Showing posts with label jamii. Show all posts
Showing posts with label jamii. Show all posts

Tuesday, October 24, 2017

HAPA SIJUI MWALIMU YUPI NI BORA:-)

Anayeingia na bia/Kilimanjaro darasani au....
....anayeingia darasani  na silaha ?

Tuesday, July 4, 2017

HAPA VIPI TENA?

Sasa hapa imekaaje tena? wasomaji tusaidiane hapa. Duh kaaazi kwelikweli hapa.

Tuesday, March 28, 2017

JE? UNGEKUWA WEWE UNGEFANYA NINI?

Pale unapotuma pesa nyumbani kwenu  zaidi ya miaka mitano urekebishiwe nyumba yako. Halafu siku ya kurudi unakuta hali kama hii. Je? hapo unafanyaje?
Ndiyo;- Niliwahi kusimuliwa kisa kama hiki na rafiki mmoja yalimpata kama haya. Uaminifu umepotea siku hizi .

Saturday, April 23, 2016

AFRIKA- KUMEKUCHA.....


NAWATAKIENI MWISHO MWEMA WA JUMA.... PAMOJA TUTAFIKA......KAPULYA

Friday, February 5, 2016

CHAGUA LA BLOG YA MAISHA NA MAFANIKIO KUWA HII NI PICHA YA WIKI...

Ama kweli  haya ndio maisha yetu wengi wetu...tutafika kweli? Najiuliza  itabidi ninunue gari mpya kila kukicha kwa mtindo huu...kaaaazi kwelikweliii!  mizigo michache ndio msingo harakahara haina baraka !

Friday, January 15, 2016

Thursday, September 3, 2015

SWALI NILILOULIZWA NA MSOMAJI /MFUATILIAJI WA MAISHA NA MAFANIKIO:-

Swali lenyewe lipo hivi:- Hivi ni  kitu gani akina mama/wanawake kinawafanya wampende mtoto fulani zaidi kati ya watoto wao wa kawazaa?
Akaendelea:- Utamkuta mama ana watoto wanne, lakini anampenda mmoja zaidi ya wengine? Hii inakuwaje kwa upande wako? akanipa hili swali mimi......akaendelea nakuuliza kwa kuwa nadhani una watoto.....halafu akaendelea kusema ....Pia nadhani utakuwa umeshawahi kuisikia hii au inatokea.
Jibu langu lilikuwa kama ifuatavyo:- Binafsi kama mama nawapenda wanangu sawasawa na sijawahi kufikiria  KUWAPENDA  TOFAUTI.
Baadaye nikakumbuka kwanini niwashirikishe ninyi wasomaji/ ndugu zangu. Maana naamini palipo na wengi pana mengi
Hata hivo nami nikajiwa na swali:- Je?  Hiki kitu kipo? na kama kipo kwa akina mama/wanawake tu?  na sio akina baba/wanaume? Maana nao pia ni wazazi. NAOMBA TUJADILI KWA PAMOJA......Kapulya wenu!

Wednesday, September 2, 2015

UJUMBE WA WIKI HII KUTOKA KWA KAPULYA!

Msione nipo kimya nipo sema tu mambo ya afya hayapo sawa sanma na majukumu ni mengi basi kila kitu kimejichanganya...Ila tupo Pamoja.....Kapulya.

Friday, July 18, 2014

UJUMBE WA LEO !!!

Ni kwamba katika maisha ipo hivi: Pale unapowafurahisha  wengine, ndipo furaha yako inazidi kuongezeka. Kwa hiyo pale upatapo nafasi jaribu kumfurahisha labda rafiki, au wale walio karibu nawe.
PAMOJA DAIMA!!!

Thursday, October 31, 2013

BLOG YA MAISHA NA MAFANIKIO IMEONA TUUFUNGE MWEZI HUU WA KUMI KWA UBUNIFU WA MCHEZO HUU!!!

