Ni wiki nyingine na Jumatatu nyingine tena ya mwisho kwa mwizi huu wa nne! Nimeamka nikiwa na mawazo mawazo basi nikachukua kitabu hiki na kusoma. Kitabu chenyewe kinaitwa MAPENZI KUCHIPUA NA KUNYAUKA. Kilichoandikwa na Munga Tahenan... nikafananisha na wimbo ule wa Remmy Ongala usemao nilidhani nimepata kumbe nimepatikana.... bahati mbaya sijaupata wimbo wenyewe....Habari yenyewe inasomeka hivi:- Karibuni tujadili pamoja.
Ifuatayo ni habari ya mwanamke ambaye aliwahi kuja kwangu kwa ushauri kuhusu ndoa yake: Mama Kotilda Mkataha aliolewa mwaka 1980 na mume msomi aliyekuwa na wadhifa mkubwa kwenye taasisi moja ya fedha ya serikali.
Ndoa hii ilifungwa kwa sababu, Kotlida hakuwa na njia, lakini anasema, tangu wakiwa kwenye uchumba, alikuwa tayari na wasiwasi kama ndoa yao ingekuwa ni ya amani. Anasema, wakati bado wachumba, huyo bwana aliwahi kumpiga kibao kwenye kituo cha UDA kwa kosa la kuchelewa kufika kituoni kama walivyokuwa wamekubaliana.
Ndoa ilikuwa ni ya mateso makubwa hata kabla haijafungwa. Mwezi mmoja baada ya ndoa, Mume alimachisha mkewe kazi kwa kwenda kufanya fujo ofisini kwa bosi wake kwa madai kuwa bosi huyo alikuwa na uhusiano na mkewe. Kotlida alianza kuishi kwa mashrti. Hakuna kutoka, hata kwenda kwa jirani bila kuomba ruhusu na kutoa maelezo marefu kwa nini aende huko.
Kusimangwa, kukosolewa, kuitwa mjinga na mbumbumbu, ikaanza kuwa sehemu ya maisha ya mama huyu, Hali iliendelea hivi na Kotlida akawa anajiambia, kuna siku hali itabadilika. Lakini. kwa bahati mbaya, hali haikubadilika. Wakati anakuja kwangu, alikuwa ameshaanza kuamini kwamba, huenda ni kweli alikuwa anastahili kutendewa vile na mumewe.
Huku ndiko tunakoita kufujwa. Mpenzi mmoja anapomuumiza mwingine kwa kauli zake au limwili, mara kwa mara, tunasema hapo kuna kufujana.
Mpenzi mmoja anapokuwa na mamlaka aliyojipa dhidi ya uhuru na haki ya mwenzake, tunasema hapo imekuwa kufujana. Mara nyingi, wanaofuja ni wanaume. Miongoni mwa matatizo ya ndoa ambayo mtu hashauriwi kuendelea kuyavumulia ni kufujwa. Ndani ya kufujwa kuna maumivu makubwa ya hisia na mwili.
Ni vizuri hata hivyo, nikasema kwamba, neno kufuja ni jinsi ya kuelezea hali hii, ambapo mtu mwingine angeweza kuita matesa katika ndoa, kuonewa katika ndoa au kutumia istilahi yoyote.
Swali langu:- Kwanini alipoona mambo yanazidi hakuondoka?
Showing posts with label mateso. Show all posts
Showing posts with label mateso. Show all posts
Monday, April 28, 2014
Tuesday, August 25, 2009
MATESO YA MTOTO FILIMINA
Nimepata email kutoka kwa msomaji wa blog hii (ameomba nihifadhi jina lake) amenitumia taarifa ifuatayo ambayo imesikitisha sana, nami bila kusita kutokana na kuguswa na habari hiyo nimeona niiweke hapa kibarazani ili kuomba msaada kwa wadau walioko nyumbani Tanzania jijini Dar Es Salaam, wasaidie kumuokoa binti huyu. Naomba kuwasilisha.
Dada Yasinta,
Nimeshawishika kuwasiliana na wewe ili kujaribu kutafuta namna ya kumsaidia mtoto Fina ambaye ni yatima anayeishi katika mazingara ya mateso makubwa kupita kiasi.
Najua hunifahamu na wala sijawahi kuwasiliana na wewe hata siku moja lakini ningependa ufahamu kuwa mimi ni mmojawapo kati ya wasomaji wazuri wa blog yako.
