Showing posts with label mboga. chakula. Show all posts
Showing posts with label mboga. chakula. Show all posts

Monday, June 24, 2013

NIMERUDI KUJA KUANGALIA BUSTANI YANGU MARA MOJA...HIVI NDIVYO BUSTANI ILIVYO BAADA YA MWEZI MMOJA...MTOTO WA MKULIMA NI MKULIMA!!

 HAPA NI MBOGA YA MABOGA ..TENA ILE YA NJOMBE(NYAMUZA) AU PITIKI/SUKUMA WIKI..IMEKUWA HIVI BAADA YA MWEZI MMOJA
 NYANYA ZIMEANZA KUTOA MAUA
 SALLADI AINA YA RUCCULA
 STRAWBERRY/STROBERI
 AINA YA VIUNGO/ÖRTKRYDDOR
 VIAZI MVIRINGO
 VITUNGUU
 FIGIRI
Na hapa ni matokeo ya mboga ya maboga mnayaona mchuma wa kwanza. Kwa hiyo leo ni chakula kila nikipendacho ugali, mboga na maharaga hivi hapa maharage yapo jikoni. Mchicha bado kidogo haujakua ..nitawaonyesha ukikua...Si mnakumbuka hapa....... KARIBUNI TUJUMUIKE KATIKA MLO HUU WA MIKONO YA KAPULYA WENU:-)JUMATATU NJEMA SANA KWA WOTE

Monday, August 6, 2012

TUANZE JUMATATU HII KIHIVI:- KILIMO....UKIITUMIA MIKONO YAKO KAMA INAVYOTAKIWA :-MATOKEO YAKE NDIYO HAYA...UTAKUWA MLO WA MCHANA WA LEO MBOGA/MAJANI YA MABOGA!!!

MBOGA YA MABOGA KWENYE UNGO...
Ni furaha ilioje kuweza kula chakula ulichopande mwenyewe, hapa ni majani ya maboga na ndiyo yatakuwa mlo wa mchana wa leo:-) Napenda kuwakaribisheni wote karibuni tujumuike..Si mnajua kulima analiama mmoja lakini walaji ni wengi.... Ndiyo nimeanza  kuitengeneza....

Friday, July 6, 2012

MAENDELEO YA BUSTANI YA KAPULYA ILIVYO LEO....!!!

Haya ndiyo matokeo/maendeleo ya bustani ya kapulya  kutoka  siku hii na siku hii na hapa ni leo mambo ndiyo haya... karibuni wote ila msisahau UNGA WA MUHOGO/MAHINDI...KAPULYA....

 Figiri
 Mchicha
mboga maboga tena kutoka Njombe/Iringa

Tuesday, June 19, 2012

JINSI NILIVYOWAZA NINI CHA KUPIKA JIONI YA LEO/NIMETAMANI MBOGA!!!



Nimeiangalia picha hii na kujikuta :-) ebu angalia hayo matembele na naona hapo kwenye hilo kapu kuna zaidi ila nikakaza moyo na kuendelea kuwaza.....

Jioni inaingia nimekaa hapa nawaza nini cha kupika mwanamke mimi...Ghafla natoka nje naangalia bustani . Uwiiiii..bado  bado kabisa. Naingia tena mtandaoni ili kupata mawazo nakutana na picha hii. Kamoyo kanadunda na hamu ya kupa huo mchicha, matembele,chaina ...halafu naangalia akina mama walivyojipanga hapa nami naanza kupata wazo nitawauzia majirani mboga zangu...ujanja eeeh:-)  Picha kutoka kwa Mjengwa.

Monday, June 11, 2012

KAPULYA NA BUSTANI YAKE LEO....

Kama wengi mnakumbuka wiki kadhaa zilizopita nilikuwa na shughuli ya kulima bustani  kwa hiyo  hapa ni mwendolezo au niseme .....


 inaendelea kama muonavyo hapa ni leo na mimea imeanza kuchipua ukiangalia sana utaona
....mdada anaendelea kumwangilia ili mimea ikua kwa haraka  mpiga picha ni dada Camilla...haya tutaendelea kuona mafanikia baada ya wiki tena...JUMATATU NJEMA NA JIONI NJEMA ....

Tuesday, May 29, 2012

BUSTANI YANGU INAVYOONEKANA KWA SASA..AU JANA JUMATATU!!!

 Hapa ni kaeneo ambako huwa nalima bustani  za mbogamboga za aina mbalimbali. Na jana Jumanne ya 28/5-12 ndio nimepanda . nimepanda Corrot, maharagwe, mchicha, maboga, figiri, vitunguu, nyanya, nk. Kutokana na hali ya hewa kuwa si nzuri sana mwaka huu inasemekana nimechelewa kidogo....Ila baada ya wiki chacha nategemea mimea itakuwa imeanza kuota...au kuwa kama ...


...katika bustani hii hapa . Majibu tutayapanda karibuni. Hii ndiyo moja ya shuguli nilizozifanya jana. PAMOJA DAIMA SANA!!!

Wednesday, December 28, 2011

JAMANI, MBOGA, MBOGA, MCHICHA UNAPITA MBOGA YA MCHANA/JIONI!!!

Jipatie mboga ya haraka kwa mchana huu au labda jioni ...bei pouwa .

Thursday, July 29, 2010

Nipo likizo na pia nimekuwa mkulima wa bustani na hapo mnaona matokeo yake!!

Mkulima ni mmoja na walaji ni wengi
Hapa mnaona matunda ni mboga ya maboga tena ile ya ubenani (Nyamuza)


Karibuni wote tujumuike kula ugali na mboga ya maboga na hapo kwenye boxi ni mchicha kwa hiyo likizo nzima ni mbogamboga tu na bila kusahau nitakuwa naweka akiba kwa wakati wa baridi. LIKIZO INAENDELEA NA TUNAPATA MVUA NYINGI SANA HAPA MWAKA HUU. TUTAONANA WAKATI MWINGINE KILA LA KHERI. NA KUMBUKENI SISI SOTE NI NDUGU.