Napenda kuwatakieni wote mwisho wa mwezi huu wa kumi. Naamini umekuwa mwezi mzuri kwa wengi na kwa wale walikuwa na majukumu kupita kiasi basi nawaombeeni mwezi uanzao kesho uwe mzuri. NAWATAKIENI WOTE MWENZI MPYA WA KUMI NA MOJA UWE MZURI NA WENYE AMANI NA FURAHA. MWAPENDWA WOTE....KAPULYA

Monday, September 23, 2013

SIMTAKI......UAMUZI MZITO!!!

Leo nimeamaka nikiwa nikiwaza habari ambayo niliwahi kusoma.....Ilikuwa saa 11 jioni. Msichana mmoja kwa jina la Veronika alikuwa akitoka shuleni kwake. Alikuwa kidato cha nne. Alikuwa anaelekea kwenye shule ya Sekondari ya wavulana. Ilimbidi amwone Robert, rafiki yake wa kiume. Veronika alikuwa akifikiri moyoni: "Sina budi kumwona Robert leo. Siwezi kusubiri tena"

Wakati huo huo huo wavulani walikuwa wakitoka shuleni pia. Punde si punde alimwona Robert akitoka katika kikundi cha wavulana wengine akimji. Alikuwa akitabasamu lakini Veronika aliweza kuona kwamba Robert alikuwa na mshangao pia kumwona yeye pale. Kwa kawaida walikuwa wanakutana kwenye stendi ya basi. Na maongezi yaliendelea hivi:-

ROBERT: Habari za jioni  Veronika? Nina furahi kukuona .

VERONIKA: Sijambo, Robert ....ah.....Ninataka kuzungumza nawe. Je? kuna mahali pa faragha shuleni kwako- mahali ambapo tunaweza kukaaa na kuzungumza bila mtu kutubugudha?

Robert alimtazama kwa fadhaa kidogo lakini hakumuuliza zaidi.

ROBERT: Ndiyo, nadhani tunaweza kwenda kule maktaba. Leo ni ijumaa na ni mwanzo wa pumziko la wiki, hatuna masomo. Nina hakika hapatakuwa na mtu.

Veronika alimfuata bila kusema kitu. Waliketi mwishoni kabisa mwa chumba cha maktaba wakimpa kisogo mfanya kazi wa makataba ambaye alikuwa akishughulika na kadi za vitabu.

ROBERT: Kuna matatizo gani Veronika? Mbona unaonekana kuwa na wasiwasi na huzuni?

Veronika alimtazama Robert, halafu aliinamisha kichwa .

ROBERT: Veronika kuna nini? huna budi kuniambia unajua mimi ni rafiki yako. Unahofu nini? labda umeshindwa mrihani wako wa katikati ya muhula?
Veronika: Hapana Robert. Ni kitu kikubwa kuliko hicho.... Ni ...nina mimba.

ROBERT: Nini? Una uhakika?
Robert alishikwa na bumbuwazi. Mawazo mengi yalipita ghafla akilini mwake.

VERONIKA:  Ndiyo, nina hakika. Lakini simtaki. Robert, simtaki mtoto huyu. Wazazi wangu wakisikia juu ya jambo hili hawatanipokea tena nyumbani kwetu. Pia itakuwa ni mwisho wa masomo yangu. Unajua, mwaka kesho ningeanza masomo ya uuguzi.

ROBERT: Najua.....Utafanya nini sasa? Ninaona njia moja tu: Ondelea mbali "kitu" hicho.

Veronika alifikiri:"kitu" hicho ni mtoto. Moyo wake ulikuwa unamwambia kuwa alichokuwa anapanga sasa ni jambo  baya sana. Lakini Veronika hakustahimili ile aibu wala wajibu wa tendo lake. Sasa alikuwa amekata shauri.

