Showing posts with label nchi. Show all posts
Showing posts with label nchi. Show all posts
Tuesday, May 5, 2015
ENZI HIZO WATU WOTE WALIKUWA SAWA....
Ni kweli, zamani kulikuwa na Kanisa moja, hospital moja, chama kimoja, shule moja kila kijiji, watu walikuwa wakitembeleana na walikuwa wajamaa...pia hata chakula tulikuwa tunakula sahani moja ...
Tuesday, April 15, 2014
KWA NINI URAIA WA NCHI MBILI?
Mara nyingi sana nimekuwa nikujiuliza hili swali na pia nimekuwa nikisikia ya kwamba itatokea na kwamba swala hili lipo jikoni yaani BUNGENI lakini hakuna kinachotokea. Sijui kama kuna Mtanzania ambaye anapenda kuwa raia wa nchi nyingine kuliko nchi aliyozaliwa. Naamini kabisa kama Mtanzania ya kwamba HAKUNA MTANZANIA ASIYE IPENDA TANZANIA NCHI YETU. KATIKA TEMBEA TEMBEA NIMEKUTANA NA HII EBU UNGANA NAMI KUMSOMA KAKA Peter H.A. Owino KARIBUNI PIA NAKUMBUKA NILIWAHI KUANDIKA/KUDODOSA BONYEZA http://ruhuwiko.blogspot.se/2009/10/uraia-wa-nchi-mbili.htmlKUJIKUMBUSHA
Tanzania na Diaspora.
Wakati watanzania tunaendelea kushuhudia kikao cha marekebishia ya Katiba kikiendelea napenda kujumuika na baadhi ya waliopata nafasi kuchangia kuhusu swala la uwezekano wa uraia wa nchi mbili (Due citizenship).
Katika ya nchi yetu tuipendayo kwa sasa haitambui uraia wa nchi mbili, kwa maana kuwa ukichukua uraia wa nchi nyingine unapoteza haki ya kama raia wa Tanzania, Swala hili linapaswa kuangaliwa kwa makini wakati huu wa marekebisho ya katiba, Kwa maoni yangu iwe ruksa kwa Mtanzania kuwa na uraia wa Tanzania hata kama utakuwa umechukua uraia wan chi nyingine, swala hili lisipoangaliwa makani ama likiangaliwa haraka haraka linaweza tafsiriwa kuwa watanzania hao wanatamaa ya kutaka huku na kule, si sahii kulitafsiri namna lightly namna hiyo, wengi wa watanzania waliokwenda kuishi kasha kuombauraia kuishi nchi nyingine hawakuwa na maana wa kuukana Utanzania na ukiangalia mpaka sasa hakuna anayetamba ama kuupondda U-Tanzania popote alipo.
Wengi wa watanzania wanaoishi ughaibuni ama nchi yoyote nje ya Tanzania na kupata uraia wa nchi hiyo bado wanajitambulisha kama watanzania, uraia wanaopewa ni haki ambayo wengi wao wameifanyia kazi muda mrefu sana katika nchi waliyopo, na ili kupata baadhi ya haki muhimu inabidi watambulike kama raia, kwa maana hiyo inabidi kuomba uraia wan chi waliyopo, lakini hii haimaanishi hata kidogo kuwa sasa Tanzania basi. Hata watanzania waliokuwa wakubwa kisiasa waliishi nje lakini inafika wakati wanarudi nyumbani kama kina Abrahaman Babu na Mzee Kambona nyumbani ni nyumbani huna ujanja.
Watanzania hao amabao baada ya kupata uraia wa nchi wanayoishi sasa wanatakiwa kuomba visa kuingia Tanzania, yani Mswahili wa Tarime au Ndanda sasa wanakuja Tanzania kama mgeni!, wanalipishwa kiingilio kwa dola katika mipaka yote ya Tanzania. Kuwapa haki katika nchi yao mama (Tanzania) ni swala muhimu katika kuendeleza Tanzania pia, maana yangu ni kuwa wengi wanafanya kazi nje ya nchi lakini mawazo yao ni Tanzania wengi ama wote wanandugu ambao bado wanawasiliana nao kila mara, katika kuwasiliana huko wengi wanawekeza Tanzania sababu ndio kwao na ndipo siku wakikata kauli wengi watarudishwa na kulazwa walipolala ndugu zao wengine.
Raia wengi tunajua ugumu wa Maisha yaliyopo Tanzania tuna wahitimu wengi ambao wanamaliza na kufaulu vizuri bila kupata ajira, wapo wenye bahati ambao humaliza na kuanza kazi moja kwa moja lakini wengi hawana bahati hiyo. Mtanzania ambaye amekwenda kujiendeleza nje analiona hili swala na anajua labda hayupo kwenye kundi la wenye bahati kwa maana kuwa atarudi nyumbani na hakuna ajira na wanaopata ajira wengi kama walimu wanaanzia mshahara wa shilingi 277,00=, kiasi ambacho ambacho ukijiuliza mwalimu huyu ambaye amepanga na kutumia public transport anafikaje mwisho wa mwezi hupati jibu, ukipata bahati unaweza anzia taasisi zinazolipa 750,000= kwa mwezi, lakini ni watanzania wangapi wanabahati hiyo?.
Nchi kama Uholanzi mshahara wa mwezi unaanzia Euro 1440 sawa Tsh 3,240,000 Norway wanaanzia euro 2000 na Uingereza ni zaidi ya hapo, kwa haraka haraka watu hawa wanaweza kuishi kwa amani huko walipo nabado wakasaidia ndugu zao ambao wapo Tanzania.
Nchi kama uingereza ukiwa raia una haki kuishi kwa kutegemea Serekali kwa chakula malazi ,matibabu yaani hata kama hufanyi kazi, kwa maana hiyo Mtanzania huyu akipata kazi na anaishi nchi ambayo kwa kawaida huwezi kujinunulia kiwanja na kujenga unless uwe Millionea siku zote atakuwa na mawazo ya kuja kuijenga nyumba yake nyumbani na ya kisasa kama anayoiona huko nje, na kwa vile anaishi nje basi hii nyumba yake wataishi watanzania ambao kama walivyo wengi wetu hawana uwezo wa kujenga kwa haraka na kwa mishahara halali. Tutakaporuhusu Mtanzania anayepata uraia nje kuendelea na uraia wake wa Tanzania kama atapenda basi ataendelea kulala na kuwaza Tanzania.
Mimi nimeishi nje ya Tanzania kwa muda sasa kwahiyo naelewa umuhimu wa kuendelea kuwa raia wa Tanzania, naelewa umuhimu wa siku moja kuja zikwa pale walipozikwa ndugu zangu.
Wajumbe wa Bunge wa katiba watumie busara katika kujadili hili swala bila kusahau kuwa watanzania wanaoishi je na wamepewa uraia huko wanapenda kuendelea kuwa watanzania, wajumbe watakuwa wametenda jema kuruhusu uraia wa nchi mbili hasa kwa watanzania waliobahatika kupata uraia wa nchi nyingine katika njia ya kutafuta maisha kwa ajili yao wenyewe na ndugu zao.
