Friday, December 31, 2010

SALAMU ZA MWAKA MPYA KUTOKA KWA MAMA MAISHA NA MAFANIKIO NA FAMILIA YAKE

mwaka mpya 2010
Nasubiri mwaka 2011!!!
Marafiki wapendwa!
Ukaribisheni mwaka mpya uwe wa Mafanikio, Amani, Mwanga na Furaha katika maisha yetu.
Nakutakieni wote, wewe na familia yako kila jema na furaha tele katka mwaka mpya 2011.
KHERI KWA MWAKA MPYA 2011. KUMBUKENI WOTE MNAPENDWA!!!!
Nimena si mbaya kama tukiuvuka mwaka huu kwa kipande hiki cha mziki si mnajua mziki na kazi au mziki,sherehe aaahh ngoja tuserebuke!!

Thursday, December 30, 2010

"MJADALA ULIOVUNJA REKODI KATIKA BLOG YA MAISHA NA MAFANIKIO MWAKA 2010"

Ndugu wasomaji wa blog hii ya MAISHA NA MAFANIKIO, katika kupitia mada mbalimbali nilizowahi kuweka humu ili kupata ile ambayo ilivuta hisia za wasomaji wengi na kuleta changamoto, nimevutiwa na mada hii ambayo ilileta vuta ni kuvute miongoni mwa wadau wa blog hii.
Kwa hiyo basi nimeichagua mada hii kuwa ndio mada iliyovunja rekodi kwa mwaka 2010.
Natoa shukrani kwa wadau wote mlioshiriki katika kuichangia mada hii.
Naomba muungane nami katika kujikumbusha kile kilichotokea katika mjadala huu.
Hospitali ya Ludewa/ Mambo ndio haya!!


Akina mama ambao wanawauguza ndugu zao katika hosptali ya Wilaya ya Ludewe wakisonga Ugali nje ya wodi ya akina mama wanaosubiri kujifungua, kati ya akina mama 100,000.wajawaito 200 hupoteza maisha katika Wilaya hiyo kutokana na ukosekanaji wa miundombinu.
Wanawake wajawazito toka katika vijiji 76 vinavyo zunguka Wilaya ya Ludewa wakiwa wamelala na wengine wakila chakula huku wakiwa wamesubilia siku zao za kujifungua katika hospitali ya Wilaya ya Ludewa Mkoa wa Iringa kati ya akina mama 100,000 wajawazito 200 hufariki kutokana na ukosefu wa huduma

Inasikitisha: Baadhi ya akina mama wajawazito wakiwa nje ya wodi ya wazazi katika hospitali ya Wilaya ya Ludewa ambapo jengo hilo lina vitanda 6 na kila kitanda hutumiwa na akina mama wajawazito wawili. Wengine hulazimika kulala chini. (picha na Albart Jackson).
Na: Yasinta Ngonyani kl. 1:14 AM

NA HAYA YALIKUWA NI MAONI YA WADAU...........

Koero Mkundi said...
Bora umeona na wewe Yasinta maan ningeona mie ninganangwa kweli na wahafidhina....
haya sijui na wewe utaitwa Femisist, kama mie...
Nakusikitikia kwa kuingia katika vita hii, jiandae kushambuliwa dada.....
April 8, 2010 7:20 AM

Yasinta Ngonyani said...
Koero mdogo wangu!Wala siogopi kabisa waiti watavyo na wanishambulie watavyo kwani atayefanya hivyo basi hajui utu na bado hajajua wanawake wana mateso gani na sio haki kupata mateso kama hayo. Tuna haki na tunatakiwa kupata.
April 8, 2010 7:40 AM

Anonymous said...
siku zotw huwa nanyata katika uwanja wako lakini leo nitacomment,huku ni ludewa kwetu na hii ilibiniwa kutokana na wananchi wanaoishi mjini ludewa kuwa na wageni mpaka 3 kwa mara moja (rejea extended family theory ya kiafrika) wakisubiri kujifungua hivyo ukabuniwa mradi huu wa kuwa na jengo lao.angalau sasa wanapumua...pia jengo hili lilitaifishwa toka kwa mjasiliamali mzalendo enzi za mwalimu......wageni wa hapa wengi ni wakisi,wamatumba,wamanda wapangwa ni wachache kwani huhudumiwa na lugarawa mission hospital

April 8, 2010 8:21 AM

Mija Shija Sayi said...
Mimi huwa nasema serikali inatakiwa ipinduliwe maana haifanyi kazi zake ipasavyo, sasa mwakilishi wa jimbo hili sijui ni nani ambaye anashindwa hata kupeleka ripoti serikalini kwa hospitali Ludewa hazina huduma nzuri.
Yasinta ukipata na picha za wodi za wanaume na watoto pia tuletee tuone nao wako katika hali gani.
April 8, 2010 9:19 AM

Baraka Chibiriti said...
Kwakweli maisha yetu yanasikitisha sana tena sanaaaa....basi tuu Mungu anatusaidia sana kutulinda kuendelea kwenda mbele na maisha haya ya tabu. Poleni sana akina mama jamani.
April 8, 2010 10:02 AM

John Mwaipopo said...
namnukuu mija shija sayi "Yasinta ukipata na picha za wodi za wanaume na watoto pia tuletee tuone nao wako katika hali gani."
nadhani za wanaume zitakuwa nzuri tu.
April 8, 2010 10:10 AM

Anonymous said...
kiukweli hii ni waiting home ya akina mama wanaosubiri siku zao zotomie,sio ward,kiuhalisia ward yao na inatosheleza mahitaji.na hii nyumba iko nje ya mazingira ya hosp yenyewe.si kweli kuwa kuna huduma mbovu za wazazi .............wa mkondachi
April 8, 2010 10:54 AM

Koero Mkundi said...
Ngoja ninukuu annony wa hapa.
"kiukweli hii ni waiting home ya akina mama wanaosubiri siku zao zotomie,sio ward,kiuhalisia ward yao na inatosheleza mahitaji.na hii nyumba iko nje ya mazingira ya hosp yenyewe.si kweli kuwa kuna huduma mbovu za wazazi .............wa mkondachi"
Mwisho wa kunukuu.
Kama hiyo kweli ni waiting home, ina maana kuwa hakuna vituo vya afya katika vijiji hivyo tajwa mpaka watu wakimbilie katika kituo hicho cha Afya cha Ludewa ambapo inabidi walundikwe kwenye hizo nyumba za kusubiri kujifungua.
kwa hiyo hata huyo mbunge wao hayajui madhila ya watu wake maana kama angeyajua basi wanawake hao tunaowaona hapo wangeshaondolewa tatizo hilo.
Ikumbukwe kamba walioshinda kwa ushindi wa kishindo walituahidi maisha bora kwa kila mtanzania na ujenzi wa zahanati kwa kila kata. sasa miaka mitano ndio hiyo inaishia........Je watakuja na msamiati gani?
Mimi nadhani kuna haja ya wananchi kuambiwa ukweli kuwa CCM imechoka na sasa ikae pembeni ili watu wenye utambuzi na uwezo wa kuongoza washike hatamu......hakuna haja ya kuimba CCM nambari wani kila baada ya miaka mitano wakati hata hawapo kwenye 100 bora.
Kwanza takwimu zinaonyesha kuwa kuna idadi kubwa ya vijana hapa nchini ukilinganisha na wazee.....nadhani tunatosha kabisa kuondoa huu unafiki, watu mpaka meno yanang'oka kwa uzee lakini wamo tu kwenye siasa.....

nasema wameshindwa waondoke.....
nakubali kuwa wazee wanao mchango wao kwa taifa lakini kama hawazalishi idea za kulikwamua taifa hili kuondokana na tabia ya kuombaomba, lakini wameshindwa, basi wapumzike na tunawaahidi kuwalea na kuwatunza mpaka mungu atakapowachukua mbele ya haki ambapo huko watajua kile walichopanda tangu kuwepo kwao hapa duniani.
Narudia ena waondoke hawatufai.....
April 8, 2010 1:05 PM

Anonymous said...
Nikubali kutoka kwa koero kuwa huduma za uzazi katika vijiji si njema ndio maana akina mama hawa huja katika hospitali ya wilaya kwa huduma mapema zaidi na hutakiwa kusubiri katika nyumba hii.wanashauriwa kuja mapema ili kuepuka any complication ambayo inaweza kujitokeza ilikupata huduma mara uchungu unapoanza.viji vyenye angalau ya huduma ni manda,luilo,madunda,mlangali,makonde na lupingu kidooogo,but still vituom hivi si vya kutegemea sana kwani huduma thabiti pekee ni hapa ludewa na lugarawa mission hosp pekee.Koero pia hii ni wilaya katyi ya chache zinazowakilishwa na wabunge maprofesa,hapa yupo mh.Prof Raphael Mwalyosi.hao wasomi wataalamu wa afy ahawaja motishwa kwani huku ni moja ya wilaya ni tata kimazingira.......wa mkondachi
April 8, 2010 2:40 PM

Ramson said...
Name Raphael Mwalyosi
Surname Mwalyosi
First Names Raphael Benedict
Alternate Name
Title Prof
Country of Birth Tanzania

Positions
From To Organisation Position
2005 Ludewa Constituency
MP for Ludewa
Date of Birth 3 Dec 1946
Political Affiliation CCM

eMail
Telephone
Address
Notes EDUCATION
School Name/Location Course/Degree/Award Start Date End Date Level
University of Agriculture, Norway PhD 1988 1990 PHD
University of Dar es Salaam MSc. 1975 1979 MASTERS DEGREE
University of Dar es Salaam BSc. 1971 1974 GRADUATE
Tabora Boys' Secondary School A-Level Education 1969 1970 HIGH SCHOOL
Tabora Boys' Secondary School O-Level Education 1965 1968 SECONDARY
Madunda Middle School Primary Education 1961 1964 PRIMARY
Lufumbu Primary School Primary Education 1957 1960 PRIMARY
--------------------------------------------------------------------------------
CERTIFICATIONS
Certification Name or Type Certification No. Issued Expires
No items on list
--------------------------------------------------------------------------------
EMPLOYMENT HISTORY
Company Name Position From Date To Date
University of Dar es Salaam/IRA Professor 1999 2005
University of Dar es Salaam/IRA Associate Professor 1993 1999
University of Dar es Salaam/IRA Senior Reseacher 1988 1993
University of Dar es Salaam/IRA Reseacher 1984 1988
Rufiji Basin Development Authority Ecologist 1979 1984
Tanzania National Parks Reseacher 1974 1979
--------------------------------------------------------------------------------
[ Retrieved on 13/7/2006 - www.parliament.go.tz ]
April 8, 2010 3:04 PM

Anonymous said...
Namshukuru ramso kwa kupachika cv ya mheshimiwa wetu,na kama ujuavyo wataalamu wa mazingira ni wakereketwa wa nature zaidi kuliko vitu vingine kwani alishawahi endesha IRA pale UDSM IRA ni Institute of Resourcr assesment.Lakini kipimo cha picha hii tu kitatutosha kujudge au tukusanye takwimu zaidi lakini hata hali ya shle si njema sana na barabara hata uchumi pia au siju tumpate injiania aongeze na kasi ya uchimbaji wa makaa yetu ya mawe na chuma cha pua kule liganga,nina hamu nishuudie maana tangu nazaliwa niu habari ya upembuzi yakinifu mara mtalamu mshauri maka leo...daa twachoka......wa mkondachi
April 8, 2010 3:42 PM

Mbele said...
Hii makala imenigusa kiasi cha kuiweka kwenye blogu yangu, pamoja na utangulizi ambamo nimegawa vidonge kwa wahusika. Bofya hapa.
April 8, 2010 4:23 PM

PASSION4FASHION.TZ said...
Maisha bora kwa kila mtanzania.....?kweli? au watanzania ni wadanganyika kama watoto wadogo,wanaoambiwa usilie nikirudi nitakuletea pipi,mtoto ananyamaza na anakuwa na hope kuwa mama akirudi ataniletea pipi.
Jamani carne hii watu bado wanaishi maisha kama haya kweli? kinachosikitisha zaidi wanawake ndio wapiga kura wazuri wa kuichagua CHUKUA CHAKO MAPEMA(CCM) wanawake tuamkeni CCM haina shukurani wala fadhila, hawa wanawake wanahitaji msaada wa kuelimishwa,nahisi bado kuna watu wanamawazo finyu kuwa bila CCM haitakuwa Tanzania,kwa hali kama hii basi hayo maisha bora kwa kila mtazania zitabaki kuwa ndoto za alinacha!
April 8, 2010 4:52 PM

kamala Lutatinisibwa Lutabasibwa said...
kwani nyie si mko mijini?? mbona mimi nimebanana vijijini natoa hudma kwa wana vijiji. sasa nuoe kama wasomi na wabunge mko mijini mnalilia lia tu. anayeona huruma akawe diwani
lakini kwa wanawake ni kawaida kwani ndio wapiga kura wakuu
April 8, 2010 4:53 PM