VERONIKA: Ninajua nitafanya nini. Nitakwenda kwa rafiki yangu Sarah. Yeye ni muuguzi kule hospitalini. Nitamwomba anipatie dawa ya kuondoa mimba, nina hakika atanisaidia. Hakuna mtu mwingine atakayejua. Hapo maisha yataendelea tena kama mwanzo.
Maneno haya ya mwisho Veronika aliyasema kwa sauti ya kunongóneza. Robert alikuwa ameshika kichwa chake kwa mikono yake miwili naye hakuthubutu kumtazama Veronika. Yeye pia alitambua kuwa anahusika lakini alifikiri: "Kwa kweli, hakuna njia nyingine, au sivyo? Hakujua. Lakini Veronika alikuwa amekwisha amua tayari. Basi, alimuuliza tu....

ROBERT: Utakwenda kumwona rafiki yako lini?

VERONIKA: Kesho......

Inasikitisha kweli kuona jinsi hali hii inavyorudiwa rudiwa mara nyingi siku hizi. Katika namna zoto za maisha kutoa mimba kumekuwa ni jambo la kawaida, jambo linalotokea mara kwa mara. Magazetini huandika kinaganaga jinsi watoto wanavyookotwa kwenye mapipa ya takataka, katika vyoo vya uma, n.k. Kutoa mimba kunaonekana kama njia ya kuondoa kitu kisichotakiwa ; njia ya kusahau kitu ambacho kisingelikuwa kimetokea.....ITAENDELEA......Habari hii nimeipata katika kitabu cha NJIA YETU KWA MAPENDO NA NDOA...



Tuesday, September 17, 2013

UJUMBE /SWALI WA/LA LEO!!!

Kama huwezi kujisamehe mwenyewe na uliyoyafanya, utawezaje kuwasamehe wengine?
NAWATAKIENI WOTE JUMANNE NJEMA SANA NA KUMBUKENI TUPO PAMOJA DAIMA!!!Kapulya!

Thursday, August 15, 2013

NAOMBA TAFSIRI YA NENO KIONGOZI/VIONGOZI...MAANA LINANIKERA MNO.......!!!

Nimeamka leo nikiwaza hili neno KIONGOZI/VIONGOZI nikashindwa kuliwazua nikaamua kuchukua KAMUSI  SANIFU YA KISWAHILI CHETU. Nayo ikaniambia hivi:-KIONGOZI/VIONGOZI.....
1. mtangulizi wa jambo fulani au wa kikundi cha watu, mkubwa anayesimamaia shughuli maalumu kwa kueleza au kuelekeza. AU...
2. Kitu kinachosaidia kuonyesha au kuelekeza......
Je? hawa viongozi wanaongoza kweli au wanajiongoza? Naomba tutafakari au jadili kwa pamoja.
Ndimi Kapulya wenu:-)

Tuesday, July 16, 2013

JUMANNE YA LEO TUANGALIE KATON HII...EBU SOMA MWENYEWE.....

USHOGA NI HATARI
Leo na katuni hii tuache umbea jamani hakikisha kwanza hilo jambo ndo ufanye tuacha tabia ya kugombanisha ndoa za watu. Nawatakieni wote mtakaopita hapa JUMANNE NJEMA SANA. NA KUMBUKENI WOTE MNAPENDWA.

Monday, July 1, 2013

TUANZA MWEZI HUU MPYA NA JUMATATU HII NA SWALI HILI:-TABIA YA KUWAACHIA WAZAZI WATOTO MPAKA LINI?

BIBI NA WAJUKUU WAKE

Mara nyingi nimekuwa nikijiuliza kuhusu hii tabia ambayo, bado inazidi kukua tu katika jamii zetu. Hasa inapokuja kwa sisi wadada/wanawake. Hii tabia ya kuwaacha watoto kwa wazazi, hivi hii haijalishi ya kwamba wazazi wamekwisha fanya kazi yao yaani kuku/kututunza sisi na sasa ni wewe/sisi inabidi pale inapowezekana tuwatunze wao?
Utakuta wazazi wanawatunza wajukuu na hapo hapo wanakuwa na majukumu mengine na ulemuda wa kupumzika unakuwa haupo. Halafu utakuta wanaweke wengine wameolewa, na kabla yake amezaa na yule/hao watoto anawaacha kwa wazazi je Huyo mume wake hawapendi watoto hao? Afadhali anemwacha mtoto kwa ajili ya kwenda shule.
Je? huu kweli ni uungwana...???

