Showing posts with label shukrani. Show all posts
Showing posts with label shukrani. Show all posts

Thursday, December 31, 2015

SALAMU/BARUA KUTOKA BLOG YA MAISHA NA MAFANIKIO:- SHUKRANI KWA WOTE!!!

Mmmhh! huyu Twiga kanipita urefu nitafika huko kweli...

Habari zenu jamani!!
Yamebakia masaa machache tu kuumaliza mwaka huu 2015 na kuingia katika mwaka mpya 2016. Hakika miaka inayoyoma na watu tunazidi kuzeeka. Ninachotaka kusema ni kwamba, blog ya MAISHA NA MAFANIKIO inapenda kuwashukuru wanablog wenzake wote, wasomaji wote na watembeleaji wote kwa ushirikiano mzuri tulioonyeshana.

Najua katika maisha watu wote hawawezi kuwa sawa yaani kimawazo. Lakini katika hizi blog zetu kwa asilimia kubwa imekuwa ni changamoto kwetu. Tumekuwa hatupendi kupoteana, mara mmoja wetu anapokuwa kimya kwa muda basi wengine tunakuwa hatuna raha tunachukua hatua ya kumtafuta. Hii yote inaonyesha ni jinsi gani ukaribu wa wanaBLOG sisi tu/ulivyo, hakika najivuna sana kwa uwepo wenu na kwa hili napenda kusema SISI SOTE NI NDUGU. NA PIA NAPENDA KUWATAKIENI WOTE KILA DOGO NA PIA KILA KUBWA MTENDALO LIWE JEMA. NA MWAKA 2016 UWE WENYE MAFANIKIO. KAMA KUNA KITU ULIAHIDI KUFANYA MWAKA HUU BASI JITAHIDI UFANYA KABLA HAUJAISHA. KWANI KUMBUKA HAKUNA KISICHOWEZEKANA. NA PIA KAMA KUNA KITU AU MTU NILIMKWANZA BASI NAOMBA TUSAMEHEANE KWANI HAKUNA BINADAMU ALIYEKAMILIKA. PAMOJA DAIMA. KAPULYA WENU!!!!

Friday, March 6, 2015

UKIPATA WASAA EBU WASIKILIZENI HAWA VIJANA NA WIMBO WAO SHUKURANI.....


Nimeusikiliza  hawa vijana maneno yao nimeyapenda sana. Kwa kweli inabidi kumshukuru Mungu kwa lolote ufanyalo ana pia kumshukuru kwa wewe kuwa wewe. Binafsi nawatakieni Dogo Muu ft. Aslay waifikie ndoto yao.

Friday, January 31, 2014

MWISHO WA MWEZI JANUARI TUUMALIZE ZILIPENDWA HATA KAMA SIELEWI ILA MZIKI UNACKEZEKA...KARIBUNI!!!!!!.....


AU TU LABDA TUSIKILIZE NA HUU WIMBO WA MONICA....


Mara nyingi ukiwa sambamba sana na walezi huwa unakumbuka vitu vingi sana.....nadhani mmenielewa...haya tuendelee kuselebuka ...tuonane mwezi ujao.  Oh! Napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutulinda salama wote tulioumaliza mwezi huu na pia napenda kuwaombea wote waliotutangulia na pia wagonjwa. Na pole nyingi kwa ndugu zetu wa Morogoro /Kilosa mji kasoro bahari, Mungu awape nguvu. IJUMAA NJEMA.

Sunday, January 27, 2013

UJUMBE WA JUMAPILI HII YA NNE YA MWAKA 2013 NI KAMA IFUATAVYO!!

Unapotafakari mema ya Mungu ya leo:-

WASAMEHE WALIOKUKOSEA,
WAKUMBUKE WALIOKUSAHAU na UILINDE AMANI YA MOYO ISIPOTEE.
Kwani utakuwa na furaha daima!!!
JUMAPILI NJEMA NDUGU ZANGUNI!!!!

Wednesday, November 7, 2012

NIPO INGAWA SIPO ILA NIPO!!!!

Kutokana na taarifa niliyowapa hapo jumapili basi ndiyo maana nitakuwa kidogo sionekani sana hapa ila nipo na pia napenda kutoa SHUKRANI ZA DHATI kwa wale wote waliuotufariji. TUPO PAMOJA NA MUNGU AWAZIDISHIE UPENDO. MUWE SALAMA WOTE!!!

