Showing posts with label sala. Show all posts
Showing posts with label sala. Show all posts
Sunday, March 15, 2015
SALA YA LEO...AMBAYO IMETUNGWA NA KAPULYA WENU.
Sunday, June 29, 2014
MAISHA NA MAFANIKIO NAWATAKIENI JUMAPILI NJEMA NA WIMBO HUU!!!
MWENYEZI MUNGU NA AWE PAMOA NASI DAIMA
Sunday, February 16, 2014
HILI NI CHAGUA LA MAOMBI/SALA YA JUMAPILI YA LEO NA MAISHA NA MAIFANIKIO KWA WATU WOTE!!!
Eh, Mungu uliye Mtakatifu, sisi ni watenda dhambi, hatuwezi kujiokoa twakuomba Bwana Yesu uingie katika mioyo yetu na utusamehe dhambi zetu. Amina.
Naona si mbaya kama tukimalizia na kumsikiliza dada Rose Muhando na wimbo huu UNASHANGAZA
JUMAPILI IWE NJEMA KWENU NA AMANI PIA UPENDO VITAWALE DAIMA.
Naona si mbaya kama tukimalizia na kumsikiliza dada Rose Muhando na wimbo huu UNASHANGAZA
JUMAPILI IWE NJEMA KWENU NA AMANI PIA UPENDO VITAWALE DAIMA.
Sunday, November 4, 2012
JUMAPILI YA LEO NAPENDA KUSALI SALA HII KWA MAREHEMU WOTE AKIWEPO MAMA MKWE WANGU AMBAYE KATUACHA JANA!!!
Na tuwaombee marehemu
Ewe Baba Mwenyezi, Mpaji wa maisha na afya, twakuomba uwaangalie kwa rehema marehemu pia wagonjwa wote, hasa wao wanaotakiwa maombi yetu, ili kwa baraka yako juu yao, na juu ya wao wawatumikiao, ikiwa mapenzi yako warudishiwe afya yao ya -mwili na ya roho,na pia marehemu wote wastarehe kwa amani, nao wakutolee shukrani katika kanisa lako takatifu; kwa Yesu Kristo, Bwana wetu. Amina.
JUMAPILI NJEMA KWA WOTE NA UPENDO UTAWALE NDANI YA MIOYO YENU.
Ewe Baba Mwenyezi, Mpaji wa maisha na afya, twakuomba uwaangalie kwa rehema marehemu pia wagonjwa wote, hasa wao wanaotakiwa maombi yetu, ili kwa baraka yako juu yao, na juu ya wao wawatumikiao, ikiwa mapenzi yako warudishiwe afya yao ya -mwili na ya roho,na pia marehemu wote wastarehe kwa amani, nao wakutolee shukrani katika kanisa lako takatifu; kwa Yesu Kristo, Bwana wetu. Amina.
JUMAPILI NJEMA KWA WOTE NA UPENDO UTAWALE NDANI YA MIOYO YENU.
Sunday, September 16, 2012
Ngoja leo tusali Sala ya Wazazi wakiwaombea Watoto wao
Tunawaangalia , Ee BwanaHawa uliotujalia.Katika hawa tunajiona sisi wenyewe. Je, kweli tulikuwa hivi sisi
Tulipokuwa watoto? Tulipigana hivi? Tulipaiga kelele hivi? Tulileta furaha namna hii. Na mateso namna hii kwa wazazi wtu? Tunashangaa na kujiuliza....Tunajaribu kukumbuka-----Kukumbuka jinsi ilivyokuwa
Tulipokuwa watoto wadogo bado. Tukiwatazama watu wakubwa.
Wakati mwingine wanatutia wasiwasi, Bwana. Au kwa namna nzuri zaidi, tunajitia wasiwasi sisi wenyewe
Kwani si rahisi kuwa sawa daima. Lakini kuna furaha pia, furaha kubwa wanayotuletea. Nao hutufanya tuone fahari,kwani ni watoto wema.
Tunakushukuru kwa ajili yao Bwana, wao ndiyo zawadi yako bora kwetu,baada yetu sisi wenyewe. Utusaidie tuunganisha mikono yetu na mkono yako Ili, Ee Baba,Wawe kweli Watoto wetu.
