Sunday, March 23, 2014
KUMBUKUMBU...LEO NI MIAKA MITATU TANGU MPENDWA WETU ASIFIWE NGONYANI ATUTOKE
Saturday, March 23, 2013
KUMBUKUMBU...LEO NI MIAKA MIWILI TANGU MPENDWA WETU ASIFIWE NGONYANI ATUTOKE
Saturday, November 26, 2011
LEO NI 26/11/2011 NDIYO SIKU ALIYOZALIWA ASIFIWE NGONYANI


Wednesday, November 23, 2011
TUTAKUKUMBUKA DAIMA ASIFIWE NGONYANI!!!
Tuesday, November 22, 2011
ASIFIWE NGONYANI (1989- 2011). Kioo kingine cha maisha yetu, kwa maisha yetu na wenzetu
"..see you in ZION, holding hands together standing by MY FATHER'S SIDE. Meet you in ZION singing songs together....." LUCIANO


AHSANTE MZEE WA CHANGAMOTO/KAKA MUBELWA BANDIO!!!
Monday, November 21, 2011
NI WIKI YA PEKEE KWANGU/KWETU-ITAKUWA NI WIKI YA KUMKUMBUKA ASIFIWE!!!
Ni hivi blog ya MAISHA NA MAFANIKIO inapenda kuwaambia kwamba wiki hii haitakuwa kama kawaida. Nitawaambia kwa nini, ila kwa kifupi ni kwamba itakuwa wiki ya kumuenzi mdogo wangu marehemu Asifiwe. Kwa namna nyingine haitakuwa kama kawaida hapa kibarazani. NINA IMANI TUTAKUWA PAMOJA /MTAKUWA PAMOJA NAMI NATANGULIZA SHUKRANI ZANGU ZA DHATI. KAPULYA.
Saturday, April 23, 2011
KUMBUKUMBU:- LEO UMEFIKA MWEZI MMOJA TANGU ASIFIWE WETU ATUTOKE!!

Hapa china nilitumiwa barua pepa na kaka Raymond Mkandawile ujumbe huu ufuatao. Nami nimeupenda ni ujumbe mzuri na nimeona ni vizuri niuambatanishe hapa. Ahsante sana.Ujumbe wenyewe ni huu :-
Duania tu wapitaji na hakuna ajuaye siku yake ni lini. Hivyo hatuna budi kujiandaa na kuwa tayari kila itwapo leo.Dada yetu Asifiwe pumzika kwa amani na sisi pia tunafuta....bwana alitoa na yeye ametwaa jina lake libarikiwe.
Si vibaya kama tukisikiliza na nyimbo hizi ambazo Asifiwe alikuwa akisikiliza sana....
HALAFU HUU PIA ALIUPENDA PIA....
WOTE TWAJUA UMETUACHA KIMWILI LAKINI KIROHO UPO NASI NA TUTAKUKUMBUKA NA KUKUPENDA DAIMA!!!
Tuesday, April 5, 2011
NIMEMKUMBUKA KWELI MDOGO WANGU ASIFIWE LEO
Asifiwe! Asifiwe! sauti zetu sikia,
Asifiwe! Asifiwe! kweli unatusikia?
Asifiwe! Asifiwe! mbona hujaitikia?
Asifiwe umekwenda, dunia 'meikimbia,
Wajua tulikupenda, ila Mungu kazidia,
Mauti yamekutenda, wewe umetangulia,
Pumzika kwa amani, Asifiwe Ngonyani.
Umetwachia majonzi, hakika twakulilia,
Tumejawa na simanzi, hatuwezi elezea,
Mdogo wetu mpenzi, uchungu 'metuachia,
Pumzika kwa amani, Asifiwe Ngonyani.
Ulijawa na adabu, nao ukarimu pia,
Kwa wako utaratibu, ni nuru imepotea,
Umekwenda kama bubu, kwa heri hukutwambia,
Pumzika kwa amani, Asifiwe Ngonyani.
Wewe mtu mwuungwana, kwa njema yako tabia,
Tulikupenda kwa sana, nd'o maana twaumia,
Mfano wako hakuna, kwa pengo kulizibia,
Pumzika kwa amani, Asifiwe Ngonyani.
Kuondoka kwatuliza, kila tukifikiria,
Twatamani tungeweza, kifo tungekizuia,
Mwaka huu kumaliza, nayo inayof'atia,
Pumzika kwa amani, Asifiwe Ngonyani.
Lakini sisi ni nani, Mungu tukamwamulia?
Tukamwuliza kwa nini, wewe amekuchukua?
Mwamuzi ndiye Manani, aloiumba dunia,
Pumzika kwa amani, Asifiwe Ngonyani.
Pengo halitozibika, wewe ulotuachia,
Daima 'takukumbuka, wema'wo kusimulia,
Tukimwomba Rabuka, mwanga kukuangazia,
Pumzika kwa amani, Asifiwe Ngonyani.
Upumzike salama, kwa Mola twakuombea,
Akupe pahala pema, nuru kukuangazia,
Asifiwe mtu mwema, buriani twakwambia,
Pumzika kwa amani, Asifiwe Ngonyani.
Shairi hili nimeliandika maalumu kwa marehemu Asifiwe Ngonyani, mdogo wa kike wa dada yetu, rafiki yetu na mwanablog mwenzetu Yasinta Ngonyani. Asifiwe alipatwa na mauti Jumatano 23.03.2011. Asifiwe umetuacha kimwili tu, kiroho tungali pamoja nawe. Tunakuombea pumziko salama la milele. Amina. AHSANTE SANA MTANI FADHY KWA SHAIRI HILI!!