Showing posts with label WALEZI. Show all posts
Showing posts with label WALEZI. Show all posts

Monday, June 18, 2012

TUENDELEE NA JUMATATU HII KUWA NA YASINTA:- KWA KUWASHUKURU WALEZI HAWA!!!

Nimekaaa hapa na mawazo tele , nikawa nakumbuka Songea Mahenge hapa ndipo nilipoanza kujitegemea. Na ndiyo nimeona nitoe shukrani zangu za dhati kwa wazazi /walezi wangu. Mama Nachihauli na baba Nyoni ahsanteni sana. Kwa yote mliyonifunza katika maisha na leo najua ni vipi kuishi na watu. MUNGU AZIDI KUWAZIDISHIA MEMA.......Hapa ni mwaka jana 2011 miezi kama hii.
Halafu hapa ni mama yangu wa hiari, baada ya kutoka Songea nikawa naishi Matetereka/Madaba na huko nikakutana na mama huyu. Mama Mgaya. Hakika sina maelezo zaidi ya kumshukuru kwa kunilea kama vile nilikuwa binti yake. Na bado ananilea mpaka leo AHSANTE MAMA kwa yote. MWENYEZI MUNGU NA AKUZIDISHIE UPENDO ULIO NAO Hapa pia ni mwaka jana ni NJOMBE KIHESA.
NINAWAPENDA NA NITAWAPENDA MILELE KWA YOTE MLIYONIFUNZA NA MNAYONIFUNZA.