Showing posts with label huru. Show all posts
Showing posts with label huru. Show all posts

Saturday, October 18, 2008

JAMHURI YA SAHARA MAGHARIBI


Marocco ilijitoa kwenye Umoja wa Nchi Huru za Afrika Mwezi Novemba 1984 baada ya Umoja huo kuitambua rasmi Jamhuri ya Sahara Magharibi kama Nchi Huru.

UMOJA WA NCHI HURU ZA AFRIKA

Umoja wa Nchi huru za Afrika uliundwa tarehe 25 mei 1963 na Nchi Huru 32 huko Addis Ababa. Malengo ya Umoja huu ni kudumisha Umoja wa Udugu baina ya Wanachama wake, Ukoloni katka Afrika na kukuza ushirikiano wa Kimataifa. Baraza la Wakuu wa nchi hizi hukutana kila mwaka kuratibu masuala mbalimbali ya Kisiasa, Kiutamaduni, Afya, Sayansi na Ulinzi. Mpaka mwaka 1987 Umoja huu ulikuwa na Wanachama 50

BENDERA ZA CHAMA CHA SWAPO+CHAMA CHA ANC+CHAMA CHA PAC


Chama cha SWAPO kinachopigania Uhuru wa Namibia, Vyama vya ANC na PAC vinavyopigania haki na kupinga siasa ya ubaguzi wa rangi huko Afrika ya kusini, vinashiriki katka vikao Umoja wa Nchi Huru za Afrika (OAU) kama wasikilizaji

Friday, October 17, 2008

SERENGETI NATIONAL PARK


Kuna mtu anaweza kuniambia anaona nini katika picha hii. au niseme ni wanyama gani hao. Hapa picha hii ni mapema alfajiri nimepiga.