Tuesday, December 31, 2013

SALAMU ZA MWAKA MPYA KUTOKA KWA MAMA MAISHA NA MAFANIKIO NA FAMILIA YAKE !!!

Marafiki,ndugu, na wasomaji  wapendwa!
Ukaribisheni mwaka mpya uwe wa Mafanikio, Amani, Mwanga na Furaha katika maisha yetu.
Nakutakieni wote, wewe na familia yako kila jema na furaha tele katika mwaka mpya 2014.
KHERI KWA MWAKA MPYA 2014. KUMBUKENI WOTE MNAPENDWA!!!!
Nimeona si mbaya kama tukiuvuka mwaka huu kwa kipande hiki cha mziki si mnajua mziki na kazi au mziki,sherehe aaahh ngoja tuserebuke!!.....
TUMWOMBE MUNGU TUONANE NA KUSEMA TENA MWAKA 2014..NA UWE MWAKA WA MATUMAINI----NANGONYANI/KAPULYA

Sunday, December 29, 2013

TUMALIZA JUMAPILI YA MWAKA HUU 2013 NA MWIMBO HUU WA DADA BAHATI BUKUKU :- DUNIA HAINA HURUMA.


NAWATAKIENI WOTE JUMAPILI HII YA MWISHO KWA MWAKA HUU 2013 IWE NJEMA SANA WAKATI TUKIUSUBIRI MWAKA 2014. JUMAPILI NJEMA SANA....KAPULYA

Thursday, December 26, 2013

NAPENDA KUWAKUMBUSHENI TUSISAHAU KULA MATUNDA...BOXING DAY NJEMA!!!!!

Namshukuru Mwenyezi Mungu Noeli imekwisha vizuri pamoja na kwamba Noeli yangu imeishia mzigoni. Kila la kheri. TUSISAHAU MATNDA:-D....Nangonyani

Tuesday, December 24, 2013

SALAMU ZA CHRISTMAS KUTOKA KWA KAPULYA.....

Nawatakieni wote sikukuu hii ya Christmas/Noeli iwe yenye baraka, amani, upendo na furaha. Mwenyezi Mungu na awe pamoja nanyi kwa kila mtakachofanya. CHRISTMAS NJEMA/GOD JUL!!

Monday, December 23, 2013

TUANZE JUMATATU HII KIHIVI NA NENO AMANI!!!

AMANI:- Ni kitu cha thamani sana. Ambacho kila mtu angependa kuwa naye au hata kuwa na ndoto.
NAWATAEKIENI WIKI HII YA NOEL IWE NJEMA NA NOELIENDE SALAMA. KAPULYA

Sunday, December 22, 2013

NI DOMINIKA YA NNE YA MAJILIO MWAKA A..PIA BADO SIKU CHACHE NA NDIPO ITAKUWA KUZALIWA KWAKE YESU MKOMBOZI WETU

"Bikira atachukua mimba, atamzaa mtoto wa kuime, naye ataitwa Emanuali" Maana yake "Mungu yupo pamoja nasi."
NAPENDA KUWATAKIENI WOTE JUMAPILI HII KABLA KUZALIWA KWAKE BWANA WETU YESU KRISTO IWE NJEMA KWA WOTE. KAMA ILIVYOANDIKWA MUNGU YUPO PAMOJA NASI. WOTE MNAPENDWA....KAPULYA

Friday, December 20, 2013

MWEZI DESEMBA:- A MONTH OF DECEMBER SIMPLY STANDS FOR......

D- days of
E- evaluation
C- celebration
E- encouragment
M- memorizing the
B- blessings
E- establing next year plans and
R- renewing your relationship with God.

BASI NGOJA NIWATAKIENI MWANZO MWEMA WA MWISHO WA JUMA HILI AMBALO LINATUPELEKA SIKUKUU YA KUZALIWA BWANA WETU KRISTO.

Thursday, December 19, 2013

HATIMAYE NIMEPATA MBOGA YA LIKUNGU AMBAYO NIIPENDAYO..NYASA SAFI SANA

 Hapa ni katika maandalizi ya hii mboga tamu ya likungu ..halafu likungu ni tamu zaidi liwapo bado halijakaushwa sana yaani linatoka tu kukamatwa na kukanda na kuchemsha na chumvi  halafu ugali wa muhogo weweeeee....utajiuma kidogolo...
Na hapa tayari limekaushwa kwa moto kwa akiba au kwenda kuuza...nadhani waliowahi kula wananielewa....Ni mboga nzuri sana ..Alhamis njema kwa wote.

