Showing posts with label mwaka. Show all posts
Showing posts with label mwaka. Show all posts

Friday, December 27, 2019

SALAMU/BARUA KUTOKA BLOG YA MAISHA NA MAFANIKIO:- SHUKRANI KWA WOTE!!!

Habari zenu jamani!!
Zimebakia siku chache tu kuumaliza mwaka huu 2019 na kuingia katika mwaka mpya 2020. Hakika miaka inayoyoma na watu tunazidi kuzeeka. Ninachotaka kusema ni kwamba, blog ya MAISHA NA MAFANIKIO inapenda kuwashukuru wanablog wenzake wote, wasomaji wote na watembeleaji wote kwa ushirikiano mzuri tulioonyeshana.
Najua katika maisha watu wote hawawezi kuwa sawa yaani kimawazo. Lakini katika hizi blog zetu kwa asilimia kubwa imekuwa ni changamoto kwetu. Tumekuwa hatupendi kupoteana, mara mmoja wetu anapokuwa kimya kwa muda basi wengine tunakuwa hatuna raha tunachukua hatua ya kumtafuta. Hii yote inaonyesha ni jinsi gani ukaribu wa wanaBLOG sisi tu/ulivyo, hakika najivuna sana kwa uwepo wenu na kwa hili napenda kusema SISI SOTE NI NDUGU. NA PIA NAPENDA KUWATAKIENI WOTE KILA DOGO NA PIA KILA KUBWA MTENDALO LIWE JEMA. NA MWAKA 2020 UWE WENYE MAFANIKIO. KAMA KUNA KITU ULIAHIDI KUFANYA MWAKA HUU BASI JITAHIDI UFANYA KABLA HAUJAISHA. KWANI KUMBUKA HAKUNA KISICHOWEZEKANA. PAMOJA DAIMA. KAPULYA WENU!!!!

Tuesday, February 19, 2013

MUDA UNAPITA,.....LAKINI......

Bwana wewe nikuambie siri moja ya maisha,…’Mzee mmoja alikuwa kakaa karibu nami kwenye daladala kaniambia, tulikuwa tumekaa wote kwenye daladala na muda huo nilikuwa nimechoka, sikupenda kusumbuliwa, hamu yangu ilikuwa kupata usingizi kidogo, kwasababu najua nina zaidi ya masaa mawili ndani ya daladala hadi kufika kwangu, siunajua tena foleni.


Nikamwangalia yule mzee, alikuwa kaniangalia kuonyesha kuwa ana jambo muhimu nikaona nimsikilize na kumwambia , `Niambie mzee, huenda likanisaidia katika maisha yangu…’

‘Katika mipangilioa yako ya maisha , fanya juhudi pangilia mambo yako, fanya kazi kwa bidii na ipende dunia kama vile utaishi milele..siunaniona mimi hapa nimezeeka nina miaka sitini, lakini najihisi kama nina miaka mingine sitini mbele, sijipweteki, na kusema aah, mimi mzee basi tena, nasubiri cha kupewa, nani atakupa hivihivi dunia hii. Najitosa hivyohivyo kama vile nitaishi milele, ingawaje kwa kweli naukumbuka sana, na kuujutia ujana wangu…’ akaniangalia kwa macho makali. Akaongezea kusema `wakati ni mali, lakini wakati ni ukuta, unahitaji mipangilio…’ akatikisa kichwa na kuendelea kusema;

`Pili muabudu sana mungu wako kama vile utakufa leo, au hata sasa hivi, huwezi jua, hapa gari linaweza likadondoka, tukawa wote marehemu au nikafa mimi peke yangu, au hata bila kudondoka gari unaweza ukakauka ghafla, na ukafa. Sasa ni bora umwabudu aliye na mamlaka na hiyo roho yako kwasababu hujui muda gani ataichukua roho hiyo. Omba, muabudu mola wako kama vile hapo unapoomba ni sekunde au dakika yako ya mwisho…’ akainama chini na nilijua anamuomba mola wake!

Nilijiukuta nimelala na nilipoamuka yule mzee akawa hayupo, ina maana aliteremka kituo nyuma wakati mimi nimelala, nilijuta sana, kwani alionekana ana busara na mengi yakunieleza, lakini nimechelewa keshaondoka.

Mzee huyu namfananisha na mwaka huu, unayoyoma, ni muda mchache umebakia tutauita jina jingine, mwaka jana au sio , na tutaukaribisha mwaka mpya. Mwaka huu tulikuwa nao na tulikuwa na mengi ya kufanya, na sijui mangapi tulifanikiwa kuyafanya na mangapi hatukufanikiwa, sidhani wengi wetu tuna kawaida ya kuweka kumbukumbu hizo, sidhani. Kumbukumbu hizo tunaziona kwenye bajeti za serikali, bajetiza makazini, lakini sio bajeti ya mtu mmoja mmoja.