Sababu nchi nyingi wanazoishi Wazanzania nje ya Tanzania system yao ya kufanya kazi ni 100% kazi hivyo watanzania wengi wanajifunza na kunakili mifumo hiyo ili siku wakirudi nyumbani wawaambukize watanzania wenzao maana nchi nyingi za nje unaposema kazi unamaaninisha kazi na si kazi ya kuingia saa unayotaka na kusign na kuondoka, unakula kwa jasho lako kihalali na ukijituma unapata, Japo ni kidogo lakini watanzania walio nje wanaweza na wamekuwa wakichangia kihalali kidogo walicho nacho katika kuendeleza uchumi wa Tanzania wengi wakati wa mapumziko huja Tanzania na wengi wao hawaji mikono mitupo ama hawaji kutengemea ndugu za walioko Tanzania badala yake huja wamekamilika na vitu ambayo wengi huvituma bandarini na kulipia ushuru, siku wakiwa wanaondoka kurudi makazini wengi wao huondoka watupu na kuanza upya katika arakati za kukusanya ili akirudi tena Tanzania aendelee pale alipoachia mara ya mwisho.
Mtanzania anayeishi nje hana sehemu ya kuishi kwa furaha zaidi ya Tanzania, hana sehemu anayoishi kwa amani zaidi ya Tazania, Mtanzani huyu hana sehemu aliyo na marafiki wengi zaidi ya Tanzania, Mtanzania huyo ambaye wazazi na ndugu zake wote wako Tanzania leo anaadhibiwa kwa kitendo cha kwenda kutafuta kipato ambacho hakipereki popote bali Tanzania.
Miaka ya sabini ilikuwa inaeleweka pale alipoadhibiwa mtanzania aliyekwenda kusoma Urusi, Denmak, Hungary na akakataa kurudi, sababu tuliitaji wataalam wetu ambao hatukuwa nao wa kutosha na wengi wao waliperekwa na gharama za serekali, Zanzibar tulikuwa na chuo kimoja tu tena cha ualimu pekee na sasa kuna vyuo zaidi ya vitatu vikubwa,bara kulikuwa na
chuo kikuu kimoja tukilicho kuwa kinahitimisha wanafunzi 15 tu na sasa tunavyuo zaidi ya 30 wanaohitimu ni zaidi ya 110,000 kwa mwaka, kwa miaka hii wengi wako nje kwa gharama zao katika kutafuta kilicho bora kwa ajili ya watanzania wenzao na sasa akifanikiwa kupewa uraia na nchi husika ili aishi kwa amani na haki zote za kufanya kazi kusoma nk Tanzania inamwambia sasa hapa ni wewe ni mgeni ukija kumuona mama ama baba yako ama kuendeleza nyumba yako unayojenga kijijini kwenu kule Butiama basi lipa kiingilio (visa)!!.
chuo kikuu kimoja tukilicho kuwa kinahitimisha wanafunzi 15 tu na sasa tunavyuo zaidi ya 30 wanaohitimu ni zaidi ya 110,000 kwa mwaka, kwa miaka hii wengi wako nje kwa gharama zao katika kutafuta kilicho bora kwa ajili ya watanzania wenzao na sasa akifanikiwa kupewa uraia na nchi husika ili aishi kwa amani na haki zote za kufanya kazi kusoma nk Tanzania inamwambia sasa hapa ni wewe ni mgeni ukija kumuona mama ama baba yako ama kuendeleza nyumba yako unayojenga kijijini kwenu kule Butiama basi lipa kiingilio (visa)!!.
Watanzania walioko nje hawako nje sababu hawaipendi Tanzania na anafikiria hiyo atakuwa anajidanganya, Tanzania iko miyoni mwetu na hata serikali ingeweza hata ingeruhusu tukatengeneza system ya kupiga kura wakati chaguzi kuu zinapowadia. Wawakilishi wa vyama vya siasa katika bunge hili lililopewa heshima ya kurekebisha katiba tunawaomba kuingiza swala hili katka katiba mpya, Mheshimiwa Membe amekuwa akisikiliza na kwa makini kilio hiki cha watanzania walioko nje, pia mheshimiwa Kikwete amekuwa akikumbana na hili ombi kila wakati akikutana na watanzania waishio nje, katika kikao chake cha mwisho na watanzania Uingereza pale Wembley Mheshimiwa Raisi alisema swala hili limeingizwa kwenye rasimu kwahiyo liko ndani ya bunge kujadiliwa, napenda kumpongeza Mh Dr Kikwete kwa kutambua kilio hicho mpaka kumteua Singo kuwakilisha diaspora (thank you Mr President) katika kikao hicho.
Lakini sababu kwa walio wengi swala hili si muhimu kwao huko bungeni tunaomba mfungue macho na kulipa umuhimu. mnapojadili mjue mnamuongelea Masatu, Juma, Asha, Owino, Yasunta na wengi ambao huko waliko japo wamepewa uraia lakini wanahesabiwa kama wageni hawatakubalika kama wenyeji unless wameishi zaidi ya miaka 30, mjue mnamjadili mtu ambaye anakuja Tanzania sio kuchuma ama kujifunza Kiswahili na mila za Tanzania la hasha mnajadili maisha ya mtu amabaye amewaachia watanzania wenzake nafasi za ajira Dar , Mwanza ama Ndada na kwenda kutafuta huko nje ya nchi na anachopata japo kidogo lakini anakula na wakwao –WA-TANZANIA.
Mungu bariki Tanzania yetu.
Peter H.A. Owino
Rorya
Tanzania.
Live in UK
Peter H.A. Owino
Rorya
Tanzania.
Live in UK
Nami nasema tena na tena MUNGU IBARIKI SANA TANZANIA YETU. PAMOJA DAIMA!!!
Wednesday, March 20, 2013
TANZANIA NCHI YANGU ...NAKUPENDA TANZANIA
Nitakutangaza nchi yangu tanzania,nakupenda Tanzania nchi yangu Tanzani na najivuna kuwa mTanzania.JUMATANO NJEMA KWA WOTE...
Wednesday, February 20, 2013
TANZANIA YETU NA ...KARIBU TANZANIA!!!!
Tanzania, mito, bahari, milima, mabonde, watu, ngoma mila,utamaduni ndio asili yake..TUPO PAMOJA
Saturday, December 1, 2012
Neno La Leo: Fikiri Kuwa, Sayari Tunayoishi ( Dunia) Ni Jehenamu Ya Sayari Nyingine...!
