Showing posts with label huruma. Show all posts
Showing posts with label huruma. Show all posts

Monday, May 12, 2014

HIVI UNADHANI UMELETWA DUNIANI KUFANYA NINI?

Mama Theresa: Alitoa kila alichokuwa nacho kwa ajili ya masikini.

 Nimeakuwa nikiwaza sana kuhusu huyu mama Therese, nikawa najiuliza hivi ile ndoto yangu ya kuwa sista  kama kweli ningefanikiwa je? ningekuwa kama yeye? au je yeye alikuwa hivyi kwa vile alikuwa kama alivyo? au je? kuna mtu mwingine tena kama Yeye? Kama tujuavyo mtu ukipata cheo, au kubahatika kuwa na hali nzuri. Huwa hawawajali kabisa wenzao lakini labda mafanikio yako ni kwababu yao kimalezi na mawazo. Kidogo ulicho nacho gawana na wenzako na Mungu atakujalia..... baadaye nikakumbuka nilisoma sehemu habari ya mama Theresa HAPA...Ebu msoma Mama Theresa.... 
-------------------------------------------------------------------------------------------------------
Maisha. Kila mmoja anaweza kuwa na fasihi yake kuhusu maisha. Wale wanao yafasihi maisha kwa kufuata mafundisho ya imani zao wana fasihi yao wanasayansi wana fasihi yao, na wengine wengi wana fasihi yao, huku pengine kila mmoja pia akiwa na fasihi yake.
Lakini swali hilo nalo je; binadamu amekuja hapa duniani kufanya nini? Huenda hili ndilo ambalo litapata majibu tofauti kupita kiasi. Litapata majibu tofauti kwa sababu kila mtu huamini au kudhani amekuja kuishi hapa duniani ili kutafuta ustawi. Kwa bahati mbaya ustawi wenyewe nao unapimwa kwa kiwango cha fedha na mali mtu alizozipata.