Mwaka huu tupo nao kwenye kiti una mengi ya kutuambia, lakini tunajifanya tumechoka, tunajifanya tupo busy…labda tungelitulia tukatafakari na kuwa nao bega kwa bega k wa mipango, huenda tungelifanikiw sana. Tumekuwa tukikimbizana na hili na lile na huenda hayo tunayokimbizana nayo haya maana, tunapoteza muda mwingi kwenye vilevi, kucheza bao, kuongea na kufanya mambo ambayo ukiangalia ni ya kupotezea muda, muda uishe ulale, siku ipite. Ndio siku inapita, umri unakwisha na mwaka huo unakwisha, tukiamuka tutaukuta haupo tena!

Tukiangalia katika maisha yapo mambo mengi yanaharibu miili yetu hasa vyakula, vinywaji, vipodozi, hasira zisizo na msingi na mambo kadha wa kadha ambayo unayaona mazuri kwa umri wa miaka hadi telathini ujanani yaani, lakini ukifikia zaidi ya umri huo, hayo hayo uliyokuwa ukiyaona mazuri yanageuka kuwa sumu mwilini mwako. Mfano vyakula vya mafuta, pombe, starehe , madawa, vipodozi na mambo anuai, ni mazuri, yanastarehesha katika umri wa ujanani, lakini ikifikia uzeeni hayo matamu yanageuka kuwa machungu, yanakuwa sumu. Tunajikuta tunaamndamwa na presha, kisukari, ugonjwa wa moyo, vidonda vya tumbo nk, kwasababu ya yale matamu tuliyokuwa tukiyafadi ujanani. Kosa hatukua na mipangilio, hatukuali kusoma na kujifunza uzuri na ubaya wa hilo unalilofanya au kula!

Sasa wakati umefika kabla mwaka haujaisha kaa na huu mwaka kabla haujaisha, kumbuka yale ya muhimu, panga matarajio ukiwa na malengo kuwa utaishi milele. Na mipango hiyo haiwezi kuja kichwani tu, chukua karatasi pata muda, hata ikibidi soma, tafuta , uliza, kaa na mkeo au mumeo, angalieni matarajio, majukumu na mambo mbali mbali ya kimaisha yapangeni vyema na jinsi gani ya kuyatatua matatizo, jinsi gani ya kupata kipato, jinsi gani ya kusaidiana na hata kama huna kitu lakini kwa kujua nini kifanyike na kipi cha muhimu kwanza inasaidia, kuliko kulala, au kunywa pombe, au kusubiri mwisho wa siku ukaanza kupiga mayowe , kurusha mawe kwenye mabati eti unashagilia mwaka umekwisha, lakini umekwishaje? Ulikuwa nawo kweli wewe au ulikuwa umelala…!

Mkumbuke mola wako, kwani imani ni kitu muhimu sana, mola wako ndiye mwenye mamlaka na mwili wako, wangapi ulikuwa nawo siku za karibuni au mwaka huu sasa hawapo, je ina maana wao walikuwa na makosa na wewe uliyebakia huna makosa. Kumbuka wangapi wapo mahospitalini wagonjwa, wengine hawana viungo, wengine wanaomba mola awachukue kwa mateso wanayopata ya kansa au mengineyo, je wao walikuwa wanjua haya, je wao walimkosea Mungu ndio maana wanapata mateso haya, na wewe ni mbora zaidi yao ndio maana leo upo mzima. Hapana, wao hawajakosa, na wala wewe sio mbora sana mbora zaidi ni yule mcha mungu, ni yule anayemuomba mungu kuwa sala yangu hii huenda ikawa ya mwisho kuwa mzima, kuwa hai…nahivyo Sali kama vile hutaiona sekunde inayofuata.

Ujumbe huu nimetumiwa na msomaji wa Maisha na Mafanikio aishiye Arusha. Binafsi umenigusa sana nimeona nisiwe mchoyo niwajumuishe na wenzangu.

Thursday, January 31, 2013

Neno La Leo: Mwaka Ni Kama Noti Ya Elfu Kumi Ya Bongo, Ukiichenji​, Inapukutik​a!



Ndugu zangu,
Leo ni mwisho wa mwezi wa mwaka mpya. Na mwaka ulivyo ni kama noti ya shilingi elfu kumi ya Bongo. Ukiichenji tu, utashangaa inavyopukutika!
Ukae sasa ukijua, kuwa kesho ndio Februari Mosi. Hivyo, mwaka mpya wa 2013, kama ilivyo kwa noti elfu kumi, ndio tutakuwa tumeuchenji. Subiri sasa uone siku, wiki na miezi inavyopukitika. Fumba na kufumbua utasikia tumeshaingia Juni tunaelekea Bajeti ya Serikali ya Julai, na ukitoka hapo utafikiri mwaka unateremsha milima ya Kitonga.
Inatukumbusha nini?
Umuhimu wa kupanga mambo yetu. Inahusu muda na matumizi ya muda. Na mwanadamu usipokuwa makini na muda, itakuwa sawa na kisa kile cha mzazi aliyeulizwa na wanawe; " Mbona nguo za Krismasi hatujanunuliwa?"
Mzazi akawajibu wanawe; " Jamani, Krismasi ya mwaka huu imekuja ghafla sana!"
Kana kwamba hakujua, kuwa kwenye kalenda ya mwaka tarehe ya Krismasi imeshawekwa, Desemba 25!
Ndio, Afrika mvua hainyeshi ghafla, huwa kuna dalili zake. Na katika maisha, mambo mengi hayaji ghafla, bali hutukuta tukiwa hatujajiandaa. Jiandae na mwaka unaoanza kupukutika kuanzia kesho, kama noti ya shilingi elfu kumi. Kila la kheri.
Nimetumiwa na kaka Maggid Mjengwa.

