Showing posts with label mwisho wa maisha. Show all posts
Showing posts with label mwisho wa maisha. Show all posts

Saturday, March 26, 2011

MAZISHI RUHUWIKO: TUUNGANE PAMOJA KWA KUMSINDIKIZA MPENDWA WETU ASIFIWE NGONYANI KATIKA SAFARI YAKE YA MWISHO

Asifiwe Ngonyani
Kuzaliwa 26/11/1989
Kuiacha dunia 23/3/2011
Kuzikwa 26/3/2011

Asifiwe Ustarehe kwa amani peponi Amina

Habari nilizozipata leo kutoka nyumbani Ruhuwiko ni kwamba watu wengi SANA wamemiminika na wanazidi kumiminika.TWAMSHUKURU MUNGU KWA HILI.
Leo tarehe 26/3/2011 siku ya jumamosi saa tatu tukwenda kuchukua mwili wa Asifiwe katika sehemu ya kuhifadhi miili katika Hospitali ya mkoa Songea. Baada ya hapo mwili wa Asifiwe unapelekwa nyumbani Ruhuwiko kwa buruani ambayo itakuwa saa tano. Saa sita mchana maandamano kwenda kanisani Ruhuwiko. Saa saba nusu mchana misa inaanza katika Kanisa la Ruhuwiko. Na baada ya hapo wote tunaandamana ili kumsindikiza mpendwa wetu ASIFIWE NGONYANI KWA SAFARI YAKE YA MWISHO. MWENYEZI MUNGU TWAKUOMBA UIPOKEE ROHO YAKE PEPONI AMINA.

FAMILIA YA MZEE NGONYANI NA FAMILIA YA NGONYANI/KLESSON ITATOA SHUKURANI ZA DHATI KWA USHIRIKIANO WENU KATIKA KIPINDI HIKI KIGUMU!!!!