Amina.
JUMPILI NJEMA KWA WOTE
Tulipokuwa watoto? Tulipigana hivi? Tulipaiga kelele hivi? Tulileta furaha namna hii. Na mateso namna hii kwa wazazi wtu? Tunashangaa na kujiuliza....Tunajaribu kukumbuka-----Kukumbuka jinsi ilivyokuwa
Tulipokuwa watoto wadogo bado. Tukiwatazama watu wakubwa.
Wakati mwingine wanatutia wasiwasi, Bwana. Au kwa namna nzuri zaidi, tunajitia wasiwasi sisi wenyewe
Kwani si rahisi kuwa sawa daima. Lakini kuna furaha pia, furaha kubwa wanayotuletea. Nao hutufanya tuone fahari,kwani ni watoto wema.
Tunakushukuru kwa ajili yao Bwana, wao ndiyo zawadi yako bora kwetu,baada yetu sisi wenyewe. Utusaidie tuunganisha mikono yetu na mkono yako Ili, Ee Baba,Wawe kweli Watoto wetu.
Amina.
JUMPILI NJEMA KWA WOTE
Sunday, August 12, 2012
SALA YA LEO NI KUWAOMBEA WATU WOTE DUNIANI!!!
Salam Maria, umejaa neema, Bwana yu nawe, umebarikiwa kuliko wanawake wote, na Yesu mzao wa tumbo lako amebarikiwa. Maria Mtakatifu mama wa Mungu, utuombee sisi wakosefu sasa na saa ya kufa kwetu. Amina. JUMAPILI NJEMA NDUGU ZANGUNI NA WOTE MNAPENDWA!!!!
Sunday, May 13, 2012
JUMAPILI NJEMA NA TUSALI SALA YA BABA YETU!!
SALA KUU
Baba yetu uliye Mbinguni,
Jina lako litukuzwe,
Ufalme wako ufike,
Utakalo lifanyike , duniani kama Mbinguni.
Utupe leo mkate wetu wa kila siku,
Utusemehe makosa yetu, kama tunavyowasamehe na sisi waliotukosea.
Usitutie katika vishawishi, lakini utuokoe maovuni.(Kwa kuwa ufalme ni wako, na nguvu, na utukufu, hata milele. Amina
HII SALA IMEBEBA MAOMBI YOTE, LIKIWEMO LA KUSAMEHEWA DHAMBI NA KUOMBA RIZIKI.
UKISALI HII , HUNA HAJA YA KUSALI VINGINE VYOVYOTE.
FANYA HIVYO KILA SIKU, KILA UPATAPO MUDA.
Basi ngoja dada Rose Muhando aikamilishe jumapili hii ni wimbo huu UTAMU WA YESU!!
JUMAPILI NJEMA SANA KWA WOTE NA WOTE MNAPENDWA!!
Baba yetu uliye Mbinguni,
Jina lako litukuzwe,
Ufalme wako ufike,
Utakalo lifanyike , duniani kama Mbinguni.
Utupe leo mkate wetu wa kila siku,
Utusemehe makosa yetu, kama tunavyowasamehe na sisi waliotukosea.
Usitutie katika vishawishi, lakini utuokoe maovuni.(Kwa kuwa ufalme ni wako, na nguvu, na utukufu, hata milele. Amina
HII SALA IMEBEBA MAOMBI YOTE, LIKIWEMO LA KUSAMEHEWA DHAMBI NA KUOMBA RIZIKI.
UKISALI HII , HUNA HAJA YA KUSALI VINGINE VYOVYOTE.
FANYA HIVYO KILA SIKU, KILA UPATAPO MUDA.
Basi ngoja dada Rose Muhando aikamilishe jumapili hii ni wimbo huu UTAMU WA YESU!!
JUMAPILI NJEMA SANA KWA WOTE NA WOTE MNAPENDWA!!
Sunday, February 12, 2012
NI JUMAPILI YA PILI YA MWEZI HUU NA TUSALI SALA HII!!!