Monday, January 2, 2012

NIMEONA TUUANZA MWAKA MPYA 2012! KWA MTINDO HUU!!!!!!

Mwaka mpya huwa ni wakati wa malengo mapya na mwelekeo mpya. Kila binadamu ana malengo yake hapa duniani. Mimi nina malengo yangu na wewe pia una yako. Kila kukicha huwa tunajitahidi kuyatimiza. Tunapasua vichwa kujaribu kuyatimiza malengo yetu . Ndio maisha.

Bila shaka na wewe umeshaketi chini na kujiuliza swali hili:- ninataka kutimiza malengo gani mwaka huu? Je? ni kurudi shule kuongeza ujuzi? Je? ni kuoa au kuolewa? Je? ni kujitolea zaidi katika jamii yako/yangu? Je? ni kutunza na kulinda mazingira? Msururu wa malengo unaweza kuwa mkubwa. Kama kutimiza malengo fulani fulani ndio mkakati wako wa mwaka huu basi zingatia ushauri ufuatao:-

Weka malengo yanayotimizika au yenye uhalisia-Jiangalie ulipo, angalia vitendea kazi ulivyonavyo, tazama kwa makini ujuzi ulionao kisha yapime vizuri malengo yako.

Jiulize swali au maswali:- Nitayatimizaje malengo yangu? ukishafanya hivyo jiwekee utaratibu wa jinsi ya kutimiza malengo yako. Yaani mpango wa utekelezaji wako.

Nenda utaratibu -Mwaka ndio kwanza umeanza, yakaribiribie malengo yako kwa mwendo wa taratibu. Usiwe na haraka wala pupa. Si unakumbuka kwamba mambo mazuri hayataki haraka?

Usiogope kurekebisha malengo-Kadri mwaka unavyoanza kusonga mbele, unaweza kugundua kwamba huenda kutimiza malengo fulani. Hiyo inawezekana kutokea kwa sababu mbalimbali zikiwemo za kiuchumi, kiafya au kibinafsi. Usihofu kurekebisha malengo yako.

Usiogope kushindwa-Yawezekana kabisa ukashindwa kutimiza malengo fulani fulani. Kwa sababu zaweza kuwa kama hizo nilizozitaja hapo juu, usiogope. Cha muhimu ni kujaribu na kujaribu na kujaribu. Jitahidi kadri unavyoweza, nina uhakika ukijaribu utafanikiwa kwa hiyo mwisho wa siku hadithi ya kushindwa wala haitokuwepo.

La muhimu ni kuomba msaada inapobidi yapo mambo mengine ambayo hutaweza kuyatekeleza peke yako. Hilo linapotokea, usiwe mgumu kuomba msaada.
Kwa mara nyingine tena nawatakieni wasomaji wa blogya MAISHA NA MAFANIKIO kila la kheri katika mwaka huu wa 2012.

Wednesday, December 21, 2011

SALAMU/BARUA KUTOKA BLOG YA MAISHA NA MAFANIKIO:- SHUKRANI KWA WOTE!!!

Habari zenu jamani!!
Zimebakia siku chache tu kuumaliza mwaka huu 2011 na kuingia katika mwaka mpya 2012. Hakika miaka inayoyoma na watu tunazidi kuzeeka. Ninachotaka kusema ni kwamba, blog ya MAISHA NA MAFANIKIO inapenda kuwashukuru wanablog wenzake wote, wasomaji wote na watembeleaji wote kwa ushirikiano mzuri tunaoonyeshana. Najua katika maisha watu wote hawawezi kuwa sawa yaani kimawazo. Lakini katika hizi blog zetu kwa asilimia kubwa imekuwa ni changamoto kwetu. Tumekuwa hatupendi kupoteana, mara mmoja wetu anapokuwa kimya kwa muda basi wengine tunakuwa hatuna raha tunachukua hatua ya kumtafuta. Hii yote inaonyesha ni jinsi gani ukaribu wa wanaBLOG sisi tu/ulivyo, hakika najivuna sana kwa uwepo wenu na kwa hili napenda kusema SISI SOTE NI NDUGU. NA PIA NAPENDA KUWATAKIENI WOTE KILA DOGO NA PIA KILA KUBWA MTENDALO LIWE JEMA. NA MWAKA 2012 UWE WENYE MAFANIKIO. KAMA KUNA KITU ULIAHIDI KUFANYA MWAKA HUU BASI JITAHIDI UFANYA KABLA HAUJAISHA. KWANI KUMBUKA HAKUNA LISILOWEZEKANA/KISICHOWEZEKANA. NAONA TUTAENDELEA MWAKANI NA KIPENGELE CHETU CHA MARUDIO YA MADA, MATUKIO MBALIMBALI PIA PICHA.. bila ninyi kipengele hiki hakingeweza kuwa. MBARIKIWE WOTE MTAKAOPITA KATIKA BLOG HII NA NYINGINE ZOTE. PAMOJA DAIMA. KAPULYA WENU!!!!

