BIBI NA WAJUKUU WAKE
Mara nyingi nimekuwa nikijiuliza kuhusu hii tabia ambayo, bado inazidi kukua tu katika jamii zetu. Hasa inapokuja kwa sisi wadada/wanawake. Hii tabia ya kuwaacha watoto kwa wazazi, hivi hii haijalishi ya kwamba wazazi wamekwisha fanya kazi yao yaani kuku/kututunza sisi na sasa ni wewe/sisi inabidi pale inapowezekana tuwatunze wao?
Utakuta wazazi wanawatunza wajukuu na hapo hapo wanakuwa na majukumu mengine na ulemuda wa kupumzika unakuwa haupo. Halafu utakuta wanaweke wengine wameolewa, na kabla yake amezaa na yule/hao watoto anawaacha kwa wazazi je Huyo mume wake hawapendi watoto hao? Afadhali anemwacha mtoto kwa ajili ya kwenda shule.
Je? huu kweli ni uungwana...???