Hebu tujiulize wale wenye fedha kupindukia hawahangaiki hata kuliko wale ambao hawana hata senti ya kula kesho? Bila shaka ni kuwa wanahangaika sana. Hii ina maana kwamba kama binadamu angekuja hapa duniani ili kutafuta ustawi wa fedha na mali watu hawa wasingehangaika kiasi hiko kwani tayari wangekuwa wamepata hicho ambacho kimewaleta.
Kuhangaika kwao kuna maana kwamba binadamu hakuja hapa duniani kutafuta usitawi wa fedha au mali. Kama ni hivyo binadamu amekuja kutafuta kitu gani basi? Ni swali gumu sana na siyo wengi ambao wametafuta jibu wamefanikiwa kulipata.
Ili mtu aweze kujibu swali hili karibu na usahihi inambidi kwanza ajue yeye ni nani. Bila kujua yeye ni nani mtu hawezi kujua kwamba amekuja au kuletwa hapa duniani kufanya nini.
Kwa lugha rahisi na ya kawaida sana binadamu ni mwili na roho yake. Kazi ya mwili ni kuhifadhi roho yake yaani mawazo na uwezo wote unaotokana na kufikiri. Iwe ni kwa imani au sayansi. Binadamu anagawanyika rahisi sana kwa njia au maelezo hayo tu.
Binadamu huzaliwa kukua na badae kufa. Kama kifo ndiyo mwisho wa binadamu basi ni rahisi sana kusema binadamu amekuja hapa duniani kufanya nini lakini kama kifo siyo mwisho wa binadamu kuna ugumu kidogo katika kueleza lengo la binadamu hapa duniani.
Kama kifo ndiyo mwisho wa kuwepo binadamu ina maana kwamba binadamu anapaswa kujitazama kama mwili zaidi kuliko kama kitu kingine. Hii ni kwa sababu kufa kwa mwili wake kutakuwa na maana ya kumalizika kwake. Ukiacha imani inayotokana na mafundisho ya dini zetu wengi wetu huwa tunaamini kwamba binadamu ni mwili na anapokuwa amekufa huwa ndiyo mwisho wake. Imani hii hujitokeza sana kwenye matendo yetu.
Lakini ninavyofahamu mimi ni kwamba maisha ni zaidi ya mwili. Ni katika mkabala huo ambapo tunaamini kwamba binadamu hakuja hapa duniani kukamilisha majukumu ya kimwili na matamanio yake bali amekuja hapa duniani kwa sababu nyingine zaidi.
Wengi wetu tunaamini kwamba tumekuja hapa duniani kwa ajili ya kutafuta fedha pamoja na ‘kutanua’ tunaamini kwamba tumekuja hapa duniani kutafuta vyeo na kuwakanyaga wengine na tunaamini kwamba tumekuja hapa duniani kutafuta umaarufu. Lakini historia haituonyeshi hivyo haikubaliani na imani hiyo ingawa tunajaribu kuikumbatia isituponyoke.
Badala yake ingetakiwa kuanza kujiuliza maswali hayo; baada ya kupata mali na ‘kutanua’, baada ya kupata madaraka na kuwakanyaga wengine na baada ya kupata umaarufu halafu kitafuata kitu gani? Jibu ni rahisi kwamba kutafuata utupu. Ni wengi sana ambao walijidanganya kwamba wamekuja hapa duniani kutafuta vitu hivyo na baada ya kuvipata wakagundua kwamba sivyo walivyovifuata.
Kwa maelezo mafupi na ya moja kwa moja ni kwamba binadamu amekuja duniani kutoa. Kwenye imani ya dini nyingi inaelezwa kwamba binadamu amekuja hapa duniani kumwabudu Mungu. Kuabudu mana yake kufanya ibada na ibada ina maana ya matendo yetu yote mema kuanzia asubuhi tunapoamka hadi tunaporejea tena kitandani.
Binadamu ameletwa duniani kuifanya dunia kuwa mahali pazuri panapofaa mtu kuishi na baadae kuondoka akiwa ameiacha dunia ikiwa salama zaidi kwa wengine. Wale wote walioishi miaka 150 tu iliyopita wameondoka. Wengi wameondoka kama mawe yanavyoondoka kwa kubanduliwa na misukosuko ya jua na mvua, lakini wengine wameondoka na kuiacha dunia mambo ambayo yamefanya maisha yetu kuwa bora zaidi. Hawa ndiyo ambao wangefanya kile ambacho kimemleta binadamu hapa duniani.
Kila mtu anacho kitu cha kutoa. Lakini ni vigumu kwa mtu kuwa na cha kutoa kama mtu huyo hafanyi ibada, yaani hatendi mema. Kama mtu ametawaliwa na mwili ni vigumu kwake kutenda mema, hivyo kuwa vigumu kwake kujua kile ambacho kimemleta binadamu hapa duniani.
Ili kuthibitisha kwamba binadamu ameletwa hapa duniani kwa ajili ya kutoa unaweza kutoa kuanzia leo, hebu jaribu kutoa ili uone matokeo yake, toa kidogo katika ziada uliyonayo kwa wosia nayo, toa upendo kwa wanaoukosa, toa huruma kwa wanaohitaji toa chochote unachoweza kukitoa kwa wanaokihitaji. Bila shaka ukiweza kufanya hivyo, utagundua siri ni kwa nini binadamu aliletwa hapa duniani..

Wednesday, March 6, 2013

NENO LA JIONI YA LEO :- JE WEWE UNASAMEHE?......JE, UNAPASWA KUONA KWAMBA UMEKOSEWA KIMAKUSUDI?

Kuna hali nyingi maishani zinazomfanya mtu akasirike. Tuseme kwamba unaendesha gari, na karibu ligongwe na gari lingine. Utatendaje? Umesoma kuhusu visa vingi vya madereva wenye hasira waliowashambulia madereva wengine. Hata hivyo, ukiwa Mkristo, bila shaka hungependa kufanya jambo kama hilo. Itakuwa bora zaidi kutua kidogo ili kuchanganua mambo. Labda wewe pia una makosa kwa sababu ulikengeushwa na jambo fulani. Au huenda gari la yule dereva mwingine lilikuwa na tatizo. Somo ni kwamba tunaweza kupunguza hasira, hisia za kukata tamaa, na hisia nyingine zisizofaa tukitumia uelewaji, tukiona mambo kwa njia tofauti, na kuwa tayari kusamehe. Andiko la Mhubiri 7:9linasema hivi: “Usiwe na haraka kuudhika katika roho yako, kwa maana kuudhika hukaa katika kifua cha wajinga.” Usione kwamba umekosewa kimakusudi. Mara nyingi, huenda tukafikiri kwamba mtu fulani ametukosea kimakusudi lakini huenda sivyo ilivyo; labda ni kwa sababu tu ya kutokamilika au kutoelewana. Jitahidi kuwa na maoni yenye usawaziko kuelekea matendo unayoona kuwa si ya fadhili, na uwe tayari kusamehe kwa upendo. Utakuwa mwenye furaha zaidi ukisamehe.—Soma 1 Petro 4:8 NA JIONI IWE NJEMA SANA KWA WOTE

Thursday, February 18, 2010

HADITHI YA MWANA MPOTEVU

Hiii hadithi inanikumbusha mambo mengi sana sijui wenzangu mnasemaje?

