Hapa ni baadhi ya akina mama wakichambua Korosho kwenye moja ya kiwanda wilayani Tunduru mkoani Ruvuma......Nimekumbuka mbali sana wakati naishi Litumbandyósi na Kingole kuilikuwa/kuna Korosho nyingi sana. Basi mimi na kaka zangu tulikuwa tukizishughulikia hizo wewe acha tu, yaani mpaka mikono pia vidole vilikuwa vinachubuka maana Korosho zina mafuta fulani hivi yaliyosababisha iwe hivyo. Ila kwa kweli ilikuwa raha sana....picha hii nimeitoa kwa mdogo wangu Ester Ulaya.