Tuesday, September 17, 2013

UJUMBE /SWALI WA/LA LEO!!!

Kama huwezi kujisamehe mwenyewe na uliyoyafanya, utawezaje kuwasamehe wengine?
NAWATAKIENI WOTE JUMANNE NJEMA SANA NA KUMBUKENI TUPO PAMOJA DAIMA!!!Kapulya!

3 comments:

ray njau said...

Bila shaka, si lazima kuomba msamaha kwa aksidenti ambayo hukusababisha. Na huenda nyakati nyingine likawa jambo la hekima kuwa mwangalifu kuhusu yale unayosema. Mithali moja ya zamani inasema: “Katika wingi wa maneno hapakosi kuwa na maovu; bali yeye azuiaye midomo yake hufanya akili.” (Mithali 10:19; 27:12) Lakini, unaweza kuwa mwenye adabu na mwenye kusaidia.

Hata hivyo, je, si kweli kwamba watu wengi wameacha kuomba msamaha, hata katika mambo yasiyohusisha mahakama? Huenda mke akalalamika nyumbani, ‘Mume wangu haombi msamaha kwa jambo lolote.’ Huenda msimamizi akalalamika kazini, ‘Wafanyakazi wangu hawakubali makosa yao, nao huomba msamaha mara chache sana.’ Huenda mwalimu akaripoti shuleni, ‘Watoto hawazoezwi kusema samahani.’

Huenda mtu asiombe msamaha akiogopa kwamba ombi lake litakataliwa. Huenda akakosa kueleza jinsi anavyohisi akiogopa kwamba atapuuzwa. Kwani huenda mtu aliyekosewa akamwepuka kabisa mkosaji na kufanya iwe vigumu sana kusuluhisha mambo.

Huenda wengine wakasita kuomba msamaha kwa sababu ya kutojali hisia za wengine. Huenda wakawaza, ‘Kuomba msamaha hakutarekebisha kosa nililofanya.’ Hata kuna wengine wanaosita kuomba msamaha kwa sababu ya mambo yanayoweza kuwapata wakifanya hivyo. Wanajiuliza, ‘Je, nitahesabiwa makosa na hivyo kuombwa nilipe fidia?’ Hata hivyo, sababu kuu inayofanya watu wasikubali makosa ni kiburi. Mtu aliye na kiburi sana asiweze kusema “naomba msamaha,” anaweza kukata kauli, ‘Sitaki kujiaibisha kwa kukubali kosa langu. Jambo hilo litanishushia cheo.’

Rachel Siwa said...

Mmmhh ujumbe wa leo.duhh umewaza kwa sauti KADALA.

sam mbogo said...

Kwa harakaharaka,wengi sisi waswahili/tanzania,kuomba msamaa ni marachache sana. kiukweli kuomba msamaa inategemea na nafsi ya mtu mwenyewe,mazingira yaliyo tukuza hayakutujengea utaratibu huu ,wakusema samahani kwa vinywa vyetu.huwa hatupendi kutamka samahani au nisamehe.kwa hiyo usitegemee sana mtu yeyote awae mweusi au mweupe asiposema samahani na uka mjaji kama haja kutendea haki.yaweza mtu huyo katika makuzi yake neno hilo la samahani halikutumika au halijazoeleka,pia yawezekana mtu huyo akawa na matatizo yake tu ambayo kama wewe unaye tarajia kuobwa samahani ungekuwa katika nafasi aliyo nayo yeye unge wezakujuwa kwanini mtu huyu hasemi samahani.maranyingi ubinafsi unatutawala sote anaye taka aombwe samahani,na anyaye takiwa kutoa au kusema samahani. muhimu ni kumsamehe nakujiweka huru,beinafsi huwezi juwa msamaha wako utakuwa umesaidia kwa kiasi gani huyo mtu asiye sema nisamehe. kaka s.