Sunday, April 30, 2017

NAWATAKIENI JUMAPILI HII YA MWISHO WA MWEZI HUU WA NNE.

Neno la leo; Mathayo 6.
1 Angalieni msifanye wema wenu machoni pa watu, kusudi mtazamwe na wao; kwa maana mkifanya kama hayo, hampati thawabu kwa Baba yenu aliye Mbinguni.
JUMAPILI NJEMA!

Saturday, April 29, 2017

NI JUMAMOSI YA MWISHO YA MWEZI HUU WA NNE :- TUMALIZA KIHIVI....

Nawatakieni jumamosi hii ya ya mwisho wa mwezi huu wa nne iwe njema sana pia ya furaha na amani. PANAPO MAJALIWA .....

Friday, April 28, 2017

NENDA KAMPENDE MKE WAKO

Nimetumiwa na simulizi hii na rafiki binafsi imenigusa sana nikaona niiiweka hapa kama kawaida nisemavyo sipendi kunyimana elimu. KARIBUNI!

Kijana mmoja alikua akimpenda sana Mama yake, kwakua Mama yake almlea kwa shida sana tena kwa upendo wa hali ya juu kijana yule alilipa fadhila kwa kuhakikisha kua Mama yake hakosi kitu chochote.

Baada ya kuoa yeye alihama nyumbani kwao na kwenda kuishi mbali kidogo na Mama yake, lakini katika mji uleule. Pamoja na umbali huo lakini kila siku alienda kumsalimia Mama yake na wadodgo zake.

Alikua akiwapelekea zawadi na fedha za matumizi. Mara nyingi akitoka kazini alikua akitumia muda mwingi nyumbani kwao na wakati mwingine hata chakula cha usiku alikula kule na kurudi nyumbani akiwa maeshiba.

Hali hiyo iliendelea kwa muda na hata walipobarikiwa kupata mtoto bado aliendelea kuwapenda ndugu zake na kutumia muda mwingi wa ziada akiwa nyumbani kwao kuliko nyumbani kwake.

Ingawa hakua akimdharau mkewe wala kumnyanyasa lakini alimpenda Mama yake zaidi. Siku moja jioni akiwa ametoka kazini, alifika nyumbani kwa Mama yake.

Aligonga mlango na kwa bahati nzuri Mama yake alifungua mlango. Lakini wakati akitaka kuingia akiwa na kapu la zawadi mkononi Mama yake alimzuia na kumuambia kuwa hakuna kuingia.

Kijana alishangaa akidhani kua ni utani lakini Mama alikataa katakata na kumuambia. “Mwanangu najua unanipenda sana lakini sasa ni zamu ya mkeo. Wewe ushakua mkubwa umeoa unafamilia yako, nenda kampende mkeo”.

Kijana alishangaa kwani yote aliyokua akiyafanya ni kwakua Mama yake aliteseka kwaajili yake. “Najua unayafanya yote kwa upendo ila mkeo anahitaji upendo pia. Mimi ni Mama yako, ni mtu mzima, lakini yule mkeo, bado ni binti lakini mna mtoto mdogo.

Kama unavyonipenda mimi mama yako nenda kampende Mama wa watoto wako ili aweze kuwalea watoto wenu waje kuwa na upendo kama wewe. Upendo unaonionyesha nikwakua Baba yako alinionyesha upendo wa hali ya juu.

Baba yako alinipenda sana, akanionyesha upendo, moyo wangu ukawa na amani nikawa na kazi ya kuwalea nyinyo kwa furaha. Sasa na nyinyi mna furaha unanihudumia.

Lakini wewe muda mwingi unautumia hapa, mkeo unamuacha peke yake mpweke. Mwanamke akiwa mpweke anakua na kisirani, akishakua na kisirani anakua na hasira na akiwa na hasira basi hutafuta sehemu ya kuzipeleka na anaweza kuzipeleka kwa watoto.

Akizipeleka kwa watoto watalelewa vibaya na hawatakuja kuwa watoto wazuri kama wewe. Nakupenda lakaini sikutaki tena kwangu, nenda kampende mkeo, tengeneza familia yako, hii ni ya kwangu na nishaitengeneza.

Mwanangu unanipenda sana lakini ipo siku nitakufa kama Baba yako, usihuzunike lakini ipo siku hawa wadogo zako wakiume wataoa, hawatakua na muda tena na wewe. Hawa dada zako wataolewa na kuwa na familia zao.

Watakua bize na familia zao kiasi kwamba hamtaonana, hiyo haimaanishi kuwa hawatakua wanakupenda, hapana watakupenda lakini maisha ndiyo yalivyo. Kama ambavyo mimi nilikua na Kaka zangu na Dada zangu.

Kama ambavyo Baba yako alikua na Kaka zake na Dada zake waliokua wakipendana lakini sasa kila mmoja ana familia yake. Wewe utabaki na mkeo na wanao, hao ndiyo watakua familia yako kama ambavyo Baba yako alibaki na mimi na nyinyi.