Thursday, June 6, 2013

BLOG MPYA KUANZISHWA...KARIBU KATIKA ULIMWENGU WA KUBLOG...

Ni blog  mpya iliyoanzishwa hivi karibuni kwa kutaka kujua zaidi ni nini inaibui tembelea hapa... karibu sana ndugu yetu.

Friday, March 1, 2013

Inuka Twende Ni Kwa Walioagana​- MAGGID MJENGWA

Ndugu zangu,
Hakuna wawili watembeao pamoja pasi na maelewano.
Ukiwaona wanadamu wawili wanatembea pamoja, basi, wana makubaliano. Ni watu waliopatana.
Kwenye kundi la watu wa mataifa tofauti ukimsikia Mtanzania anamtamkia Mtanzania mwenzake, tena kwa Kiswahili; " E bwana inuka twende zetu!", na Mtanzania huyo mwingine akabaki amekaa bila kushtuka, basi, utilie mashaka UTanzania wake.
Ndio, " Inuka twende ni kwa waliogana". Ni watu wenye kufahamiana. Ni ndugu.
Nimeanza kuingiwa na hofu kuwa Watanzania tumeanza kupoteana kama ndugu. " Inuka twende' yetu imeanza kuangaliwa kwa sura ya udini, ukabila na itikadi.
Hatujafika pabaya sana, lakini, tunakoelekea ni kubaya. Tumeshaziona ishara. Miongoni mwetu Watanzania tumeanza kuzisikia kaauli za ; " Umewasikia jamaa zetu Wakrito? Umewasikia jamaa zetu Waislamu? Umewasikia jamaa zetu WaZanzibar? Umewasikia jamaa zetu wa Bara?......"
Hizi ni ishara za undugu unaosambaratika. Zamani sisi sote tulikuwa ni ndugu. Tulitembea pamoja, ishara ya watu tuliopatana.
Leo kuna Watanzania wanaoambiwa; " E bwana wee, siku hizi nakuona unatembea na kuongea na wale jamaa zetu wa upande mwingine!"
Ndio, Watanzania tumeacha kuwa ndugu. Tunagawanyika kwenye mapande. Ni kwa kuzitazama tofauti za dini, kabila na itikadi.
Hatujafikia pabaya, lakini, tunakoelekea ni kubaya. Tukumbuke; " Inuka twende ni kwa waliogana". Watanzania tulishaagana. Tulishakubaliana. Tulijua tunakokwenda kama Taifa. Kama ndugu. Tumeanza sasa kusambaratika.
Tuinuke sasa twende kupambana na yote yenye kutugawa kama ndugu wa taifa moja. Tuna kila sababu, nia na uwezo wa kushinda mapambano haya dhidi ya ubaguzi wa aina zote.
Na hilo ni Neno La Leo.
Maggid Mjengwa,
Iringa.
0788 111 765
mjengwablog.co.tz