Wednesday, December 18, 2013

NAPENDA KUTOA SHUKRANI WA WOTE MLIOTUFARIJI KWA MSIBA WA BIBI YETU..

Shukrani nyingi ziwafikieni wote mliokuwa pamoja nasi katika sala na kutufariji kwa kupitia hapa Maisha na Mafanikio na pia mail pia ujumbe wa simu ya kiganjani. Mwenyezi Mungu na azidi kuwapa upendo. Na sasa hivi tu nimepata taarifa kuwa zoezi la kumsindikiza bibi yetu kwenye nyumba ya milele zimeenda safi. Ahsante Mungu...Pumzika kwa amani bibi yetu mpendwa.

Sunday, December 15, 2013

TUMEPATWA NA MSIBA LUNDUSI/PERAMIHO KWA AKINA NGONYANI

PUMZIKA KWA AMANI BIBI NAPINGI
Hapa ilikuwa 2001 nyumbani Lundusi/Peramiho. Ni baba yangu mkubwa na mke wake na mjukuu wao. Lakini kwa vile baba yangu alilelewa na wao basi sisi watoto wake tumezoea tangu utoto kuwaita babu na bibi...hii ni historia fupi sana. Kwa hiyo leo asubihi mapema nimetumiwa taarifa kuwa bibi hatunaye tena. Amekuwa ameugua muda mrefu sasa. Bibi tutakukumbuka daima kwa yote mema na mazuri uliyotuachia. Sisi tulikupenda lakini Mungu anakupenda zaidi. Lihidimiwe jina lake. PUMZIKA KWA AMANI BIBI TUPO KATIKA MAOMBI.  MUNGU AIPE FAMILIA YA NGONYANI KOKOTE ILIPO NGUVU KWA KIPINDI HIKI KIGUMU.

Friday, December 13, 2013

HAPO SASA UNAUZA VIATU MWENYEWE UNAPIGA ZA KUKU......KAAZIII KWELIKWELI!!!

Hapa nimekumbuka mzee mmoja alikuwa akivua samaki halafu anaziuza zote na yeye mwenyewe na familia wanakula mboga maji au maharagwe. Au kuna wengine walikuwa wakilima mpunga basi wanauza wote na wenyewe wanakula ugali kila siku kwa raha zao zoteee! Haya ngoja niwatakieni Alhamis njema

Wednesday, December 11, 2013

HUU NI MLO WANGU WA LEO MCHANA UGALI NA SUKUMAWIKI/MBOGA MABOGA!!!

Mlo aupendao Kapulya ndo huu Ugali kwa mboga maboga. Halafu sasa napenda kupika mboga hii bila mafuta wala kitunguu. Ni maji, chumvi, nyanya na pilipili kama ipo kwa mbaliiii.....mmmhhh hapo ndo utauona utamu wa mboga hii. Mboga ni kazi ya mikono yangu mwenyewe. Awekaye akiba basi hana shida kifuku kikija:-) MUWE NA JIONI NJEMA NA WALE WENYE MCHANA AU ASUBUHI BASI NA IWE NJEMA, NA USIKU UWE MWEMA PIA. Kapulya!!!!

TUSISOME MAWAZO YA WENGINE!

Ni hatari kwa mtu kudhani kwamba, anajua kila ambacho kinaendelea kwenye mawazo au hisia za mpenzi wake. Kuna uwezekano mkubwa hisia zako zinaweza zisiwe sahihi, kama ambavyo mara nyingi imekuwa ikitokea. Kuna migogoro mingi ambayo chanzo chake ni hisia potofu, hisia zitokanazo na mtu kujaribu kuingia kwenye mawazo au hisia za mwenzake.

Hebu fikiria, umeingia ndani mwako kutoka huko utokako. Unamkuta mumeo/mkeo akiwa amekunja uso. Kabla hujamuuliza chochote unaanza kufikiria kwamba, amekasirika kwa sababu leo umechelewa kurudi nyumbani kwa nusu saa tu. Unaanza kuwaza kwa kulaani kwamba, mumeo/mkeo siyo mtu wa maana kwa sababu ya wivu. Unaweza kufikiria kwamba, usiku huo utamwambia ukweli na kama ni kugombana ni afadhali iwe hivyo, halafu unamuuliza "Vipi mbona uko hivyo, nini tena?"