Kwa kuwa nimeona kuwa blog yako inasomwa na wasomaji wengi nimeona nipitishie kilio cha binti huyu kupitia blog yako ili kutafuta namna ya kumsaidia.
Mimi naishi maeneo ya Tabata Kisukulu lakini ninaye girlfrind wangu anayeishi Tabata Kimanga jirani na mama huyo anayemtesa binti huyo yatima asiye na baba wala mama. Nimekuwa nikimtembelea Girlfrind wangu karibu kila siku na nimekuwa nikishuhudia mateso anayofanyiwa huyo binti
Nyumba anayoishi mama huyo iko Tabata Kimanga, unashuka kituo maarufu kiitwacho njia panda, mbele kidogo unafuata njia ya kushoto, utakuta gereji, ukiuliza kwa mama Enok au mama Frank maarufu kwa kuwauzia mafundi gereji maji ya baridi utampata.
Baada ya kuona mateso anayofanyiwa binti huyo, niliijaribu kuwauliza baadhi ya majirani na walikiri kuwa hilo ni jambo la kawaida, kwani binti amekuwa akipigwa kila siku takribani mara tatu kwa siku kwa makosa yasiyo na msingi kabisa.
Naamini wote tunafahamu malezi na namna ya kumuadhibu mtoto, lakini ikiwa mtoto anaadhibiwa hadi kuchomwa moto hiyo ni hatari, na tena kwa jinsi alivyo makini humchoma sehemu za mapajani ili isiwe rahisi kuonekana.
Nimefanya uchunguzi makini katika kipindi hiki cha mwishoni mwa juma na nimepata habari muhimu kadhaa ambazo mtu asipokuwa makini anaweza kudhani kuwa binti huyu haonewi. Huyu mama kwa kutaka kujenga mazingira ya kutoonekana kwamba anamtesa huyu binti, amekuwa akimsingizia mambo mengi kwa majirani na hata shuleni anaposoma ili ionekane kwamba ni mtoto jeuri, malaya na asiyesikia.
Ni mzuri kwa kutengeneza uongo na anaongea sana, ila naamini hata majirani watakuwa ni mashahidi wazuri katika kuthibitisha hili. Ni mateso makubwa sana anayopata binti huyu na hata kama ni mkosaji lakini adhabu anayopewa ni kubwa kuliko kawaida. Inaniuma sana na ninahisi si siku nyingi anaweza hata kumuua. naomba nikiri kwamba katika maisha yangu yote sijawahi kuona mateso ya namna hii, tena yanayofanywa na mwanamke ambaye na yeye anao watoto na anayejua uchungu wa kuzaa............ sasa nimejua ni nini maana ya roho mbaya tena mbaya zaidi naishuhudia kwa mwanamke.........
Nakuomba sana dada Yasinta uiweke habari hii katika blog yako ili jamii ya Watanzania na vyombo vinavyohusika vifahamu. Niliwasiliana na Chama Cha Waandishi Wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA), na waliahidi kufuatilia swala hili.
Ukweli ni kwamba dada kila nimuonapo binti huyu roho inaniuma sana na nimeshindwa kuvumilia unyama huu. Naamini labda mungu anayo makusudi yake, kwamba nilione hili ili nichukue hatua, na hatua yenyewe ndio hii ya wewe kunisaidia kumuokoa mtoto huyu. Jamani dhamira inanishitaki na naona kuna kitu kinanisukuma nimsaidie binti huyu kama binadamu mwenzangu....
Nimefanya uchunguzi wa kujua shule anayosoma na jina la mwalimu mkuu na namba yake ya simu, na nimepata taarifa zifuatazo:
Jina la Binti ni Filimina (Jina la baba yake sijalipata bado)na anasoma darasa la Tatu C
Jina la shule ni Tumaini Tabata Kimanga
Jina la mwalimu mkuu ni Mwalimu Mang’enya
Namba ya simu ya mwalimu mkuu ni +255 718 900190
Naomba ushirikiano wako,
Dada Yasinta,
Nimeshawishika kuwasiliana na wewe ili kujaribu kutafuta namna ya kumsaidia mtoto Fina ambaye ni yatima anayeishi katika mazingara ya mateso makubwa kupita kiasi.
Najua hunifahamu na wala sijawahi kuwasiliana na wewe hata siku moja lakini ningependa ufahamu kuwa mimi ni mmojawapo kati ya wasomaji wazuri wa blog yako.
