Ni shule ya msingi kijijini kwetu Litumbandyosi
Showing posts with label shule. Show all posts
Showing posts with label shule. Show all posts
Wednesday, July 10, 2019
Tuesday, July 25, 2017
ELIMU:- WAZAZI TUNAFIKIRI WATOTO WANAPATA ELIMU KUMBE WANAFANYA MIRADI KUINGIZA FEDHA KWENYE MFUKO WA SHULE...
Tutafika kweli kwa mtindo huu? Nimekumbuka mbali sana wakati ule nasoma shule ya msingi, kubeba tofali, kulima mashamba, kukata nyasi, kusomba kuni nk. aise kwa kweli tumehinya sana miaka ile...
Wednesday, March 12, 2014
SEHEMU FULANI TANZANIA :- TWENDEN WADOGO ZANGU TUTACHELEWA NAMBA....
Picha hii imenikumbusha enzi hizo:Amka, amka kumekucha x2 Twendeni shuleni. au Panda, panda panda, panda mlima panda panda.....hapo mtu ulishaoga na sasa josho linakuvuja tena ...Duh kaazi kwelikweli....Je? hapa ni mazingira ya wapi katika Tanzania yetu?
Tuesday, November 26, 2013
TULIO WENGI TUNAKUMBUKA HIKI NI NINI!!!
Lakini wengi nadhani tunakumbuka vya matete...ni vihesabio/kalukuleta za zamani hizo. Hicho ni kihesabio cha dada Camilla wakati akiwa Mdunduwalo/Ndirima shule ya msingi na ni baba yangu katengeneza. Ametengeneza kwa visoda. Je? wewe umewahi kutumia vihesabio vya aina hii?
Monday, June 17, 2013
LEO TUANZE JUMATATU NA KUANGALIA SHULE HIZI ZA KATA YA WINO TARAFA YA MADABA WILAYANI SONGEA!!!
Ifinga ni kijiji ambacho kipo kata ya Wino kutoka barabara kubwa kama inavyoonyesha kwenye kibao ni km 48. Kijiji hiki kinajulikana sana kwa kilimo cha mpunga na machungwa...Mwaka 1992 tulifanya safari mpaka Ifinga tulichukua chumvi nasi tulipata machungwa mengi sana . Kijiji hiki wanakula sana wali hakuna ugali. Ninachoshangaa mwaka ule kulikuwa hakuna hata shule sasa leo napita hapa naona kibao Ifinga Matumbi Secondary school..nikaona ni lazima nipige picha..najiuliza sijui ni maendeleo au ili mradi kila kijiji kiwe na shule?
Kwa sababu mwanzo kulikuwa na shule yetu hii Wilima ndiyo ilikuwa ya kata. Lakini nayo sasa imeendelea na kuwa High school. Nakumbuka mengi sana kuhusu shule hii....Wilima Sekondari. Kuna nyingi kumbukumbu zinazowahusu watu wengi...Jumatata njema....
Kwa sababu mwanzo kulikuwa na shule yetu hii Wilima ndiyo ilikuwa ya kata. Lakini nayo sasa imeendelea na kuwa High school. Nakumbuka mengi sana kuhusu shule hii....Wilima Sekondari. Kuna nyingi kumbukumbu zinazowahusu watu wengi...Jumatata njema....
Monday, March 5, 2012
JE? HAPA BORA ELIMU AU ELIMU BORA?

Ama kweli maisha ni kujitegemea nikawa najisemea mwenyewe!!! Halafu nikawa najiuliza kweli hawa wanafunzi watasoma kweli au watakuwa wanafikiria jinsi ya kuanza kupika? halafu pia kusoma bila kula nako si vizuri.....maswali mengiiiiiiii....tujadili pamoja...
Monday, August 29, 2011
NYIMBO ZA MCHAKAMCHAKA/KUMBUKUMBU

Wednesday, September 8, 2010
NIMEMALIZA SHULE!!!

Vijana hawa wananikumbusha siku tuliyokuwa tukiisubiri kwa hamu kubwa sana, 'kumaliza shule' tukiamini ati baada ya kuondokana na adha ya kudamka alfajiri, kushikana mashati na 'konda', kuwahi 'namba' na 'mstarini'... yaani ndoto za kila aina alimradi kujiaminisha usumbufu utakuwa umekwisha kabisa.
Tulijiona sisi ndiyo 'top' hakuna mwingine duniani kama sisi. Hisia za 'kumaliza shule' na kubaki nyumbani wakati wengine wanaamka asubuhi wakiwa na heka heka za ama kwenda shuleni au kazini, zilitutawala.
Siku hizi, tofauti na zamani nilipomwona 'madha mnoko', huwa najivuna sana kuwa na Mama asiye na longolongo wala 'kukopesha maneno' kwani, aliponisikia nikijitapa eti 'nimemaliza shule' siku moja aliniambia,
"...wewe, umemaliza shule ipi? Subi, hujamaliza shule. Umehitimu Elimu ya Msingi tu. Umeimalizaje shule wakati hujafika hata Sekondari? Umesahau methali mlizofundishwa, Elimu ni bahari; Elimu haina mwisho? au ulidhani ukishakariri na kuandika kwenye daftari ukafunga na ulichofundishwa kimefungwa kwenye mkoba? Yaani mwalimu akishafuta ubao na kwenye akili yako vinafutika? (kichwani mwangu nawaza, 'kwani si ndiyo kazi ya shule? unaandika, mnakusanya madaftari, mwalimu anatia 'pata' kama hesabu umekosea fanya masahihisho tu, basi').
Umevuka madarasa ya shule ya awali, sababu ya kuitwa 'msingi' ni kwa kuwa umeweka msingi wa elimu na maisha yako. Ni sawa na kujenga nyumba. Ili iweze kusimama imara, lazima msingi uwepo, tena uwe ni msingi ulio imara. Msingi ndiyo kigezo cha uimara wa nyumba. Umeweka msingi, bado kuta, madirisha, paa, na fenicha na vifaa vingine vya ndani. Lakini la muhimu ni msingi. Ikiwa uliweka msingi imara, nyumba yako itakuwa imara, utaweza kujenga nyumba kuuuubwa au hata orofa, inategemea na uimara wa msingi wake."
Ni baada ya kwenda kwa Bibi na kuwatembelea ndugu, ninarejelewa kauli ya Mama, 'hujamaliza shule' nhe he, ndipo nilipotia akilini, kumbe tulichokuwa tukifurahia 'standadi seven kumaliza shule' ilikuwa ni furaha ya muda tu, tena ya kitoto, bado ilikuwepo kazi kubwa mbele yetu; Kuna kusaidia kazi za nyumbani sasa zaidi ya wengine na; Kuna kuchukua fomu za shule za "private" tena kujaza zaidi ya moja, na kwa ambaye matokeo ya maendeleo yake shuleni kila mhula hayakuwa mazuri, hali kwake ilikuwa ni mbaya, yaani atazijaza fomu za 'private school' hata tano ili walao abahatishe moja ikiwa atakataliwa kwingineko. Nakumbuka nilizijaza mbili, Majengo Secondary na Uru Seminary. Kisha kuna kufanya tena mtihani wa kuomba kujiunga na shule hizo na, ni lazima ufaulu, la sivyo uaibike kwa kuzurura mtaani na kufanya kazi nyumbani wakati wenzio wanaongozana kwenda na kutoka shuleni! Shabash! Hakuna kumaliza shule!
Naam, huo ndiyo wakati nilipoanza kufahamu kuwa ninayahama maisha ya utoto na kuingia ujanani.
Hongereni vijana mliohitimu elimu ya msingi, shule bado hamjaimaliza. Elimu haina mwisho!
Nimeipenda sana simulizi hii kwani imenikumbusha pia enzi zile namaliza darasa la saba. Ni kweli yaani ile asubuhi kuwahi namba ukichelewa tu viboko hivyo. Halafu kukimbia mchaka mchaka, nakumbuka baada ya mchaka kchaka kulikuwa hakuna tena kuoga maji ni kuaa hivyohivyo darasani na mijasho inakutiririka. Mweeh kwa kweli tunatoka mbali na kweli elimu haina mwiho. Na ukitaka kujua nilipoipata basi unaweza kubonyeza hapa
Thursday, April 15, 2010
Ubakaji unavyodidimiza elimu Karagwe
kubakwa kama hawatopata ulinzi wa kutosha
kutoka kwa jamii
SUALA la ubakaji kwa wanafunzi ni kosa la jinai kisheria na ki jumla linadidimiza maendeleo ya wanafunzi wa kike ambao ni waathirika wakuu.
Wanafunzi hawa huishia kupata mimba au magonjwa mbalimbali hali ambayo huwaathiri kitaaluma na hata na kjamii kwa ujumla. Haja ya kulipinga suala hili hasa kipindi hiki ambacho serikali inapigania kwa nguvu zote haki za mtoto wa kike awapo shule na pindi apatapo mimba akiwa shuleni.
Serikali ilishapitisha pia utaratibu wa kumruhusu mwanafunzi apatapo mimba kurejea masomoni pindi anapojifungua kwa minajili ya kunusuru maendeleo yake kielimu.
Suala la ubakaji katika wilaya ya Karagwe iliyopo mkoa wa Kagera bado lipo juu hivyo kutishia maendeleo ya elimu kwa mtoto wa kike.