Sasa kama hukumuonyesha upendo mkeo sasa hivi unafikiri utaishi naye vipi ndugu wakikutelekeza kwasababu ya majukumu yao. Nenda kampende mkeo, mpeleke zawadi.

Kwangu utakuja mara moja moja nikikuhitaji, utakuja ukisikia naumwa na utanitumia matumizi mwisho wa mwezi. Katengeneze familia yako, nenda kanitengenezee wajukuu wazuri, wenye upendo kama ulivyo wewe Baba yao.

Mama alimaliza na kabla kijana hajasema chochote alifunga mlango na kuingia ndani. Kijana alilazimika kurudi nyumbani, alimkuta mkewe kanyongonyea.

Alimkabidhi lile kapu la zawadi na kumuambia zawadi zako hizi. Mke aliruka kwa tabasamu akimshukuru mumewe kwa zawadi ile, kwani muda ulikua umepita bile kupeleka zawadi nyumbani wala kuwahi vile.

****MWANAUME; Wapende ndugu zako lakini jua mwisho wa siku mtu pekee ambaye mtazeeka pamoja ni Mke wako. Kama huamini hembu muangalie Baba yako kule kijijini vipi bado anaishi na shangazi yako?

Lakini hembu muambie Bibi na Babu yako, si wako wawili tu, tena mmewatafutia na mfanyakazi ili awasaidie. Ndiyo huyo mwanamke unayemnyanyasa leo anathamani kuliko huyo Dada yako anayemtukana mkeo kila siku na wewe unachekelea.

Wednesday, April 26, 2017

BAADA YA KUJIFICHA MUDA WA WIKI MOJA HAPA KISIWANI LANZAROTE/USPANIA SASA NIPO NANYI TENA...

Kapulya na mbwembwe zake kama kawaida kamera ilipomnasa
 Baada ya kujinyoosha hapo juu nilinaswa nikiwa nikiangalia mazingira ya hiki kisiwa cha Lanzarote huku Uispania

 Baada ya matembezi ya muda mrefu mtu huwa na njaa na hapa ni chakula kikuu cha Kispania kinaitwa PAELLA...ni chakula kitamu:-)
Sikuishia hapo nilikwenda kwa makumbusho maalufu yaliyopo katika kisiwa hiki cha Lanzarote kuangalia mimia hii ya Cactus....ila sasa nimerudi na nipo nanyi tena kama kawaida....Kapulya wenu

Monday, April 24, 2017

TUANZE JUMATATU HII KWA KUANGALIA BAADHI YA CHANGAMOTO ZA MAISHA YA VIJIJINI

 KUSAIDIANA:- Hakuna baba wala mama..wote mzigo kuchwani, baada ya kazi za shamba kuelekea nyumbani....hii kidogo inaleta furaha.
Mama na mwanae huku mzigo wa kuni kichwani kwa ajili ya kupikia chakula nyumbani.  Hivi ndivyo baadhi ya jamii vjijini yalivyo.

Tuesday, April 18, 2017

NIMEJIFICHA HAPA TANGU JANA...LIKIZO KIDOGO

Hapa ni jana jioni ....mlo wa jioni ....
Na hapa ni leo asubuhi. Tukutane wakati mwingine...Chao.

Sunday, April 16, 2017

AMEFUFUKA MWOKOZO YESU



KHERI YA PASAKA  NDUGU ZANGU WOTE  TUNAOFURAHIA UFUFUKO WAKE MFALME WETU WA AMANI. BARAKA NA FURAHA VITAWALE NDANI YA MIOYO YETU PIA NYUMBA ZETU. PASAKA NJEMA.