Mumeo/mkeo anakujibu "Hapana, nina taarifa mbaya, nimesimamishwa kazi kutokana na tuhuma fulani...." Unabaki ukiwa umepanua mdomo, kwa sababu uliingia kwenye mawazo yake na ukawa umekosea sana. Mfano huu ni wa jambo dogo, kuna wakati tunaweza kuingiza mawazoni mwetu fikra kwamba, wenzetu hawatupendi kwa kudhani kwetu kwamba tunaweza kujua yale yanayoenda mawazoni mwao. Kutokana na kufikiri kwetu hivi, tunaweza kuanza kufanya mambo ambayo sasa ndiyo yatapelekea wapenzi wetu kuacha kutupenda.
HABARI HII NIMEITOA KWENYE KITABU CA MAISHA NA MAFANIKIO KILICHOANDIKWA NA MUNGA TEHENAN...JITAMBUE
--------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
Hii huwa inatokea mara nyingi sana na watu wengi wamepoteza marafiki zao kwa hili jambo la kusoma mawazo...ni bora kuuliza....

Monday, December 9, 2013

TUANZA WIKI HII NA TAARIFA HII/BUSTANI MPAKA MWAKANI MWEZI WA SITA :-(

 Hapa ilikuwa mwezi wa sita-tisa mwaka huu ..ni kutoka tu nje na kuchuma mboga na kula ......
THELUJI IMEANZA
Na sasa eneo hilo hilo leo linaonekana hivi. Inabidi nisubiri mpaka mwakani mwezi wa sita tena. Kaaazi kwelikweli....mmhhh labda nitumie makopo sijui?? Je mna ushauri wowotw ule?

Sunday, December 8, 2013

NAWATAKIENI JUMAPILI NJEMA ....LEO NA MTOKA WA NYEUPE HIVI NDIVYO NILIVYOTOKEZEA IJUMAA..!!!MWANAMTINDO KAPULYA:-)

 Leo mdada kavalia nyeupe ilikuwa ijumaa kulikuwa na sherehe na hivyo ndivyo alivyotokezea ....:-)
Anashangaa kama vile anatoka usingizini....Mpiga picha ni kaka Erik. Nawatakieni wote Jumapili njema sana na iwe yenye upendo na baraka. na pia maandalizi mema ya Noel.

Saturday, December 7, 2013

SIKU ZAKE ZIMEKWISHA :- A Tribute Poem for Nelson Mandela by Dr. Maya


TUENDELEE NA MAOMBOLEZO YA BABU YETU NELSON MANDELA ..SHAIRI HILI LIMENIGUSA SANA...DR.MAYA  AHSANTE SANA...

Friday, December 6, 2013

AFRIKA TUMEPATWA NA MSIBA BABU YETU NELSON ROLIHLAHLA MANDELA HATUNAYE TENA.

Nelson Mandela wakati wa uhai wake
 
1918-2013....ni pengo kubwa umeacha. Utakumbukwa daima. Mwenyezi Mungu ailaze roho yako mahali pema. Amina.


TUTAKUKUMBUKA DAIMA MKOMBOZI WETU. AMINA

Thursday, December 5, 2013

MATUNDA NI MUHIMU KATIKA AFYA ZETU TUZINGATIE...

Huu ni mlo wangu wa leo mchana mchanganyiko wa matunda mbalimbali. Kama ilivyo ni kwamba matunda ni muhimu katika afya zetu. Usisahau kula hata tunda moja tu  kwa siku....Kila la kheri kwa wote....

Tuesday, December 3, 2013

JUMANNE YA LEO TUTEMBEE KWETU LITUMBANDYÓSI /NYUMBANI NI NYUMBANI!!!

 Hapa ni sokoni petu ukitaka dagaa, viazi vitamu, samaki nk.utapata bila matatizo:-) 
 Na hapa usipotaka dagaa au samaki basi waweza kujipatia kiti moto ...
Na hapa ndo unga tayari umeshasagwa kwa hiyo hakuna shida. Isipokuwa  ni  kuandaa chakula tu sasa....Nimeutamani huu unga basi tu...NAWATAKIENI JUMANNE NJEMA..

