1. Huondoa halafu mbaya ya kinywa:-
Tofauti na vyakula vingine kama kitunguu swaumu. Tangawizi husaidia uwe na halafu nzuri pale unapopumua na kufanya maeneo ya mdomo kuwa safi.
2. Msukumo wa damu:-
Tangawizi husaidia msukumo wa damu mwilini kwa sababu huupa mwili joto ambalo mara nyingi mwili huhitaji wakati wa usukumaji wa damu mwilini
3. Huondoa magonjwa ya asubuhi:-
Licha ya kuwa tiba ya magonjwa kama kikohozi na mafua, tangawizi pia husaidia kupunguza magonjwa ya asubuhi kama uchovu na mninginio. Kwa akina mama wajawazito, tangawizi huwapunguzia homa za asubuhi wanapoamka, pia hutumika kama kichocheo cha utulivu.
4. Mfumo wa chakula:-
Husaidia mwili kunyonya virutubisho kwenye chakula. Hii husaidia sana pale unapoamua kupunguza uzito wa mwili na kupata virutubisho vilivyo muhimu.
5. Kurekebisha sukari ya mwili:-
Tangawizi husaidia katika kuweka sawa kiwango cha sukari kwenye damu. Wagonjwa wa kisukari wanashauriwa kutumia tangawizi badala ya chai.
6. Hamu ya kula:-
Huongeza hamu ya kula chakula. Kwa wale wenye mfumo mbaya wa umengényaji wa chakula wanashauriwa kutumia tangawizi ili kupata mfumo mzuri wa mmengényo wa chakula.
7. Uzalishaji wa mate:-
Tangawizi husaidia uzalishaji wa mate mdomoni. Kuongezeka kwa mate mdomoni husaidia kutengeneza vichocheo muhimu vinavyosaidia wakati wa kula na kupunguza uwezekano wa magonjwa ya meno.
8. Kuyeyusha mafuta
Tangawizi husaidia kupunguza kuganda kwa mafuta mwilini ambayo yana madhara makubwa mwilini. Hasa magonjwa ya kiharusi na shinikizo la damu.
9. Kuondoa sumu mwilini:-
Tangawizi husaidia kupunguza kichefuchefu na kutapika. Pia husaidia sana kwa wale watu waliotumia sana madawa na kuwa na sumu nyingi mwilini.
10. Tangawizi humsaidia mtu mwenye vidonda vya tumbo kwa kupunguza maumivu na hata kuponya vidonda hivyo kama vitakuwa kwenye hatua ya awali sana.
PANAPO MAJALIWA!!!
Showing posts with label Afya. Show all posts
Showing posts with label Afya. Show all posts
Monday, April 11, 2016
Wednesday, March 23, 2016
SABABU 4 AMBAZO KAMWE HUPASWI KUACHA KWENDA HAJA NDOGO PALE MAUMBILE YANAPOTAKA UFANYE HIVYO…
ANAHITAJI KWENDA HAJA NDOGO
Wote tunajua kwamba pale tunapokuwa tumebanwa kweli kweli na haja ndogo(mkojo).Wakati mwingine huwa tunalazimika kwa muda mrefu kukaa bila kwenda haja ndogo na
hata mwishowe kuhisi kana kwamba kibofu kinataka kupasuka.
Wakati mwingine tunakuwa katika sehemu ambazo hakuna maliwato yaliyoko karibu na
wakati mwingine huwa tunakuwa na marafiki tukipiga soga kiasi kwamba hutuwia
vigumu kuacha kukatisha mazungumzo ili kukidhi hitaji hilo la kimaumbile, lakini pia
wakati mwingine huweza kuwa na foleni ndefu kwenda maliwato hasa katika maeneo ya
Mighahawa au maeneo ya jumuia.
Zipo sababu nyingi kwa nini wakati mwingine yatupasa kuvumilia/kutunza mkojo kwa
muda mrefu iwezekanavyo kutokana na maeneo tuliyopo kutokuwa rafiki katika kukidhi
hitaji hilo la kimaumbile lakini ni vyema tukijua kwamba jambo hilo lina athari kubwa
kiafya kwetu.
Kwa nini inasisitizwa kwamba tunapokuwa na hitaji hilo la kimaumbile tutafute mahali pa
kujisitiri haraka iwezavyo. Ni kwamba kibofu cha mkojo ni chombo ambacho kinaweza
kubeba/kutunza hadi lita 0.5 za mkojo. Wakati kibofu kikiwa kimejaa kama theluthi mbili
ubongo huwa unapata hisia kwamba ni lazima ukojoe. Lakini kwa sababu mawasiliano
kati ya kibofu cha mkojo na ubongo ni sehemu ya mfumo wa neva involuntary, unaweza
kuamua ni muda gani unaweza kukojoa - hivyo kuna wengi ambao wanaweza kukaa na
mkoja kwa muda mrefu, lakini hata hivyo ni vyema tukijua kwamba jambo hilo ni hatari
kwa afya zetu.
Hizi hapa ni sababu nne(4) kwa nini hupaswi kukaa na mkojo kwa muda mrefu.
1. Unaweza kupata maambukizi kwenye njia ya mkojo
Kama hukojoi kuna hatari bakteria kuwa wengi/kuzidi katika mkusanyiko wa mkojo huo
watafiti wa (illusterad vetenskap) wanasema wakati unapokojoa bakteria wanatoka nje
ya vimelea(bomba la mkojo). Bakteria, mara nyingi koli bakteria kutoka kwenye utumbo
inaweza kusababisha magonjwa ya maambukizi kwenye njia ya mkojo ambayo inaweza
kukua na kuwa hatari kwa figo. Hii kwa upande mwingine inaweza kusababisha sumu
kwenye damu utafiti umegundua hivyo.
2. Kibofu cha mkojo chaweza kuvuja mara kwa mara.
Kama unatunza mkojo mara nyingi kibofu cha mkojo wako kitatanuka na kuwa kilegevu.
Hii inaweza kusababisha tatizo la udhaifu wa kibofu kuwa mtepetevu ambapo mkojo
unaweza kuwa unatoka wenyewe matone matone kila wakati na matone huishia
kwenye nguo ya ndani na hapo ndipo mtu hujikuta unanuka mkojo mara kwa mara.
3. Unaweza kusababsha uharibifu wa figo:-
Mkojo unaozalishwa katika figo wakati unapoutunza mkojo huo kwa muda mrefu kiasi
cha kibofu cha mkojo kukaza kwa kuzidiwa basi figo hufanya kazi ya kupeleka mkojo
katika njia ya bomba la mkojo kwa shinikizo (presha) na unapoendelea kuzuia ndipo
unaposababisha athari kiafya. Utafiti wa Illustrared Vetenskap umebainisha kwamba hali
hiyo inaweza kusababisha uharibifu wa figo.
4. Kibofu cha mkojo kinaweza kupasuka na tumbo lako kujaa mkojo.
Kibofu cha mkojo kinaweza kupasuka. Lakini ni nadra, kwa kawaida watu ambao
wamepata tatizo la kibofu cha mkojo au ulevi ambapo mwili waweza "kusahau" kukojoa.
Wakati kibofu cha mkojo kikipasuka mkojo hutawanyika katika tumbo na unaweza
kueneza maambukizi na pia huwa na maumivu makali sana na athari nyingine kiafya.
NIMEONA NIWASHIRIKISHE HABARI HII ILI TUWE MAKINI KWENDA DAIMA HAJA
NDOGO PALE TUNAPOHITAJI, ILI KUEPUKA HIZI HATARI.
CHANZO: NEWSNER VATENSKAP.
Wednesday, March 9, 2016
AFYA:- KAMA UANATAKA KUACHANA NA POMBE ZINGATIA HAYA.....
Kama ni mlevi na unahisi huwezi kuacha kunywa kwa siku moja, anza kwa kupunguza kiwango cha kunywa, yaaani kama unakunywa bia tatu kwa siku , anza kunywa moja, baadae moja kwa siku mbili mpaka utakapozoea kuishi bila pombe/kileo.
Epuka kuweka kilevi au pambe nyumbani au sehemu ya kazi ili kuepuka majaribu.
Usipende kuruka mlo, kula chakula mara tatu (3) mpaka mara nne (4) kwa siku ili kuupatia mwili virutubisho vyote muhimu.
Ondoa dhamira potofu kwamba huwezi kuishi pasipo kunywa pombe. Kumbuka mwili wako umeumbwa kikamilifu kukabili hali zote za maisha, hivyo usihisi kuwa pombe ndio kichochea chako kila unapotaka kufanya jambo fulani.
Zingatia mlo kamili, na jifunze kula matunda kwa mwingi. Hasa kama ulikuwa huli.
Anza kufanya mazoezi na upange ratiba yako ule muda ambao ulikuwa ukitumia kunywa pombe.
Kumbuka mambo mabaya yaliyokutokea kutokana na pombe katika maisha yako. Hii itakusaidia kutothubutu tena kunywa pombe.
Ongeza unywaji wa maji, jiwekee mazoea ya kunywa maji angalao glasi tano (5) kwa siku.
Kuwa na tabia ya kujizawadia/kujipongeza kutokana na uamuzi wako mzuri wa kutokunywa pombe.
Ni muhimu kuwashirikisha ndugu, jamaa na marafiki wa karibu kuhusu uamuzi wako wa kuacha pombe/kileo na pia usijione mjinga kwa wale watakao kucheka.
PANAPO MAJALIWA.KAPULYA WENU!
Epuka kuweka kilevi au pambe nyumbani au sehemu ya kazi ili kuepuka majaribu.
Usipende kuruka mlo, kula chakula mara tatu (3) mpaka mara nne (4) kwa siku ili kuupatia mwili virutubisho vyote muhimu.