Thursday, February 14, 2013

NINATISHIWA UHAI WANGU...EVARIST CHAHALI

Evarist Chahali
JUMAMOSI Februari 2 mwaka huu itabaki katika kumbukumbu zangu kwa muda mrefu, pengine katika uhai wangu wote.Majira ya saa 3 asubuhi nilikurupushwa usingizini na kelele za mlango uliokuwa ukigongwa kwa nguvu. Wakati ninajiandaa kwenda kufungua mlango, nikasikia sauti yenye dharura ikisema, “bwana Chahali, polisi hapa, tafadhali fungua mlango.”
Nilichanganyikiwa kwani tangu nifike nchi hii zaidi ya miaka 10 iliyopita sijawahi kufanya kosa lolote au kukwaruzana na vyombo vya dola/sheria. Baada ya kufungua mlango, askari waliovalia kiraia walijitambulisha na kuonyesha vitambulisho vyao. Pia walinisihi kuwa nisiwe na hofu ya kudhani kwamba nimefanya kosa lolote.
Kwa kifupi, walinieleza kuwa wamepewa ujumbe kutoka moja ya taasisi za intelijensia za hapa kuwa kuna tishio la uhakika dhidi ya maisha yangu. Hata hivyo, walieleza kuwa kwa vile wao walipewa tu ujumbe huo na kutakiwa kuuwasilisha kwangu, hawakuwa na maelezo ya ziada. Walisisitiza kuwa nichukue tahadhari muhimu na kunipa maelekezo ya mawasiliano ya dharura.
Kwa vile nilikurupushwa usingizini, awali taarifa hiyo ilionekana kama ndoto iliyokuwa inaendelea hata baada ya kutoka usingizini. Ilinichukua takriban saa tatu kuzinduka kutoka katika mshituko huo, na kutambua uzito wa taarifa niliyopewa na polisi hao.
Nikaamua kwenda kituo kimoja cha polisi kupata ufafanuzi zaidi. Mara baada ya kujitambulisha, mazingira ya namna suala hilo lilivyokuwa likishughulikiwa kituoni hapo lilinipa picha kuwa jambo hilo lina uzito. Kwa kifupi, baada ya kitambo nilipewa ufafanuzi ambao haukutofautiana na maelezo niliyopewa awali na polisi walionitembelea katika makazi yangu.
Kikubwa ni kuwa taarifa hiyo ilionyesha kuwa tishio hilo dhidi ya maisha yangu linatokea huko nyumbani. Swali linaloendelea kunisumbua kichwa ni KWA NINI iwe hivyo.
Wakati si vigumu kwangu kuhisi wahusika wa mpango huo wa kijahili, napata shida kuelewa kwanini wahusika hao watumie fedha za walipakodi kuandaa operesheni ya kutaka kunidhuru ilhali ninaamini kwa asilimia 100 kuwa mimi si tishio kwa usalama wa Taifa letu.
Ndiyo, baadhi ya ninayoandika kwenye makala zangu na tweets zangu huko kwenye mtandao wa kijamii wa twitter yanaweza kuwachukiza baadhi ya watu, lakini kwa hakika kuchukizwa huko si sababu ya kutaka kunidhuru.
Hadi wakati ninaandika makala hii nimekuwa nikiishi kwa tahadhari kubwa. Faraja kubwa kwangu inatokana na sababu tatu za msingi. Kwanza, kwa vile nilizaliwa na kukulia katika familia inayomtanguliza Mungu katika kila jambo, nina imani kubwa kuwa mamlaka pekee kuhusu uhai wangu (yaani kuwa hai au kufa) ni Mungu pekee. Hakuna mwanadamu anayeweza kupora jukumu hilo la Mungu na kufanikiwa kufupisha uhai wa yeyote.
Pili, nina imani kubwa na taasisi za usalama za hapa Uingereza. Kimsingi, wenzetu hawa wanathamini sana usalama na uhai wa binadamu pasi kujali mhusika ni mzaliwa wa hapa au ni ‘mgeni’ kama mimi. Ushauri na sapoti ninayoendelea kupata inanipa matumaini makubwa kuwa nipo kwenye ‘mikono salama.’
Lakini tatu ni ukweli kwamba takriban miaka mitano sasa nimekuwa nikiishi na uelewa kwamba kuna baadhi ya watu huko nyumbani wanaoniona kama kimelea cha maradhi hatari ambacho kikiachwa bila kudhibitiwa kitazua balaa.
Kwa sababu hiyo, tangu wakati huo nimekuwa nikiishi kwa tahadhari japo si kubwa kama hii ninayolazimika kuichukua sasa. Lakini ili uweze kuchukua tahadhari ni lazima uwe na mbinu na ujuzi wa kuchukua tahadhari husika. Kwa bahati nzuri, watu hao wanafahamu fika kuwa nina ujuzi wa kutosha na kuelewa na kumudu fika mbinu za kuishi kwa tahadhari.
Hata hivyo, kumudu mbinu ni suala moja na kuishi kwa kutumia mbinu hizo ni kitu kingine. Si jambo la kupendeza hata kidogo kuishi ukiwa na uelewa kuwa siku moja, mahala fulani unaweza kukumbana na madhara fulani. Lakini kadri unavyolazimika kuishi kwa namna hiyo inakuwa kama sehemu muhimu ya maisha yako, na ndivyo ilivyo kwangu.zaidi soma hapa