Tuesday, December 28, 2010

SALAMU/BARUA KUTOKA BLOG YA MAISHA NA MAFANIKIO:- SHUKRANI KWA WOTE!!!

Habari zenu jamani!!
Zimebakia siku chache tu kuumaliza mwaka huu 2010 na kuingia katika mwaka mpya 2011. Hakika miaka inayoyoma na watu tunazidi kuzeeka. Ninachotaka kusema ni kwamba, blog ya MAISHA NA MAFANIKIO inapenda kuwashukuru wanablog wenzake wote, wasomaji wote na watembeleaji wote kwa ushirikiano mzuri tulioonyeshana.

Najua katika maisha watu wote hawawezi kuwa sawa yaani kimawazo. Lakini katika hizi blog zetu kwa asilimia kubwa imekuwa ni changamoto kwetu. Tumekuwa hatupendi kupoteana, mara mmoja wetu anapokuwa kimya kwa muda basi wengine tunakuwa hatuna raha tunachukua hatua ya kumtafuta. Hii yote inaonyesha ni jinsi gani ukaribu wa wanaBLOG sisi tu/ulivyo, hakika najivuna sana kwa uwepo wenu na kwa hili napenda kusema SISI SOTE NI NDUGU. NA PIA NAPENDA KUWATAKIENI WOTE KILA DOGO NA PIA KILA KUBWA MTENDALO LIWE JEMA. NA MWAKA 2011 UWE WENYE MAFANIKIO. KAMA KUNA KITU ULIAHIDI KUFANYA MWAKA HUU BASI JITAHIDI UFANYA KABLA HAUJAISHA. KWANI KUMBUKA HAKUNA KISICHOWEZEKANA. PAMOJA DAIMA. KAPULYA WENU!!!!

Monday, December 27, 2010

MUDA UNAPITA,LAKINI.....

‘Bwana wewe nikuambie siri moja ya maisha,…’Mzee mmoja alikuwa kaka karibu nami kwenye daladala kaniambia, tulikuwa tumekaa wote kwenye daladala na muda huo nilikuwa nimechoka, sikupenda kusumbuliwa, hamu yangu ilikuwa kupata usingizi kidogo, kwasababu najua nina zaidi ya masaa mawili ndani ya daladala hadi kufika kwangu, siunajua tena foleni.


Nikamwangalia yule mzee, alikuwa kaniangalia kuonyesha kuwa ana jambo muhimu nikaona nimsikilize na kumwambia , `Niambie mzee, huenda likanisaidia katika maisha yangu…’

‘Katika mipangilioa yako ya maisha , fanya juhudi pangilia mambo yako, fanya kazi kwa bidii na ipende dunia kama vile utaishi milele..siunaniona mimi hapa nimezeeka nina miaka sitini, lakini najihisi kama nina miaka mingine sitini mbele, sijipweteki, na kusema aah, mimi mzee basi tena, nasubiri cha kupewa, nani atakupa hivihivi dunia hii. Najitosa hivyohivyo kama vile nitaishi milele, ingawaje kwa kweli naukumbuka sana, na kuujutia ujana wangu…’ akaniangalia kwa macho makali. Akaongezea kusema `wakati ni mali, lakini wakati ni ukuta, unahitaji mipangilio…’ akatikisa kichwa na kuendelea kusema;

`Pili muabudu sana mungu wako kama vile utakufa leo, au hata sasa hivi, huwezi jua, hapa gari linaweza likadondoka, tukawa wote marehemu au nikafa mimi peke yangu, au hata bila kudondoka gari unaweza ukakauka ghafla, na ukafa. Sasa ni bora umwabudu aliye na mamlaka na hiyo roho yako kwasababu hujui muda gani ataichukua roho hiyo. Omba, muabudu mola wako kama vile hapo unapoomba ni sekunde au dakika yako ya mwisho…’ akainama chini na nilijua anamuomba mola wake!

Nilijiukuta nimelala na nilipoamuka yule mzee akawa hayupo, ina maana aliteremka kituo nyuma wakati mimi nimelala, nilijuta sana, kwani alionekana ana busara na mengi yakunieleza, lakini nimechelewa keshaondoka.

Mzee huyu namfananisha na mwaka huu, unayoyoma, ni muda mchache umebakia tutauita jina jingine, mwaka jana au sio , na tutaukaribisha mwaka mpya. Mwaka huu tulikuwa nao na tulikuwa na mengi ya kufanya, na sijui mangapi tulifanikiwa kuyafanya na mangapi hatukufanikiwa, sidhani wengi wetu tuna kawaida ya kuweka kumbukumbu hizo, sidhani. Kumbukumbu hizo tunaziona kwenye bajeti za serikali, bajetiza makazini, lakini sio bajeti ya mtu mmoja mmoja.