Anonymous said...
Yasinta asante sana kwa kutujulisha yote haya mungu akuzidishie akupe afya njema wewe na familia yako. Ubarikiwe sana.Unapatwa na uchungu unalia unashindwa kujua ufanye nini? Mimi natokea Ludewa. Huu ni ujumbe ambao mkuu wa nchi ulitakiwa umfikie halafu ajitetee. Nafahamu si Ludewa peke yake lakini ni wilaya na vijiji vingi vina mapungufu haya. Huu ni upuuzi wa serikali yetu halafu tunawachagua viongozi wale wale wenye kujaza matumbo yao na kuwasahau wananchi. My take fukuza kazi watu wote husika kuanzia wizarani mpaka tukafike Ludewa kwenyewe huu ni upuuzi. Wanaludewa tufanyeje kukabiliana na hili? Kama tunaweza kufanya kitu basi wajameni tuwasiliane.Kukaa mbali na nyumbani hakuna maana tutashindwa kuleta msaada
April 8, 2010 5:21 PM

Yasinta Ngonyani said...Anony wa April 8, 2010 5:21 PM! Asante unajua ni kweli nimelia sana kutokana na jambo hili. Nimeshuhudia jambo hili kwa macho yangu wakati naishi Kijiji cha Kingoli kulikuwa na zahanati, lakini hakuna sehemu ya akina mama wajawazito kujifungulia na akina mama wengi walikuwa wana kufa. Hoospitali ya karibu ilikuwa ni Peramiho na kufika huko usafiri wake ulikuwa ni kutembea na mgonjwa/mamamjamzito amebebwa katika machela. Kufika Peramiho inachukua siku mbil. Je huu kweli uungwana?
April 8, 2010 5:44 PM

Anonymous said...
Hii picha imenisikitisha sana. Kwa hakika najua hiyo sio wodi ya hao akina mama wajawazito kama alivyosema mchangiaji mmmoja. Nafahamu utaratibu uliopo kule maeneo ya kwetu, ni kwamba akina mama wajawazito huwa wanapangiwa tarehe za kusogea jirani na hospitali ili kujitazamania kusudi siku ya kujifungua isiwe shida kufika hospital na kupata huduma inayostahili. Nafahamu hivyo kwa vile binafsi natoka jirani na hospitali kubwa na ya uhakika ya misheni Peramiho (kuna mpango wa kuifanya hospitali ya rufaa). Na katika utaratibu wa hiyo hospitali ni kwamba hata kama unatoka km kadhaa toka hospital ni lazima uende kujitazamia hapo hospital na tarehe za kwenda hapo wanakupangia wao wenyewe. Pale kwetu usafiri wa kufika Peramiho ni masaa 24 lakini hiyo hospital ni wakali sana, lazima uende kabla. Ukiuliza wanakupata vipi mpaka wakuamuru kwenda hapo mapema ni kwamba kama mjamzito anahudhuria clinic basi hapo ndio wanapokupata na kukuingiza katika utaratibu huo. Sasa hoja ninayotaka kusema hapa ni kwamba huu ni mpango mzuri sana hasa kwa maeneo ambayo huduma za hospital zipo mbali. Lakini sasa inabidi kuyafanya hayo mazingira yawe mazuri, yavutie na akina mama wakiwa hapo wawe na amani na sio kuwaweka katika mazingira kama hayo ya kwenye picha.
Inasikitisha sana kwa kweli hizo picha.
April 8, 2010 9:40 PM

Yasinta Ngonyani said...
ninenukuu toka kwa Hapa kwetu yaani Pro.Mbele kwa vile nimeyapenda haya maelezo yake! "Inasikitisha kuwa katika nchi yetu, yenye mali nyingi, hali ya watu katika vijiji vingi na mijini ni mbaya kiasi hiki.
Wenye madaraka wanafuja utajiri wa Tanzania. Kwa mfano, hivi karibuni tu, CCM imeagiza magari 200 kwa ajili ya kampeni za uchaguzi. Fedha hizi zingeweza kutumiwa kuboreshea huduma za afya kwenye hospitali kama hii ya Ludewa, au kuwapa mitaji hao akina mama, wakabadilisha maisha yao.
Wako ambao wanachuma mishahara na marupurupu kwa mamilioni ya shilingi. Wako ambao wanatumia mamilioni kwenye sherehe na starehe. Wengine wamechota na labda bado wanachota, mamilioni ya shilingi na kuyahamishia nje, kwenye akaunti binafsi. Badala ya kutumia hela kuboresha huduma za afya sehemu kama hii ya Ludewa, Tanzania imetumia mabilioni ya shilingi, tangu miaka ya mwanzo ya Uhuru, kwa kuwapeleka wachache nje, kwa matibabu au hata tu kuchekiwa afya, mambo ambayo yangeweza kufanywa katika hospitali za nchini, kama vile Muhimbili. Ninafahamu jinsi gharama ya matibabu ilivyo mbaya katika nchi kama Marekani. Fedha zilizotumika miaka yote hii zingekuwa zimeboresha huduma katika hospitali sehemu mbali mbali za nchi." Mwisho wa kunukuu. Ni kweli inaumiza na kusikitisha shana na ningependa hii serikali ipinduliwe kabisa! Upendo Daima.
April 9, 2010 12:44 AM

Mija Shija Sayi said...
Yasinta, swali muhimu linakuja sasa wa kuipindua ni nani katika jamii yetu hii iliyofunzwa nidhamu ya WOGA?
April 9, 2010 1:18 AM

Yasinta Ngonyani said...
Da Mija ni sisi vijana wa leo au? ni lazima kuna mmoja asiye mwoga.
April 9, 2010 3:19 PM

Albert Paul said...
"Tanzania na Watanzania tuna amani" hii ndio hirizi iliyofungwa kwenye vichwa vyetu imiminayo nidhamu ya "WOGA" kwenye akili zetu. Mawazo haya "POTOFU" tumeyakumbatia kiasi kwamba yanatufanya tunashindwa kutetea haki zetu ipasavyo na kukosa umoja miongoni mwetu.
April 9, 2010 7:53 PM

penina Simon said...
Ha ha ha maybe yatasaidia jamani,manake mimi kwa uzoefu wangu sidhani kama mimba ni ugonjwa, ila hufuata unavyojiendekeza,
Mfano inaweza kukufanya uteme mate kila wkt na ukiendekeza utajikuta unatembea hadi na kikopo. Au kukuletea uchovu na ukiiendekeza basi utaamuka sa4,5..
etc.
April 10, 2010 3:23 PM

samuel blandes said...
Inasikitisha,Kliniki au hospitali kama hizo ziko nyingi nchini.Serikali isikimbilie kuongeza idadi ya majimbo ya uchaguzi au idadi ya wilaya ni matumizi mabaya.Gharama za kujenga kliniki 20 na kuziendesha vizuri ni nafuu kuliko gharama za kuongeza jimbo mmoja la uchaguzi.Kupanga ni kuchagua.
Rwegasira
Singapore
April 11, 2010 8:29 AM

Chacha o'Wambura a.k.a Ng'wanambiti! said...
Enzi za Prof Mwalyosi pale IRA mambo yalibadilika yakaifaya IRA ikatoka kuwa Institute of Resource Assessment ikawa Institute of Resource Assassination kwani Environmental Impact assessments za ajabu ajabu zilikuwa na bado zinafanywa na watu wa taasisi hiyo. Utaona miradi mikubwa ambayo utategemea kuwa haitopitishwa lakini waapi!!!
Hayo yanayotokea Ludewa yako kila pahala na ukistaajabu ya hospitali za wilaya utakuta kuwa hata hospitali za mikoa kama Mara utayakuta :-(
April 12, 2010 8:19 AM

nkwera said...
Yasinta
Hii picha umepewa au umepiga mwenyewe?
Mimi ninaishi mita chache kutoka kwenye nyumba hizo.
1. Hiyo siyo wodi ya akina mama, wodi ya akina mama wajawazito Ludewa ina vitanda zaidi ya 6o
2. Nyumba hiyo ipo ukingoni mwa eneo la hospitali na hutumiwa na wote wenye wagonjwa hapo hospitali lakini hawana pa kufikia. Bionafsi naona ni jambo jema hata nyumba si nzuri
3. Akina mama wanaosubiri kujifungua au wenye magonjwa hatarishi walishajengewa na vosacom foundation jengo zuri tu, ungeweza kuomba picha zake au kupiga mwenyewe:-) Habari zake zinapatikana hapa http://www.jambonetwork.com/blog/?p=59059
Hali ni mbaya vijijini lakini picha ulizotumia si sahihi na sielewi ulikuwa na nia gani kutumia picha hizo. Bottom line, those are not wards and probably you know it!
pdn
April 13, 2010 8:27 PM

Yasinta Ngonyani said...
Kaka nkwera ahsante kwa taarifa na hiyo link nitapita kuangalia.
April 13, 2010 10:51 PM

Simon. said...
poleni sana ndugu zetu watanzania wa huko ludewa na maeneo ya jirani na hapo ambao mnategemea matibabu kutoka katika hiyo hospitali. lakini sio ninyi tu huko hata sehemu mbali mbali za hii nchi wote wanateseka sana hasa linapokuja suala la hospitali na huduma za kina mama wajawazito nchini..hii ni kutokana na usimamizi wa serikali yetu kuwa ni wa kubabaisha!NADHANI NI WAKATI MUAFAKA SASA KWA SERIKALI KUWA SERIOUS KATIKA KUTATUA MATATIZO SUGU YANAYOWASUMBUA WALIPA KODI WA NCHI HII!!! tumeshachoka na sanaa zao!
April 15, 2010 5:36 PM

Anonymous said...
dada yasinta nipo mbioni kutangaza nia ya kushirikiana na wananchi kuondoa kero hizi sasa hakuna haja mpaka kusubiri "KUOMBWA NA WAZEE"wenye nia ya dhati trujitokeze si ubunge tu hata udiwani uongozi wa vijiji na mitaa unahitaji watu makini na wenye upeo wa kuondoa kero na si kuiongeza kero kama hizi.IWE NI WODI ISIWE NI WODI IREKEBISHWE HUDUMA ZA HAPA HAZIKIDHI VIWANGO VYA AFYA.Tuzindukesasa na tusababishe hali njema
April 20, 2010 10:56 AM


Tuesday, December 28, 2010

SALAMU/BARUA KUTOKA BLOG YA MAISHA NA MAFANIKIO:- SHUKRANI KWA WOTE!!!

Habari zenu jamani!!
Zimebakia siku chache tu kuumaliza mwaka huu 2010 na kuingia katika mwaka mpya 2011. Hakika miaka inayoyoma na watu tunazidi kuzeeka. Ninachotaka kusema ni kwamba, blog ya MAISHA NA MAFANIKIO inapenda kuwashukuru wanablog wenzake wote, wasomaji wote na watembeleaji wote kwa ushirikiano mzuri tulioonyeshana.

Najua katika maisha watu wote hawawezi kuwa sawa yaani kimawazo. Lakini katika hizi blog zetu kwa asilimia kubwa imekuwa ni changamoto kwetu. Tumekuwa hatupendi kupoteana, mara mmoja wetu anapokuwa kimya kwa muda basi wengine tunakuwa hatuna raha tunachukua hatua ya kumtafuta. Hii yote inaonyesha ni jinsi gani ukaribu wa wanaBLOG sisi tu/ulivyo, hakika najivuna sana kwa uwepo wenu na kwa hili napenda kusema SISI SOTE NI NDUGU. NA PIA NAPENDA KUWATAKIENI WOTE KILA DOGO NA PIA KILA KUBWA MTENDALO LIWE JEMA. NA MWAKA 2011 UWE WENYE MAFANIKIO. KAMA KUNA KITU ULIAHIDI KUFANYA MWAKA HUU BASI JITAHIDI UFANYA KABLA HAUJAISHA. KWANI KUMBUKA HAKUNA KISICHOWEZEKANA. PAMOJA DAIMA. KAPULYA WENU!!!!

Monday, December 27, 2010

MUDA UNAPITA,LAKINI.....

‘Bwana wewe nikuambie siri moja ya maisha,…’Mzee mmoja alikuwa kaka karibu nami kwenye daladala kaniambia, tulikuwa tumekaa wote kwenye daladala na muda huo nilikuwa nimechoka, sikupenda kusumbuliwa, hamu yangu ilikuwa kupata usingizi kidogo, kwasababu najua nina zaidi ya masaa mawili ndani ya daladala hadi kufika kwangu, siunajua tena foleni.