Takwimu zinaonyesha kuwa watoto zaidi ya 54 walibakwa katika kipindi cha mwaka 2009, takwimu hizo kwa mujibu wa wakazi wa karagwe wanadai ni ndogo sana ukilinganisha na idadi halisi ya kesi zinazotokea hasa vijijini.
Mbali na ubakaji, wanafunzi kupewa mimba na wengine kuolewa kwa mwaka 2009 pekee walifikia 44 Karagwe ikiwa wilaya ya pili kwa ukubwa wa tatizo hilo ikitanguliwa na wilaya ya Chato yenye wanafunzi 74 waliopata mimba kwa kipindi hicho hicho.
Kwa mkoa wa Kagera kwa ujumla, Katika kipindi cha Januari 2009 hadi Desemba 2009 jumla ya wanafunzi 365 walipata mimba katika kipindi cha Januari mpaka Desemba 2009 kati ya hao wanafunzi 148 walikuwa ni wa shule za msingi na 217 walikuwa wa sekondari.
Wilaya pia ina jumla ya shule za msingi 212, kati ya hizo, shule 204 ni za Serikali na 8 za binafsi zenye jumla ya wanafunzi 105,229 wasichana wakiwa 53,491 na wavulana 51,738.
Shule za sekondari katika wilaya ya Karagwe zipo jumla ya 43 (zikiwemo 34 za serikali na 9 za binafsi). Ongezeko hili limeenda sambamba na sera ya nchi lengo likiwa ni kuchukua ongezeko la watoto wanaomaliza darasa la saba.
Mbaraka Ismaili mkazi wa kijiji cha Kagenyi wilayani Karagwe ambaye mtoto wake wa miaka 14 Fatuma Mbaraka alibakwa na mzee wa miaka 54 Ali Migeyo mwishoni mwa mwaka jana anasema kesi nyingi za kubakwa watoto zinafichwa na kuzimaliza kimila bila kufikishwa mbele ya sheria.
“Kesi za kubakwa wanafunzi hapa kwetu Karagwe zinaishia huko mitaani, aidha wanakubaliana na kumalizana kwa kuoana au kulipana kiasi fulani cha fedha, suala hili linajumuisha uongozi wa vijiji na kata ambao ndio wapo mstari wa mbele kushauri watu wamalizane,†anasema Mbaraka.
Mbaraka pia anasema kuwa “imezoeleka kusikia kesi za wanafunzi kubakwa au kupewa mimba katika maeneo yetu, na hakuna mtu anashangaa hilo, ni tabia mbaya ambayo serikali lazima ichukue hatua ili kunusuru watoto wetu wa kike.†Kwa hapa shule ya msingi Kagenyi tu kwa mwaka jana tulishuhudia kesi tatu za watoto wadogo kubakwa na kupewa mimba, kesi mbili kati ya hizo wazazi walimalizana wao kwa wao kulipana kwa kushirikiana na polisi na ni moja tu ndiyo ilipelekwa mahakamani.
Mbaraka aliwalaumu polisi na viongozi wa vijiji kuwa kikwazo kikubwa katika upatikanaji wa haki za wanafunzi wanaobakwa na wale wanaopewa mimba kwani ndio waliokua mstari wa mbele kuwashawishi wazazi kuyamaliza bila kupelekana mahakamani.
Fatuma Mbaraka anayesadikiwa kubakwa na mzee wa miaka 54 Novemba mwaka 2009, anasema watoto wanaobakwa wengi wao huacha shule kutokana na aibu wanayoipata.
“Mimi mwenyewe baba ndiye ananilazimisha kwenda shule, ila nina mazingira magumu sana kwani kila niendako nachekwa na wenzangu na wananiita mzazi, walimu toka nimebakwa sijawahi kusikia waseme kitu wala kuniita na kuniuliza,†anasema Fatuma huku akitoa machozi.
Mkurugenzi wa wilaya ya Karagwe Consolata Kamuhabwa anasema kuwa tatizo la ubakaji kwa wanafunzi ni sugu ingawa hatua kali zinachukuliwa dhidi ya watuhumiwa pindi wanapofikishwa mbele za sheria.
Kamuhabwa anasema moja ya sababu ya kuongezeka kwa ubakaji kwa wanafunzi ni imani kuwa wanafunzi hawana magonjwa ya zinaa hasa ukimwi, hili ni tatizo kubwa katika wilaya ya Karagwe.
“Watu wengi wanaamini kuwa kumbaka mtu mzima wanajiweka katika hali ya hatari kwa kupata ukimwi lakini kwa mwanafunzi inakua si rahisi kupata magonjwa kama ukimwi,†anasema Kamuhabwa.
Kamuhabwa anatoa sababu zingine zinazosababisha kuongezeka kwa matukio ya kubakwa kwa wanafunzi kuwa ni imani za kishirikina, matumizi makubwa ya madawa ya kulevya kama bangi na pombe kali aina ya gongo.
Anasema “mkuu wa wilaya hii kanali Fabiani Masawe amekuja na mikakati mikubwa ya kutokomeza tatizo hili kwa njia ya adhabu kali, kutoa elimu kwenye vyombo vya habari hasa redio za hapa Karagwe kama radio Karagwe na Fadeco FM ambazo zinasikilizwa zaidi na wakazi wa wilaya hii."
Afisa ustawi wa jamii wa wilaya Mary Kashaija anasema changamoto kubwa inayoikabili wilaya ni wazazi wa watoto wanaobakwa na wale waliobakwa kukaa pamoja na kuelewana kutoyafikisha masuala hayo mbele ya sheria.
“Tabia hiyo inachochea kuongezeka kwa tatizo la ubakaji kwani wanajua hata wakibaka basi watamalizana au kulipa fedha kwa wazazi na hivyo kutochukuliwa hatua, hali hiyo inaturudisha nyuma katika mapambano dhidi ya ubakaji kwa wanafunzi,†anasema Kashaija.
Kashaija alisema "tatizo hili ni kubwa sana, huwezai kaa wiki tatu bila kusikia kesi ya kubakwa wanafunzi,kesi zipo nyingi sana ukilinganisha na zile ambazo hazitufikii, kesi za kubaka na kutokuletwa kwetu ni nyingi kuliko zile zinazoletwa."
Inafikia hatua hata wazazi kuharibu ushahidi kwa kutokutoa ushahidi ili masuala hayo yaishe kwa wao kulipwa, kesi nyingi zinaisha bila adhabu yoyote kwa kukosa ushahidi, hali inatisha kwa kweli lakini tunakabiliana nayo kupitia elimu kwa njia ya vyombo vya habari, alisistiza afisa huyo wa ustawi wa jamii wilaya.
Mkazi wa kayanga wilayani karagwe Ester John alisema kuwa jamii inapaswa kutafakari kwa kuangalia suala zima la ubakaji ili kutafuta ufumbuzi kwani watoto wengi wa kike ndoto zao za elimu zinazimwa kwa tamaa ya baadhi ya wanaume kwa kuwabaka na kuwapa mimba wangali shule za msingi.
“hapa Karagwe tatizo la ubakaji ni kubwa sana mpaka sasa inaonekana kama ni kawaida jambo ambalo linasikitisha kwa kweli, tunaomba serikali itusaidie watoto wetu wanaangamia jamani,†anasema Ester.
Kesi kukosa ushahidi.
Sheria ya Kujamiiana ya mwaka 1998 inaeleza wazi kuwa kufanya mapenzi na mtoto, chini ya umri wa miaka 18 ni kitendo cha ubakaji, kwa kuwa kinafanywa kwa ulaghai na si hiari ya mtoto huyo.
Wanafunzi hawa huishia kupata mimba au magonjwa mbalimbali hali ambayo huwaathiri kitaaluma na hata na kjamii kwa ujumla. Haja ya kulipinga suala hili hasa kipindi hiki ambacho serikali inapigania kwa nguvu zote haki za mtoto wa kike awapo shule na pindi apatapo mimba akiwa shuleni.
Serikali ilishapitisha pia utaratibu wa kumruhusu mwanafunzi apatapo mimba kurejea masomoni pindi anapojifungua kwa minajili ya kunusuru maendeleo yake kielimu.
Suala la ubakaji katika wilaya ya Karagwe iliyopo mkoa wa Kagera bado lipo juu hivyo kutishia maendeleo ya elimu kwa mtoto wa kike.
Takwimu zinaonyesha kuwa watoto zaidi ya 54 walibakwa katika kipindi cha mwaka 2009, takwimu hizo kwa mujibu wa wakazi wa karagwe wanadai ni ndogo sana ukilinganisha na idadi halisi ya kesi zinazotokea hasa vijijini.
Mbali na ubakaji, wanafunzi kupewa mimba na wengine kuolewa kwa mwaka 2009 pekee walifikia 44 Karagwe ikiwa wilaya ya pili kwa ukubwa wa tatizo hilo ikitanguliwa na wilaya ya Chato yenye wanafunzi 74 waliopata mimba kwa kipindi hicho hicho.
Kwa mkoa wa Kagera kwa ujumla, Katika kipindi cha Januari 2009 hadi Desemba 2009 jumla ya wanafunzi 365 walipata mimba katika kipindi cha Januari mpaka Desemba 2009 kati ya hao wanafunzi 148 walikuwa ni wa shule za msingi na 217 walikuwa wa sekondari.
Wilaya pia ina jumla ya shule za msingi 212, kati ya hizo, shule 204 ni za Serikali na 8 za binafsi zenye jumla ya wanafunzi 105,229 wasichana wakiwa 53,491 na wavulana 51,738.