Ondoa dhamira potofu kwamba huwezi kuishi pasipo kunywa pombe. Kumbuka mwili wako umeumbwa kikamilifu kukabili hali zote za maisha, hivyo usihisi kuwa pombe ndio kichochea chako kila unapotaka kufanya jambo fulani.
Zingatia mlo kamili, na jifunze kula matunda kwa mwingi. Hasa kama ulikuwa huli.
Anza kufanya mazoezi na upange ratiba yako ule muda ambao ulikuwa ukitumia kunywa pombe.
Kumbuka mambo mabaya yaliyokutokea kutokana na pombe katika maisha yako. Hii itakusaidia kutothubutu tena kunywa pombe.
Ongeza unywaji wa maji, jiwekee mazoea ya kunywa maji angalao glasi tano (5) kwa siku.
Kuwa na tabia ya kujizawadia/kujipongeza kutokana na uamuzi wako mzuri wa kutokunywa pombe.
Ni muhimu kuwashirikisha ndugu, jamaa na marafiki wa karibu kuhusu uamuzi wako wa kuacha pombe/kileo na pia usijione mjinga kwa wale watakao kucheka.
PANAPO MAJALIWA.KAPULYA WENU!
Monday, March 7, 2016
JUMATATU HII TUANZE HIVI! MUHIMU:- FAIDA KUMI ZA KUNYWA MAJI MOTO YENYE LIMAO KILA UNAPOAMKA
1. Huongeza kinga yako ya mwili hasa kupambana na magonjwa madogo madogo kama vile mafua na kikohozi kutokana na kuwa na vitamini C
2. Husafisha mfumo wako wa chakula, kuondoa sumu mwilini na kuzuia gesi kujaa tumboni mara kwa mara.
3. Huleta hewa safi kinywani.
4. Hukuongezea uchangamfu na kufanya siku yako ianze vizuri sana.
5. Husaidia majeraha kupona kwa haraka kutokana na kuwa (ascorbic acid) asidi ya kutosha. Pia huimarisha mifupa.
6. Husaidia mmengènyo wa chakula utakachokula asubuhi au mchana kwa kuondoa vikwazo vyote vinavyoweza kuzuia umengényaji wa chakula.
7. Huimarisha ngozi yako, kuondoa makunyanzi na kukupa muonekano mzuri.
8. Husaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza uzito kwani maji moto ya limao huyeyusha mafuta ya kutosha
9. Huyapa macho yako afya nzuri na kuimarisha kuona
10. Huondoa hali ya kuhitaji kahawa kila asubuhi ambayo si nzuri kiafya.
2. Husafisha mfumo wako wa chakula, kuondoa sumu mwilini na kuzuia gesi kujaa tumboni mara kwa mara.
3. Huleta hewa safi kinywani.
4. Hukuongezea uchangamfu na kufanya siku yako ianze vizuri sana.
5. Husaidia majeraha kupona kwa haraka kutokana na kuwa (ascorbic acid) asidi ya kutosha. Pia huimarisha mifupa.
6. Husaidia mmengènyo wa chakula utakachokula asubuhi au mchana kwa kuondoa vikwazo vyote vinavyoweza kuzuia umengényaji wa chakula.
7. Huimarisha ngozi yako, kuondoa makunyanzi na kukupa muonekano mzuri.
8. Husaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza uzito kwani maji moto ya limao huyeyusha mafuta ya kutosha
9. Huyapa macho yako afya nzuri na kuimarisha kuona
10. Huondoa hali ya kuhitaji kahawa kila asubuhi ambayo si nzuri kiafya.
Thursday, December 5, 2013
MATUNDA NI MUHIMU KATIKA AFYA ZETU TUZINGATIE...
Huu ni mlo wangu wa leo mchana mchanganyiko wa matunda mbalimbali. Kama ilivyo ni kwamba matunda ni muhimu katika afya zetu. Usisahau kula hata tunda moja tu kwa siku....Kila la kheri kwa wote....
Friday, September 13, 2013
MDADA KAPULYA SI MTU WA KUTULIA ..MSIMU WA BUSTANI UNAKARIBIA KWISHA NA SASA WAJA MSIMU KUCHUMA UYOGA NAYE NI MPENZI SANA WA KAZI HII KWA HIYO LEO ALIKWENDA MSTUNI NA HAPA NI MATOKEO YAKE....
Kuchuma uyoga ni kitu ambacho nakipenda sana , unakuwa na wakati mzuri wa kutafakari, pia mazoezi nahalafu unapata mboga ..Mboga hii mimi nimeipata bure leo mstuni lakini kama ningekwenda kuinunua dukani kwa kilo ni kama kwa kila shilinga 23000/= . Nami nilipata lita kama tano hivi. Sasa kazi nyingine unaporudi nyumbani ni kuusafisha na ndio hapo nafanya kutoa mchanga na takataka nyingine,,,,
Baada ya masaa matatu uyoga tayari umetolewa takataka zote na upo safi kwa kuliwa.....
...Uyoga upo kwenye plain pan tayari kwa kuandaliwa kwa ajili ya mlo wa jioni......
.....baada ya dakika tano umepungua kiasi hiki na maji mengi yamejitokeza ..naendelea kukausha maji...
---Maji yamekakamia na hapa sasa ni kuweka chumvi, sukari kiduchu kwa ajili ya ladha..na pilipili manga kidogo na kikubwa zaidi siagi kama kijiko kimoja cha mezani unakaanga kwa dakika kumi....
...baada ya hapo unaweka krimu ya maziwa na kama huna krimu basi weka unga wa ngano kijiko kimoja cha mezani na maziwa kikombe cha chai,,,,
Na mwisho mlo ukapatikana hivi:- Wali, kuku, uyoga uloungwa kama nilivyosema hapo juu ikiwa na nyanya kutoka bustanini kwetu, tango na majani ya ruccula. Na hivi ndivyo ilivyoisha IJUMAA YA KAPULYA na mpishi ni YEYE MWENYEWE KAPULYA:-) TUTAONANA TENA PANAPO MAJALIWA !!
Baada ya masaa matatu uyoga tayari umetolewa takataka zote na upo safi kwa kuliwa.....
...Uyoga upo kwenye plain pan tayari kwa kuandaliwa kwa ajili ya mlo wa jioni......
.....baada ya dakika tano umepungua kiasi hiki na maji mengi yamejitokeza ..naendelea kukausha maji...
---Maji yamekakamia na hapa sasa ni kuweka chumvi, sukari kiduchu kwa ajili ya ladha..na pilipili manga kidogo na kikubwa zaidi siagi kama kijiko kimoja cha mezani unakaanga kwa dakika kumi....
...baada ya hapo unaweka krimu ya maziwa na kama huna krimu basi weka unga wa ngano kijiko kimoja cha mezani na maziwa kikombe cha chai,,,,
Na mwisho mlo ukapatikana hivi:- Wali, kuku, uyoga uloungwa kama nilivyosema hapo juu ikiwa na nyanya kutoka bustanini kwetu, tango na majani ya ruccula. Na hivi ndivyo ilivyoisha IJUMAA YA KAPULYA na mpishi ni YEYE MWENYEWE KAPULYA:-) TUTAONANA TENA PANAPO MAJALIWA !!
Monday, February 18, 2013
KULA MATUNDA NI MUHIMU KWA AFYA ZETU..TUSISAHAU
Matunda ya aina mbalimbali ni muhimu kwa afya zetu...tujaribu kuzingatia kula matunda ,,ikiwezekana kila baada ya mlo JUMATATU NJEMA KWA WOTE...
Tuesday, January 29, 2013
MILO AMBAYO NINGEPENDA SIKU YA LEO NILE NI HII HAPA...!!!
Chai ya rangi na ndizi mzuzu za kuchemsha
Mlo kama huu kwangu ni mali sana kuliko chai ya maziwa kwa mikate. Vyakula vyetu kama viazi, mihogo, magimbi na ndizi hakika jamani tuendelee kula kwanza unakula unashiba na halafu vina faida. Karibuni....na mchana...mmmmmhhh
Mchana, Nimekaa hapa naota mlo huu ugali, samaki, chuzi, mbogamboga na kachumbali kidogo bila kusahau pilipili... ila duh naona niishie kula kwa macho tu....au ...na jioni sijui itakuwaje ..hii ndiyo mara nyingi akina mama huwa tunawaza ili familia ipate chakula..tuna kazi kweli kweli......
Monday, July 9, 2012
Neno La Leo: Vita Hii Ya Serikali Na Madaktari Ikome Sasa!!!!
Ndugu zangu,
NCHI yetu ingali katika huzuni ya uwepo wa mgogoro kati ya madaktari wetu na Serikali yetu. Ni huzuni iliyochanganyika na hofu na mashaka. Suluhu ya kushikana mikono haijapatikana.
Inasikitisha, maana, hii ni nchi yetu, wanaogoma ni madaktari wetu na inayogomewa ni Serikali yetu. Ni wananchi wa nchi hii wenye kutaabika na hata kupoteza maisha yao kutokana na mgomo huu.
Hili ni jambo la kuhuzunisha sana. Ni jambo lenye kuitia doa nchi yetu. Huko nyuma kuna tuliosisitiza, na hapa narudia kusisitiza msimamo wangu kama Mtanzania ninayeipenda nchi yangu, kuwa hakuna njia nyingine ya kuumaliza mgogoro huu bali ni kwa njia ya mazungumzo ya kindugu na kirafiki. Wahusika wana lazima ya kukaa kwenye meza moja kama Watanzania na kuitafuta suluhu ya mgogoro huu kwa manufaa ya nchi yetu na watu wake.