Nikamwangalia yule mzee, alikuwa kaniangalia kuonyesha kuwa ana jambo muhimu nikaona nimsikilize na kumwambia , `Niambie mzee, huenda likanisaidia katika maisha yangu…’

‘Katika mipangilioa yako ya maisha , fanya juhudi pangilia mambo yako, fanya kazi kwa bidii na ipende dunia kama vile utaishi milele..siunaniona mimi hapa nimezeeka nina miaka sitini, lakini najihisi kama nina miaka mingine sitini mbele, sijipweteki, na kusema aah, mimi mzee basi tena, nasubiri cha kupewa, nani atakupa hivihivi dunia hii. Najitosa hivyohivyo kama vile nitaishi milele, ingawaje kwa kweli naukumbuka sana, na kuujutia ujana wangu…’ akaniangalia kwa macho makali. Akaongezea kusema `wakati ni mali, lakini wakati ni ukuta, unahitaji mipangilio…’ akatikisa kichwa na kuendelea kusema;

`Pili muabudu sana mungu wako kama vile utakufa leo, au hata sasa hivi, huwezi jua, hapa gari linaweza likadondoka, tukawa wote marehemu au nikafa mimi peke yangu, au hata bila kudondoka gari unaweza ukakauka ghafla, na ukafa. Sasa ni bora umwabudu aliye na mamlaka na hiyo roho yako kwasababu hujui muda gani ataichukua roho hiyo. Omba, muabudu mola wako kama vile hapo unapoomba ni sekunde au dakika yako ya mwisho…’ akainama chini na nilijua anamuomba mola wake!

Nilijiukuta nimelala na nilipoamuka yule mzee akawa hayupo, ina maana aliteremka kituo nyuma wakati mimi nimelala, nilijuta sana, kwani alionekana ana busara na mengi yakunieleza, lakini nimechelewa keshaondoka.

Mzee huyu namfananisha na mwaka huu, unayoyoma, ni muda mchache umebakia tutauita jina jingine, mwaka jana au sio , na tutaukaribisha mwaka mpya. Mwaka huu tulikuwa nao na tulikuwa na mengi ya kufanya, na sijui mangapi tulifanikiwa kuyafanya na mangapi hatukufanikiwa, sidhani wengi wetu tuna kawaida ya kuweka kumbukumbu hizo, sidhani. Kumbukumbu hizo tunaziona kwenye bajeti za serikali, bajetiza makazini, lakini sio bajeti ya mtu mmoja mmoja.

Mwaka huu tupo nao kwenye kiti una mengi ya kutuambia, lakini tunajifanya tumechoka, tunajifanya tupo busy…labda tungelitulia tukatafakari na kuwa nao bega kwa bega k wa mipango, huenda tungelifanikiw sana. Tumekuwa tukikimbizana na hili na lile na huenda hayo tunayokimbizana nayo haya maana, tunapoteza muda mwingi kwenye vilevi, kucheza bao, kuongea na kufanya mambo ambayo ukiangalia ni ya kupotezea muda, muda uishe ulale, siku ipite. Ndio siku inapita, umri unakwisha na mwaka huo unakwisha, tukiamuka tutaukuta haupo tena!

Tukiangalia katika maisha yapo mambo mengi yanaharibu miili yetu hasa vyakula, vinywaji, vipodozi, hasira zisizo na msingi na mambo kadha wa kadha ambayo unayaona mazuri kwa umri wa miaka hadi telathini ujanani yaani, lakini ukifikia zaidi ya umri huo, hayo hayo uliyokuwa ukiyaona mazuri yanageuka kuwa sumu mwilini mwako. Mfano vyakula vya mafuta, pombe, starehe , madawa, vipodozi na mambo anuai, ni mazuri, yanastarehesha katika umri wa ujanani, lakini ikifikia uzeeni hayo matamu yanageuka kuwa machungu, yanakuwa sumu. Tunajikuta tunaamndamwa na presha, kisukari, ugonjwa wa moyo, vidonda vya tumbo nk, kwasababu ya yale matamu tuliyokuwa tukiyafadi ujanani. Kosa hatukua na mipangilio, hatukuali kusoma na kujifunza uzuri na ubaya wa hilo unalilofanya au kula!

Sasa wakati umefika kabla mwaka haujaisha kaa na huu mwaka kabla haujaisha, kumbuka yale ya muhimu, panga matarajio ukiwa na malengo kuwa utaishi milele. Na mipango hiyo haiwezi kuja kichwani tu, chukua karatasi pata muda, hata ikibidi soma, tafuta , uliza, kaa na mkeo au mumeo, angalieni matarajio, majukumu na mambo mbali mbali ya kimaisha yapangeni vyema na jinsi gani ya kuyatatua matatizo, jinsi gani ya kupata kipato, jinsi gani ya kusaidiana na hata kama huna kitu lakini kwa kujua nini kifanyike na kipi cha muhimu kwanza inasaidia, kuliko kulala, au kunywa pombe, au kusubiri mwisho wa siku ukaanza kupiga mayowe , kurusha mawe kwenye mabati eti unashagilia mwaka umekwisha, lakini umekwishaje? Ulikuwa nawo kweli wewe au ulikuwa umelala…!

Mkumbuke mola wako, kwani imani ni kitu muhimu sana, mola wako ndiye mwenye mamlaka na mwili wako, wangapi ulikuwa nawo siku za karibuni au mwaka huu sasa hawapo, je ina maana wao walikuwa na makosa na wewe uliyebakia huna makosa. Kumbuka wangapi wapo mahospitalini wagonjwa, wengine hawana viungo, wengine wanaomba mola awachukue kwa mateso wanayopata ya kansa au mengineyo, je wao walikuwa wanjua haya, je wao walimkosea Mungu ndio maana wanapata mateso haya, na wewe ni mbora zaidi yao ndio maana leo upo mzima. Hapana, wao hawajakosa, na wala wewe sio mbora sana mbora zaidi ni yule mcha mungu, ni yule anayemuomba mungu kuwa sala yangu hii huenda ikawa ya mwisho kuwa mzima, kuwa hai…nahivyo Sali kama vile hutaiona sekunde inayofuata.

Ujumbe huu nimetumiwa na msomaji wa Maisha na Mafanikio aishiye Arusha. Binafsi umenigusa sana nimeona nisiwe mchoyo niwajumuishe na wenzangu.

Saturday, December 25, 2010

NA NOELI ILIVYOKUWA LEO HAPA KWETU........


maandalizi kwa ajili ya mapishi ya pilau, mchele,viungo vya pilau, viazi mviringo, vitunguu maji na saumu, mafuta, chumvi, nyanya ,limau na nyama ya kuku badala ya ngómbe.




Hapa ni vitunguu na viungo



Mchele umetumbukia pia viazi.




Mpishi yupo katikati ya mapishi!!







Na hapa tunaona matokeo yake
Kachumbali

Hapa ni sahani yangu mmmhhh utamu.....
Edna karibu maana ulilalam ika jana kuwa hakuna halufu ya pilau na pia wengine wote mnakaribishwa kuna chakula kingiiiiiii pia vinywaji. Puh! kuwa mpishi ni kazi kwelikweli!!!
NAWATAKIENI WOTE NOELI NJEMA SANA!!!!


BWANA YESU AMEZALIWA LEO HORINI TWENDE TUKAMWONE NA ROZI MHANDO!!!



Leo ni jumamosi pia ni siku aliyozaliwa bwana wetu Yesu Kristu hasa kwa wakatoliki leo ndio sherehe kubwa. HAYA CHRISTMAS NJEMA WOOOOOOOOOOOOTE KWA MARA NYINGINE TENA NA MWISHO MWEMA WA JUMA!!! TUTAONANA TENA WAKATI MWINGINE!!!

Friday, December 24, 2010

SALAMU ZA CHRISTMAS KUTOKA SWEDEN!!!

Katika familia yetu mimi siwezi kuwa karibu na mti wa Chritsmas. Bahati nzuri tuna hili ua kubwa kama mti ndani ya nyumba kwa hiyo tukaona tuupambe ili uwe mti wa Christmas na hapa unaona jinsi zawadi zilivyojaa najiuliza kama nimekuwa mtoto mzuri kustahili kupata zawadi leo ...Nitawajuza



Na hapa ndipo tutakapo kaa na kula mlo wetu wa christmas pamoja karibuni jjamani tujumuike!!

Na hapa ndio maakuli yenyewe kwa kutumia mikono yetu wenyewe. Ila pilau halikuwepo, labda kesho.

Na hapa sherehe imeanza , kama upo karibu unakaribishwa sana. Skål och GOD JUL ALLIHOPA!!!

Thursday, December 23, 2010

KESHO 24/12 HAPA NDIO CHRITSMAS /JULAFTON!!

Napenda kuwatakieni wote Christmas njema. Ingawa kwa mimi naamini Christmas ni 25/12.Lakini sio mbaya kusherekea mara mbili. Haya sasa angalieni, kila mtu na bahati yako nimetumiwa jogoo huyu rasmi kutoka Kunyumba. Adoli doli adoli .... ila sijui nani atanisaidia kumchinja.Mmmmm, Kaaaazi kwelikweli. CHRISTMAS NJEMA SANA WAPENDWA.... PICHA ZAIDI ZINAKUJA

Wednesday, December 22, 2010

PICHA YA WIKI HII:- JE UMEWAHI KUONA HII?

Nimeipenda picha hii, kwa nini kupoteza muda, mimi nakusuka wewe na wewe msuke binti yako . Safi sana..... ukitaka kupendeza....Lakini huyu mama anaonaje anapomsuka huyo binti?

Tuesday, December 21, 2010

HIVI NI IBILISI AU NI TAMAA?

Ilikuwa 2009 nilipokuwa nyumbani Songea Ruvuma. Nilikuwa nimeenda kusuka kwa waMasai, sehemu ya kusukia ilikuwa nje tu. Tena barabarani kabisa au nisema kando ya barabara.

Watu wakawa wanapita wa kila aina, bahati mbaya au nzuri akapita mwanadada mmoja ambaye ilionekana wamasai hao walikuwa wakimfahamu. Wakaanza kusema, he! Angalia mwanadada yule! Mmoja wao akawa anasema, miezi michache iliyopita alikuwa nusu kufa dada huyu, AMEATHIRIKA(VVU) na alikuwa amedhoofika sio mchezo. Lakini nasikia amepata dawa za kuongeza siku na sasa mwangalie alivyonawiri, mmmhh!

Maongezi yakawa yanaendelea, lakini maongezi yenyewe yalikuwa yakiashiria tamaa ya kimwili walivyo wamasai wale kwa kummezea mate kimwana Yule. Muda wote nilikuwa kimya nikisikiliza maongezi yao. Mara wakawa wanaulizana wapi anaishi binti Yule, na lengo ilikuwa ni kutaka kumwendea na kujivinjari naye. Mwenzenu nikabaki mdomo wazi, mweh!!!
Leo katika kuwaza kwangu ndipo mkasa huu au tukio hili likanipitia na ndio maana leo nimeona tutafakari pamoja. Je? Hii ni tamaa? Au Je? Ni kukosa kufikiri kwa makini? Maana wote walishajua kuwa ameathirika, sasa iweje wammezee mate ya kufanya naye tendo !!!?……

Monday, December 20, 2010

KATIKA MAISHA KUNA KUPENDWA NA KUCHUKIWA NA WATU


Mada hii ni marejeo niliandika mwaka 2008 bila ya kuwa na sababu isipokuwa kutaka kujua maana ya haya maneno inga kapulya.
Kupenda/upendo ni kitu cha ajabu sana mara nyingi nimekuwa nimejiuliza kwa nini sisi binadamu tuna upendo tofaoti kwa kila mtu. Nikisema hivi nina maana kuna wakati mtu inaweza kutokea unampenda mtu kiasi kwamba huwezi kujizuia. Na cha ajabu mara nyingine uanaweza kumpenda mtu ambaye hujawahi kumwona ana kwa ana(uso kwa uso) na upendo ukawa wa nguvu kali sana.

Halafu sasa inaweza kuwa kinyume kabisa. Yaani watu tunaweza kuwa na chuki. Unaonana na mtu siku moja tu na utasikia simpendi kabisa jamaa huyu. Au hata kuangalia tu picha yake unapatwa na chuki. Nashangaa sana kwa uwezo kama huu ambao MUNGU amatupa na pia SHETANI anaingilia na kuharibu.Swali:- Hivi hii inatokana na nini?
Leo nimeona niimbe mwenyewe ila samahani hamtaisikia sauti yangu:
Upendo, upendo, upendo ni amri ya bwana, Yesu alisema pendaneni, pendaneni kama nilivyowapenda. Nanyi pia, nanyi pia mpendane palipo na upendo Mungu yupo nasi tupendane tupendanex2.
Lakini pia si mbaya kama tukimsikiliza Mr Nice na ujumbe wake wa kikulacho ki nguoni mwako haya karibu....!!!