Shule za sekondari katika wilaya ya Karagwe zipo jumla ya 43 (zikiwemo 34 za serikali na 9 za binafsi). Ongezeko hili limeenda sambamba na sera ya nchi lengo likiwa ni kuchukua ongezeko la watoto wanaomaliza darasa la saba.
Mbaraka Ismaili mkazi wa kijiji cha Kagenyi wilayani Karagwe ambaye mtoto wake wa miaka 14 Fatuma Mbaraka alibakwa na mzee wa miaka 54 Ali Migeyo mwishoni mwa mwaka jana anasema kesi nyingi za kubakwa watoto zinafichwa na kuzimaliza kimila bila kufikishwa mbele ya sheria.
“Kesi za kubakwa wanafunzi hapa kwetu Karagwe zinaishia huko mitaani, aidha wanakubaliana na kumalizana kwa kuoana au kulipana kiasi fulani cha fedha, suala hili linajumuisha uongozi wa vijiji na kata ambao ndio wapo mstari wa mbele kushauri watu wamalizane,†anasema Mbaraka.
Mbaraka pia anasema kuwa “imezoeleka kusikia kesi za wanafunzi kubakwa au kupewa mimba katika maeneo yetu, na hakuna mtu anashangaa hilo, ni tabia mbaya ambayo serikali lazima ichukue hatua ili kunusuru watoto wetu wa kike.†Kwa hapa shule ya msingi Kagenyi tu kwa mwaka jana tulishuhudia kesi tatu za watoto wadogo kubakwa na kupewa mimba, kesi mbili kati ya hizo wazazi walimalizana wao kwa wao kulipana kwa kushirikiana na polisi na ni moja tu ndiyo ilipelekwa mahakamani.
Mbaraka aliwalaumu polisi na viongozi wa vijiji kuwa kikwazo kikubwa katika upatikanaji wa haki za wanafunzi wanaobakwa na wale wanaopewa mimba kwani ndio waliokua mstari wa mbele kuwashawishi wazazi kuyamaliza bila kupelekana mahakamani.
Fatuma Mbaraka anayesadikiwa kubakwa na mzee wa miaka 54 Novemba mwaka 2009, anasema watoto wanaobakwa wengi wao huacha shule kutokana na aibu wanayoipata.
“Mimi mwenyewe baba ndiye ananilazimisha kwenda shule, ila nina mazingira magumu sana kwani kila niendako nachekwa na wenzangu na wananiita mzazi, walimu toka nimebakwa sijawahi kusikia waseme kitu wala kuniita na kuniuliza,†anasema Fatuma huku akitoa machozi.
Mkurugenzi wa wilaya ya Karagwe Consolata Kamuhabwa anasema kuwa tatizo la ubakaji kwa wanafunzi ni sugu ingawa hatua kali zinachukuliwa dhidi ya watuhumiwa pindi wanapofikishwa mbele za sheria.
Kamuhabwa anasema moja ya sababu ya kuongezeka kwa ubakaji kwa wanafunzi ni imani kuwa wanafunzi hawana magonjwa ya zinaa hasa ukimwi, hili ni tatizo kubwa katika wilaya ya Karagwe.
“Watu wengi wanaamini kuwa kumbaka mtu mzima wanajiweka katika hali ya hatari kwa kupata ukimwi lakini kwa mwanafunzi inakua si rahisi kupata magonjwa kama ukimwi,†anasema Kamuhabwa.
Kamuhabwa anatoa sababu zingine zinazosababisha kuongezeka kwa matukio ya kubakwa kwa wanafunzi kuwa ni imani za kishirikina, matumizi makubwa ya madawa ya kulevya kama bangi na pombe kali aina ya gongo.
Anasema “mkuu wa wilaya hii kanali Fabiani Masawe amekuja na mikakati mikubwa ya kutokomeza tatizo hili kwa njia ya adhabu kali, kutoa elimu kwenye vyombo vya habari hasa redio za hapa Karagwe kama radio Karagwe na Fadeco FM ambazo zinasikilizwa zaidi na wakazi wa wilaya hii."
Afisa ustawi wa jamii wa wilaya Mary Kashaija anasema changamoto kubwa inayoikabili wilaya ni wazazi wa watoto wanaobakwa na wale waliobakwa kukaa pamoja na kuelewana kutoyafikisha masuala hayo mbele ya sheria.
“Tabia hiyo inachochea kuongezeka kwa tatizo la ubakaji kwani wanajua hata wakibaka basi watamalizana au kulipa fedha kwa wazazi na hivyo kutochukuliwa hatua, hali hiyo inaturudisha nyuma katika mapambano dhidi ya ubakaji kwa wanafunzi,†anasema Kashaija.
Kashaija alisema "tatizo hili ni kubwa sana, huwezai kaa wiki tatu bila kusikia kesi ya kubakwa wanafunzi,kesi zipo nyingi sana ukilinganisha na zile ambazo hazitufikii, kesi za kubaka na kutokuletwa kwetu ni nyingi kuliko zile zinazoletwa."
Inafikia hatua hata wazazi kuharibu ushahidi kwa kutokutoa ushahidi ili masuala hayo yaishe kwa wao kulipwa, kesi nyingi zinaisha bila adhabu yoyote kwa kukosa ushahidi, hali inatisha kwa kweli lakini tunakabiliana nayo kupitia elimu kwa njia ya vyombo vya habari, alisistiza afisa huyo wa ustawi wa jamii wilaya.
Mkazi wa kayanga wilayani karagwe Ester John alisema kuwa jamii inapaswa kutafakari kwa kuangalia suala zima la ubakaji ili kutafuta ufumbuzi kwani watoto wengi wa kike ndoto zao za elimu zinazimwa kwa tamaa ya baadhi ya wanaume kwa kuwabaka na kuwapa mimba wangali shule za msingi.
“hapa Karagwe tatizo la ubakaji ni kubwa sana mpaka sasa inaonekana kama ni kawaida jambo ambalo linasikitisha kwa kweli, tunaomba serikali itusaidie watoto wetu wanaangamia jamani,†anasema Ester.
Kesi kukosa ushahidi.
Sheria ya Kujamiiana ya mwaka 1998 inaeleza wazi kuwa kufanya mapenzi na mtoto, chini ya umri wa miaka 18 ni kitendo cha ubakaji, kwa kuwa kinafanywa kwa ulaghai na si hiari ya mtoto huyo.
Hivyo, kumfukuza mtoto huyo shule ni kumuadhibu kwa mara nyingine, kwani adhabu ya kwanza kapewa na yule aliyefanya naye mapenzi kwa nguvu au kwa ulaghai na kumpa mimba na ya pili ni kufukuzwa shule.
Kesi nyingi za kubaka wanafunzi wilayani Karagwe huisha kwa watuhumiwa kuachiwa huru kutoikana na kukosa ushahidi wa kutosha kwani wakazi wengi hawana mazoea ya kutoa ushahidi pindi kesi zifikapo mahakamani.
Kashaija anasema kesi nyingi hukosa ushahidi kutokana na gharama kubwa za mashahidi kusafiri kutoka kijijini mpaka wilayani kipindi cha kutoa ushahidi jambo ambalo linakatisha tamaa wazazi kutokana na kuelemewa na gharama na hivyo kuamua kulipana bila kufika mahakamani.
“Wilaya hii ni kubwa sana, utakuta mtu anatoka umbali wa kilometa 100 ili kufika mahakama ya wilaya kutoa ushahidi, kutokana na gharama za nauli kutoka huko mpaka mjini, mashahidi hao hushindwa kusafiri na hivyo kesi kuwa na ushahidi hafifu,†anasema afisa huyo wa Ustawi wa Jamii.
Raisi Jakaya Mrisho kikwete na Mkewe Mama Salma Kikwete wamekuwa mstari wa mbele katika kupigania haki za mtoto wa kike kielimu nchini kote huku raisi akiwataka wakuu wote wa wilaya na mikoa kuhakikisha wanakomesha tabia hizi za mimba kwa watoto wa kike.
Mapambano hayo yanaenda na sera ya kumlinda mtoto wa kike inayomtaka mwanafunzi aliyepata mimba kurudi shule na kuendelea na masomo pindi wajifunguapo ingawa wengi wao wamekuwa hawapendi kurudi shule kutokana na kuona aibu.
Kesi nyingi za kubaka wanafunzi wilayani Karagwe huisha kwa watuhumiwa kuachiwa huru kutoikana na kukosa ushahidi wa kutosha kwani wakazi wengi hawana mazoea ya kutoa ushahidi pindi kesi zifikapo mahakamani.
Kashaija anasema kesi nyingi hukosa ushahidi kutokana na gharama kubwa za mashahidi kusafiri kutoka kijijini mpaka wilayani kipindi cha kutoa ushahidi jambo ambalo linakatisha tamaa wazazi kutokana na kuelemewa na gharama na hivyo kuamua kulipana bila kufika mahakamani.
“Wilaya hii ni kubwa sana, utakuta mtu anatoka umbali wa kilometa 100 ili kufika mahakama ya wilaya kutoa ushahidi, kutokana na gharama za nauli kutoka huko mpaka mjini, mashahidi hao hushindwa kusafiri na hivyo kesi kuwa na ushahidi hafifu,†anasema afisa huyo wa Ustawi wa Jamii.
Raisi Jakaya Mrisho kikwete na Mkewe Mama Salma Kikwete wamekuwa mstari wa mbele katika kupigania haki za mtoto wa kike kielimu nchini kote huku raisi akiwataka wakuu wote wa wilaya na mikoa kuhakikisha wanakomesha tabia hizi za mimba kwa watoto wa kike.
