Monday, December 31, 2018

UJUMBE WA MWISHO WA MWAKA 2018 KUTOKA KWANGU KUJA KWENU

UJUMBE :-
HATA SURA NZURI ITAZEEKA, NA MWILI MZURI UTACHOKA, ILA ROHO NZURI HUBAKI  KUWA NZURI MILELE NA MILELE.
NACHUKUA NAFASI HII KUWASHUKURUNI SANA KWA MWAKA HUU 2018 KWA USHIRIKIANO WENU. AHSANTE SANA SANA . NI MIMI KAPULYA WENU.

Wednesday, December 26, 2018

MWOKOZI YESU AMEZALIWA


NI MATEGEMEO YANGU KUWA SIKUKUU HII YA KUZALIWA MWOKOZI WETU IMEKUWA NJEMA KWA WENGI WETU. NAMI NACHUKUA NAFASI HII NA KUSEMA NAWATAKIENI  WOTE NOELI NJEMA

Monday, December 17, 2018

LEO NIMEKUMBUKA MITINDO YA ZAMANI JINSI WATU WALIVYOKUWA WAKIPEANA HISIA ZAO

Hapa itakuwa anaenda kisimani ndoo kaficha sehemu, hivi unafikiri kwa nini hawaangaliani?
Hapa yaonekana mdada anaenda kutafuta kuni

...na mtindo huu ni kiboko wote wanaonekana kuwa na aibu ...


....hii ni  baadhi ya mitindo ya hapo kale.  Au pia watu walikuwa wakiandika barua au kumtuma mtu. Siku hizi eti mtu anatuma sms ya kawaida au WhatsApp

Thursday, December 13, 2018

TAREHE HII HAPA LEO NI SIKUKU YA MTAKATIFU LUCIA...

Kwa hiyo mimi nimeona itapendeza zaidi kama nikiitumia mikono yangu kwa kutengeneza aina hii maalumu ya mikate(LUSSEKATTER)  ili kujumuika ndugu, marafiki pia majirani kwa kusherehea siku hii....


.....pia aina hii ya biskuti (pepparkaka) GINGERBREAD


Na hapa ni maagizo  jinsi inavyokuwa. Nakumbuka binti yetu aliwahi kuigiza duh! niliogopa sana maana hiyo mishumaa inawaka kwa ukweli ......ila walijiandaa na ndoo za maji...

Monday, December 10, 2018

HAPO KALE KARIAKOO YETU ILIVYOKUWA........

NAWATAKIENI WOTE JUMATATU NJEMA SANA. PANAPO MAJALIWA TUTAONANA TENA!

Wednesday, December 5, 2018

NIMEYATAMANI SANA HAYA MATUNDA...............


Hapa ni mbula au sisi wangoni twasema  mabuni ni matamu sana pia juisi yake ni tamu mno.
Na hapa ni masuku, sasa ndio msimu wake 

Tuesday, December 4, 2018

NI MWEZI MPYA TENA ...TUANZE NA MSEMO HUU KUUANZA MWEZI HUU WA KUMI NA MBILI!

Msemo/ujumbe wa leo:-
Njia bora ya kuacha kuwaza ni jinsi gani unafikiri ya kwamba unajifahamu/jijua ni kuzingatia kile unachokijua, unajua.
TUKUTANE TENA PANAPO MAJALIWA!