Kwa sasa kila upande unamwona mwenzake ndiye mwenye makosa. Hivyo, kila upande umejichimbia handakini na kuendeleza ' vita vya kuviziana'. Ukweli, katika vita hivi hakutakuwa na mshindi, maana, kama taifa, sote tumeshashindwa. Na tunaendelea kushindwa zaidi, maana, watu wetu wanaangamia kwa kukosa tiba ya uhakika.
Kimsingi madai ya madaktari ni ya msingi na yanazungumzika. Na hoja za Serikali ni za msingi na zinazungumzika. Hivyo, pande zote mbili zinaweza kuzungumza na kufikia muafaka. Si jambo la hekima kwa sasa kwa madaktari kuendelea na mgomo wao wakati milango ya mazungumzo haijatiwa komeo la shaba, na si hekima vile vile kwa Serikali ' kugomea' kuzungumza na madaktari kwa kisingizio kuwa suala hilo liko mahakamani. Naungana na viongozi wa kidini walioisihi Serikali kufuta shauri hilo na kuimaliza kadhia hii kwenye meza ya mazungumzo.
Ni vema na ni busara sasa kwa madaktari wakatangaza, kwa manufaa ya nchi yetu, kuahirisha mgomo wao mara moja na kurudi kazini kuwahudumia Watanzania kwa moyo wote. Wafanye hivyo hata katika mazingira magumu waliyonayo, wakati juhudi za kufikia muafaka na Serikali zikiendelea.
Maana, mgomo wowote ni jambo la hasara. Kila siku inayokwenda kukiwa na mgomo ina maana ya hasara kwa nchi na watu wake. Ni hasara ya fedha na uhai. Ndio maana ya pande zote mbili zinapaswa kuhakikisha zinakutana na kutafuta suluhu ya kushikana mikono.
Na huko twendako, endapo kutatokea hali ya kutoelewana baina ya Serikali na madaktari, basi, Chama cha Madaktari kianze sasa kufikiria namna njema ya kuendesha migomo tofauti na hii ya sasa. Mathalan, katika kuishinikiza Serikali ingewezekana kuanza na mgomo kwa Hospitali moja na si nchi nzima.
Ingewezekana pia isiwe kwa hospitali nzima bali vitengo kadhaa huku huduma kwenye vitengo vingine zikiendelea. Hata hilo pia lingewaletea usumbufu wananchi na kufikia kuishinikiza Serikali kwenye kujadiliana na madaktari katika kuboresha maslahi yao.
Lakini hili la ' Wild Strike' kwa maana ya mgomo wa nchi nzima lina' hatari ya kiafya' kwa taifa. Tusifike mahala tukachangangia kuifanya nchi yetu wenyewe iende kwa kutambaa kutokana na migomo.
Nimepata kuandika, kuwa katika nchi zetu hizi, mganga wa tiba aliyesomeshwa kwa fedha za walipa kodi na kwa miaka mingi anahitajika sana. Mganga wa tiba msaidizi anahitajika sana. Na hata kama angelikuwapo Msaidizi wa Mganga Msaidizi wa tiba , naye angehitajika sana. Vivyo hivyo kwa wakunga wakuu na wasaidizi, wauguzi wakuu na wasaidizi wao. Wote hao anahitajika sana.
Na katika nchi zetu hizi, Serikali hazipaswi kufikia hatua ya kuwatisha na hata kuwafukuza kazi madaktari. Hilo la mwisho lifanyike tu pale ambapo njia nyingine zote za kumaliza tofauti na kusuluhisha migogoro na madaktari zitakapokuwa zimeshindikana. Na kwa nini ishindikane?
Naam, Watanzania tungependa kuona vita hii baina ya Serikali na madaktari ikimalizwa haraka kwa kutafutwa suluhu ya kushikana mikono. Inawezekana.
Habari hii nimetumiwa na Mwenyekiti Mjengwa......
Wednesday, April 25, 2012
MAPAPAI :- UTAMU ,FAIDA NA MATUMIZI YAKE!!
Kama kawaida ni kile KIPENGELE CHETU CHA MARUDIO MBALIMBALI YA MADA, PICHA NA VITU VINGINE MBALIMBALI. NA LEO TUANGALIE KUHUSU MAPAPAI. Hiii niliiweka hapa kibarazana lakini kama mnijuavyo huwa napenda kurudia kusoma kitu ili nielewe zaidi. kusoma maoni mazuri ya wasomaji gonga KAPULYA. Karibuni sana.
Hapa ni mti wa papai, leo nimekumbuka faida mbili za majani ya mipapai moja ni dawa ya tumbo hasa kama una tatizo la choo kubwa . Unachukua hayo majanai na unachemsha na halafu unakunywa yale maji yake. Pili ni sabuni unaweza au niseme mimi nimewahi kufulia nguo ila usifulie nguo nyeupe basi itakuwa kijana. Nguo nyingine zote sawa kabisa.
Na hapa ni tunda lenyewe nalo lina faida zake kwanza ni kwa ajili ya kula ni tamu sana na pia nalo kama una tatizo la choo kubwa ni nzuri. Halafu jambo jinginge papai ni kilainisho kizuri sana cha chama hasa nyama ya ngómbe. Toa hizo mbege weka kwenye chombo, pondaponda papai na uchanganya na hizo mbegu koroga taratibu katakata nyama vipande vidogovodogo weka humu kwenye mpondo na subiri masaa kadhaa. Hakika utaifaidi nyama yako mno itakuwa lainiiii. Ila kusema kweli nimetamani kweli papai ni muda sasa sijala:-). PANAPO MAJALIWA BASI TUONANE TENA KATIKA KIPENGELE HIKI JUMATANO IJAYO!!!!!!
Tuesday, February 7, 2012
Sakata La Mgomo Wa Madaktari; Tafsiri Yangu

Nimetumiwa habari hii na Kaka Maggid Mjengwa.
Ndugu zangu,
Mgomo wa madaktari wetu ni habari kubwa. Umeingia sasa kwenye wiki ya pili. Hata kama ungekuwa ni wa siku mbili, bado ungesababisha madhara makubwa kwa nchi. Kwamba sasa una zaidi ya siku kumi na nne ni balaa kubwa kwa nchi yetu.
Mgomo wa madaktari wetu ni habari kubwa. Umeingia sasa kwenye wiki ya pili. Hata kama ungekuwa ni wa siku mbili, bado ungesababisha madhara makubwa kwa nchi. Kwamba sasa una zaidi ya siku kumi na nne ni balaa kubwa kwa nchi yetu.
Tafsiri yangu;
Uliopo ni mgogoro kati ya madaktari na Serikali. Na kwenye mgogoro kama huu, siku zote,wenye kuathirika zaidi ni wananchi walio wengi.
Ni ukweli, kuwa karibu kila Mtanzania anayeamka asubuhi, ama nimgonjwa au ana ndugu, jamaa au rafiki aliye mgonjwa.
Hivyo basi, kuna mamilioni ya Watanzania wenye kutaabika kila siku na maradhi ya aina mbali mbali. Ni Watanzania wenye kutegemea sana huduma ya tiba inayotolewa na madaktari wetu. Na katika nchi zetu hizi, daktari ni rafiki muhimu sana wa mwananchi.
Ni jambo baya sana, pale Serikali inapoingia kwenye mgogoro namadaktari. Inapoingia kwenye mgogoro na marafiki wa wananchi. Hakuna mahali popote duniani wananchi wakatokea kuwachukia madaktari.
Hivyo basi, ni balaa pia pale Serikali inaposhindwa kumaliza tofauti zake na madaktari wawananchi kwa njia ya mazungumzo na hata kufikia hatua ya madaktari kugoma.
Katika nchi zetu hizi, mganga wa tiba aliyesomeshwa kwa fedha zawalipa kodi na kwa miaka mingi anahitajika sana. Mganga wa tiba msaidizi anahitajika sana. Na hata kama angelikuwapo Msaidizi wa Mganga Msaidizi wa tiba , naye angehitajika sana. Vivyohivyo kwa wakunga wakuu na wasaidizi, wauguzi wakuu na wasaidizi wao. Wote hao wanahitajika sana.
Na katika nchi zetu hizi, Serikali hazipaswi kufikia hatua yakuwatisha na hata kuwafukuza kazi madaktari. Hilo la mwisho lifanyike tu pale ambapo njia nyingine zote za kumaliza tofauti nakusuluhisha migogoro na madaktari zitakapokuwa zimeshindikana. Nakwanini ishindakane?
Tufanye nini sasa?
Taarifa kwamba Kamati ya kudumu ya Bunge inayohusika na masuala yahuduma za jamii imepanga kukutana na madaktari wetu ni hatua njema na ya busara. Maana, katika mgogoro huu taarifa zimekuwa zaidi za upande mmoja; upande wa Serikali. Niwakati sasa pande zote mbili zikasikilizwa na Kamati hiyo ya Bunge. Ndio, ni wakati pia hata madaktari wetu wakapewa nafasi tuwasikie.
Huu si wakati wa kufanya ’ propaganda’ za kisiasa kwenye masuala ya afya za wananchi.Na hata pale Waziri wa Afya alipokaririwa jana Bungeni akitamka kuwahali ya huduma za mahospitalini zimerejea katika hali yake ya kawaida ni mfano wa ’Propaganda’ za kisiasa ambazo Watanzania hatuzihitaji kwa sasa.
Hivi ni hali gani hiyo iliyorejea kwenye kawaida yake kwenye hospitali zetu baada ya mgomo huu wa madaktari unaoendelea sasa? Kwamba askari wetu wa Jeshi la Wananchi wamelazimika kwenda kutibu wagonjwa Muhimbili hiyo haiwezikuwa ni ’ Hali ya kawaida’. Kwamba madaktari wameripoti lakini hawaonekani mawodini hiyo haiwezi kuwa ’ hali ya kawaida’. Na kama ni kawaida, hivi ni nini tafsiri ya ’ kawaida’?