Mapambano hayo yanaenda na sera ya kumlinda mtoto wa kike inayomtaka mwanafunzi aliyepata mimba kurudi shule na kuendelea na masomo pindi wajifunguapo ingawa wengi wao wamekuwa hawapendi kurudi shule kutokana na kuona aibu.
Vincent Mnyanyika, HakiElimu (Gazeti la Mwananchi)
Ngoja tumaliza na kumsikiliza dada yetu Saida Karolina wimbo huu (nkyalimuto)
Friday, March 19, 2010
Ijumaa ya leo ngoja tuwasikilize hawa watoto, ni somo shuleni!!
Hapa ni dada Camilla akitupigia Trombone/trombon ni moja ya soma shuleni
Na hapa ni Erik naye akitupigia Violine/fiol =kiswahili fidla ni somo pia shuleni
Monday, February 22, 2010
Siri ya mafanikio Ruhuwiko Sekondari
wakisikiliza hoja kwa umakini
KILA anapotembea shuleni na maeneo mengine mkoani Ruvuma, Mkuu wa shule ya sekondari ya Ruhuwiko, Meja Paul Rugwabuza kifua chake kiko mbele. Kwanza ni kwa vile yeye ni mwanajeshi hivyo lazima awe mkakamavu, lakini pili ni kutokana na matokeo mazuri ya shule anayoiongoza.
Anaonekana mwenye furaha kwa sababu jukumu alilopewa la kusimamia elimu ya watoto katika shule hiyo inayomilikiwa na Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) limefanikiwa kwa asilimia kubwa.
"Kitaaluma shule hii imekuwa ikipiga hatua mwaka hadi mwaka hususani kwa kuzingatia matokeo ya kidato cha cha nne na sita viwango vizuri zaidi vya ufaulu ambavyo shule inaweza kujivunia sana ni vya kidato cha sita kwani tangu shule ianze," alisema Meja Rugwabuza katika mahafali ya tano ya kidato cha sita yaliyofanyika hivi karibuni.
"Mfano mzuri wa matokeo ya mock wa kidato cha sita mwaka 2009 katika Mkoa wa Ruvuma kulikuwa na daraja la kwanza 17, daraja la pili 108, daraja la tatu 84 na daraja la nne walikuwa wanne. Hakukuwa na mwanafunzi aliyefeli hivyo tunatarajia kupeleka wanafunzi wengi zaidi kujiunga na elimu ya juu (vyuo vikuu)."
Mbali ya mock, matokeo ya kidato cha sita mwaka 2006 yanaonyesha mmoja alipata daraja la I, daraja la II walikuwa 15, daraja la III walikuwa saba na mmoja daraja la IV.
Mwaka 2007 wanne walipata daraja la I, daraja la II walikuwa 20, daraja la III walikuwa 18, daraja la IV walikuwa sita; na mwaka 2008 mmoja amepata daraja la I, daraja la II walikuwa 30, daraja la III walikuwa 36 na daraja la IV walikuwa 13.
Hata nafasi kitaifa, Ruhuwiko huwa inashika nafasi nzuri. Mathalani mwaka 2006 shule ilishika nafasi ya 16 kati ya shule 57, mwaka 2007 ilishika nafasi ya 38 kati ya shule 230 hivyo iko ndani ya malengo kusudiwa ya maendeleo ya shule.
Takwimu hizo za kitaifa ndizo anajivunia Meja Rugwabuza aliyerithi mikoba ya mtangulizi wake Meja Celestin Mwangasi (amehamia Makongo Sekondari) kuiongoza shule hiyo iliyoko kilomita nne kutoka Songea mjini.
Mbali ya uwezo wa darasani, imeelezwa wana nidhamu nzuri na mitihani yao ya ndani wamekuwa wakifanya vizuri kwa viwango vinavyokubalika.
Matarajio ya baadaye ya Ruhuwiko, Meja Rugwabuza anasema yamo katika mpango wa maendeleo ya shule wa miaka tisa (2006-2015) unaotilia mkazo mambo mengi ambayo ni pamoja na upatikanaji wa maji safi na salama kwa afya za wanafunzi, walimu na wafanyakazi.
Katika kukabiliana na tatizo la utoro wa wanafunzi na kuondoa visingizio vya hapa na pale shule imeendelea mazingira ya shule kwa kuongeza bidhaa kwenye duka la shule, kujenga kibanda cha kutengeneza nywele, kuweka uzio kwenye bweni la wasichana na kumalizia pia bwalo la chakula kwa wanafunzi wa bweni.
Shule hiyo iliyoanzishwa mwaka 1995 inatoa elimu ya sekondari kwa vijana wote kuanzia kidato cha kwanza hadi cha sita na kwa kuzingatia umuhimu wa maendeleo ya teknolojia ya mawasiliano wameajiri walimu wawili wenye diploma hivyo kuwa na walimu watatu. Matarajio yao ya hivi karibuni ni kuanza kufundisha hata watu wazima muda wa jioni.
"Vijana wengi wanaomaliza kidato cha sita katika shule hii wanajiunga na vyuo vikuu na taasisi nyingine za elimu ya juu.
Pamoja na kujivunia mafanikio hayo shule pia inawawezesha vijana kukabiliana na umasikini kwa kutoa elimu ya ujasiriamali na kompyuta ili mwanafunzi anayehitimu katika shule hii aweze kukabiliana na mazingira yanayomzunguka," anasema Meja Rugwabuza.
Pamoja na mafanikio hayo shule hiyo inakabiliwa na changamoto mbalimbali katika uendeshaji na utekelezaji wa mipango yake ya maendeleo ikiwemo tatizo la kukatika mara kwa mara umeme hivyo kusababisha shule kutumia jenereta. Kutokana na gharama za mafuta kupanda imeongeza gharama za uendeshaji.
Changamoto nyingine ni ujenzi wa ukumbi wa mikutano na mitihani ambao huo uko katika hatua za awali. Nguvu kubwa ya vifaa na fedha inahitajika kwani shule peke yake haiwezi kumudu kwa muda mfupi.
"Tatizo jingine ni kupanda kwa gharama za uendeshaji kutokana na kupanda sana kwa bei ya chakula na vifaa. Hata hivyo, shule imejitahidi kuepuka kupandisha sana gharama za malipo ya ada ili lengo la kuwapatia elimu watoto wengi zaidi liweze kufanikiwa," anaeleza Meja Rugwabuza.
Japo shule hiyo inakabiliwa na changamoto hizo na nyingine kadhaa zinaoendana na uboreshaji wa elimu, Ruhuwiko haijatetereka katika utendaji wake na mfano mzuri ni matokeo yake ya mitihani ya taifa ya kidato cha sita kwa miaka mitatu mfululizo. Matokeo hayo yamechangia kwa kiasi kikubwa kuwafanya watu wengi kuvutiwa na elimu ambayo inatolewa na shule hiyo.
Meja Rugwabuza anasema mafanikio ya shule hiyo kwa kiasi kikubwa yanatokana na ushirikiano mkubwa uliopo baina ya walimu, wafanyakazi, wanafunzi pamoja na wanajumuiya wa shule hiyo akiwemo Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini Dk Emmanuel Nchimbi.
Dk Nchimbi amekuwa na mchango mkubwa katika maendeleo ya shule hiyo hususan kwa misaada yake ya mabati na saruji. Aliipatia shule hiyo mabati 240 na saruji mifuko 1000 msaada ambao umefanikisha kukamilika kwa ujenzi wa bweni la wasichana.
"Napenda kukushukuru Mbunge na Naibu Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kwa misaada mbalimbali ambayo umekuwa ukitupatia na mara zote umekuwa mstari wa mbele kwa kutusaidia kila unapopata nafasi ya kufanya hivyo ,"anasema mkuu wa shule mbele ya Dk Nchimbi.
Dk Nchimbi, kwa upande wake aliipongeza shule hiyo kwa kufanikiwa kuongeza ufaulu mwaka hadi mwaka na kuwataka waendelee kuweka mkazo zaidi katika masomo ili kuongeza ufaulu zaidi.
"Nawashauri wanafunzi wa kujenga tabia ya kujiendeleza na kusoma kwa bidii ili waweze kufanya vizuri katika mitihani yao ya mwisho ikiwa ni pamoja na kuchukua tahadhari ili wasiambukizwe virusi vya ukimwi,"anasema.
Amewataka wanafunzi hao wachukue tahadhari mapema na wawe makini na wenye nidhamu kwa kuacha kujiingiza katika vitendo viovu kama uvutaji bangi, uzinzi pamoja na kufanya ngono ili wasiambukizwe ukimwi.
"Nawapongeza kwa mafanikio makubwa mliyopata kwa kuweza kuongeza ufaulu mwaka hadi mwaka, ila nawashauri wanafunzi kuwa makini na msijiingize katika vitendo vitakavyowaingiza katika mtego wa kuambukizwa virusi vya ukimwi kwani taifa na jamii linawahitaji,"anasema.
Naye mwanafunziwa kidato cha sita shuleni hapo Frank Milinga, anasema kutokana na uongozi bora wa shule hiyo wameweza kuonyesha juhudi kubwa katika taaluma, nidhamu, michezo na utawala kwa jumla hivyo kuiwezesha shule hiyo kufanya vizuri katika mitihani ya ndani na nje.