Kwa kuwa nimeona kuwa blog yako inasomwa na wasomaji wengi nimeona nipitishie kilio cha binti huyu kupitia blog yako ili kutafuta namna ya kumsaidia.
Mimi naishi maeneo ya Tabata Kisukulu lakini ninaye girlfrind wangu anayeishi Tabata Kimanga jirani na mama huyo anayemtesa binti huyo yatima asiye na baba wala mama. Nimekuwa nikimtembelea Girlfrind wangu karibu kila siku na nimekuwa nikishuhudia mateso anayofanyiwa huyo binti
Nyumba anayoishi mama huyo iko Tabata Kimanga, unashuka kituo maarufu kiitwacho njia panda, mbele kidogo unafuata njia ya kushoto, utakuta gereji, ukiuliza kwa mama Enok au mama Frank maarufu kwa kuwauzia mafundi gereji maji ya baridi utampata.
Baada ya kuona mateso anayofanyiwa binti huyo, niliijaribu kuwauliza baadhi ya majirani na walikiri kuwa hilo ni jambo la kawaida, kwani binti amekuwa akipigwa kila siku takribani mara tatu kwa siku kwa makosa yasiyo na msingi kabisa.
Naamini wote tunafahamu malezi na namna ya kumuadhibu mtoto, lakini ikiwa mtoto anaadhibiwa hadi kuchomwa moto hiyo ni hatari, na tena kwa jinsi alivyo makini humchoma sehemu za mapajani ili isiwe rahisi kuonekana.
Nimefanya uchunguzi makini katika kipindi hiki cha mwishoni mwa juma na nimepata habari muhimu kadhaa ambazo mtu asipokuwa makini anaweza kudhani kuwa binti huyu haonewi. Huyu mama kwa kutaka kujenga mazingira ya kutoonekana kwamba anamtesa huyu binti, amekuwa akimsingizia mambo mengi kwa majirani na hata shuleni anaposoma ili ionekane kwamba ni mtoto jeuri, malaya na asiyesikia.
Ni mzuri kwa kutengeneza uongo na anaongea sana, ila naamini hata majirani watakuwa ni mashahidi wazuri katika kuthibitisha hili. Ni mateso makubwa sana anayopata binti huyu na hata kama ni mkosaji lakini adhabu anayopewa ni kubwa kuliko kawaida. Inaniuma sana na ninahisi si siku nyingi anaweza hata kumuua. naomba nikiri kwamba katika maisha yangu yote sijawahi kuona mateso ya namna hii, tena yanayofanywa na mwanamke ambaye na yeye anao watoto na anayejua uchungu wa kuzaa............ sasa nimejua ni nini maana ya roho mbaya tena mbaya zaidi naishuhudia kwa mwanamke.........
Nakuomba sana dada Yasinta uiweke habari hii katika blog yako ili jamii ya Watanzania na vyombo vinavyohusika vifahamu. Niliwasiliana na Chama Cha Waandishi Wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA), na waliahidi kufuatilia swala hili.
Ukweli ni kwamba dada kila nimuonapo binti huyu roho inaniuma sana na nimeshindwa kuvumilia unyama huu. Naamini labda mungu anayo makusudi yake, kwamba nilione hili ili nichukue hatua, na hatua yenyewe ndio hii ya wewe kunisaidia kumuokoa mtoto huyu. Jamani dhamira inanishitaki na naona kuna kitu kinanisukuma nimsaidie binti huyu kama binadamu mwenzangu....
Nimefanya uchunguzi wa kujua shule anayosoma na jina la mwalimu mkuu na namba yake ya simu, na nimepata taarifa zifuatazo:
Jina la Binti ni Filimina (Jina la baba yake sijalipata bado)na anasoma darasa la Tatu C
Jina la shule ni Tumaini Tabata Kimanga
Jina la mwalimu mkuu ni Mwalimu Mang’enya
Namba ya simu ya mwalimu mkuu ni +255 718 900190
Naomba ushirikiano wako,
Wednesday, July 22, 2009
MAISHA HAYA JAMANI!!!!!!