Ndugu zangu,
Kwamba kuna viumbe kwenye sayari nyingine wenye kukesha wakiomba kwenye nyumba zao za ibada, kuwa Mungu wao awaepushe na balaa la kuwaleta kwenye sayari dunia. Dunia iliyo zaidi ya tambala bovu. Dunia iliyojaa wanadamu wenye roho za wivu, kinyongo, inda, husda na nyinginezo. Wanadamu wenye kutakiana mabaya badala ya mema.
Na mfano ni huyu aliyeomba sana kwa Mungu ashushiwe rehma. Siku moja akashukiwa na malaika. Akaambiwa, kuwa Mungu amepokea maombi yake. Kwamba anamtaka mwanadamu huyu achague jambo moja ili ashushiwe. Na akishachagua moja, basi, Mungu atampa jirani yake mara mbili ya kitu alichochagua.
Mwanadamu yule akamwambia malaika; " Basi, niache kwanza nitafakari". Baada ya kutafakari kwa muda,mwanadamu yule akatamka; " Namwomba Mungu anipe chongo!" Kwamba kwa vile alimwonea kinyongo jirani yake apate mara mbili ya atakachokipata, mwanadamu yule aliona ni heri Mungu amtoboe jicho lake moja, awe chongo, na jirani yake atobolewe mawili, awe kipofu!
Naam, fikiri kuwa sayari tunayoishi yaweza ni jehenamu ya sayari nyingine. Kumbuka, nimesema fikiri, hivyo basi fikiri kwa bidii...yaweza kukusaidia kupata jibu la kwanini nchi yetu ni masikini, na watu wake pia.
Na hilo ni Neno La Leo.
Maggid Mjengwa
Iringa.
0788 111 765
Nimetumiwa na http://mjengwablog.com.
Kwamba kuna viumbe kwenye sayari nyingine wenye kukesha wakiomba kwenye nyumba zao za ibada, kuwa Mungu wao awaepushe na balaa la kuwaleta kwenye sayari dunia. Dunia iliyo zaidi ya tambala bovu. Dunia iliyojaa wanadamu wenye roho za wivu, kinyongo, inda, husda na nyinginezo. Wanadamu wenye kutakiana mabaya badala ya mema.
Na mfano ni huyu aliyeomba sana kwa Mungu ashushiwe rehma. Siku moja akashukiwa na malaika. Akaambiwa, kuwa Mungu amepokea maombi yake. Kwamba anamtaka mwanadamu huyu achague jambo moja ili ashushiwe. Na akishachagua moja, basi, Mungu atampa jirani yake mara mbili ya kitu alichochagua.
Mwanadamu yule akamwambia malaika; " Basi, niache kwanza nitafakari". Baada ya kutafakari kwa muda,mwanadamu yule akatamka; " Namwomba Mungu anipe chongo!" Kwamba kwa vile alimwonea kinyongo jirani yake apate mara mbili ya atakachokipata, mwanadamu yule aliona ni heri Mungu amtoboe jicho lake moja, awe chongo, na jirani yake atobolewe mawili, awe kipofu!
Naam, fikiri kuwa sayari tunayoishi yaweza ni jehenamu ya sayari nyingine. Kumbuka, nimesema fikiri, hivyo basi fikiri kwa bidii...yaweza kukusaidia kupata jibu la kwanini nchi yetu ni masikini, na watu wake pia.
Na hilo ni Neno La Leo.
Maggid Mjengwa
Iringa.
0788 111 765
Nimetumiwa na http://mjengwablog.com.
Saturday, October 20, 2012
Neno La Leo: Hakuna Ugumu Wa Kurudi Misri...
Habari hii nimetumiwa na kaka Mjegwa.....
-------------------------------------------------------------------------------------
Ndugu zangu,
Yanayotokea katika nchi yetu kwa sasa yanatutaka tufikiri kwa bidii. Kama nchi kuna safari tumeifunga. Na tulivyo Waafrika, tu mahodari wa kufunga safari, lakini si mahodari wa kupanga safari. Kufunga na kupanga safari ni vitu viwili tofauti.
Ndugu zangu,
Ni vigumu leo kwa Wana wa Israel kuamua kurudi tena Misri, hata kama, pamoja na chawa na kunguni walioaacha Misri, bado, kuna wanaokumbuka samaki na masufuria ya pilau waliyoayaacha Misri. Lakini, kijamii, na kwa kuingalia jamii yetu hii ilikotoka, ilipo sasa na inakoelekea, na tuone sasa, kuwa hakuna ugumu wa kurudi tena Misri. Na hapa nitazungumzia umuhimu wa sisi WaTanzania kujitambua.
Nahofia, kuwa moja ya kiini ya haya yanayotukuta sasa ni dhambi ya Ubaguzi iliyoanza kututafuna pole pole. Taratibu tunapoteza uwezo wetu wa kujitambua. Ni ukweli sasa, kuwa Watanzania hatujitambui, na kibaya zaidi, baadhi ya viongozi wetu wa kisiasa na kidini wanapoonyesha wazi wazi kuwa hawajitambui.
Maana, tumeanza sasa kuzungumza lugha za ' Wao Wakristo' na ' Sisi Waislamu'. Tunasahau, kuwa sisi ni ndugu wa damu. Kuwa SISI ni Watanzania Kwanza. Na lililo la kwanza kwetu ni ' Nchi Yetu' na maslahi yake.
Hii ni Nchi Yetu Sote. Kila Mtanzania kwa nafasi yake ana lazima ya kupigania Usalama wa Taifa letu. Usalama wa Nchi Yetu tuliyozaliwa. Hatuwezi kuilinda na kuijenga Nchi Yetu kwenye mazingira ya kubaguana. Kwenye mazingira ya kugawanyika kwa misingi ya udini, ukabila na rangi. Na hapa nitamrejea tena Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere na dhana ya Ujenzi wa Umoja wa Kitaifa.
Ni Mwalimu Nyerere aliyeuanzisha na kuusimamia mradi mkubwa wa Ujenzi wa Umoja wa Kitaifa, hata hivyo, tunaona sasa unavyoporomoka na kuliacha taifa letu mashakani. Ndio, Mwalimu alijenga misingi imara ya Ujenzi wa Umoja Wa Kitaifa ( Nation Building).
Kuijenga jamii ya Watanzania yenye kuamini kwenye ukweli kuwa sisi sote ni ndugu. Kwamba Nchi yetu haina dini. Yenye kupiga vita ubaguzi wa aina zote, iwe wa rangi, kabila au dini. Ilimchukua Mwalimu na taifa letu miaka mingi sana kuijenga misingi hiyo iliyowawezesha pia Watanzania kuwa na mioyo ya uzalendo kwa Taifa lao.
Tunaona sasa, kazi hiyo iliyochukua miaka mingi, kutokana na ubinafsi na uroho wa madaraka ya baadhi ya wanasiasa wetu, wanapelekea kubomoka kwa misingi hiyo na kuliacha taifa letu kwenye hatari ya kuangamia.