Kulikuwa na baba mmoja aliyekuwa na watoto wawili wa kiume. Siku moja yule wa mwisho akamwambia baba yake : baba mimi sasa ni mkubwa naomba haki yangu nataka kuondoka kwenda mbali kutafuta maisha. Baba yake akampa pesa nyingi tu. Akaondoka akaenda zake na pesa zote.

Muda si mrefu akapata marafiki wengi tu. akawa anakula na kunywa nao pamoja na yeye ndiye aliyekuwa analipa kila kitu.

Lakini muda si mrefu pesa zote zikamwishia. Akawa hana kitu cha kula. Marafiki zake wote hawakumpa wala kumsaidia chochote isipokuwa walimtupa barabarani.

Siku moja akaondoka akaenda kwa mkulima mmoja na kusema ya kwamba anaomba chakula, aina yoyote ile, na halafu atafanya kazi kwake. Mkulima akamhurumia akampa chakula na akamwambia kazi yake ni kuchunga nguruwe wake.

Hata hiyo kijana bado alikuwa ana njaa. Akaanza kuwaza: kwa nini napata taabu hapa wakati baba yangu ana chakula kingi tu. Narudi nyumbani kwa baba tena. Nataka kufanya kazi kwa baba kuliko hapa.

Mara akaanza safari ya kurudi kwa baba yake. Na kusema baba, naomba radhi nimekosa. Ilibidi nisirudi na wala usinipokee tena hapa nyumbani kwako. Lakini baba kwa uchungu wa furaha akamkumbatia na kumpokea. Kwa furaha kubwa baba akamfanyia kijana wake sherehe kubwa kwa kufurahia kwa sababu kijana wake alikuwa amerudi tena kwake.

Kaka mtu akawa anarudi toka kazini(shambani) akakutana na babake asemaye. Mdogo wako amerudi tena nyumbani njoo tumsherehekee. Alipotea sasa amerudi tena.

Swali: Je? Hadithihii wewe inakufundisha nini?
Na je? ungekuwa wewe ni yule kaka mkubwa ungefanyaje?

Hebu sikiliza hapa lugha ya mwenzetu wasukuma mimi nimeipenda kwani nimeelewa neno moja moja hata hivyo najivunia lugha zetu za asili zinasikika.


Au kama hujaelewa hapo basi sikiliza hapa lugha yetu ya kiswahili

Monday, October 19, 2009

Salma: Kwa nini alifungiwa ndani kwa miaka 24?