Alikuwa ni Binti wa nne kuzaliwa hapo mnamo mwaka 1967 kati ya watoto nane katika familia hiyo, akiwa ametanguliwa na kaka zake watatu. Alipofikisha umri wa kwenda shule hapo mnamo mwaka 1974 alipelekwa kusoma shule iliyopo kijiji cha jirani takribani kilomita 4 akiwaacha kaka zake wakisoma shule iliyoko umbali wa mita 200 kutoka nyumbani.
Inasemekana kuwa eti aliandikishwa kusoma katika shule hiyo ya jirani lakini kutokana na shule hiyo kupokea wanafunzi wengi kupita kiasi ndipo walipogawanywa na wengine kupelekwa kijiji cha jirani ambapo kulikuwa na nafasi.
Kulikuwa uwezekano mkubwa wa baba yake kufanya mipango ya kuhakikisha kuwa mwanae huyo hasomi mbali na nyumbani lakini hazikufanyika juhudi zozote kufanikisha jambo hilo na badala yake aliachwa na hivyo aliendelea kusoma katika shule hiyo.
Alilazimika kuamka majira ya saa kumi alfajiri kila siku akiwa na wanafunzi wenzie walitembea kilomita hizo nne kwenda na kurudi na huku wakipigwa na baridi kali na wakati mwingine kunyeshewa na mvua, lakini alivumilia na baada ya miaka saba alimaliza darasa la saba mwaka 1980.Baada ya kumaliza masomo kama ilivyokuwa kwa kaka zake hakubahatika kuendelea na masomo ya sekondari, ingawa baba yake alikuwa na uwezo wa kuwaendeleza na masomo wanae lakini hakuona umuhimu wa kufanya hivyo ingawa yeye alisoma mpaka darasa la nane la mkoloni na kuajiriwa serikalini kama karani katika chama cha ushirika wilayani.
Mnamo mwaka 1981 kaka yake binamu ambaye alilelewa na wazazi wake na ambaye alikuwa ni dereva alimchukua na kumpeleka Moshi kwa madai kwamba amemtafutia chuo cha kujifunza mambo ya Typing.
Alipofika huko alifikia kwa mama mmoja wa kisomali ambaye alikuwa na familia ya watoto nane, watano wa kike na wakiume watatu. Cha kushangaza alijikuta akiamshwa asubuhi na mapema na mama huyo na kukabidhiwa furushi la nguo akafue. Binti wa watu akatahamaki, kulikoni apewe kazi ya kufua wakati alikuwa ameahidiwa kusomeshwa mambo ya Typing? Yule mama kama vile alikuwa akisoma mawazo yake akamwambia kuwa yeye pale ni House Girl, na akapewa ratiba ya siku nzima. Alikuwa akiamka alfajiri saa kumi na kuanza usafi wa nyumba akimaliza apike chai ya watu wote kisha achukue nguo za familia nzima kuzifua, akimaliza anaosha vyombo vilivyotumika kwa chai ya asubuhi, kisha anaenda sokoni na kadhalika na kadhalika ilimradi ilikuwa ni kazi mtindo mmoja.
Alikuwa akitukananwa na kudhalilishwa kama vile hakuwa na wazazi, lakini alivumilai kwa kuwa hakuwa na pa kwenda.
Hakuwahi kumuona yule kaka yake binamu kuja kumjulia hali wala nini alijikuta akiwa ametelekezwa ugenini asijue kwa kukimbilia.
Baada ya miezi mitatu ya mateso bila malipo ndipo siku moja akakutana na mjomba wake ambaye alikuwa ni mfayabiashara maeneo ya sokoni, walisalimiana lakini mjomba wake alimshangaa kutokana na kumuona akiwa amekonda sana, alimuuliza sababu ya kukonda kiasi kile na alitaka kujua anaishi pale Moshi na nani?
Yule binti alisimulia mateso anayoyapata na kutokana jinsi alivyokuwa amekonda mjomba wake hakuvumilia alilia sana na pale pale alikata tiketi ya basi na kusafiria naye hadi kijijini kwao ambapo alimlaumu sana dada yake kwa kitendo chake cha kumtoa mwanae na kumpeleka kufanya kazi za ndani na kuteseka kiasi kile, mama wa yule binti alishangaa sana kwani yule binamu yake aliyemchukua alikuwa kila akipita pale kijjini na gari alikuwa anatoa salamu kutoka kwa huyo binti kuwa ni mzima na anaendelea na masomo vizuri.
