Showing posts with label mchicha. Show all posts
Showing posts with label mchicha. Show all posts

Friday, August 23, 2019

KAZI YA MIKONO YANGU....BUSTANI

Hapa ni zao la zabibu
Na hapa nimepanda mchicha na figiri ila nimechelewa kidogo. Lakini nina matumaini nitakula tu:-)

Monday, July 3, 2017

BUSTANI...NILIMTEMBELEA DADA YANGU MMOJA KWENYE BUSTANI YAKO HII NZURI

MCHICHA NA MAHARAGWE
Jana nilimtembelea dada yangu kwenye bustani yake. Ana bustani nzuri sana niliipenda sana na kumwonea wivu:-)  ila kwa upendo wake alinichumia mchicha mwingi tu nilimshukuru sana. Bustani yangu mwaka huu inasuasua....ila sijakata tamaa na hivyo nimeiona ya huyu dada nimepata nguvu zaidi......karibuni mtaona bustani yangu

Wednesday, July 24, 2013

MAPISHI:- LEO MLO NILIOANDAA NI HUU ANGALIA HAPA CHINI !!!!

 Hapa ni mishikaki ya kidali cha kuku ambayo imeandaliwa kwa kuwekwa kwenye mafuta kidogo,soya kidogo, kitunguu saumu,tangawizi na limau. Na baada ya hapo ikatundikwa kama mishkaki kama muonavyo tayari kwa mchomo....
 Na hapa ni sahani zitakazotumika kwa vile tutakuwa nje basi vilibebwa vingine pia kwenye sinia hilo. ambavyo ni nyanya, tikiti maji, njegere mbichi kutoka bustanini na zeituni za rangi mbili kijani na nyeusi.
 Mishkaki imeweka kwenye moto tayari kwa kuchomwa na dada Kapulya ...bahati mbaya haonekani kwenye picha kwani anakimbia ndani na nje kuangalia wali....
 Baada ya dakika kumi mishkaki inaonekana hivi nimechoma dakika tano kila upande..tayari kuliwa ..KARIBUNI TUJUMUIKE....
Na hii ni sahani ya Kapulya mshkaki mmoja, tikiti maji na nyanya pembeni, njegere, wali, na kitamu zaidi MCHICHI KUTOKA BUSTANI YANGU....MMMMMHHH. Hakika kulima raha..si mnaona eeeeh ..KARIBUNI ..ILA NIMEUKOSA UGALI..NITAANDAA KESHO NA MBOGA MABOGA:-)..HAYA MUWA NA JIONI/USIKU AU LABDA MCHANA AU ASUBUHI NJEMA. KAPULYA/KADALA.