Sunday, December 19, 2010

LEO NI JUMAPILI YA MWISHO YA MAJILIO!!!

Ee Bwana na Mungu wangu,
Uliye mwanzo na mwisho wangu,
Kuanzia sasa najuweka mikononi mwako,
Unitumie kulingana na mapenzi yako,
Kisha unifundishe njia ya kupanda ngazi ya kukufikia.
NAWATAKIENI JUMAPILI HII YA MWISHO WA MAJILIO YAKE YESU IWE NJEMA SANA!!!!

Saturday, December 18, 2010

PICHA YA WIKI HII!!!

Hii picha imenikumbusha mbali sana . Je wewe msomaji/mtazamaji kuna kitu hapa kinakukumbusha ?JUMAMOSI NJEMA WANDUGU WOTE MNAPENDWA!!!

Friday, December 17, 2010

KUMBUKUMBU KWA MAMA YETU ALANA NGONYANI!!!!

Hapo ni mama Alana ni huyo aliyekaa na mimi
nikimsuka mwaka 1997 kijijini Mahumbato Mbinga!!!
Nimeamka leo nikia na majonzi mengi kwani hii tarehe huwa inanikumbusha sana mama. Kwani ndio ilikuwa tarehe ambayo alituacha ni 17/8/2004, kwa hiyo leo ni miaka 6 na miezi 4. Nina mengi ya kuongea nawe mama, kuna wakati huwa nadhani upo nasi na nachukua simu na nataka kuongea nawe, nataka kuisikia sauti yako, kicheko chako pia kukumba ushauri/mawazo. Na mwisho nabaki nikitoa machozi. Mwe!!!.

Halafu natamani kweli kukusimulia jinsi wajukuu wako wanavyoendelea pia makuzi yao. Wao pia wanakukumbuka sana. Unakumbuka mara ya mwisho uliwapa zawadi Camilla ukamnunulia gauni na Erik shati na kaputula, bado wanavitunza mpaka leo. Na wanaviabudu mno.
Najua unanisikia huko uliko, sisi wote tunakukumbuka sana mama Ustarehe kwa Amani. SISI TULIKUPENDA LAKINI MWENYEZI MUNGU ANAKUPENDA ZAIDI. AMINA.
Mama ngoja nikuwekee huu wimbo wako ambao ulikuwa ukiimba tangu mimi nilipokuwa mgongoni.


AU MIMI NAMI NIKUKUMBUKE KWA WIMBO HUU HAPA CHINI NA KAKA ALBINO FULANI!!!!


Thursday, December 16, 2010

AFRIKA NA UZURI WAKE !!!!


Mara nyingi huwa najiuliza hivi watu wana picha gani kuhusu Afrika yetu??

Wednesday, December 15, 2010

2010-KUELEKEA MWAKA MPYA 2011

Tafadhali nisaidieni kupata ufumbuzi wa swali la hicho kitu kinachoitwa mwaka mpya maana nimekuwa najiuliza miaka kibao sijapata hasa kujua hicho kinachoitwa mwaka mpya nini.

Mimi nimekuwa na mtazamo ninauambatanisha ili nanyi mnisaidie kupata ufumbuzi ambao naamini utawasaidia watanzania wengi

Naitwa Salehe Msanda niko Njombe Tanzania


SWALI HICHO KITU KINACHAOITWA MWAKA MPYA NI NINI AU NI KITU GANI?

1.SIKU YA KWANZA YA MWEZI JANUARI-1/1

2.NI TUKIO LA SIKU YA KWANZA YA MWAKA.

3.NI MABADILIKO YA KUTOKA KATIKA HALI MOJA KWENDA NYINGINE NA HASA KUMALIZA SIKU 365
NA KUZIANZA ZINGINE 365.

Kila mwaka inapofika mwezi wa 12 na hasa tarehe za kuanzia 15/12 huwa kunakuwa na pilikapilika nyingi za kwanza kuelekea katika sikukuu ya kuzaliwa mkombozi wetu yesu kristo na kumaliza mwaka na kuelekea kuanza kinachoitwa mwaka mpya.

Je tumewahi kujiuliza kwa makini na kupata angalau ufumbuzi/jibu/majibu, wa kitendaliwili cha
hiki kitu kinachoitwa mwaka mpya au tunakwenda tu kimazoea na hivyo kupelekea kuishia katika kufanya mambo kimazoea na kimapokeo?

Tukirudi katika swali na huenda ikiwa moja ya majibu ya hiki kitu tunachokiita mwaka mpya tukianza na jibu la kusema mwaka mpya ni siku ya kwanza ya mwezi januari yaani tarehe 1/1.

Hapa kunajitokeza utata hasa ukizingatia kwa mfano kuna mwaka mpya wa kiislam na kikristo
ambayo yote inaanza katika miezi tafauti kuzingatia na mwaka husika.

Lakini pia kuna suala la kama ni siku ya kwanza ya mwezi januari ni nini hasa kinachapelkea kufanya
siku hiyo kuwa ni ya kwanza na kuwa na umuhimu wa kipekee.

Tukija katika masuala ya hesabu na hasa msingi mkuu wa hesabu yaani kujtmlisha
+,kutoa-,kuzindisha X,na kugawanya .Tuatjikuta tunapata mambo yafuatayo katika siku hiyo ya
kwanza ya mwaka yaani 1/1/2011

Pia ukichukua namba hizo bila ya kuzitenganisha unapata 11 na 20 na namba 11 tena.

Maana yake kwa tafsiri yangu kwa kucheza na namba kwa kuamini kuwa mwaka mpya ni siku ya
kwanza ya mwaka tunapata mambo yafuatayo

Kunakuongezeka katika masuala mbalimbali mfano masuala ya kipato ,neema na kukua

Tukio la pili ni kufuta au kuondoa kile ulichonacho na kubaki ukiwa hauna kitu na hivyo kuanza upya

Tukio la tatu unabaki na kilekile ulichokuwa nacho kiwe kizuri au kibaya itategemea na mtazamo wa
mtu halikadhalika kwa tukio la nne linatubakisha katika hali ile ile.

Ukienda katika kuzitenganisha namba hizo za 1/1/2011 za mwaka tunaotarajia kufika na kwa
kuziweka bila ya kuzitenganisha unapata mabo yafuatayo yanayofanana 11=2,20 pia sawa na 2 na 11 ya mwisho sawa na 2.

Maana yake tunatakiwa kuongeza kwa upande wa mazuri hii ni tafsiri yangu
Pia ukirudi katika msingi wa hesabu na kuamua kutoa 1-1=0,2-0=2 na 1-1=0
Maana yake tunaweza kuongeza au kupunguza na kubaki palepale tulipokuwa
Ukizijumlisha namba zote 1+1+2+0+1+1=6,maana yake tuna nafasi ya kuongeza mara sita ya kile tulichonacho

Tukija katika jibu la pili kuwa ni tukio la siku ya kwanza la mwaka mtarajiwa 2011.
Mkanganyiko unakuja hiyo siku ya kwanza mbona haina tofauti na siku zingine? Maana kutakuwa na asubuhi,mchana,jioni na hatimaye usiku kama siku zote tulizozizoea na kama kwa huku Njombe tunatarajia kutakuwa na baridi kama kawaida yake na mvua.

Mkanganyiko mwingine unakuja iwapo ni tukio la siku ya kwanza utatafaotishaje iwapo imetokea ukapoteza fahamu kuanzia mfano tarehe 29 na kuzinduku siku hiyo maana utashuhudia mambo
nilypotaja hapo juu. Kama utazinduka asubuhi utaona hiyo hali ya asubuhi ambayo umeizoea
na halikadhalika kama ni mchana,jioni na usiku na zaidi utashuhudia watu jamaa na ndugu zako
wamekuzunguka. Na iwapo hautaambiwa kuwa leo ni mwaka mpya hautakuja kupata kitu au ishara itakayokuaminisha kuwa siku hiyo ni mwaka mpya.

Pia kwa upande mwingine tukienda kwa undani matukio tunayatarajia yawe na vitu au tabia
ambazo zinatoa nafasi ya kuona uhalisia wa tuki husika mfano tukio la kuzaliwa,kuna uhalisia hapo wa kupatika kiumbe mwingine ambaye atapita katika hatua za kuelekea kuwa mtu mzima.
Matukio ya u siku na mchana,kuwa na jua na mwezi kuna uhalisi wa kile kinachotokea lakini kwa hicho tunachakiita mwaka mpya sijaona uhalisia unaoweza kutuaminisha kuwa kweli mwaka mpya ni tukio kama matukio mengine.

Tukija katika jibu la tatu la mwaka mpya ni mabadiliko nadhani hapa ndipo tunapoweza kuona uhalisi wa mambo mbalimbali na kutuaminisha kuwa mwaka mpya ni zaidi ya hicho tunachofikria sisi cha siku ya kwanza ya mwezi januari.

Mfano ni ukweli uliowazi kuwa kama tunakubaliana kuwa mwaka mpya ni mabadiliko kama ni
mtoto aliyezaliwa tarehe 1/1/2011 atakuwa amefikia hatua ya kutembea hilo ni badiliko ambalo
wanafamilia wanaritarajia na ni lazima litokea labda kwa kesi chache. Kama ulikuwa unaitwa mr
na mrs Fulani mtakuwa mnaanza kuitwa baba na mama Fulani,lakini pia kama ulikuwa unaitwa
HANDSOME BOY NA BEUTIFULY GIRL utaanza kuitwa handsome man na beautiful woman. Na wale
waliokuwa wanajiita girlfried na boyfried wataanza kujiita manfriend na womanfriends.

Mfano hai sasa hivi dunia yote inapiga kelele kuhusu mabadiliko ya tabianchi kitu ambacho
kinatotokea kama mabadiliko kutoka na baadhi ya matendo ya binaadamu katika kutafuta
kukabiliana na mabadiliko ya mienendo ya dunia ya mabadiliko yanaypotokea katika ulimwengu huu tunaoishi mengine kwa kujua na mengine bila ya kujua.

Mwaka mpya ni mbadiliko inazihirishwa hata katika masuala mbalimbali ambayo wewe na mimi
tunayafahamu,mfano kama kwa wakulima na naamini tuliowengi tumetoka katika familia za
wakulima,shamba limelimwa kwa muda mrefu zao la aina moja huwa tunase,ma limechoka maana yake kumekuwa na mabadiliko yaliyopelekea shamba hilo kuchoka.

Kwa msingi huu kama wote tunakubaliana na jibu la tatu la hicho kinachoitwa mwaka mpya ni
mabadiliko sasa nini kifanyike kuanzia katika ngazi ya familia ambayo ndiyo msingi mkuu wa ujenzi wa masuala yote yanayomuhusu binaadamu na vile vilivyopo juu ya dunia ambayo mwanaadam amebalikowa kuingozo kuiweka chini ya imaya yake na tukirudi katika msingi wa jibu la kwanza katika majibu ya hesabu za msingi wa kuanzia masuala ya msingi

1. Tubadilike kwa kujikagua katika kila Nyanja ya maisha na kutenda kwa kuaongezaa kwa
upande wa kujenga ili kuwa na dunia Tanzania salama ya kuishi kuanzia katika ngazi ya
familia.

2. Tunatakiwa kuwajibika kwa maisha yetu na viumbe tunavyvitawala si kwa chini ya asilimia
60% na asilimia zilizobaki zitajaziwa na wengine. Ukiwajibika kwa zaidi ya asilimia 60% ni
vizuri zaidi.


3. Tuwe watu wa vitendo zaidi badala ya kuzungumza sana ,kulaumu,kulaani na kulalamika kwa
katika hali halisi kulaumu,kulaani na kuongea sana hakujawahi kubadili kile unachakitaka.


4. Tunatakiwa kubadilika kutoka katika hali inayoumiza wengi na kuhakikisha tunakuwa chachu
ya kuona kila mmoja anawajibika kuifanya Tanzania kuwa yenye neema, Furaha, upendo na
ridhiko.


5. Katika ngazi ya familia na walio katika uhusiano ni wakati wakuhakikisha uhusiano
unashamili na kuifanya taasisi ya kale katika dunia hii inayoitwa taasisi ya NDOA kuwa taasisi
yenye msingi imara wa kujenga kizazi kilichopo na kinachokuja.


