Showing posts with label amani. Show all posts
Showing posts with label amani. Show all posts

Monday, September 11, 2017

NI SIKU NYINGINE PIA WIKI NYINGINE NA NI JUMATATU....

Nawatakieni siju hii ya Jumatatu na wiki hii iwe yenye furaha na amani...pia nawatakieni yote mtakayofanya yawe yenye mafanikio mazuri.  PANAPO MAJALIWA TUTAONANA TENA !

Sunday, July 23, 2017

NAWATAKIENI JUMAPILI NJEMA

......Hayo mnayajua, ndugu zangu wapenzi, basi kila mtu na awe mwepesi wa kusikia bali si mwepesi wa kusena wala kukasirika....
Yakobo 1:19..
AMANI ITAWALE NYUMBANI WENU.

Sunday, January 15, 2017

JUMAPILI NJEMA KWA WOTE...AMANI NA FURAHA ZITAWALA KATIKA NYUMBA ZETU!

Zipo furaha nyingi duniani, watu wanafurahia kufaulu mitihani, kupata ajira, mtoto, kuoa na kuolewa, kuwa na mali nyingi na mambo mengi kadha wa kadha. Lakini hebu tuone furaha iliyo kuu kuliko zote, "Ndipo wale sabini  waliporudi kwa furaha wakisema hata pepo wanatutii, YESU akawambia msifurahi kwa vile pepo wanawatii BALI FURAHINI KWA SABABU MAJINA YENU YAMEANDIKWA MBINGUNI. Kumbe furaha kuu ni jina lako kuwa limeandikwa katika kitabu cha uzima. Luka 10:17-20".  JUMAPILI NJEMA.

Sunday, February 28, 2016

NI JUMAPILI YA TATU YA KWARESMA:- UJUMBE... MSHUKURU MUNGU KWA KILA JAMBO....

Mungu akikuacha katika hali fulani:-
Basi mshukuru wala usilalamike. Kwani yeye ndiye akujuaye zaidi. Pia usidhani kama maisha yamekamilika kwa mtu yeyote.
Kuna mwenye nyumba lakini hana gari, kuna mwenye gari lakini hana watoto, kuna mwenye watoto lakini hana pesa, kuna mwenye pesa lakini hana afya, kuna mwenye afya lakini hana kazi na kuna mwenye vyote lakini hana AMANI wala FURAHA. MSHUKURU MUNGU KWA KILA JAMBO.  Nami naanza kwa kusema AHSANTE MUNGU KWA KILA JAMBO.

Friday, December 25, 2015

NAWATAKIENI WOTE KRISMASI YENYE UPENDO, AMANI, FURAHA NA BARAKA TELE!!

Kamera ya Maisha ya Mafanikio ilikuwa mitaani lao na imepata picha hii ya mtoto Yesu..Hapa Papa Franciskus akimkabidhi mtoto Yesu  ili aende akalale holini ....Mwokozi amezaliwa. Na sasa hebu tusikilize mwimbo huu ambao ni zilipendwa wale wote wenye umri kama mimi na zaidi nadhani watakuwa wanaukumbuka..KARIBUNI.

YESU NDIYO SABABU YA KUWA NA HII SHEREHE YA KRISMASI...KWA HIYO BASI TUWE NA KRISMASI YENYE UPENDO, AMANI, FURAHA NA BARAKA....KRISMASI/NOEL NJEMA.

Sunday, May 24, 2015

NAPENDA KUWATAKIENI WOTE JIMAPILI NJEMA!!

zilipendwa

JUMAPILI IWE YENYA AMANI, UPENDO NA FURAHA KWA WOTE---Kapulya wenu.

Monday, December 23, 2013

TUANZE JUMATATU HII KIHIVI NA NENO AMANI!!!

AMANI:- Ni kitu cha thamani sana. Ambacho kila mtu angependa kuwa naye au hata kuwa na ndoto.
NAWATAEKIENI WIKI HII YA NOEL IWE NJEMA NA NOELIENDE SALAMA. KAPULYA

Friday, October 19, 2012

DAR ES SALAAM /KARIAKOO HAKUNA AMANI LEO HII

Mwenyezi Mungu nakuomba uzidi kuiongezee Tanzania yetu ili kusizidi zaidi ya hapa. Watu wawe na upendo na amani kama mwanzo..MUNGU IBARIKI TANZANIA YETU PIA WATU WAKE....

Sunday, April 29, 2012

JUMAPILI NJEMA KWA WOTE WATAKAOPITA HAPA!!

Upendo na Amani Ametujalia Mungu!!
Hili ndilo neno la Jumapili ya leo!!