Mwaka huu tupo nao kwenye kiti una mengi ya kutuambia, lakini tunajifanya tumechoka, tunajifanya tupo busy…labda tungelitulia tukatafakari na kuwa nao bega kwa bega k wa mipango, huenda tungelifanikiw sana. Tumekuwa tukikimbizana na hili na lile na huenda hayo tunayokimbizana nayo haya maana, tunapoteza muda mwingi kwenye vilevi, kucheza bao, kuongea na kufanya mambo ambayo ukiangalia ni ya kupotezea muda, muda uishe ulale, siku ipite. Ndio siku inapita, umri unakwisha na mwaka huo unakwisha, tukiamuka tutaukuta haupo tena!

Tukiangalia katika maisha yapo mambo mengi yanaharibu miili yetu hasa vyakula, vinywaji, vipodozi, hasira zisizo na msingi na mambo kadha wa kadha ambayo unayaona mazuri kwa umri wa miaka hadi telathini ujanani yaani, lakini ukifikia zaidi ya umri huo, hayo hayo uliyokuwa ukiyaona mazuri yanageuka kuwa sumu mwilini mwako. Mfano vyakula vya mafuta, pombe, starehe , madawa, vipodozi na mambo anuai, ni mazuri, yanastarehesha katika umri wa ujanani, lakini ikifikia uzeeni hayo matamu yanageuka kuwa machungu, yanakuwa sumu. Tunajikuta tunaamndamwa na presha, kisukari, ugonjwa wa moyo, vidonda vya tumbo nk, kwasababu ya yale matamu tuliyokuwa tukiyafadi ujanani. Kosa hatukua na mipangilio, hatukuali kusoma na kujifunza uzuri na ubaya wa hilo unalilofanya au kula!

Sasa wakati umefika kabla mwaka haujaisha kaa na huu mwaka kabla haujaisha, kumbuka yale ya muhimu, panga matarajio ukiwa na malengo kuwa utaishi milele. Na mipango hiyo haiwezi kuja kichwani tu, chukua karatasi pata muda, hata ikibidi soma, tafuta , uliza, kaa na mkeo au mumeo, angalieni matarajio, majukumu na mambo mbali mbali ya kimaisha yapangeni vyema na jinsi gani ya kuyatatua matatizo, jinsi gani ya kupata kipato, jinsi gani ya kusaidiana na hata kama huna kitu lakini kwa kujua nini kifanyike na kipi cha muhimu kwanza inasaidia, kuliko kulala, au kunywa pombe, au kusubiri mwisho wa siku ukaanza kupiga mayowe , kurusha mawe kwenye mabati eti unashagilia mwaka umekwisha, lakini umekwishaje? Ulikuwa nawo kweli wewe au ulikuwa umelala…!

Mkumbuke mola wako, kwani imani ni kitu muhimu sana, mola wako ndiye mwenye mamlaka na mwili wako, wangapi ulikuwa nawo siku za karibuni au mwaka huu sasa hawapo, je ina maana wao walikuwa na makosa na wewe uliyebakia huna makosa. Kumbuka wangapi wapo mahospitalini wagonjwa, wengine hawana viungo, wengine wanaomba mola awachukue kwa mateso wanayopata ya kansa au mengineyo, je wao walikuwa wanjua haya, je wao walimkosea Mungu ndio maana wanapata mateso haya, na wewe ni mbora zaidi yao ndio maana leo upo mzima. Hapana, wao hawajakosa, na wala wewe sio mbora sana mbora zaidi ni yule mcha mungu, ni yule anayemuomba mungu kuwa sala yangu hii huenda ikawa ya mwisho kuwa mzima, kuwa hai…nahivyo Sali kama vile hutaiona sekunde inayofuata.

Ujumbe huu nimetumiwa na msomaji wa Maisha na Mafanikio aishiye Arusha. Binafsi umenigusa sana nimeona nisiwe mchoyo niwajumuishe na wenzangu.

Wednesday, December 15, 2010

2010-KUELEKEA MWAKA MPYA 2011

Tafadhali nisaidieni kupata ufumbuzi wa swali la hicho kitu kinachoitwa mwaka mpya maana nimekuwa najiuliza miaka kibao sijapata hasa kujua hicho kinachoitwa mwaka mpya nini.

Mimi nimekuwa na mtazamo ninauambatanisha ili nanyi mnisaidie kupata ufumbuzi ambao naamini utawasaidia watanzania wengi

Naitwa Salehe Msanda niko Njombe Tanzania


SWALI HICHO KITU KINACHAOITWA MWAKA MPYA NI NINI AU NI KITU GANI?

1.SIKU YA KWANZA YA MWEZI JANUARI-1/1

2.NI TUKIO LA SIKU YA KWANZA YA MWAKA.

3.NI MABADILIKO YA KUTOKA KATIKA HALI MOJA KWENDA NYINGINE NA HASA KUMALIZA SIKU 365
NA KUZIANZA ZINGINE 365.

Kila mwaka inapofika mwezi wa 12 na hasa tarehe za kuanzia 15/12 huwa kunakuwa na pilikapilika nyingi za kwanza kuelekea katika sikukuu ya kuzaliwa mkombozi wetu yesu kristo na kumaliza mwaka na kuelekea kuanza kinachoitwa mwaka mpya.

Je tumewahi kujiuliza kwa makini na kupata angalau ufumbuzi/jibu/majibu, wa kitendaliwili cha
hiki kitu kinachoitwa mwaka mpya au tunakwenda tu kimazoea na hivyo kupelekea kuishia katika kufanya mambo kimazoea na kimapokeo?