Wednesday, September 19, 2012

SHUKRANI ZANGU...



Chacha wambura Ng´wanambiti
Katika maisha, watu wengi hufikiri watu wa karibu yaani ni familia tu. Leo nimehakikisha kitu ambacho sitaweza kusahau maishani mwangu. Watu/mtu anachukua muda wake na kufanya kitu ambacho wengi hawangefanya. Huyu kaka sijawahi kuonana naye lakini kama alivyosema hapa kwake hakika ni wachache sana wanafanya hivi. Mwenyezi Mungu na akubariki na akuzidishie upendo. Ahsante sana.

Tuesday, May 1, 2012

BADO NIPO! NA HIVI NDIVYO ILIVYOKUWA JUMATATU YANGU MDADA MIMI!!!


 HAPA NI JANA JUMATATU KATIKA KANYUMBA KADOGO KA JOTO(SUMMER HOUSE)
Maji yanaonekana swali lakini baridi kivumbi kwa hiyo......
....nilishindwa kuogelea wala. Jumatatu iliisha vizuri namshukuru Mungu na natumaini nanyi pia mlikuwa na Jumatatu njema.PAMOJA DAIMA NA WOTE MNAPENDWA SANA. 

Tuesday, April 10, 2012

SALAMU NA SHUKRANI KUTOKA KWA BLOG YA MAISHA NA MAFANIKIO!!!

Kwanza kabisa napenda kuwasalimu wote. Pia napenda kuchukua nafasi hii na kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kila dakika anipayo. Halafu nashukuru nimeisherekea sikuku hii ya kufufuka kwa Bwana wetu Kristo vema. Kwa hiyo namalizia na salamu hizi:-
Tuni/mafuatano ya sauti ndogo inaweza kukufanya/kutufanya uanze/tuanze kuimba, pia kukumbatiwa kunaweza kukufanya ujisikie vizuri. Vitu vidogo vinaweza kukufanya/kutufanya uwe/tuwe na furaha. Ni matumaini yangu SALAMU yangu hii, imekufanya UTABASAMU.....SIKU NJEMA....Yasinta/Kapulya

Wednesday, January 18, 2012

HUYU NDIYE YASINTA NGONYANI!!!

Kama kawaida ni JUMATANO NYINGINE TENA NA NI KILE KIPENGELE CHA MARUDIO YA MATUKIO MBALIMBALI. Na Makala hii nimeshawahi kuiweka hapa. Lakini nimeshindwa kuvumilia kutoiweka hapa tena. Ni ZAWADI AMBAYO SITAWEZA KUISAHAU MILELE.

Yasinta Ngonyani, Picha kwa hisani ya Maisha Blog
Ni binti halisi wa kitanzania, ingawa anaishi ughaibuni lakini hujivunia asili yake na utaifa wake, ni binti pekee aliyejitolea muda wake kuwaelemisha watu wa rika zote bila kujali rangi, kabila, itikadi, taifa wala jinsia.


Binti huyu si mjivuni na hupenda kubadilishana mawazo na watu mbali mbali, na pia hupenda kufuatilia habari za nyumbani kwao alikotoka na haoni tahayari kuongea lugha ya kwao. Daima hujitambulisha kwa jina la asili ya kwao na huona fahari kutumia jina hilo.


Binti huyu hakuona ajizi kuwajuza wanae asili ya kwao japo wamezaliwa ughaibuni, amekuwa msitari wa mbele katika malezi ya wanae ili kuhakikisha wanae hao hawajitengi na asili ya aliotoka yeye.


Si mchoyo wa ushauri na kupitia makala zake aziwekazo kibarazani kwake amekuwa ni msaada kwa wengi, amekuwa mstari wa mbele katika kuilemisha jamii bila kujali rika. Amejitolea kufundisha kile akijuacho juu ya malezi na matatizo mbali mbali yanayowakabili wanandoa na malezi ya watoto.


Kibaraza chake kimekuwa ni kitovu chenye kukutanisha wadau mbali mbali wenye fikra pevu, na kuibua mijadala yenye kuelimisha, kufundisha, kuburudisha na kuhuzunisha pia.