Ee Mungu unifanya niwe chombo cha amani yako. Penye chuki nilete mapatano, penye kukata tamaa nilete matumaini, penye huzuni furaha, Amina
JUMAPILI NJEMA KWA WOTE!!
JUMAPILI NJEMA KWA WOTE!!
Sunday, December 18, 2011
NAWATAKIENI WOTE JUMAPILI NJEMA !!!
Ee Yesu, ususamehe dhambi zetu.
Utuepushe na moto wa milele.
Ongoza roho zote mbinguni.
Hasa za wale wanaohitaji huruma yako. Amina
JUMAPILI NJEMA NA AMANI NA UPENDO VIWE NANYI DAIMA.
Utuepushe na moto wa milele.
Ongoza roho zote mbinguni.
Hasa za wale wanaohitaji huruma yako. Amina
JUMAPILI NJEMA NA AMANI NA UPENDO VIWE NANYI DAIMA.
Sunday, February 27, 2011
JUMAPILI NJEMA KWA WOTE:- Ni jumapili ya 8 ya mwaka A
Baba yetu uliye Mbinguni,
Jina lako litukuzwe,
Ufalme wako ufike,
Utakalo lifanyike , duniani kama Mbinguni.
Utupe leo mkate wetu wa kila siku,
Utusemehe makosa yetu, kama tunavyowasamehe na sisi waliotukosea.
Usitutie katika vishawishi, lakini utuokoe maovuni.(Kwa kuwa ufalme ni wako, na nguvu, na utukufu, hata milele Amina)
JUMAPILI NJEMA KWA WOTE NA MWANZO MWEMA WA WIKI...TUTAONANA TENA WAKATI MWINGINE
Jina lako litukuzwe,
Ufalme wako ufike,
Utakalo lifanyike , duniani kama Mbinguni.
Utupe leo mkate wetu wa kila siku,
Utusemehe makosa yetu, kama tunavyowasamehe na sisi waliotukosea.
Usitutie katika vishawishi, lakini utuokoe maovuni.(Kwa kuwa ufalme ni wako, na nguvu, na utukufu, hata milele Amina)
JUMAPILI NJEMA KWA WOTE NA MWANZO MWEMA WA WIKI...TUTAONANA TENA WAKATI MWINGINE
Sunday, January 30, 2011
NI JUMAPILI YA TANO NA YA MWISHO YA MWEZI HUU NAWATAKIENI JUMAPILI NJEMA!!!
Katika jumapili hii ya mwisho na ya tano ya mwezi huu basi nimeona tuimalize kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa sala hii :- SALA YA MKE KUMWOMBEA MUMEWE Ee Bwana , ni ajabu, Jinsi fikra zangu zinavyomrudia kila mara Huyu, mume wangu, Mwenzi anayeshiriki maisha yangu kwa namna ya pekee. Ninapofagia nyumba na mazingira yake, Nataka kutengeneza nyumba nzuri kwa ajili yake. Ninapopika chakula vizuri,Napenda kumfurahisha. Ninaponunua nguo mpya na kujaribu kuonekana mrembo, Ni kwa ajili yake tena, Ee Bwana. Na ninaweza kukuambia kwamba Ninamwonea fahari, Anafanya kazi kwa bidii ili kupata riziki yetu; Ni mtu mwenye haki, mwadilifu, Naye hujitahidi kutufurahisha. Kwangu, yeye ni mpole na mwangalifu. Hunijali na kuonyesha kweli kwamba anajali. Hunifanya mimi nijiamini mwenyewe, Anajua jinsi ya kuondoa hofu zangu, Hunipatia usalama na upendo ambao nahitaji sana. Ee Bwana, ninakuomba, Umbariki na umlinde. Katika safari zake, umfikishe salama. Kazini mwake, umpe fanaka Na hapa, nyumbani petu naomba apate amani na heri. Bwana, unisaidie mimi pia Niweze kuwa yule mke anayehitaji. Unifanye niwe mtu anayeweza kumwamini daima, Mwanamke ambaye anaweza kumfurahia, Niweze kumsaidia asahau matatizo yake, Niweze kuondolea mbali hofu zake na kupunguza uchungu wake. Bwana, Wewe ndiwe uliyenipa mume huyu, Na katika yeye,Umenipatia sehemu ya nafsi yako mwenyewe. Ninakusifu kwa ajili yake, Ee Bwana.