Wednesday, April 12, 2017

KUTOKUWA KARIBU NA FAMILIA KUNAVYOATHIRI TABIA ZA WATOTO

MALEZI katika mazingira yetu ya Kiafrika ni suala nyeti. Hatuna historia ya kupuuza watoto tunaowazaa. Kwa kutambua umuhimu wa malezi katika kujenga jamii yenye ustawi, tumekuwa na desturi ya kuelekeza nguvu zetu nyingi katika malezi ya watoto wetu. Kwa mfano, tangu mtoto anapozaliwa, ilikuwa ni lazima alale kitanda kimoja na wazazi wake kwa muda unaozidi miaka miwili. Mtoto mchanga hakuachwa alale kwenye kitanda chake mapema.
Aidha, alikulia mikononi mwa watu wazima aliowafahamu vyema kwa sababu ama aliishi nao kwenye boma la wazazi wake au walitoka miongoni mwa jamii inayomzunguka. Muda mwingi alibebwa mgongoni kwa mama yake au dada zake kuthibitisha kuwa ukuaji wa mtoto ulifuatiliwa kwa karibu mno na wazazi wake.
Jambo hili halieleweki kwa wageni wa bara hili wanaodhani ni aina ya udhalilishaji wa mtoto. Kitendo cha kumbeba mtoto mgongoni  kimethibitika kisayansi kusaidia kujenga muunganiko wa kihisia kati ya mzazi na mtoto.
Wakati wa jioni, familia zilikuwa na desturi ya watoto kukaa na wazazi wao kijinsia. Baba aliota moto na watoto wa kiume akiwasimulia mambo mbalimbali ya kimaisha. Kadhalika, mama naye alifanya kazi za jikoni kwa ushirikiano wa karibu na watoto wa kike. Chakula kilipokuwa tayari kililiwa kwa ushirikiano. Muda wa chakula ulifahamika na kila mtoto aliwajibika kupata chakula. Desturi hii ya kukaa karibu na watoto na kufanya mambo mengi kwa pamoja mbali ya kuwasaidia wazazi kuwafundisha watoto maarifa na ujuzi wa aina mbalimbali, ilikuza uhusiano wa karibu wa kifamilia ambao uliwahakikishia usalama wao. Hali ya mtoto kumwamini na kujisikia salama mikononi mwa mzazi inategemea uwapo endelevu wa mzazi kimwili na kihisia tangu anapozaliwa.
Hata hivyo, kadri mwanadamu anavyozidi ‘kuendelea’ na ‘kustaarabika’, ndivyo desturi hii ya kupatikana kwa wazazi nyumbani inavyozidi kukosa umaarufu. Kwa mfano; ipo dhana inajengeka katika jamii kwamba maendeleo halisi ni vitu. Matokeo ya imani hii ni kutufanya tutumie muda mwingi kujilimbikizia vitu kwa gharama ya uhusiano na ustawi wa familia zetu.
Kadhalika, zipo changamoto nyingine za kijamii zinazotishia desturi hii ya familia. Kuna masuala kama kazi/ajira zinazowatenganisha wazazi na familia, misukosuko ya kimahusiano inayozaa talaka na/ama kulazimisha malezi ya mzazi mmoja, ujio wa shule za bweni kwa watoto wadogo pamoja na matatizo kadha wa kadha yanayofanya watoto wadogo wakue katika mazingira magumu yasiyo na uangalizi mzuri.
Kwa hiyo, tafiti zinazochunguza matokeo/athari za mazingira ya kimalezi katika ukuaji wa mtoto ni jitihada za kutafuta majibu ya changamoto hizi zisizokwepeka. Kwa kifupi, tunaweza kutaja mambo mawili kwa kutumia matokeo ya tafiti hizo. Kwanza, uhusiano wa mzazi na mtoto ndiyo unaoamua uhusiano kati ya mtoto na watu wengine na namna mtoto huyo atakavyojitazama yeye mwenyewe na watu wengine akiwamo mzazi wake.
Suala la pili ni matokeo ya umbali -kimwili na kihisia – unaotokea katika kipindi cha awali kabisa cha maisha yake, unaoweza kujenga hitilafu za kitabia kwa mtoto.
Mwandishi ni mwalimu wa Saikolojia katika Chuo Kikuu cha Kikatoliki Mwenge (MWECAU). 

Tuesday, April 11, 2017

WATOTO UWALEAVYO NDIVYO WAKUAVYO...MICHEZO !

 Michezo hii huwajengea watoto tunu njema kama umakini, furaha, urafiki, ubunifu, kuchemsha bongo na pia kutulia nyumbani na mengine mengi.
Hapa wakicheza mdako...nimekumbuka mbali sana maana nilikuwa nikipenda sana huu mchezo...hapa pia yahitaji umakini maana wakati wote ni kuhesabu tu...Vipi nawe ndugu msomaji una mchezo ambao ulicheza enzi hizo?

Friday, April 7, 2017

PICHA YA WIKI...SIO MCHEZO HARUSI MTINI

Napenda kuwatakieni wote Ijumaa njema sana wote mtakaopita hapa leo pia mwisho wa juma uwe mwema...ni wenu kapulya.

Thursday, April 6, 2017

NGOJA LEO TUANGALIE:- MISINGI SITA YA KUWA NA FURAHA KATIKA MAISHA

TABASAMU 
1. Usimchukie yeyote hata kama atakukosea sana.
2. Ishi maisha ya kawaida hata kama upo juu kimaisha.
3. Tarajia baraka hata kama magumu yanakusonga.
4. Toa hata kama wewe umenyimwa.
5. Onyesha tabasamu hata kama moyo unavuja damu.
6. Usiache kuwaombea wengine hata kama yako hayajajibiwa.

Tuesday, April 4, 2017

LEO NGOJA TUKUMBUKE ZILIPENDWA...TANZANIA YETU NI NCHI YA FURAHA


Leo nimekumbuka zamani nilipokuwa msichana mdogo nilikuwa nikisikia sana hizi nyimbo kwa hiyo leo nimekumbuka .....tuungane tunaozikumbuke hizi nyimbo .

Monday, April 3, 2017

MWEZI HUU WA NNE TUANZE NA PICHA HII...AMA ZAKO AMA ZANGU....


Pale unyanyasaji unapozidi hali inakuwa hivi....ama zako ama zangu ...Duh! kazi kwelikweli. TUACHE unyanyasaji na TUPENDA KWA DHATI.