Mama wa binti yule alilia sana kwa uchungu, ingawa baba wa binti hakuonekana kujali sana, kwani wakikutana na huyo binamu aliyemchukua huyo binti hununuliwa pombe kwa hiyo hakuonekana kujali wala kumlaumu binamu kwa kitendo chake cha kikatili.
Binamu alipofika moshi aliambiwa kuwa binti ametotoka na ameiba nguo na pesa kiasi cha shilingi elfu ishirini, miaka hiyo ya themanini elfu ishirini ilikuwa ni kiasi kikubwa cha pesa, kumbe ilikuwa ni uongo kwani binti alikuwa ametumwa sokoni na alipewa shilingi hamsini za kununua mahitaji fedha ambazo hata hivyo alizisalimisha kwa mama yake mara alipofika tu.
Siku iliyofuata binamu alifika na kudai kuwa binti ni mwizi na kamfedhehesha sana, mama wa binti alimkata kalima, na kumuuliza sababu ya kumpeleka binti yake kuwa mtumishi wa ndani wakati alimuahidi kuwa atamsomesha Typing?Alimkabidhi ile shilingi hamsini na kumuambia aipeleke kwa msomali wake.
Kumbe huo ndio ulikuwa mwanzo wa mateso ya binti huyu.
Mwishoni mwa 1981 alichukuliwa na mama yake mdogo waliyechangia baba na mama yake na kupelekwa Dar kwa ahadi ya kusomeshwa, alipofika jiji Dar alijikuta akiwa ni muhudumu wa kuku wa mayai, kwani huyo mama yake mdogo alikuwa ni mfugaji wa kuku.
Mnamo August 16,1982, binti huyu alipata pigo la mwaka baada ya kupata taarifa za kufariki kwa mama yake ghafla kwa ugonjwa wa moyo.Ilimlazimu kurudi kijijini haraka ili kuhudhuria mazishi ya mama yake, ingawa hata hivyo alichelewa.
Baada ya mazishi Binti yule alimueleza baba yake kuwa alipokuwa Dar hakuwa akisoma kama alivyoahidiwa, safari hii tena akachukuliwa na mama yake mdogo tumbo moja na mama yake na kupelekwa Arusha alipokuwa akiishi huyo mama yake mdogo ili akasomee hayo mambo ya Typing, na alipofika kule kweli alijiunga na chuo cha kusomea typing, lakini mama yake mdogo alikuwa ni mkorofi kweli kwani ilikuwa kila akichelewa kidogo tu alikuwa akipigwa sana kwa madai kwamba alikuwa kwa wanaume, na pia alikuwa akitumikishwa kufanya kazi za hapo nyumbani kupita kiasi.Yule mama alikuwa na mradi wake wa mambo ya ususi, wakati huo kulikuwa hakuna mambo ya saloon. Kwa hiyo akimaliza kazi za nyumbani alikuwa anamsaidia mama yake huyo kazi zake za ususi.
Mateso yalipozidi ilibidi atoroke na na kurudi kijijini. Baada ya kutoonekana kwa siku mbili mama yake mdogo alisafiri hadi kijijini na kumkuta binti akiwa nyumbani kwao ametulia.
Baada ya mashauriano ikaamuliwa binti abaki pale kijijini.Miezi kadhaa baadae binti akapata mchumba, akalipiwa na mahari, haikuchukua muda hata kabla ya kufunga ndoa binti akapata ujauzito, na hivyo ndoa ikaahirishwa mpaka baadae atakapojifungua.
Baada ya miezi tisa binti alijifungua mtoto wa kiume, jambo ambalo lilifurahiwa na pande zote mbili. Hata hivyo swala la kufungwa kwa ndoa likawa linapigwa danadana hatimaye kijana muoaji akatoa taarifa kuwa haoi tena.Kisa, yalipenyezwa maneno ya fitna na baadhi ya ndugu ili kuvunja ule uchumba, mpaka leo sababu haijulikani.
Mnamo mwaka 1985 binti akalazimika kwenda Dar kwa kaka yake mkubwa ambaye alikuwa ni mtumishi serikalini ili kutafutiwa shughuli ya kufanya.Alipofika akatafutiwa kazi na kaka yake na hivyo kumudu kujitegemea kwa muda mfupi.
