Tuesday, January 10, 2012

LEO TUANGALIE VITENDAWILI VYA KISWAHILI:- KITENDAWILI…..

1. Haukamatika wala haushikiki.........
2. Anataga huku akitambaa...................
3. Ninapompiga mwanangu watu hucheza...................
4. Ubwabwa wa mwana mtamu........................
5. Kuku wangu katagia mayai mibani.................

38 comments:

ray njau said...

Vitendawili vigumu kuliko mawe!Hapa nimeshindwa nami nakupa mji nenda Songea.

Goodman Manyanya Phiri said...

Nimekipenda kitendawili: "Ninapompiga mwanangu watu hucheza..................."

Sijui maana ya kitendawili.

Nafurahia lakini ukweli ndani yake kwamba labda kila unapompiga mwanao maadui zako hufurahia ujinga wako.

Ukweli ni kwamba ziko namna nyingi za kumlea mwanao kwa nidhamu bila kumpiga.

o'Wambura Ng'wanambiti! said...

duh....nimepita kapa maana nikitoa majibu watu wanaweza kuvunjika mbavu...sasa sijui utawalipia gharama za kwenda huko India!!!

Rachel Siwa said...

Hahhahahahhaa kaka Manyanya umeniacha hoiiiiii,jibu NGOMAAAA, Nipe thawadi dada Yasinta!!!!!Mbarikiwe wooote!

sam mbogo said...

Majibu- 1 jibulake ni mwanga.
- 2 ushanga
- 3 ngoma
-4 matandu/ukoko
-5 nanasi
kaka s

Mija Shija Sayi said...

Nadhani kuna haja ya kukumbushana zaidi, Yasinta viongeze..

Kaka Manyanya kula tano kwa tafsiri...

Kaka Sam duh! Yaani umezipatia zote!!

Yasinta Ngonyani said...

Wapendwa ndugu zanguni kwa kweli inabidi tukumbushane daima maana naona watu wameanza kusahau ...ila Dada Rachel na kaka Sam mmepata hapo kwenye jawabu la Ngoma na kaka Sam hapo kwenye jawabu la Nanasi ...jaribuni tena mshindi zawadi nono imeandaliwa:-)

Yasinta Ngonyani said...

Naona ni afadhali nitoe majibu au je kuna mtu anataka kujaribu? Maana naona kama vitendewili vilikuwa vigumu kweli au?

Yasinta Ngonyani said...

Haya majibu yake ni haya:-
1. Moshi
2. Mboga
3. Ngoma
4. sungizi
5. Nanasi.
Nadhani siku nyingine mtaweza tu labda nifanye hii kila wiki kuchemsha bongo kiduchu:-)

Unknown said...

Weka vitendawili vingine naomba

Vansh Chavda said...

1. Moshi
2. Boga
3. Ngoma
4. Usingizi
5. Nanasi

Unknown said...

Mwanangu akiwa na wenzake hatambuliki

Unknown said...

Naomba mnisaidie hiki kitendawili Maiti anasema lakini walombeba wako kimya

Unknown said...

Hii leo imenisaidia mtoto wangu wa primary school kupata majawabu ya vitendawili amepatiwa Kama kazi ya nyumbani....asanteni.

Unknown said...

Chungu na mafiga

Unknown said...

Sijui "nimpigano mwanangu watu hucheza"--------------

Unknown said...

Nina mwanangu ukimpa chakula Amalia ukimnyima halii

Unknown said...

Nyota

Unknown said...

kitendawili isemayo ubwabwa wa mwana ni mtamu

sijui jibu lake

Unknown said...

Kitendawili ukiona njigi utathani njege na ukiona njege utathani njigi

Anonymous said...

Nina mwanangu nikimpa chakula analia nikimnyima chakula halii jibu nini

Anonymous said...

Usingizi

Anonymous said...

Pooo mbili zavuka

Anonymous said...

Gari

Anonymous said...

Poo mbili zavuka -macho

Anonymous said...

Jibu lake sikujui naomba nipewe jibu

Anonymous said...

Ngoma

Anonymous said...

Nisaidie vitendawili hivi1, hesabu yake haina faida
2, maji ya kisima changu hayanyweki

Anonymous said...

Naomba jibu la kitendawili hiki nina mwanangu nikimpa chakula angalia nikimnyima chakula halii

Anonymous said...

Nina swali, sijui kitendawili ya kurunzi

Anonymous said...

Ukimgusa mwanangu mimi hucheka

Anonymous said...

Nina mtoto wangu nikimpa chakula analia

Anonymous said...

Nisaidien ich kitendawili maji ya kisima changu hayanyweki jibu lake

Anonymous said...

Redio

Anonymous said...

redio

Anonymous said...

Nikimpiga mwanangu nalia mwenyewe jibu lake nn jamani

Anonymous said...

Nikimpiga mwanangu naliq mwenyewe jibu Lake ni kitunguu

Anonymous said...

Ngoma