6. Tukiamini kuwa mwaka mpya ni mabadiliko na tunatakiwa kubadilika kwa kutenda tutafika
mahali kila mmoja wetu atakuwa na furaha ya kweli . Maana inasadikiwa na ndio ukweli
ulivyo KATIKA KUTENDA HAKUNA KUSHINDWA ILI KUNAKUPA MATOKEO YASIYOTARAJIWA
na kama tukiamua kwa nia ya dhati mabadiliko yatakuja kwa haraka, tuache kukata tamaa
haraka na kutarajia kuwa mabadiliko yatakuja haraka kama unavyotuma mesege. Maana
tumekumbwa na electronic life style na kufikiria kila kitu kitatokea kwa mkabala wa
electronic.

Watanzania tusherehekee mwaka mpya kwa mtazamo kuwa mwaka ni suala la mabadiliko katika Nyanja mbalimbali za maisha na mabadiliko hayo yanatakiwa kutufikisha katika kuona maisha ni mazuri na ya kuvutia.

KILA LA KHERI KATIKA KUELEKEA MWAKA MPYA

Monday, December 13, 2010

TANZANIA- DR. REMMY MTORO ONGALA HATUNAYE TENA!!

Remmy Ongala [1947-2010]
Mwenyezi Mungu na aipokee roho ya Dr. Remmy Ongala na ailaze mahali pema peponi. Amina.



NGOJA LEO TUANGALIE METHALI ZETU:- METHALI ZAFAA SANA KWA MAFUNDISHO YA ADILI!!!

1.Asiyefunzwa na mamaye, hufunzwa na ulimwengu.
2. Baada ya dhiki, faraja.
3. Baba wa kambo si baba.
4. Chema chajiuza, kibaya chajitembeza.
5. Chombo kilichopikiwa Sakaki, hakiachi kunuka vimba.
6. Damu nzito kuliko maji.
7. Dawa ya moto ni moto.
8. Fadhili za punda, mashuzi; na msihadhari ni ngómbe.
9. Fumbo mfumbie mjinga , mwerevu hulingámua.
10. Ganda la mua la jana, chungu kaona kivuli.
11. Gonga gogo usikilize mlio Wake.
12. Hakuna siri ya watu wawili.
13. Hasira, hasara.
14. Ihsani haiozi.
15. Jungu kuu halikosi ukoko.
16. Jambo usilolijua ni kama usiku wa kiza
17. Kila mlango na ufunguo Wake.
18. Kulea mimba si kazi´, kazi kulea mototo

Friday, December 10, 2010

KUMBUKUMBU+MAISHA

miti ya miembe
Najua hii habari/makala nilishawahi kuiweka lakini leo nimeamka na bado namfikiria/namkumbuka rafiki yangu Claire Mputa yaani kokote ulipo Claire jaribu kunitafuta nitafurahi kuwasiliana nawe tena.Haya ebu jikumbushe tena habari hii.
Nakumbuka ilikuwa mwaka 1983 nilikuwa naishi Lundo (Nyasa) wakati huo. Siku moja mchana nilikuwa naosha vyombo. Nilikuwa nasugua sufuria na vyungu hii ilikuwa kazi yangu. Kama mjuavyo Nyasa ni kula samaki sana. Kuna mtu alitupa miiba ya samaki ovyo na kwa mimi kutojua ni sehemu ile ile niliyokuwa nikiosha vyombo. Kwa bahati mbaya nilipiga magoti bila kujua napiga magoti kwenye miiba. Mmh kazi kwelikweli.

Baada ya siku goti lilianza kuvimba, nilichofanya tangu siku ile ya kwanza sikumwambia mtu nini kimenipata. Sababu kubwa ni kwamba ningeambiwa nibaki nyumbani. Sio kwenda shule ni mgonjwa. Na goti lilizidi kuvimba, lakini nilijikakamua na kuvumilia na maumivu yote. Kisa nilikuwa sitaki kubaki nyumbani bila kuhudhuria masomo.

Lakini siku moja wakati nipo shule nilikosa raha sana kwa maumivu. Rafiki yngu mmoja aitwae Claire Mputa aliona goti langu limevimba sana. Akanishauri niende hospitali naye atanisindikiza. Hata hivyo nilikataa kisa ni kile kile kuogopa kukosa masomo yatanipita. Lakini Claire aliweza kunishauri.

Ilichukua muda mrefu kufika hospitali kwani sasa goti lilikuwa limevimba mno na nilikuwa nachechemea na pia lilikuwa linauma sana, kwani kidonda kilianza kutunga usaa (infection). Kwa hiyo tulikuwa tunatembea polepole sana. Na hapo hatukuwa sisi tu kulikuwa na wanafunzi wengine pia waliokuwa wagonjwa wao walitangulia . Baada ya muda, yaani tulikuwa tunakaribia kufika hospitali tukawakuta wale wanafunzi wenzetu waliotangulia wamechepuka maporini ambako kulikuwa na miembe mingi iliyoshonana. Claire akaniambia; Yasinta twende tukaangalie wanafanya nini? Basi tukaenda kuangalia wote mie na Claire, tulipofika, tukawakuta wanafanya ule mchezo unaofanywa na wanandoa (ngono). Tulishangaa sana na kuondoka, kumbe wao walikuwa si wagonjwa walitaka tu kukwepa masomo na kwenda kufanya ule uchafu. Yaani ilikuwa kinyume kabisa na mimi, na sikutarajia kama wanafunzi kwa umri ule tuliokuwa nao wangeweza kufanya yale tuliowakuta wakiyafanya.

Haya, tulipofika hospital kama kawaida kukaa foleni. Mara ikaja zamu yangu Claire Mputa akanishika mkono na kunisindikiza ndani ya chumba ambacho kilikuwa maalum kwa mambo ya vidonda. Nakumbuka yule daktari alikuwa mzee kidogo, aliitwa Kataulaki. Alinitisha alipochukua mkisu mkubwa nilifikiri anataka kuukata mguu wangu. Lakini hakufanya hivyo alinitibu na mimi na Claire Mputa tukarudi tena shuleni.

Kikubwa ninachotaka kusema hapa ni kwamba kama Claire asingenishauri kwenda hospitali basi leo hii nisingekuwa na mguu wa kushoto. Na pia nisingeyaona yale nilioyaona kule miembeni, kwani yalinifunza kwa kiasi fulani. Napenda kuchukuwa nafasi hii kuwashukuru rafiki yangu Claire Mputa na pia yule Daktari Kataulaki
Napenda kuwaambia ahsanteni sana. IJUMAA NJEMA TUTAONANA TENA WAKATI MWINGINE!!!!!

Tuesday, December 7, 2010

Elimu/kujitegemea na ushirikiano kati ya wanafunzi na wazazi!!.

Sokoni/Julmarknad!!


Wikiend iliyopita ambayo ilikuwa kama ifuatavyo. Sasa tuendelee:- Wanafunzi wa darasa la sita ambalo binti yetu naye anasoma wanataka kufanya safari (skolresa) darasa zima ili kuona mazingira mengine. Na safari kwa kila mwanafunzi ni 700kr ni sawa na 140000Tsh.

Wakawa wanajiuliza tufanyeje ili tupate hizi pesa?. Mmmh! Tuchangishe pesa kila mtu/kichwa kitoe 700kr Hapana, tupite kuuliza kila nyumba kama tunaweza kusafisha magari , Hapana.

Bahati nzuri sasa ni kipindi cha majilio(christmas) na wikiend hii iliyopita kulikuwa na soko kwa ajili ya christimas (Julmarknad) basi wakapata wazo kuwa watushirikishe wazazi kutengeneza chochote kile kama vile keki, pipi, kuoka mikate, kutengeneza Kanawa, chai, chokleti nk. Hakika hutaamini jinsi wazazi tulivyo/walivyowaunga mkono, wacha kazi za kuoka zianze...... binafsi nilioka mikate kama 100 vile.

Na baada ya kuoka ikabidi wazazi na watoto/wanafunzi waende sokoni jumamosi na jumapili siku ya mapumziko. Tukaacha shughuli nyingine na kumbuka hii shughuli itafanyika nje na baridi sio mchezo. Hilo halikuwa tatizo Kabila wazazi na watoto tulikwenda huko sokoni (julmarknad) na Kuuza hivyo vitu ili watoto wapate ppesa na kuweza kufanya safari (skolresa) yao. Kwa kweli huu ni mfano ambao kama sisi waTanzania tungeiga nina imani tungekuwa na maendeleo. Sio kila kitu kutaka kupata kwa mteremko tu. Ebu ingia hapa na usoma makala hiii inafanana sana Milano yako na huu.

Monday, December 6, 2010

Dunia ni duara

Leo tarehe 19-08-2009, nilikumbuka tukio moja lilitokea tarehe 25-3-2008, tukio lenyewe lilikuwa hivi:

Dunia hii ni duara, na watu kama tulivyo, kukutana ni wajibu, tofauti na milima. Katika kukutana ndipo tunapojenga urafiki, udugu na hata uchumba, ndio ni kweli hata uadui pia. Lakini tusisahau kuwa kama binadamu tulivyo, kukoseana na hata kujengeana uadui kupo, lakini hili ni nadra, na linapotokea huwa lina sababu, kwani ibilisi huja na visa vyake ili viwe fundisho kwetu.

Diana baada ya kukaa kwenye kampuni moja kwa muda mrefu, alipata bahati ya kuomba sehemu nyingine. Alifanya hivi ili kupata sehemu itakayokidhi mahitaji yake, lakini pia alishachoka kufanya kazi na meneja wake ambaye kila siku waliishia kugombana. Siku alipopewa barua ya ajira sehemu nyingine, ambayo ilimuahidi kipato kikubwa, alitamani dunia yote ijue kuwa yeye sasa hivi, sio yule Diana waliyemjua ni Diana mwingine. Kwa raha aliyokuwa nayo, aliingia ofisisni kwa taksi, na akiwa amechelewa.

Alipofika asubuhi ofisini, aliwasabahi wale waliokuwa karibu naye huku akiwapa mkono wa kwaheri. Alimwendea bosi wake ambaye walikuwa hawaivani, na alipoulizwa kwanini kachelewa alijibu kwa dharau, `tatizo la usafiri,’ Bosi alipotaka kuja juu akaona huo ndio muda muafaka wa kumpa bosi vipande vyake, na kweli alimpa bosi vipande vyake, na kumwambia sasa hivi yeye na kampuni yake basi.Bosi wake Mr. JeuriMbaya ambaye licha ya ukali wake katika kazi, kitu ambacho wengi walimuona ana roho mbaya, alikuwa muungwana pale panapohitajika, alichofanya ni kumtakia kila-laheri, na kumwambia kama katika utendaji wake wakazi walikwazana, basi anaomba msamaha, kwani yeye alikuwa akitimiza wajibu wake tu. Diana alimwangalia kwa jicho la dharau, akageuka na kuelekea kwenye meza yake, huku moyoni akisema, bosi wa namna yako hastahili kufanya kazi na mimi.

Hapo mezani alitumia muda mwingi kuwajulisha marafiki zake kuwa yeye sasa atakuwa katika ofisi za Kampuni kubwa ya Kimarekani, ambapo pia ameahidiwa kupekwa masomoni.Ilipofika jioni, Diana alichukuliwa na taksi, ya mshikaji wake na moja kwa moja walielekea Kaunta. Huko alikunywa kama amesingiziwa. Waliondoka maeneo hayo usiku akiwa hajitambui. Njiani kwa vile walikuwa wamelewa chakari, wakapata ajali mbaya, ajali hiyo ilimvunja Diana mguu na kujikuta anapelekwa Muhimbili.

Kwa vile Kampuni yake mpya ilishaingia mkataba naye, ilimsaidia na kumhakikishia kuwa ajira yake bado ipo ingawaje alikuwa hajaanza kazi. Hii ilimpa faraja sana Diana, na akaendelea na matibabu yake huku akijua hawezi kumrudia meneja JeuriMbaya.. Hapo Muhimbili alikaa miezi miwili. Alipotoka, alipewa mapumziko ya mwezi mzima nyumbani.

Siku ikafika, na hali ya mguu wake ilisharejea vyema, ikabidi aripoti ofisini kwake, kwenye ofisi mpya. Alikariribishwa kwa bashasha na kila mmoja akimpa pole kwa huruma na upendo. Hali hii hakuizoea huko alikotoka. Alifurahi moyoni, na kusema `hapa ndipo nilipokuwa nikapataka…

`Diana tuna bahati kubwa sana, kwani tumepata meneja utawala mpya, ambaye utakuwa katibu muhtasi wake, naye kaajiriwa karibuni, kwahiyo twende ofisini kwake ukatambulishwe’ Aliambiwa na Ofisa utawala.

Akiwa na bashasha ya kumuona meneja wake mpya, ambaye alihisi atakuwa Mzungu, alitabasamu akamtafadhali Ofisa Utawala na kuchepuka kwanza chooni ili aweze kujikwatua. Hii ilikuwa sehemu ya mambo ambayo alifundishwa kuwa anatakiwa apendeze ili kumvutia bosi wake pamoja wageni.

