Showing posts with label MARAFIKI WABAYA. Show all posts
Showing posts with label MARAFIKI WABAYA. Show all posts

Monday, October 30, 2017

TUANZE JUMATATU HII YA MWISHO WA MWEZI HUU NA UJUMBE HUU....PUNGUZA MZIGO, PUNGUZA MARAFIKI WANAFIKI,PUNGUZA KABISA TENA WAPUNGUZE SANA TU, WAPUNGUZE ILI UWE MWEPESI



*Punguza marafiki ambao ukiwaambia unataka kufanya kitu wanakujibu "utawezaaa?" Punguzaaaa!*

*Punguza marafiki ambao kutwa wanataka mchafue meza bar. Punguzaaaa!*

*Punguza marafiki ambao umeongea nao kitu mkiwa wawili mwisho wa siku unakikuta kimeenea sehemu nyingine. Punguzaaaa!*

*Punguza marafiki ambao wako sahihi kila siku wenyewe hawataki kuambiwa wamekosea. Punguzaaaa!* 

*Punguza marafiki ambao wakija kwako wao urafiki unahamia kwa mumeo au mkeo aliyekaa sebuleni wakati wewe kakuacha nje. Punguzaaaa!* 

*Punguza marafiki ambao wanakuwa na urafiki na maadui zako kwa ukaribu zaidi. Punguzaaaa!*

*Punguza marafiki wa kwenye raha tu ukiwa na shida unajikuta peke yako. Punguzaaaa!* 

*Punguza marafiki wanaokusifu huku wakijua umekosea. Punguzaaaa!*

*Punguza marafiki ambao kila ukiwapigia simu na wao utawasikia yaani nilitaka kukupigia sasa hivi. Punguzaaaa!*

*PUNGUZA MIZIGO ISIYOKUWA NA UMUHIMU*
JUMATATU NJEMA  MAANA WIKI IJAYO ITAKUWA JUMATATU YA MWEZI MPYA WA KUMI NA MOJA:-)