Binafsi napenda kumuita dada na kwangu mimi ni zaidi ya dada, kwani amekuwa ni mwalimu mzuri kwangu nikijifunza mambo mengi kupitia kibaraza chake nimekuwa nikijifunza mengi, na sisiti kukiri kwamba chimbuko la kibaraza cha VUKANI ni kutokana na kile nilichojifuza kwake.


Ni mkweli na muwazi, na hasiti kusema wazi hisia zake, lakini huwa makini sana ili kuepuka kumuumiza mtu mwingine kihisia, na kama kwa kusema huko kutamkera mtu mwingine, ni mwepesi kuweka sawa maelezo yake ili kuondoa msigishano wa mawazo.


Nakumbuka wakati fulani nlipopata msongo wa mawazo kutokana na tofauti zangu na wazazi wangu, alikuwa ni mtu wa kwanza kunitumia email binafsi akijaribu kuniliwaza na kunitaka nisichukue hatua yoyote kujidhuru, naomba nikiri kwamba email ile ilinisaidia sana kurudi katika hali yangu ya kawaida na nilijisikia fahari kuona kwamba kuna mtu ananipenda na kunijali japo sijawahi kuonana naye uso kwa uso.


Huu kwangu ulikuwa kama muujiza, inakuwaje, mtu kusoma mawazo yangu kupitia blog tu halafu awe karibu nami kiasi hiki, ni kitu gani kimemvuta? Kusema kweli tangu siku hiyo niliamni kuwa maandishi yana nguvu sana na kupitia maandishi yawezekana mtu mwingine kukufahamu vizuri sana.


Nimekuwa karibu sana na binti huyu, na amekuwa ni mwema sana kwangu na mshauri wangu pia, na kupitia vibaraza vyetu, tumekuwa tukibadilishana mawazo na kupeana ushauri mbali mbali ili kuboresha ustawi wetu na wa familia zetu.


Huyu ndiye Yasinta Ngonyani, kwa kumsoma zaidi bofya hapa.


-------------------------------------------------------------------------------------------------Makala hii iliandikwa na mdogo wangu wa hiari Koero Mkundi mwaka 2009/08/14 bado nimevutiwa sana na hii makala na nimeona niiweke hapa kwangu pia kama kumbukumbu na pia kujikumbusha yaliyopita kwani si vibaya. Pia nachukua nafasi hii kwa kumshukuru sana mdogo wangu huyu wa hiari Koero Mkundi kwa kazi nzuri anazozifanya kwa kumsoma zaidi kazi zake ingia hapa. Pia nauthamini sana uwepo wake Mwenyezi Mungu na akulinde na akuongoze na yote utendayo yawe mema. Kwani yeye ndiye mwezeshaji wa yote na yeye ndiye ajua anavyotuwazia maana mawazo atuwaziayo ni mema. Ni hayo tu kwa leo...Halafu sijui upo wapo Koero?
TUKUTANE TENA JUMATANO IJAYO AU WAKATI MWINGINE....


Sunday, December 11, 2011

NAWATAKIENI WOTE JUMAPILI NJEMA...


JUMAPILI NJEMA KWA WOTE AMANI NA UPENDO VITAWALE NYUMBANI MWENU

Friday, December 9, 2011

SALAMU ZA KUSHUREKEA MIAKA 50 YA UHURU TANZANIA KUTOKA SWEDEN...

Familia hii haiko nyumba katika siku hii ya kusherehekea miaka 50 ya Uhuru. Ingawa mwanafamilia mmoja hayupo katika picha. MUNGU IBARIKI TANZANIA, WABARIKI VIONGOZI WAKE, HEKIMA UMOJA NA AMANI MUNGU IBARIKI TANZANIA NA WATU WAKE IBARIKI TANZANIA ....

Tuesday, November 1, 2011

AHSANTE BABA!!!