Monday, December 2, 2013

AKIBA HAIOZI HAPA MVUA IKIKOLEA HAKUNA SHIDA HAPA!!!

Ni Jumatatu ya kwanza ya mwezi huu nami nimeona tuanza kihivi. Akiba haiozi si mnajua mvua zikianza. Ila hapa kajiandaa haswaa hakuna shida kwa kweli.......NAWATAKIENI JUMATATU NJEMA NA MWANZO MWEMA WA JUMA. TUPO PAMOJA...KAPULYA/KADALA:-)

Sunday, December 1, 2013

JUMAPILI HII YA KWANZA YA MAJILIO MWAKA A NA IWE NJEMA KWA WOTE

Napenda kuwatakieni wote Jumapili hii ya kwanza ya mwezi huu wa kumi na mbili. Na pia ni Jumapili ya kwanza ya majilio. JUMAPILI NJEMA KWA WOTE.

Thursday, November 28, 2013

MWANAMTINDO WA LEO NA MTOKO WA NYEUSI ....BLACK IS GOOD !!!!

 Hivi ndivyo lilivyokuwa vazi langu leo koti ndefu nyeusi na suruali vimenunuliwa UNIQUE,blauzi/line toka Vila clothes.
 Hapa mdada anaonekana kuwa mbali kweli kimawazo.....
 ....hapa anawaza sijui nibadili kazi na kuwa mwana mtindo....anaendelea kufikiri
Na mwisho inaonekana hajapata jibu bado kwa hiyo anaendelea kufikiri. Je wasomaji mnaonanaje  kuhusu hili na kuhusu vazi la leo?....NAWATAKIENI WOTE KAMA ILIVYO HAPO ULIPO IKIWA ASUBUHI, MCHANA, ALASIRI, JIONI AU USIKU..BINAFSI NI JIONI HAPA NA NAANZA KUJIANDAA KUPIKA MLO WA JIONI.

MAISHA YA NDOA:- NIMEULIZWA SWALI HILI NA RAFIKI/MFANYAKAZI MWENZANGU!!!!

AKIWA MAWAZONI
Habari za leo Yasinta, ni siku nyingi hatujaonana. U- hali gani? Vipi familia ni wazima wa afya?  Nikamjibu, salama tu na familia wote wazima. Sijui wewe na familia yako? Akaguna...mmmhhh! Sina uhakika, sijisikii vizuri niko katika mawazo mengi. Sijisikii raha kabisa kuwa na mume wangu. Lakini ni ajabu kwa kuwa huwa hawi nyumbani muda wote. Anafanyia kazi zake mbali kidogo anaweza akawa hayupo nasi wiki moja au mbili. Kwa hiyo ilibidi nimfurahie/tufurahiane arudipo lakini ni kinyume. Yasinta, mimi bado kijana..38 na yeye 35, nipo njia panda, sifurahii maisha niliyo nayo. Pia mwenzangu naye haonyeshi kama ananijali.  Nifanye nini? Nisaidie?
Duh! Hapo Kapulya akabaki hoi maana ushauri wangu.....si wa kiataalamu wa mambo ya ndoa. Nikakumbuka Maisha na Mafanikio, kuwa nikiweka hapa kwa pamoja tutaweza kumsaidia rafiki yangu. Na ndio maana nawaombeni tujadili kwa pamoja.  Kwani kesho laweza kukupata wewe au mimi au yule n.k. Nawatakieni kila la kheri na mjadala mwema. SIKU IWE NJEMA......Kapulya

Tuesday, November 26, 2013

TULIO WENGI TUNAKUMBUKA HIKI NI NINI!!!

Lakini wengi nadhani tunakumbuka vya matete...ni vihesabio/kalukuleta za zamani hizo. Hicho ni kihesabio cha dada Camilla wakati akiwa Mdunduwalo/Ndirima shule ya msingi na ni baba yangu katengeneza. Ametengeneza kwa visoda. Je? wewe umewahi kutumia vihesabio vya aina hii?

Monday, November 25, 2013

TUANZA JUMATATU HII NA SWALI HILI KUTOKA KWA KAKA BWAYA ...KUHUSU MAISHA NA FURAHA!!!

