

Wednesday, October 10, 2018

UTALII WILAYANI NYASA:- LEO TUFANYA UTALII KWENYE UFUKWE ULIOPOMJINI LIULI

     

Utalii ni sekta inayokua kwa kasi sana Duniani. Imechangia katika kukua kwa uchumi wa nchi nyingi sana, imeongeza ajira nyingi sana, zipo zile za moja kwa moja na zingine ambazo si za moja kwa moja.

Sehemu zinazo wavutia sana watalii si mbuga za wanyama, si milima, si mapango bali fukwe nzuri na tulivu za bahari na maziwa.
Uswisi inajulikana kama 'the playing ground of europe' kutokana na ziwa dogo la Geneva, Visiwa caribean, Zanzibar, Mombasa na kadhalika zimekuwa zikiwavutia sana watalii kutokana kuwa na fukwe zinazovutia.
Ziwa Nyasa ni moja ya maziwa safi bado halijaharibiwa na shughuli za kibinadamu.Lina fukwe nzuri,safi na salama,maji meupe kwa ajili ya michezo mbalimbali...kama mashindano ya kuogelea, mbio za madau au maboti.
Watu wa Nyasa, ili nionekane mkweli kuhusu fukwe zetu mimi naonesha mfano-Ufukwe wa LIULI.
Na John Joseph, Liuli
 

Friday, May 20, 2016

IJUMAA YA LEO TWENDE MPAKA LIULI MKOANI RUVUMA NA NGOMA YA KIODA/CHIHODA


IJUMAA NJEMA KWA WOTE NA NGOMA HII YA KIODA/CHIHODA KUTOKA KWETU LIULI....

Monday, March 3, 2014

JUMATATU YA LEO TWENDE KUWATEMBELEA NDUGU /JIRANI ZETU HUKO MBINGA!!!

Najua Mbinga kuna milima na mabonde mengi sana. Lakini hapa nimejiuliza hawa waliojenga hizi nyumba ama kweli wana moyo kweli...hapa ni MBUJI ROCH  ILIYOPO LIULI MBINGA...Basi ufikapo Mbinga usikose kutembelea ..

Thursday, June 6, 2013

LEO TUBURUDIKE NA KIODA KUTOKA KWETU LIULI KARIBUNI!!!


Liuli ni moja ya vijiji ambacho kipo kando ya ziwa Nyasa ni maarufu kwa hospitali na jiwe hili hapa chini ...pia kahitoria kidogo juu ya hili jiwe na mji wa Liuli..

Jiwe la Pomonda

Miongoni mwa miji muhimu katika wilaya ya Nyasa ni mji wa Liuli. Mji huu unayo bandari muhimu ambayo hutumiwa na meli zinazofanya safari katika ziwa Nyasa kwa upande wa Tanzania. meli za Mv Iringa na Mv Songea zimekuwa zikitia nanga katika bandari hiyo ikiwa ni sehemu ya kukuza uchumi, usafirishaji bidhaa na kadhalika.
Katika rekodi za kihistoria kuna mengi ya kukumbukwa katika mji wa Liuli, lakini jambo muhimu ni kuwepo kwa Jiwe hilo ambalo linalinganishwa na sura ya binadamu. Ukkchunguza jiwe hilo utaona linafanana kidogo au kuwa na maumbile fulani yenye sura ya binadamu.
Ni historia nzuri na tamu kwa wakazi wa nyasa na vitongoji vyake. Jiwe hilo lipo karibu kabisa na Bandari ya Liuli ambapo kila abiria au msafiri yeyote anapotumia bandari hiyo ataweza kuliona. Ni moja ya vivutio vya Utalii katika mji wa Liuli. KARIBUNI WATALII, KARIBUNI LIULI kujionea mengineyo.

Friday, May 15, 2009