Tukirudi katika swali na huenda ikiwa moja ya majibu ya hiki kitu tunachokiita mwaka mpya tukianza na jibu la kusema mwaka mpya ni siku ya kwanza ya mwezi januari yaani tarehe 1/1.

Hapa kunajitokeza utata hasa ukizingatia kwa mfano kuna mwaka mpya wa kiislam na kikristo
ambayo yote inaanza katika miezi tafauti kuzingatia na mwaka husika.

Lakini pia kuna suala la kama ni siku ya kwanza ya mwezi januari ni nini hasa kinachapelkea kufanya
siku hiyo kuwa ni ya kwanza na kuwa na umuhimu wa kipekee.

Tukija katika masuala ya hesabu na hasa msingi mkuu wa hesabu yaani kujtmlisha
+,kutoa-,kuzindisha X,na kugawanya .Tuatjikuta tunapata mambo yafuatayo katika siku hiyo ya
kwanza ya mwaka yaani 1/1/2011

Pia ukichukua namba hizo bila ya kuzitenganisha unapata 11 na 20 na namba 11 tena.

Maana yake kwa tafsiri yangu kwa kucheza na namba kwa kuamini kuwa mwaka mpya ni siku ya
kwanza ya mwaka tunapata mambo yafuatayo

Kunakuongezeka katika masuala mbalimbali mfano masuala ya kipato ,neema na kukua

Tukio la pili ni kufuta au kuondoa kile ulichonacho na kubaki ukiwa hauna kitu na hivyo kuanza upya

Tukio la tatu unabaki na kilekile ulichokuwa nacho kiwe kizuri au kibaya itategemea na mtazamo wa
mtu halikadhalika kwa tukio la nne linatubakisha katika hali ile ile.

Ukienda katika kuzitenganisha namba hizo za 1/1/2011 za mwaka tunaotarajia kufika na kwa
kuziweka bila ya kuzitenganisha unapata mabo yafuatayo yanayofanana 11=2,20 pia sawa na 2 na 11 ya mwisho sawa na 2.

Maana yake tunatakiwa kuongeza kwa upande wa mazuri hii ni tafsiri yangu
Pia ukirudi katika msingi wa hesabu na kuamua kutoa 1-1=0,2-0=2 na 1-1=0
Maana yake tunaweza kuongeza au kupunguza na kubaki palepale tulipokuwa
Ukizijumlisha namba zote 1+1+2+0+1+1=6,maana yake tuna nafasi ya kuongeza mara sita ya kile tulichonacho

Tukija katika jibu la pili kuwa ni tukio la siku ya kwanza la mwaka mtarajiwa 2011.
Mkanganyiko unakuja hiyo siku ya kwanza mbona haina tofauti na siku zingine? Maana kutakuwa na asubuhi,mchana,jioni na hatimaye usiku kama siku zote tulizozizoea na kama kwa huku Njombe tunatarajia kutakuwa na baridi kama kawaida yake na mvua.

Mkanganyiko mwingine unakuja iwapo ni tukio la siku ya kwanza utatafaotishaje iwapo imetokea ukapoteza fahamu kuanzia mfano tarehe 29 na kuzinduku siku hiyo maana utashuhudia mambo
nilypotaja hapo juu. Kama utazinduka asubuhi utaona hiyo hali ya asubuhi ambayo umeizoea
na halikadhalika kama ni mchana,jioni na usiku na zaidi utashuhudia watu jamaa na ndugu zako
wamekuzunguka. Na iwapo hautaambiwa kuwa leo ni mwaka mpya hautakuja kupata kitu au ishara itakayokuaminisha kuwa siku hiyo ni mwaka mpya.

Pia kwa upande mwingine tukienda kwa undani matukio tunayatarajia yawe na vitu au tabia
ambazo zinatoa nafasi ya kuona uhalisia wa tuki husika mfano tukio la kuzaliwa,kuna uhalisia hapo wa kupatika kiumbe mwingine ambaye atapita katika hatua za kuelekea kuwa mtu mzima.
Matukio ya u siku na mchana,kuwa na jua na mwezi kuna uhalisi wa kile kinachotokea lakini kwa hicho tunachakiita mwaka mpya sijaona uhalisia unaoweza kutuaminisha kuwa kweli mwaka mpya ni tukio kama matukio mengine.

Tukija katika jibu la tatu la mwaka mpya ni mabadiliko nadhani hapa ndipo tunapoweza kuona uhalisi wa mambo mbalimbali na kutuaminisha kuwa mwaka mpya ni zaidi ya hicho tunachofikria sisi cha siku ya kwanza ya mwezi januari.

Mfano ni ukweli uliowazi kuwa kama tunakubaliana kuwa mwaka mpya ni mabadiliko kama ni
mtoto aliyezaliwa tarehe 1/1/2011 atakuwa amefikia hatua ya kutembea hilo ni badiliko ambalo
wanafamilia wanaritarajia na ni lazima litokea labda kwa kesi chache. Kama ulikuwa unaitwa mr
na mrs Fulani mtakuwa mnaanza kuitwa baba na mama Fulani,lakini pia kama ulikuwa unaitwa
HANDSOME BOY NA BEUTIFULY GIRL utaanza kuitwa handsome man na beautiful woman. Na wale
waliokuwa wanajiita girlfried na boyfried wataanza kujiita manfriend na womanfriends.

