Tuesday, December 27, 2016
BARABARANI SEHEMU FULANI MKOANI RUVUMA ...JE? UNAJUA WAPI?
Thursday, October 3, 2013
ZILIPENDWA...UNAWAFAHAMU WATU HAWA AU UNAJUA HAPA NI WAPI?
Wametulia hapo bila wasiwasi inaonekana ni mahali pazuri na penye utulivu...Haya karibuni kufumbua fumbo la leo....:-) Sijui itakuwa mwaka gani hapa????
Wednesday, April 21, 2010
Ngoja leo tuangalie baadhi ya Vitendawili/Mafumbo = Gåtor
KISWIDI:- Vad kan gå men inte springa?
KISWAHILI:- 2. Wakati tunapokuwa nje na miguu yetu tunajion kweli tupo ndani. Ni nini hicho?
KISWIDI;. Först när man är ute med fötterna är man riktigt inne. Vad är det?
KISWAHILI:- 3. Ni nini kinakuwa kikubwa na kikubwa zaidi wakati unataka kitoke/kukitoa?
KISWIDI:- Vad är det som blir större och större ju mer man ta bort?
KISWAHILI:- 4. Ni kitu gani cheusi na cheupe na kina miguu 236 na kinaruka angani/hewani?
KISWIDI:- Vad är det som är svart och vit och har 236 ben och flyger i luften?
KISWAHILI:- 5. Hivi kwa nini tunanunua nguo?
KISWIDI:- Varför köper vi egentligen kläder?
Monday, November 9, 2009
VECKANS GÅTA= FUMBO LA WIKI HII
Vad är det som har fyra ben på morgonen,
Två ben på dagen och tre ben på kvällen?
KISWAHILI:-
Ni nini ambacho kina miguu mnne asubuhi,
Miguu miwili mchana na miguu mitatu jioni?
Je? Jibu lake ni nini?
Monday, July 13, 2009
FUMBO UFUMBIWA MJINGA
Aaah wapi, mwisho wake lini mbona...
A-a-, mtani sikiza nikwambie, kwetu tumezaliwa ndugu kaka na dada, na kwa bahati, mzee wetu alikuwa na shamba lenye mali mingi, mifugo hene hene na ardhi yenye tuvimawe tudogo tudogo na thijakwambia tena tune visima vyenye maji chumvi na maji poa. Asa siku moja kadogo kangu 'Nkiki Iki' katundu sana hako, kakawa kanachimbua vijiwe na kwenda kuchezea mabento na watoto wa jirani zetu. Mzee 'Miiwi Alewode Soni', babake mtoto wa jirani, akaviona vile vijiwe, basi akamwambia Nkiki 'uwe unavichimbua na kuvileta muchezee halafu atakayemmanga mwenzie mi ntambadilishia nimpe gololi'. Ikawa ndo mchezo wao. Sa kumbe Mzee wetu akamstukia Nkiki ndo akamkamata Nkiki na siye wote akatuketisha chini akatwambia 'iwe marufuku kuchimbua vijiwe vile. Wakati wake bado na aliviacha kwa makusudi'. Ndiposa akatupa siri kuwa tule tivijiwe bwana kumbe mzee Miiwi (babake na mtoto wa jirani) alikuwa akivifanyia biashara Ng'ambo. Mzee akatwambia kuwa tule tujiwe tofauti na mazao ya nafaka, huwa hatuozi tule, hivyo hutwo utatufwaa sana kwa biashara tukishakuwa na akili mukichwa na ikiwa shughuli za mifugo ama nafaka itakuwa haikidhi mahataji yetu. Zaidi sana alitaka tujue jinsi ya kushirikishana na wadogo zetu na familia yetu yote ya baba mkubwa, mamdogo na shangazi hadi kijiji kiuzima tuviuze ili wote tuwe angalao na ubora fulani wa maisha. Aliamini hivyo kwa dhati marehemu Mzee wetu.