"Bado shule yetu inakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo ya ukosefu wa vitabu vya kutosha vya kiada na ziada, upungufu wa mabweni, vifaa vya maabara, ukumbi wa mikutano pamoja na gari la shule," anasema mwanafunzi huyo anayetarajiwa kuhitimu mwezi huu.
Wanafunzi hao wamewaomba wadau mbalimbali kuongeza jitihada za kuwasaidia ili kupata ufumbuzi wa tatizo hilo ikiwa ni pamoja na wazazi kuwasilisha michango ya ada kwa wakati
Anaonekana mwenye furaha kwa sababu jukumu alilopewa la kusimamia elimu ya watoto katika shule hiyo inayomilikiwa na Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) limefanikiwa kwa asilimia kubwa.
"Kitaaluma shule hii imekuwa ikipiga hatua mwaka hadi mwaka hususani kwa kuzingatia matokeo ya kidato cha cha nne na sita viwango vizuri zaidi vya ufaulu ambavyo shule inaweza kujivunia sana ni vya kidato cha sita kwani tangu shule ianze," alisema Meja Rugwabuza katika mahafali ya tano ya kidato cha sita yaliyofanyika hivi karibuni.
"Mfano mzuri wa matokeo ya mock wa kidato cha sita mwaka 2009 katika Mkoa wa Ruvuma kulikuwa na daraja la kwanza 17, daraja la pili 108, daraja la tatu 84 na daraja la nne walikuwa wanne. Hakukuwa na mwanafunzi aliyefeli hivyo tunatarajia kupeleka wanafunzi wengi zaidi kujiunga na elimu ya juu (vyuo vikuu)."
Mbali ya mock, matokeo ya kidato cha sita mwaka 2006 yanaonyesha mmoja alipata daraja la I, daraja la II walikuwa 15, daraja la III walikuwa saba na mmoja daraja la IV.
Mwaka 2007 wanne walipata daraja la I, daraja la II walikuwa 20, daraja la III walikuwa 18, daraja la IV walikuwa sita; na mwaka 2008 mmoja amepata daraja la I, daraja la II walikuwa 30, daraja la III walikuwa 36 na daraja la IV walikuwa 13.
Hata nafasi kitaifa, Ruhuwiko huwa inashika nafasi nzuri. Mathalani mwaka 2006 shule ilishika nafasi ya 16 kati ya shule 57, mwaka 2007 ilishika nafasi ya 38 kati ya shule 230 hivyo iko ndani ya malengo kusudiwa ya maendeleo ya shule.
Takwimu hizo za kitaifa ndizo anajivunia Meja Rugwabuza aliyerithi mikoba ya mtangulizi wake Meja Celestin Mwangasi (amehamia Makongo Sekondari) kuiongoza shule hiyo iliyoko kilomita nne kutoka Songea mjini.
Mbali ya uwezo wa darasani, imeelezwa wana nidhamu nzuri na mitihani yao ya ndani wamekuwa wakifanya vizuri kwa viwango vinavyokubalika.
Matarajio ya baadaye ya Ruhuwiko, Meja Rugwabuza anasema yamo katika mpango wa maendeleo ya shule wa miaka tisa (2006-2015) unaotilia mkazo mambo mengi ambayo ni pamoja na upatikanaji wa maji safi na salama kwa afya za wanafunzi, walimu na wafanyakazi.
Katika kukabiliana na tatizo la utoro wa wanafunzi na kuondoa visingizio vya hapa na pale shule imeendelea mazingira ya shule kwa kuongeza bidhaa kwenye duka la shule, kujenga kibanda cha kutengeneza nywele, kuweka uzio kwenye bweni la wasichana na kumalizia pia bwalo la chakula kwa wanafunzi wa bweni.
Shule hiyo iliyoanzishwa mwaka 1995 inatoa elimu ya sekondari kwa vijana wote kuanzia kidato cha kwanza hadi cha sita na kwa kuzingatia umuhimu wa maendeleo ya teknolojia ya mawasiliano wameajiri walimu wawili wenye diploma hivyo kuwa na walimu watatu. Matarajio yao ya hivi karibuni ni kuanza kufundisha hata watu wazima muda wa jioni.
"Vijana wengi wanaomaliza kidato cha sita katika shule hii wanajiunga na vyuo vikuu na taasisi nyingine za elimu ya juu.
Pamoja na kujivunia mafanikio hayo shule pia inawawezesha vijana kukabiliana na umasikini kwa kutoa elimu ya ujasiriamali na kompyuta ili mwanafunzi anayehitimu katika shule hii aweze kukabiliana na mazingira yanayomzunguka," anasema Meja Rugwabuza.
Pamoja na mafanikio hayo shule hiyo inakabiliwa na changamoto mbalimbali katika uendeshaji na utekelezaji wa mipango yake ya maendeleo ikiwemo tatizo la kukatika mara kwa mara umeme hivyo kusababisha shule kutumia jenereta. Kutokana na gharama za mafuta kupanda imeongeza gharama za uendeshaji.
Changamoto nyingine ni ujenzi wa ukumbi wa mikutano na mitihani ambao huo uko katika hatua za awali. Nguvu kubwa ya vifaa na fedha inahitajika kwani shule peke yake haiwezi kumudu kwa muda mfupi.
"Tatizo jingine ni kupanda kwa gharama za uendeshaji kutokana na kupanda sana kwa bei ya chakula na vifaa. Hata hivyo, shule imejitahidi kuepuka kupandisha sana gharama za malipo ya ada ili lengo la kuwapatia elimu watoto wengi zaidi liweze kufanikiwa," anaeleza Meja Rugwabuza.
Japo shule hiyo inakabiliwa na changamoto hizo na nyingine kadhaa zinaoendana na uboreshaji wa elimu, Ruhuwiko haijatetereka katika utendaji wake na mfano mzuri ni matokeo yake ya mitihani ya taifa ya kidato cha sita kwa miaka mitatu mfululizo. Matokeo hayo yamechangia kwa kiasi kikubwa kuwafanya watu wengi kuvutiwa na elimu ambayo inatolewa na shule hiyo.
Meja Rugwabuza anasema mafanikio ya shule hiyo kwa kiasi kikubwa yanatokana na ushirikiano mkubwa uliopo baina ya walimu, wafanyakazi, wanafunzi pamoja na wanajumuiya wa shule hiyo akiwemo Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini Dk Emmanuel Nchimbi.
Dk Nchimbi amekuwa na mchango mkubwa katika maendeleo ya shule hiyo hususan kwa misaada yake ya mabati na saruji. Aliipatia shule hiyo mabati 240 na saruji mifuko 1000 msaada ambao umefanikisha kukamilika kwa ujenzi wa bweni la wasichana.
"Napenda kukushukuru Mbunge na Naibu Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kwa misaada mbalimbali ambayo umekuwa ukitupatia na mara zote umekuwa mstari wa mbele kwa kutusaidia kila unapopata nafasi ya kufanya hivyo ,"anasema mkuu wa shule mbele ya Dk Nchimbi.
Dk Nchimbi, kwa upande wake aliipongeza shule hiyo kwa kufanikiwa kuongeza ufaulu mwaka hadi mwaka na kuwataka waendelee kuweka mkazo zaidi katika masomo ili kuongeza ufaulu zaidi.
"Nawashauri wanafunzi wa kujenga tabia ya kujiendeleza na kusoma kwa bidii ili waweze kufanya vizuri katika mitihani yao ya mwisho ikiwa ni pamoja na kuchukua tahadhari ili wasiambukizwe virusi vya ukimwi,"anasema.
Amewataka wanafunzi hao wachukue tahadhari mapema na wawe makini na wenye nidhamu kwa kuacha kujiingiza katika vitendo viovu kama uvutaji bangi, uzinzi pamoja na kufanya ngono ili wasiambukizwe ukimwi.
"Nawapongeza kwa mafanikio makubwa mliyopata kwa kuweza kuongeza ufaulu mwaka hadi mwaka, ila nawashauri wanafunzi kuwa makini na msijiingize katika vitendo vitakavyowaingiza katika mtego wa kuambukizwa virusi vya ukimwi kwani taifa na jamii linawahitaji,"anasema.
Naye mwanafunziwa kidato cha sita shuleni hapo Frank Milinga, anasema kutokana na uongozi bora wa shule hiyo wameweza kuonyesha juhudi kubwa katika taaluma, nidhamu, michezo na utawala kwa jumla hivyo kuiwezesha shule hiyo kufanya vizuri katika mitihani ya ndani na nje.
"Bado shule yetu inakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo ya ukosefu wa vitabu vya kutosha vya kiada na ziada, upungufu wa mabweni, vifaa vya maabara, ukumbi wa mikutano pamoja na gari la shule," anasema mwanafunzi huyo anayetarajiwa kuhitimu mwezi huu.
Wanafunzi hao wamewaomba wadau mbalimbali kuongeza jitihada za kuwasaidia ili kupata ufumbuzi wa tatizo hilo ikiwa ni pamoja na wazazi kuwasilisha michango ya ada kwa wakati
Habari hii imeandikwa na Joyce Joliga katika gazeti la mwanancchi. Nimeona si vibaya kama wasomaji wa blog hii pia wakisoma. Kwani wote tuna nia moja
Monday, February 8, 2010
Kibanga Ampiga Mkoloni
elimu ni ufungu wa maisha
Katika upekuzi wangu jana nikawa nimekifuma kitabu hiki na mwisho nikakutana na hadithi hii ungana nami kuisoma ina toka katika kitabu cha 6 Tujifunnze Lugha Yetu!