Hapa kuna ukweli unaopaswa kusemwa, na si kitu kingine bali ni ukweli. Watanzania tunatakakujua; ni kwanini watendaji wa Wizara husika wameshindwa kulitatua suala la madaktari wetu na hata kutufikisha hapa tulipo?
Yumkini, kulikuwa na hali ya kuyapuuzia madai ya madaktari katika hatua za awali. Yawezekana pia watendaji wa Wizara hawakuwa karibu na wawakilishiwa madaktari hao ili kutoa fursa ya kuongea na kutafuta ufumbuzi watatizo. Labda ndio maana tumefika mahali sasa mgogoro umekomaa na wahusika kuonyesha hali ya kutunishiana misuli. Kuna mahali kosa limefanyika. Ni wapi?
Ndio hapa, kuwa hata kama Kamati ya Bunge itafaulu kusuluhisha mgogoro huu, bado Watanzania tutahitaji iundwe Tume huru itakayochunguza namna watendaji wa wizara husika walivyolishughulikia suala hili kwa upande wao.
Tume hiyo itusaidie kuupata ukweli mzima ili kama taifa, tujifunze. Na wakati tume kama hiyo itakapokuwa ikifanya kazi yake, itakuwa ni busara, kwa watendaji wakuu wa wizara husika wajiweke pembeni kwa maana ya kujiuzulu ili kupisha uchunguzi huo.
Kama Tume itabaini kuwa hakukuwa na mapungufu makubwa katika utendaji wao na hususan walivyolishughulikia suala hili la mgogoro na madaktari, basi, itajulikana hivyo, na wana nafasi ya kurudi tena kwenye nafasi za utendaji Serikalini. Inahusu umma kurudisha imani yake kwa Serikali yao. Ndio maana ya umuhimu wa wahusika kupisha pembeni kuruhusu uchunguzi ufanyike. Maana, haitakuwa busara kuliacha suala hili likapita kama yanavyopita mengine ili hali limegharimu maisha ya Watanzania.
Na kubwa zaidi kwa sasa, ni kwa pande zote katika mgogoro huukutambua; kuwa kwa sasa mvutano unaoendelea hautatoa mshindi, ni kwa vile, katika kilichotokea na kinachoendelea kufanyika sasa, sote, kama taifa, tumeshindwa.
Huu ni wakati wa kutanguliza busara na hekima. Tufanye yote, lakini,njia mujarab ya kutanzua mgogoro huu uliopo sasa ni mazungumzo katika mazingira ya kuheshimiana, basi.
Mungu Ibariki Tanzania, Mungu Ibariki Afrika.
Maggid Mjengwa,
Dar es Salaam, Jumamosi, Februari 4, 2012 http://mjengwablog.com/
Uliopo ni mgogoro kati ya madaktari na Serikali. Na kwenye mgogoro kama huu, siku zote,wenye kuathirika zaidi ni wananchi walio wengi.
Ni ukweli, kuwa karibu kila Mtanzania anayeamka asubuhi, ama nimgonjwa au ana ndugu, jamaa au rafiki aliye mgonjwa.
Hivyo basi, kuna mamilioni ya Watanzania wenye kutaabika kila siku na maradhi ya aina mbali mbali. Ni Watanzania wenye kutegemea sana huduma ya tiba inayotolewa na madaktari wetu. Na katika nchi zetu hizi, daktari ni rafiki muhimu sana wa mwananchi.
Ni jambo baya sana, pale Serikali inapoingia kwenye mgogoro namadaktari. Inapoingia kwenye mgogoro na marafiki wa wananchi. Hakuna mahali popote duniani wananchi wakatokea kuwachukia madaktari.
Hivyo basi, ni balaa pia pale Serikali inaposhindwa kumaliza tofauti zake na madaktari wawananchi kwa njia ya mazungumzo na hata kufikia hatua ya madaktari kugoma.
Katika nchi zetu hizi, mganga wa tiba aliyesomeshwa kwa fedha zawalipa kodi na kwa miaka mingi anahitajika sana. Mganga wa tiba msaidizi anahitajika sana. Na hata kama angelikuwapo Msaidizi wa Mganga Msaidizi wa tiba , naye angehitajika sana. Vivyohivyo kwa wakunga wakuu na wasaidizi, wauguzi wakuu na wasaidizi wao. Wote hao wanahitajika sana.
Na katika nchi zetu hizi, Serikali hazipaswi kufikia hatua yakuwatisha na hata kuwafukuza kazi madaktari. Hilo la mwisho lifanyike tu pale ambapo njia nyingine zote za kumaliza tofauti nakusuluhisha migogoro na madaktari zitakapokuwa zimeshindikana. Nakwanini ishindakane?
Tufanye nini sasa?
Taarifa kwamba Kamati ya kudumu ya Bunge inayohusika na masuala yahuduma za jamii imepanga kukutana na madaktari wetu ni hatua njema na ya busara. Maana, katika mgogoro huu taarifa zimekuwa zaidi za upande mmoja; upande wa Serikali. Niwakati sasa pande zote mbili zikasikilizwa na Kamati hiyo ya Bunge. Ndio, ni wakati pia hata madaktari wetu wakapewa nafasi tuwasikie.
Huu si wakati wa kufanya ’ propaganda’ za kisiasa kwenye masuala ya afya za wananchi.Na hata pale Waziri wa Afya alipokaririwa jana Bungeni akitamka kuwahali ya huduma za mahospitalini zimerejea katika hali yake ya kawaida ni mfano wa ’Propaganda’ za kisiasa ambazo Watanzania hatuzihitaji kwa sasa.
Hivi ni hali gani hiyo iliyorejea kwenye kawaida yake kwenye hospitali zetu baada ya mgomo huu wa madaktari unaoendelea sasa? Kwamba askari wetu wa Jeshi la Wananchi wamelazimika kwenda kutibu wagonjwa Muhimbili hiyo haiwezikuwa ni ’ Hali ya kawaida’. Kwamba madaktari wameripoti lakini hawaonekani mawodini hiyo haiwezi kuwa ’ hali ya kawaida’. Na kama ni kawaida, hivi ni nini tafsiri ya ’ kawaida’?
Hapa kuna ukweli unaopaswa kusemwa, na si kitu kingine bali ni ukweli. Watanzania tunatakakujua; ni kwanini watendaji wa Wizara husika wameshindwa kulitatua suala la madaktari wetu na hata kutufikisha hapa tulipo?
Yumkini, kulikuwa na hali ya kuyapuuzia madai ya madaktari katika hatua za awali. Yawezekana pia watendaji wa Wizara hawakuwa karibu na wawakilishiwa madaktari hao ili kutoa fursa ya kuongea na kutafuta ufumbuzi watatizo. Labda ndio maana tumefika mahali sasa mgogoro umekomaa na wahusika kuonyesha hali ya kutunishiana misuli. Kuna mahali kosa limefanyika. Ni wapi?
Ndio hapa, kuwa hata kama Kamati ya Bunge itafaulu kusuluhisha mgogoro huu, bado Watanzania tutahitaji iundwe Tume huru itakayochunguza namna watendaji wa wizara husika walivyolishughulikia suala hili kwa upande wao.
Tume hiyo itusaidie kuupata ukweli mzima ili kama taifa, tujifunze. Na wakati tume kama hiyo itakapokuwa ikifanya kazi yake, itakuwa ni busara, kwa watendaji wakuu wa wizara husika wajiweke pembeni kwa maana ya kujiuzulu ili kupisha uchunguzi huo.
Kama Tume itabaini kuwa hakukuwa na mapungufu makubwa katika utendaji wao na hususan walivyolishughulikia suala hili la mgogoro na madaktari, basi, itajulikana hivyo, na wana nafasi ya kurudi tena kwenye nafasi za utendaji Serikalini. Inahusu umma kurudisha imani yake kwa Serikali yao. Ndio maana ya umuhimu wa wahusika kupisha pembeni kuruhusu uchunguzi ufanyike. Maana, haitakuwa busara kuliacha suala hili likapita kama yanavyopita mengine ili hali limegharimu maisha ya Watanzania.
Na kubwa zaidi kwa sasa, ni kwa pande zote katika mgogoro huukutambua; kuwa kwa sasa mvutano unaoendelea hautatoa mshindi, ni kwa vile, katika kilichotokea na kinachoendelea kufanyika sasa, sote, kama taifa, tumeshindwa.
Huu ni wakati wa kutanguliza busara na hekima. Tufanye yote, lakini,njia mujarab ya kutanzua mgogoro huu uliopo sasa ni mazungumzo katika mazingira ya kuheshimiana, basi.
Mungu Ibariki Tanzania, Mungu Ibariki Afrika.
Maggid Mjengwa,
Dar es Salaam, Jumamosi, Februari 4, 2012 http://mjengwablog.com/
Tuesday, January 31, 2012
ULIKUWA UNAJUA MATUNDA HAYA YANAITWA MABUNGO?.....
Tuesday, December 27, 2011
"UJUMBE ULIOVUNJA REKODI KATIKA BLOG YA MAISHA NA MAFANIKIO MWAKA 2011
Ndugu wasomaji wa blog hii ya MAISHA NA MAFANIKIO, katika kupitia mada mbalimbali nilizowahi kuweka humu ili kupata ile ambayo ilivuta hisia za wasomaji wengi na kuleta changamoto, nimevutiwa na ujumbe huu ambao ulileta vuta ni kuvute miongoni mwa wadau wa blog hii. Kwa hiyo basi nimeichagua ujumbe huu kuwa ndio ujumbe uliovunja rekodi kwa mwaka 2011. Natoa shukrani kwa wadau wote mlioshiriki katika kuchangia ujumbe huu. Naomba muungane nami katika kujikumbusha kile kilichotokea katika ujumbe huu.