Mzee alituhenyesha kwenye elimu na akahakikisha tunasoma kweli kweli, yaani hata na wazee wenzie kijijini alihakikisha wanapelekwa shule kwa mwendo wa PUGU (Pata Ujuzi Gawia Umma). Lakini alitusisitizia pia kuwa elimu izingatie kilimo, mifugo, uvuvi na viwanda ghafi kwa sababu bado ni mali sana hivo, na vile vijiwe vibakie tu maana haviozagi hivo.

Kwa bahati nzuri ama mbaya, Mzee wetu aliugua na akafariki katika umri wa KiBiblia kama alivyojikadiria mwenyewe, sasa kumbe kaka zangu na dada zangu walikuwa wanamwonaga Mzee wetu mwanga na kauzibe flani katika mipango yao. Unaambiwa ile Mzee anakata roho tu, kwanza wao wakaanza na kuandaa zinga la sherehe kisha wakasherehekea kivyao kwa siri, alafu ndo wakaandaa bonge la mazishi na kwenye maziko wakihakikisha wanaweka sementi na kofuli kwenye kaburi la Mzee ili asijenyanyuka; si walijua fika kuwa makamuzi waliyopanga kuyafanya yanaweza kumwamsha Mzee kutoka ufuni?
Sasa mtani wewe ikiwa umeshawakalisha kaka zako na ndugu zako chini na ukawaita Wazee ili mzungumze kuhusu dhuluma wanazokufanyieni ninyi ndugu zao wa kuzaliwa damu moja wachilia mbali wale watoto wa shangazi, mjomba na kijijini, na Wazee waliokua na Mzee wetu hawasikiii, eeeh, yaani woooote ninyi mmegeuka kuwa ombaomba na hamjui kesho itakuwaje, eeeh, kaka zako na dada zako baada kusomeshwa na Mzee na kuachiwa urithi wamegeuka kuwa watoto wa mjini yaani siku hizi wao wanavaa kata-k, pullneck wananunua vitu supamarkiti, vekesheni udosini, watoto wao hawasomi tena Kamachumu, ninyi wadogo zao shule hamuioni na kama Mzee aliwaacha ndo mpo Sekondari mjue Chuo Kikuu mtaishia kukisikia tu, na kama mna watoto ndiyo hata haijulikani mliwazaa kwa sababu ipi, we unafikiri we uta...
..kwanza zamani si Mzee alikuwa anasema ni marufuku kufunga milango ya vyumba vyenu kwa kuwa sisi sote ni ndugu siri ya nini? Basi alipoitwa na Mungu tu, kaka zako na dada zako wamevuruga utaratibu siku hizi hata kupita korido ya nyumbani kwenu ni kwa mahesabu maana ukikaribia mlango tu ni kula mbata kwa kwenda mbele. Yaani umewekewa kauzibe huwezi kukaribia hata kizingiti cha chumbani labda uwe na cheti maalum! Cheti maalum cha kumwona kaka yako au dada yako tena kwa ruhusa maalum kutoka kwa Sektretari wake ambaye ni kutoka kijiji cha jirani. Kuingia chumbani kwao tena kama ilivyokuwa zamani kabla Mzee hajafariki ni ndoto tena macho yako uyageuzie kule mbali kila unapopita kuelekea kibarazani.
Sasa mtani, kweli kwa hali hiyo wewe utaendelea kuwa wa kawaida? Uvumilivu huo uwe labda umetunukiwa na Mwenyezi Mungu lakini kama ni mtu wa kawaida kabisa kabisa kama mdogo wangu mwingine 'Ote Kilemie Mnu' aliyefikwa na maji ya shingo, walahi nakuhakikishia akikujia nanihii akakwambia hii ishu ndogo sana kwangu naweza kuwasubiri kaka zako na dada zako siku moja wamekutana pale kwao kama kawaida yao WaChagga kuhiji kila Krismasi basi nasubiri wakitoka Kanisani wameshakula, wakati wanaendelea na mbege zao wakiteremshia na ndafu mi nawatumia salam kupitia vijana wangu, mtani we hapo utawaza mara mbili wewe?