Aliongozana na ofisa utawala, mama wa makamo, mama ambaye aliijua kazi yake vilivyo. Na kwa uzoefu wa siku nyingi, aliona amuelekeze yule binti wake mambo kadhaa kabla hajampeleka kwa bosi wake mpya. Diana alijisikia vibaya, hakupenda kukosolewa, lakini alijikaza akijua kuwa anabembeleza ajira.Kabla ya kuingia kwa meneja huyo ilibidi wapitie kwa meneja wengine mbalimbali, na kila sehemu alipokelewa vizuri na kukaribishwa ofisi mpya.

Mwishowe walifika kwenye ofisi iliyoandikwa `Meneja utawala’ Waligonga mlango wa Meneja Utawala na kukaribishwa ndani.Walipoingia walimkuta meneja Utawala akiwa ameinama na kugeukia upande mwingine, kwahiyo sura yake ilikuwa haionekani vizuri.‘Karibuni tafadhali, natafuta faili moja hapa, la huyu katibu wangu Mhtasi, unasema anaitwa nani vile…’

Aliwakaribisha huku akitaka kulifunua lile faili, bila kuwaangalia.‘Tafadhali bosi hatutaki kuchukua muda wako mwingi, yeye kwa vile mtakuwa naye karibu atajitambulisha kwako vizuri, kama unavyojua alikuwa anaumwa, kabla hata hajaanza kazi hapa….’ Aliongea ofisa utawala.

‘Oooh, karibuni sana,..’ aligeuka akiwa amenyosha mkono.Mshangao alioupata Diana ulimfanya aishiwe na nguvu, na kama asingekuwa ameegemea meza angejikuta kadondoka chini. Hakuamini macho yake…

‘Ahsante, sh-shi-kamoooo bosi’ Alijikuta akitoa salama ambayo hajawahi kumsalimia bosi wake kabla.Aliyekuwa amesimama mbele yake si mwingine ila ni bosi wake wa zamani, ambaye waliachana naye kwa mizengwe, sasa ni bosi wake mpya, Mr.Jeuri Mbaya.JE KAMA WEWE UNGEKUWA NI DIANA UNGEFANYAJE

Makala hii nimeipenda na nimeona si vibaya nikiiweka hapa ili wengi wajifunza nimeipata toka hapa.

Sunday, December 5, 2010

JUMAPILI HII YA PILI YA MAJILIO TUPATE UJUMBE HUU:- Life Is a Gift

Ujumbe huu nimetumiwa na rafiki mmoja na nimeupenda na nimeona ni vema nisiwe mchoyo na ndio maana nimeona niweke hapa Maisha na Mafanikio.


Today before you say an unkind word -
Think of someone who can ' t speak.

Before you complain about the taste of your food -
Think of someone who has nothing to eat.

Before you complain about your husband or wife -
Think of someone who ' s crying out to GOD for a companion.
Today before you complain about life -
Think of someone who went too early to heaven.

Before whining about the distance you drive
Think of someone who walks the same distance with their feet.

And when you are tired and complain about your job -
Think of the unemployed, the disabled, and those who wish they had your job.

And when depressing thoughts seem to get you down -
Put a smile on your face and think:
you ' re alive and still around.

"B POSITIVE & THINK POSITIVE"

Saturday, December 4, 2010

UJUMBE WA JUMAMOSI YA LEO NA YA PILI YA MWEZI HUU !!!

Nimegundua kazi tano ngumu katika dunia hii:-

1. Kumpaka LIPSTIK KUKU.
2. Kumpakata TEMBO.
3. Kumpenda MENDE.
4. Kumvalisha nguo MBU.
5. Na la mwisho KUKUSAHAU wewe.

Hebu tumsikilize Mr. Ebbo na mwimbo wake wa mbado


JUMAMOSI NJEMA SANA KWA WOTE.

Friday, December 3, 2010

PICHA YA WIKI HII:- MTINDO WA NYWELE!!!!

SIJUI ANAFANYA NINI?
Wiki hii tuangalie mtindo wa nywele. Ebu angalia wanadada hawa ni wanandugu au? labda marafiki? au labda imetokea tu kuwa hivyo? Maana wanafanana hadi jinsi ya kuweka nywele.
IJUMAA NJEMA WANDUGU!!!

Thursday, December 2, 2010

Huolewa na baba zao

Kila jamii ina visa asili, yaani imani ambazo zinaonekana kama kweli, wakati hazina ushahidi wa aina yoyote kuwa zina ukweli. Lakini, kila kisa asili, kina chimbuko lake. Chimbuko hilo husema kuhusu ambavyo jamii hiyo imekuwa ikiyatafsiri mambo.

Moja ya visa asili katika jamii yetu na jamii nyingine duniani ni kwamba, mwanamke anapoolewa na mwanamume na wakaishi kwa muda mrefu, hatimaye watu hao hutokea wakafanana sura.
Lakini, je kuina ukweli wowote katika jambo hili? Jibu ni kwamba, kuna ukweli ambao hata hivyo unahitaji maelezo zaidi ya yale ambayo tumeyazoea, yasiyo na uchambuzi.
Ni kweli, kuna wanawake ambao wanafanana sura na wanaume ambao wako nao kwenye ndoa.
Hata hivyo, suala la kuishi kwa muda mrefu halina ukweli. Kufanana kwa mke na mume huweza kujitokeza hata kabla hawajaoana.

Si watu wengi ambao wanajua kwamba, baba anapokuwa anampiga mama, yaani mkewe, watoto wanapoona vipigo hivyo, huathirika na wanakuja kutumia uzoefu huo ukubwani. Kama mume anampiga mkewe mara kwa mara kwa mfano, watoto wa kiume kwenye familia hii, wako kwenye uwezekano mkubwa sana wa kuja kuwapiga wake zao.

Tafiti nyingi zinaonesha kwamba, wanaume ambao huwapiga wake zao, wanane kati ya kila kumi walishuhudia baba zao au walezi wao wa kiume wakiwapiga wake zao.
Lakini, pia inaonesha kwamba, wale watoto wa kike ambao waliona mama zao wakipigwa na baba zao, wako kwenye nafasi kubwa ya kuja kuolewa na wanaume ambao nao wanapiga.
Kinachotokea ni kwamba, watoto hawa wa kike, ukubwani hutafuta wanaume ambao wana tabia kama za baba zao, wakiamini bila wenyewe kujua kwamba, wakiwapata wanaume hao watalipiza namna mama zao walivyofanyiwa na baba zao.

Bahati mbaya, badala ya kulipiza, hujikuta wanashindwa kutoka kwenye uhusiano huo wa mateso kwa visingizio mbalimbali. Hii hata hivyo, haina maana kwamba, wanawake wote wanaoteswa kwenye uhusiano wanaendelea kukaa humo kwa sababu hii. Wengine hukaa humo kutokana na utegemezi wa kihisia au kutokana na kutojiamini na hata sababu za kijamii, zikiwemo imani za dini.

Hata hivyo, wataalamu wamegundua kwamba, suala sasa siyo baba kumpiga mama peke yake, bali uhusiano kati ya mtoto wa kike na baba yake. Inaelezwa kwenye tafiti kadhaa kwamba, kama mtoto wa kike anaelewana vizuri sana na baba yake, kuna uwezekano mkubwa kwamba, mtoto huyo atakuja kuolewa na mtu ambaye anafanana na baba huyo.
Awali, tafiti zilipoonesha uwezekano huo, ilionekana kama porojo, lakini hivi karibuni jambo hilo limethibitishwa na vyombo vingi vya kiutafiti.
Hii imefanyika baada ya vyombo hivyo kuwatumia wanawake wengi katika kujaribu kuthibitisha jambo hilo.

Taarifa za kitafiti ambazo zimeripotiwa kwenye jarida la Evolution and Human Behavior, zinaonesha kwamba, mtoto wa kike ambaye ana uelewano wa karibu sana na baba yake utotoni, akija kuwa mkubwa, bila kujua atakuja kuvutwa na mtu ambaye anafanana sura na huyo baba yake.
Baadhi ya watafiti wanasema, labda hapo ndipo mahali ambapo panachimbuka ile imani kwamba, mtu na mkewe wakiishi kwa muda mrefu huja kufanana.
Pengine siyo suala la muda mrefu, bali zaidi ni kwamba, mwanamke ambaye anafanana na mumewe ni mwanamke ambaye alipokuwa mdogo alipendwa au kuelewana sana na baba yake.
Watafiti wengi waliofanyia kazi suala hili wanasema wamegundua kwamba, mtoto wa kike ambaye hakuwa na uelewano mzuri na baba yake, kwa kawaida havutwi kabisa na wanaume ambao wana sura kama ya baba yake.

Labda hii inaweza pia kuelezea ni kwa nini baadhi ya wanawake wazuri sana huolewa na wanaume ambao ni wabaya wa sura (kama jamii inavyowahukumu). Ni kwamba, inawezekana baba yake msichana alikuwa na sura nzuri na hawakuwa na uhusiano mzuri. Ni wazi, mwanamume mwenye sura ya aina ya baba yake hatamvuta. Lakini, hapa inategemea uzuri huo ulikuwaje, kwa sababu anachofuata msichana siyo uzuri au ubaya wa sura, bali sura inayofanana na ya baba yake au isiyofanana na ya baba yake.

Lakini, kama mtoto wa kike alielewana sana na baba yake ambaye ana sura mbaya kwa mujibu wa vipimo vya jamii, atajikuta akivutwa na wanaume wenye sura kama ya baba yake (mbaya) ambapo itakuwa rahisi kwake kuolewa na mmoja kati yao na siyo na wale wenye sura nzuri.
Hebu fikiria kuhusu mtoto wa kike ambaye anafanana na baba yake, halafu anaelewana sana na huyo baba.

Ina maana kwamba, atakuja kuolewa na mwanamume ambaye siyo tu kwamba, anafanana na baba yake, lakini pia ambaye anafanana naye (mwanamke). Kwa kuwa kuna idadi kubwa ya watoto wa kike wanaofanana sura na kuelewana na baba zao, ina maana ndoa za wanaofanana nazo ni nyingi. Lakini, je utafiti huu unataka kuwafundisha wale akina baba ambao jamii inawahukumu kwamba, wana sura mbaya, kutokuwa karibu na watoto wao wa kike ili kuwaepusha kuja kuolewa na wanaume wenye sura kama zao? Bila shaka hilo si lengo la utafiti huu.

Ukweli ni kwamba, kama msichana amempenda mwanamume, maana yake ameona kwake ni mzuri, tofauti na jamii inavyoona.
Kama jamii imepanga viwango vya uzuri na ubaya, ni suala la mtu kuviamini au kutoviamini viwango hivyo. Watafiti wote wanakubaliana jambo moja kwenye utafiti huu, kwamba huenda wanawake huchagua wenza kwa kigezo hiki cha maelewano yao yalivyokuwa na wazazi wao.
Ni kwamba, mwanamke anaweza kumwona mwanamume mwenye sura nzuri, ambayo pengine ni kinyume na ile ya baba yake (mbaya), na akajua kwamba ni sura nzuri.

Lakini, linapokuja suala la kuoa, akachagua sura mbaya ambayo ni ya baba yake. Ninaposema sura nzuri au mbaya, ninazungumzia jamii inavyoona, kwani ukweli ni kwamba, hakuna sura mbaya au nzuri, bali mtu mwenyewe anayetazama anavyoona.
Inaelezwa kwamba, suala ni yupi mzuri kwenye ubongo wa binadamu, halipangwi na wale tunaowaona, bali zaidi hupangwa na wale ambao tulikuwa na uhusiano nao wa dhati na mzuri sana tulipokuwa wadogo. Hapa, baba kwa mtoto wa kike ndivyo ilivyo.
Nimekutana na hii kwa kaka Shabani Kaluse. Na pia, makala hii iliwahi kuandikwa katika gazeti la Jitambue.

Tuesday, November 30, 2010

"MJADALA ULIOVUNJA REKODI KATIKA BLOG YA MAISHA NA MAFANIKIO MWEZI SEPTEMBER 2009"

Ndugu wasomaji wa blog hii ya MAISHA NA MAFANIKIO, katika kupitia mada mbalimbali nilizowahi kuweka humu ili kupata ile ambayo ilivuta hisia za wasomaji wengi na kuleta changamoto , nimevutiwa na mada hii ambayo ilileta vuta ni kuvute miongoni mwa wadau wa blog hii.
Kwa hiyo basi nimeichagua mada hii kuwa ndio mada iliyovunja rekodi kwa mwezi september 2010. Natoa shukrani kwa wadau wote mlioshiriki katika kuichangia mada hii.
Naomba muungane nami katika kujikumbusha kile kilichotokea katika mjadala huu.