Ndio, msingi wake ni ubaguzi wa kisiasa unaotokana na ubinafsi na tamaa ya mali kwa baadhi ya tuliowapa dhamana za kufanya maamuzi makubwa kwa niaba yetu. Ni hali ya baadhi ya tuliowapa dhamana za uongozi kuishiwa chembe chembe za uzalendo; mapenzi kwa nchi yao.Ni watu wenye kulinda maslahi yao na ya wanaowazunguka. Wako tayari hata kutumia mbinu za Umafia kutimiza malengo yao. Kuna Watanzania wengi sasa wanaopoteza mioyo ya uzalendo kwa nchi yao.
Kuna hata wenye kufikia kutamka; 'Nchi hii ina wenyewe'. Kuna anayetamka hilo kwa lengo la kumtishia mwenzake au kulazimisha kitu fulani kifanyike. Lakini, kuna wenye kutamka hivyo kuashiria kukata tamaa. Kuwa hata wafanye nini, hakuna anayewasikiliza ama kuwajali. Hizi si dalili njema kwa taifa. Kuna wanaoiba mali ya umma mchana wa jua kali. Hakuna anayewagusa.
Ukiuliza utajibiwa; “Ah! Nchi ina wenyewe!”. Kwamba kuna baadhi yetu hawajisikii kuguswa na nchi hii, hawajisikii kuwa na nguvu ya kupiga vita maovu yanayotusumbua. Baadhi yetu wameanza kupungukiwa na mapenzi na nchi yao.
Juni 16, 2004 nilipata kuandika hili kwenye gazeti la Majira; kuwa Tanzania ina vyote, kasoro Watanzania. Niliandika; kuwa Tanzania ni nchi nzuri sana. Ni nchi ya kujivunia. Kwamba Tanzania ni nchi kubwa sana kwa eneo. Ni nchi yenye rasilimali nyingi; ardhi yenye rutuba, mito, maziwa, milima, mabonde, bahari na vivutio vingi vya asili.
Hata hivyo, Tanzania ni moja ya nchi masikini sana duniani. Kwa nini? Ndio, kikubwa kinachokosekana Tanzania ni Watanzania. Tanzania tunayoijenga sasa ni mkusanyiko tu wa watu wa makundi mbali mbali wenye kwenda kwa staili ya 'kila mtu na lwake'. Idadi ya Watanzania wenye uzalendo na mapenzi kwa nchi yao inazidi kupungua. Ubinafsi umekithiri, na ubinafsi mbaya zaidi ni ule wenye kufanywa na viongozi.
Ndugu zangu, Hakuna ugumu wa kurudi Misri. Tuna lazima ya kupanga safari ya kurudi tena Misri. Inawezekana.
Na hilo ni Neno la Leo.
Maggid Mjengwa,
Iringa,
0788 111 765, 0754 678 252
http://mjengwablog.com
-------------------------------------------------------------------------------------
Ndugu zangu,
Yanayotokea katika nchi yetu kwa sasa yanatutaka tufikiri kwa bidii. Kama nchi kuna safari tumeifunga. Na tulivyo Waafrika, tu mahodari wa kufunga safari, lakini si mahodari wa kupanga safari. Kufunga na kupanga safari ni vitu viwili tofauti.
Ndugu zangu,
Ni vigumu leo kwa Wana wa Israel kuamua kurudi tena Misri, hata kama, pamoja na chawa na kunguni walioaacha Misri, bado, kuna wanaokumbuka samaki na masufuria ya pilau waliyoayaacha Misri. Lakini, kijamii, na kwa kuingalia jamii yetu hii ilikotoka, ilipo sasa na inakoelekea, na tuone sasa, kuwa hakuna ugumu wa kurudi tena Misri. Na hapa nitazungumzia umuhimu wa sisi WaTanzania kujitambua.
Nahofia, kuwa moja ya kiini ya haya yanayotukuta sasa ni dhambi ya Ubaguzi iliyoanza kututafuna pole pole. Taratibu tunapoteza uwezo wetu wa kujitambua. Ni ukweli sasa, kuwa Watanzania hatujitambui, na kibaya zaidi, baadhi ya viongozi wetu wa kisiasa na kidini wanapoonyesha wazi wazi kuwa hawajitambui.
Maana, tumeanza sasa kuzungumza lugha za ' Wao Wakristo' na ' Sisi Waislamu'. Tunasahau, kuwa sisi ni ndugu wa damu. Kuwa SISI ni Watanzania Kwanza. Na lililo la kwanza kwetu ni ' Nchi Yetu' na maslahi yake.
Hii ni Nchi Yetu Sote. Kila Mtanzania kwa nafasi yake ana lazima ya kupigania Usalama wa Taifa letu. Usalama wa Nchi Yetu tuliyozaliwa. Hatuwezi kuilinda na kuijenga Nchi Yetu kwenye mazingira ya kubaguana. Kwenye mazingira ya kugawanyika kwa misingi ya udini, ukabila na rangi. Na hapa nitamrejea tena Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere na dhana ya Ujenzi wa Umoja wa Kitaifa.
Ni Mwalimu Nyerere aliyeuanzisha na kuusimamia mradi mkubwa wa Ujenzi wa Umoja wa Kitaifa, hata hivyo, tunaona sasa unavyoporomoka na kuliacha taifa letu mashakani. Ndio, Mwalimu alijenga misingi imara ya Ujenzi wa Umoja Wa Kitaifa ( Nation Building).
Kuijenga jamii ya Watanzania yenye kuamini kwenye ukweli kuwa sisi sote ni ndugu. Kwamba Nchi yetu haina dini. Yenye kupiga vita ubaguzi wa aina zote, iwe wa rangi, kabila au dini. Ilimchukua Mwalimu na taifa letu miaka mingi sana kuijenga misingi hiyo iliyowawezesha pia Watanzania kuwa na mioyo ya uzalendo kwa Taifa lao.
Tunaona sasa, kazi hiyo iliyochukua miaka mingi, kutokana na ubinafsi na uroho wa madaraka ya baadhi ya wanasiasa wetu, wanapelekea kubomoka kwa misingi hiyo na kuliacha taifa letu kwenye hatari ya kuangamia.
Ndio, msingi wake ni ubaguzi wa kisiasa unaotokana na ubinafsi na tamaa ya mali kwa baadhi ya tuliowapa dhamana za kufanya maamuzi makubwa kwa niaba yetu. Ni hali ya baadhi ya tuliowapa dhamana za uongozi kuishiwa chembe chembe za uzalendo; mapenzi kwa nchi yao.Ni watu wenye kulinda maslahi yao na ya wanaowazunguka. Wako tayari hata kutumia mbinu za Umafia kutimiza malengo yao. Kuna Watanzania wengi sasa wanaopoteza mioyo ya uzalendo kwa nchi yao.