Kama mnakumbuka mwezi uliopita niliweka picha hii hapa kibarazani na baadaye kulitokea na maoni. Na baadhi ya maoni aliyotoa msomaji mmoja ambaye ni kaka Bwaya ambaye alikuwa ameadimika kwa muda mrefu na sasa yupo nasi tena. Nachukua nafasi hii kumkaribisha Kaka Bwaya......Haya na maoni yenyewe yalisomeka hivi;-
Bwayasaid...
Tafiti zinaonyesha kuwa watu waishio katika maisha yanayoonekana kuwa duni, ndio wenye furaha zaidi. Mfano ni hawa. Swali: kwa nini? Naomba tusaidiane kujadili swali hili kwa pamoja....JUMATATU NJEMA!!!

Sunday, November 24, 2013

HIVI NDIYO ULIVYOKUWA MLO WA ASUBUHI YA JUMAPILI YA LEO /CHAPATI KWA CHAI!!

 Chapati zinasukumwa huku chai ikiandaliwa
 chapati zinakaangwa
 chapati tayari kwa kuliwa
Na hivi ndivyo meza ilivyoandaliwa Jumapili hii ya leo. Chapati bado zipo na chai pia karibuni kujumuika nasi. NAWATAKIENI WOTE MTAKAOPITA HAPA JUMAPILI YENYE BARAKA NA UPENDO. MWENYEZI MUNGU NA AWE NANYI. AMINA......KAPULYA/KADALA.

Friday, November 22, 2013

HIVI NDIVYO ILIVYOKUWA HAPO KALE UJAMAA, UMOJA, USHIRIKIANO NA UNDUGU !!!

 
Lakini leo /sasa kila mtu na chake. Hakuna tena ule umoja wa kunywa pamoja, kula pamoja na kusali pamoja. Je? kwa nini umoja wetu umepotea?----Nawatakieni wote Ijumaa njema ila usiwe ugimbi/ ulanzi/ pombe...mwingi/nyingi ,,Lol

Thursday, November 21, 2013

NIMEONA TUBAKI MKOANI RUVUMA:-TATIZO LA UMEME SONGEA KITENDAWILI!!!

Katika pitapita nimekutana na habari hii ambayo imenikasirisha na kunikatisha tamaa sana maana nilikuwa katika harakati ya kuingiza umeme katika nyumba yangu. Ila najipa moyo na kuendelea ebu soma hapa habari hii iliyoandikwa Na Albano Midelo.
------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
 












 


 
 
 
Hapa ni baadhi ya vijana katika mji wa Songea wakifanya maandamano ya amani kudai umeme wa uhakika mjini Songea.
 