Mlemavu wa viungo Salma Mkomwa

Mama yake asimulia kisa cha kupata ulemavu

SIMULIZI ya msichana Salma Mkomwa (26) wa Morogoro kufungiwa nyumbani kwao kwa miaka 24 bila kutoka ndani imewashtua wengi hasa baada ya kujitokeza kwenye vyombo vya habari kuomba msaada wa kumwezesha kujikwamua.
Wengi wamekuwa wakijiuliza kisa cha kufungiwa kwa msichana huyo mlemavu kwa kipindi chote hicho. Wapo waliowashutumu wazazi wake na wengine wakidhani kwamba walistahili kupewa elimu juu ya malezi ya mtoto wao badala ya shutuma, alimradi kila mtu alisema lake.
Ili kujua kisa na mkasa, nilifunga safari hadi Kijiji cha Kichangani, Morogoro anakoishi msichana huyo kujua kulikoni? Nilikutana na kuzungumza kwa kina na mama yake, Mwanangavia Sewa.
Alijibu swali la kwa nini alimfungia binti yake kwa miaka 24... "Hatukuwa na uwezo wa kufanya chochote na wala hatukujua hata pa kuanzia baada ya Salma kuanza matatizo haya. Sababu kubwa ni kwamba hali ilikuwa ngumu."
Baada ya majibu hayo, mama huyo alianza kueleza mambo ambayo anadhani ndiyo chanzo cha binti yake huyo ambaye ni mtoto wa pili kati ya sita aliojaaliwa kupata ulemavu huo.
Akiwa na mimba ya miezi tisa, alifunga safari ya kutoka hapo Morogoro kwenda Handeni, Tanga kwa ajili ya kujifungua. Anakumbuka hiyo ilikuwa mwaka 1982.
Wiki moja kabla ya kumpata mtoto huyo, alikwenda shambani kuvuna ndizi, baada ya kupata mkungu wake, alijitwisha tayari kwa safari ya kurudi nyumbani. Akiwa njiani alidondoka.
"Kama unavojua mambo ya kijijini nilijifungua kwa mkunga sikujifungulia hosipitali lakini mwanangu Salma alikuwa mzima kabisa" anasema na kuendelea:
"Lakini wiki moja baada ya kujifungua mtoto akawa analia kupita kiasi kuna kulia kwa mtoto kawaida lakini yeye alizidi hadi kuwashtua watu nyumbani. Tukampeleka Zahanati ya Mzindu, Handeni walipompima wakasema mtoto hana tatizo lolote, wakatupa vidonge lakini hali ilibaki vilevile."
"Baada ya mwezi mmoja miguu ilianza kuvimba usawa wa magoti. Ikabidi nifunge safari kurudi Morogoro na kwenda Hospitali ya Mkoa.
Nilipomfikisha akapigwa x-ray sehemu za magoti ili kujua tatizo. Majibu yakaonyesha kuwa sehemu hizo zimeachana na damu haitembei.
"Madaktari wakasema nimechelewa hawezi kunyooshwa tena mifupa imekomaa. Wakati huo alikuwa na umri wa mwezi mmoja. Nadhani hii yote imetokana na kutojifungulia hospitali labda tatizo lingeweza kujulikana mapema."
Baada ya majibu hayo ilirudi nyumbani. Hali ya Salma iliendelea kuwa mbaya. Aliishia kupewa dawa za kutuliza maumivu na kupunguza uvimbe uliokuwapo miguuni.
Alipofikisha miaka mitano alipata nafuu. Uvimbe ulikoma hata kulialia kulipungua. Wakati wote huo mikono yake haikuwa na tatizo hata kidogo lakini siku zilivyozidi kusonga nayo ikawa inajikunja pamoja na miguu.
"Madaktari walishindwa jinsi ya kufanya na hatukuweza hata kununua gari la kumsaidia ndiyo maana ilibidi akae tu ndani kwa muda wote huo."
Habari kuhusu Salma zilijulikana baada ya Taasisi ya Faraja Trust Fund ambayo inashughulika na watoto wanaoishi katika mazingira magumu kutembelea nyumbani kwao.
Hata hivyo, hawakuwa wamekwenda kwa ajili yake bali mdogo wake wa kiume ambaye amekataa kwenda shule akiwa darasa la tano.
"Ilikuwa kama ndoto na sitakuja kusahau siku ile ambayo alikuja mlezi kutoka Faraja ambaye alikuwa akishugulika na watoto ambao wanaishi katika mazingira magumu na wasiopenda shule akiwemo mdogo wangu ndipo akanikuta," anasema Salma.
"Siku alipokuja nilikuwa ndani. Aliniona lakini aliondoka bila kuniambia kitu chochote hadi mwaka 2006 alipokuja tena na mama Ligaya alinipiga picha na kuipeleka katika Kituo cha Faraja."
Alipelekwa katika kituo hicho na baada ya kufika huko, Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Dk Lucy Nkya kwa kushirikana na shirika hilo walimpokea na kumpatia baiskeli pamoja nyuzi sita kwa ajili ya kuanza kufuma kwa kuwa tayari alikuwa na ujuzi huo.
"Namshukuru Mungu picha hizo zilipokwenda huko zilipokewa na hatimaye nilipata baiskeli ambayo inanisaidia katika maisha yangu kwani siwezi kutembea bila ya baiskeli."
Katika kipindi alichokuwa ndani alikuwa akijifunza kushona kwa kutumia chelewa za ufagio kwani hakuwa na uwezo wa kununua sindano ya kufumia vitambaa.
"Ninaweza kufuma vifuko vya kuhifadhia simu na tai na namshukuru Mungu naviuza Sh2,000 na watu wananunua. Shirika (Faraja), lilinipeleka katika maonyesho ya Sabasaba na hapo watu mbalimbali walielewa nini ninachofanya. Niliuza bidhaa zangu na kupata Sh200,000 na kupata msingi wa kuuza mkaa."
Fedha zinazopatikana katika shughuli zake wakati mwingine humsaidia mama yake ambaye ni mfanyabiashara wa mbogamboga hasa anapokosa bidhaa.
Salma hawezi kutembea wala kutambaa na hiyo ni changamoto kubwa katika maisha yake kwani anapokosa mtu wa kumsogeza alipo hulazimika kubaki hapo alipo liwepo jua au mvua.
Anayo tamaa kubwa ya kupata elimu lakini anasema wazazi wake hawana uwezo wa kumpeleka shule. Anatamani angejitokeza msamaria mwema kumsaidia pengine hiyo ingekuwa sehemu ya kujikomboa kimaisha.
"Nitashukuru pia kama nitapata mahala pa kuishi kwani hapa mazingira ni magumu. Baba ana wake wawili wote wanakaa katika nyumba hii na ana watoto 14 ambao wanamtegemea baba huyo na nyumba hiyo hivyo."
"Naomba tu Mungu mama yangu asitangulie mbele za haki kwani nitapata shida lakini kama nina nyumba yangu kidogo afadhali nitaweza kujisitiri."
Mwanamke aliyemfichua msichana huyo ni Jalia Lupapulo ofisa wa kituo hicho cha faraja chenye makao yake Kihonda, Morogoro. Anaungana naye kuomba wasamaria wema wamsadia akisema hajawahi kusoma. Kituo hicho hivi sasa kipo katika mchakato wa kumtafutia mwalimu maalumu.
Baadhi ya wataalamu wa tiba ya mifupa wanasema kwamba tatizo Salma linaweza kutibika kwa kupunguza kiwango cha ulemavu alichonacho.
"Nikimuona naweza nikajua tatizo ni nini hata kama ana umri mkubwa anaweza akasaidiwa tatizo likapungua ama siyo kwisha kabisa," alisema daktari mmoja.
Na Mahija Mpera gazeti la mwananchi