Kuna hata wenye kufikia kutamka; 'Nchi hii ina wenyewe'. Kuna anayetamka hilo kwa lengo la kumtishia mwenzake au kulazimisha kitu fulani kifanyike. Lakini, kuna wenye kutamka hivyo kuashiria kukata tamaa. Kuwa hata wafanye nini, hakuna anayewasikiliza ama kuwajali. Hizi si dalili njema kwa taifa. Kuna wanaoiba mali ya umma mchana wa jua kali. Hakuna anayewagusa.
Ukiuliza utajibiwa; “Ah! Nchi ina wenyewe!”. Kwamba kuna baadhi yetu hawajisikii kuguswa na nchi hii, hawajisikii kuwa na nguvu ya kupiga vita maovu yanayotusumbua. Baadhi yetu wameanza kupungukiwa na mapenzi na nchi yao.
Juni 16, 2004 nilipata kuandika hili kwenye gazeti la Majira; kuwa Tanzania ina vyote, kasoro Watanzania. Niliandika; kuwa Tanzania ni nchi nzuri sana. Ni nchi ya kujivunia. Kwamba Tanzania ni nchi kubwa sana kwa eneo. Ni nchi yenye rasilimali nyingi; ardhi yenye rutuba, mito, maziwa, milima, mabonde, bahari na vivutio vingi vya asili.
Hata hivyo, Tanzania ni moja ya nchi masikini sana duniani. Kwa nini? Ndio, kikubwa kinachokosekana Tanzania ni Watanzania. Tanzania tunayoijenga sasa ni mkusanyiko tu wa watu wa makundi mbali mbali wenye kwenda kwa staili ya 'kila mtu na lwake'. Idadi ya Watanzania wenye uzalendo na mapenzi kwa nchi yao inazidi kupungua. Ubinafsi umekithiri, na ubinafsi mbaya zaidi ni ule wenye kufanywa na viongozi.
Ndugu zangu, Hakuna ugumu wa kurudi Misri. Tuna lazima ya kupanga safari ya kurudi tena Misri. Inawezekana.
Na hilo ni Neno la Leo.
Maggid Mjengwa,
Iringa,
0788 111 765, 0754 678 252
http://mjengwablog.com
Tuesday, July 10, 2012
UNAKUMBUKA? WIMBO WA TANZANIA!!!
1, Tanzania Tanzania,
Nakupenda kwa moyo wote,
Nchi yangu Tanzania,
Jina lako ni tamu sana,
Nilalapo nakuota wewe,
Niamkapo ni heri mama wee,
Tanzania Tanzania
Nakupenda kwa moyo wote.
2. Tanzania Tanzania,
Ninapokwenda safarini,
Kutazama maajabu,
Biashara nayo makazi,
Sitaweza kusahau mimi,
Mambo mema ya kwetu kabisa,
Tanzania Tanzania
Nakupenda kwa moyo wote.
3. Tanzania Tanzania,
Watu wako ni wema sana,
Nchi nyingi zakuota,
Nuru yako hakuna tena,
Na wageni wakukimbilia,
Ngome yako imara kweli wee,
Tanzania Tanzania
Heri yako kwa mataifa.
4. Nchi nzuri Tanzania,
Karibu wasio kwao,
Wenye shida na taabu,
Kukimbizwa na walowezi,
Tanzania yawakaribisha,
Mpigane kuime chema wee,
Yanzania Tanzania
Mola awe nawe daima.
Monday, April 23, 2012
TUANZE JUMATATU YETU KIHIVI:- JE UNAJUA HAPA NI WAPI?
Wengi wanaotokea kusini kwetu wanajua hapa ni wapi ila hata wale wasiotoka huko nadhani mtajua hapa ni wapi...haya tuona kama tunakumbuka Geografia ya nchi:-)....Jumatatu njema
Wednesday, January 25, 2012
Madaktari watangaza mgomo nchi nzima
MADAKTARI wametangaza rasmi kuanza mgomo katika hospitali zote za rufaa na vituo mbalimbali vya afya nchini kote hadi hapo madai yao yatakaposhughulikiwa na Serikali.
Pia wamepitisha azimio la kumtaka Rais Jakaya Kikwete kuifumua na kuiunda upya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kwa kuwaondoa kwenye nyadhifa zao Waziri Dk Haji Mponda na Naibu wake, Dk Lucy Nkya kutokana na kile wanachodai kuwa ni kudhalilisha taaluma yao.Dk Uliomboka pia aliwataja Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Blandina Nyoni na Mganga Mkuu wa Serikali, Dk Deo Mtasiwa kwamba wanapaswa kuwajibishwa na Rais.
Akitangaza mgomo huo, Dar es Salaam jana Mwenyekiti wa Kamati ya Muda ya Jumuiya ya Madaktari hao, Dk Stephene Ulimboka alisema hatua hiyo inalenga kupata ufumbuzi wa madai waliyotoa kwa muda mrefu na kuongeza kwamba, leo wanatarajia kukutana na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.
Dk Ulimboka alitaja baadhi ya madai yao kuwa ni kuwawekea mazingira bora ya kazi madaktari kwa kupeleka vifaa vya kazi hospitalini na kwenye vituo vya afya, kuboresha malipo ya posho na kuwapatia sitahili zote wanataalamu hao.
Hata hivyo, tafauti na ilivyokuwa awali, kikao cha jana ambacho kilikuwa cha majumuisho, kilitumika pia kupokea ripoti ya mikutano iliyokuwa ikiongozwa na Chama cha Madaktari Tanzania (MAT) na kupokea majukumu ya kuongoza harakati hizo.
“Kuanzia leo tunatangaza kuwa madaktari wote wanaoguswa na hili kote nchini kuacha kufanya kazi hadi hapo Serikali itakapotekeleza madai yetu, tunataka Serikali iboreshe mazingira ya kutolea huduma za afya, ili kumwezesha daktari kumpatia huduma mgonjwa katika kiwango kinachostahili,” alisema Dk Ulimboka.
Alitaja madai mengine matatu ambayo kamati anayoiongoza inasimamia kuhakikisha yanatekelezwa kuwa ni pamoja na madaktari kurejeshewa nyumba za kuishi kama inavyoelekezwa kwenye ‘Standard order’ ya Serikali, ambayo inasema daktari atapatiwa nyumba ya kuishi na Serikali na kama sivyo atapatiwa asimilia 30 ya mshahara.
Alisema kipengele hicho kiliondolewa kinyemela bila wao kushirikisha wala kuelezwa sababu za kuondolewa kwake, jambo linalowaongezea ugumu wa maisha na kuwafanya wadharaulike.
Madai mengine yalihusu nyongeza za mishahara, ambayo alisema kumekuwa na ugumu wa kutekeleza suala hilo kila mara hadi wanapofanya mgomo.
“Mwaka 2005 wakati tunaanza kazi, mshahara wa daktari ulikuwa unafikia Sh124, 000, lakini baada ya mgomo ndipo ukapandishwa hadi kufikia karibu ya laki 700,000 sisi tunataka suala hili lirekebishwe na nyongeza yake isisubiri shinikizo,” alisema.