We acha wewe mtani wangu! Mi nlivyowaza kuhusu maswahibu yangu basi ndiyo sababu iliyonifanya niwaze kununua bastola japo sijui kitako na kichwa vinatofautianaje. Ni mengi yamenichosha. We fikiria mtu unaposhindwa kutofautisha kati ya raha na karaha aisee, we unafikiri...
...ebu kwanza subiri kidogo kuna mdundiko unapita hapa sijui mtoto wa nani wanamcheza leo, hizi ni raha ndogo ndogo mtu huwezi kuziacha zipite hivi hivi. Yana mwisho haya! Na pia napenda kusema asante Da Subi kwa mada hii.
Monday, December 8, 2008
MAPENDO NI KITU GANI?:-INAENDELEA
Kuna mifano mingi ya upendo wa kweli katka maisha ya kila siku. Kuna upendo wa baba unaojihakikisha kwa kumpeleka mtoto wake mgonjwa hospitalini. Baba anapaswa kutembea porini maili kumi na tano bado baada ya safari ndefu, lakini baba anasukumwa na upendo, anapata nguvu na ananuia kufika hospitalini. Wala hawezi kusema, “Inatosha sifanya zaidi ya hapa.”
Kuna pia upendo wa mama ambaye kila siku huleta faraja, nguvu na kitulizo kwa watoto wake.
Upendo wataka kukua
Upendo ni kama uzima. Wote tunajua ya kwamba mungu ndiyo chanzo cha uzima wote. Uzima, unaishi, unakua na kubadilika. Hivi ndivyo upendo ulivyo. Ni lazima utiririke na kukua. Ni budi uenee, utafute maeneo na mahali papya pa kusitawisha na kutajirisha. Upendo upo kwenye matengenezo wakati wote. Tunajua upo, lakini kila mara unahitaji kufanywa upya na kukua. Kama sivyo upendo unakufa.
Ufanyacho upendo
Upendo kidogo ni kama jua, ambalo ni rafiki yetu wa daima. Hufukuza baridi, huimarisha mazao yetu na kuyaivisha. Hivyo ndiyo ufanyavyo upendo, kama jua. Katika kupendana, yule mwenye kupendwa hubadilika. Anabadilishwa kutoka hali ya mashaka, wasiwasi, hofu, upweke na kutoamini, anakuwa mtu mwingine kabisa. Mwanzoni alikuwa mwenye hofu na mashaka, sasa ni mwenye kujiamini na kuthubutu kutenda. Badala ya uchungu na upweke, imekuwa furaha na heri. Ni kama nyoka abadilishaye ngozi yake ya zamani kwa wakati fulani, na kubaki na ngozi mpya. Kwa upendo aliopata mtu huyu amafanywa kuwa mpya.
Mara nyingi twasikia watu wakisema, “Huyu mvulana anampendaje msichana huyu?” au , “nini cha kuvutia alichonacho Bwana huyu?” Haina maana kuuliza kwa nini twampenda mtu mwingine. Kama ni mapendo kweli,hatumpendi mtu kwa kuwa ana vitu fulani vya kuvutia wala hatumpendi ingawa ana kasoro, bali tunampenda mtu aliye ndani ya yote haya.
Upendo: fumbo la ajabu
Kama nilivyosema juu ya upendo kuwa ni kutoa nafsi yako. Hii bado haielezi kikamilifu maana ya upendo. Kwani upendo ni fumbo la ajabu. Ni fumbo kwa sababu maana yake ni nzito mno hata kika siku tunajifunza kitu zaidi juu yake.
Na kwa kweli, tunaweza kupata maana kamili ya upendo kutoka kwa Mungu peke yake ambaye Neno lake latuambia:-
Upendo huvumulia, hufadhili,
Upendo hauhususu,
Upendo hautabakari, haujivuni
Haukosi kuwa na adabu, hautafuti mambo yake,
Hauoni uchungu, hauhesabu mabaya
Haufurahi udhalimu, bali hufurahi pamoja na kweli,
Upendo huvumulia yote, huamini yote, hutumaini yote na husatahimili yote.