“TANESCO wanakata na kurudisha umeme bila taarifa na hata ratiba ya mgao haijulikani hali inasababisha hasara kubwa kwa wananchi ikiwemo kuungua vifaa vya umeme na vyakula vinavyohifadhiwa kwenye majokofu kuharibika’’,anasema diwani wa kata ya mjini manispaa ya Songea Joseph Fuime.
Fuime alidai kuwa tatizo la umeme Songea haliwezi kupatiwa ufumbuzi wa kudumu kwa kuendelea kutumia mashine chakavu za kufua umeme ambazo vipuri vyake vinaharibika mara kwa mara badala yake alishauri serikali kuunganisha mkoa wa Ruvuma na umeme wa giridi ya Taifa.
“Serikali iliahidi mara baada ya kuanza kuchimbwa makaa ya mawe ya Ngaka wilayani Mbinga kutajengwa kinu cha kufua umeme katika mji wa Songea hata hivyo tangu mwekezaji ameanza kuchimba makaa ya mawe hadi sasa hakuna dalili za kufungwa kinu hicho pia mwekezaji ameshindwa hata kuwalipa fidia wananchi wanaoishi katika eneo la mgodi’’,alidai Fuime ambaye pia ni katibu wa CHADEMA mkoa wa Ruvuma.
Uchunguzi uliofanywa katika maeneo mengi ya mji wa Songea umebaini kuwa vibaka wakati wa usiku wameongezeka na kusababisha nyumba nyingi kukatwa nyanya za madirishani na wengine kuibiwa vitu mbalimbali zikiwemo simu za mikononi,mavazi,kompyuta za mkononi na samani mbalimbali.
Waandishi wanakwama kutuma habari zao kwa haraka na hata vituo vya matangazo vilivyopo mjini Songea vikiwemo Redio Maria,radio Jogoo,TBC Taifa, vinashindwa kurusha matangazo kwa wananchi kutokana na kukatika kwa umeme mara kwa mara.
John Mapunda mfanyabiashara soko kuu la Songea anasema Kukatika kwa umeme na kuwaka bila taarifa katika mji wa Songea kunawasababishia hasara kubwa wafanya biashara wa vyakula hasa wanaouza samaki wabichi kutoka ziwa Viktoria, Tanganyika, Nyasa na bwawa la Mtera ,wao wanatunza samaki hao katika makojofu ambayo yanatumia umeme wa TANESCO hivyo samaki wengi wanaoza.
"TANESCO katika manispaa ya Songea inaonyesha dhahiri kuwa mashine zao haziwezi kufua umeme wa kukidhi hata katika mji wa Songea,wananchi tunahoji kwanini umeme huo umesambazwa hadi mji mdogo wa Peramiho badala ya kusubiri umeme gridi ya Taifa’’,alihoji Mapunda. Frank Mbunda mkazi wa Mahenge mjini Songea anadai kuwa TANESCO wameshindwa kumaliza tatizo sugu la umeme ambalo linachangia umasikini kwa wakazi wa Songea ambao wanashindwa kufanyakazi zao za kiuchumi.
Mwanaharakati Mohamed Kudeka mkazi wa Songea anatoa wito kwa serikali kuachana na umeme wa majenereta ambao matatizo yake ya kuharibika kwa vipuri yamekuwa yanajirudiarudia na kusababisha kero kubwa kwa wakazi wa mji wa Songea ambao wanashindwa kufanya kazi za kiuchumi na kusababisha umaskini.
“Mchawi ni ugonjwa wa majenereta ambayo vipuli vyake vimechoka na kuchakaa,tumechoka na kero hii kama sio ubovu wa vipuri utasikia mafuta ya kuendeshea mitambo yamekwisha,mara fundi wa kufunga vipuri anatoka nje ya nchi TANESCO tuambieni ukweli tumechoka’,anasisitiza.
Brighton Mwandata mmiliki wa studio ya kurekodi muziki Matarawe mjini Songea anasema umeme katika mji wa Songea haujapatiwa ufumbuzi wa kudumu anashindwa kurekodi kutokana na tatizo la kukatika kwa umeme mara kwa mara wakati mwingine inamgharimu kukodisha jenereta kwa gharama kubwa. Ingia hapa kwa kusoma zaidi habari hii.

Tuesday, November 19, 2013

AKINA MAMA WAPO KIWANDANI KUCHAMBUA KOROSHO HUKO TUNDURU MKOANI RUVUMA!!!

Hapa ni baadhi ya akina mama wakichambua Korosho kwenye moja ya kiwanda wilayani Tunduru mkoani Ruvuma......Nimekumbuka mbali sana wakati naishi Litumbandyósi na Kingole kuilikuwa/kuna Korosho nyingi sana. Basi mimi na kaka zangu tulikuwa tukizishughulikia hizo wewe acha tu, yaani mpaka mikono pia vidole vilikuwa vinachubuka maana Korosho zina mafuta fulani hivi yaliyosababisha iwe hivyo. Ila kwa kweli ilikuwa raha sana....picha hii nimeitoa kwa mdogo wangu Ester Ulaya.

Monday, November 18, 2013

HABARI NJEMA:- NI KWAMBA LEO NIMEPATA UNGA WA MAHINDI:- LEO MLO UGALI NA MBOGAMBOGA:-)!!!

Habari za wikiendi ndugu zanguni...kama mnakumbuka vizuri niliwaambia kuwa niliishiwa unga wa ugali. Sasa katika kutafuta tafuta nimepata kama muonavyo katika picha. Unga ni mweupe kama wa mahindi ya nyumbani. Huu unatoka Venusuela...Haya sasa karibuni kula ugali:-) NAWATAKIENI WOTE MWANZO MWEMA WA JUMATATU!!!

Saturday, November 16, 2013

JUMAMOSI :- MAISHA YANA MITIHANI YAKE!!

Ukiwa MTEMBEZI utafaidi mengi ..jana nilitembela hapa na nikakutana na wazo hili ambalo nimelipenda sana na nikaona kwa nini lisiwekwe hapa Maisha na Mafanikio ..Haya karibu!!
 
