Thursday, January 31, 2019

SI KILA MARA UNAPASWA KUUSIKILIZA



Ni mara nyingi sana tumeshindwa kufika mahali tulipopaswa kufika kwa wakati. Ni mara nyingi pia labda tumefanya makosa makazini au kwenye shughuli zetu za kila siku,yote hii ni kwasababu ya kuusikiliza kila wakati. Tumeshindwa kuwa na sauti kwake,unatupelekesha sana....

Maisha yanakwenda kwa kasi kweli kweli. Kila siku shughuli na mahitaji yetu yanaongezeka. Muda wa kufanya kazi unaongezeka....

Kadiri muda wa kufanya kazi unavyoongezeka ndivyo muda wa kupumzika nao unapungua,mahitaji mapya yanaongezeka. Kadiri siku zinzavyokwenda ndivyo mahitaji mapya yanaibuka zaidi kila siku,vile tulivyo navyo leo  tunaviona havifai tena tunataka vipya....

Ni kweli miili yetu nayo inachoka sana na kuhitaji pumziko kwa mfano ili kukusanya nguvu mpya ya kuendelea kuwajibika. Lakini jambo moja kubwa pengine tusilolijuwa ni kwamba mwili haujawahi kuridhika na chochote,kila siku/saa utahitaji kitu kipya. Ukipumzika leo kesho mwili utataka kupumzika tena na kesho kutwa hivyo hivyo na siku inayofuata,hakuna mwisho....

Wengi tumeshapata hasara au pengine kushindwa kutimiza mambo fulani fulani katika maisha  kwasababu ya mwili. Tunashindwa au tulishindwa kwasababu ya kuusikiliza mwili na kuupa kila utakacho lakini bahati mbaya sana mwili unaendelea kuhitaji tu. Unatufurusha tu kila siku....

Wapendwa,kama nilivyosema huko juu,mwili nao una mahitaji yake lakini mwili huu huu hauridhiki,hakuna wakati utasema hapana,ukiupa kuku leo kesho utatamani Sato. Hautaishia hapo keshokutwa utataka dagaa wakavu,siku inayofuata utataka nyama ya kukaanga na mlolongo unakuwa mreefu sana,hakuna kukoma labda afya iwe na kasoro....

Mwili ni kama mtoto mdogo. Mtoto anapoamka anataka kitumbua hapo hapo atataka kwenda kucheza. Kuna wakati tunawazuia watoto kutenda mambo fulani kwasababu tunajuwa yanaweza kuwadhuru au hayana faida kwao. Miili yetu nayo ni hivyo hivyo,si kila utakachohitaji basi uhangaike kuupa....

Wakati wa kuamka asubuhi unaweza kufika lakini mwili unakataa huku unafahamu kabisa kuwa ni lazima uamke ili ukawajibike,ukiusikiliza mwili wako utaharibu kazi. Mwili unaweza kukuharibia malengo yako na zaidi maisha kwa ujumla wake....

Si kila unaomtamani mwanamke/mwanaume basi uupatie mwili unachokitaka. Haitatokea ukaridhika,ukiupa mwili utakacho leo kesho utataka tena kwa mwingine mwishowe utaharibu ndoa yako na familia kwa ujumla....

Si kila unapotamani bia basi unywe. Si kila unapotamani nguo basi ununue. Utaharibu bajeti za mambo mengine halafu mwili hautakoma kutaka vingine....

Tujifunze kuukatalia mwili na vurugu zake. Upatie mwili yale ya muhimu tu. Kama unahitaji kulala,lala kwa muda sahihi na baada ya hapo amka ukafanye kazi. Mwili utakutaka uendelee kulala tu,ukiusikiliza inakula kwako. Utaharibu kazi na matokeo yake utaishia kufukuzwa kwenye nyumba uliyopanga au utashindwa kuihudumia familia yako....

Uvivu ni matokeo ya kuusikiliza mwili. Karibia tabia zote hasi ni matokeo ya kusikiliza mwili kuliko pindukia. Tabia kama ulevi,umalaya,matumizi ya madawa ya kulevya n.k ni matokeo ya jambo hili....

Kuanzia leo sema hapana kwa mwili wako. Kataa kuwa mtumwa wa mwili wako leo na maisha yako yatabadilika kabisa....

Uwe na wakati mwema......

Chanzo:- nimetumiwa na rafiki nikaona sio vema kubaki na ujumbe mzuri wa burasa kama huu  peke yangu. Elimu ni kugawana.

Friday, January 25, 2019

HEBU LEO TUANGALIE BAADHI YA MANENO LA HEKIMA....!

1. Kila jambo na wakati wake
2. Aba na haba hujaza kibaba
3. Maji hayatoki yakishushwa kwa moto.
4. Siku njema huonekana asubuhi.
5. Dalili ya mvua ni mawingi
6. Dawa ya moto ni moto
7. Fimbo ya mbali haini nyoka
8. Asiyefunzwa na mamaye hafunzwa na ulimwengu
BASI  NIWATAKIENI IJUMAA NJEMA NA MWISHO MWEMA WA JUMA.

Thursday, January 24, 2019

KUMBUKUMBU .....ENZI HIZOOO! WATU TUMETOKA MBALI KWA KWELI

Aina za mafuta ya kupikia pa kupaka kwenye mkate nadhani PRIDE na SUPA-GHEE
Aina nyingine ni tan bond
Dada ana mzinga wa redio/ kaseti ili kupata pozi
Basi la Iringa enzi hizo

Thursday, January 10, 2019

VIFAA MBALIMBALI VYA KUTUNZIA MAJI/KWENDA KUCHOTA MAJI KISIMANI AU SEHEMU NYINGINE

 Hapa ni ndoo tena za aina tatu au nne hivi 
 Hapa ni VIBUYU
 MTUNGI
Hapa ni kabila la wamasai wao hubeba mgongoni na hutumia madumu/madungu .
Binafsi nimezoea tumia ndoo na mtungi na kubeba kichwani. Je wewe mwenzangu?

Wednesday, January 9, 2019

UJUMBE WA LEO : TUYAKUMBATIE MALENGO/MAWAZO MAPYA ILI KULETA UHALISIA ....

Ukikumbatia ulicho nacho utaona mafanikio yake. NAWATAKIENI SIKU HII YA JUMATANO IWE NJEMA SANA.  PAMOJA DAIMA. Ni mimi Kapulya wenu.

Saturday, January 5, 2019

LEO NI SIKU YANGU YA KUMBUKUMBU YA KUZALIWA

 Namshukuru  mwenyezi kwa kunipa afya njema mpaka leo nimeiona kumbukumbu  yangu ya kuzaliwa. Pia napenda kuwapa hongera kwa wote waliozaliwa mwezi  huu wa kwanza  na watakaozaliwa mwezi huu.
 Kwa vile nilikuwa mwema familia, ndugu na marafiki wamenipondeza kwa zawadi.HONGERA SANA KWA SIKU YA KUZALIWA MIMI.