Mnamo mwaka 1990 akapata mchumba mwenyeji wa Singida ambaye alikuwa ameachana na mkewe na hivyo kuanza maisha mapya akiwa na mumewe huyo bila ya kufunga ndoa.Maisha hayakuwa mazuri sana kwani bwana huyo alikuwa na wivu sana, kwani alikuwa hataki kumuona akiongea na mwanaume yeyote, na ikitokea amemkuta na mwanaume ni lazima kutatokea ugomvi mkubwa ajabu.
Maisha na bwana yule hayakuwa mazuri sana, kwani kila siku hali ilizidi kuwa mbaya na kibaya zaidi ni pale yule bwana alipoachishwa kazi. Ilibidi binti aanzishe biashara ili kumudu kujikimu, lakini bwana yule wivu ulimzidi, kila akiongea na mteja ni bwana ake.
Binti yakamshinda, mnamo mwaka 1993 mwishoni akaondoka na kurudi kwa kaka yake akiacha vitu vyake vyote kwa yule bwana, kwani yule bwana ndiye aliyehamia kwa binti lakini alizuia vitu vyote kwa madai kuwa ni vya kwake.
Baadae binti akjikuta ni mjamzito, lakini hakutaka kumwambia yule bwana ingawa alikuwa na uhakika kuwa ule ujauzito ni wa yule bwana.Mwanzoni mwa mwaka 1994 binti aliamua kurudi kijijini kwao, wakati huo ujauzito wake ulikuwa na miezi mitano.
Ujauzito ulipofikisha miezi sita binti yule alipotea akawa hajulikani alipo. Ndugu zake walifanya juhudi kumtafuta bila mafanikio, lakini baada ya siku mbili alirudi mwenyewe akiwa amechoka sana, lakini alikuwa kama amechanganyikiwa, alipopelekwa hospitalini hakuonekana kuwa na ugonjwa wowote na mapigo ya moyo ya kiumbe kilichokuwa tumboni yalikuwa yanaenda vizuri.
Ilibidi awekwe chini ya uangalizi wa bibi yake mzaa mama kwani ilihofiwa kuwa angetoroka tena na kupotelea porini.Mwezi mmoja baadae, ujauzito ulipokuwa na miezi saba, binti yule alipata kifafa cha Mimba na hatimaye roho yake ikaachana na mwili, ilikuwa ni May 12, 1994.
Huo ndio ukawa ni mwisho wa binti huyu.
Simulizi hii ni Dedication kwa binti huyu ambaye ni dada wa rafiki yangu.
Inasemekana kuwa eti aliandikishwa kusoma katika shule hiyo ya jirani lakini kutokana na shule hiyo kupokea wanafunzi wengi kupita kiasi ndipo walipogawanywa na wengine kupelekwa kijiji cha jirani ambapo kulikuwa na nafasi.
Kulikuwa uwezekano mkubwa wa baba yake kufanya mipango ya kuhakikisha kuwa mwanae huyo hasomi mbali na nyumbani lakini hazikufanyika juhudi zozote kufanikisha jambo hilo na badala yake aliachwa na hivyo aliendelea kusoma katika shule hiyo.
Alilazimika kuamka majira ya saa kumi alfajiri kila siku akiwa na wanafunzi wenzie walitembea kilomita hizo nne kwenda na kurudi na huku wakipigwa na baridi kali na wakati mwingine kunyeshewa na mvua, lakini alivumilia na baada ya miaka saba alimaliza darasa la saba mwaka 1980.Baada ya kumaliza masomo kama ilivyokuwa kwa kaka zake hakubahatika kuendelea na masomo ya sekondari, ingawa baba yake alikuwa na uwezo wa kuwaendeleza na masomo wanae lakini hakuona umuhimu wa kufanya hivyo ingawa yeye alisoma mpaka darasa la nane la mkoloni na kuajiriwa serikalini kama karani katika chama cha ushirika wilayani.
Mnamo mwaka 1981 kaka yake binamu ambaye alilelewa na wazazi wake na ambaye alikuwa ni dereva alimchukua na kumpeleka Moshi kwa madai kwamba amemtafutia chuo cha kujifunza mambo ya Typing.