Madai mengine ni malipo kwa madaktari pindi wanapofanya kazi katika mazingira hatarishi na kupendekeza walipwe asimilia 30 ya mshahara wao, posho wakati wa kazi ya ziada ambayo kwa sasa wanalipwa asimilia 10 ya mshahara wao.
Kuhusu mshahara, alisema yapo mapendekezo ambayo alisema wataitaarifu Serikali watakapokutana na viongozi wake.
Madaktari hao leo wanatarajia kuendelea na mkutano wao katika ukumbi wa Don Bosco.Rais wa MAT, Dk Namala Mkopi alisema alikabidhi majukumu kwa kamati iliyoundwa na wanachama baada ya kuonekana kuwa hadi sasa Serikali imekuwa ikiwazungusha.
“Wanachama wamesema hapo mlipofikia tunashukuru mmejitahidi vya kutosha na sasa tunaomba mtukabidhi majukumu ili shughuli hii iweze kusimamiwa na kamati ya madaktari,” alisema Dk Mkopi.
Hatua hiyo imelenga kuongeza wigo wa washiriki ambao watawahusisha madaktari wasio wanachama wa MAT na wafanyakazi wengine katika sekta hiyo ya afya.
Chanzo: Gazeti la Mwananchi.....kupitia http://simulizi.blogspot.com/.
Pia wamepitisha azimio la kumtaka Rais Jakaya Kikwete kuifumua na kuiunda upya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kwa kuwaondoa kwenye nyadhifa zao Waziri Dk Haji Mponda na Naibu wake, Dk Lucy Nkya kutokana na kile wanachodai kuwa ni kudhalilisha taaluma yao.Dk Uliomboka pia aliwataja Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Blandina Nyoni na Mganga Mkuu wa Serikali, Dk Deo Mtasiwa kwamba wanapaswa kuwajibishwa na Rais.
Akitangaza mgomo huo, Dar es Salaam jana Mwenyekiti wa Kamati ya Muda ya Jumuiya ya Madaktari hao, Dk Stephene Ulimboka alisema hatua hiyo inalenga kupata ufumbuzi wa madai waliyotoa kwa muda mrefu na kuongeza kwamba, leo wanatarajia kukutana na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.
Dk Ulimboka alitaja baadhi ya madai yao kuwa ni kuwawekea mazingira bora ya kazi madaktari kwa kupeleka vifaa vya kazi hospitalini na kwenye vituo vya afya, kuboresha malipo ya posho na kuwapatia sitahili zote wanataalamu hao.
Hata hivyo, tafauti na ilivyokuwa awali, kikao cha jana ambacho kilikuwa cha majumuisho, kilitumika pia kupokea ripoti ya mikutano iliyokuwa ikiongozwa na Chama cha Madaktari Tanzania (MAT) na kupokea majukumu ya kuongoza harakati hizo.
“Kuanzia leo tunatangaza kuwa madaktari wote wanaoguswa na hili kote nchini kuacha kufanya kazi hadi hapo Serikali itakapotekeleza madai yetu, tunataka Serikali iboreshe mazingira ya kutolea huduma za afya, ili kumwezesha daktari kumpatia huduma mgonjwa katika kiwango kinachostahili,” alisema Dk Ulimboka.
Alitaja madai mengine matatu ambayo kamati anayoiongoza inasimamia kuhakikisha yanatekelezwa kuwa ni pamoja na madaktari kurejeshewa nyumba za kuishi kama inavyoelekezwa kwenye ‘Standard order’ ya Serikali, ambayo inasema daktari atapatiwa nyumba ya kuishi na Serikali na kama sivyo atapatiwa asimilia 30 ya mshahara.
Alisema kipengele hicho kiliondolewa kinyemela bila wao kushirikisha wala kuelezwa sababu za kuondolewa kwake, jambo linalowaongezea ugumu wa maisha na kuwafanya wadharaulike.
Madai mengine yalihusu nyongeza za mishahara, ambayo alisema kumekuwa na ugumu wa kutekeleza suala hilo kila mara hadi wanapofanya mgomo.
“Mwaka 2005 wakati tunaanza kazi, mshahara wa daktari ulikuwa unafikia Sh124, 000, lakini baada ya mgomo ndipo ukapandishwa hadi kufikia karibu ya laki 700,000 sisi tunataka suala hili lirekebishwe na nyongeza yake isisubiri shinikizo,” alisema.
Madai mengine ni malipo kwa madaktari pindi wanapofanya kazi katika mazingira hatarishi na kupendekeza walipwe asimilia 30 ya mshahara wao, posho wakati wa kazi ya ziada ambayo kwa sasa wanalipwa asimilia 10 ya mshahara wao.
Kuhusu mshahara, alisema yapo mapendekezo ambayo alisema wataitaarifu Serikali watakapokutana na viongozi wake.
Madaktari hao leo wanatarajia kuendelea na mkutano wao katika ukumbi wa Don Bosco.Rais wa MAT, Dk Namala Mkopi alisema alikabidhi majukumu kwa kamati iliyoundwa na wanachama baada ya kuonekana kuwa hadi sasa Serikali imekuwa ikiwazungusha.
“Wanachama wamesema hapo mlipofikia tunashukuru mmejitahidi vya kutosha na sasa tunaomba mtukabidhi majukumu ili shughuli hii iweze kusimamiwa na kamati ya madaktari,” alisema Dk Mkopi.
Hatua hiyo imelenga kuongeza wigo wa washiriki ambao watawahusisha madaktari wasio wanachama wa MAT na wafanyakazi wengine katika sekta hiyo ya afya.
Chanzo: Gazeti la Mwananchi.....kupitia http://simulizi.blogspot.com/.
Monday, August 29, 2011
BREAKING NEWS:MNADHIMU MKUU WA JWTZ (SHIMBO) CHINI YA ULINZI WA POLISI WA INTERPOL

Shimbo na wizi wa Trilioni 3: Apata mshtuko na kuzirai!
Hali ilivyokuwa:
JK alienda AFRICA YA KUSINI majuzi na alikuwa anajaribu kuomba msaadakuisaidia TZ, wakamwambia hatutaweza kukusaidia maana una watu wanahela ambazo ni zaidi ya ambazo tungekusaidia. Ndipo wakamfahamisha juuya Mnadhimu wetu kuwa na account huko yenye zaidi ya TZS zaidi yatrilioni 3. Habari hii ilimshtua JK naye akataka ufanyike uchunguziambao uliibuka na usahihi wa taarifa toka SA kwani ilikutwa kwelijamaa ana hela hizo.
Inasemekana Interpol wamempatia Afande Shimbo ukweli wa Account zakenje ya nchi zenye pesa nyingi sana na amechukuliwa chini ya Ulinzi waInterpol kwenda Africa ya kusini kwa matibabu.
Amekuwa akiwakata posho wanajeshi wanaoenda kujitolea kusaidia mataifaya nje na wa ndani.