Sunday, December 19, 2010
Sunday, November 28, 2010
LEO NI JUMAPILI YA KWANZA YA MAJILIO/IDAG ÄR FÖRSTA ADVENT!!!!!
Jumapili ya kwanza ya majilio/Först Advent!!!Nimeipenda sala hii ya kaka Baraka Chibiriti na nimeona ni vizuri kuitumia jumapili hii ya leo.Ukizingatia ni jumapili ya kwanza ya majilio haya hebu tusali kwa pamoja.
Nia yangu naileta kwako Bwana Mungu wangu, nakuomba Bwana unisikie ninalia kwa uchungu. Nakuomba uipokee sala yangu, sikiliza na sauti ya kilio changu. Ninajua Bwana siku zote wewe hupatikani kwenye gasia, ninajua siku zote wewe hupatikani kwenye vurugu.
Bwana nijaie utulivu wa moyo na nipe nguvu nimshinde mwovu shetani, shusha roho wako anipe faraja. Bwana niongoze ili nitimize nia yangu ya kuwa mtumishi wako mwema!
Ee Bwana upo wapi mimi ninakutafuta, nitazame kwa huruma nateseka Mungu wangu...nakuomba uipokee sala yangu na uisikilize sauti ya kilio changu.
Hata kama nipo kama takataka mbele za watu...lakini mbele yako mimi nina thamani kubwa sana siku zote, kwa hili niajua na ninauhakika kwamba wewe pekee ndiwe wenye kunithamini, nakuomba uipokee sala yangu na uisikilize sauti ya kilio changu.
Ee Bwana wangu nijalie nikabili njia zangu, nimshinde huyu mwovu shetani hanifai kabisa. Bwana Mungu wangu wewe ndiwe tegemeo la maisha yangu yote hapa Duniani, nitausifu na kuku tegemea wewe daima siku zote za maisha yangu!
Sunday, May 9, 2010
Jumapili ya leo na tusali sala hizi na pia tusikilize wimbo huu uitwao Neema yake!!!
SALA YA ASUBUHI
Siku mpya inaanza, Nimuabudu Mungu kwanza: Mungu wangu baba yangu, Upokee shukrani yangu. Wewe kwa usiku mzima, ulikuwa kwangu daima: kunilinda kwa amani na mitego ya shetani. Kwako baba wa milele, Ninaomba neema tele: Niepuke dhambi zote, Nikutumikie pote. Ubariki kazi yangu, Shida na furaha Zangu. Mama safi ee Maria, Nipe msaada wako pia. Ee malaika kiongozi, Nipeleke kwa Mwokozi. Yesu nijalie neema, Niwe daima mkristo mwema. Amina.
NIA NJEMA
Nia na kusudi langu, Kumheshimu Mungu wangu. Najiunga kwa imani Na mkombozi msalabani. Roho, mwili chote changu Pendo na uzima wangu, Wazo neno tendo lote, Namtolea Mungu yote. Mungu wangu nakupenda, Wala dhambi sitatenda. Iwe kazi, nipumzike, Amri zako tu nishike. Utakalo nitimize. Kila kazi nimalize. Litukuzwe jina lako, Siku nzima iwe yako. Kwa utii navumilia Shida na matata pia. Nipe, Bwana neema zako, Niongeze sifa yako. Amina.
SALA YA JIONI
Sasa siku inakwisha. Kwako, Mungu, napandisha. Moyo wangu kwa shukrani, Nipumzike kwa amani. Mema mengi umenipa, Ninashindwa kukulipa. Baba mwema, ondolea Yote niliyokosea. Yesu mpenzi, Unijie, Ombi langu usikie: Unifiche mtoto wako Ndani ya jeraha zako. Ewe mama, nipe neema, Raha na usiku mwema. Roho mlinzi, ukakeshe, Pepo asinikoseshe. Naiweka roho yangu Mikononi mwa Babangu. Bila hofu napumzika, Mwisho kwako nitafika. Amina.