Zamani za ukoloni, palitokea Mzungu mmoja. Mzungu huyo hakuwa mtu mwema. Alikuwa mkali na mkatili sana. Kwa ajili ya ukatili wake watu walimwita mkoloni. Wanancgi wote walimchukia sana popote pale alipokwenda.
Mzungu huyo alikuwa Bwana Shamba. Alikuwa na bakora iliyokuwa imetengenezwa kwa mkwaju. Kila alipokwenda kukagua mashamba, alikuwa na bakora hiyo mkononi. Alipendelea sana kuitwa "Bwana Mkubwa". Mkolono huyo alifurahia sana kupiga watu. Aliwapiga watu waliposhindwa kupalilia mashamba. Aliwapiga pamba yao ilipokuwa chafu. Aliwapa taabu sana.
Katika kijiji cha Kwachaga, Wilaya ya Handeni, alikuwapo mzee mmoja aliyeitwa Kibanga. Mzee huyu alikuwa mwenye nguvu, hodari na shujuaa. alikuwa fundi wa mieleka. Ingawa alikuwa mwenye nguvu, alikuwa mpole. Hivyo watu wa Kwachaga walimpenda na kumtegemea kuwaongoza vitani.
Siku moja yule Mzungu alifika Kwachaga kukagua mashamba ya mihogo. Jumbe pamoja naye wakatembelea mashamba. Kwa bahati mbaya mwaka ule haukuwa na mvua ya kutosha. Kwa hiyo mihogo haikustawi. Kila wakati yule Mzungu alipotazama mashamba alitikisa kichwa na kufoka. Mwisho akamwagiza Jumbe kuitisha mkutano wa watu wote wa kijij. Waliporudi kijijini Jumbe akapiga mbiu. Watu wote wakakusanyika. Walipofika tu, yule Mkoloni akaanza kuwatukana, akawaambia, "Ninyi watu weusi ni wavivu sana. Hamfanyi kazi sawa sawa. Mashamba yenu ni mabaya sana". Jumbe akataka kumjibu ili kumweleza kwa nini mihogo haikustawi. Kabla hajamweleza yule Mzungu alimrukia na kumpiga kofi. Kisha akasema, "Sitaki kijibiwa na wewe, mvivu wa wavivu". Watu wote wakakaa kimya. Hakuna aliyeweza kufanya kitu.
Kibanga akajitokeza, akasimama. Akamtazama yule Mkoloni kwa dharau sana. Kisha akamwuliza, "Kutuita sisi wavivu ndiyo nini? Na kumpiga Jumbe wetu mbele yetu, maana yake nini?"
Kabla ya kumaliza kusema, Mkoloni aliamka kitini kwa hasira , akataka kumpiga Kibanga. Alishika bakora yake mkononi. Akasedma, "Nitakuadhibu vibaya kima we! Unajifanya kuwa shujua? Huwezi kucheza na bwana mkubwa. Nitakupiga, kisha utakwenga jela miezi sita." Lakini Mkoloni hakuwahi kumwadhibu Kibanga. Aliadhibiwa yeye. Kabla ya kumfikia, Kibanga alimpiga chenga. Kisha akamrukia, akamnyangánya bakorta yake. Akaitupa, ikaokotwa na vijana, wakaificha.
Kibanga alimshika yule Mzungu akamwambia. "Wewe umezoea kutoa amri kila siku, lakini leo utashika adabu, mbwe wee!" Papo hapo alimnyanyua juu na kumbwaga chini, puu! Yule Mkolono akaumia sana. Kabla ya kuamka, Kibanga alimwinua tena na kumbwaga chini kama furushi la pamba. Akamkalia.
Hapo yule Mkoloni akawa hana la kufanya. Bila ya bakora alikuwa hana nguvu. Akaomba radhi akilia, "Samahani! Naumia! Nihurumie! Sitafanya tena hivyo." Kibanga alimjibu kwa dharau, "Sikuachi mbwa wee! Leo utakiona cha mtema kuni! Ulijiona una nguvu. Leo nitakutengeneza."
Wazee wakamshika Kibanga na kumwomba asimpiga tena. Akamwacha. Kwa shida yule Mkoloni akajikokota kwenda hemeni. Alikuwa amejaa vumbi huku damu zikimtoka. Wazee wengine wakamfuata nyuma. Walinyamaza kimya, wakimhurumia. lakini vijana walifurahi sana.
Baadaye waliimba wimbo wa kumsifu Kibanga.
Jioni yule Mkoloni aliomba radhi kwa wazee. Mzee mmoja akasimama na kumwambia, "Umefanya vizuri kuomba radhi, nasi tunaipokea. Lakini tangu leo usijivunie ubwana. Jivunie utu. Ninyi wakaoloni mna kiburi. Mnatudharau. Kama ungetuuliza tungekuambia kwa nini migogo haikustawi. Haya yote yamekupata kwa sababu ya kiburi chako. Katika nchi hii tuanaamini kuwa kiburi si maungwana".
Baada ya hapo wazee wakamsamehe, lakini hawakumpa bakora yake. Ikabaki nyumbani kwa Jumbe. Yule Mkoloni akaondoka. Tangu siku hiyo hakufika tena Kwachaga. Kila mara alipokutana na watu aliyakumbuka maneno ya yule mzee, "Kiburi si maungwana".
Siku hizi kijiji cha Kwachaga kina maendele mazuri ya kilimo na mifugo. Maendeleo yote yamepatikana kwa sababu ya uongozi bora wa Serikali ya wananchi.
Mzungu huyo alikuwa Bwana Shamba. Alikuwa na bakora iliyokuwa imetengenezwa kwa mkwaju. Kila alipokwenda kukagua mashamba, alikuwa na bakora hiyo mkononi. Alipendelea sana kuitwa "Bwana Mkubwa". Mkolono huyo alifurahia sana kupiga watu. Aliwapiga watu waliposhindwa kupalilia mashamba. Aliwapiga pamba yao ilipokuwa chafu. Aliwapa taabu sana.
Katika kijiji cha Kwachaga, Wilaya ya Handeni, alikuwapo mzee mmoja aliyeitwa Kibanga. Mzee huyu alikuwa mwenye nguvu, hodari na shujuaa. alikuwa fundi wa mieleka. Ingawa alikuwa mwenye nguvu, alikuwa mpole. Hivyo watu wa Kwachaga walimpenda na kumtegemea kuwaongoza vitani.
Siku moja yule Mzungu alifika Kwachaga kukagua mashamba ya mihogo. Jumbe pamoja naye wakatembelea mashamba. Kwa bahati mbaya mwaka ule haukuwa na mvua ya kutosha. Kwa hiyo mihogo haikustawi. Kila wakati yule Mzungu alipotazama mashamba alitikisa kichwa na kufoka. Mwisho akamwagiza Jumbe kuitisha mkutano wa watu wote wa kijij. Waliporudi kijijini Jumbe akapiga mbiu. Watu wote wakakusanyika. Walipofika tu, yule Mkoloni akaanza kuwatukana, akawaambia, "Ninyi watu weusi ni wavivu sana. Hamfanyi kazi sawa sawa. Mashamba yenu ni mabaya sana". Jumbe akataka kumjibu ili kumweleza kwa nini mihogo haikustawi. Kabla hajamweleza yule Mzungu alimrukia na kumpiga kofi. Kisha akasema, "Sitaki kijibiwa na wewe, mvivu wa wavivu". Watu wote wakakaa kimya. Hakuna aliyeweza kufanya kitu.
Kibanga akajitokeza, akasimama. Akamtazama yule Mkoloni kwa dharau sana. Kisha akamwuliza, "Kutuita sisi wavivu ndiyo nini? Na kumpiga Jumbe wetu mbele yetu, maana yake nini?"
Kabla ya kumaliza kusema, Mkoloni aliamka kitini kwa hasira , akataka kumpiga Kibanga. Alishika bakora yake mkononi. Akasedma, "Nitakuadhibu vibaya kima we! Unajifanya kuwa shujua? Huwezi kucheza na bwana mkubwa. Nitakupiga, kisha utakwenga jela miezi sita." Lakini Mkoloni hakuwahi kumwadhibu Kibanga. Aliadhibiwa yeye. Kabla ya kumfikia, Kibanga alimpiga chenga. Kisha akamrukia, akamnyangánya bakorta yake. Akaitupa, ikaokotwa na vijana, wakaificha.
Kibanga alimshika yule Mzungu akamwambia. "Wewe umezoea kutoa amri kila siku, lakini leo utashika adabu, mbwe wee!" Papo hapo alimnyanyua juu na kumbwaga chini, puu! Yule Mkolono akaumia sana. Kabla ya kuamka, Kibanga alimwinua tena na kumbwaga chini kama furushi la pamba. Akamkalia.
Hapo yule Mkoloni akawa hana la kufanya. Bila ya bakora alikuwa hana nguvu. Akaomba radhi akilia, "Samahani! Naumia! Nihurumie! Sitafanya tena hivyo." Kibanga alimjibu kwa dharau, "Sikuachi mbwa wee! Leo utakiona cha mtema kuni! Ulijiona una nguvu. Leo nitakutengeneza."
Wazee wakamshika Kibanga na kumwomba asimpiga tena. Akamwacha. Kwa shida yule Mkoloni akajikokota kwenda hemeni. Alikuwa amejaa vumbi huku damu zikimtoka. Wazee wengine wakamfuata nyuma. Walinyamaza kimya, wakimhurumia. lakini vijana walifurahi sana.