Hela nyingi zaidi ni pale alipokata fungu kubwa sana toka fedha zashukrani toka Comoro baada ya Tanzania kuisaidia nchi hiyo. Fedha hizozilitakiwa kugawiwa kwa wanajeshi kwa kuisaidia nchi hiyo lakini mkuuhuyu alizipiga panga na hawakujua kuwa alikuwa kafungua akaunti nje yanchi na kuzihamishia kule.
Ameshindwa kueleza kwa undani alizipataje pesa hizi kwenye akaunti naaliishiwa nguvu na kudondoka!
Si Shimbo pekee...
Kuna kijana mdogo sana anaitwa PTE Gwilla, huyu yupo Kurugenzi ya DPAana-deal na salaries za wanajeshi... Kinachoshtua ni askari mdogo sanalakini alikuwa ana maghorofa mawili makubwa, magari aina ya Coastermawili na benki alikutwa na zaidi ya 73mil TZS (kwa mshahara wakeasingeweza kuwa na vitu hivi)
Uchunguzi umeonyesha Gwilla alikuwa anacheza na mishahara ya wanajeshikwa muda mrefu (4yrs) kwa aidha mishahara hewa, kukata 500 kwa kilamwanajeshi (4yrs) na zaidi akawa anakula hela za likizo za wanajeshikwa zaidi ya miaka 3 (2009-2011).
Huyu naye kakamatwa na anashikiliwa Mgulani.
Kuna mwingine...
Ni Mkurugenzi wa malipo jeshini, Brigedia (CC) Zakayo, naye kalambamabilioni ya hela (kiasi sijakinasa vema bado lakini ni zaidi ya EPA)naye anashughulikiwa kwa karibu.
So far, niseme kazi nzuri Interpol, walau watu wataanza kuelewa kuwawatakuja kugundulika wakifanya uhuni wa namna hii.
HABARI HII KWA HISANI YA JAMII FORUM
Friday, August 19, 2011
Monday, October 11, 2010
SWALI :- NANI ALIZIPA HIZI NCHI MAJINA NA LUGHA ZAKE??

Siku, miezi na hadi miaka imepita huku nikijiuliza hivi KWA NINI au NI NANI alisema/amua haya majina ya hizi nchi zetu? Pia lugha za nchi? Kwa mfano nchi Tanzania lugha kiswahili. KWA NINI?
Na ndio nikaona niliweka hili swali hapa kibarazani ili tujadili kwa pamoja. Kwani Umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu.
Na ndio nikaona niliweka hili swali hapa kibarazani ili tujadili kwa pamoja. Kwani Umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu.
Friday, March 26, 2010
Mgomo utamuathiri kila Mtanzania
Tanzania iko katika wasiwasi wa mgomo mkubwa ambao haujawahi kutokea nchini. Wafanyakzi wamekuwa na madai takriban matatu ya msingi ambayo wanataka Serikali iyashughulikie. Dai la kwanza ni Ongezeko la kima cha chini cha mshahara ambapo wameiomba serikali kupandisha kima hicho kutoka sh. 80,000 hadi 315,000 lakini Serikali iliongeza asilimia kidogo sana na ku[pandisha hadi sh. 84,000 tu. Dai lingine wanaomba kodi na makato mbali mbali yapunguzwe na ombi lingine serikali ipanue wigo wa kodi ili kumpunguzia mzigo mfanyakazi.
Kwasababu haya hayajatekelezwa kama walivyoomba sasa wafanyakazi wamedhamiria kugoma nchi nzima kuishinikiza serikali kutekeleza mahitaji yao. Jambo hili ni la hatari kwa mustakabali wa ustawi, maendeleo na usalama wa taifa letu. Hatua hii italeta adha kubwa kwa watanzania wote kuanzia wagomaji wenyewe mapaka ndugu zao. Na kibaya zaidi wananchi wengi wasio na hatia wataumia na wengine watakufa kutokana na madhara ya mgomo huo. Mama lishe wanaoishi kwa kuwauzia chakula wafanyakazi hawatafanya biashara, wanaopata riziki kwa kuosha magari hawatapata ridhiki kwa siku hizo. Wagonjwa watakufa kwa kukosa huduma. na kadhia mbali mbali zitaibuka.
Jambo lingine la hatari ni kuporomoka kwa uchumi wa Tanzania kwani siku za mgomo taifa litapoteza fedha nyingi sana. Madhara hayo yataendelea kwa muda mrefu hata bada ya mgomo huo kwisha Nilifanya mkutano na waandishi wa habari tarehe 22 machi mwaka huu, kuwasihi wafanyakazi wasigome, kuisihi Serikali iyashughulikie malalamiko hayo. Lakini hakukuwa na respond nzuri kutoka vyombo vya habari jambo ambalo limenifanya nihisi kuwa vyombo vya habari vinashabikia mgomo huo. Ni redio chache, na magazeti machache tu yaliripoti.
Kimsingi mgomo utayumbisha nchi na sekta zote. Maana mgomo wa nchi nzima, hata hivyo vyombo vya habari havitauza magazeti maana wafanyakazi ndio wanaonunua zaidi magazeti. Huwezi kukuta mama lishe, mmachinga, mfyatua tofali ananunua magazeti. Kipindi hicho kila mtu atakuwa anatunza hela yake isiishe mapema.
Makampuni mengi yataingia hasara na mwisho wa yote mgomo ukiisha kila sekta itaendelea na msukosuko wake na hatimaye upunguzaji mkubwa wa wafanyakzi utafuatia ili kuweka mambo sawa.
Kugoma ni sawa na kujilipua maana wafanyakazi watawatesa mpaka ndugu zao na watajiathiri wenyewe. Mgomo ni sawa na unamdai mtu halafu unamnyima mapato.
Malamiko haya ni ya msingi sana na serikali lazima isizibe masikio Ni wakati muafaka kwa wafanyakazi kufuta mgomo, kurudi mezani na Serikali ili kila upande ujue madhara na kuchukua hatua muafaka. Watanzania wanasifa kuu ya huruma, upendo na uvumilivu ni vema wajiangalie katika kioo hicho.
Na Jacob Malihoja
Kwasababu haya hayajatekelezwa kama walivyoomba sasa wafanyakazi wamedhamiria kugoma nchi nzima kuishinikiza serikali kutekeleza mahitaji yao. Jambo hili ni la hatari kwa mustakabali wa ustawi, maendeleo na usalama wa taifa letu. Hatua hii italeta adha kubwa kwa watanzania wote kuanzia wagomaji wenyewe mapaka ndugu zao. Na kibaya zaidi wananchi wengi wasio na hatia wataumia na wengine watakufa kutokana na madhara ya mgomo huo. Mama lishe wanaoishi kwa kuwauzia chakula wafanyakazi hawatafanya biashara, wanaopata riziki kwa kuosha magari hawatapata ridhiki kwa siku hizo. Wagonjwa watakufa kwa kukosa huduma. na kadhia mbali mbali zitaibuka.
