Friday, October 19, 2012

DAR ES SALAAM /KARIAKOO HAKUNA AMANI LEO HII

Mwenyezi Mungu nakuomba uzidi kuiongezee Tanzania yetu ili kusizidi zaidi ya hapa. Watu wawe na upendo na amani kama mwanzo..MUNGU IBARIKI TANZANIA YETU PIA WATU WAKE....

2 comments:

ray njau said...

Ulinzi na usalama ni jambo la msingi kwa serikali yoyote.Na ni wajibu wetu raia kutii sheria za nchi na maelekezo yanayotolewa na mamlaka husika.Uhuru wako unaishia pale wa mwenzako unapoanzia.[Tunapomuomba Mungu adumishe amani katika jamii yetu ni muhimu sisi wenyewe tujichunguze na tuone kama tunazingatia maagizo yake katika utii kwa serikali].
----------------------------------Kila nafsi na ijitiishe kwa mamlaka zilizo kubwa, kwa maana hakuna mamlaka isipokuwa kwa njia ya Mungu; mamlaka zilizopo zimesimamishwa na Mungu katika vyeo vyao vya kadiri.Kwa hiyo yeye anayepinga mamlaka amechukua msimamo kupingana na mpango wa Mungu; wale ambao wamechukua msimamo kupingana nao watapokea hukumu juu yao wenyewe.Kwa maana wale wanaotawala ni kitu cha kuogopesha, si kwa kitendo chema, bali kwa kibaya. Basi, je, unataka usiogope hiyo mamlaka? Endelea kufanya mema, nayo itakusifu wewe;kwa maana hiyo ni mhudumu wa Mungu kwako kwa faida yako. Lakini ikiwa unafanya mabaya, ogopa: kwa maana haichukui upanga bila kusudi; kwa maana hiyo ni mhudumu wa Mungu, mlipiza-kisasi ili kuonyesha ghadhabu juu ya yeye anayefanya mabaya.

Kwa hiyo kuna sababu ya lazima kwenu muwe mkijitiisha, si kwa sababu ya ghadhabu hiyo tu, bali pia kwa sababu ya dhamiri yenu.Kwa maana hiyo ndiyo sababu mnalipa kodi pia; kwa maana wao ni watumishi wa Mungu kwa watu wote wakitumikia daima kwa kusudi hili.Wapeni wote haki zao, yeye anayetaka kodi, kodi; yeye anayetaka ushuru, ushuru; yeye anayetaka woga, woga huo; yeye anayetaka heshima, heshima hiyo._Waroma 13:1-7

Yasinta Ngonyani said...

Nakubaliana nawe kaka Ray ni lazima kwanza wenyewe tuzingatie sheria na ndipo tupelekeo maombi yetu kwa Mungu. Na tuache U-SISI NA U-WAO, MAANA SISI NI SISI HAKUNA WAO.