Hapa Mwenyewe Mzee Ngonyani

Unajua/mnajua kama kumbukumbu nyingine zinakuja wakati ukisikiliza mziki? Basi mimi leo nilikuwa nasikiliza mziki na mara nikakumbuka kisa hiki ambacho kilinipata. Nikiwa nikiishi kijiji cha Kingoli. Nakumbuka nilikuwa darasa la tano. Kwanza nianze na KUMSHUKURU BABA kwa tabia yake aliyokuwa nayo ya kila usiku kupita na kuangalia watoto wamelala? Kwani siku hii aliokoa Maisha yangu. Siku hiyo kama kawaida, nilikuwa na homework , basi baada ya chakula cha jioni nikachukua koroboi yangu na kuanza kusoma. Nilikuwa nimejilaza kitandani na nikaweka karoboi kifuani huku nikisoma. Muda ukapita, nikapitiwa na usingizi. Si mnajua huwezi kulala tu bila kugeuka. Nikawa nimegeuka bila kufikiri ya kwamba koroboi bado inawaka. Halafu mbaya zaidi nilikuwa nimejifunika blanketi. Kama baba angechelewa kidogo tu basi leo nisingekuwa hapa. AHSANTE BABA.

Huu hapa ndio wimbo ambao umenikumbusha kisa hiki.....

Sunday, October 30, 2011

NINAWATAKIENI JUMAPILI NJEMA, NINAPENDA KUMSHUKURU MUNGU KWA KUFIKA JUMAPILI YA MWISHO YA MWEZI HUU!!!

Hapa katika picha ilikuwa mwezi wa saba wakati nikiwa Ruhuwiko. Kama kawaida Kapulya hakukosa kumdadisi BABA PADRE wakati alipofika nyumbani kwake kusoma misa ya kumkumbuka mpendwa wetu Asifiwe.

Jumapili ya leo nawaomba muungane nami na kuimba wimbo ni katika nyimbo za zamani za Bikira Maria...ambazo ni nyimbo maarufu sana ziliimbwa sana karibu na kila mwumini, naamini mtakuwa mnaufahamu ni huu hapa haya tuimbe pamoja moja, mbili, tatu :- "Sisi wana wadunia tukumbuke maneno aliyosema Bikira Maria, alipo watokea watoto wa Fatima; Lucia, Francisco na Yasinta, alisema tusali....tusali rozari na tupate amani, na tuwaombee wale wakosefu wasio na mwombezi". Ahsante kaka Baraka Chibiriti kwa kunikumbusha wimbo huu:-)

Hata hivyo naona tusikilize na nyimbo nyingize za zamani pia....

JUMAPILI NJEMA KWA WOTE!!!!!

Tuesday, October 18, 2011

NAPENDA KUTOA SHUKRANI ZANGU KWA WOTE KWA MAOMBI YENU/ JIONI HII NINAJISIKIA NAFUU NA NAAMINI NIPO SALAMA..AHSANTENI!!!


Kwa ajili yenu wapendwa

Napenda kuwashukuruni wote kwa maombi yenu mazuri.Kweli nasema upendo wenu na mshikamano ni mafanikio makubwa kwa mimi na pia kwenu. . Kwa hiyo kwa jambo hili napenda KUWASHUKURUNI WOTE. NA NASEMA PAMOJA DAIMA bila kusahahu UPENDO DAIMA!!!!!

Monday, August 8, 2011

"KAPULYA" BLOG YA MAISHA NA MAFANIKIO:- INAPENDA KUMSHUKURU MUNGU KUWA TUMESAFIRI SALAMA...MENGINE YANAKUJA BAADAYE:-) NIMIRUDIIII





Nimefika jana jioni .Hapa ni Jumamosi ya tarehe 6/8 nikiwa Silver Sand Dar Es Salaam.......Kapulya huyooooooo!!