NA NAPENDA KUWATAKIENI WOTE JUMAPILI/DOMINIKA NJEMA. NI JUMAPILI YA 19 YA MWAKA HUU NA YA PILI YA MWEZI HUU WA TANO!!!!
Siku mpya inaanza, Nimuabudu Mungu kwanza: Mungu wangu baba yangu, Upokee shukrani yangu. Wewe kwa usiku mzima, ulikuwa kwangu daima: kunilinda kwa amani na mitego ya shetani. Kwako baba wa milele, Ninaomba neema tele: Niepuke dhambi zote, Nikutumikie pote. Ubariki kazi yangu, Shida na furaha Zangu. Mama safi ee Maria, Nipe msaada wako pia. Ee malaika kiongozi, Nipeleke kwa Mwokozi. Yesu nijalie neema, Niwe daima mkristo mwema. Amina.
NIA NJEMA
Nia na kusudi langu, Kumheshimu Mungu wangu. Najiunga kwa imani Na mkombozi msalabani. Roho, mwili chote changu Pendo na uzima wangu, Wazo neno tendo lote, Namtolea Mungu yote. Mungu wangu nakupenda, Wala dhambi sitatenda. Iwe kazi, nipumzike, Amri zako tu nishike. Utakalo nitimize. Kila kazi nimalize. Litukuzwe jina lako, Siku nzima iwe yako. Kwa utii navumilia Shida na matata pia. Nipe, Bwana neema zako, Niongeze sifa yako. Amina.
SALA YA JIONI
Sasa siku inakwisha. Kwako, Mungu, napandisha. Moyo wangu kwa shukrani, Nipumzike kwa amani. Mema mengi umenipa, Ninashindwa kukulipa. Baba mwema, ondolea Yote niliyokosea. Yesu mpenzi, Unijie, Ombi langu usikie: Unifiche mtoto wako Ndani ya jeraha zako. Ewe mama, nipe neema, Raha na usiku mwema. Roho mlinzi, ukakeshe, Pepo asinikoseshe. Naiweka roho yangu Mikononi mwa Babangu. Bila hofu napumzika, Mwisho kwako nitafika. Amina.
NA NAPENDA KUWATAKIENI WOTE JUMAPILI/DOMINIKA NJEMA. NI JUMAPILI YA 19 YA MWAKA HUU NA YA PILI YA MWEZI HUU WA TANO!!!!
Sunday, April 25, 2010
NGOJA LEO TUSALI KWA PAMOJA :- SALA YA ASUBUHI
Siku mpya inaanza, Nimuabudu Mungu kwanza,Mungu wangu baba yangu, upokee shukrani yangu. Wewe kwa usiku mzima, ulikuwa kwangu daima,kunilinda kwa amani na mitego ya shetani. Kwako baba wa milele, Ninaomba neema tele, Niepuke dhambi zote. Nikutumikie pote. Ubariki kazi yangu, Shida na furaha Zangu. Mama safi ee Maria, Nipe msaada wako pia. Ee malaika kiongozi, Nipeleke kwa Mwokozi. Yesu nijalie neema, Niwe daima mkristo mwema. Amina.
NA KUMBUKENI NI JUMAPILI YA 17 YA MWAKA. JUMAPILI NJEMAZ WOOOOTE!!!
NA KUMBUKENI NI JUMAPILI YA 17 YA MWAKA. JUMAPILI NJEMAZ WOOOOTE!!!
Sunday, April 11, 2010
Nakuomba Mola Wangu
Nimechoka nimechoka, nimechoka peke yangu,
Mwenzenu nataabika, nahisi dunia chungu,
Nimechoka hangaika, namhitaji mwenzangu,
Nakuomba Mola wangu, nipatie mke mwema.
Nahitaji nami oa, kwani muda umefika,
Nimpate aso doa, mke alokubalika,
Niwe nayo njema ndoa, siyo ya kukurupuka,
Nakuomba Mola wangu, nipatie mke mwema.
Binti ntayempata, ajue kumcha Mungu,
Asiwe mwenye kunata, awe'shimu ndugu zangu,
Aitike nikimwita, hata mbele ya wenzangu,
Nakuomba Mola wangu, nipatie mke mwema.