WANAUME NA KAULI HIZI: 'HUYO SIO WA KUOA, NI WA KUCHEZEA TU'

Bila shaka wewe msomaji unayesoma hapa utakubaliana na mimi kuwa umeshawahi kuzisikia kauli hizi kutoka kwa wanaume pale anapozungumziwa mwanamke mzuri kwa sura na umbo.

Kwa kawaida vipimo vya uzuri wa mwanamke kwa wanaume vimegawanyika. Wanaume wengi hupima uzuri wa mwanamke kwa sura au umbo, lakini linapokuja swala la kuoa, suala la tabia na mwenendo hupewa nafasi kubwa.

Na ndio maana wakati mwingine unaweza kushangaa kukuta mwanaume ambaye ni hodari wa kuchagua wanawake wazuri, lakini ukija kumuona mke aliyemuoa, utakuta ni mbaya kwa sura na umbo, lakini kwa upande mwingine utakuta mke huyo ni mzuri katika maeneo mengine kama vile, tabia nzuri,upendo, wema, na anayemudu malezi ya watoto katika familia.

Sifa nyingine ni zile za kumkubali mwingine kirahisi, kuwa tayari kusaidia yanapojitokeza matatizo katika familia, mpenda amani na kumfanya mume wake aone kuwa hakukosea kumchagua yeye kuwa mke wake. Kwa kifupi wanawake wa aina hii hata kama wangekuwa ni wabaya kwa sura na umbo bado wako kwenye nafasi ya kuonekana kuwa ni wazuri, na huolewa kirahisi zaidi.

Wanawake wazuri kwa sura na umbo ambao tabia na mienendo yao hairidhishi wako kwenye nafasi kubwa ya kuishi bila kuolewa, na kwa bahati mbaya zaidi wanawake wengi wanaohesabika kuwa ni wazuri, tabia na mienendo yao ni ya kutilia mashaka. Wanaume wengi huvutiwa na wanawake hao kujenga uhusiano nao hasa wa kimwili tu na si vinginevyo, na ndio maana wanawake wazuri kwa sura na umbo wanalo soko kubwa sana kwa wanaume, lakini huishia kuchezewa zaidi kuliko kuolewa.

Wanaume nao kwa upande wao wamejenga dhana kwamba wanawake wazuri sana sio wa kuoa na hivyo kuwaogopa. Wanaamini kwamba wanawake wazuri sana ni wasumbufu, kitu ambacho kina ukweli kwa kiasi fulani. Wanaume wanaamini kwamba wanawake wazuri sana kwa sura na umbo huwasababishia waume zao maradhi ya moyo,shinikizo la damu na wakati mwingine hata kuwafanya kupata matatizo fulani ya kiakili, na hiyo inatokana na waume hao kuwa katika mashaka ya wake zao kuchukuliwa na wanaume wengine wakati wowote kutokana na uzuri wao. Hata hivyo wanawake wazuri nao huwaendesha waume zao wakijua kuwa ni wazuri na soko lao liko juu na waume zao nao huwanyenyekea wakihofia kuachwa.

Na ndio maana usishangae kuona kuwa wale wanawake ambao watu wamekuwa wakiamini kuwa ndio wabaya kwa sura au umbo lakini tabia na mienendo yao ni mizuri ndio wanaoolewa na hata ndoa zao zinadumu, tofauti na za wale wanaoonekana kuwa ni wazuri sana kwa sura na umbo na ambao tabia na mienendo yao si mizuri, ndoa zao hazina umri mrefu.

Na maoni yake yalikuwa kama ivyoatavvyo hebu tujikumbushe ndugu zanguni:-

Fadhy Mtanga said...
Mimi niseme nini? Yote umemaliza weye. Maneno mengi ntaharibu utamu. Habari ndo hiyo.
Usichoke.!
Godwin Habib Meghji said...
kwa hili sina uhakika, itabidi nifanye utafiti kwanza ndio nikubaliane na wewe au kukupinga
Candy1 said...
Nobody is perfect sio...au kila mtu ana kasoro, labda wapo wachache ambao wazuri kwa umbo na kitabia vile vile though ni kama kutaka kwenda kuchimba almasi DAR (lol)...true said sister, mwenzio ana hiki wewe huna na ulichonacho wewe mwenzio hana...
Ramson said...
dada yasinta naomba kwanza nikupongeze kwa mada hii nzuri, maana umepiga bakora kwa wanaume na wanawake.

Labda nikuulize swali dada yangu, hebu ninong'oneze, ili watu wengine wasisikie, hivi na wewe unaangukia katika sifa ipi? maana kila nikiangalia picha yako hapo kibarazani, Mashaallah... umejaaliwa kwa sura na umbo..sasa mzee mzima, baba watoto wako hapati Presha kuwa ataporwa siku moja?.....LOL.

Ni hivi mimi nitatoa maoni tofauti kidogo, kusema ukweli kama unazungumzia wanawake wazuri kwa sura na umbo si kwamba tu wanayo matatizo katika ndoa zao bali pia hata huko mashuleni na vyuoni wana kazi kweli kweli...

Takwimu zisizo rasmi zinaonesha kuwa wanawake wenye sura maumbo mazuri kusoma kwao kunakuwa ni kwa kusuasua sana ukilinaganisha na wale wanawake wanaosemwa kuwa wana sura ngumu, yaani sio wazuri kwa sura na umbo, hawa huelekeza nguvu zao zaidi katika masomo na kwa kuwa hawabughuziwi na wanaume wakware wanakuwa huru na hujisomea kwa bidii na mwishowe hufaulu. lakini wanawake warembo kwa sura na umbo muda mwingi wanahangaikia uzuri wao na kuwa bize na wanaume kwa kuwa soko lao liko juu, kila mtu anawataka, na badala ya kutumia muda mwingi kusoma hutumia muda mwingi kuzunguka na wanaume na matokeo yake wote tunayajua...lakini hata hivyo wsiku hizi wamekuwa ni wajanja sana wengi hutumia miili yao kuwahadaa waalimu au maprofesa kwa kuwapa ngono ili wawezeshwe kufaulu katika mitihani na ndio maana likaibuka neno la Digrii za chupi,msichana anaonekana kabisa hana uwezo darasani lakini mwisho wa siku unamuona amefaulu na kusonga mbele. Digrii za chupi siku hizi ziko kila mahali na hata katika ajira zetu mambo ni hayo hayo....wanatumia miili yao kila mahali kuanzia shuleni, katika ajira mpaka kupanda vyeo..na hili madhara yake wote tunayajua.

Naomba nieleweke hapa sisemi kuwa wanawake wote wazuri kwa sura na umbo wana matatizo hayo, nimesema baadhi yao.
kamala Lutatinisibwa Lutabasibwa said...
Ramson na uzuri wa Yasinta, heri mimi sijasema, amina

ila sijui kama kuna wanaume wanaomchezea mwanamke. kama ni kuchezea basi wanachezeana. mkwani wakati mwanaume anamchezea mwanamke anakuwa anafanya nini? si anafurahia mchezo tena anadansi kabisa? si mwanamke (hasa wa mujini) anacheza zaidi? iweje asingiziwe mwanaume> acha hizo
viva afrika said...
m speach less, viva blogers, viva MAISHA.
Mwanasosholojia said...
Leo naona dada Yasinta tumeamka na mawazo yanayofanana, umekwenda mbali zaidi, mi nimeishia jirani kidogo kibarazani kwangu, ila maswali yanabaki yale yale na ugumu wake katika kuyatafutia ufumbuzi...masuala ya mahusiano yana utata wake kutokana na utata walionao wanaoingia katika mahusiano! Hongera dadangu kwa mada nzuri
Master said...
"You cannot find a man who is right, you need to make the man right!"
Huwa nawaambia wadada ambao nawakuta wanahaha na waume zao.
Usemi huu unawafanya wasite kidogo, watafakari kwa makini.
Nakosea nini?
Namkosea ama ananikosea?
Nimeshindwa ama tunashindwana?
Atabadilika kweli? Nitambadilisha kweli? Au nibadilike?

Ndoa ni changamoto, inahitaji kila kukicha utunge mkakati mpya kutokana na "actions, which create equal and opposite reactions". Samahani, hiyo ina tafsiri ya Kiswahili kweli?

Ok, kwahiyo hakuna "right man" je, kuna "perfect woman?"
Usemi utakuwaje hapo sasa?

Je, ni kwanini 'uzuri" unasababisha watu wawe tofauti, wajisikie,wabweteke, wawe wenye dharau na madaha, wajithaminishe zaidi?
Nadhani ni kwasababu almasi hutokana na mkaa, lakini hutoka ng'avu zaidi, yenye thamani zaidi.
Hivyo mtu mzuri hujitenga na kujiona wa thamani na pekee zaidi.

Si ajabu tangu utotoni, mtoto anayeelekea kuwa mzuri atasikia "eh, mtoto mzuri huyu jamani!" kisha atapewa zawadi na kubebwa, atakuwa katikati ya macho na mwangaza wa kila mtu.

Tabia zinazoweza kujijenga ni zile za dharau na tamaa. Wazungu wanaita vanity. Tamaa ya kuwa zaidi ya zaidi. Kujisikia binafsi, kutothamini wengine, kukubali yule tu ambaye atatoa au kugawa vitu na vito vya thamani ya urembo alionao!

Si ajabu, mwanamke na hata mwanaume mzuri huharibika haraka. Ni wachache wanaoweza kujizuia kujisikia.

Kuwa na hakika kwamba utampata mwanamke mzuri na mwema pia, ni sawa kweli na kuchimba almasi Dar es salaam!

Lakini jamani, si tunafahamu kwamba hata almasi inabidi isuguliwe kupata mng'ao safi na unaoipa thamani zaidi?!

Hivyo, ukiopoa kizuri, endelea kusugua mwenzangu, futa vumbi kila dakika, sugua na mate ikibidi na hakikisha unajiona kwenye mng'ao!
Usipojiona, wengine watakuja na vichubulio maalumu....
Kissima said...
Du! Mengi yamesemwa,lakini naimani hayajaisha, hata kama nikiyarudia.


Wanawake wazuri kwa umbo na sura wengi wao wanaishia kuwa na watoto ambao kila mmoja anakuwa na baba yake,huishia kutelekezwa na wanawake wa aina hii ni vigumu sana kuolewa.Kwa hili, ninamifano hai kabisa ya kina dada wa aina hii na maswahibu yanayowakumba, yani ukiwakuta barabarani huwezi tambua kuwa wameshazaa na kuzaa,watoto wanaachwa kwa bibi zao na babu zao, wao wanapeta mtaani.
Shabani Kaluse said...
Hii mada ya leo dada Yasinta Kaaazi kweli kweli.....
naona walionitangulia wamemaliza kila kitu sina cha kuongeza ila RAMSON, MASTER NA KISIMA.... KAAAAZI KWELI KWELI KWELI.....
Haya mjadala uendelee, naona hapa sijamuona mzee wa changamoto..LOL
chib said...
Nimefurahia maoni ya wadau
Mzee wa Changamoto said...
Beres aliimba akasema "step aside now, another man wants to take over, cause you don't know what you got and now it's time to loose it"
Sina hakika na MAANA ya UZURI, lakini najua kuwa yategemea na upande uliosimama kuangalia uangaliacho. Kwani KUOA na KUCHEZEA vyatofautishwa na nini? MTAZAMO. Unaweza kuchezea unachooa ama kuoa ulichochezea. Kwa hiyo pengine kuoa na kuchezea ni HATUA za KIMTAZAMO anazokuwa nazo mtu na SIO SIFA ANAYOZALIWA NAYO AMA ANAYOAMBATANA NAYO MTU. Anayeonekana kuchezewa hapa, anaweza kuolewa pale na akawa bora kuliko anavyodhaniwa. Kwenye ndoa (poleni ambao hamjazionja) kuna mengi ya kujifunza (kama utakuwa tayari kjifunza) na kama ilivyo kwa kitu chochote kile kihusichacho mtu zaidi ya wewe mwenyewe, kuna kupoteza kitu il uongeze kitu" Na hii yaweza kuwa muda, fikra, upendo, michezo na mengine mengi.
Kwa hiyo asiye tayari kukubaliana na UZURI wa alie mbele yake anaweza kudhani huyo ni wa kuchezea na ni kwa kuwa hajaamua KUPOTEZA FIKRA HIZO ili aweze KUONGEZA FIKRA ZA UZURI WA NDANI ALIONAO ALIYE MBELE YAKE basi atakaa kutotambua thamani ya kilichopo mbele yake.
Hakuna mtu anayeweza kuonesha UZURI WAKE HALISI kwa yule ambaye hana hakika kama ni wake na hakuna anayeweza kutoa kla alichonacho kama hadhani anaweza kuwa salama asipobaki na kitu.
Kwangu kusema kwa "ni wa kuchezea" ni kujidhihirishia kuwa huna uwezo wa kusoma kilicho ndani ya aliye mbele yako.
Na ndoa njema ni ile ambayo Mume na Mke wanajuana mapungufu yao na wanaweza kuwianisha kwa kusaidia wakijua ni wapi pa kumsaidia nani ili awe anavyotaka kuwa. HAKUNA ALIYEKAMILIKA na sote hatuna mapungufu ya aina moja. Kwa maana nyingine ni kuwa ukiwa na mtu , na ukabahatika kukuta wewe ni jasiri katika mapungufu yake na yeye ndiye jasiri katika mapungufu yako hapo utakwa umepata MATCH ambayo itadumu. Lakini kabla hamjajuana hivyo, ni lazima kudhihirishiana na katika "stage" hii ndipo mmoja anapodhani yu-zaidi ya mwingine na kusema huyo hamfai na hawezi kumuoa ama kuolewa naye hivyo ANAMCHEZEA TUUU.
Kama una uhusiano ama unataka kuoa ni lazima ukmbuke kuwa wanasema ndoa inakupa maximuma 80% ya ulichotaraji (kama utawekeza) na nyingine 20% utaziona nje. Suala ni kujitahidi kuchukua hizo 20% kuziweka ndani ya 80%, lakini mara nyingi tunaona watu wanaacha 80% na kukimbilia 20%. Wakitambua hilo, ni KILIO CHA MBWA (MDOMO JUU). Ndio maana mapenzi ya "kimada" huvutia ukiwa na mke na ukimuacha na yeye "anatema".
Ni upungufu wa fikra.
Naacha
PASSION4FASHION.TZ said...
Yasinta hakika leo umeamua kusema,hakika mada ya leo kiboko,haipendelei upande wowote mmm! kama mdau mmoja kasema speechless,sina la kuongeza nitaharibu.
mumyhery said...
kumbe!!!
Yasinta Ngonyani said...
Kwanza nnapenda kusema nimeyapenda sana maoni yenu.Na ninawapendeni wote.
Ni kweli hii mada imekuwa si ya kubagua, nimeandika kwa kuangalia pande zote. Kwani mara nyingi wengi wengi wamekuwa wakisema napendelea upande mmoja.