NIMEJIFUNZA KUTOKA KWA CHRISTINA
Akiwa mjini Arusha akifanya manunuzi baada ya kuruhusiwa kutoka KCMC

Huwa tunajifunza kupitia kwa wengine hususan kwa yale mambo magumu na yaliyojificha. Naomba nikiri kwamba pamoja na kusoma ushuhuda mbalimbali kupitia magazeti na blogs, lakini sikuwahi kuzipa uzito shuhuda hizo. Naomba nikiri kuwa tukio la hivi karibuni lilipompata rafiki yangu na wifi yangu Christina aishiye Dar es salaam Tanzania nimejifunza kuwa imani ikichangizwa na ibada ina nguvu sana.Christina Kaluse ni wifi yangu wa hiyari ambaye ni mke wa mwanablog mwenzangu na ambaye ni mwanautambuzi anayetuelimisha kupitia kibaraza chake cha Utambuzi na Kujitambua, huyu si mwingine bali ni mwanablog Shaban Kaluse, ukitaka kusoma habari zake waweza kubofya hapa.Nimekuwa nikiwasiliana na Christina kwa takriban miaka miwili sasa, na tangu kufahamiana na familia hii ya mwanablog mwenzangu, nimejikuta nikiwa karibu nao tukiwasiliana mara kwa mara kama ilivyo kwa baadhi ya wanablog wengine.Nisiwachoshe, niwasimulie kisa cha kuandika kile nilichojifunza kwa wifi yangu huyu Christina au mama Abraham.Nakumbuka ilikuwa ni siku ya jumatatu ya Januari 31, 2011, majira ya mchana, nilipata ujumbe mfupi kupitia simu yangu ya kiganjani kutoka kwa Christina, na ujumbe wenyewe ulisomeka hivi, ‘Yasinta naomba uungane nami kwenye maombi, nimepofuka jicho moja’ .Ujumbe huo ulinishtua sana, nikaamua kumpigia simu ambapo tuliongea kwa muda mrefu sana.Kwa kifupi aliniambia kuwa mnamo siku ya jumatano ya Januari 19, 2011, akiwa dukani kwake, (Christina anamiliki duka la vifaa vya ushonaji na ubunifu wa mavazi maeneo ya Tabata jijini Dar es salaam) aliingiwa na vumbi kidogo kwenye jicho lake la mkono wa kushoto, na alijaribu kulisafisha jicho hilo kwa maji safi lakini halikupata nafuu na liliendelea kumuuma.Alikata shauri kurudi nyumbani kwake ambapo sio mbali na mahali ilipo ofisi yake, alipofika nyumbani aliendelea kulisafisha jicho lake hilo kwa maji safi, lakini halikupata nafuu yoyote.Usiku kucha hakulala pamoja na kumeza vidonge vya kutuliza maumivu.Ilipofika asubuhi akiongozana na mumewe walikwenda hospiali maarufu hapo jijini Dar iitwayo Regency ambapo alionana na daktari bingwa wa macho na baada ya vipimo iligundulika kuwa mboni ya jicho imepata kidonda na daktari huyo alidai kuwa huenda lile vumbi liliambatana na mchanga na hivyo wakati alipokuwa analisafisha ule mchanga ukawa umejeruhi mboni ya jicho hilo.Kumbe huo ukawa ni mwanzo wa safari ya jicho hilo kupofuka, Christina alinieleza kuwa pamoja na kupatiwa matibabu katika hospiali hiyo lakini hakupata nafuu yoyote na usiku kucha alikuwa akikesha kwa maumivu makali ya jicho hata pamoja na kumeza vidonge vya usingizi lakini hakupata lepe la usingizi.Ilipofika siku ya jumamosi ya January 29, 2011,ikiwa ni siku kumi tangu aanzwe na tatizo hilo, jicho likapoteza uwezo wa kuona na mboni ya jicho ikageuka na kuwa kama ina mtoto wa jicho, kwa maelezo yake Christina alisema kuwa hata yule daktari bingwa wa macho pale Regency alionekana kuchanganyikiwa kutokana na hali ile na alionekana kukata tamaa, lakini hata hivyo alimwandikia dawa nyingine na kumtaka akazitumie kisha arudi siku ya jumanne.Aliporudi nyumbani walishauriana na mumewe na wakakata shauri kuhamia katika Hospitali ya CCBRT ambayo ndiyo hospitali maarufu hapo nyumbani ambayo inasifika kwa kutibu matatizo mbalimbali ya ulemavu yakiwemo matatizo ya macho.Siku hiyo ya jumatatu ya Januari 31, 2011 aliyonitumia ujumbe mfupi, ndiyo siku ambayo alikwenda CCBRT. Baada ya vipimo, daktari aliyempima bila kutafuna maneno alimweleza waziwazi kuwa jicho limeshapofuka, na alimlaumu eti amechelewesha jicho huko vichochoroni mpaka limepofuka ndio anakwenda kwao…..Kauli hiyo ilimshangaza sana Christina, kwani tangu alipopata tatizo hilo alikwenda kupata matibabu kwenye Hospiali ya Regency ambayo inatambulika na inasifika kwa matibabu, sasa iweje alaumiwe na kuambiwa kuwa alikuwa vichochoroni? Christina alionesha kushangazwa kwake na maadili ya Daktari yule.Yule Daktari ambaye ni Mtanzania mwenzetu (Hospitali hiyo inayo pia wataalamu wa kigeni) alimweleza kuwa tiba pekee iliyobaki ni kuweka uzingativu kwenye kutibu kidonda tu, na hata akipona hataweza kuona kabisa kwani jicho limeshambuliwa na bacteria kiasi kwamba limeharibiwa kabisa. Hata hivyo alikiri kushindwa kubaini aina ya bakeria waliomshambulia, pamoja na kukwangua kidonda hicho na kupima maabara.Aliandikiwa aende siku ya Jumanne ya Februari 1, 2011, kwa ajili ya operesheni ndogo ya kuliweka dawa na kulifunga.Wakati naongea naye kwenye simu walikuwa wamekata shauri yeye na mumewe wamgeukie Mungu wakaamua waende kwenye maombi.Nilimuuliza zaidi ya mara mbili kuwa ana imani akienda kwenye maombi atapona, na alinijibu kwa kujiamini kabisa kuwa daktari pekee aliyebaki ni mungu.Ingawa tunatofautiana kimadhehebu, Christina yeye ni Msabato na mimi ni Mkatoliki, lakini nilimuahidi kuungana naye katika maombi.Ni kweli siku iliyofuata alinijulisha kuwa aliombewa na Mwinjilisti mmoja wa kanisa la Wasabato la Chang’ombe SDA aitwae James Ramadhan Rajabu na maumivu yakatoweka na jicho likafunguka na likaanza kuona siku hiyo hiyo….ingawa hata hivyo bado lilikuwa linaonekana kama lina mtoto wa jicho.Aliniambia kuwa anasafiri kwenda Moshi KCMC kuendelea na matibabu lakini bado imani yake kwa Yesu ni kubwa na anaamini atapona, kwani Mungu ndiye atakayekuwa Daktari mkuu atakayewaongoza Madaktari watakaomtibu huko KCMC.Tuliendelea kuwasiliana hata alipokuwa huko Moshi KCMC, na alinijulisha kuwa awali madaktari wa KCMC walikanusha kuwa jicho lake limepofuka baada ya vipimo, ingawa hawakuweza kuona aina ya bacteria waliomshambulia.Walishauri alazwe halafu watajaribu kuwasiliana na daktari mwingine bingwa aliyeko Nairobi ili kuangalia kama anaweza kuja hapo KCMC kushughulikia kesi yake ambayo hata wao iliwachanganya sana, hasa baada ya kuwaeleza kuwa CCBRT wameshindwa kutibu jicho lake.Siku iliofuata yule daktari kutoka Nairobi alifika na baada ya kulipima jicho lake mara kadhaa hakupata majibu ya kueleweka, aliamua kuchuna sehemu ya kidonda na kuchukua sampuli ambayo ingepelekwa Nairobi kwa ajili ya vipimo katika maabara kasha. Aliamuandikia dawa za matone ambazo zitazuia wale bacteria wasiendelee kushambulia jicho lake wakati akisubiri majibu.Katika kipindi chote alichokuwa amelazwa hapo KCMC akisubiri majibu ya vipimo vyake kutoka Nairobi, alikuwa akiendelea na maombi kwa kushirikiana na Mwinjilisti James pamoja na Wainjilisti wengine wa dhehebu lake la Kisabato aliowataja kwa majina ya Mwinjilisti Japhet Magoti Matotiwa kanisa la Manzese, na Mwinjilisti Benson Kilango Izoka wa kanisa la Bombo SDA Tanga.Baada ya siku tatu yule Daktari alirudi na majibu, lakini cha kushangaza alikuta kidonda kimepona kwa asilimia 75. Hali ile haikumshangaza yule daktari peke yake bali pia Madaktari wenzie nao walishangazwa na kule kupona kwake kwa haraka.Kwa mujibu wa majibu aliyokuja nayo, iligundulika kuwa jicho la Christina lilishambuliwa na Fangasi.Aliandikiwa dawa na siku iluyofuata ikiwa ni siku ya tano tangu alazwe Hospitalini hapo aliruhusiwa kurudi nyumbani Dar, lakini alitakiwa kurudi klinik baada ya wiki mbili ili kuangaliwa kama anaendeleaje.Baada ya kurudi Dar, aliendelea na dawa pamoja na maombi, na ilimchukua wiki moja tu kupona kabisa, na jicho kurudi katika hali yake ya kawaida.Aliporudi Moshi KCMC, Daktari alithibitisha kuwa amepona kabisa, na hakusita kuweka bayana kuwa kupona kwake kumekuwa ni kwa miujiza kwa sababu kutokana na hali ya jicho lake walidhani ingechukua muda mrefu hadi kupona.Jana nilizungumza naye kwa muda mrefu sana akinisimulia safari hii ndefu ya ugonjwa wake huo na jinsi maombi pamoja na imani ilivyomsaidia kupona kwa haraka.Kwa kweli nimejifunza jambo moja kubwa sana kutokana na mkasa huu uliompata wifi yangu huyu wa hiyari ya kutokata tamaa pale tupatapo changamoto za kimaisha kama vile ugonjwa na hali zetu kimaisha.Kama Christina angekata tamaa na kusikiliza ushauri wa Daktari wa CCBRT, ni wazi kuwa leo hii angekuwa amepofuka jicho moja. Lakini yeye mwenyewe alidai kuwa alikataa katu katu kukubaliana na maelezo ya Daktari yule na aliiambia nafsi yake kuwa jicho lake halijapofuka na halitapofuka.Naamini hata wewe unayesoma hapa kuna jambo utakuwa umejifunza.Napenda kuchukua nafasi hii kumpongeza Christina kwa kuwa na ujasiri wa kukabiliana na changamoto hiyo. Namuomba Mungu aendelee kuibariki familia yao, awape ujasiri wa kukabiliana na changamoto mbalimbali za maisha, na asiwape moyo wa kukata tamaa.Nimejifunza kutoka kwa Christina.