Ajaaliwe nidhamu, nidhamu ya kwelikweli,
Ajawe na ufahamu, kufikiri mara mbili,
Hekima nayo muhimu, mazingira kukabili,
Nakuomba Mola wangu, nipatie mke mwema.
Sitaki mwenye kiburi, huyo ataniumiza,
Sitoitoa mahari, mwenye kukiendekeza,
Napenda ajidhihiri, hivyo asije nitweza,
Nakuomba Mola wangu, nipatie mke mwema.
Awe amefunzwa vema, awe na njema tabia,
Yawe maisha salama, asiruke na dunia,
Mola 'tatupa uzima, tutamtumainia,
Nakuomba Mola wangu, nipatie mke mwema.
Awe na uvumilivu, majira hayafanani,
Siku tukila pakavu, asizue tafrani,
Asitende jambo ovu, kuniweka matatani,
Nakuomba Mola wangu, nipatie mke mwema.
Sitochagua kwa dini, kabila ama kwa rangi,
Nitampenda moyoni, yeyote mi' simpingi,
Anifae maishani, ndilo jambo la msingi,
Nakuomba Mola wangu, nipatie mke mwema.
Na watoto tuwazae, Mungu akitujalia,
Tasa 'simnyanyapae, dunia kuichukia,
Kwa dhiki nikamfae, apate kujivunia,
Nakuomba Mola wangu, nipatie mke mwema.
Kuna kitu namwahidi, kwake nitakuwa mwema,
Sitofanya ukaidi, nitamw'eshimu daima,
Kwani kwake sina budi, kumwongoza kwa hekima,
Nakuomba Mola wangu, nipatie mke mwema.
Nitakuwa mwaminifu, kamwe sitomwumiza,
'Tamjali mara alfu, dhikini kumliwaza,
Na watu watamsifu, maana atapendeza,
Nakuomba Mola wangu, nipatie mke mwema.
Kaditama nimalize, kwa beti zangu dazeni,
Afaaye 'jitokeze, nimweke mwangu moyoni,
Mmoja tu nimtuze, huyo huyo maishani,
NAKUOMBA MOLA WANGU, NIPATIE MKE MWEMA.
Nimechoka hangaika, namhitaji mwenzangu,
Nakuomba Mola wangu, nipatie mke mwema.
Nahitaji nami oa, kwani muda umefika,
Nimpate aso doa, mke alokubalika,
Niwe nayo njema ndoa, siyo ya kukurupuka,
Nakuomba Mola wangu, nipatie mke mwema.
Binti ntayempata, ajue kumcha Mungu,
Asiwe mwenye kunata, awe'shimu ndugu zangu,
Aitike nikimwita, hata mbele ya wenzangu,
Nakuomba Mola wangu, nipatie mke mwema.
Ajaaliwe nidhamu, nidhamu ya kwelikweli,
Ajawe na ufahamu, kufikiri mara mbili,
Hekima nayo muhimu, mazingira kukabili,
Nakuomba Mola wangu, nipatie mke mwema.
Sitaki mwenye kiburi, huyo ataniumiza,
Sitoitoa mahari, mwenye kukiendekeza,
Napenda ajidhihiri, hivyo asije nitweza,
Nakuomba Mola wangu, nipatie mke mwema.
Awe amefunzwa vema, awe na njema tabia,
Yawe maisha salama, asiruke na dunia,
Mola 'tatupa uzima, tutamtumainia,
Nakuomba Mola wangu, nipatie mke mwema.
Awe na uvumilivu, majira hayafanani,
Siku tukila pakavu, asizue tafrani,
Asitende jambo ovu, kuniweka matatani,
Nakuomba Mola wangu, nipatie mke mwema.
Sitochagua kwa dini, kabila ama kwa rangi,
Nitampenda moyoni, yeyote mi' simpingi,
Anifae maishani, ndilo jambo la msingi,
Nakuomba Mola wangu, nipatie mke mwema.
Na watoto tuwazae, Mungu akitujalia,
Tasa 'simnyanyapae, dunia kuichukia,
Kwa dhiki nikamfae, apate kujivunia,
Nakuomba Mola wangu, nipatie mke mwema.