Tuesday, August 25, 2009

MATESO YA MTOTO FILIMINA

TTTTuwapende mayatima
Nimepata email kutoka kwa msomaji wa blog hii (ameomba nihifadhi jina lake) amenitumia taarifa ifuatayo ambayo imesikitisha sana, nami bila kusita kutokana na kuguswa na habari hiyo nimeona niiweke hapa kibarazani ili kuomba msaada kwa wadau walioko nyumbani Tanzania jijini Dar Es Salaam, wasaidie kumuokoa binti huyu. Naomba kuwasilisha.

Dada Yasinta,

Nimeshawishika kuwasiliana na wewe ili kujaribu kutafuta namna ya kumsaidia mtoto Fina ambaye ni yatima anayeishi katika mazingara ya mateso makubwa kupita kiasi.

Najua hunifahamu na wala sijawahi kuwasiliana na wewe hata siku moja lakini ningependa ufahamu kuwa mimi ni mmojawapo kati ya wasomaji wazuri wa blog yako.
Kwa kuwa nimeona kuwa blog yako inasomwa na wasomaji wengi nimeona nipitishie kilio cha binti huyu kupitia blog yako ili kutafuta namna ya kumsaidia.

Mimi naishi maeneo ya Tabata Kisukulu lakini ninaye girlfrind wangu anayeishi Tabata Kimanga jirani na mama huyo anayemtesa binti huyo yatima asiye na baba wala mama. Nimekuwa nikimtembelea Girlfrind wangu karibu kila siku na nimekuwa nikishuhudia mateso anayofanyiwa huyo binti
Nyumba anayoishi mama huyo iko Tabata Kimanga, unashuka kituo maarufu kiitwacho njia panda, mbele kidogo unafuata njia ya kushoto, utakuta gereji, ukiuliza kwa mama Enok au mama Frank maarufu kwa kuwauzia mafundi gereji maji ya baridi utampata.

Baada ya kuona mateso anayofanyiwa binti huyo, niliijaribu kuwauliza baadhi ya majirani na walikiri kuwa hilo ni jambo la kawaida, kwani binti amekuwa akipigwa kila siku takribani mara tatu kwa siku kwa makosa yasiyo na msingi kabisa.