WAZO LA LEO: Maisha yana mitihani yake, ukiona kwako ni kugumu, ujue kuwa kuna wenzako kwao ni kugumu mara mbili yako, ukipatwa na mitihani ka hiyo...usikate tamaa, pambana, ukijua kuwa wewe sio wa kwanza kupata mitihani kama hiyo, wapo waliopata mitihani hiyo na wakaishinda, kwanini wewe usiweze...kumbuka baada ya dhiki, mara nyingi ni faraja.
BONGE LA WAZO ....JUMAMOSI NJEMA SANA

Friday, November 15, 2013

HAYA NI MAPISHI YA IJUMAA YA LEO KUKU.....KARIBUNI

Ijumaa ya leo itakuwa kuku ambayo ni:- kuku mzima, viazi, karoti, kitunguu, kitunguu saumu, tangawizi, nyanya kopo, binzari, mafuta, chumvi na maji..... Picha zaidi zinakuja baada ya muda tu....Kwa hiyo mnakaribishwa kujumuika nasi.

Na hapo ndivyo ilivyoonekana sahani yangu...wali, kuku, kiazi, karoti na mboga majani /figili ambayo imeliwa na mikono yangu mwenyewe......Karibuni chakula kipo kingiiiii kweli. Jioni njema sana na panapo majaliwa tutaonana tena kesho.

NAWATAKIENI MWISHO MWEMA WA JUMA NA IJUMAA IWE NJEMA KWA WOTE..


IJUMAA NJEMA KWA WOTE...KAPULYA...KADALA ...

Tuesday, November 12, 2013

NIMETAMANI JIONI HII NILE/NIPIKE UGALI ILA SINA UNGA NA NDIPO NILIPOKUMBUKA MAISHA YA UTOTONI!!

Mmmmmhhh!! Mwenzenu nimeka hapa nikiwa na mawazo kibao ....maisha haya hakika nimekumbuka mno ...UGALI WA MUHOGO na samaki halafu ukiongezea na matembele au kisamvu....basi tu . Sasa leo kisa cha kukumbuka hili ni kwamba ninajiuliza nipike nini maana nilitaka kupika ugali lakini sasa UNGA sina na kama mnakumbuka nililima bustani na niliweka akiba sasa unga sina  nipo hoi hapa. Mboga ipo  ila sina unga. Basi mawazo yakaja na kukumbuka wakati nilipokuwa KADALA kama huyo binti kutwanga na kuchekecha na mwisho mtu unakuwa unga tu mwili mzima...JE KUNA ANAYEKUMBUKA KAMA KAPULYA HAPA?

BLOG YA MAISHA NA MAFANIKIO IMECHAGUA NGOMA HII IKIWA IMECHEZWA NA "ZAMBIA NGONI" IMENIKUMBUSHA LIZOMBE.....NGOMA YA ASILI


Msione kimya nipo  niseme tu nilikuwa nimebanwa  ila sasa nipo. Napenda kuwatakieni wote kila la kheri.Kapulya

Friday, November 8, 2013

SARESARE MAUA....IJUMAA NJEMA KWA WOTE

 Nimependa sana vazi hili
Kwa hiyo katika pita pita kwenye maduka nikaona hii blauzi(tunika) nikanunua ila  nimeipenda zaidi ya huyu dada hapo juu. Mimi nimenunu indiska, mpiga picha kaka Erik:-).NAWATAKIENI WOTE MWISHO MWEMA WA WIKI HII....IJUMAA IWE NJEMA KWA WOTE.

Wednesday, November 6, 2013

HUU NI UJUMBE WA JUMATANO YA LEO...tABASAMU/KICHEKO

 
Utamu wa maisha hutegemea hali ya nchi. Lakini Uzuri na kichekesho sio bima ya kufaulu katika maisha. Huu ni ujumbe wangu wa leo jumatano hii..Kila la kheri kwa wote mtakaopita hapa.

Monday, November 4, 2013

TUANZE JUMATATU HII KIHIVI :- KAPULYA SI MDADISI WA MASWALI TU BALI NA UTAMADANI WAKE PIA ANGALIA HAPA

Msifikiri anakusanya scalf na mawe tu kama mlivyoona hapa hapana anakusanya na vingine kama ,,,,,angalia hapa.....