Kuna kitu namwahidi, kwake nitakuwa mwema,
Sitofanya ukaidi, nitamw'eshimu daima,
Kwani kwake sina budi, kumwongoza kwa hekima,
Nakuomba Mola wangu, nipatie mke mwema.
Nitakuwa mwaminifu, kamwe sitomwumiza,
'Tamjali mara alfu, dhikini kumliwaza,
Na watu watamsifu, maana atapendeza,
Nakuomba Mola wangu, nipatie mke mwema.
Kaditama nimalize, kwa beti zangu dazeni,
Afaaye 'jitokeze, nimweke mwangu moyoni,
Mmoja tu nimtuze, huyo huyo maishani,
NAKUOMBA MOLA WANGU, NIPATIE MKE MWEMA.
Shairi limetungwa na Fadhy mtanga nami nimevutiwa nikaona niweka hapa ili tujifunze kwa pamoja. NA NAPENDA KUWATAKIENI WOTE JUMAPILI/DOMINIKA NJEMA. NI JUMAPILI YA 15 YA MWAKA HUU!!!!
Friday, March 5, 2010
Heri ya Siku ya Kuzaliwa Mume,Baba na Shemeji pia Rafiki yetu
Ni siku yako leo mwl. Klayson
Tunaanza na kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa sala hii :- SALA YA MKE KUMWOMBEA MUMEWE
Ee Bwana , ni ajabu,
Jinsi fikra zangu zinavyomrudia kila mara
Huyu, mume wangu,
Mwenzi anayeshiriki maisha yangu kwa namna ya pekee.
Ninapofagia nyumba na mazingira yake,
Nataka kutengeneza nyumba nzuri kwa ajili yake.
Ninapopika chakula vizuri,Napenda kumfurahisha.
Ninaponunua nguo mpya na kujaribu kuonekana mrembo,
Ni kwa ajili yake tena, Ee Bwana.
Na ninaweza kukuambia kwamba
Ninamwonea fahari,
Anafanya kazi kwa bidii ili kupata riziki yetu;
Ni mtu mwenye haki, mwadilifu,
Naye hujitahidi kutufurahisha.
Kwangu, yeye ni mpole na mwangalifu.
Hunijali na kuonyesha kweli kwamba anajali.
Hunifanya mimi nijiamini mwenyewe,
Anajua jinsi ya kuondoa hofu zangu,
Hunipatia usalama na upendo ambao nahitaji sana.
Ee Bwana, ninakuomba,
Umbariki na umlinde.
Katika safari zake, umfikishe salama.
Kazini mwake, umpe fanaka
Na hapa, nyumbani petu naomba apate amani na heri.
Bwana, unisaidie mimi pia
Niweze kuwa yule mke anayehitaji.
Unifanye niwe mtu anayeweza kumwamini daima,
Mwanamke ambaye anaweza kumfurahia,
Niweze kumsaidia asahau matatizo yake,
Niweze kuondolea mbali hofu zake na kupunguza uchungu wake.
Bwana, Wewe ndiwe uliyenipa mume huyu,
Na katika yeye,Umenipatia sehemu ya nafsi yako mwenyewe.
Ninakusifu kwa ajili yake, Ee Bwana.
Na leo twakumbuka siku muhimu saana maishani mwako. Siku iiliyoanzisha yote mazuri/mema tujivuniayo maishani kwa uwepo wako. Ni SIKU HII ULIYOZALIWA
Zaidi mtembelee Mwalimu Klayson http://matetereka.blogspot.com/
Tunapenda kusindikiza siku hii na mwanamziki ambaye anampenda sana kwa wimbo huu wa DR. REMMY ONGALA Uitwao NARUDI NYUMBANI ni.
Ee Bwana , ni ajabu,
Jinsi fikra zangu zinavyomrudia kila mara
Huyu, mume wangu,
Mwenzi anayeshiriki maisha yangu kwa namna ya pekee.
Ninapofagia nyumba na mazingira yake,
Nataka kutengeneza nyumba nzuri kwa ajili yake.