Monday, February 11, 2013

JUMATATU HII TUANZA HIVI:-DHULUMA KWA WATOTO YATIMA...


Je huu kweli ni uungwana... tutafakari pamoja..kila la kheri!!

Monday, December 3, 2012

MWANAFUNZI ABAKWA MPAKA ANAPOTEZA FAHAMU MKOANI RUVUMA!!!

JESHI LA POLISI mkoa wa Ruvuma limefanikiwa kumtia mbaroni Daud Ndunguru (19) wa mtaa wa Hoahoa uliopo Mbinga mjini na linaendelea kumsaka na mwingine jina lake ambaye halikufahamika mara moja linaendelea kumsaka kwa tuhuma za kumbaka mwanafunzi wa kike wa umri wa miaka 12 (jina lake limehifadhiwa) anayesoma darasa la nne katika moja ya shule za msingi zilizopo Mbinga mjini na kumsababishia maumivu makali na kupoteza fahamu.

Habari zilizopatikana jana mjini hapa ambazo zimethibitishwa na kamanda wa polisi wa mkoa wa Ruvuma Deusdedit Msimeki zimeeleza kuwa tukio hilo lilitokea desemba 2 mwaka huu huko katika mtaa wa Kihaha nje kidogo ya Mbinga mjini ambako mwanafunzi wa kike inadaiwa alibakwa na watu wawili akiwemo Daud Ndunguru ambaye alikamatwa muda mfupi baada ya kumfanyia kitendo cha kinyama msichana huyo na mwenzake ambaye jina lake halikuweza kufahamika alikimbia na kutokomea kusikojulikana.

Habari zaidi za tukio hilo zimefafanua zaidi kuwa watu hao wawili akiwemo Ndunguru majira ya saa 4:30 usiku walimvizia njiani msichana huyo na kumlazimisha atoe nguo alizokuwa amevaa na kisha kumfanyia kitendo cha ubakaji jambo ambalo limesababisha msichana huyo kupata maumivu makali sehemu za siri na kusababisha kupoteza fahamu.

Hata hivyo kamanda Msimeki alisema kuwa kufuatia kuwepo kw purukushani hizo majirani watoka na kwenda kwenye eneo la tukio ambako walifanikiwa kumkamata Ndunguru na mwenzake alikimbia huku msichana huyo akiwa amepoteza fahamu na walimchukua na kwenda nae kituo cha polisi cha kati cha polisi ambapo walichukua hati ya polisi ya matibabu (PF3) na kwenda nae hospitali ya serikali ya wilaya ya Mbinga ambako amelazwa na anaendelea kupata matibabu na hali yake inaendelea vizuri.
Kamanda Msimeki alisema kuwa mtuhumiwa Ndunguru anatarajiwa kufikishwa mahakamani pindi upelelezi wa tukio hilo utakapo kamilika na jeshi la polishi mkoani Ruvuma linaendelea kumsaka mtuhumiwa mwingine wa tukio hilo anayedaiwa kukimbia na kutokomea kusikojulikana baada ya kumfanyia kitendo cha kinyama msichana huyo
Habari hii nimeipata hapa