Alipofika huko alifikia kwa mama mmoja wa kisomali ambaye alikuwa na familia ya watoto nane, watano wa kike na wakiume watatu. Cha kushangaza alijikuta akiamshwa asubuhi na mapema na mama huyo na kukabidhiwa furushi la nguo akafue. Binti wa watu akatahamaki, kulikoni apewe kazi ya kufua wakati alikuwa ameahidiwa kusomeshwa mambo ya Typing? Yule mama kama vile alikuwa akisoma mawazo yake akamwambia kuwa yeye pale ni House Girl, na akapewa ratiba ya siku nzima. Alikuwa akiamka alfajiri saa kumi na kuanza usafi wa nyumba akimaliza apike chai ya watu wote kisha achukue nguo za familia nzima kuzifua, akimaliza anaosha vyombo vilivyotumika kwa chai ya asubuhi, kisha anaenda sokoni na kadhalika na kadhalika ilimradi ilikuwa ni kazi mtindo mmoja.
Alikuwa akitukananwa na kudhalilishwa kama vile hakuwa na wazazi, lakini alivumilai kwa kuwa hakuwa na pa kwenda.
Hakuwahi kumuona yule kaka yake binamu kuja kumjulia hali wala nini alijikuta akiwa ametelekezwa ugenini asijue kwa kukimbilia.
Baada ya miezi mitatu ya mateso bila malipo ndipo siku moja akakutana na mjomba wake ambaye alikuwa ni mfayabiashara maeneo ya sokoni, walisalimiana lakini mjomba wake alimshangaa kutokana na kumuona akiwa amekonda sana, alimuuliza sababu ya kukonda kiasi kile na alitaka kujua anaishi pale Moshi na nani?
Yule binti alisimulia mateso anayoyapata na kutokana jinsi alivyokuwa amekonda mjomba wake hakuvumilia alilia sana na pale pale alikata tiketi ya basi na kusafiria naye hadi kijijini kwao ambapo alimlaumu sana dada yake kwa kitendo chake cha kumtoa mwanae na kumpeleka kufanya kazi za ndani na kuteseka kiasi kile, mama wa yule binti alishangaa sana kwani yule binamu yake aliyemchukua alikuwa kila akipita pale kijjini na gari alikuwa anatoa salamu kutoka kwa huyo binti kuwa ni mzima na anaendelea na masomo vizuri.
Mama wa binti yule alilia sana kwa uchungu, ingawa baba wa binti hakuonekana kujali sana, kwani wakikutana na huyo binamu aliyemchukua huyo binti hununuliwa pombe kwa hiyo hakuonekana kujali wala kumlaumu binamu kwa kitendo chake cha kikatili.
Binamu alipofika moshi aliambiwa kuwa binti ametotoka na ameiba nguo na pesa kiasi cha shilingi elfu ishirini, miaka hiyo ya themanini elfu ishirini ilikuwa ni kiasi kikubwa cha pesa, kumbe ilikuwa ni uongo kwani binti alikuwa ametumwa sokoni na alipewa shilingi hamsini za kununua mahitaji fedha ambazo hata hivyo alizisalimisha kwa mama yake mara alipofika tu.
Siku iliyofuata binamu alifika na kudai kuwa binti ni mwizi na kamfedhehesha sana, mama wa binti alimkata kalima, na kumuuliza sababu ya kumpeleka binti yake kuwa mtumishi wa ndani wakati alimuahidi kuwa atamsomesha Typing?Alimkabidhi ile shilingi hamsini na kumuambia aipeleke kwa msomali wake.
Kumbe huo ndio ulikuwa mwanzo wa mateso ya binti huyu.
Mwishoni mwa 1981 alichukuliwa na mama yake mdogo waliyechangia baba na mama yake na kupelekwa Dar kwa ahadi ya kusomeshwa, alipofika jiji Dar alijikuta akiwa ni muhudumu wa kuku wa mayai, kwani huyo mama yake mdogo alikuwa ni mfugaji wa kuku.
Mnamo August 16,1982, binti huyu alipata pigo la mwaka baada ya kupata taarifa za kufariki kwa mama yake ghafla kwa ugonjwa wa moyo.Ilimlazimu kurudi kijijini haraka ili kuhudhuria mazishi ya mama yake, ingawa hata hivyo alichelewa.
Baada ya mazishi Binti yule alimueleza baba yake kuwa alipokuwa Dar hakuwa akisoma kama alivyoahidiwa, safari hii tena akachukuliwa na mama yake mdogo tumbo moja na mama yake na kupelekwa Arusha alipokuwa akiishi huyo mama yake mdogo ili akasomee hayo mambo ya Typing, na alipofika kule kweli alijiunga na chuo cha kusomea typing, lakini mama yake mdogo alikuwa ni mkorofi kweli kwani ilikuwa kila akichelewa kidogo tu alikuwa akipigwa sana kwa madai kwamba alikuwa kwa wanaume, na pia alikuwa akitumikishwa kufanya kazi za hapo nyumbani kupita kiasi.Yule mama alikuwa na mradi wake wa mambo ya ususi, wakati huo kulikuwa hakuna mambo ya saloon. Kwa hiyo akimaliza kazi za nyumbani alikuwa anamsaidia mama yake huyo kazi zake za ususi.