Monday, June 13, 2011

SHUKRANI ZANGU KWA WALEZI/WALIMU

Leo napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa WALEZI/WALIMU kwa kazi kubwa waifanyayo. Sijui kama wewe mwenzangu umewahi siku moja kufikiria ya kuwa hakuna mlezi/walezi wazuri kama walimu. Fikiria mtoto aanzapo chekechea, unampeleka huko chekechea/”shule ya Vidudu” na wewe mwenyewe unaenda kazini na baadaya ukishamaliza kazi unaenda kumchukua.
Na unakutana mtoto mwenye furaha tele kabisa. Na pia inawezekana baada ya muda mtoto atakuwa kamzoea zaidi mwalimu kuliko hata wewe na mwalimu atamfahamu zaidi mwanao kuliko wewe/mimi mwenyewe.
Nimejaribu kufikiria sana, sisi wazazi jinsi tulivyo na muda mchace sana kuwa na watoto wetu. Je? wewe pia umefikiria hili? Yaani hapa unaweza kusema walimu wa chekechea wao ndio wazazi kamili. NA INAWEZEKANA HATA KUANZA KUTEMBEA NA HATA KUSEMA MANENO YA KWANZA ANAANZIA HUKOHUKO CHEKECHEA.
Kwa kweli mnastahili PONGEZI WALIMU.
Na baada ya miaka ya kuanza shule ifikapo, hapo ndio inakuwa pia mtoto anaondoka asubuhi kwenda shule. Muda wote anakuwa na MWALIMU/WALIMU. Na mwalimu/walimu ndiye/ndio wamleao kwa asilimia kubwa. Kwani anakuwa muda mwingi san ana mtoto /watoto wako/wetu kuliko sisi WAZAZI. Nimejaribu kufikiria kwa mfano mimi mwenyewe binafsi, mara nyingi tunaagana asubuhi na halafu tutaonana tena kesho alasiri nirudipo katika mihangaiko yangu . Na kwa wengine huwa hawakutani kabisa na watoto asubuhi. Kwa vile labda baba au mama anahitajika kuwahi sana kazini, na anaporudi jioni watoto wanakuwa wamelala na kesho yako hivyo hivyo huondoka kabla watoto hawajaamka.


Kwa hiyo mimi kama mzazi napenda kutoa shukrani zangu kwa WALEZI/WALIMU WOTE KWA KAZI NZURI MUIFANYAYO. MAANA MNASTAHILI KWA KWELI. AHSANTENI SANA!!!!

Wednesday, April 27, 2011

HONGERA KWA SIKU YA KUZALIWA KWAKO DA´MIJA MWANAMKE WA SHOKA!!!


Napenda kukutakia siku yako ya kuzaliwa kheri na baraka tele. Mwenyezi Mungu na akulinde uwe salama pia uwe na afya njema siku zote. Na pia uwe bibi kizee ili uweze kucheza na wajukuu wako pia vijukuu. HONGERA SANA KWA SIKU YAKO HII TUKUFU KWA KUONGEZA LIMWAKA:-) UWE NA SIKU NZURI NA WALA USITHUBUTU KUTUNYIMA HIYO KEKI!!!
Zaidi unaweza kumwona mwanamke huyu wa shoka kwa kubonyeza Da´Mija.

Sunday, February 20, 2011

UJUMBE WA JUMAPILI HII YA NANE YA MWAKA!!

Unapotafakari mema ya Mungu ya leo:-

WASAMEHE WALIOKUKOSEA,

WAKUMBUKE WALIOKUSAHAU na UILINDE AMANI YA MOYO ISIPOTEE.

Kwani utakuwa na furaha daima!!!




JUMAPILI NJEMA NDUGU ZANGUNI!!!!

Friday, January 7, 2011

SHUKRANI ZANGU KWA DA´MIJA NA WENGINE WOTE!!!

Sijui nianze vipi? Ngoja nianze hivi AHSANTE sana kwa kunipa heshima hii kubwa katika blog yako na kwa vile macho yangu kwa sasa yamejaa machozi ya furaha basi sitasema mengi. AHSANTENI, Ah nimeipenda HESHIMA hii na napenda iwe moja ya kumbukumbu ambazp sitasahau maishani mwangu ndio maana nimeona niiweka hapa MAISHA NA MAFANIKIO ili iwe karibu nami. Kwa mara nyingine tena AHSANTENI SANA!!!!


Ninachomheshimia Da Yasinta..


Wadau jana mwanablogu mwenzetu Yasinta Ngonyani alisherehekea siku yake ya kuzaliwa. Nilifikiria nizawadie nini nikaona ni bora nimpe tuzo ya kuwa mwanamke wa shoka wa wiki hapa bloguni. Haikuishia hapo nikawa nimetoa changamoto kwamba kuna sababu nyingine iliyonifanya nimchague kama mwanamke wa shoka, nashukuru wadau mliochangia kwani hii ni njia bora ya kutiana moyo pia.
Sasa ngoja nami niseme kinachonifanya nimuheshimu huyu dada.