 Hapa ni baadhi ya bangili za mdada huyu alizokusanya/nunua  napenda sana bangili na bado naendelea kukusanya....
 Hapo ni baadhi ya mikufu niliyonayo zawadi na nyingine ni kazi ya mikono ya wanangu
Na hapa ni baadhi ya heleni ambazi ni kazi ya mikono ya watu ambao wamebarikiwa kuwa na kipaji kama hiki.....TUDUMISHE UTAMADUNI WETU....JUMATATU NJEMA KWA WOTE

Saturday, November 2, 2013

JUMAMOSI YA LEO NA UJUMBE HUU...

Katika maisha vitu si muhimu.
NAWATAKIENI WOTE JUMAMOSI HII YA KWANZA YA MWEZI HUU IWR NJEMA..NA TUWAOMBEE MAREHEMU WOTE MAANA NI SIKUKUU YA MAREHEMU LEO.

Thursday, October 31, 2013

BLOG YA MAISHA NA MAFANIKIO IMEONA TUUFUNGE MWEZI HUU WA KUMI KWA UBUNIFU WA MCHEZO HUU!!!

Napenda kuwatakieni wote mwisho wa mwezi huu wa kumi. Naamini umekuwa mwezi mzuri kwa wengi na kwa wale walikuwa na majukumu kupita kiasi basi nawaombeeni mwezi uanzao kesho uwe mzuri. NAWATAKIENI WOTE MWENZI MPYA WA KUMI NA MOJA UWE MZURI NA WENYE AMANI NA FURAHA. MWAPENDWA WOTE....KAPULYA

Tuesday, October 29, 2013

NIMETAMANI SANA CHAKULA HIKI MIHOGO KWA SAMAKI

Nimetumiwa picha hii na mdogo wangu Sarah Mgaya sasa hivi ni mihogo na samaki ni chakula ambacho nimekula sana nawaza kusema ndicho kilichonikuza. Kama si hivyo basi ugali wa muhogo na samaki...nimetamani mno...ahsante

Monday, October 28, 2013

TUANZA JUMATATU HII NA ENZI HIZOOO JE MNAKUMBUKA???

Binafsi nimekumbuka sana maana ndo nilikuwa kadala/kachiki tu ...Muwe na jumatatu njema wote!!

Sunday, October 27, 2013

NAPENDA KUWATAKIENI DOMINIKA HII YA WATAKATIFU WOTE IWE NJEMA KWA WOTE...

 
Napenda kuwatakieni wote jumapili njema sana na Furaha na upendo zitawale ndani ya  mioyo na nyumba zenu. Ujumbe wa leo:NINAMPENDA  MUNGU NA   NDIO MAANA MOYO WANGU UNAMTUKUZA NA KUMSHANGILA UKISEMA: Ee Bwana na Mungu wangu, Uliye mwanzo na mwisho wangu, Kuanzia sasa najiweka mikononi mwako, unitumie kulingana na mapenzi yako. Kisha unifundishe njia ya kuipanda ngazi ya kufikia. AMINA....KAPULYA
 

Friday, October 25, 2013

IJUMAA YA LEO NA KAZI YA MIKONO YA KAPULYA...KUOKA MIKATE!!

Nimechoka kununua mikata, nikaamua kuoka mwenyewe leo. Halafu ni mitamu zaidi kwa kweli. Ni rahisi sana. Maji lita moja, unga wa ngano lita moja na nusu, chumvi kijiko cha mezani cha chakula, Sukari vijiko 2 vya mezani, mafuta ya kula kikombe kimoja kidogo cha chai(1dl) na hamira pkt moja (50g) au kama ya unga ni vijiko 2 vya chai. Unachanganya vyote na moja kwa moja unakanda unga mpaka unaona umekuwa laini. Unafunika na kitambaaa kizuri kwa dakika 30 ili uumuke. Baadaye unatengeneza utakavyo na kuumua tena dakika 30. Baada ya hapo unapaka maji au maziwa na kuingiza kwenye oven kwa dakika 8-10 na hapo mikate tayari. NAWATAKIENI IJUMAA PIA MWANZO MZURI WA MWISHO WA JUMA HILI. IJUMAA NJEMA!!!

Wednesday, October 23, 2013

JUMATANO YA LEO NIMEAMUA KUTEMBELEA IRINGA-ISMILA!!!

Ismila ni mojawapo wa vivutio vya utalii ambao upo ndani ya mkoa wa IRINGA yetu...karibuni wote kutembelea sehemu hii ya kumbukumbu. JUMATANO  NJEMA KWA WOTE.