Na haya yalikuwa maoni ya wadau.....
Na haya yalikuwa maoni ya wadau.....
Anonymous said...
dada yasinta ..nimeguswa sana na kisa cha christina..kwa sababu hakijatofautiana sana na cha mume wangu..kweli tunatakiwa tujifunze kutokata tamaa.
March 1, 2011 9:23 AM
Anonymous said...
Unajuwa ,Yasinta mkasa hu ni ushahidi tosha,kwa sisi binadamu,tunapo kabiliwa na shida au tatizo,liwe la mardhi nk,imani nikitu muhimu sana.vile vile mungu nimkubwa, na ananiayake na makusudi yake itokeapo shida ama tatizo kama hilo.mimi huamini kilakitu kitokeacho kwa binaadamu nimapenzi ya mungu.kama ni mkono wa binadamu na hila zake basi utateseka kwa muda lakini ,kwa imani na mapenzi ya mungu utapona.Lakini kama yeye ameaamua hataufanyeje utapofuka tu.na mwisho nisawa na tunavyo amini kuhusu kifo.unakuta mtu anapata ajali mbaya sana amboyo labda katika gari lile wote wamepoteza maisha, na ni mtu mmoja tu ka pona.hapo yatasemwa mengi,ikiwemo bahati,au mungu atasifiwa kwa sana,na wakati mwingine utambiwa jamaa alisali sana kabla hajaanza safari.Hivyo imamani ,jitihada,uvumilivu na uelawa/ufahamu nimsingi katika kukuvusha katika shida au tatizo linalo kukabili . kaka s
March 1, 2011 10:46 AM
Mija Shija Sayi said...
Mungu ni mwema. Tunaambiwa kwamba wanaadamu tumepewa jina moja tu ambalo kwalo kila kitu kinawezekana ukiamini hivyo. Jina la YESU.Tunaambiwa kwamba ktk majina yooooote hapa duniani hakuna lipitalo nguvu Jina la YESU, na yote yatalitii jina hilo, sasa FUNGUS nalo si ni jina?FUNGUS imelitii jina la YESU.Mbarikiwe wote...
March 1, 2011 12:11 PM
Koero Mkundi said...
Nimeishiwa maneno..... Nakumbuka niliwahi kumtumia kaka Shaban Email ya kumjulia hali na alinijibu tu kwa kifupi kuwa yuko KCMC Moshi akimuuguza mkewe ambaye alilazwa huko kwa kuumwa na Jicho. Nasikitika kwamba sikuwahi kuwasiliana naye tena, sijui ni usahaulifu au ni kitu gani.....Ni mara nyingi katika baadhi ya makala zangu za huko nyuma nimewahi kuandika juu ya somo la imani, na nimekuwa nikieleza kwa kirefu sana jinsi imani ilivyo na nguvu, lakini naomba nikiri kuwa pamoja na kuandika sana juu ya imani lakini siamini kama ninayo imani inayomfikia Christina. Huo ndio ukweli wenyewe.Dunia hii imetawaliwa na mapepo ya kila aina na kama mtu asipokuwa na imani basi anaweza kwenda na maji. Ahsante sana dada Yasinta kwa juhudi zako za kushirikiana na Christina katika maombi, na pia kupata muda wa kufanya naye mazungumzo hadi kutuwekea ushuhuda huu ambao kwa kweli utawafunua wengi.Mwisho napenda kuwapongeza Wainjilisti James Ramadhan Rajabu, Benson Izoka ambaye namfahamu ingawa sidhani kama yeye ananifahamu, Mwinjilisti Magoti huyu nimeshawahi kukutana naye pale Manzese SDA kwenye Effort moja, na washiriki wengine ambao kwa njia moja au nyingine walishirikiana na Christina kwenye maombi katika kipindi chote cha madhila yake.Mungu ashukuriwe.nami nimejifunza kutoka kwa Christina...
March 1, 2011 12:21 PM
Mija Shija Sayi said...
Dah! dah! Yasinta nimekukubali wewe ni shapu si mchezo..siamini..Nafikiri umeelewa naongelea nini.Ubarikiwe.
March 1, 2011 2:50 PM
Anonymous said...
Samahani kwa mwandishi, naomba kuweka kumbukumbu sawa. Mwinjilisti James Ramadhan Rajabu ni wa Kanisa la Tabata Chang'ombe.Ukitaja Chang'ombe tu, mtu mwingine anaweza kudhani ni Temeke Chang'ombe.nami natoa pole na pongezi kwa dada Christina kwa ujasiri wake.Imani ina nguvu sana. nami nimejifunza pia.Liz wa Tabata
March 1, 2011 5:31 PM
Masangu Matondo Nzuzullima (MMN) said...
Ni kisa cha kugusa moyo. Yote yawezekana ati!
March 1, 2011 6:05 PM
Lisa said...
Inafunza sana if you have faith as small as a mustard seed, you can say to this mountain, 'Move from here to there' and it will move.Yasinta topic ni ushuhuda wakutosha hakuna lisilo wezekana kwa yesu hongera sana kristina mungu awabariki wote.
March 1, 2011 7:40 PM
Swahili na Waswahili said...
Hongera sana da Christina kwa kunga'nga'nia njia ya uzima na kweli!Mungu azidi kukubariki,Kuhusu ccbrt nami nilishakwenda pale kwa vipimo, nikaonekana ninatazizo la macho na natakiwa kuvaa miwani haraka sana, wakanipatiwa yanayo nifaa na bei yake,Mungu ni mwema siku hiyo pia nikuwa na ahadi Ubalozi saa 8 mchana,hapo ilikuwa saa 6.Nikawaambia nitarudi kesho kuichukua,kwenda ubalozi nikapata visa na tukashauriana na baba watoto tukaona tuachane nayo,kuja huku nikapimwa tena nikaambiwa tatizo langu si kuivaa miwani kwa sasa labda niaka 15/20 ijayo.Wakaniuliza ulipima wapi?nikawaambia na kuwapa vyeti vyangu vya huko yaani walilaumu sana.Asante da yasinta kwa kuungana nasi na mafundisho haya!Mungu wetu hashindwi na jambo kama kweli unamuamini na kufuatanjia zake!.
March 2, 2011 12:38 AM
Celestina said...
Kweli hata mim nimejifunza kutoka kwa dada Tina kutokata tamaa.mungu ndo kila kila kitu katika maisha yetu,hata kwa bible amesema 'sitawaacha waaibike wanitengemeao.'Be blessed.
March 2, 2011 12:21 PM
Chacha o'Wambura a.k.a Ng'wanambiti! said...
Nguvu ya imani hakuna awezaye kuipinga!Pole sana da Tina na hongera kwa ujasiri!
March 2, 2011 3:12 PM
NN Mhango said...
Pamoja na tukio hili kugusa nyoyo na kufunza, tuchunge kutoa hitimisho la jumla kuwa imani ni tiba. Inategemea na imani. Maana kuna imani nyingine ni potofu zinaleta maangamizi kama vile ugaidi na mauaji ya kinyama ya albino. Shukrani dada Yacinta kukubali kushiriki nasi tukio hili.
March 2, 2011 8:52 PM
Jeff Msangi said...
Kisa au mkasa wa aina yake.Nilichoambulia mimi ni kitu kinachoitwa Power of Faith au Nguvu ya Imani.Ukiamini hakuna kisichowezekana.Asante Yasinta kwa ushuhuda huu wa Christina.The Lord is alive
March 3, 2011 1:46 AM
Salehe Msanda said...
Habari za siku kadhaa,Nimerudi kutoka mapumzikoNi kweli hilo somo tosha na ni muhimu kila wakati kuwa na matumaini kuliko kukata tamaa na hasa suala lenyewe kama linahusiana na afya yako. maana afya haina mbadala.Tumshukuru muumba kwa kuweza kumuongoza wifi yako kufikia uamuzi wa kuamini kuwa mungu yuko naye na atapona.Ni somo zuri na lina mafundisho mengi kutokana na kile kilichotokea na kwa watu wataalamu wa afya tunanaowaamini na kuwakadhi dhamana ya maisha yetu.Kila la kheri.