Mfano hai sasa hivi dunia yote inapiga kelele kuhusu mabadiliko ya tabianchi kitu ambacho
kinatotokea kama mabadiliko kutoka na baadhi ya matendo ya binaadamu katika kutafuta
kukabiliana na mabadiliko ya mienendo ya dunia ya mabadiliko yanaypotokea katika ulimwengu huu tunaoishi mengine kwa kujua na mengine bila ya kujua.

Mwaka mpya ni mbadiliko inazihirishwa hata katika masuala mbalimbali ambayo wewe na mimi
tunayafahamu,mfano kama kwa wakulima na naamini tuliowengi tumetoka katika familia za
wakulima,shamba limelimwa kwa muda mrefu zao la aina moja huwa tunase,ma limechoka maana yake kumekuwa na mabadiliko yaliyopelekea shamba hilo kuchoka.

Kwa msingi huu kama wote tunakubaliana na jibu la tatu la hicho kinachoitwa mwaka mpya ni
mabadiliko sasa nini kifanyike kuanzia katika ngazi ya familia ambayo ndiyo msingi mkuu wa ujenzi wa masuala yote yanayomuhusu binaadamu na vile vilivyopo juu ya dunia ambayo mwanaadam amebalikowa kuingozo kuiweka chini ya imaya yake na tukirudi katika msingi wa jibu la kwanza katika majibu ya hesabu za msingi wa kuanzia masuala ya msingi

1. Tubadilike kwa kujikagua katika kila Nyanja ya maisha na kutenda kwa kuaongezaa kwa
upande wa kujenga ili kuwa na dunia Tanzania salama ya kuishi kuanzia katika ngazi ya
familia.

2. Tunatakiwa kuwajibika kwa maisha yetu na viumbe tunavyvitawala si kwa chini ya asilimia
60% na asilimia zilizobaki zitajaziwa na wengine. Ukiwajibika kwa zaidi ya asilimia 60% ni
vizuri zaidi.


3. Tuwe watu wa vitendo zaidi badala ya kuzungumza sana ,kulaumu,kulaani na kulalamika kwa
katika hali halisi kulaumu,kulaani na kuongea sana hakujawahi kubadili kile unachakitaka.


4. Tunatakiwa kubadilika kutoka katika hali inayoumiza wengi na kuhakikisha tunakuwa chachu
ya kuona kila mmoja anawajibika kuifanya Tanzania kuwa yenye neema, Furaha, upendo na
ridhiko.


5. Katika ngazi ya familia na walio katika uhusiano ni wakati wakuhakikisha uhusiano
unashamili na kuifanya taasisi ya kale katika dunia hii inayoitwa taasisi ya NDOA kuwa taasisi
yenye msingi imara wa kujenga kizazi kilichopo na kinachokuja.


6. Tukiamini kuwa mwaka mpya ni mabadiliko na tunatakiwa kubadilika kwa kutenda tutafika
mahali kila mmoja wetu atakuwa na furaha ya kweli . Maana inasadikiwa na ndio ukweli
ulivyo KATIKA KUTENDA HAKUNA KUSHINDWA ILI KUNAKUPA MATOKEO YASIYOTARAJIWA
na kama tukiamua kwa nia ya dhati mabadiliko yatakuja kwa haraka, tuache kukata tamaa
haraka na kutarajia kuwa mabadiliko yatakuja haraka kama unavyotuma mesege. Maana
tumekumbwa na electronic life style na kufikiria kila kitu kitatokea kwa mkabala wa
electronic.

Watanzania tusherehekee mwaka mpya kwa mtazamo kuwa mwaka ni suala la mabadiliko katika Nyanja mbalimbali za maisha na mabadiliko hayo yanatakiwa kutufikisha katika kuona maisha ni mazuri na ya kuvutia.

KILA LA KHERI KATIKA KUELEKEA MWAKA MPYA

Tuesday, March 30, 2010

Robo mwaka inakatika...Tumesonga mbele ama nyuma???

Amani, Heshima na Upendo kwenu.



