Showing posts with label tatizo. Show all posts
Showing posts with label tatizo. Show all posts

Thursday, April 19, 2012

KUMRADHI JAMANI!!

NAOMBA KUWAOMBENI RADHI KWA BADILIKO LA GHAFLA LILILOJITOKEZA KATIKA BLOG YA MAISHA NA MAFANIKIO KATIKA BLOG LIST. NALIFANYIA KAZI TATIZO HILO. TUPO PAMOJA......

Wednesday, November 5, 2008

TATIZO NI LIPI?

Mpaka watu wawe na roho mbaya ya:-

Usafirishaji haramu wa watu/biashara ya watu(Human Trafficking) ni nini?
Usafirishaji na biashara haramu ya watu (Human Trafficking) ni nini?

Usafirishaji na biashara haramu ya watu (human trafficking) ni uhamisho wa mtu kutoka kwenye jumuiya yake na kwenda sehemu nyingine ndani au nje ya nchi kwa ahadi za uongo, matokeo yake ni kunyonywa kunyanyaswa, na kutumikishwa kwa kupindukia bila ya ujira kwa faida ya mtu mwengine, hii hujulikana kama utumwa mamboleo na ni moja ya matishio makubwa ya haki za binadamu. Ingawa usafirishaji na biashara haramu ya watu (human trafficking) huwatokea wanaume, wanawake na watoto, lakini inaonekana wanawake na watoto ndio wanaoathirika zaidi.


Usafirishaji na biashara haramu ya watu hutokea duniani kote na unyonyaji wa watu hutofautiana kati ya nchi na nchi (watoto kutoka Togo wanatumikishwa na kunyanyaswa katika mashamba ya kakoa Ghana, Wasichana wa Colombia wanalazimishwa ukahaba Japan n.k.)

Usafirishaji haramu wa watu/biashara ya watu katika Tanzania

Hali ya Usafirishaji na biashara haramu ya watu Tanzania.

Usafirishaji na biashara haramu ya watu (human trafficking) hutokea ndani ya Tanzania na kimataifa. Watu huletwa Tanzania kutoka Kenya, Uganda, Malawi na Burundi. Usafirishaji na biashara haramu ya watu unaoonekana kutapakaa sana ni ule wa ndani kwa ndani ya nchi unaolenga kuwanyonya watoto katika kazi za ndani.
Tanzania pia inatumiwa kama nchi ya kupitishia wahanga wa usafirishaji na biashara haramu ya watu toka nchi za pembe ya Afrika(Ethiopia, Somalia) wanaopelekwa Afrika kusini: Kuna wimbi la wahamiaji haramu wanaoingia
Tanzania ambao serikali ya Tanzania inahisi miongoni mwao wapo wahanga wa usafirishaji na biashara haramu ya watu. Kuna ushahidi wa matukio ambayo yanaonyesha kuna wahanga wa usafirishaji na biashara haramu kutoka India na Pakistan kuletwa Tanzania.

Watoto wahanga wa usafirishaji na biashara haramu ya watu waliosaidiwa na Shirika la Kimataifa la Uhamiaji/International Organization for Migration (IOM) wengi wao hutokea sana mikoa ya Iringa, Morogoro, Mbeya, Mwanza Singida na Dodoma. Zipo dalili kubwa kwamba Dar es Salaam na Zanzibar ndio vituo vikubwa wanaopelekwa wahanga hao. Watoto hao kawaida hutolewa vijijini kwa kuahidiwa maisha bora na elimu mjini na ndugu zao wa karibu au watu wanaoaminiwa na wazazi wao. Wakati mwingine watoto hawa hutolewa na wazazi wao kwa ndugu kwa mategemeo watoto wao watapata maisha bora wakiwa mjini.
Lakini wakati mwingine hali huwa sio kama walivyotegemea. Unyonyaji ni pamoja na kumlazimisha muhanga kufanya ukahaba, kazi za ndani, biashara za mitaani, kuosha magari bila kupewa nafasi ya elimu na matibabu, bila chakula au chakula kidogo sana, kunyanyaswa kijinsia, kutukanwa, kupigwa, kutishwa na kufanyishwa kazi bila ya ujira. Wengi wa watoto hawa wakifanikiwa kutoroka, huishia mitaani.