March 3, 2011 11:02 AM
emu-three said...
Kweli imani ni tiba, hasa unapokabiliwa na magonjwa ambayo `wataalamu wetu' wanasema `haiwezekani...usikate tamaa na muombe mungu wako kwa imani yako...utafanikiwa, lakini hakikisha kuwa `imani' ipo!
March 3, 2011 12:44 PM
Upepo Mwanana said...
Nijuavyo mimi, madakatari bingwa wa macho kwa Tanzania ni wachache sana, na hata hospitali kubwa zenye majina makubwa , nyingine hazina madakatari bingwa wa macho, ukifika unapokelewa na wasaidizi ambao kwa sera za nchi yetu ati wanatambulika kama madaktari.Hata CCBRT madaktari bingwa ni wachache, na wamejaa wasaidizi.Wanchi siku hizi tunapaswa kujifunza japo huduma ya kwanza na elimu kidogo ya magonjwa tujimudu na bidhaa feki hizi zinazojiita madaktari bingwa! Namkumbuka Kaka yangu Chib, nina imani anaweza kutoa mchango zaidi katika masuala haya ya macho!
March 3, 2011 1:25 PM
Mija Shija Sayi said...
Yasinta upo?
March 5, 2011 5:45 PM
chib said...
Habari hii imenigusa sana, tena moyoni kabisa.Nasikitika iwapo mtu ataangukia kwa mtu asiye elewa sawa tatizo la mwingine na kuishia kumwaga uongo ili aonekane kama anajua.Hospitali alizopitia Christina, nazifahamu vyema tena sana.Nina mengi ya kusema kutokana na maelezo ya Christina, lakini kusema bila kuona, ni sawa na kumwaga uongo zaidi. Kwangu kila moja linawezekana, kwa upande wa kupona haraka, na pia kwa upande wa maelezo ya madaktari. Sijui nisemee upande upi. Ila bado natafakari kwa KCMC kumuita mtaalamu kutoka Nairobi kuja kuchukua sampuli tu...., bado haijaingia kichwani kabisa.Baadaye nikipata muda, nitatoa mada ndefu kuhusu vidonda katika uso wa jicho. Nashukuru Tembe kwa kunikumbuka, japo nipo nahudumia waafrika wenzangu mbali na nyumbani.Lakini tupo pamoja
March 8, 2011 5:08 PM
Anonymous said...
NAOMBA NAMBA YA CHRISTINA .IMANI YAKE IMENITIA MOYO
March 10, 2011 7:16 AM
dada yasinta ..nimeguswa sana na kisa cha christina..kwa sababu hakijatofautiana sana na cha mume wangu..kweli tunatakiwa tujifunze kutokata tamaa.
March 1, 2011 9:23 AM
Anonymous said...
Unajuwa ,Yasinta mkasa hu ni ushahidi tosha,kwa sisi binadamu,tunapo kabiliwa na shida au tatizo,liwe la mardhi nk,imani nikitu muhimu sana.vile vile mungu nimkubwa, na ananiayake na makusudi yake itokeapo shida ama tatizo kama hilo.mimi huamini kilakitu kitokeacho kwa binaadamu nimapenzi ya mungu.kama ni mkono wa binadamu na hila zake basi utateseka kwa muda lakini ,kwa imani na mapenzi ya mungu utapona.Lakini kama yeye ameaamua hataufanyeje utapofuka tu.na mwisho nisawa na tunavyo amini kuhusu kifo.unakuta mtu anapata ajali mbaya sana amboyo labda katika gari lile wote wamepoteza maisha, na ni mtu mmoja tu ka pona.hapo yatasemwa mengi,ikiwemo bahati,au mungu atasifiwa kwa sana,na wakati mwingine utambiwa jamaa alisali sana kabla hajaanza safari.Hivyo imamani ,jitihada,uvumilivu na uelawa/ufahamu nimsingi katika kukuvusha katika shida au tatizo linalo kukabili . kaka s
March 1, 2011 10:46 AM
Mija Shija Sayi said...
Mungu ni mwema. Tunaambiwa kwamba wanaadamu tumepewa jina moja tu ambalo kwalo kila kitu kinawezekana ukiamini hivyo. Jina la YESU.Tunaambiwa kwamba ktk majina yooooote hapa duniani hakuna lipitalo nguvu Jina la YESU, na yote yatalitii jina hilo, sasa FUNGUS nalo si ni jina?FUNGUS imelitii jina la YESU.Mbarikiwe wote...
March 1, 2011 12:11 PM
Koero Mkundi said...
Nimeishiwa maneno..... Nakumbuka niliwahi kumtumia kaka Shaban Email ya kumjulia hali na alinijibu tu kwa kifupi kuwa yuko KCMC Moshi akimuuguza mkewe ambaye alilazwa huko kwa kuumwa na Jicho. Nasikitika kwamba sikuwahi kuwasiliana naye tena, sijui ni usahaulifu au ni kitu gani.....Ni mara nyingi katika baadhi ya makala zangu za huko nyuma nimewahi kuandika juu ya somo la imani, na nimekuwa nikieleza kwa kirefu sana jinsi imani ilivyo na nguvu, lakini naomba nikiri kuwa pamoja na kuandika sana juu ya imani lakini siamini kama ninayo imani inayomfikia Christina. Huo ndio ukweli wenyewe.Dunia hii imetawaliwa na mapepo ya kila aina na kama mtu asipokuwa na imani basi anaweza kwenda na maji. Ahsante sana dada Yasinta kwa juhudi zako za kushirikiana na Christina katika maombi, na pia kupata muda wa kufanya naye mazungumzo hadi kutuwekea ushuhuda huu ambao kwa kweli utawafunua wengi.Mwisho napenda kuwapongeza Wainjilisti James Ramadhan Rajabu, Benson Izoka ambaye namfahamu ingawa sidhani kama yeye ananifahamu, Mwinjilisti Magoti huyu nimeshawahi kukutana naye pale Manzese SDA kwenye Effort moja, na washiriki wengine ambao kwa njia moja au nyingine walishirikiana na Christina kwenye maombi katika kipindi chote cha madhila yake.Mungu ashukuriwe.nami nimejifunza kutoka kwa Christina...
March 1, 2011 12:21 PM
Mija Shija Sayi said...
Dah! dah! Yasinta nimekukubali wewe ni shapu si mchezo..siamini..Nafikiri umeelewa naongelea nini.Ubarikiwe.
March 1, 2011 2:50 PM
Anonymous said...
Samahani kwa mwandishi, naomba kuweka kumbukumbu sawa. Mwinjilisti James Ramadhan Rajabu ni wa Kanisa la Tabata Chang'ombe.Ukitaja Chang'ombe tu, mtu mwingine anaweza kudhani ni Temeke Chang'ombe.nami natoa pole na pongezi kwa dada Christina kwa ujasiri wake.Imani ina nguvu sana. nami nimejifunza pia.Liz wa Tabata
March 1, 2011 5:31 PM
Masangu Matondo Nzuzullima (MMN) said...
Ni kisa cha kugusa moyo. Yote yawezekana ati!
March 1, 2011 6:05 PM
Lisa said...
Inafunza sana if you have faith as small as a mustard seed, you can say to this mountain, 'Move from here to there' and it will move.Yasinta topic ni ushuhuda wakutosha hakuna lisilo wezekana kwa yesu hongera sana kristina mungu awabariki wote.
March 1, 2011 7:40 PM
Swahili na Waswahili said...
Hongera sana da Christina kwa kunga'nga'nia njia ya uzima na kweli!Mungu azidi kukubariki,Kuhusu ccbrt nami nilishakwenda pale kwa vipimo, nikaonekana ninatazizo la macho na natakiwa kuvaa miwani haraka sana, wakanipatiwa yanayo nifaa na bei yake,Mungu ni mwema siku hiyo pia nikuwa na ahadi Ubalozi saa 8 mchana,hapo ilikuwa saa 6.Nikawaambia nitarudi kesho kuichukua,kwenda ubalozi nikapata visa na tukashauriana na baba watoto tukaona tuachane nayo,kuja huku nikapimwa tena nikaambiwa tatizo langu si kuivaa miwani kwa sasa labda niaka 15/20 ijayo.Wakaniuliza ulipima wapi?nikawaambia na kuwapa vyeti vyangu vya huko yaani walilaumu sana.Asante da yasinta kwa kuungana nasi na mafundisho haya!Mungu wetu hashindwi na jambo kama kweli unamuamini na kufuatanjia zake!.
March 2, 2011 12:38 AM
Celestina said...
Kweli hata mim nimejifunza kutoka kwa dada Tina kutokata tamaa.mungu ndo kila kila kitu katika maisha yetu,hata kwa bible amesema 'sitawaacha waaibike wanitengemeao.'Be blessed.
March 2, 2011 12:21 PM
Chacha o'Wambura a.k.a Ng'wanambiti! said...
Nguvu ya imani hakuna awezaye kuipinga!Pole sana da Tina na hongera kwa ujasiri!
March 2, 2011 3:12 PM
NN Mhango said...
Pamoja na tukio hili kugusa nyoyo na kufunza, tuchunge kutoa hitimisho la jumla kuwa imani ni tiba. Inategemea na imani. Maana kuna imani nyingine ni potofu zinaleta maangamizi kama vile ugaidi na mauaji ya kinyama ya albino. Shukrani dada Yacinta kukubali kushiriki nasi tukio hili.
