Showing posts with label chumba cha kulala. Show all posts
Showing posts with label chumba cha kulala. Show all posts

Monday, October 24, 2011

CHUMBANI/CHUMBA CHA KULALA KIWEJE?

Habari zenu ndugu zangu natumaini wikiendi yenu wote imekuwa sio ya pilikapilika sana.

Haya mwenzenu leo nina swali ambalo limekuwa likinikera muda sasa. Lakini jana nilishindwa kuvumilia na wakati nipo kazini nikawauliza wafanyakazi wenzangu. Jambo lenyewe ni kuhusu chumba cha kulala. Na swali lenyewe ni hivi je? chumba cha kulala kinatawa kiweje? Yaani pembeni mwa chumba kuwa na vimeza na je hapa kwenye vimeza kuwe na nini? na je? kuwa na TV? Computer? na aina nyingine ya vitu? au kuwa na kitanda tu?...na baadaye baada ya pitapita /udadisi wangu nikakutana na habari hii hapa chini ambayo nimeiunganisha. haya tusaidiana kupeana ushauri.
---------------------------------------------------------------------------------------------

naamini baadaya ya siku ndefu kutafuta riziki, na baada ya siku ndefu kuongea na watu tofauti, kukasirishwa na watu tofauti na wakati mwengine inafika mda mwili wako unakuwa umechoka unachohitaji na kupumzika katika kitanda chako cha nyumbani.. wengi nimesikia wakisema huwawia vigumu kupumzika vizuri kitanda kingine tofauti na alichonacho nyumbani.. sababu ni kwamba labda godoro la nyumbani ni zuri kuliko sehemu nyengine ama tu ukilala nyumbani unapumzika vizuri zaidi ukiwa pembeni ya mtu aliyekaribu na moyo wako..

ndio swala la chumbani linapoingia, sehemu ya kulala hupaswa kukufanya uchovu uliokuwa nao wote kutoweka, chumba cha kulala hakitakiwi kuwa na vitu vingi vya kufanya hata hewa isiingie, sijui viatu, kapu la nguo chafu, ma vengine vingi.

hupendeza chumba chako cha kulala kiwe na kitanda tu peke yake, lakini kwa watu ambao nyumba zao ni ndogo basi kabati ndani ya chumba sio vibaya lakini muda eote liwe limefungwa, na hata kama umeweka viatu kwenye chumba chako basi hakikisha kabla hujavipeleka chumbani viatu vyako unaviweka kwanza sehemu ya hewa nje ili uvundo na jasho viweze kutoka ndio uvipeleke chumbani, na wenye makapu ya nguo chafu chumbani akikisha makapu hayo yanamifuniko kuzuia harufu mbaya ya nguo zilizovaliwa siku za nyuma kabla ya kufuliwa.

chumbani mambo mengi sana hufanyika ukiacha kulala, hata kupumzika tu na mwenzi wako mkiongelea mambo fulani ya maisha yenu. kwahiyo hutaki kufanya hivyo na harufu mbaya ikiwapitia pembeni. Habari hii nimekutana nayo hapa.