Sababu

Elimu ni moja ya sababu kubwa. Upatikanaji mkubwa wa elimu mjini huvutia vijana wa kike na kiume kutoka vijijini, wahanga wengi waliosaidiwa na IOM ni watoto walioacha shule au hawajawahi kwenda shule kabisa kijijini mwao (watoto wa kike 24 kati ya 34 waliosaidiwa mwaka 2007 hawakuwahi kwenda shule kabisa).
Kupoteza wazazi wote wawili. Hali hii husababisha watoto kulazimika kutegemea walezi.

Tuesday, October 28, 2008

JE? HUU NI UUNGWANA KUWADANGANYA WATU HIVI?

Sofia Mhagama mwenye umri wa miaka 16 ameenda Dar es Salaam na Shangazi yake Emilia Soko kutoka katika kijiji cha Mpandangindo mkoani Ruvuma. Sofia ni mtoto watatu kuzaliwa katika familia ya watoto saba. Wazazi wa Sofia hawana kipato cha kutosha kuhudumia familia nzima. Baba yake Sofia, mzee Mhagama ni mzee mashuhuri sana kijijini Mpandangindo. Shangazi yake Sofia aitwaye Emilia Soko alihamia Dar es Salaam kutoka Mpandangindo miaka ya themanini mwanzoni. Tangu Shangazi Emilia alipohamia mjini amekuwa akitembelea kijijini kwao Mpandangindo mara kwa mara. Kila wakati shangazi Emilia alipokuwa anakuja kijijini kuleta zawadi nyingi kutoka mjini pamoja na vitu vingi vya kisasa ambavyo ni shida sana kupatikana kijijini. Kila mtu kijijini aliona kuwa maisha ya Shangazi Emilia yamebadilika sana toka ahamie mjini na kuwa bora zaidi kutokana na vitu na misaada aliyokuwa anawapa wazazi wake kijijini.

Baada ya miaka Shangazi Emilia alitembelea tena kijijini kwao Mpandangindo kwa ajili ya kusherekea sikukuu ya krismas pamoja na wazazi kama ilivyo kawaida yake alikwenda pia kuwatembalea familia ya mzee Mhagama, baba yake Sofia. Shangazi Emilia alimwelezea mzee Mhagama masikitiko yake juu ya hali ngumu ya maisha ambayo inamkabili mzee Mhagama na familia yake. Emilia alimwambia kaka yake kwamba angependa kujitolea kumsaidia mtoto mmoja wa kike, Sofia. Mama yake Sofia hakuelewa kwa nini Emilia amemchagua Sofia wakati kulikuwa na wadogo zake ambao wangefaidika kielimu maana Sofia alikuwa anasaidia kazi za pale nyumbani. Sofia alikuwa anatambulika sana kwa kipaji cha kuimba kijijini pale. Mama Sofia alihisi kuwa hiyo inaweza kuwa ndio sababu kubwa Emilia kumchagua mwanae Sofia. Mzee Mhagama hupenda sana kumsifia binti yake kwa marafiki zake wakati akiwa anakunywa ulanzi, hupenda kusema "mtoto wangu Sofia ana sauti nyororo ya kumtoa nyoka pangoni". Wazazi wa Sofia walikubali kwa shingo upande kumtoa binti yao Sofia maana walikuwa wanampenda sana binti yao.
Sofia kwa sasa anaishi nashangazi yake mjini Dar es Salaam. Shangazi yake aliwaahidi wazazi wa Sofia kwamba akifika mjini, Sofia atapata kazi inayomlipa vizuri na nafasi ya kwenda shule. Kwa bahati nzuri kuna ndugu wengine wa Sofia wanaoishi Dar, kwa hiyo Sofia alijua kuna watu wa kuwategemea wakati wa shida akifika Dar, Sofia hakujua jinsi jiji la Dar lilivyo kuwa ya kwamba ni vigumu kutembea mwenyewe na hata kwenda kuwatafuta ndugu zake ambao wako Dar. Shangazi yake Sofia, naye alivunja ahadi yake: Sofia hakuruhusiwa kwenda shule na amefanywa kuwa mtumishi wa ndani kwa shangazi yake bila malipo. Sofia anafanyishwa kazi masaa mengi na kama akikataa hupigwa na kutishiwa kufukuzwa nyumbani kwa shangazi yake na kuachwa mitaani. Sofia anatamani sana kurudi kwao Mpandangindo kwa familia yake na pia kwenda shule, lakini hawezi.

Swali je? hii ni haki kufanya hivyo?