Baadaye waliimba wimbo wa kumsifu Kibanga.
Jioni yule Mkoloni aliomba radhi kwa wazee. Mzee mmoja akasimama na kumwambia, "Umefanya vizuri kuomba radhi, nasi tunaipokea. Lakini tangu leo usijivunie ubwana. Jivunie utu. Ninyi wakaoloni mna kiburi. Mnatudharau. Kama ungetuuliza tungekuambia kwa nini migogo haikustawi. Haya yote yamekupata kwa sababu ya kiburi chako. Katika nchi hii tuanaamini kuwa kiburi si maungwana".
Baada ya hapo wazee wakamsamehe, lakini hawakumpa bakora yake. Ikabaki nyumbani kwa Jumbe. Yule Mkoloni akaondoka. Tangu siku hiyo hakufika tena Kwachaga. Kila mara alipokutana na watu aliyakumbuka maneno ya yule mzee, "Kiburi si maungwana".
Siku hizi kijiji cha Kwachaga kina maendele mazuri ya kilimo na mifugo. Maendeleo yote yamepatikana kwa sababu ya uongozi bora wa Serikali ya wananchi.
Monday, November 30, 2009
NYIMBO ZA MCHAKAMCHAKA/KUMBUKUMBU
Leo nimekumbuka wakati nasoma shule hasa shule ya msingi saa kumi na moja alfajiri kuwahi shule kisa nini? Kuwahi namba na kukimbia mchakamchaka huku mnatweta kama nini na mkiimba nyimbo:- Kwa mfano:-
1. Panda mlima panda, panda, panda, pasnda usichoke........x2
2. Iddi amin akifa mimi siwezi kulia nitamtupa kagera awe chakula cha mamba.x2
3.Jua lille literemke mama, mwezi nao uteremke mama haiyahiyaaa hiyaa hiyaa mamaaaa.....x2
4. Alisema, alisema, alisemaaa Nyerere alisema vijana wangu wote mwalegea shart tuanze mchakamchakax2.....
Kama kun mtu anakumbuka wimbo mwingine basi karibu kuongezea hapa.
1. Panda mlima panda, panda, panda, pasnda usichoke........x2
2. Iddi amin akifa mimi siwezi kulia nitamtupa kagera awe chakula cha mamba.x2
3.Jua lille literemke mama, mwezi nao uteremke mama haiyahiyaaa hiyaa hiyaa mamaaaa.....x2
4. Alisema, alisema, alisemaaa Nyerere alisema vijana wangu wote mwalegea shart tuanze mchakamchakax2.....
Kama kun mtu anakumbuka wimbo mwingine basi karibu kuongezea hapa.
Tuesday, October 6, 2009
Nimekumbuka zamani wakati nasoma+ Ubunifu wa kutengeneza vihesabio!!!

1. Kwaheri baba na mama twaenda shuleni x2
Kusoma huko shuleni pamoja na mwalimu.
Kuandika huko shuleni pamoja na mwalimu.
2. Kwaheri baba na mama twaenda shuleni x2
Kuhesabu huko shuleni pamoja na mwalimu.
Kuchora huko shuleni pamoja na mwalimu.
3. Kwaheri baba na mama twaenda shuleni x2
Kuimba huko shuleni pamoja na mwalimu.
Twaimba sote pamoja pamoja na mwalimu.
Thursday, September 17, 2009
HATUA SITA ZA KUSAIDIA KUDHIBITI MIMBA SHULENI
MAANDALIZI ya safari yangu kwa ajili ya kumpeleka mtoto wa dada yangu kujiunga na masomo ya sekondari Morogoro yalikwenda vizuri na asubuhi yake nilijona mtu mwenye bahati.
Tulifika mapema kwenye kituo kikuu cha mabasi, Ubungo na tulipokuwa tunaelekea kwenye basi moja ambalo tulitaka kukata tiketi, tuliwaona wasichana kadhaa walioonekana kuwa ni wanafunzi, ni kweli nao walikuwa wanakwenda katika shule hiyo. Alikuwepo mwanamume mmoja aliyevalia vizuri ambaye alijitambulisha kuwa mwalimu wa shule hiyo.
Mwalimu huyo, ambaye alikuwa na vitambulisho vya kazi aliwaambia wazazi waliokuwa wanawasindikiza watoto wao wasisumbuke kwani yeye ametumwa kwa ajili hiyo. Hivyo, wazazi, walezi na sisi wengine tuliotumwa tulimkabidhi mwalimu huyo watoto nasi tukarudi nyumbani.
Kwa haiba aliyokuwa nayo mwalimu yule, kwa umri wake na hata upole alioonyesha, alivyokuwa anazungumza taratibu na alivyotuaminishia usalama, haraka tulinong’onezana kuwa ni mlokole. Niliporudi nyumbani asubuhi ile niliwachekesha wazazi wake kwamba 'nimekbidhi binti yao kwa mwalimu mlokole'.
Hilo lilikuwa kosa kubwa. Utaratibu ule ulikuwa tofauti na fikra zake moyoni, alikuwa mbwa mwitu. Mwalimu huyo ambaye, nahifadhi jina lake, ndiye alikuja kutupa pigo kubwa kwa kumkatisha masomo binti yetu baada ya kumpa ujauzito. Tumefungua kesi kortini.
Pamoja na kuchukua hatua hizo, tumekuwa tukijiuliza nini ki kifanyike ili, siyo tu kwa sisi kupata haki kutokana na binti yetu kupewa ujauzito na mwalimu anayepaswa kuwa mlezi wake, bali pia kuwadhibiti walimu wengine wa kiume wenye tabia ya kuwarubuni wanafunzi wa kike na kuwapa mimba.
Hii ni kwa sababu tuliokumbwa na kero siyo sisi tu bali wazazi wengi, na kumekuwa na malalamiko kila kona unayopita, kuhusu wanafunzi wa kike kukatishwa masomo baada ya kugundulika wamepata ujauzito shuleni.
Japokuwa baadhi ya wasichana hupewa mimba shuleni na wanafunzi wenzao wa kiume, watu wa mitaani pamoja na wafanyakazi, ukweli ni kwamba wengi wao hukatishwa masomo kwa kupewa mimba na walimu wao.
Taarifa mbalimbali na uchunguzi uliofanywa katika maeneo mengi, walimu wanahusika kwa kiasi kikubwa. Walimu hao huwapata wanafunzi kwa urahisi kwa vishawishi kadha wa kadhaa vikiwemo vya kuongezewa alama, kupewa maswali ya ziada (twisheni) na kupangiwa kazi nyepesi.
Kuna ukweli pia kwamba baadhi ya wasichana hupata ujauzito kutokana na kutokuwa na maadili mazuri, papara au ulibukeni wa maisha lakini wengine hulazimika kujenga mahusiano ya kimapenzi na walimu wao kwa kufundishwa masomo ya ziada ili wafaulu mitihani yake.
Kwa mfano, hivi karibuni, tulisikia katika baadhi ya vyombo vya habari vikiripoti kuwa mwalimu mkuu wa shule moja iliyoko Kusini mwa Tanzania amepandishwa kizimbani akikabiliwa na shtaka la kumpa mimba mwanafunzi wake.
Katika tukio kama hili, kwa hali ya kawaida unaweza usiamini wala kupata picha inakuwaje, lakini ndiyo hali halisi ya maisha yalivyo katika ulimwengu wa sasa. Kama mzazi wa kiume anaweza kujenga uhusiano wa kimapenzi na mtoto aliyemzaa sembuse mwalimu?.
Ukichunguza kwa makini utagundua chanzo cha tatizo hili ni tamaa ya walimu na ukiukwaji mkubwa wa kanuni za maadili kazini. Walimu hupaswa kuwa walinzi wa wanafunzi na waongoza maadili kinyume cha hivyo ni utovu wa nidhamu.
Mapendekezo yangu.
Kwanza wazazi wote wenye wanafunzi wa kike wahakikishe wanafungua kesi dhidi ya wahusika ili hatua za kisheria zichukuliwe.
Endapo binti atadai hajui, kwa lengo la kumficha mhusika, basi binti huyo ashitakiwe binafsi.
Pili, wazazi tusikubali vishawishi vya wavulana au walimu au watu wengine weyote walihusika kwamba wasishtakiwe ila waachiwe wawatunze mabinti na ujauzito walionao. Imebainika hufanya hivyo kwa muda tu, baada ya miezi michache huwapa talaka na huo unakuwa mwisho wao.
Tatu, napendekeza serikali iweke uzito kwa upande wa walimu kwamba watakaobainika kuhusishwa tu kuwa na uhusiano wa kimapenzi na wanafunzi waachishwe kazi. Nina uhakika hakuna anayependa kuachishwa kazi hivyo wataachana na tamaa yao kwa wanafunzi.
Hatua hizo zinaweza kuchangia kupunguza kuwepo kwa matukio kama haya na walimu watajitahidi kuishi juu ya tuhuma za kimapenzi.
Nne, uwepo utaratibu wa kuwapima wanafunzi wa kike kila mara na kuwapa ushauri nasaha kwamba wajifunze na wazoee kusema "hapana" wanapofuatwa na walimu wao kimapenzi.
Tano, iko haja ya kuweka sheria kuzuia wanafunzi kufika kwa walimu kama hawana uhusiano wa kidugu. Shule za seminari na zinazoendeshwa na masista zimeweza, kwa nini ishindikane katika shule za serikali?