Kwanza namshukuru MUNGU kwa baraka ya uhai ambayo mimi nawe tunayo.
Pili nikupe pole kwa harakati za maisha ambazo sote twazipitia kufanikisha yale mema tupendayo.
Nafurahi kuwasiliana na kila mmoja wetu kuweza kuwaza changamoto zilizo mbele yetu kama JAMII YA WANA-BLOG wenye lengo la kuigusa jamii na kisha tujiulize kama tunasonga mbele ama nyuma katika harakati zetu. Nashukuru kwa blogs na tovuti mpya ambazo zinachipuka na kuendeleza nia njema ya kuigusa jamii. Kaka Luta Kamala aliwahi kuandika akijuliza KWANINI TUNA-BLOG? (http://kamalaluta.blogspot.com/2009/07/swali-kwa-wenye-blogu.html) na hata Kaka Chambi Chachage aliuliza kama uwepo wa blog zetu unakuza ama kufifisha tasnia nzima ya uandishi (http://udadisi.blogspot.com/2009/08/blogu-zinachochea-au-zinafifisha.html). Jibu halisi tunalo mioyoni mwetu kulingana na dhamira tulizonazo.
Lakini kwa ujumla, haijalishi ni sababu gani ilikufanya u-blog, mwisho wa safari sote tunajikuta na zao moja ambalo ni JAMII. Awekaye picha anataka kuionesha jamii alichokiona, ahabarishaye anataka kuihabarisha jamii. Yule aandikaye Utambuzi anataka jamii ijitambue. Anayeweka kumbukumbu ni sababu anataka jamii ije isome baadaye. Atangazaye biashara anataka jamii ijue ilipo huduma. Afunzaye mapishi, mitandao, mavwazi, mitindo nk, woote wanalenga katika kuielimisha jamii.
Kwa maana nyingine sote twaiandikia JAMII.
Lakini je, mwaka huu ambao unamaliza robo yake ya kwanza wiki hii unaonekana kuwa hatua gani kwetu? Tumeshuhudia KUTHAMINIKA KWA KAZI ZA BLOGGERS kwa aina mbalimbali.
Tuliona wenzetu wakitunukiwa vyeti vya kuthamini kazi zao, tumesikia wengine (kupitia utambulisho wa blog zao) wamepata nafasi ya kushiriki vipindi vya idhaa za kimataifa kufanya uchambuzi wa habari. Hivi juzi tumemuona Kaka Michuzi akishiriki Diaspora huko London kwa nafasi yake kama blogger. Hizi ni chachu kwetu kuwa kuna kuonekana mchango wa kile tufanyacho na pia kuna kukua kwa ueleweka wa kazi zetu.
Ninalowaza ni VIPI TUNAWEZA KUWEKA NGUVU NA JITIHADA ZETU PAMOJA KUWEZA KUITUMIKIA VEMA JAMII?
Mafanikio ya blogger mmoja mmoja yanaweza kudhihirisha kuwa TUNAWEZA na tunalostahili kufanya ni kushirikiana na kuwa makini katika kila jema tutendalo.

Tunapoianza robo ya pii ya mwaka 2010, tuangalie nyuma na kujiuliza, robo ya mwaka inakatika....Tumesonga mbele ama nyuma??
Na hii iwe CHANGAMOTO YETU sote

Baraka kwenu nyote

http://www.changamotoyetu.blogspot.com

Saturday, January 2, 2010

MWAKA MPYA 2010!!!!!!!

Mwaka mpya huwa ni wakati wa malengo mapya na mwelekeo mpya. Kila binadamu ana malengo yake hapa duniani. Mimi nina malengo yangu na wewe pia una yako. Kila kukicha huwa tunajitahidi kuyatimiza. Tunapasua vichwa kujaribu kuyatimiza malengo yetu . Ndio maisha.

Bila shaka na wewe umeshaketi chini na kujiuliza swali hili:- ninataka kutimiza malengo gani mwaka huu? Je? ni kurudi shule kuongeza ujuzi? Je? ni kuoa au kuolewa? Je? ni kujitolea zaidi katika jamii yako? Je? ni kutunza na kulinda mazingira? Msururu wa malengo unaweza kuwa mkubwa. Kama kutimiza malengo fulani fulani ndio mkakati wako wa mwaka huu basi zingatia ushauri ufuatao:-

Weka malengo yanayotimizika au yenye uhalisia-Jiangalie ulipo, angalia vitndea kazi ulivyonavyo, tizama kwa makini ujuzi ulionao kisha yapime vizuri malengo yako.

Jiulize swali au mawswali:- Nitayatimizaje malengo yangu? ukishafanya hivyo jiwekee utaratibu wa jinsi ya kutimiza malengo yako. Wazungu wanasema weka vyema Action Plan yako.

Nenda utaratibu -Mwaka ndio kwanza umeanza, yakaribiribie malengo yako kwa mwendo wa taratibu. Usiwe na haraka wala pupa. Si unakumbuka kwamba mambo mazuri hayataki haraka?

Usiogope kurekebisha malengo-Kadri mwaka unavyoanza kusonga mbele, unaweza kugundua kwamba huenda kutimiza malengo fulani. Hiyo inawezekana kutokea kwa sababu mbalimbali zikiwemo za kiuchumi, kiafya au kibinafsi. Usihofu kurekebisha malengo yako.

Usiogope kushindwa-Yawezekana kabisa ukashindwa kutimiza malengo fulani fulani. Kwa sababu zaweza kuwa kama hizo nilizozitaja hapo juu, usiogope. Cha muhimu ni kujaribu na kujaribu na kujaribu. Jitahidi kadri unavyoweza, nina uhakika ukijaribu utafanikiwa kwa hiyo mwisho wa siku hadithi ya kushindwa wala haitokuwepo.

La muhimu ni kuomba msaada inapobidi yapo mambo mengine ambayo hutoweza kuyatekeleza peke yako. Hilo linapotokea, usiwe mgumu kuomba msaada.

Kwa mara nyingine tena nawatakieni wasomaji wa blogya MAISHA kila la kheri katika mwaka huu wa 2010