Kwanza kabisa, ni uwezo wake wa kuhakikisha karibu kila siku anabandika kitu bloguni kwake tena chenye ubunifu, Yasinta kwa hilo nakupa hongera sana.
Pili, ni hili ambalo kaka M-3 pia amelisema, ni uwezo wake wa kutembelea blogu nyingi na kutoa maoni, kuna wakati huwa nakutana na blogu mpya kabisa nikizifungua nakuta Yasinta alishapita tena siku nyiiingi. Kubwa zaidi mtu ukipotea bloguni ni lazima akuulizie na akiona kimya Yasinta hurusha e-mail...! Yasinta hii inaonyesha jinsi ulivyo na moyo wa utu kwa wengine...
Kwa kweli kwa hayo na mengine waliyoyasema wachangiaji waliopita, sina budi kusema YASINTA WE SALUTE YOU!!! UNA MOYO WA UPENDO KWELIKWELI UNAOTAKIWA KUIGWA.
UBARIKIWE SANA.


Hapo chini ni wachangiaji walivyomuelezea Yasinta..

mimi nafikiri ume mbandika kwenye blog yako,kutokana namichango yake katika blog mabilimbali.pia nayeye kama mwanamke, mtanzania kwa kiasi fulani ameonyesha nia ya kuwakomboa wanawake wenzie hasa kwa misimamo yake,hisia zake, nahata uwazi kwa upande mwingine.pia ni mdada ambaye anajiwakilisha yeye kama yeye katika blog kwa kuamini kile akiandikacho,ambacho uhodari huo wa kuthubutu ni njia moja wapo ya mwanamke kujitambua, kuwa yeye ninani,nahtimaye kujikomboa, kimawazo,fikra na vitendo.ingawa nikimwangalia Yasinta,alikotoka ni mbali sana nahata kufikia hapo alipo umejitahidi.ombi kwako,unajuwa mchezo wa KOMBOLELA unavyo chezwa,butuua......uwakomowe wenzako. kaka sam

emu-three said...
MIMI NAMHESHIMU SANA HUYU DADA. Nasema namheshimu kwa sababu ya `ucheshi wake' udadisi wake na ni mtu wa watu, kama angekuwa Tanzania ningemshauri agombee ubunge.
Siku moja nilisema ngoje niwe wa kwanza kuwatembelea wenzangu kwenye blog zao, cha ajabu kila nilipopita nilimkuta keshafika...ana upendo na watu na anajali sana kazi za wenzake, ndio maana lazima aache ujumbe kukupa moyo.
Mimi nimshukuru sana kwani alinipa moyo kwenye `kijiwe' changu, nilikuwa nimekata tamaa kabisa, unaandika watu hawafiki hawachangii, lakini akanipa moyo na hata kunisaidia kunitangaza. NAMSHUKURU SANA NDIO MAANA NASEMA NEMHESHIMU KAMA DADA YANGU!
Ahsante na Da mija na wewe ni miongoni mwao!

Swahili na Waswahili said...
Mimi namkubali sana kwa mengi nikiandika hapa unaweza kunistopisha!
kifupi amejaaliwa upendo,utuwema,busara,

Anastahili kuwa mwanamke wa wiki na zaidi!na mengi ya kuigwa kutoka kwake!

Nakupenda dada Mkubwa Yasinta binti wa Ngonyani!!!!!!!!!.

John Mwaipopo said...
naona utufumbulie fumbo wewe mwenyewe

kamala Lutatinisibwa Lutabasibwa said...
si mwanamke! anasuka harafu ana blogu! mimi kule kwetu naowaona wengi wanaopaswa kuwa wa wiki ila hawana blogu! ila yasinta si anaishi ulaya?
Makala hii imeandikwa na Da mija ukitaka kumsoma daidi gonga hapa

Wednesday, January 5, 2011

LEO NI SIKU YANGU YA KUZALIWA

Napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunilinda salama mpaka kufika siku hii ya leo na kuongeza limwaka limoja zaidi. Namshukuru kwa kuniepusha na mambo mabaya, magonjwa na pia vishawishi. Kijana wangu Erik amepata nafasi kuchagua hii picha anasema ameipenda.

kutimiza miaka bila mziki hapana. Haya wote UNGANENI NAMI NA WIMBO WA TUSELEBUKE NI KITOTO/LIZOMBE....


Namshukuru Mungu kwa yote, familia yangu pia ninyi marafiki zangu!!!