Sita ni kwamba chanzo kingine cha matukio ya mamba ni kushiriki starehe. Wazazi wawazuie watoto wao; wavulana kwa wasichana kujiingiza kupita kiasi kwenye burudani kwani ni nchimbuko kubwa la maasi ya maadili na mwishowe kupeana mimba.
Hii ilitoka mwananchi la tarehe 23/6/2009 na mwandishi Elizabeth Suleyman.
Tulifika mapema kwenye kituo kikuu cha mabasi, Ubungo na tulipokuwa tunaelekea kwenye basi moja ambalo tulitaka kukata tiketi, tuliwaona wasichana kadhaa walioonekana kuwa ni wanafunzi, ni kweli nao walikuwa wanakwenda katika shule hiyo. Alikuwepo mwanamume mmoja aliyevalia vizuri ambaye alijitambulisha kuwa mwalimu wa shule hiyo.
Mwalimu huyo, ambaye alikuwa na vitambulisho vya kazi aliwaambia wazazi waliokuwa wanawasindikiza watoto wao wasisumbuke kwani yeye ametumwa kwa ajili hiyo. Hivyo, wazazi, walezi na sisi wengine tuliotumwa tulimkabidhi mwalimu huyo watoto nasi tukarudi nyumbani.
Kwa haiba aliyokuwa nayo mwalimu yule, kwa umri wake na hata upole alioonyesha, alivyokuwa anazungumza taratibu na alivyotuaminishia usalama, haraka tulinong’onezana kuwa ni mlokole. Niliporudi nyumbani asubuhi ile niliwachekesha wazazi wake kwamba 'nimekbidhi binti yao kwa mwalimu mlokole'.
Hilo lilikuwa kosa kubwa. Utaratibu ule ulikuwa tofauti na fikra zake moyoni, alikuwa mbwa mwitu. Mwalimu huyo ambaye, nahifadhi jina lake, ndiye alikuja kutupa pigo kubwa kwa kumkatisha masomo binti yetu baada ya kumpa ujauzito. Tumefungua kesi kortini.
Pamoja na kuchukua hatua hizo, tumekuwa tukijiuliza nini ki kifanyike ili, siyo tu kwa sisi kupata haki kutokana na binti yetu kupewa ujauzito na mwalimu anayepaswa kuwa mlezi wake, bali pia kuwadhibiti walimu wengine wa kiume wenye tabia ya kuwarubuni wanafunzi wa kike na kuwapa mimba.
Hii ni kwa sababu tuliokumbwa na kero siyo sisi tu bali wazazi wengi, na kumekuwa na malalamiko kila kona unayopita, kuhusu wanafunzi wa kike kukatishwa masomo baada ya kugundulika wamepata ujauzito shuleni.
Japokuwa baadhi ya wasichana hupewa mimba shuleni na wanafunzi wenzao wa kiume, watu wa mitaani pamoja na wafanyakazi, ukweli ni kwamba wengi wao hukatishwa masomo kwa kupewa mimba na walimu wao.
Taarifa mbalimbali na uchunguzi uliofanywa katika maeneo mengi, walimu wanahusika kwa kiasi kikubwa. Walimu hao huwapata wanafunzi kwa urahisi kwa vishawishi kadha wa kadhaa vikiwemo vya kuongezewa alama, kupewa maswali ya ziada (twisheni) na kupangiwa kazi nyepesi.
Kuna ukweli pia kwamba baadhi ya wasichana hupata ujauzito kutokana na kutokuwa na maadili mazuri, papara au ulibukeni wa maisha lakini wengine hulazimika kujenga mahusiano ya kimapenzi na walimu wao kwa kufundishwa masomo ya ziada ili wafaulu mitihani yake.
Kwa mfano, hivi karibuni, tulisikia katika baadhi ya vyombo vya habari vikiripoti kuwa mwalimu mkuu wa shule moja iliyoko Kusini mwa Tanzania amepandishwa kizimbani akikabiliwa na shtaka la kumpa mimba mwanafunzi wake.
Katika tukio kama hili, kwa hali ya kawaida unaweza usiamini wala kupata picha inakuwaje, lakini ndiyo hali halisi ya maisha yalivyo katika ulimwengu wa sasa. Kama mzazi wa kiume anaweza kujenga uhusiano wa kimapenzi na mtoto aliyemzaa sembuse mwalimu?.
Ukichunguza kwa makini utagundua chanzo cha tatizo hili ni tamaa ya walimu na ukiukwaji mkubwa wa kanuni za maadili kazini. Walimu hupaswa kuwa walinzi wa wanafunzi na waongoza maadili kinyume cha hivyo ni utovu wa nidhamu.
Mapendekezo yangu.
Kwanza wazazi wote wenye wanafunzi wa kike wahakikishe wanafungua kesi dhidi ya wahusika ili hatua za kisheria zichukuliwe.
Endapo binti atadai hajui, kwa lengo la kumficha mhusika, basi binti huyo ashitakiwe binafsi.
Pili, wazazi tusikubali vishawishi vya wavulana au walimu au watu wengine weyote walihusika kwamba wasishtakiwe ila waachiwe wawatunze mabinti na ujauzito walionao. Imebainika hufanya hivyo kwa muda tu, baada ya miezi michache huwapa talaka na huo unakuwa mwisho wao.
Tatu, napendekeza serikali iweke uzito kwa upande wa walimu kwamba watakaobainika kuhusishwa tu kuwa na uhusiano wa kimapenzi na wanafunzi waachishwe kazi. Nina uhakika hakuna anayependa kuachishwa kazi hivyo wataachana na tamaa yao kwa wanafunzi.
Hatua hizo zinaweza kuchangia kupunguza kuwepo kwa matukio kama haya na walimu watajitahidi kuishi juu ya tuhuma za kimapenzi.
Nne, uwepo utaratibu wa kuwapima wanafunzi wa kike kila mara na kuwapa ushauri nasaha kwamba wajifunze na wazoee kusema "hapana" wanapofuatwa na walimu wao kimapenzi.
Tano, iko haja ya kuweka sheria kuzuia wanafunzi kufika kwa walimu kama hawana uhusiano wa kidugu. Shule za seminari na zinazoendeshwa na masista zimeweza, kwa nini ishindikane katika shule za serikali?
Sita ni kwamba chanzo kingine cha matukio ya mamba ni kushiriki starehe. Wazazi wawazuie watoto wao; wavulana kwa wasichana kujiingiza kupita kiasi kwenye burudani kwani ni nchimbuko kubwa la maasi ya maadili na mwishowe kupeana mimba.
Hii ilitoka mwananchi la tarehe 23/6/2009 na mwandishi Elizabeth Suleyman.
Tuesday, March 17, 2009
TUPO DARASANI+MAISHA
Monday, March 16, 2009
UTARATIBU WA SHULE
Ngoja leo tuangalie kuhusu utaratibu wa shule, nikiwa na maana utaratibu wa shule hapa Sweden na Tanzania. Kwani binafsi nimamaliza shule Tanzania na sasa naishi hapa. Kama si kusei nilipokuwa mdogo nakumbuka hata siku moja sijawahi kuona au kmwona au hata kusikia ya kwamba mzazi anakwenda shuleni kusikia maendeleo ya mtoto wake. Pia sijawahi kuona mzazi anakwenda shuleni siku moja kuwa na mtoto wake. Yaani kuona anafanya nini kweli yupo shuleni?
Hapa niishipo sasa nimeona na pia binafsi ni mzazi. Kwa hiyo kama mzazi nina jukumu kwabwa la kuwalea watoto wangu. Lakini pia ni sheria na pia ni utaratibu kila mzazi anaitwa shuleni kwenda kuona/kusikiliza maendeleo ya mtoto wako. Na hapo sio inaanza shule ya mzingi tu, hapana, ni tangu chekechea. Na sio mzazi/wazazi na mwalimu tu hapana na mtoto mwenyewe anakuwepo. Na jambo hili huwa linafanyika kila muhula mpya unapoanza. Unaambiwa jinsi mwanao alivyo na juhudi aa jinsi alivyo mzembe na kama anahitaji mwongozo gani. Leo nimekuwa shuleni kusikiliza maendeleo ya mtoto wangu ndio maana nimekumbuka kwa nini nilipokuwa nasoma mimi au mbona wazazi wangu walikuwa hawaji kusikiliza maendeleo yangu. Halafu nimekumbuka kumbe hakuna utaratibu kama huu.
Hapa niishipo sasa nimeona na pia binafsi ni mzazi. Kwa hiyo kama mzazi nina jukumu kwabwa la kuwalea watoto wangu. Lakini pia ni sheria na pia ni utaratibu kila mzazi anaitwa shuleni kwenda kuona/kusikiliza maendeleo ya mtoto wako. Na hapo sio inaanza shule ya mzingi tu, hapana, ni tangu chekechea. Na sio mzazi/wazazi na mwalimu tu hapana na mtoto mwenyewe anakuwepo. Na jambo hili huwa linafanyika kila muhula mpya unapoanza. Unaambiwa jinsi mwanao alivyo na juhudi aa jinsi alivyo mzembe na kama anahitaji mwongozo gani. Leo nimekuwa shuleni kusikiliza maendeleo ya mtoto wangu ndio maana nimekumbuka kwa nini nilipokuwa nasoma mimi au mbona wazazi wangu walikuwa hawaji kusikiliza maendeleo yangu. Halafu nimekumbuka kumbe hakuna utaratibu kama huu.
Monday, September 8, 2008
WAKATI NASOMA SHULE YA MSINGI
Subscribe to:
Posts (Atom)