Mateso yalipozidi ilibidi atoroke na na kurudi kijijini. Baada ya kutoonekana kwa siku mbili mama yake mdogo alisafiri hadi kijijini na kumkuta binti akiwa nyumbani kwao ametulia.
Baada ya mashauriano ikaamuliwa binti abaki pale kijijini.Miezi kadhaa baadae binti akapata mchumba, akalipiwa na mahari, haikuchukua muda hata kabla ya kufunga ndoa binti akapata ujauzito, na hivyo ndoa ikaahirishwa mpaka baadae atakapojifungua.
Baada ya miezi tisa binti alijifungua mtoto wa kiume, jambo ambalo lilifurahiwa na pande zote mbili. Hata hivyo swala la kufungwa kwa ndoa likawa linapigwa danadana hatimaye kijana muoaji akatoa taarifa kuwa haoi tena.Kisa, yalipenyezwa maneno ya fitna na baadhi ya ndugu ili kuvunja ule uchumba, mpaka leo sababu haijulikani.
Mnamo mwaka 1985 binti akalazimika kwenda Dar kwa kaka yake mkubwa ambaye alikuwa ni mtumishi serikalini ili kutafutiwa shughuli ya kufanya.Alipofika akatafutiwa kazi na kaka yake na hivyo kumudu kujitegemea kwa muda mfupi.
Mnamo mwaka 1990 akapata mchumba mwenyeji wa Singida ambaye alikuwa ameachana na mkewe na hivyo kuanza maisha mapya akiwa na mumewe huyo bila ya kufunga ndoa.Maisha hayakuwa mazuri sana kwani bwana huyo alikuwa na wivu sana, kwani alikuwa hataki kumuona akiongea na mwanaume yeyote, na ikitokea amemkuta na mwanaume ni lazima kutatokea ugomvi mkubwa ajabu.
Maisha na bwana yule hayakuwa mazuri sana, kwani kila siku hali ilizidi kuwa mbaya na kibaya zaidi ni pale yule bwana alipoachishwa kazi. Ilibidi binti aanzishe biashara ili kumudu kujikimu, lakini bwana yule wivu ulimzidi, kila akiongea na mteja ni bwana ake.
Binti yakamshinda, mnamo mwaka 1993 mwishoni akaondoka na kurudi kwa kaka yake akiacha vitu vyake vyote kwa yule bwana, kwani yule bwana ndiye aliyehamia kwa binti lakini alizuia vitu vyote kwa madai kuwa ni vya kwake.
Baadae binti akjikuta ni mjamzito, lakini hakutaka kumwambia yule bwana ingawa alikuwa na uhakika kuwa ule ujauzito ni wa yule bwana.Mwanzoni mwa mwaka 1994 binti aliamua kurudi kijijini kwao, wakati huo ujauzito wake ulikuwa na miezi mitano.
Ujauzito ulipofikisha miezi sita binti yule alipotea akawa hajulikani alipo. Ndugu zake walifanya juhudi kumtafuta bila mafanikio, lakini baada ya siku mbili alirudi mwenyewe akiwa amechoka sana, lakini alikuwa kama amechanganyikiwa, alipopelekwa hospitalini hakuonekana kuwa na ugonjwa wowote na mapigo ya moyo ya kiumbe kilichokuwa tumboni yalikuwa yanaenda vizuri.
Ilibidi awekwe chini ya uangalizi wa bibi yake mzaa mama kwani ilihofiwa kuwa angetoroka tena na kupotelea porini.Mwezi mmoja baadae, ujauzito ulipokuwa na miezi saba, binti yule alipata kifafa cha Mimba na hatimaye roho yake ikaachana na mwili, ilikuwa ni May 12, 1994.
Huo ndio ukawa ni mwisho wa binti huyu.
Simulizi hii ni Dedication kwa binti huyu ambaye ni dada wa rafiki yangu.
Subscribe to:
Posts (Atom)