Naamini wote tunafahamu malezi na namna ya kumuadhibu mtoto, lakini ikiwa mtoto anaadhibiwa hadi kuchomwa moto hiyo ni hatari, na tena kwa jinsi alivyo makini humchoma sehemu za mapajani ili isiwe rahisi kuonekana.
Nimefanya uchunguzi makini katika kipindi hiki cha mwishoni mwa juma na nimepata habari muhimu kadhaa ambazo mtu asipokuwa makini anaweza kudhani kuwa binti huyu haonewi. Huyu mama kwa kutaka kujenga mazingira ya kutoonekana kwamba anamtesa huyu binti, amekuwa akimsingizia mambo mengi kwa majirani na hata shuleni anaposoma ili ionekane kwamba ni mtoto jeuri, malaya na asiyesikia.

Ni mzuri kwa kutengeneza uongo na anaongea sana, ila naamini hata majirani watakuwa ni mashahidi wazuri katika kuthibitisha hili. Ni mateso makubwa sana anayopata binti huyu na hata kama ni mkosaji lakini adhabu anayopewa ni kubwa kuliko kawaida. Inaniuma sana na ninahisi si siku nyingi anaweza hata kumuua. naomba nikiri kwamba katika maisha yangu yote sijawahi kuona mateso ya namna hii, tena yanayofanywa na mwanamke ambaye na yeye anao watoto na anayejua uchungu wa kuzaa............ sasa nimejua ni nini maana ya roho mbaya tena mbaya zaidi naishuhudia kwa mwanamke.........

Nakuomba sana dada Yasinta uiweke habari hii katika blog yako ili jamii ya Watanzania na vyombo vinavyohusika vifahamu. Niliwasiliana na Chama Cha Waandishi Wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA), na waliahidi kufuatilia swala hili.
Ukweli ni kwamba dada kila nimuonapo binti huyu roho inaniuma sana na nimeshindwa kuvumilia unyama huu. Naamini labda mungu anayo makusudi yake, kwamba nilione hili ili nichukue hatua, na hatua yenyewe ndio hii ya wewe kunisaidia kumuokoa mtoto huyu. Jamani dhamira inanishitaki na naona kuna kitu kinanisukuma nimsaidie binti huyu kama binadamu mwenzangu....

Nimefanya uchunguzi wa kujua shule anayosoma na jina la mwalimu mkuu na namba yake ya simu, na nimepata taarifa zifuatazo:

Jina la Binti ni Filimina (Jina la baba yake sijalipata bado)na anasoma darasa la Tatu C
Jina la shule ni Tumaini Tabata Kimanga
Jina la mwalimu mkuu ni Mwalimu Mang’enya
Namba ya simu ya mwalimu mkuu ni +255 718 900190

Naomba ushirikiano wako,

Wednesday, May 20, 2009

KATIKA MAISHA NI VIZURI KUWAFARIJI MWENYE MATATIZO

Huu ni ushauri wangu mimi kwa wewe uliye na rafiki aliye na matatizo:-

1) Kama rafiki yako ana matatizo usiogope kumwuuliza hali yake kwa ujumla hata kama hali yake inaonekana si nzuri. Kama una matatizo halafu watu/marafiki wanakuuliza U HALI GANI utajisikia amani yaani kuna watu ambao wanakujali haupo peke yako.

Wakati mwingine kunatokea mambo, ambayo si kweli na watu wanafikiri kuwa tayari yule mwenye matatizo amepata msaada. Yaani mtu wa kuongea naye. Wakati kumbe wewe upo peke yako kwa hiyo kuuliza ni muhimu sana.

2) Piga simu au nenda ili kujua mpatwa matatizo ana hali gani. Pia pika chakula, nenda kwake na mle pamoja. Wakati matatizo yanapotokea, inakuwa ngumu kuelezea vitu ulivyozoea kufanya kila siku. Kama una watoto inakuwa ngumu zaidi kuwatunza wakati upo kwenye matatizo/majonzi. Kwa hiyo ni vizuri kusaidiana.

3) Onyesha upendo wako, bila kuonekana ni usumbufu kwa mpatwa matatizo, uwe nusu nusu. Usizidishe au usipunguze. HAPO NDIPO UTAWEZA. Kama nilivyosema hapa juu huu ni ushauri wangu mimi.!!!!