Jambo lingine la hatari ni kuporomoka kwa uchumi wa Tanzania kwani siku za mgomo taifa litapoteza fedha nyingi sana. Madhara hayo yataendelea kwa muda mrefu hata bada ya mgomo huo kwisha Nilifanya mkutano na waandishi wa habari tarehe 22 machi mwaka huu, kuwasihi wafanyakazi wasigome, kuisihi Serikali iyashughulikie malalamiko hayo. Lakini hakukuwa na respond nzuri kutoka vyombo vya habari jambo ambalo limenifanya nihisi kuwa vyombo vya habari vinashabikia mgomo huo. Ni redio chache, na magazeti machache tu yaliripoti.
Kimsingi mgomo utayumbisha nchi na sekta zote. Maana mgomo wa nchi nzima, hata hivyo vyombo vya habari havitauza magazeti maana wafanyakazi ndio wanaonunua zaidi magazeti. Huwezi kukuta mama lishe, mmachinga, mfyatua tofali ananunua magazeti. Kipindi hicho kila mtu atakuwa anatunza hela yake isiishe mapema.
Makampuni mengi yataingia hasara na mwisho wa yote mgomo ukiisha kila sekta itaendelea na msukosuko wake na hatimaye upunguzaji mkubwa wa wafanyakzi utafuatia ili kuweka mambo sawa.
Kugoma ni sawa na kujilipua maana wafanyakazi watawatesa mpaka ndugu zao na watajiathiri wenyewe. Mgomo ni sawa na unamdai mtu halafu unamnyima mapato.
Malamiko haya ni ya msingi sana na serikali lazima isizibe masikio Ni wakati muafaka kwa wafanyakazi kufuta mgomo, kurudi mezani na Serikali ili kila upande ujue madhara na kuchukua hatua muafaka. Watanzania wanasifa kuu ya huruma, upendo na uvumilivu ni vema wajiangalie katika kioo hicho.
Na Jacob Malihoja
Saturday, October 10, 2009
URAIA WA NCHI MBILI
Kwa Pro. Mbele nimesoma kuhusu watu kuwa na uraia wa nchi mbili. Kwa hapa Sweden sheria ni kwamba ukisha ishi mika 5 unaruhusiwa kuwa raia wa nchi. Kwa mimi sioni umuhimu wa kuwa raia wa nchi nyingine kwa hiyo mimi bado ni raia wa nchi moja na nina passport ile ya kijani.
Watoto wetu ni raia wa Sweden tu. Huwa tunapata shida sana kuomba ruhusa (VIZA) kwenda TZ kwani kwa wao na baba yao wanaruhusiwa kuwa ndani ya nchi miezi mitatu tu. Lakini mimi sihitaji ruhusa.
Ila ningefurahi sana kama kungekuwa na hii sheria ya uraia wa nchi mbili hapo ndiyo ningechukua nafasi na kuwa raia wa nchi mbili. Ila sasa hapana, mimi ni mTanzania tu. Kwa undani zaidi soma blog ya Pro. Mbele URAIA WA NCHI MBILI
Watoto wetu ni raia wa Sweden tu. Huwa tunapata shida sana kuomba ruhusa (VIZA) kwenda TZ kwani kwa wao na baba yao wanaruhusiwa kuwa ndani ya nchi miezi mitatu tu. Lakini mimi sihitaji ruhusa.
Ila ningefurahi sana kama kungekuwa na hii sheria ya uraia wa nchi mbili hapo ndiyo ningechukua nafasi na kuwa raia wa nchi mbili. Ila sasa hapana, mimi ni mTanzania tu. Kwa undani zaidi soma blog ya Pro. Mbele URAIA WA NCHI MBILI
Wednesday, August 5, 2009
AFRIKA YETU + MUNGU IBARIKI AFRIKA
Monday, March 30, 2009
UPENDO KWA NCHI YANGU +MAISHA
Sijui kama wenzangu mmewahi kujisikia hivi, mwenzenu leo nimeamuaka na kujiona ya kwamba:- Ninaringa kwa kuwa Mtanzania nchi yangu yenye sifa zote za ustaarabu.
Ninaringia rangi yangu nyeusi, macho meupe, ngozi yangu nyororo, ninapendeza na nywele zangu nyeusi na kiswahili ni lugha yangu.
Ninajivunia nchi yangu ya Tanzania yenye miji ya kuvutia iliyojengeka. Angalia Dar es salaam, Mwanza nayo Dodoma bila kusahau kwenye marashi mji wetu Zanzibar. Halafu ukienda Arusha, Tanga, Kilimanjaro, Mbeya, Iringa na Songea.
Mnajua kuna vivutio vingi ndani ya Tanzania vinavyotufanya sote tujivunie kwa mfano kuna bahari fahari ya Taifa, Ziwa nyasa, viktoria, Tanganyika pia mlima mkubwa barani afrika Kilimanjaro. Bila kusahau mbuga za wanyama Serengeti, Ngorongoro, Tarangire, Mikumi n.k.
Ninaringia rangi yangu nyeusi, macho meupe, ngozi yangu nyororo, ninapendeza na nywele zangu nyeusi na kiswahili ni lugha yangu.
Ninajivunia nchi yangu ya Tanzania yenye miji ya kuvutia iliyojengeka. Angalia Dar es salaam, Mwanza nayo Dodoma bila kusahau kwenye marashi mji wetu Zanzibar. Halafu ukienda Arusha, Tanga, Kilimanjaro, Mbeya, Iringa na Songea.
Mnajua kuna vivutio vingi ndani ya Tanzania vinavyotufanya sote tujivunie kwa mfano kuna bahari fahari ya Taifa, Ziwa nyasa, viktoria, Tanganyika pia mlima mkubwa barani afrika Kilimanjaro. Bila kusahau mbuga za wanyama Serengeti, Ngorongoro, Tarangire, Mikumi n.k.
Tuesday, January 27, 2009
KISWAHILI NI LUGHA YA WATU GANI?
Nimekuwa nikijiuliza mara nyingi kiswahili ni lugha ya watu gani? Kwani sasa naona watu/nchi nyingi sana wanaongea kiswahili. Na pia nimesikia ya kwamba inasemekana ya kwamba imependekezwa kiswahili kiongewe Afrika nzima.
Swali:- Wenzangu mnafikiri itasaidia nini? Na kwa nini Afrika nzima waongee kiswahili? Wakati kiswahili ni lugha yetu ya TAIFA?.
Swali:- Wenzangu mnafikiri itasaidia nini? Na kwa nini Afrika nzima waongee kiswahili? Wakati kiswahili ni lugha yetu ya TAIFA?.
Saturday, October 18, 2008
UMOJA WA NCHI HURU ZA AFRIKA

Subscribe to:
Posts (Atom)