Tuesday, January 27, 2009

MAISHA YA KIJIJINI

Nimekuja wakati mzuri wa kilimo. Angaieni hapo halafu simeni, mi sisemi kitu

KISWAHILI NI LUGHA YA WATU GANI?

Nimekuwa nikijiuliza mara nyingi kiswahili ni lugha ya watu gani? Kwani sasa naona watu/nchi nyingi sana wanaongea kiswahili. Na pia nimesikia ya kwamba inasemekana ya kwamba imependekezwa kiswahili kiongewe Afrika nzima.


Swali:- Wenzangu mnafikiri itasaidia nini? Na kwa nini Afrika nzima waongee kiswahili? Wakati kiswahili ni lugha yetu ya TAIFA?.

Friday, January 16, 2009

UZAZI WA MPANGO

Hili swali limekuwa likinikera sana akilini mwangu:- Na sasa nimeona inabidi sasa tuanze kuamasisha uzazi wa mpango. Kwa sababu kuna wengi wanafikiri watoto ni rasilimali.

Jamiii inabidi tuzingatie uzazi wa mpango. Ili kuepuka watoto wa mitaani. Pia ni lazima kujali afya ya mama na malezi ya mtoto n.k.

Kama tukirudi nyuma tunakumbuka kulikuwa na kitu kilikuwa kinaitwa nyota ya kijani. Nashangaa sasa kwa nini tunayumba.

Kwa hiyo inabidi tuanze kuhamasisha kwani hali imekuwa mbaya, watoto wanazaliwa kila "asubuhi" wakati wazazi hawana uwezo wa kuwapa watoto hao:- kama vile chakula, malezi, malazi, elimu nk.

Mfano mzuri ni katika bara letu la Afrika:- Watoto huonekana kama baraka, na kuwa na watoto wengi huonekana kuwa ni baraka kubwa. Hivi ndivyo ilivyo. Lakini, mara nyingine, badala ya baraka mtu hukuta huzuni, uchungu na masikitiko.

Tuzae watoto ambao tunajua tunaweza kuwapa malezi bora kuliko kuzaa wengi kwa sababu ya tu eti nina watoto wengi, huku ukijua huwezi kuwapa malezi BORA.

Friday, January 9, 2009

SONGEA

Raha kwali kuwa nyumbani sasa nimekuwa hapa nyumbani kwa muda wa wiki moja. Na nimekula kila kitu ambacho sijala kwa muda mrefu. Ila kwa sasa nina kazi kidogo ninapaka rangi nyumba na pia kupanda miti jana nilipanda miti ya kawaida 120 na miti ya matunda pia. Jua kali na joto kweliiiiiiii. Ila ni raha sana kuwa nyumbani.

PIA NAPENDA KUWASHUKURU WOTE KWA KUNITAKIA SAFARI NJEMA ASANTENI SANA.