March 2, 2011 8:52 PM
Jeff Msangi said...
Kisa au mkasa wa aina yake.Nilichoambulia mimi ni kitu kinachoitwa Power of Faith au Nguvu ya Imani.Ukiamini hakuna kisichowezekana.Asante Yasinta kwa ushuhuda huu wa Christina.The Lord is alive
March 3, 2011 1:46 AM
Salehe Msanda said...
Habari za siku kadhaa,Nimerudi kutoka mapumzikoNi kweli hilo somo tosha na ni muhimu kila wakati kuwa na matumaini kuliko kukata tamaa na hasa suala lenyewe kama linahusiana na afya yako. maana afya haina mbadala.Tumshukuru muumba kwa kuweza kumuongoza wifi yako kufikia uamuzi wa kuamini kuwa mungu yuko naye na atapona.Ni somo zuri na lina mafundisho mengi kutokana na kile kilichotokea na kwa watu wataalamu wa afya tunanaowaamini na kuwakadhi dhamana ya maisha yetu.Kila la kheri.
March 3, 2011 11:02 AM
emu-three said...
Kweli imani ni tiba, hasa unapokabiliwa na magonjwa ambayo `wataalamu wetu' wanasema `haiwezekani...usikate tamaa na muombe mungu wako kwa imani yako...utafanikiwa, lakini hakikisha kuwa `imani' ipo!
March 3, 2011 12:44 PM
Upepo Mwanana said...
Nijuavyo mimi, madakatari bingwa wa macho kwa Tanzania ni wachache sana, na hata hospitali kubwa zenye majina makubwa , nyingine hazina madakatari bingwa wa macho, ukifika unapokelewa na wasaidizi ambao kwa sera za nchi yetu ati wanatambulika kama madaktari.Hata CCBRT madaktari bingwa ni wachache, na wamejaa wasaidizi.Wanchi siku hizi tunapaswa kujifunza japo huduma ya kwanza na elimu kidogo ya magonjwa tujimudu na bidhaa feki hizi zinazojiita madaktari bingwa! Namkumbuka Kaka yangu Chib, nina imani anaweza kutoa mchango zaidi katika masuala haya ya macho!
March 3, 2011 1:25 PM
Mija Shija Sayi said...
Yasinta upo?
March 5, 2011 5:45 PM
chib said...
Habari hii imenigusa sana, tena moyoni kabisa.Nasikitika iwapo mtu ataangukia kwa mtu asiye elewa sawa tatizo la mwingine na kuishia kumwaga uongo ili aonekane kama anajua.Hospitali alizopitia Christina, nazifahamu vyema tena sana.Nina mengi ya kusema kutokana na maelezo ya Christina, lakini kusema bila kuona, ni sawa na kumwaga uongo zaidi. Kwangu kila moja linawezekana, kwa upande wa kupona haraka, na pia kwa upande wa maelezo ya madaktari. Sijui nisemee upande upi. Ila bado natafakari kwa KCMC kumuita mtaalamu kutoka Nairobi kuja kuchukua sampuli tu...., bado haijaingia kichwani kabisa.Baadaye nikipata muda, nitatoa mada ndefu kuhusu vidonda katika uso wa jicho. Nashukuru Tembe kwa kunikumbuka, japo nipo nahudumia waafrika wenzangu mbali na nyumbani.Lakini tupo pamoja
March 8, 2011 5:08 PM
Anonymous said...
NAOMBA NAMBA YA CHRISTINA .IMANI YAKE IMENITIA MOYO
March 10, 2011 7:16 AM
Ebu tumaliza kwa kusikiliza wimbo huu:-
Tuesday, December 20, 2011
NIMEULIZWA SWALI HILI NA RAFIKI MMOJA!!!
Swali:- Hivi Yasinta kukoroma/kuforota (snoring) ni UGONJWA, URITHI au NI KWA AJILI YA UNENE? Maana mwenzio nina shida sana yaani silali kabisa mume wangu anakoroma sana. ....Nikakumbuka pia nilikuwa na rafiki mmoja akija kusalimia tulikuwa na taabu sana na ikabidi kumtenga na alale mbali kidogo nasi. JE? MNAWEZA KUNISAIDIA KUMJIBU RAFIKI YANGU HUYU? NATANGULIZA SHUKRANI....PIA NAWATAKIENI JUMANNE NJEMA...Kapulya
Tuesday, October 4, 2011
PICHA YA WIKI...MAZOEZI NI MAHIMU KWA AFYA YAKO!!!
Wednesday, April 20, 2011
Kwa nini watu wanapima joto kwenye paji la uso??
Wakati Mwili unapovamiwa na wadudu (bakterie) au virus, kwa kawaida joto huwa linapanda. Hii ndiyo sababu joto la mwilini linaweza kusaidia kugundua kama mtu ni mgonjwa. Wengi watakapo kumpima mtu joto anapojisikia kuumwa wanaweka mkono kwenye paji la uso. Hii yote ni kwasababu tu paji la uso halivaliwi nguo.(Yaani lipo wazi tu na ni rahisi kupima joto kwa haraka)
Kwa vile joto haliwezi kupimwa sawasawa na mkono, kwa hiyo mbinu hii haitoshi. Hivi karibuni kumeanzishwa aina mpya checha za vipimajoto, ambavyo vitaweza kupima joto katika paji la uso. Katika utafiti inaonyesha kwamba joto la paji la uso linayumba na 1,5 C kutoka joto kamili la Mwili. Kwa maana hii njia hii sio nzuri.
Njia nzuri zaidi ni kupima joto makalioni. Pia sikioni au mdomoni. Lakini upungufu ni sawasawa. Ni muhimu/lazima kuongeza nusu C kwa kupata joto kamili.
Chanzo: Illustrerad Vetenskap nr 6/2011
Kwa vile joto haliwezi kupimwa sawasawa na mkono, kwa hiyo mbinu hii haitoshi. Hivi karibuni kumeanzishwa aina mpya checha za vipimajoto, ambavyo vitaweza kupima joto katika paji la uso. Katika utafiti inaonyesha kwamba joto la paji la uso linayumba na 1,5 C kutoka joto kamili la Mwili. Kwa maana hii njia hii sio nzuri.
Njia nzuri zaidi ni kupima joto makalioni. Pia sikioni au mdomoni. Lakini upungufu ni sawasawa. Ni muhimu/lazima kuongeza nusu C kwa kupata joto kamili.
Chanzo: Illustrerad Vetenskap nr 6/2011
Tuesday, February 15, 2011
MAPAPAI :- UTAMU ,FAIDA NA MATUMIZI YAKE!!


Friday, February 11, 2011
BREAKING NEWS: LITTLE MAKULILO AZALIWA

On February 10th, 2011 at 5:42pm, Pacific Time, Marie Makulilo has delivered our cute little Makulilo named BENEDIKT FULBRIGHT MAKULILO. Benedikt has 8.8lbs (weight) and 21 inches (length)
The logic behind the names (Benedikt Fulbright Makulilo)
The logic behind the names (Benedikt Fulbright Makulilo)
The name Benedikt (with letter "K" instead of "C" because of Kiswahili and Germany spelling of Benedikt), which comes from the Latin word meaning "the blessed", in honour of both Saint Bendict of Nursia and Pope Benedict XVI. And the name Fulbright is in honour of the prestigious FULBRIGHT scholarship. Fulbright Scholarship is the scholarship which has been named after William James Fulbright, and it has lot of meaning in realizing my dreams today, and MAKULILO is the honor of unsung hero Boniface Makulilo, my father
Thank you all for your prayers and encouragement.
The Makulilos (Marie, Ernest and Benedikt)
Blog www.makulilo.blogspot.com
www.scholarshipnetwork.ning.com
Thank you all for your prayers and encouragement.
The Makulilos (Marie, Ernest and Benedikt)
Blog www.makulilo.blogspot.com
www.scholarshipnetwork.ning.com
Tuesday, January 18, 2011
JUMANNE YA LEO EBU TUMSIKILIZE DADA HUYU NA STORY YAKE!!
Maisha haya jamani......zaidi bonyeza hapa china kwa pkupata habari yote nzima.
http://www.youtube.com/watch?v=QZ8vRS_FTWM
Tuesday, December 21, 2010
HIVI NI IBILISI AU NI TAMAA?

Watu wakawa wanapita wa kila aina, bahati mbaya au nzuri akapita mwanadada mmoja ambaye ilionekana wamasai hao walikuwa wakimfahamu. Wakaanza kusema, he! Angalia mwanadada yule! Mmoja wao akawa anasema, miezi michache iliyopita alikuwa nusu kufa dada huyu, AMEATHIRIKA(VVU) na alikuwa amedhoofika sio mchezo. Lakini nasikia amepata dawa za kuongeza siku na sasa mwangalie alivyonawiri, mmmhh!
Maongezi yakawa yanaendelea, lakini maongezi yenyewe yalikuwa yakiashiria tamaa ya kimwili walivyo wamasai wale kwa kummezea mate kimwana Yule. Muda wote nilikuwa kimya nikisikiliza maongezi yao. Mara wakawa wanaulizana wapi anaishi binti Yule, na lengo ilikuwa ni kutaka kumwendea na kujivinjari naye. Mwenzenu nikabaki mdomo wazi, mweh!!!
Leo katika kuwaza kwangu ndipo mkasa huu au tukio hili likanipitia na ndio maana leo nimeona tutafakari pamoja. Je? Hii ni tamaa? Au Je? Ni kukosa kufikiri kwa makini? Maana wote walishajua kuwa ameathirika, sasa iweje wammezee mate ya kufanya naye tendo !!!?……
Subscribe to:
Posts (Atom)