Nawashukuru wote kwa mchango wenu nami nimezidi kujifunza mengi toka kwenu ambayo sikujua. Ni kweli hakuna hapa duniani aliye sawa kabisa, kila mtu ana kasoro yake.
Ni kweli pia ukiwa na sura nzuru na umbo zuri kazi kwelikweli. lakini mimi sioni kama kuna watu WABAYA na WAZURI. Kama nakumbuka vizuri muimbaji mkongwa dr. Remmy Ongala aliimba kama wewe ni mbaya basi oa mke mbaya na kama wewe ni mzuri basi ou mke mbaya. hapo utakuwa umepunguzi mgogoro wa kusema mimi MZURI na mimi MZURI.

Na mwisho napenda kumjibu kaka Ramson! kwanza asante kwa swali, pili asante kwa sifa uliyonipa, tatu hizo picha zote ni mume wangu ndiye mpigapicha wangu, nne katika ndoa yetu kuna neno liitwalo KUAMIANA. Kuporwa siku moja.....Lol.

karibuni tena na tena !!!!!!
Chacha Wambura said...
Da Yasinta (of course na wadau wengine), hivi yule mwanamziki aloimba ule wimbo ulopigiwa kelele saaaana kuwa 'wanawake wazuriwazuri wameolewa wamebaki manungaembe' alikuwa na maana gani?.

Kwa mujibu wa maada yako wazuri hawaolewi na kwa mujibu wa muziki huo wazuri ndo wanaolewa. Mbona nachanganyikiwa?

Mnijuze wajameni!!!

Tumalize mwezi na maswali haya Je? uliwahi kuzitumia hizi? ama kuziona tu?

Shilingi Mia moja
Na shilingi mia moja tena.
Penye wengi hapaharibiki kitu, ina wezekana ulitumia kwa kutumwa dukani... na labda kuna walioziona tu...!!!! NAWATAKIENI MWISHO WA MWEZI MWEMA:-)

Monday, November 29, 2010

Nyumbani ni nyumbani...


Nadhani wote tumeianza Jumatatu vizuri, binafsi nipo salama na siku yangu imeanza vizuri na ninamshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa kunilinda na nimeiona siku ya leo.

Sunday, November 28, 2010

LEO NI JUMAPILI YA KWANZA YA MAJILIO/IDAG ÄR FÖRSTA ADVENT!!!!!

Jumapili ya kwanza ya majilio/Först Advent!!!

Nimeipenda sala hii ya kaka Baraka Chibiriti na nimeona ni vizuri kuitumia jumapili hii ya leo.Ukizingatia ni jumapili ya kwanza ya majilio haya hebu tusali kwa pamoja.

Nia yangu naileta kwako Bwana Mungu wangu, nakuomba Bwana unisikie ninalia kwa uchungu. Nakuomba uipokee sala yangu, sikiliza na sauti ya kilio changu. Ninajua Bwana siku zote wewe hupatikani kwenye gasia, ninajua siku zote wewe hupatikani kwenye vurugu.
Bwana nijaie utulivu wa moyo na nipe nguvu nimshinde mwovu shetani, shusha roho wako anipe faraja. Bwana niongoze ili nitimize nia yangu ya kuwa mtumishi wako mwema!

Ee Bwana upo wapi mimi ninakutafuta, nitazame kwa huruma nateseka Mungu wangu...nakuomba uipokee sala yangu na uisikilize sauti ya kilio changu.
Hata kama nipo kama takataka mbele za watu...lakini mbele yako mimi nina thamani kubwa sana siku zote, kwa hili niajua na ninauhakika kwamba wewe pekee ndiwe wenye kunithamini, nakuomba uipokee sala yangu na uisikilize sauti ya kilio changu.
Ee Bwana wangu nijalie nikabili njia zangu, nimshinde huyu mwovu shetani hanifai kabisa. Bwana Mungu wangu wewe ndiwe tegemeo la maisha yangu yote hapa Duniani, nitausifu na kuku tegemea wewe daima siku zote za maisha yangu!

Saturday, November 27, 2010

UJUMBE WA JUMAMOSI YA LEO!!



Halafu angalia/sikiliza na hii hapa kaaazi kwelikweli

Friday, November 26, 2010

Je umewahi kuona Maajabu haya hapa ni Njombe: Mwamba Wenye Ramani ya Afrika

Mwamba huu wenye ramani ya bara la Afrika unaitwa Lwivala, upo katika pori la hifadhi ya msitu Lwivala kijiji cha Igodivaha Wilaya ya Njombe, inaweza isiwe rahisi kuamini lakini huo ndio ukweli wenyewe. Picha kutoka Mjengwa.

Ijumaa njema!! UHURU, hivi ni lini mtu anakuwa huru???



Wimbo huu kila nikiusikiliza napatwa na furaha lakini pia napatwa na huzuni kiasi kwamba natokwa na machozi. Sijui wenzangu pia mnajisikia hivyoo:-( HATA HIVYO NAWATAKIENI MWISHO WA JUMA MWEMA !!!!!!!

Thursday, November 25, 2010

UTAFITI: KUNYONYESHA HUZUIA KANSA YA MATITI KWA ASILIMIA 25-60

Tusiacha kunyonyesha vichanga wetu jamani
Mara nyingi nimekuwa najiuliza hivi kwa nini akina mama hapa hawapendi kunyonyesha watoto wao. Utakuta mtoto ana miezi mitatu amekwisha achishwa kunyonya. Anapewa hii mipira (kidanganyio) kutwa nzima kisa eti akima mama wanaogopa matiti yao yatakuwa kama chapati....kwa mimi wala sielewi kabisa . Ebu soma hii makala hapa chini.......
Ambayo nimeipata kutoka kwa kaka Matondo nikaona si mbaya kama tukijikumbusha na pengine kuna waliokosa kuisoma.
----------------------------------------------------------------------------------------------
Mbali na ukweli kwamba kunyonyesha ndiyo chanzo cha lishe bora kabisa kwa mtoto, wanasayansi sasa wanadai kwamba kunyonyesha pia kunaweza kupunguza uwezekano wa mama kupata kansa ya matiti kwa asilimia 25 hadi 60.

Hizi ni habari njema kwa akina mama wa Afrika ambao kimsingi huchukulia kunyonyesha kama mojawapo ya wajibu wao baada ya kupata mtoto. Pengine hii inaweza kuwa ndiyo sababu iliyofanya saratani ya matiti isijidhihirishe sana Afrika.

Wasiwasi wangu ni juu ya kizazi kipya ambacho kinaiga mambo ya Kimagharibi kwa pupa. Nimeshasikia kwamba mabinti wengi sasa hawana hamu tena ya kunyonyesha vichanga vyao wakichelea kuharibu matiti na miili yao. Ukijumlisha na vitu vingine vinavyoingia Afrika vikiwemo vyakula vilivyolimwa "kisayansi", madawa na mabadiliko mazima ya mfumo wetu wa maisha, sitashangaa kama kansa itafumuka na kuwa ugonjwa wa kawaida tu muda si mrefu ujao. Hili likitokea, atakayefaidika bila shaka ni makampuni ya madawa ya nchi za Kimagharibi - na naamini kwamba hiki ndicho wanachotaka. Tuweni waangalifu na tuache mambo ya kuiga vitu kiholela bila kuelewa hasa kiini chake.
Ukitaka kusoma zaidi gonga hapa.

Tuesday, November 23, 2010

Ni muhimu kufanya mazoezi !!!!

Ni muhimu kufanya mazoezi, ni kwamba unauweka mwili wako safi na pia unaepuka ma magonjwa madogo madogo.Bibi anasema, usidhani wewe tu unaweza , hata mimi naweza usidhani umri ni kitu ha ha ha ha:-)!!!! Mmmmmhhh!! nawaza kwa sauti hivi huyu bibi ana mifupa kweli?




Monday, November 22, 2010

MAONI YA MTAKATIFU SIMON KITURURU KUTOKA KWENYE MADA/PICHA YENYE KICHWA CHA HABARI:- NIMEUPENDA UBUNIFU HUU!!

Ya nini kupoteza pesa kuwanunulia watoto vifaa vya kuchezea wakati inawezekana kutengeneza. Yaani hapo vitu vunavyohitajika ni dungu baada ya mafita ya kula kwisha, mwanzi, ndala zilichoka kwa ajili ya matairi bila kusahau ufundi. Haya basi kimbia gari halimgoji mtu Erik ndiye dereva ...tena bei nafuu kabisssssaaaaaaaaaaaaaaa-
natafuta kitoweo kwa manati:-)
Nimeyapenda maoni haya ambayo yanasemaukweki wa sasa na ule wa zamani. nakumbuka wakati nilipokuwa mdodo/kabinti nilikuwa nabeba kigunzi au kile kilixhokuwa kwenye mkungu wa ndizi kama mtoto. Zamani tulikuwa hatununuliwo vitu kama sasa. Ukitaka kujikumbusha ni picha gani basi bonyeza ubunifu. Ahsante sana Mt. Simon Kituiruru- Na hivi ndivyo alivyoanza mt. Simon:-

Si utani! Ubunifu ni muhimu!

Tatizo kiitwacho maendeleo kinafunda watu wengi tu kuwa ujanja ni kununua na ununuacho ghali zaidi ndio ushahidi wewe mjanja zaidi au tu Bab KUBWA kuliko ukiwa unatatua mambo mwenyewe kiubunifu wako mwenyewe.

Kwa mfano siku hizi BONGO(mijini) unakuta hata manati watoto wanataka wanunuliwe.

Ukilinganisha na enzi zetu ukipenda kuchezea magari unajitengenezea kwa waya au hata makopo na ikibidi unaiba ndala nyumbani ukachonge matairi ikiwa ni kutatua tu tatizo la kutaka kucheza gari kibunifu ambalo unajua Mzazi anaweza asikununulie.

Tunako kwenda sijui nini kitatokea kama ubunifu ni jinsi ya kununua na wapi pa kununua wakati mengi tu unaweza kubunia na kutatua mwenyewe.

Fikiria hata chakula kwenye menu za bongo ubunifu ni hafifu sana. Ni yale yale CHIPSI mayai, ugali kwa maharage na kadhalika... wakati kibano kilitakiwa kitengeneze ubunifu kama kibano cha uhaba wa chakula kilivyowaletea ubunifu wa PIZZA kwa Waitaliano masikini.


Nawaza tu kwa sauti!