Ninapopika chakula vizuri,Napenda kumfurahisha.
Ninaponunua nguo mpya na kujaribu kuonekana mrembo,
Ni kwa ajili yake tena, Ee Bwana.
Na ninaweza kukuambia kwamba
Ninamwonea fahari,
Anafanya kazi kwa bidii ili kupata riziki yetu;
Ni mtu mwenye haki, mwadilifu,
Naye hujitahidi kutufurahisha.
Kwangu, yeye ni mpole na mwangalifu.
Hunijali na kuonyesha kweli kwamba anajali.
Hunifanya mimi nijiamini mwenyewe,
Anajua jinsi ya kuondoa hofu zangu,
Hunipatia usalama na upendo ambao nahitaji sana.
Ee Bwana, ninakuomba,
Umbariki na umlinde.
Katika safari zake, umfikishe salama.
Kazini mwake, umpe fanaka
Na hapa, nyumbani petu naomba apate amani na heri.
Bwana, unisaidie mimi pia
Niweze kuwa yule mke anayehitaji.
Unifanye niwe mtu anayeweza kumwamini daima,
Mwanamke ambaye anaweza kumfurahia,
Niweze kumsaidia asahau matatizo yake,
Niweze kuondolea mbali hofu zake na kupunguza uchungu wake.
Bwana, Wewe ndiwe uliyenipa mume huyu,
Na katika yeye,Umenipatia sehemu ya nafsi yako mwenyewe.
Ninakusifu kwa ajili yake, Ee Bwana.
Na leo twakumbuka siku muhimu saana maishani mwako. Siku iiliyoanzisha yote mazuri/mema tujivuniayo maishani kwa uwepo wako. Ni SIKU HII ULIYOZALIWA
Zaidi mtembelee Mwalimu Klayson http://matetereka.blogspot.com/
Tunapenda kusindikiza siku hii na mwanamziki ambaye anampenda sana kwa wimbo huu wa DR. REMMY ONGALA Uitwao NARUDI NYUMBANI ni.
Sunday, February 28, 2010
TUMALIZE DOMINIKA HII YA MWISHO YA MWEZI HUU FEBRUARI KWA WIMBO HUU!!
Napenda kuwatakieni wote jumapili/dominika hii kwa wimbo huu. Na pia ni Dominika/Jumapili ya mwisho ya mwezi huu Februari. Duh! Jamani siku zinakimbia kweli. Ok, JUMAPILI/DOMINIKA NJEMA KWA WOTE JAMANI
Sunday, February 7, 2010
Jumapili hii ya sita ya mwaka tusali sala hii!!!!!!
Ee Mungu unifanya niwe chombo cha amani yako. Penye chuki nilete mapatano, penye kukata tamaa nilete matumaini, penye huzuni furaha, Amina
Sunday, January 31, 2010
NAPENDA KUWATAKIENI WOTE JUMAPILI NJEMA KWA SALA HII
Mungu nakuomba unisaidie niwakumbuke wenye njaa ninapokuwa na chakula, wagonjwa nianpokuwa na afya nzuri, wote wanaoteseka kwa sababu ya vita ninapokuwa na amani, wasio na nyumba ninapokuwa nimelala na pia kuwa ndani ya nyumba yenye joto, pia nakuomba unisaidia niwakumbuke yatima kila ninapokuwa na wazazi wangu.
Na pia nakuomba:Bikira Maria mama wa msaada na uibariki familia yangu, kaka zangu, dada zangu, wazazi wangu na watu wote dunia hii katika dhambi: AMINA
JUMAPILI NJEMA KWA WOTE JAMANI NA PIA NI JUMAPILI YA TANO NA YA MWISHO YA MWEZI HUU!!!!!!!!JANUARI
Na pia nakuomba:Bikira Maria mama wa msaada na uibariki familia yangu, kaka zangu, dada zangu, wazazi wangu na watu wote dunia hii katika dhambi: AMINA
JUMAPILI NJEMA KWA WOTE JAMANI NA PIA NI JUMAPILI YA TANO NA YA MWISHO YA MWEZI HUU!!!!!!!!JANUARI
Subscribe to:
Posts (Atom)


