Showing posts with label mavuno. Show all posts
Showing posts with label mavuno. Show all posts
Thursday, September 20, 2018
PALE UNAPOLIMA UNATUMAINA KUVUNA NA SASA MATOKEO TUNAYAONA
Hapo mwaona baadhi ya mazao niliyovuna nyanya, tikiti maji ambalo ndani ni njano tamu sana, zabibu na pia mwaona kwa pembeni ni pilipili ni raha sana kula vyakula ulivyolima mwenyewe kwa mikono yako. KARIBUNI TULE NDUGU ZANGU.
Sunday, May 22, 2016
NAWATAKIENI JUMAPILI NJEMA...UJUMBE- MAVUNO....
ZAO LA MAHINDI
Unapopanda mbegu huwa unategemea kuvuna mazao mengi...Hii picha nimetumiwa na ndugu yangu wa karibu sana. Utavuna ulichopanda. NAWATAKIENI WOTE JUMAPILI NJEMA SANA.
BASI TUMALIZIE NA WIMBO HUU WA MAVUNO WA MIRELLE BASWIRA NA CHRISTINA SHUSHO.........KARIBUNI!
Wednesday, August 27, 2014
MSIMU WA MAVUNO UMEFIKA /YAANI MWISHO WA BUSTANI KWA MWAKA HUU NA HAYA NDIYO BAADHI YA MATOKEO....!!!!
viazi mviringo (sisi wangongo twasema matosani)
Vitunguu saumu/swaumu
Na hapa ni vitunguu maji / au ni vitunguu vya kawaida
NAWATAKIENI SIKU NA KAZI NJEMA
Thursday, September 26, 2013
NIMELAZIMIKA KUVUNA NYANYA ZANGU KWA AJILI YA BARIDI KUWAHI MAPEMA KULIKO MATARAJIO YANGU....
Hizi ni nyanya zangu ambazo zilikuwa bado kuiva kama mnavyoona ...nimeamka leo asubuhi nimeshikwa na butwaa nyasi zote zilikuwa nyeupe theruji kabisa kitu ambacho zikutarajia kwa haraka hivi. Kwa hiyo imenibidi kuzivuna kabla hazijaharibika sana na kuzihifadhi. Vipi SIJUI kwa kweli..Je nikizihifadhi kwenye boxi zitaiva? Maana hapa ni nusu ya tulizokula....
Hahahaaa:-) na nikaamua nivune tu na vitunguu vilivyobakia ...mkulima wa ajabu anaanza kula kabla hajavuna na sasa vimebaki sita (6) tu....KARIBUNI KUNISAIDIA KULA NYANYA HIZO!!!
Hahahaaa:-) na nikaamua nivune tu na vitunguu vilivyobakia ...mkulima wa ajabu anaanza kula kabla hajavuna na sasa vimebaki sita (6) tu....KARIBUNI KUNISAIDIA KULA NYANYA HIZO!!!
Thursday, July 18, 2013
KILIMO CHA BUSTANI NA MAUA CHA DADA YASINTA...KARIBUNI !!!!!
Habari zenu..kuna wengi wameniuuliza vipi kuhusu bustani pia mapishi nipi na bustani ipi ila pilikapilika ni nyingi na hizi likizo lakini leo nimeona sio mbaya nichukue muda na kuwaonyesha maendeleo ya bustani yangu...Karibuni
Nyanya zimeanza kukomaa karibu nitakula
Kushoto ni mchicha na kulia ni figiri mnaona ilivyokua
Njegere zimeanza kuchanua
Viazi mviringo(matosani) navyo vimwanza kuchanua
Mdada huyu ni mpenzi wa maua pia mawe hapa mnaona maua yako yanavyoendelea.Kwa kuwa mtundu nikajaribu kupandikiza pilipili pia maana pitiku bila pilipili mmmmhh na matokeo ni haya
Sikuchoka nikajaribu kupandikiza dodoki Nanasi na tangawizi---Dodoki kwenye hicho chombo cha bluu, nanasi chombo cha blauni na tangawizi chombo cheupe. Kwa msingi kwa kweli unaweza kupanda kila kitu na kuvuna. Haya nawatakieni Alhamisi njema na karibuni kula mazao.
Subscribe to:
Posts (Atom)
